SIRI PART3: MTUNZI PATRICK CK
JASUSI/GAIDI
SEASON 3 : EPISODE 1
DAR ES SALAAM –
TANZANIA
Saa tisa za alasiri
televisheni ya taifa ilikatisha
kipindi kilichokuwa
kinaendelea na kujiunga na
matangazo ya moja kwa moja
kutoka ikulu jijini Dar es
salaam ambako Rais wa
jamhuri ya muungamo wa
Tanzania alitarajia kutoa
hotuba kwa watanzania.Kama
ilivyokuwa siku
iliyotangulia,simu janja zote
ambazo zilikuwa zimewashwa
muda huo ziliunganishwa na
matangazo yale ya moja kwa
moja kutoka ikulu kwa lengo la
kumuwezesha kila mwananchi
kusikiliza ujumbe ambao Rais
wa Jamhuri ya muungano wa
Tanzania alitaka kuwapa
watanzania.Tayari wanahabari
walikwisha weka sawa kamera
zao na aliyekuwa akisubiriwa
ni Rais
Mlango ulifunguliwa na
Rais Dr Fabian Kelelo
akajitokeza akiwa
ameambatana na Mufti wa
Tanzania Sheikh Seleman
Majid.Muongozaji wa shughuli
ile alitoa maelezo machche na
kumkaribisha Rais aweze
kuzungumza na
watanzania.Rais alianza kwa
kuwatania kidogo waandhishi
wa habari kisha akaendelea
“Ndugu watanzania
wenzangu awali ya yote
ninamrejeshea utukufu Mungu
wetu aliye juu kwa
kutukutanisha tena siku
hii.Poleni sana wale wote
ambao mmeendelea
kuwapoteza wapendwa wenu
kufuatia vurugu zinazoendelea
na wale wote ambao mnauguza
majeraha nawatakiwa uponaji
wa haraka.
Ndugu watanzania,jana
nilizungumza nanyi kwa kirefu
na kuwasisitiza umuhimu wa
kutunza amani
yetu.Ninashukuru sana kwa
wengi kunielewa na taarifa
niliyoipata ni kwamba vurugu
zimepungua na hii ni dalili
njema kwamba tunaelekea
kuzuri.Bado naendelea
kuwasihi ndugu watanzania
tuachane na vurugu hizi
ambazo hazina maslahi kwetu
na hata kwa dini
zetu.Tunachokivuna katika
machafuko haya ni hasara
badala ya faida.Ndugu zetu
wengi wamepoteza
maisha,wengine hawajulikani
walipo,wengine wamepata
ulemavu wa kudumu na
wengine wanaendelea kuuguza
majeraha hospitali.Wengi wetu
tumepoteza mali,nyumba
zimechomwa moto,majengo ya
serikali yamechomwa na
kuharibiwa,miundo mbinu
imeharibiwa,biashara
zimefungwa nk.Ndugu zangu
kwa ujumla tunachovuna
katika machafuko haya ni
hasara kubwa na tuna kazi
kubwa ya kuijenga nchi yetu
baada ya machafuko haya
kumalizika” Rais akanyamaza
kidogo halafu akaendelea
“Jana baada ya kumaliza
kutoa hotuba yangu,nilipigiwa
simu na Mufti wa Tanzania
akaniomba tuonane leo
tuzungumze.Leo kuanzia
asubuhi nilikuwa na kikao
kirefu naye na kubwa
tulilolijadili ni kuhusiana na
vurugu hizi zinazoendelea
nchini namna tutakavyoweza
kuzmaliza.Imekuwa ni desturi
yetu kukaa mezani kila pale
inapojitokeza mikwaruzano
baina ya dini zetu na mara zote
katika mazungumzo ya pamoja
tumekuwa tukimaliza tofauti
na amani ikamalaki.
Tumezungumza mambo
mengi katika kikao hicho
kirefu na tumekubaliana kuwa
na kikao kikubwa
kitakachowahusisha viongozi
wakuu wa dini zote hapa
nchini ili tutafute
muafaka.Naahidi kikao hicho
kitafanyika mapema sana ili
tukae meza moja serikali na
viongozi wa dini tujikwamue
hapa tulipokwama na maisha
yarejee kama kawaida.Kwa
kuwa mambo mengi
nilizungumza jana leo naomba
nimpe nafasi Mufti ana neno la
kuzungumza na watanzania.”
akasema Dr Fabian na
kumkaribisha mufti wa
Tanzania Sheikh Seleman
Majid ambaye alianza kwa dua
kisha akaendelea
“Ndugu zangu,awali ya
yote nami nataka nianze kwa
kuwapa pole nyingi wale wote
ambao wamepoteza ndugu zao
hadi sasa katika machafuko
haya yanayoendelea hapa
nchini kwetu na wale wote
waliopata majeraha mbali
mbali nawaombea wapate
nafuu ya haraka.
Ndugu zangu watanzania
kwa siku kadhaa sasa nchi yetu
imekumbwa na machafuko
makubwa kabisa kuwahi
kutokea hapa
nchini.Machafuko haya
yalianzia katika nchi ya jirani
na yakaenea kama moto wa
nyika hadi kufika hapa
Tanzania.Ndugu zangu dunia
inashangaa nini kimetokea
Tanzania?Katika historia ya
nchi yetu hakujawahi kutokea
machafuko kama haya
yanayoendelea ya waumini wa
dini
kushambuliana.Mheshimiwa
rais alieleza kwa kirefu jana
namna ambavyo watanzania
tumekuwa tukiishi kwa amani
na upendo mkubwa licha ya
tofauti zetu za kidini.Tumeishi
kindugu tukishirikiana katika
mambo mbali mbali
sherehe,misiba n.k.
Hatujawahi kubaguana hata
siku moja kwa imani zetu.Nini
kimetufikisha hapa? Swali hili
ameliuliza Rais jana wakati
anatoa hotuba yake na kwa
swali hilo ndiyo lilinifanya
nitake kuonana na
mheshimiwa Rais ili kwa
pamoja tutafute majawabu ya
nini kimetufikisha hapa.
Tumekuwa na kikao kirefu
na tumezungumza kwa upana
kuhusu jambo
hili.Tumekubaliana kwamba
tuwe na kikao kikubwa cha
viongozi wakuu wote wa dini
ili kwa pamoja tuweze
kuzungumza na kutafuta
muafaka lakini wakati kikao
hicho kikiandaliwa
tumekubaliana kwamba sisi
viongozi wa dini
tuwahamasishe waumini wetu
watulie na waache
vurugu.Suala hili ni pana zaidi
ya tunavyodhani hivyo basi
tunataka kuipa serikali nafasi
iweze kulishughulikia hili
jambo na kupata chanzo
chake.Tunapoendelea
kushambuliana na kuuana
tunaifanya serikali ishindwe
kulishughulikia suala hili hivyo
Rais ametuomba kila kiongozi
wa dini ajitahidi kuhakikisha
anawahamasisha waumini
wake watulie waache vurugu ili
serikali ishughulikie kutafuta
chanzo cha jambo hili.
Ndugu zangu kufuatia
maelekezo hayo ya Rais,niko
hapa kuzungumza na ndugu
zangu wa upande wa waislamu
kuwasihi wasiendelee kushiriki
katika vurugu.Uislamu ni dini
ya amani na hata
tunaposalimiana tunasema
Assalam alaikum maana yake
amani iwe nawe. Dini ya
Uislamu ina mitazamo
inayofanana na dini nyingine
kuhusu suala hili la amani na
usalama.Katika mtazamo wa
Uislamu usalama una maana
ya amani na utulivu katika
jamii. Neno amani kwa ujumla
limezungumziwa katika karibu
aya 140 za Qur'ani ambacho ni
kitabu kitakatifu cha
Mwenyezi Mungu.Usalama na
amani vina mfungamano na
Mwenyezi Mungu Muumba.
Mwenyezi Muumba
mwenyewe amejitaja kuwa ni
"Assalam" kwa maana ya
amani na Mwenye amani na
salama na kwa msingi huo kila
usalama na amani ni mwangwi
wa dhati yake tukufu. Dhati ya
mwanadamu pia daima huwa
katika hali ya kustawi na
kufanya harakati za kuelekea
kwenye amani na utulivu
kamili ambao haupatikani ila
kwa amani na usalama , yaani
dhati ya Mwenyezi Mungu
Muumba.Aya ya 208 ya
Suratul Baqara inasema:
Enyi Mlioamini!
Ingieni katika usalama
nyote. Wala msifuate
nyayo za She'tani; hakika
yeye kwenu ni adui
aliyewazi.
Vilevile aya ya 61 ya Suratul
Anfal inasema:
Na (wapinzani wako)
wakielekea kwenye
amani nawe pia elekea,
na mtegemee Mwenyezi
Mungu. Hakika Yeye
ndiye Mwenye kusikia na
Mwenye kujua.
Neno "Islam" pia
linatokana na msingi wa neno
"Silm", na kwa hakika lina
maana ya kumfuata Mwenyezi
Mungu ambaye Yeye
mwenyewe ndiye amani na
usalama mutlaki na utulivu
kamili.
Neno jingine ni "sulh" ambalo
lina maana na amani,
maelewano na uhusiano
mwema baina ya wanadamu.
Uislamu umetumia neno hilo
ukitaka kuwepo upendo,
kuheshimiana, kujiepusha na
uchokozi na uhasama na
kuchupa mipaka ya wanadamu
wengine.
