Riwaya: Scolastica Temu

Riwaya: Scolastica Temu

SEHEMU YA 23

TULIPOKOMEA....


Kisha alinyanyuka na kuelekea huko maliwatoni. Akakumbuka kuwa wakati Kisengo akipelekwa kuoneshawa, yeye alibaki, hivyo hakupajua. Akaamua kwenda mapokezi haraka kumwona yule kijana. Alimkuta akiendelea kuikodolea macho ile tamthiliya kwenye runinga. Akamuuliza na akaelekezwa. Muda mfupi baadaye alikuwa akitoka huko maliwatoni huku akiwa amenawa mikono vizuri kwa sabuni. Na sasa alijiamini kuwa yuko salama zaidi.
Alipokuwa akirudi chumbani, alikutana na Kisengo naye akiingia.

***ENDELEA***


“Nimepata,” Kisengo alisema huku akimwangalia Scolastica sawia usoni.
Aliyetangulia kuingia ni Scolastica, naye Kisengo alipoingia, kama awali aliufunga mlango kwa funguo. Akamfuata Scolastica kitandani ambako kile kijimeza chenye bia nacho kilikuwa kimesogezwa zaidi hapo kitandani. Akajikalisha kwa madaha huku akimtazama Scolastica na kuachia tabasamu la kilevi, mkono wa kushoto ukimpapasa shingo taratibu na wakati mwingine ukiteleza kwenye zile nywele zilizomwagika mgongoni.

Pale alipoketi alikuwa akitazamana na chupa zake mbili kubwa za bia na moja ilikuwa mbele zaidi, ikiwa imewekwa hivyo na Scolastica. Akamkabidhi Scolastica ile vocha aliyomwagiza.
“Nakupenda kwa kunijali,” Scolastica alimwambia huku akiliachia lile tabasamu lake la kinafiki lakini lililonekana kama tabasamu halisi machoni mwa yeyote asiyemjua kwa kina.

“Usijali Flora, mi’ ninajisikia kukupenda zaidi,” Kisengo
alibwabwaja kwa sauti yenye kitetemeshi cha mbali huku akiendelea kumpapasa mgongoni na sasa wakati mwingine akihamia kwenye mapaja yale makubwa yaliyotanuka ndani ya gauni lake lililomshika maungoni.
“Kipi kinakufanya ujisikie kunipenda wakati umeniona tu leo? Kama si uongo ni nini? Kama huo si umalaya ni nini?” tabasamu la Scolastica liliendelea kuchanua kwa namna ya kirafiki zaidi. Alionesha kuwa hata hayo maswali yake ni masihara tu.

Sasa naye akionesha kuwa na ushirikiano, aliutumia mkono wake wa kulia kutua katika maungio ya miguu ya Kisengo na kupapasa taratibu, akitomasa na kuminyaminya kwa namna ambayo ilimchanganya Kisengo na kumtia msisimko mkali. Alimwona anavyotaabika, yeye akaendelea kumfanyia vituko hivyo kisha ghafla akaacha. Akaishika vocha, akaikwangua, kisha akaziingiza namba.

Kisengo alishusha pumzi ndefu baada ya ule mkono wa Scolastica kuahirisha kufanya kile ulichokuwa ukikifanya. Macho yake yaliyokolea ulevi wa ashiki na ulevi wa pombe, yakawa yametua usoni kwa Scolastica kwa namna ya kuzidiwa na hawaa, hanjam na uchu usiokadirika. Ni kama alikuwa akitaka kutamka neno asiweze.
Kwa mbali Scolastica alijisikia kucheka lakini hakufanya hivyo, badala yake alitwaa chupa yake ya bia na kuipeleka kinywani. Alipokunywa kidogo na kuirudisha mezani, akamgeukia Kisengo na kumwambia, “Tumalize kwanza bia zetu, tukisogeze kimeza hiki mbali ndipo tuanze mambo yetu.” Tabasamu la kibwege likamtoka Kisengo. Kama aliyekurupushwa, akaitwaa ile chupa iliyokuwa mbele yake, akagugumia funda zito. Wakati funda hilo likishuka kooni, alisimama na kuanza kuchojoa nguo. Alianza na shati. Alipomaliza, aliangaza huku na kule, labda akitafuta pa kulitundika shati hilo. Hakupaona. Akaamua kuliweka kwenye kingo ya kitanda upande wa kichwa.

