Riwaya: UCHU

Riwaya: UCHU

Asante Mkuu Mareche, respect. Mkuu Fisherscom kinachosumbua hapa ni njaa/shauku/uchu wa kusoma palipo bakia.
 
Mkuu Fisherscom kinachosumbua hapa ni njaa/shauku/uchu wa kusoma palipo bakia.

Ni kweli mkuu....hiyo shauku ndo inatakiwa ili upate ladha kamili ya riwaya vinginevyo tutaanza kulaumu ooooh riwaya imepoa....mara oooh haina utamu,haivutii nk..
 
Ni kweli...hii ilikuwa moja ya riwaya zake za mwisho mwisho kabla ajaanza kujishughulisha na issue za Tanzania Chamber of commerce

R I P Aristablus Elvis Musiba...hakika pengo lako linaonekana. Umetuachia hazina kubwa mno ya riwaya zako....
Zilitujengea hamasa kubwa sana mioyoni mwetu...
Zilitujaza moyo wa uzalendo na kujua harakati mbalimbali za ukombozi na mapinduzi ya muafrika...
Zilitupa mshawasha ....dah hadi machozi yanataka kunitoka aisee nikiangalia kizazi kilichopo sasa hata kusoma gazeti tu ni kaaaazi kweli kweli.
 
duh imeniongezea uelewa wa masuala ya Rwanda na Burundi

Ni sehemu ya kazi ya riwaya...
Kuburudisha...
Kuelimisha....n.k
Hongera kwa kupata elimu/uelewa wa masuala ya Rwanda na Burundi. Definetly hata burudani pia unaendelea kuipata mkuu ntamaholo
 
Last edited by a moderator:
Ni sehemu ya kazi ya riwaya...
Kuburudisha...
Kuelimisha....n.k
Hongera kwa kupata elimu/uelewa wa masuala ya Rwanda na Burundi. Definetly hata burudani pia unaendelea kuipata mkuu ntamaholo

nina jamaa yangu ni mhutu kwa baba na mtutsi kwa mama. nilichukua episode ile ya mapadre wakimsimulia Willy Gamba, nikamtumia kwa messenger ya facebook. alinisifia eti naijua historia ya Rwanda.

burudani nayopata haina kifani
 
Last edited by a moderator:
mkuu mambo ya kubembelezana kama tunaimbisha demu humu yameshapitwa na wakati. kama mmeamua kuanzisha riwaya malizeni moja kisha muanze nyingine na sio kama mnavyofanya kutuwekea miriwaya nane ambayo haiishi.

kama mnaweka basi malizeni na kama hamtaki chapeni lapa vile vile maana mnaofanya ni utoto na ni ujinga wa hali ya juu.

km unakanusha kuwa hamjatumwa kupiga promo basi malizieni na msifikiri tutawabembeleza hapa

Daah watu wamegeuka mbogo sasa humu ndani... kidi kudi jus kam zis wei pliiiiz uokoe jahazi 😀😱
 
Last edited by a moderator:
Hivi kidikudi hii riwaya ya UCHU mbona sielewi nahisi kama kuna NJAMA ili isimalizwe na kama si HUJUMA hii tunaomba mtujulishe kwani mioyo yetu imejaa HOFU tunaomba tufikie KIKOMO cha riwaya hii. mkuu nimecheza na majina ya mtunzi wala sina dhamira ya kukulaumu sababu najua majukumu na mikwamo ni yetu viumbe ukiwa huru naimani mzigo utauweka.
 
GISENYI--VII

Mpinda alipofika kwenye nyumba
aliyokuwa amefikia, aliteremka haraka
kutoka ndani ya gari na kuingia ndani ya
nyumba hii, akawagongea wenzake
waliokuwa ndani ya vyumba, akiwataka
kwenye mkutano pale sebuleni.
Alifikiria na kuona kwamba Mwenyezi
Mungu alikuwa ameyajibu maombi yake.
Hii ilikuwa nafasi aliyoisubiri kwa muda
mrefu sana. Na yeye vilevile kama
wenzake wa Rwanda aliona nafasi hii
ilikuwa inazifaa pande zote tatu
zilizokuwa zinahusika kwenye harakati
hizi za mapambano. Kati ya wote
waliokuwa katika sakata hilo, alijiona
ndiye mwenye fursa ya kufaidika zaidi
ingawaje Serikali ya Rwanda ndio
ingefaidika zaidi kwa kuhakikisha kuwa
haina mgogoro au wasiwasi wa
kushambuliwa na Wahutu wenye
msimamo mkali chini ya wanamgambo
wa Intarahamwe na Banyamulenge
ambao nao wangefaidika kwa
kutobuguziwa tena na Serikali ya Zaire,
na wangeendelea na maisha yao raha
mstarehe.
Makamanda hawa walipokusanyika pale
sebuleni Mpinda aliwaeleza kila kitu jinsi
mambo yalivyokuwa wamejipa.
"Tunachotakiwa kufanya ni kukishawishi
na kukikahakikishia kikao cha Serikali ya
Rwanda na viongozi wa Banyamulenge
kuwa tutakapoanzisha vita hii ni kweli
uwezo wa kushinda tunao?. Pande zote
zimekubali kuwa sababu tunayo na nia
tunayo, swala hapa ni uwezo, wakiridhika
kuwa uwezo upo, basi mambo tayari",
Mpanda aliwaeleza wenzake.
"Mkuu, wala tusipoteze muda wa kufikiri,
sisi tumekuwa hapa tukijaribu
kuwashawishi siku zote, tusingekuwa na
uhakika na uwezo wetu kivita tusingekuja
kuomba watuunge mkono, uwezo tunao.
Nenda kawaeleze kwa uhakika kama
watatoa msaada kidogo tu, basi nchi yetu
tumeikomboa kutoka kwenye mikono ya
utawala wa Kidikteta na kifashisti", Col.
Mkengeri, mmoja wa makamanda wa
wapinzani wa serikali ya Zaire alijibu.
Wenzake wote walitingisha vichwa
kukubali maneno yake.
"Azimio, tunakwenda wote kushiriki kikao
hicho", Mpinda alijibu.

ITAENDELEA
 
Hivi kidikudi hii riwaya ya UCHU mbona sielewi nahisi kama kuna NJAMA ili isimalizwe na kama si HUJUMA hii tunaomba mtujulishe kwani mioyo yetu imejaa HOFU tunaomba tufikie KIKOMO cha riwaya hii. mkuu nimecheza na majina ya mtunzi wala sina dhamira ya kukulaumu sababu najua majukumu na mikwamo ni yetu viumbe ukiwa huru naimani mzigo utauweka.
nimependa ubunifu wako
 
Back
Top Bottom