Ili kuweza kupatikana
amani na uadilifu, Uislamu
umeweka safari yenye awamu
tatu tofauti. Kwanza ni
usalama na amani ya ndani ya
nafsi. Katika awamu hii watu
wote wa jamii wanatakiwa
kutakasa nafsi zao na
kuzipamba kwa taqwa na
uchamungu.Katika awamu hii,
muumini anapaswa
kukomesha mpambano na vita
liyopo baina ya matamanio na
matakwa yake ya kinafsi na
yale ya kiroho, na kufikia
amani na usalama wa ndani ya
nafsi ili pande hizo mbili za
kinafsi na kiroho ziishi pamoja
kwa amani na kumsaidia
mwanadamu kufikia kilele cha
ukamilifu. Ni baada ya hapa
ndipo mwanadamu
anapokuwa tayari kwa ajili ya
harakati ya kijamii na
wanadamu wenzake kuelekea
kwenye malengo aali na ya juu
zaidi. Aya ya 103 ya Suratu Aal
Imran inasema:
“Na shikamaneni na
Kamba ya Mwenyezi
Mungu nyote kwa
pamoja, wala
msifarikiane”
Kwa msingi huo amani ya
ndani ya nafsi ndiyo msingi wa
ukamilifu wa kimaadili na
kiroho kwa ajili ya kuwa na
taathira kubwa zaidi katika
jamii ya Kiislamu.
Awamu ya pili ya amani na
usalama katika Uislamu ni
amani na usalama wa jamii.
Baada ya kuwa tayari kinafsi
kwa kuitakasa na kuisafisha,
mwanadamu huwa
ametengeneza mazingira
mazuri kwa ajili ya muungano
mpana zaidi wa kijamii na
wanadamu wenzake. Hapa
ndipo inapokuja amri ya
Mwenyezi Mungu inayowataka
Waislamu kuwa na umoja na
kujenga udugu. Sehemu moja
ya aya ya kwanza ya Suratul
Anfal inasema:
“Basi mcheni
Mwenyezi Mungu na
msuluhishe mambo baina
yenu, na mtiini Mwenyezi
Mungu na Mtume wake
ikiwa nyinyi ni
waumini.”
Kwa utaratibu huo
Waislamu hutoka katika
minyororo ya ubinafsi,
ubaguzi, dhulma na sifa
nyingine mbaya na kuwa watu
wema na wenye faida kwa
jamii.
Awamu ya tatu ya amani
na usalama inahusiana na
usalama na amani kwa wasio
Waislamu. Miongoni mwa
misingi na kanuni
zinazotawala jamii ya Kiislamu
ni kuishi kwa amani na
usalama na wasio Waislamu.
Kinyume na fikra na dhana za
wanafikra wengi wasio
Waislamu na propaganda
chafu za nchi za Magharibi,
Uislamu ni dini ya amani na
kuishi kwa usalama na wasio
Waislamu. Hii ni pamoja na
kwamba, huwezi kupata hata
aya moja ya Qur'ani
inayowalazimisha watu
kukubali dini hiyo kwa vita na
mabavu. Vita katika Uislamu
vina sura ya kujihami na
kujilinda mbele ya
mashambulizi yanayolenga
jamii ya Waislamu au watu
wengine wanaodhulumiwa au
kwa ajili ya kuzuia uchokozi na
hujuma za adui.
Suala la kuishi kwa amani
na usalama na wasio
Waislamu limesisitizwa sana
katika aya za Qur'ani tukufu na
hadithi, sira na mwenendo wa
Mtume na Aali zake
watoharifu. Suala hili pia
limejengeka juu ya nguzo ya
utukufu wa kiumbe
mwanadamu. Katika mtazamo
wa Uislamu wanadamu wasio
Waislamu wana heshima na
utukufu wa kidhati na
kimaumbile kutokana na
kushirikiana kwao na
Waislamu katika maumbile na
ubinadamu japo
wanatofautiana katika dini na
imani. Uhakika huu
unathibitishwa na sira,
mwenendo na maisha ya
Mtume Muhammad (saw).
Mfano wa wazi wa
mwenendo huo wa amani na
suluhu na wasio Waislamu ni
Mapatano ya Ungwana
yaliyofikiwa baina ya Mtume
(saw) na washirikina wa
Makka kabla ya kutangazwa
dini ya Uislamu, Mapatano ya
Hudaibiyya, mwenendo wa
Mtume Muhammad (saw) na
jinsi alivyokuwa akiamiliana
na tawala na wafalme wa
maeneo mbalimbali kama Iran
na Roma na kutumia njia ya
kutuma barua kwa watawala
na wafalme wa zama hizo
baada ya kuunda dola la
Kiislamu mjini Madina. Kwa
mfano tu Mtume (saw) alisema
katika amri aliyompa Amru
bin Hazm wakati alipomtuma
Yemen kwamba: Kila Myahudi
au Mkristo atakayekubali
Uislamu na kudhihirisha
Uislamu halisi atakuwa
mmoja kati ya waumini,
atakuwa na haki sawa na za
Waislamu na kushirikiana
nao katika vipindi vyote vya
shida na raha. Na kila
mtu atakayeamua kubakia
katika dini yake ya Uyahudi
au Unaswara kamwe
hatalazimishwa kuacha dini
yake, kwa sababu ujumbe wa
dini na risala za Mitume wote
wa Mwenyezi Mungu ni
kuleta amani, uadilifu,
kueneza masuala ya
kiroho,kumkamilisha
mwanadamu na kumfikisah
kwenye saada na ufanisi",
mwisho wa kunukuu.
Kwa msingi huo, katika
mtazamo wa Uislamu suala la
usalama na kuishi kwa amani
na wanadamu wengine wenye
itikadi na imani tofauti, ni
jambo lenye thamani na
umuhimu mkubwa. Hii ni
kutokana na ukweli kwamba,
ni katika mazingira ya amani
na usalama ndipo wanadamu
wanapoweza kuelekea kwenye
ukamilifu wa kimaada na
kiroho, bali hata kuweza
kumjua na kumwabudu
Mwenyezi Mungu.
Hivyo suala la kujenga na
kuimarisha amani na usalama
na vilevile juhudi za kulingania
amani na usalama wa
kimataifa na kuishi pamoja
kwa amani wanadamu wote
kwa msingi wa Tauhidi na
kumpwekesha Mwenyezi
Mungu, uadilifu na usafi wa
nafsi bila ya kujali dini, rangi,
na tofauti zao nyingine ndio
lengo la mwisho la Uislamu na
wafuasi halisi wa dini hiyo. Ni
wazi kuwa, kufuata
mafundisho ya dini hiyo
kunaweza kuwa suluhisho la
kumwondoa mwanadamu
katika kinamasi cha vita,
mapigano na migogoro ya
dunia ya sasa.
Ndugu zangu waislamu
nimejaribu kutoa ufafanuzi
mrefu kidogo kuhusu uislamu
na amani.Dini zote hapa
duniani zinahubiri amani.Hata
akija kiongozi wa dini ya
kikristu ataeleza namna biblia
takatifu inavyosisitiza
amani.Ninawataka ndugu
waislamu na wasio waislamu
mnaonisikiliza hivi sasa kokote
mliko wekeni silaha zenu chini
na turejee kuishi kwa amanai
kama ilivyokuwa hapo
kabla.Tuiachie serikali ilifanyie
uchunguzi jambo hili tujue
nani katufikisha hapa? Nani
waliotufarakanisha hadi ndugu
tukaanza kuuana? Nawasihi
tuweke mbele maslahi ya nchi
yetu.Tuna nchi moja tu na
tazameni kilichotupata baada
ya kuvuruga amani.Tumekosa
hata sehemu ya kukimbilia
kwani sisi kwa miaka mingi
tumekuwa ni kimbilio la wale
wote ambao amani imepotea
katika nchi zao.
Mufti alimaliza hotuba
yake kwa kuendelea
kuwasisitiza waumini wa dini
ya kiislamu na wa dini
nyingine kuachana na vurugu
ili amani irejee.Baada ya
kumaliza kutoa hotuba Mufti
na Dr Fabian wakaenda
kupata chakula cha mchana
pamoja.
WASHINGTON DC –
MAREKANI
Saa tano za asubuhi, Mark
Piller makamu wa Rais wa
Marekani aliwasili katika
nyumba kubwa aliyokuwa
akiishi jenerali Akiki
Rwamirama.Lilikuwa ni jumba
kubwa la kifahari lililokuwa na
viwanja vya michezo mbali
mbali kama vile mpira wa
kikapu,mpira wa wavu na
tenisi.Kulikuwa na miti mingi
kulizunguka jumba hilo na
kulifanya kuwa na utulivu
mkubwa,ni sauti za ndege
mbali mbali ndizo zilisikika.
Jenerali Akiki hakuwa na
taarifa kama Mark Piller
angekwenda
kumtembelea.Alikuwa ndani
ya sebule kubwa akitazama
runinga akifuatilia taarifa za
habari za vyombo mbali mbali
vya habari duniani na kubwa
alilokuwa analifuatilia ni
taarifa za kuhusiana na kile
kilichokuwa kinaendelea
Afrika mashariki hususan
nchini Uganda.
Mlango mkubwa wa
sebuleni ukagongwa na mmoja
wa walinzi wake akaenda
kuufungua akakutana na
walinzi wa makamu wa
Rais.Nje tayari msafara wa
makamu wa Rais ulikwisha
wasili na alikwisha shuka
akipiga hatua kuelekea
ndani.Jenerali Akiki
alipojulishwa kuwa ni makamu
wa Rais amefika akainuka
haraka na kwenda kumpokea
“Mheshimiwa Rais habari
yako” akasema Mark Piller
“Mark niite Akiki
inatosha.Hayo mambo ya Rais
yamekwisha pita.Mimi si Rais
tena wa Uganda” akasema
Jenerali Akiki
“Jenerali Akiki sisi
tunaendelea kukutambua
kama Rais halali wa Uganda
hivyo tutaendelea kukupa
heshima yako ya Rais”
akasema Mark
“Nashukuru sana
Mark.Karibu”
“Ahsante jenerali
Akiki.Tunaweza kutembea
tafadhali” akasema Mark na
Jenerali Akiki akamuongoza
wakaelekea katika uwanja wa
gofu.