Akaitwaa tena chupa na kushusha funda lingine zito. Akakunja uso kidogo, akaukunjua lakini tena akaukunja. Akafumba macho na kuyafumbua. Akaonekana kujishangaa. Wakati alipokwishafungua kifungo cha suruali na zipu yake, akaishusha suruali, hapo akayumba na kurudi nyuma hatua mbili. Hata hivyo, akastahimili na kusimama vizuri. Lakini alipoinama ili aitoe suruali nzima mwilini, hakuweza, Alikwenda mbele na kuiangukia meza akionesha dhahiri kutokuwa na uwezo wa kujizuia. Chupa zilizokuwa mezani zikaanguka kitandani, bia zikilimwagikia godoro!

Scolastica alishaiona picha nzima tangu mwanzo, hivyo alikuwa ameshajitoa kitandani na kusimama kando akishuhudia. ‘Ungangari’ wa Kisengo uliendelea kuwa juu. Pamoja na kuiangukia meza ya vinywaji, hata hivyo aliamini kuwa ni ajali tu, hivyo, akajitahidi kunyanyuka tena na akafanikiwa.

Hata hivyo, hakujua kuwa bado hajawa timamu. Alijikakamua na kusimama lakini muda huohuo, alianza kurudi kinyumenyume. Hatua tatu tu, akaenda chini mzima-mzima, bila hata kuonesha dalili yoyote ya kujitetea. Alianguka kama furushi! Akauma meno kwa hasira. Akajaribu kutoa macho kwa nguvu labda ili aone vizuri!
Scolastica akamsogelea na kumuinamia huku akiendelea kuchanua lile tabasamu lake maridhawa. Kisengo akaachia kinywa wazi, akimtazama Scolastica kama asiyeyaamini macho yake. Scolastica akamuinamia zaidi na kumpapasa kidevuni kwa dhihaka, kisha kwa mnong’ono akamuuliza, “Unaikumbuka siku ile kule Komakoma uliponibaka wewe na Kibutu na Machemba?”

Uwezo wa kusikia bado ulikuwa kichwani mwa Kisengo. Kwa swali hili alimsikia vizuri na alimwelewa. Kwa jumla, ingawa nguvu katika viungo vyake ilikuwa ikmtoka kwa kasi, lakini bado alikuwa na uwezo wa kuona na kusikia huenda hata kutambua hili na lile kwa kiasi fulani.
Aliufungua mdoma na kujaribu kutamka, “Wewee…we…unasema nini…unase…” hakuweza kumalizia, mdoma ukarudi kuwa mzito.

“Umenisikia na kunielewa?” Scolastica alimuuliza kwa sauti yake ileile kama akinong’ona. “Mimi siyo Flora, ni Scolastica. Sasa umenikumbuka? Unaikumbuka vizuri ile siku mliponiteka na kuniingiza kwwenye gari pale Kinondoni kwa Manyanya na kunipeleka Komakoma? Unakumbuka mlivyonifanyia ukatili kwa kunibaka kisha kunilizamisha nizivunje laini zangu za simu?”
Kisengo aliendelea kumkodolea macho Scolastica, hali yake ikiwa vilevile, mdomo mzito, japo alimsikia kila alichokisema!

“Ningekuacha upumzike hadi kesho mchana, uamke na kwenda
zako,” Scolastica aliendelea kumwambia huku sasa akimtazama kwa macho makali bila hata chembe ya tabasamu. Sauti yake hiyo ya chini, sasa ilikuwa nzito na iliyoashiria jambo lingine tofauti kabisa na usalama. “Lakini dhamira itanisuta. Huenda malaika wangu pia akanishangaa. Na hata wewe hutanisamehe nikikuacha hai kenge mkubwa! Unapaswa kumfuata Kibutu!”

Kisengo alivuta pumzi ndefu na macho yakaanza kumlegea. Scolastica Temu akaufuata mkoba wake na kuitoa chupa ya PAK. Hakutaka kuendelea kupoteza muda. Mara baada ya kujifunga kitambaa vizuri eneo la pua na mdomo, kwa jumla uso mzima isipokuwa macho, akaifungua chupa hiyo na kumsogelea Kisengo. Alifanya kama ilivyompasa; wakati Kisengo akivuta pumzi ndefu mara mbili, chupa hiyo ilikuwa jirani sana na pua yake.
Ilitosha!

Alikufa macho yakiwa yanakodoa, kinywa wazi!
Sasa Scolastica aliamua kuangalia namna ya kuwa na hakika ya kupata mawasiliano na Machemba. Alijua kuwa kwa kitendo kile cha kumbaka siku ile, wakishirikiana bila ya soni, kwa vyovyote ni marafiki wakubwa, ambao kwa pia huenda kila mmoja ana namba ya simu ya mwingine.

