Riwaya: UCHU

Riwaya: UCHU

Poleni jamani sikuwa na maana hiyo nilisoma page kama tatu za mwisho
Samahanini sana ndugu sitorudia

Asante kwa kuwa mwelewa mkuu....ujue hamasa ya kusoma hadithi au kuangalia muvi inatokana na ile shauku ya kutaka kujua mbele kilitokea nini sasa inapotokea mtu anaanza kuongelea matukio ya mbele utamu wote unaisha yan. Ndio tunajua Willy atashinda lakini ni namna gani alipata ushindi inabaki siri ya mwandishi
 
kama kidi kudi, technian na willy gamba wangetuletea mamboz, tusingetoboana macho. kila mtu angekuwa busy kusoma riwaya
 
NGUVU YA RUSHWA


Nkubana, huku damu zikimtoka, alikimbia moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Col. Gatabazi. Alipolisukuma lango la mbele alikuta likiwa wazi. Akaingia ndani, moja kwa moja kwenye mlango wa mbele ambao ulikuwa umefungwa. Aligonga kwa nguvu mpaka Col. Gatabazi aliyekuwa anaoga, alitoka haraka huku akiwa amejifunga taulo na bastola mkononi. "Nini", aliuliza kwa shauku baada ya kuona hali aliyokuwanayo Nkubana.


"Vaa tuondoke hapa, mambo yameharibika.


"Nini?", Col. Gatabazi aliuliza tena.


"Nakwambia vaa twende, mambo yameharibika", Nkubana alimjibu huku akielekea sebuleni, akafungua friji akatoa maji baridi na kunywa huku Col. Gatabazi akimwangalia kwa mshangao.


"Huyu mtu wako ni mchawi. Kawaua vijana wangu wote na sasa yuko na Bibiane. Kwa kuwa ilikuwa tumuue Bibiane, sasa atakuwa upande wa Willy Gamba. Hivyo, lazima tayari mambo yako yataelezwa, na Jeshi la RPF litakuwa hapa sasa hivi. Lililopo tuondoke hapa tufuate majeshi yetu Kihumba".


"Hebu nieleze vizuri imekuwaje, maana siamini kabisa mtu mmoja kufanya kazi kubwa namna hiyo, tena kwa watu wenye uwezo mkubwa kama wewe?", Col. Gatabazi aliuliza kwa hofu huku akielekea chumbani kujitayarisha kwa ajili ya kuondoka eneo hilo. Nkubana alimweleza kila jambo lilivyotokea kwa Bibiane na jinsi alivyopoteza vijana wake.
 
NGUVU YA RUSWA


II


Willy Gamba akifuatana na Bibiane usiku huo, huku mkononi mwake ameshika bunduki kubwa aina ya AK 47, walitembea kwa tahadhari kubwa kuelekea nyumbani kwa Col. Rwivanga. Walipofika hawakumkuta na nyumba yake ikiwa imefungwa. Kwa vile Willy alikuwa amepewa ufunguo wa ziada, walikuwa wameamua kwa ajili ya swala la kiusalama Willy awe analala pale, Alifungua mlango na kumvuta Bibiane ndani. Aliwasha taa ya sebuleni na kumsukumia Bibiane kwenye kochi.


Kwa mara ya kwanza ndipo Willy alipomwangalia Bibiane vizuri. Alistaajabu kuona kiumbe kizuri kama hiki kilivyojiingiza kwenye vitendo vya ugaidi wa ajabu. Hakika huyu msichana alikuwa mzuri. Ukisikia mrembo, urembo hio huu. Willy katika maisha yake alishawaona wasichana warembo lakini huyu alikuwa msichana mrembo kwelikweli.


"Asante kwa kuniokoa", Bibiane alimshukuru Willy Gamba huku akiwa amelegeza macho yake na kuonyesha tabasamu la aina yake mbele ya Willy ambaye alikaa kimya akimwangalia bila kujibu.


"Sasa niko upande wako, usipate taabu kunilinda, kwa jinsi ulivyookoa maisha yangu sasa nifanye vyovyote upendavyo", Willy kwa kumwangalia Bibiane machoni aliamini kuwa anasema ukweli.


"Nenda kaoge", Willy alimweleza Bibiane huku akielekea kwenye chumba alichokuwa akilala. Bibiane aliinuka taratibu na kumfuata Willy. Chumba alichokuwa akilala kilikuwa na maliwato ya ndani. Hivyo, alimuonyesha ishara Bibiane alifungua mlango na kuingia ndani.



Wakati Bibiane anaoga, Willy aliingia jikoni na kutayarisha kahawa. Alipoangalia saa yake ilikuwa yapata usiku wa manane. Alishangaa kwa nini Col. Rwivanga alikuwa hajarejea, akajiuliza ameelekea wapi wakati huo.
 
hiki kitabu sikuwahi kukisoma kabla, hakika ni riwaya makini sana. Mkuu kidi kudi tushushie yote.
 
ikiisha uchu tunaamia kwa JORAM KIANGO

1. Malaika wa Shetani
2. Tutarudi na Roho zetu
3. Salam toka Kuzimu
4. Dar-es-Salaam Usiku
5. Najisikia Kuua Tena
 
ikiisha uchu tunaamia kwa JORAM KIANGO

1. Malaika wa Shetani
2. Tutarudi na Roho zetu
3. Salam toka Kuzimu
4. Dar-es-Salaam Usiku
5. Najisikia Kuua Tena

Aiseee...sitobanduka
 
shusheni vitu kwa wingi km siku ya kwanza jmn.wengine tupo likizo hivyo tunapata muda mwingi wa kuperuzi
 
nimesoma hadithi nyingi za willy gamba lkn hii sijui ilinipitia wapi
 
ikiisha uchu tunaamia kwa JORAM KIANGO

1. Malaika wa Shetani
2. Tutarudi na Roho zetu
3. Salam toka Kuzimu
4. Dar-es-Salaam Usiku
5. Najisikia Kuua Tena

Mkuu nina wazo....Mi naona tuipitie riwaya ya kikomo afu ndo tumuanze Ben R. Mtobwa na joram kiango wake. Unaonaje..?
CC. Khantwe,rosob,kaizer
 
Mkuu nina wazo....Mi naona tuipitie riwaya ya kikomo afu ndo tumuanze Ben R. Mtobwa na joram kiango wake. Unaonaje..?
CC. Khantwe,rosob,kaizer

Mkuu,ngoja atupie moja ya JKiango tubadilishe mandhali kidogo kabla ya kurudi kwenye ombi lako.Kwenye kikomo kuna mtu/kitu kinaitwa Elungata,nadhani humu JF kuna mtu anaitwa Elungata.
 
Last edited by a moderator:
Techman umeturambisha asali kwa nchi ya kisu
Shusha madini basiii
 
Back
Top Bottom