“Jenerali Akiki vipi maisha
yako yanakwendaje
hapa?Unayafurahia?akauliza
Mark Piller
“Maisha yanakwenda
vizuri sana mheshimiwa
makamu wa Rais.
Ninayafurahia maisha.Tayari
akili yangu imekwisha anza
kuzoea maisha haya.Kwa
ujumla hakuna tatizo
lolote.Ninashukuru sana kwa
namna
mnavyonihudumia.Ninapata
kila ninachokihitaji”akasema
Jenerali Akiki
“Ninafurahi kusikia hivyo
mheshimiwa Rais.Ninakuahidi
utaishi maisha mazuri kama
uko peponi.Utapata kila
unachokihitaji na utayasahau
maisha yako yaliyopita”
akasema Mark Piller
“Ahsante
Mark.Sikutegemea kama
baada ya kuondolewa
madarakani ningekuwa na
maisha mazuri kama
haya.Washenzi wale
wametaifisha mali zangu zote
na bila ninyi ningekuwa
masikini wa kutupwa”
akasema Jenerali Akiki
“Niliwahi kukwambia
Jenerali Akiki kwamba
yanapofanyika mapinduzi rais
aliyepinduliwa mara nyingi
lengo huwa ni kumuua lakini
kama akinusurika akakimbia
basi mali zake zote ndani na
nje ya nchi hutaifishwa na
serikali iliyochukua
madaraka.Lakini hilo
lisikuumize kichwa kwa sasa
wewe ni tajiri na utakuwa na
mali mara mbili zaidi ya zile
ulizokuwa nazo ulipokuwa
madarakani.Hata kama
ukitaka familia basi unao
uwezo wa kuanzisha familia
tena kubwa.Kila kitu
kinawezekana mheshimiwa
Akiki”akasema Mark Piller
“Mambo yanaendeleaje
Afrika Mashariki ?akauliza
Jenerali Akiki
“Mambo yanakwenda
vizuri mheshimiwa Akiki.Meli
zetu kubwa za mafuta
zimepanga foleni katika
bandari ya Tanga zikipakia
mafuta.Kwa ujumla kila kitu
kinakwenda vyema”
“Safi sana.Nataka
ikiwezekana mchukue mafuta
yote yaliyopo Uganda
muyalete huku kwa watu
ambao wana shukrani na
utu.Nimeijenga Uganda lakini
shukrani zake ni hizi.Mark
kama upo uwezekano wa
kuongeza zaidi uchukuaji wa
mafuta fanyeni hivyo
tafadhali”akasema Jenerali
Akiki
“Jenerali Akiki hilo ndilo
lililonileta hapa kwako.Jana
nilikuwa na mazungumzo
marefu na Rais kuhusiana na
mpango huu
unaoendelea.Katika
mazungumzo yetu
tumekubaliana kwamba
tutanue zaidi operesheni
hii.Unajua Afrika Mashariki ni
tajiri sana.Tunataka tusiishie
kwenye mafuta peke tunataka
twende mbali zaidi tuingie
hadi katika rasilimali nyingine
kama vile madini.Nchi kama
Tanzania imebarikiwa madini
ya kila aina.Nchi kama
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo nayo vile vile ina
madini ya thamani.Tanzania
kwa mfano ina madini ya
dhahabu,almasi,na mengine
mengi bila kusahau madini ya
Tanzanite ambayo
hayapatikani sehemu nyingine
yoyote duniani zaidi ya
Tanzania pekee.Tunataka
operesheni yetu sambamba na
mafuta iende pia katika
maeneo hayo
niliyoyataja.Nimekuja hapa
kwako kupata ushauri
unadhani nini tufanye kutanua
operesheni hii Afrika
mashariki? Akauliza Mark
Piller
“Mheshimiwa makamu wa
Rais tena imekuwa vizuri
umefika.Muda mfupi kabla
hujafika hapa nilikuwa
natazama kile kinachoendelea
Afrika mashariki.Leo kuna
jambo limetokea nchini
Tanzania”
“Kumetokea nini Tanzania
?akauliza Mark Piller
“Rais wa Tanzania
amekutana na Sheikh mkuu
wa Tanzania na wamekuwa na
kikao kirefu wakizungumzia
vurugu zinazoendelea.Kikao
hicho kinaonekana kuwa na
mwelekeo mzuri wa kumaliza
vurugu hizo
zinazoendelea.Nimezisikiliza
hotuba aliyoitoa Mufti na kwa
kiasi kikubwa inaweza
kuwashawishi waumini
kuachana na vurugu
zinazoendelea.Kwa kawaida
waumini wa dini ni watiifu
mno kwa viongozi wao hivyo
kama wameambiwa na
kiongozi wao waache vurugu
basi watafanya
hivyo.Watanzania ni wepesi
sana wa kumaliza mambo kwa
amani na kwa mujibu wa
taarifa ambayo imetolewa
leo,tayari vurugu zimeanza
kupungua nchini Tanzania na
hii inatokana na hotuba ya
jana ya Rais Dr Fabian”
akanyamaza akamtazama
Mark Piller
“Mpango huu uliojadiliana
na Rais wako ni mpango mzuri
sana na wenye manufaa kwa
Marekani lakini ili mpango
huo ufanikiwe tunaihitaji mno
Tanzania.Vurugu lazima
ziendelee nchini Tanzania ili
majeshi ya Marekani
yaendelee kukaa nchini humo
na kama ikiwezekana basi
wanajeshi waongezezwe
zaidi.Tanzania haitakiwi ipate
amani kwani ikiwa shwari
hakutakuwa na ulazima wa
vikosi vya Marekani kuendelea
kuwepo na hivyo hatutaweza
tena kuendelea na uchukuaji
wa mafuta na rasilimali
nyingine” akasema Jenerali
Akiki
“Nini unashauri kifanyike
Jenerali Akiki? Tunategemea
sana ushauri wako kwa kuwa
wewe unalifahamu vyema eneo
la Afrika mashariki.Ushauri
wowote utakaoutoa
tutauzingatia” akasema Mark
Piller
“Kunatakiwa kufanyike
kitu cha haraka sana
kuhakikisha hali inaendelea
kuwa tete nchini Tanzania ili
vikosi vya Marekani viendelee
kukaa huko kwa muda mrefu
zaidi na kama ikiwezekana
viongezwe vikosi vingine”
akasema Jenerali Akiki
“Nini basi unashauri
kifanyike kwa haraka?Mimi na
mheshimiwa Rais tulifikiria
kuanzisha kikundi cha waasi
ambacho tutakiwezesha kwa
silaha na zana nyingine za
kijeshi ambacho kitaendesha
mapigano na serikali za Afrika
mashariki ili tupate nafasi ya
kuongeza wanajeshi zaidi
katika eneo la Afrika
Mashariki.Unaonaje kuhusu
mpango huo?akauliza Mark
Piller
“Huo ni mpango mzuri
lakini si muafaka kwa
sasa.Kuanzisha kikundi cha
waasi ni mpango wa muda
mrefu.Si jambo jepesi
kuanzisha uasi hasa katika
nchi kama Tanzania.Kwa nchi
ya jamhuri ya kidemo krasia ya
Congo kule hakuna shida
kwani wamekwisha zoea
mambo kama hayo lakini kwa
sasa tunalenga zaidi Tanzania
hivyo wazo la kuanzisha
kikundi hicho cha uasi
tuliweke pembeni
tutalishughulikia
taratibu”akasema Jenerali
Akiki
“Vipi kuhusu kuwatumia
IS kufanya mashambulio mbali
mbali ya kigaidi na kuua
watu?akauliza Mark Piller
“Hilo nalo ni wazo zuri
lakini bado si mpango mzuri
tunaouhitaji kwa
sasa.Tunatakiwa kufanya kitu
cha haraka”
“Nini basi unashauri
kifanyike kwa haraka jenerali
Akiki?akauliza Mark Piller na
Jenerali akiki akainamisha
kichwa akafikiri kisha akasema
“Hapa Marekani mnao
wanasayansi wa hali ya
juu.Nataka muwatumie
wataalamu hao kutengeneza
kirusi ambacho kitakuwa ni
hatari na ambacho kinaweza
kusababisha maangamizi
makubwa kitakachokwenda
kusambazwa nchini Tanzania”
“Kirusi? Akauliza Mark
Piller
“Ndiyo Mark.Mnatakiwa
kutengeneza kirusi ambacho
kinaweza kuwa hatari zaidi na
kwenda kukisambaza nchini
Tanzania ambacho kitasambaa
kwa haraka zaidi na
kusababisha vifo vya watu
wengi.Baada ya hali kuwa
mbaya Marekani itaongeza
wanajeshi Tanzania kwa lengo
la kwenda kutoa msaada wa
kibinadamu.Faida za mpango
huu ni kwamba vikosi vya
Marekani vitaongezwa na
kukaa kwa muda mrefu Afrika
mashariki na kuendelea
kuchukua mafuta na rasilimali
nyingine kama madini”
akasema Jenerali Akiki
“Jenerali Akiki wazo lako
ni zuri lakini linaonekana ni la
hatari kubwa.Wasi wasi wangu
ni vipi kama kirusi hicho
kitaweza kuvuka katika
mipaka ya Tanzania na
kusambaa sehemu mbali mbali
duniani na hatimaye kikafika
hadi Marekani? Tunaweza
kuwa tumetengeneza silaha
ambayo inakuja kutuua sisi
wenyewe.Wanajeshi wetu
walioko Tanzania wanaweza
wakaambukizwa ugonjwa huo
wakafa au wakaja kusambaza
virusi hivyo huku Marekani”
“Mark Piller hiyo ndiyo
njia pekee na ya haraka
ambayo mnaweza mkaitumia
ili vikosi vya Marekani
viendelee kukaa Afrika
Mashariki na hasa
Tanzania.Wanasayansi wenu
watakapotengeneza kirusi
hicho hatari watatengeneza pia
na kinga yake na wanajeshi
watakaokuwa Tanzania na
wale watakaopelekwa huko
watapata kinga hiyo hivyo wao
hawatadhurika na hicho
kirusi” akasema Jenerali
Akiki.Mark Piller alishindwa
ajibu nini wakabaki
wamesimama wakitazama
farasi kila mmoja akiwaza lake.