Akaifuata suruali na kuipekua. Akakuta kuna simu mbili; moja kubwa nyingine ndogo. Akaanza na ile ndogo ambayo alihisikuwa ndiyo itakayokuwa inatumika zaidi kwa kuongea na watu. Hakupata shida kubonyeza hapa na pale na kuanza kuona orodha ya majina yaliyosajiliwa na Kisengo. Aliliona jina la Machemba mapema zaidi.
Akaenda kwenye eneo la ujumbe mbalimbali. Humo pia akakuta kuna ujumbe wa mwanamke mmoja ambaye alikuwa akituma maneno ya kimahaba yaliyokosa tafsida. Upande wa pili kulikuwa na ujumbe mwingine uliokuwa ukitumwa na Machemba kwenda kwa mwanamke huyo ambaye alisajiliwa kwa jina la Mwatum, naye akitumia maneno hayohayo makali kama vile wako chumbani wakistarehe.

Aliendelea kupekua na hatimaye akafarijika alipopata ujumbe uliooneshwa kuwa ni Kisengo kautuma kwa Machemba. ‘Inakuwaje?’ Ujumbe huo ulioneshwa kuwa umetumwa siku hii saa saba mchana. Akarudi kule ‘inbox’ na kuchunguza ujumbe ulioingia japo mwingi ulikuwa ni wa yule mwanamke, Mwatum. Akauona ujumbe kutoka wa Machemba uliosomeka, ‘Kila kitu tayari. Njoo kesho Maranatha Grocery saa 11 jioni.’
Scolastica akatikisa kichwa juu, chini huku akiiweka ile simu kubwa ya Kisengo kule mfukoni alikoitoa, na hii ndogo akaizima, akaipachika ndani ya mkoba wake.

Dakika tano baadaye alikuwa akiufungua mlango na alipotokeza koridoni, aliufunga kwa funguo. Hakuwa tayari kuziacha funguo hizo mapokezi, alizipachika mkobani mwake kisha akavuta hatu taratibu akielekea mapokezi.

ITAENDELEA KESHO

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 24

TULIPOKOMEA....


SCOLASTICA akatikisa kichwa juu, chini huku akiiweka ile simu kubwa ya Kisengo kule mfukoni alikoitoa, na hii ndogo akaizima, akaipachika ndani ya mkoba wake. Dakika tano baadaye alikuwa akiufungua mlango na alipotokeza koridoni, aliufunga kwa funguo. Hakuwa tayari kuziacha funguo hizo mapokezi, alizipachika mkobani mwake kisha akavuta hatu taratibu akielekea mapokezi.

Alimkuta kijana wa mapokezi akiwa ameegemea kiti akisinzia. Akashtuka aliposikia viatu alivyovaa Scolastica vikialika wakati akimsogelea. Akafikicha macho na kumtazama kwa mshangao wa mbali. “Anko mi’ natoka,” Scolastica alimwambia huku akitembea taratibu akiufuata mlango mkubwa lakini wakitazamana. Kijana huyo alitaka kuhoji lakini akasita. Aliamini kuwa ni umbeya kuanza kuhoji kuhusu kuondoka kwake. Mara nyingi wateja wanaokuja hapo hasa wa jinsi tofauti, wanapokamilisha lililowapeleka, huwa mwanamke au mwanamume anakuwa wa kwanza kuondoka. Mwingine hutoka baada ya dakika tano au kumi. Hata jinsi wanavyoingia huwa ni kwa awamu. Huyu anatangulia, yule anafuatia baada ya dakika kadhaa.

Ndiyo, hakuhoji, lakini alimtazama kwa macho yenye maswali mengi yaliyokosa majibu. Alijiuliza amepata kumwona wapi mwanamke huyu mzuri? Wapi, lini na anaitwa nani? Hakupata majibu. Wakati kijana huyo akiihangaisha akili kwa kujiuliza maswali hayo, naye Scolastica kwa sekunde hizo walizokutanisha macho tayari alijiwa na picha ya mtu ambaye si mgeni macho mwake. Haikuwa sura ngeni, lakini aliiona wapi? Lini? Ni hayo yaliyomwacha njiapanda. La mwisho lililomjia akilini ni kwamba, huenda kamfananisha tu na kijana yeyote ambaye labda amewahi kumwona mitaani siku za kisogoni. Akaacha kumfikria. Akausukuma mlango na kutoka taratibu.