“Unalionaje wazo hilo
Mark?akauliza Jenerali Akiki
“Jenerali Akiki
ninashindwa kukupa jibu la
haraka haraka kwani mpango
huu ni mkubwa na wa hatari
sana”
“Nini hofu yako
Mark?akauliza Jenerali Akiki
“Hofu yangu ni kwamba
tunaweza kutengeneza kirusi
hicho hatari halafu kikageuka
na kuwa kisu cha
kutuangamiza sisi
wenyewe.Kitu kama kirusi
kinaweza kusambaa kwa
haraka sana na kufika hadi
Marekani kitu ambacho
hatutaki kitokee na ndiyo
maana umeona Marekani
hatupigani vita nyumbani
tunamfuata adui huko huko
aliko.Tunataka raia wetu wawe
salama siku zote ndiyo maana
ninahofu kwamba tunaweza
kutengeneza kirusi na
kikasambaa na kufika hadi
Marekani na kuua watu wetu”
akasema Mark Piller
“Hakuna haja ya kuwa na
hofu Mark.Nimesema
wanasayansi watengeneze
kirusi na kinga yake na kila
juhudi lazima zifanyike
kuhakikisha kwamba kirusi
hicho hakivuki nje ya mipaka
ya Tanzania.Mzilenge nchi za
Tanzania,Uganda na jamhuri
ya kidemokrasia ya
Congo.Tena mkitaka
kufanikiwa zaidi tengenezeni
kirusi ambacho kitasambaa
kwa njia ya hewa ili kiweze
kusambaa kwa haraka
zaidi.Nakuhakikishia Mark
kwamba hii ndiyo njia pekee
nyepesi ya kuweza kuongeza
vikosi Afrika mashariki na
kuendelea kuchota
rasilimali.Njia nyingine kama
makundi ya waasi hizo zitakuja
baadae” akasema Jenerali
akiki
“Jenerali Akiki naomba
nilichukue suala hili na
kwenda kujadiliana na
wenzangu tuone namna
tutakavyoweza kulitekeleza
lakini ni suala zuri na ahsante
sana kwa wazo hili zuri”
akasema Mark Pilller
“Mark muda unakwenda
kwa kasi na taratibu amani
imeanza kurejea Tanzania na
kama Tanzania ikiwa na amani
basi hata Uganda nako
kutakuwa na amani.Hampaswi
kuacha jambo hili likatokea
.Wakati wakiendelea na
mikutano yao ya kutafuta
amani wanatakiwa wapigwe
tena pigo lingine kabla
majeraha yao hayajapona”
akasema Jenerali Akiki
“Ahsante sana jenerali
Akiki tutalizingatia
hilo.Ninakwenda kuzungumza
na wenzangu halafu nitakupa
mrejesho nini tumekubaliana.
RIYADH – SAUDI ARABIA
Kiza kimeanza kutanda
katika anga la jiji la
Riyadh.Katika makazi ya
Habiba Jawad idadi ya watu
waliofika kuhudhuria msiba
wa mwanae Najma aliyezikwa
mchana wa siku hiyo baada ya
kujiua kwa kujipiga risasi
ilikuwa kubwa.Ulikuwa ni
msiba mkubwa kwa Habiba
Jawad ambaye huyu alikuwa ni
mtoto wake wa pili kufariki
baada ya Edger Kaka.
Wakati watu wakiendelea
na maombolezo Habiba Jawad
aliyekuwa katika mojawapo ya
nyumba zilizopo katika makazi
yake akiwa na akina mama
waliofika kumfariji, simu yake
ikaita akaitoa haraka haraka
kutazama mpigaji kisha
akaikata ile simu.Taratibu
akainuka na kuaga anakwenda
maliwato.Hakutaka mtu yeote
amsindikize.Alitoka ndani ya
ile nyumba akafuata ujia
kuelekea katika nyumba yake
na moja kwa moja akaenda
katika ofisi yake akawasha
runinga kubwa na akaonekana
David Walker.
“Habari yako Habiba”
akasema David Walker
“Nzuri David habari yako”
“Habiba unaonekana
hauko sawa leo.Kuna tatizo
lolote?akauliza David
“Nina msiba
David.Mwanangu amefariki
jana na leo tumemzika”
“Pole sana
Habiba.Hukutujulisha kama
una msiba”
“Usijali David.Nini
kinaendelea huko? Akauliza
Habiba
“Habiba kuna jambo
ambalo limejitokeza na
tunahitaji msaada wako”
“Sema David nini
mnahitaji?akauliza Habiba
“Tumekuwa tunafuatilia
kwa karibu sana kile
kinachoendelea Tanzania na
siku ya leo Rais wa Tanzania
amekutana na kiongozi wa dini
na kubwa walilolizungumza ni
kuhusiana na vurugu
zinazoendelea katika ukanda
huo wa Afrika
mashariki.Mazungumzo hayo
ya leo kati ya rais na kiongozi
huyo yanaonekana kwa na
mwelekeo wa kumaliza vurugu
zile za kidini zinazoendelea
Afrika Mashariki.Endapo
vuruguzile zitamalizika basi
hakutakuwa na ulazima wa
vikosi vyetu kuendelea kuwepo
Afrika mashariki na lengo letu
ni kuendelea kukaa hapo kwa
muda mrefu na hata kuongeza
wanajeshi zaidi.Kwa hiyo
tumeamua kufanya kitu cha
haraka ambacho
kitatuwezesha kupeleka vikosi
zaidi vya jeshi na kukaa Afrika
mashariki kwa muda mrefu
zaidi” akasema David Walker
“Mmekuja na mpango
gani? Habiba akauliza
“Tunataka kutengeneza
kirusi ambacho kitafanya
maangamizi makubwa
ambacho kitakuwa hatari
kuzidi kirusi cha
Ebola.Tutakwenda
kukisambaza kirusi hicho
Tanzania na baada ya hali
kuwa mbaya tutatuma vikosi
zaidi vya jeshi kwenda huko
kwa lengo la kutoa msaada
lakini papo hapo operesheni
zetu zikiendelea kama
kawaida”
“David hili la kusambaza
kirusi huoni kama ni jambo la
hatari?Ni vipi kama kirusi
hicho kitavuka mipaka na
kusambaa sehemu nyingine
duniani?Mnao wanajeshi wenu
kule ni vipi kama wakipata
virusi hivyo? Akauliza Habiba
“Hilo tayari tumekwisha
lijadili kwa kirefu
sana.Mwanasayansi
anayeandaa kirusi hicho
tumempa maelekezo ya
kuhakikisha kwamba
atakapokamilisha kutengeneza
kirusi hicho aandae na kinga
yake kwa ajili ya wanajeshi
wetu na tahadhari endapo
kirusi hicho kitavuka mipaka
ya Afrika Mashariki na kuenea
sehemu nyingine duniani.Hilo
halina tatizo kabisa Habiba”
“Nini natakiwa kufanya
kwa upande wangu?akauliza
Habiba ambaye hakuonekana
kutaka maongezi marefu
“Kwa upande wako
tunataka utusaidie kupata mtu
ambaye atapeleka kirusi hicho
Tanzania.Tunataka mtu
kutoka kundi la IS”akasema
David
“David kwa nini lazima
awe ni mtu kutoka IS?akauliza
Habiba
“Habiba hili ni shambulio
la kibaolojia hivyo basi mtu
huyo hapaswi kuwa
mmarekani.Tunataka
kumtuma mtu wa kundi la IS
ili hata kama akigundulika basi
ijulikane kuwa ni kundi la IS
ndio waliofanya shambulio
hilo.Nataka ufanye
makubaliano na kundi la IS
wape fedha za kutosha waweze
kutupatia huyo mtu ambaye
anatakiwa hapa Marekani
haraka sana ili aanze
kuandaliwa.Mtu huyo
atawekewa kwanza kinga ya
kumkinga dhidi ya kirusi hicho
halafu atapandikizwa kirusi
hicho ambacho atakwenda
kukisambaza Tanzania”
akasema David Walker
“Lini huyo mtu
anahitajika?akauliza Habiba
“Tunamuhitaji haraka
iwezekanavyo.Tunataka kabla
ya amani haijarejea Tanzania
basi tuwapige na hicho
kirusi.Hatutaki kuwapa nafasi
ya kupumua.Namuhitaji huyo
mtu haraka sana.Fanya kila
uwezalo mtu huyo aweze
kupatikana haraka sana”
akasema David
“Sawa David nitajitahidi”
“Ahsante sana Habiba na
pole sana kwa tatizo hili
kubwa.Kuna chochote
tunaweza kusaidia?
“Ahsante
David.Tutawasiliana pale
nitakapokuwa nimempata
huyo mtu” akasema Habiba na
kuzima ile runinga
“Mauaji yanayoendelea
hivi sasa nchini Tanzania bado
hayatoshi na wanataka
kusambaza tena virusi na
kuendelea kuua watu.Yote hii
ni kwa sababu ya kutaka
kuchukua rasilimali ambazo
Mungu amewajalia watu wa
Afrika Mashariki.Lazima
nitafute namna ya kufanya ili
niweze kuzuia mpango huu
usifanikiwe.Ningeweza
kumpigia simu Mathew
Mulumbi lakini sifahamu
mahala alipo hivi sasa.Hata
hivyo lazima nifanye kitu.Huu
lazima uwe ni mwisho wa hiki
kikundi chenye kufanya
maangamizi makubwa
duniani” akawaza Habiba na
kuwasiliana na mtu mmoja
kutoka kundi la IS akampa
maelekezo kama alivyokuwa
ameelekezwa na David na mtu
Yule akamtaka Habiba ampe
muda alishughulikie lile suala
kisha atamjulisha.Alimtajia
kiasi cha fedha ambacho
angetakiwa kukitoa kwa ajili ya
suala lile.Baada ya kulimaliza
hilo suala Habiba akarejea
katika nyumba waliko akina
mama waliokuja kuungana
naye katika msiba.
Saa tatu za usiku
wakawasili Abu Dahir na mke
wake Nawal.Kama ilivyokuwa
kwa Mathew na Najma nao pia
walikuwa
mapumzikoni.Habiba Jawad
aliwapa wanae wote
mapumziko ya miezi
minne.Abu Dahir na Nawal
hawakuweza kuwahi mazishi
ya Najma kutokana na
kutopata taarifa kwa
haraka.Baada ya kuwasili Abu
Dahir alikwenda kuungana na
waombolezaji wengine
waliofika pale nyumbani
kuwafariji.Nawal yeye
alikwenda kuungana na akina
mama waliokuwa wanamfariji
Habiba.
Saa tano za usiku tayari
watu wengi walikwisha
ondoka.Ni watu wachache tu
waliokuwa wamebaki na ndipo
Abu Dahir alipoweza kupata
nafasi ya kuzungumza na
mama yake ili aweze
kumueleza kile kilichotokea
hadi kupelekea Najma kujiua
kwa kujipiga risasi.Habiba
Jawad akawataka Abu Dahir
na Nawal waelekee nyumbani
kwake akawakaribisha katika
sebule yake
“Mama utatusamehe sana
kwa kushindwa kuwahi
mazishi ya Najma.Tuliipata
taarifa kwa kuchelewa na
tulijitahidi sana kwa kila
namna ili tuweze kuwahi leo
lakini ilishindikana ” akasema
Abu Dahir
“Usijali Abu.Nilifahamu
hamtaweza kuwahi mazishi”
akasema Habiba
“Mama nini hasa
kilichotokea? Kwa nini Najma
alijiua?Abu Zalawi yuko
wapi?akauliza Abu Dahir
akionekana kuwa na shauku
sana ya kutaka kufahamu kila
kitu kuhusiana na tukio lile.
“Poleni sana vijana wangu
kwa hiki kilichotokea.Mpaka
sasa bado siamini kama kweli
Najma binti yangu wa pekee
amekwenda na hatutamuona
tena.Najma ameondoka na
afya na uzuri
wake.Imeniumiza sana”
akasema Habiba Jawad
“Nini hasa kimetokea
mama hadi kupelekea Najma
kuchukua maamuzi haya
magumu namna hii? Akauliza
Abu Dahir
“Ni hadithi ndefu Abu
lakini lazima nikiri kwamba
mimi ndiye niliyesababisha
kifo chake”
“Wewe ndiye uliyesabisha
kifo chake? Kivipi mama? Abu
Dahir akauliza
“Sikumuua kwa mkono
wangu lakini kuna maneno
nilimueleza na hayo ndiyo
yaliyopelekea akachukua
maamuzi yale ya kujiua”
“Ulimweleza nini mama?
Akauliza Nawal na Habiba
akamtazama Abu Dahir kisha
akasema
“Nilimueleza ukweli”
“Ukweli? Abu Dahir
akashangaa
“Ndiyo Abu.Dada yako
nilimueleza ukweli”
“Sijakuelewa
mama.Ukweli upi uliomueleza
hadi akaamua kujipiga risasi?
Abu Dahir akauliza
“Kuna mambo mengi
ambayo wewe na ndugu zako
hamkuwa mkiyafahamu hasa
kuhusu mimi na kile
kinachoendelea katika maisha
yangu.Nadhani ni wakati wa
kuweka mambo wazi ili wewe
pia ufahamu” akasema Habiba
na Nawal akasimama
“Nawal unakwenda wapi?
Habiba akauliza
“Ninadhani mazungumzo
haya yanawahusu zaidi ninyi”
akasema Nawal
“Hapana Nawal kaa.Wewe
pia ni mwanafamilia na ni
sehemu ya haya ninayotaka
kuyazungumza.Umefika
wakati wa kila kitu kuwekwa
mahala peupe” akasema
Habiba
“Huyu mama anataka
kufanya nini tena?Mbona
muelekeo wake
siuelewi?akajiuliza Nawal
“Mama kabla hujaendelea
nataka kufahamu yuko wapi
Abu Zalawi? Abu Dahir
akauliza
“Abu Zalawi hayupo na
hajui kama mke wake Najma
amefariki dunia”
“Hajui kuhusu kifo cha
Najma? Akauliza Nawal
“Ndiyo hajui chochote
kuhusu kifo cha Najma”
“Mama nashindwa
kuelewa.Hawa walikwenda
mapumzikoni kama
tulivyofanya sisi.Nini kili…..”
“Niliwarudisha mimi”
akasema Habiba na
kumkatisha Abu Dahir
“Nilimuhitaji Abu Zalawi
hivyo nikawasiliana nao na
kuwataka warudi nyumbani
mara moja.Baada ya kurejea
mimi na Abu Zalawi tulifanya
safari ya kwenda Marekani na
Abu Zalawi alibaki huko”
“Alibaki huko? Nawal
akauliza
“Ndiyo.Alibaki huko na
ninapenda kuwajulisha
kwamba AbuZalawi hatarejea
tena hapa kwetu.Amekwisha
ondoka katika maisha yetu”
“Mama sijakuelewa.Nini
kinaendelea hapa? Mama
naomba tafadhali unieleze kila
kitu.Naona kuna mambo
mengi yamejificha
hapa”Akasema Abu Dahir
“Abu kama unavyofahamu
kwamba baba yako alikuwa
mstari wa mbele sana katika
kupigania haki na aliuawa
akiwa katika mapambano ya
kudai haki za
wapalestina.Baada ya kifo
chake nilivaa viatu vyake na
kuendelea na harakati za kudai
haki.Nimekuwa nikitoa
msaada wa kifedha kwa
vikundi mbali mbali
vinavyoendesha harakati za
kudai haki za wapalestina
kutoka kwa taifa la Israel.Si
vikundi vya kipalestina tu
ambavyo vimekuwa vikipokea
msaada kutoka kwangu katika
kufanikisha harakati mbali
mbali za kudai haki bali
nimekuwa nikifadhili makundi
mengine kama vile IS
kufanikisha mipango yao
mbali mbali.Kundi la IS
linajulikana kama kundi hatari
zaidi la kigaidi kwa sasa
duniani na kitendo cha
kulifadhili kimenifanya
niwindwe na mashirika mbali
mbali ya kijasusi na hasa
Mossad.Pamoja na kuwindwa
huko na Mossad lakini hadi leo
hii hawajawahi
kunikamata.Umeshawahi
kujiuliza swali kwa nini?
Akauliza Habiba na Abu Dahir
akatikisa kichwa kwamba
hajaui.
“Kuna siri imejificha hapa
kwa nini sijawahi kukamatwa
licha ya kutajwa kuwa mfadhili
mkubwa wa makundi ya ugaidi
duniani” Habiba akanyamaza
na kuwatazama Abu Dahir na
Nawal
“Siri ambayo
hamuifahamu ni kwamba
ninafanya ufadhili huu kwa
makundi ya magaidi kwa niaba
ya Marekani”
“Marekani ? Abu Dahir
akashangaa
“Ndiyo Abu.Mimi ni
wakala wao.”
“Marekani wanafadhili
ugaidi? Abu akazidi kushangaa
“Ni vigumu kuamini Abu
lakini huo ndio ukweli”
“Marekani imekuwa
ikiendesha vita dhidi ya ugaidi
duniani na tumekuwa tukiona
namna inavyopata mafanikio
makubwa katika vita dhidi
hiyo.Iweje kwa upande wa pili
wawe na ushirika na magaidi?
Akauliza Abu
“Hiyo ni siri kubwa Abu
Dahir.Ni siri ambayo hata Rais
wa Marekani haifahamu”
akasema Habiba na
kunyamaza kidogo
“Ndani ya shirika la
ujasusi la Marekani CIA kuna
kitengo maalum ambacho
kinashughulika na jambo
hilo.Ni kitengo cha siri sana na
hata waliomo ndani ya CIA
hawakifahamu” Habiba
akanyamza baada ya Nawal
kuonyesha mshangao
“Kitengo hiki kazi yake
kubwa ni kushughulikia
mahusiano na makundi ya
kigaidi kwa maslahi ya
Marekani.Baba yako ndiye
aliyekuwa akitumiwa katika
kufadhili ugaidi na aliuawa
baada ya kwenda kinyume na
matakwa ya Marekani.Baada
ya kuuawa nilivaa viatu vyake
na kuendelea na kile
alichokuwa anakifanya”
“Siamini hayo
unayonieleza mama.Kwa muda
huu wote mmekuwa mkifanya
kazi kwa niaba ya Marekani?
“Ndiyo Abu.Tumekuwa
tukifanya kazi kwa niaba ya
Marekani.Alianza baba yako
na mimi nimefuata na utajiri
huu wote tulionao umetokana
na hicho
tunachokifanya.Wameniwezes
ha utajiri mkubwa niweze
kuutumia kufadhili ugaidi kwa
niaba yao.Hawataki
kujulikana”
“Kwa nini ukakubali mama
kubeba jukumu hili kubwa
mabegani mwako?Kwa nini
ukakubali kuchafua jina lako
kwa kuwa mfadhili wa ugaidi
duniani wakati kumbe
wafadhili wakuu wa ugaidi
wapo? Akauliza Abu Dahir
“Ilikuwa ni lazima nifanye
hivyo Abu.Hii imekuwa ni siri
yangu kubwa sana na
sikupanga kuwaeleza lakini
imebidi mfahamu kila kitu”
akasema Habiba
“Kwa nini umeamua
kutueleza mama? Akauliza
Nawal
“Kwa sababu ni wakati
muafaka kwa ninyi kufahamu
kile kinachoendelea” akajibu
Habiba
“Kama nilivyokueleza Abu
kwamba baba yako ndiye
aliyekuwa wa kwanza kuifanya
kazi hii na mimi niliendelea
pale alipoishia
yeye.Nimeifanya kazi hii kwa
muda mrefu kwa maslahi ya
marekani na sasa umefika
wakati ambao sitaki kuendelea
tena na hiki ninachokifanya
kwani hakipendezi machoni pa
Mungu.Nimekwisha kuwa
mzee sasa na ninahitaji
kujiweka karibu na Mungu
wetu na sitaki tena kuendelea
kukatili roho za watu wasio na
hatia.Katika makubaliano yetu
na kikundi hiki ni kwamba
nitaifanya kazi hii ya kufadhili
ugaidi kwa niaba yao hadi pale
nitakapovuta pumzi yangu ya
mwisho na ndiyo maana
wameniwezesha kuwa na
utajiri mkubwa sana.Kitendo
chochote cha kutaka kujiondoa
katika jambo hili ni
kuhatarisha usalama wangu na
wa familia yangu.Hivi
tuzungumzavyo ninyi wanangu
wote mnafuatiliwa na muda
wowote ambao nikijaribu
kwenda kinyume na matakwa
yao watawaondoa ndiyo
maana nimekuwa kimya
sijawahi kuwaeleza kuhusu
jambo hili.Nataka muwe
salama” akasema Habiba
“Unataka tuwe salama?
Akauliza Abu Dahir kwa ukali
“Abu chunga ulimi wako
unapozungumza nami !
akafoka Habiba akionekana
kutopendezwa na namna
mwanae alivyouliza kwa ukali
“Mama ingekuwa vyema
ungeendelea kubaki na siri hii
na ukafa nayo.Kuamua
kutueleza ukweli ni
kuhatarisha zaidi maisha
yetu.Tazama umemueleza
ukweli Najma na akaamua
kujiua” akasema Abu Dahir
“Abu imenilazimu
niwaeleze ukweli ili hata
ikitokea nikiondoka leo mjue
ni kitu gani kilikuwa
kinaendelea katika maisha
yangu” akasema Habiba na
kunyamaza akamtazama Abu
“Ili niweze kujiondoa
katika jambo hili ilinilazimu
kuja na mpango maalum na
hapo ndipo nilipoamua
kuwaleta hapa Abu Zalawi na
Nawal” akasema Habiba na
kunyamaza.Nawal alionyesha
wasi wasi mwingi
“Abu Dahir,kuna jambo
ambalo hujalifahamu bado”
akasema Habiba
“Mama una siri nyingi
umetuficha.Tafadhali kama
umeamua kueleza ukweli
tueleze kila kitu” akasema Abu
Dahir
“Ni kuhusu Abu Zalawi na
Nawal” akasema habiba
“Mama” akaita Nawal
“Nawal muache mama
aseme anachotaka kukisema”
akasema Abu Dahir
“Nawal usiwe na
hofu.Nataka kila kitu kiwe
wazi leo” akasema Habiba
“Endelea mama.Kuna nini
kuhusiana na hawa watu
wawili? Akauliza Abu Dahir
“Abu Zalawi na Najma
nimewatoa katika lililokuwa
kundi la Ammar Nazari
brigades.Wawili hawa ni
majasusi na walikuwa katika
misheni maalum na siyo
magaidi.Niliamua kuwachukua
na kushirikiana nao kwa ajili
ya kw……….”
“Mama
sijakuelewa.Umesema Nawal
na Abu Zalawi ni majasusi na
si magaidi?Nawal si alikuwa
mke wa Ammar Nazari?
Akauliza Abu Dahir na kabla
Habiba hajajibu Nawal
akasimama
“Ni kweli Abu Dahir hiki
anachokisema mama yako”
Akasema Nawal na kutazama
na Abu
“Siamini masikio yangu !
akasema Abu Dahir
“Mama yako ameamua
kuweka kila kitu wazi hivyo
hakuna haja ya kuficha
chochote.Ni kweli mimi na
Abu Zalawi ni majasusi na
tulikuwa katika kundi la
Ammar Nazari Brigades kwa
misheni maalum.Mimi ni
jasusi toka CIA Marekani na
mwenzangu Abu Zalawi
anatokea Mossad.Jina lake
halisi ni Mathew Mulumbi na
si Abu Zalawi kama
anavyojulikana.Katika kundi la
Ammari Nazari Brigades mimi
nilikuwa na kazi ya kumsaka
gaidi mmoja ambaye ana
undugu na Ammar Nazari
ambaye aliwahi kufanya
mauaji makubwa Marekani na
kukimbia hivyo niliuganishwa
na Ammar na nikawa mke
wake.Abu Zalawi yeye alitokea
Mossad na alikuwa na misheni
maalum aliyotumwa
kuitekeleza ambayo ni kumuua
Habiba Jawad.Mossad
wanafahamu kwamba Habiba
amekuwa akifadhili makundi
mbali mbali ya wanamgambo
wa kipalestina ambao
wamekuwa wakiendesha
mashambulio mbali mbali
ndani ya Israel hivyo
wanamtafuta sana Habiba na
wakamtumia Abu Zalawi ili
kuungana na Ammari Nazari
na kutengeneza njia ya kufika
kwa Habiba Jawad.Baada ya
Ammar Nazari kuuawa na
vikosi vya Israel mimi na Abu
tuliondoka na kuanza harakati
za kumsaka Habiba Jawad
lakini tulipofika hapa misheni
ikabadilika.Ile mipango ya
kumuua Habiba Jawad
ikatoweka na badala yake
tukajikuta tukiungana na
Habiba Jawad katika mipango
yake na kuwa wanafamilia”
akasema Nawal na Abu Dahir
akaonekana kuchanganyikiwa.
“Abu Zahir anachokisema
mama yako ni………..” akasema
Nawal na Abu
akamnyamazisha
“Nyamaza ! akasema Abu
Dahir kwa sauti kali
“Wewe na huyu
mwanamke wote mko
sawa.Wote mama yenu
mmoja.Wote ni mashetani
waongo wakubwa.Nawal
nilikupenda sana na nikawa
tayari kufanya chochote kwa
ajili yako.Kwa nini nawe
ukashiriki uongo huu mkubwa
wa mama? Na wewe mama
kwa nini ukanishawishi
nimuoe Nawal wakati
ukifahamu kwamba ni jasusi?
Kwa nini hukunieleza ukweli?
Akafoka Abu aliyekuwa
amepandwa na hasira
“Nilikuwa na sababu
maalum za kutaka umuoe
Nawal”
“Ulikuwa unachunguza
maisha yetu mimi na Najma
ndiyo maana ukatutaka tuwe
na mahusiano na hawa
majasusi ? Abu akauliza
“Hapana sijawahi
kuwachunguza.Nilitaka
kuwalinda”
“Mama wewe una roho ya
kishetani kabisa ndiyo maana
hujawahi kusikitika hata siku
moja kwa watu wanaouawa na
magaidi ambao
unawafadhili.Najuta kuzaliwa
nawe Habiba ! akasema kwa
ukali Abu Dahir na Nawal
aliyekuwa karibu yake
akamnasa kofi
“Iwe ni mara ya kwanza na
ya mwisho kumtusi mama
yako.Pamoja na yote
anayoyafanya na aliyoyafanya
huyu bado ni mama yako na
ataendelea kuwa mama yako
daima.Huyu ndiye
aliyekubeba tumboni mwake
miezi tisa na akakulea hadi
umefika hapa
ulipofika.Nakuonya tena
ukithubutu kumtusi mama
yako mbele yangu
nitakufundisha adabu.Hapa
unaponiona mimi sina uwezo
wa kuzaa mtoto.Nimekwisha
ondolewa kizazi.Unajua ni
uchungu gani ninaupata kwa
kukosa mtoto?Usirudie tena
kumtusi mama yako ! akasema
Nawal kwa ukali huku
akilengwa na machozi.Abu
Dahir akamtazama Nawal kwa
macho ya mshangao.
“Huna kizazi?! Akauliza
akiwa ameshika shavuni
mahala aliponaswa kofi
“Ndiyo sina kizazi na
siwezi kupata mtoto ! akajibu
Nawal bila hofu
“Nawal toka tumefunga
ndoa tumekuwa katika jitihada
mbali mbali za kutafuta mtoto
na umekuwa unanihakikishia
kwamba tutapata mtoto hivi
karibuni ! Oh Mungu wangu !
akasema Abu kwa masikitiko
“Ulikuwa ni uongo.Sina
uwezo wa kubeba mimba !
akasema Nawal.
Ghafla Abu Dahir akainua
taa ya mezani iliyokuwa katika
meza ndogo pembeni na pale
alipokuwa amekaa na kumpiga
nayo Nawal ikapasuka.Abu
Dahir akachukua birika na
kumrushia Nawal
akalikwepa.Abu alionekana
kama vile amepatwa na kichaa
“Ninyi wanawake leo
mtanitambua mimi ni nani !
akafoka Abu huku akirusha
vitu kumpiga navyo Nawal
“Abu acha ujinga huu
tafadhali ! akafoka Habiba
“Wewe mama ndiye
uliyeyataka haya yote.Una
roho mbaya sana! Akafoka Abu
na kuinua chungu cha maua
kilichokuwa dirishani kwa
lengo la kumpiga nacho mama
yake lakini Nawal alikwisha
isoma dhamira yake akajiinua
pale chini alipokuwa akaruka
na kukipiga teke chugu kile
kikaanguka na
kuvunjika.Nawal ambaye
hasira zilikwisha mpanda
akamrukia Abu mateke mawili
mfululizo yaliyomrusha Abu
hadi ukutani akajigonga kwa
kishindo na kuanguka chini
halafu akamfuata Habiba
“Mama uko
sawa?Hajakuumiza
huyu?akauliza Nawal
“Nimeumia
kidogo.Ahsante kwa kuniokoa”
akasema Habiba na Nawal
akageuka kumtazama Abu
Dahir ambaye alikuwa amelala
pale chini akionekana
kutokuwa na fahamu.Haraka
haraka akamfuata na kujaribu
kumtikisa huku akimuita jina
lake lakini hakuitika.Akageuka
kumtazama Habiba Jawad
ambaye naye alionyesha hofu
baada ya kuiona sura ya
Nawal,akainuka na kumfuata
akamtazama Abu Dahir
ambaye hakuwa na
fahamu.Bila kupoteza muda
Habiba akampigia simu
daktari wake anayeishi
pembeni ya nyumba yake
ambaye alifika mara moja
akampima Abu kisha akasema
“Anatakiwa akimbizwe
hospitali haraka sana !
Habiba akainuka
akachukua simu na kuwapigia
wasaidizi wake ambao walifika
haraka haraka na kumchukua
Abu Dahir wakamuingiza
garini wakamkimbiza
hospitali.Habiba na Nawal nao
wakaingia garini wakaelekea
hospitali.
“Mama ni vipi kama
nimempiga Abu sehemu
mbaya? Akauliza Nawal
akionekana kuwa na hofu
“Usijilaumu
Nawal.Ulifanya ulichopaswa
kukifanya.Kama usingefanya
vile Abu angenipiga na kile
chungu na pengine ningeweza
hata kupoteza maisha.Kwa
sasa tumuombee ili aweze
kuwa salama.Sitaki kupoteza
tena mtoto
mwingine.Nimekwisha poteza
watoto wawili tayari na
nimebaki na huyu mmoja”
akasema Habiba na kufuta
machozi
“Lakini mama kwa nini
uliamua kufanya hivi
ulivyofanya?Kwa nini uliamua
kuwaeleza ukweli
wanao?akauliza Nawal
“Ilikuwa lazima wafahamu
Nawal.Sikutaka kuendelea
kuwaficha kwani endapo
ningefariki dunia bila
kuwaeleza ukweli yawezekana
nao wangeendelea kufanya kile
ambacho mimi na baba yao
tumekuwa tunakifanya.Sitaki
watoto wangu waendelee
kufadhili ugaidi,sitaki
waendelee kumwaga damu za
watu kama nilivyofanya mimi”
akasema Habiba
“Ulifanya kitu kizuri
kuwaeleza ukweli lakini kwa
bahati mbaya mambo
hayakwenda kama ulivyokuwa
umekusudia” akasema
Nawal.Habiba akafuta machozi
na kusema
“Nadhani Mungu
ananiadhibu kwa mambo
niliyoyafanya.Nimefanya
mambo mengi maovu.Damu
nyingi imemwagika kwa
sababu yangu na haya ndiyo
mapigo ninayoyapata.Naomba
Mungu asimchukue Abu Dahir
kwani ni mtoto pekee
niliyebaki naye” akasema
Habiba na kuchukua simu
akampigia mmoja wa
madaktari katika hospitali
alikoelekeza apelekwe Abu
Dahir akamjulisha kuwa
mwanae amepatwa na
matatizo na anapelekwa pale
hospitali akaomba
ashughulikiwe haraka
Abu Dahir alifikishwa
hospitali ambako tayari
wauguzi walikuwa
wamejiandaa
wakimsubiri,akashushwa
haraka haraka katika gari na
kuweka katika kitanda
kikakimbizwa ndani katika
chumba cha wagonjwa
mahututi ambako alianza
kupatiwa matibabu.Dakika
chache baada ya Abu Dahir
kuingizwa katika chumba cha
wagonjwa mahututi,Habiba
Jawad na Nawal
wakawasili.Habiba
alifahamika pale hospitali
akapokewa na kupelekwa
sehemu ya kusubiri madaktari
watakapomaliza
kumuhudumia mgonjwa wake.
Baada ya dakika saba
mlango wa chumba cha
wagonjwa mahututi
ukafunguliwa na daktari
akatoka.Habiba akasimama na
kumfuata daktari akamtaka
waelekee ofisini kwake
“Kijana wangu
anaendeleaje daktari?akauliza
Habiba akionekana kuwa na
hofu
“Mama Habiba
tumejitahidi kadiri ya uwezo
wetu lakini tumeshindwa
kuokoa maisha ya
mwanao.Uchunguzi wa awali
unaonyesha ana jeraha
kichwani.Nini hasa
kilimtokea? Amepata ajali?
Akauliza Daktari na Habiba
Jawad akashindwa
kumjibu.Yeye na Nawal
wakakumbatiana wakilia.
“Ahsante Mungu kwa kila
jambo.Wewe ndiye mwenye
kutoa na kutwaa kwa muda
uutakao.Hatuwezi kupingana
na maamuzi yako japo
tungependa tuendelee kuwa
pamoja na Abu Dahir lakini
nakushukuru kwa muda
ambao umempa hapa
duniani.Naomba utupe nguvu
ya kulihimili jambo hili”
akasema Habiba machozi
yakimwagika
Habiba Jawad na Nawal
wakapelekwa katika chumba
ulikokuwa mwili wa Abu Dahir
“Saa chache zilizopita
tulikuwa wote ndegeni
tukirejea Riyadh kuhudhuria
msiba wa dada yako,sikuhisi
kama ulikuwa unayafuata
mauti yako.Abu Dahir mimi
ndiye nimesababisha kifo
chako nitalia machozi gani kwa
hili nililolifanya? Najua
ulikuwa unanipenda sana
lakini umekufa ukiwa na
hasira nami baada ya
kuufahamu ukweli kuhusu
maisha ya mama yako na
kuhusu mimi.Najuta kwa nini
sikukueleza ukweli kuhusu
mimi kuwa ni jasusi wa
CIA.Najuta kwa nini
sikukueleza ukweli kama sina
uwezo wa kukupatia mtoto
kwani ni jambo hili ndilo
lililokupa hasira
zaidi.Nisamehe Abu Dahir
huko uliko.Nisamehe ! akalia
Nawal akiwa amesimama
pembeni ya mwili wa Abu
Dahir.Wote wawili Habiba na
Nawal machozi yalikuwa
yanawabubujika.Walitumia
dakika kumi ndani ya kile
chumba kisha wakatoka na
kuondoka kurejea nyumbani
“Mama nimemuua mume
wangu.Nimemuua mwanao
pekee aliyesalia” akasema
Nawal wakiwa garini huku
akimwaga machozi.Habiba
akageuza shingo akamtazama
Nawal na kumuinamisha
kifuani kwake akamkumbatia
“Nawal narudia
kukusisitiza kwamba haya yote
yanayotokea ni mipango ya
Mungu na hupaswi kujilaumu
kwa hili lililotokea.Ilikuwa iwe
hivyo.Abu Dahir aliandikiwa
afe kifo cha namna ile hivyo
hakuna namna ambayo
ungeweza kukwepa.Lakini
tambua kwamba haya yote
yanayoendelea hivi sasa ni
matokeo ya maisha niliyoishi
mimi.Ni mapigo yatokanayo
na matendo yangu.Nimetesa
watu wengi sana.Machozi ya
akina mama waliopoteza
watoto wao katika
mashambulio yaliyofanywa na
makundi ya kigaidi ambayo
ninayafadhili hayajaniacha
salama.Machozi ya watoto
ambao wamebaki yatima
baada ya kuwapoteza wazazi
wao katika mashambulo ya
kigaidi niliyoyafadhili haya
ndiyo malipo yake.Nimepoteza
watoto wangu wote niliowazaa
na sasa nimebaki
mwenyewe.Pamoja na mapigo
haya lakini Mungu
hajaninyima kila
kitu.Amewachukua watoto
wangu lakini ameniletea
watoto wengine ambao ni
wewe na Mathew” akasema
Habiba na Nawal akainua
kichwa chake
“Mama umeongea kuhusu
Mathew.Nataka kufahamu
mahala alipo.Sijamuona katika
msiba wa Najma” akauliza
Nawal
“Mathew ameondoka
hatarejea tena kama
nilivyowaambia na hilo ni
moja kati ya mambo
yaliyopelekea Najma
akachukua maamuzi ya kujiua”
akasema Habiba
“Mathew amekwenda
wapi? Amekufa?
“Hapana hajafa.Nawal
tutazungumza baadae lakini
kwa sasa tujielekeze katika
msiba wa Abu na
tutakapomaliza tutazungumza”
akasema Habiba
DAR ES SALAAM –
TANZANIA
Ndege ya jeshi aliyopanda
Mathew iliwasili jijini Dar es
salaam.Kutoka angani ni
sehemu chache tu za jiji la Dar
es salaam ambazo zilionekana
kuwa na umeme.Sehemu
kubwa ya jiji la Dar ilikuwa
gizani kutokana na miundo
mbinu ya umeme kuharibiwa
katika machafuko yaliyokuwa
yanaendelea.
“Nimezoea kuliona jiji la
Dar es salaam kutokea angani
likiwaka taa kila sehemu lakini
leo hii jiji limetanda giza kila
sehemu.Kwa tamaa ya mali
ambazo Mungu ametujalia
ziwepo katika nchi
zetu,mabepari wametufikisha
hapa.Ni mara ya kwanza
Tanzania tumefikishwa hatua
hii ya kuchinjana wenyewe
kwa wenyewe.Ninaapa kwa
gharama zozote zile lazima
kikundi hiki cha hawa watu
waliotufikisha hapa kwa tamaa
za mali yetu nikifutilie mbali
na dunia lazima ifahamu kile
ambacho mataifa makubwa
yanafanya katika nchi
ndogo.Huu ni unyama
uliopitiliza.Ni unyonyaji usio
na mfano.Naamini haya ni
maongozi ya Mungu hadi
akanifikisha katika kundi hili
ambalo limeigeuza nchi yetu
uwanja wa mauaji.Tayari
nimefahamu kuwa ni
Marekani ndio waliotengeneza
machafuko haya kwa manufaa
yao.Hawako peke yao lazima
kuna watu wa hapa nchini au
katika nchi za Afrika mashariki
ambao wanashirikiana nao
katika kuanzisha na kuchochea
vurugu hizi.Hawa ndio
wanaotakiwa kusakwa kwa
haraka sana na kujulikana ni
akina nani na kama
tukifanikiwa kuwapata hawa
basi tutakuwa tunaweza
kusaidia kumaliza vurugu
hizi.Kuna nguvu mbili hapa
ambazo zimeifikisha Tanzania
hapa tulipofika.Ipo nguvu ya
ndani na nguvu ya nje.Inabidi
kuanza na nguvu ya ndani
kisha nitaendelea na wale wa
nje.Naapa hakuna aliyeifikisha
Tanzania hapa atabaki
salama”akawaza Mathew na
kumkumbuka Ruby
“Nilijaribu kumpigia simu
Ruby lakini
hakupatikana.Nina wasi wasi
sana na usalama wake.Gosu
Gosu naye sijui
anaendeleaje.Nawahitaji sana
hawa watu kama watakuwa
wazima katika kuhakikisha
tunaiokoa nchi yetu kutoka
katika
machafuko.Ninachoelewa
hawa jamaa kwa vile
wamekwisha ingia Afrika
Mashariki lazima wataotesha
mizizi na kuhakikisha kwamba
wanaendelea kuchota utajiri
wetu.Naomba niwakute wote
wako salama” akawaza
Mathew na kutaarifiwa
kwamba ndege inakaribia
kutua katika uwanja wa ndege
wa Julius Nyerere ambao toka
vurugu zilipoanza ulikuwa
umefungwa na ukilindwa na
wanajeshi .
Ndege ile ya jeshi la
Marekani ikiwa na vifaa mbali
mbali vya wanajeshi wa
Marekani waliokuwa nchini
Tanzania ikatua salama.Mizigo
ikapakuliwa na kuingizwa
katika magari kisha wanajeshi
waliokuja na ndege ile
wakaingia katika magari
maalum ya jeshi la Marekani
na msafara ukaondoka
kuelekea katika kambi yao
Mathew Mulumbi akiwa ni
mmoja wao
“Hawa jamaa hawajui
kama hapa nimefika
nyumbani.Watakapogundua
kwamba mimi ni mtanzania
tayari watakuwa wamechelewa
sana lakini kwa sasa ngoja
niendelee kujifanya mimi ni
mgeni wa hapa Tanzania ili
niendelee kuusoma mtandao
wao” akawaza Mathew na
kuona namna alivyokuwa
anachungwa.Ndani ya gari
alilokuwa amepanda kulikuwa
na wanajeshi wanne wenye
silaha na gari lile liliwekwa
kati kati ya msafara.
“Nadhani wameelekezwa
wanichunge ndiyo maana
wameniweka
katikati.Hawapaswi kuwa na
hofu nitafanya walivyonieleza
lakini watajuta sana na
kumlaumu Habiba Jawad kwa
kuwakutanisha na mimi.Safari
hii ninataka nifanye kitu
ambacho kitakuwa cha
kihistoria.Tumeonewa vya
kutosha na sasa ni wakati wa
kuwaonyesha haya mataifa
makubwa kwamba hata sisi
tunao uwezo na tumechoshwa
na mambo wanayotufanyia”
akawaza Mathew akiyaelekeza
macho yake nje
“Dar es salaam haikuwa
hivi.Hili ni jiji lililokuwa
linakesha lakini muda huu
barabara tupu hakuna watu
mitaani.Sipati picha namna
maisha yalivyo magumu hivi
sasa.Maduka
yamefungwa,upatikanaji wa
chakula na mahitaji muhimu
imekuwa ni shida lakini baadhi
ya watu wachache wao
wanaishi maisha mazuri na
kupata kila wanachokihitaji
wakisahau kwamba kuna
mamilioni ya watu
wanaoteseka huku Tanzania
na Afrika mashariki kwa
sababu yao.Tunatakiwa
kupambana kuhakikisha
tunairejesha nchi yetu
ilivyokuwa na ili kumaliza
vurugu hizi ni lazima
kuuchimbua mzizi wenyewe
ambao ni kikundi kile kidogo
ndani ya CIA” akawaza
Mathew huku wakiendelea
kukata mitaa ya jiji la Dar es
salaam ambayo kwa usiku huu
ilikuwa kimya.Mioto ya
matairi na moshi mzito
vilionekana katika baadhi ya
barabara na hata majengo
yanayoungua moto pia
yalikuwepo.Katika baadhi ya
barabara walikuta zimefungwa
kwa mawe makubwa
“Hali ilivyo Dar es salaam
utadhani kuna filamu
inatengenezwa kumbe ni hali
halisi .Inasikitisha sana !
Narudia tena kuahidi kwamba
wale wote waliotufikisha hapa
hakuna atakayebaki
salama.Tanzania hatukupaswa
kufikishwa hapa.Lakini hili ni
funzo kwa watanzania ili wawe
macho kulinda amani
yao.Wamekuwa wakihubiriwa
kwa miaka mingi kwamba siku
amani hii ikipotea
watajuta.Wamejaribu
kuchezea amani na wameona
madhara yake.Hakuna sehemu
ya kukimbilia imelazimu
wayakimbie makazi yao na
kujificha katika makambi.Kwa
haya wanayokutana nayo
naamini hata akija tena mtu
mwingine siku nyingine
kutaka kuwarubuni kuchezea
amani yao hawatajaribu tena”
Mathew akatolewa mawazoni
baada ya msafara wao
kukutana na kundi kubwa la
vijana waliokuwa wamebeba
mienge na silaha huku
wakiimba.Ikalazimu wanajeshi
wa Marekani kutumia risasi za
moto kuwatawanya kwani
baadhi yao walikuwa na silaha
na walianza kushambulia
magari katika ule
msafara.Baada ya kundi lile la
vijana kutawanyika magari
yakaongeza mwendo na moja
kwa moja wakaelekea katika
uwanja wa uhuru ambako
ndiko kulikuwa na kambi
kubwa ya wanajeshi wa
Marekani na vifaa vyao vyote
vilikuwa vinahifadhiwa
huko.Kambi nyingine ilikuwa
ufukweni mwa bahari ya
Hindi.
Mathew alishushwa garini
na kukabidhiwa kwa mmoja
wa viongozi wa kambi ile
ambaye alimpeleka hadi katika
hema.
“Karibu Tanzania.Jina
lako nani? Akauliza Yule jamaa
“Abu Zalawi” akajibu
Mathew kikakamavu
“Abu Zalawi nimeelekezwa
na viongozi wangu kwamba
nikupokee na kisha
nitakukabidhi kwa mtu
ambaye atakuja hapa
kukuchukua.Umewahi kufika
Tanzania kabla? Akauliza
“Hapana sijawahi” akajibu
Mathew
“Hali ni mbaya sana hasa
hapa Dar es salaam na jiji la
Tanga pia.Nadhani umejionea
hali halisi huko mitaani wakati
mkija hapa”
“Ndiyo mkuu.Tumekutana
na kundi kubwa la vijana
wakiwa na silaha na
kushambulia msafara wetu”
“Basi hiyo ndiyo hali
tunayokutana nayo kila siku
katika kujaribu kurejesha hali
ya amani tukishirikiana na
vikosi vya ulinzi vya Tanzania”
“Endelea kupumzika na
atakapofika mwenyeji wako
nitakufahamisha” akasema
Yule mwanajeshi na kutoka nje
ya lile hema akamuacha
Mathew peke yake.
“Naamini huyo mtu
anayekuja kunichukua ni
mmoja kati ya watu wa IS na
atakuwa anatumiwa na CIA
katika kuratibu na kuchochea
hizi vurugu
zinazoendelea.Imekuwa vyema
wamenielekeza sehemu husika
kwani huyo jamaa ndiye wa
kuanza naye” akawaza Mathew