Upande wwa pili wa barabara, akaiona ile baa ambayo ni kama haikuwa ya kufungwa muda huo. Wateja walikuwa wengi, muziki mkubwa ukirindima katika spika. Pia kulikuwa na pikipiki na bajaji maalum kwa wateja. Hakutaka kulisogelea eneo hilo, akijali hadhari aliyokwishajiwekea, hasa kutoonwa na wafanyakazi wenzake. Aliwajua vijana wawili waliokuwa ni wafanyakazi wenzake ambao waliishi Mwananyamala ‘A.’ Wote walikuwa ni watu wa bia. Na kwa kuwa hiyo baa ilionekana kama ndiyo kwanza ‘imetoka jikoni,’ alihisi na wao wanaweza kuwa hapo.

Alichofanya ni kuondoka taratibu, akifuata barabara kama anayekwenda Mwananyamala. Moyoni aliomba ije pikipiki yoyote, aliache eneo hilo. Na ilikuwa kama alivyoomba. Dakika kama tatu tu akiwa barabarani, akaiona pikipiki ikimsogelea. Kwanza akashtuka, akihofia isije kuwa amefuatwa na yule kijana wa mapokezi, baada ya kubaini kuwa kuna sintofahamu kule chumbani.

“Shangazi, unakwenda?” mwenye pikipiki alimuuliza.
Scolastica akamfuata haraka na kupanda. “Nipeleke hospitali,” alimwambia.
Hawakufika hospitali, Scolastica aliamua kushukia Mwananyamala ‘A.’ Kisha akapanda bajaji ya kumrudisha Kinondoni. Alipofika niiapanda ya barabara hiyo ya Mwinjuma na Rashid Kawawa, akamwamuru dereva amwache kituo cha daladala cha kwenda Magomeni.

Alipoteremka hapo akaifuata pikipiki nyingine kati ya nyingi zilizokuwa eneo hilo. Akapanda moja iliyokwenda kumwacha kituo ch daladala na Mabasi Yaendayo Haraka cha Morocco. Alipoachana na pikipiki hiyo na kuhakikisha kuwa imeshaondoka kurudi walikotoka, taratibu naye akaanza kurudi nyuma kwa mwendo wa asteaste akikiacha kituo hicho. Hatimaye akaufikia Mtaa wa Kariuki.

Muda huo tena ikamjia kichwani sura ya yule kijana wa mapokezi kule gesti. Bado kulikuwa na kitu kinamlazimisha aamini kuwa hajamfananisha bali aliwahi kumwona mahali au waliwahi kuonana mahali fulani kabla ya usiku huu. Hadi analisogelea geti la nyumbani kwake, saa sita kasoro dakika tano, bado hakuwa na ufumbuzi wa alichokiwaza.
*****
KWAMBA, ndani ya Chumba Na. 7, Madina Guest House, kuna maiti ya mtu asiyejulikana, lilikuwa ni jambo lililobainika ilipotimu saa tano adhuhuri. Samwel, ndiye aliyekuwa mhudumu wa mapokezi wa gesti hiyo, ambaye alitoa chumba hicho kwa wateja wawili usiku uliopita kati ya saa tano na saa sita. Alijua kuwa mteja mmoja, kati yao, aliondoka usiku uleule, lakini wa pili alibaki.

Utaratibu wa gesti hiyo, kama zilivyo nyingine nyingi, huduma kwa mteja hufikia kikomo saa nne asubuhi siku ya pili. Hapo mteja huenda ataondoka au ataongeza mkataba.
Saa nne ilipofika, Samwel alivuta subira.
Nne u nusu. Tano kasorobo!
Wahudumu wa usafi walikwishaanza majukumu yao tangu mapema, hasa kwa vile vyumba ambavyo wapangaji waliondoka mapema zaidi. Samwel akaamua kwenda kumgongea mlango huyo mteja aliyebaki. Aligonga mara mbili, kistaarabu.
Kimya.
Mara ya tatu aliongeza nguvu kidogo.
Kimya.
Akashangaa na sasa akaamua kugonga kwa nguvu zaidi, bila kujali kama atakuwa amembughudhi. Hata hivyo, bado haikusaidia. Ndani ya chumba hicho kulikuwa kimya kabisa. Wahudumu wawili waliosikia akigonga, nao wakasoge a na kumuuliza kulikoni.
“Kalewa sana, nini?” mhudumu wa kike aliuliza huku akimtazama Samwel.
“Hata najua?” Samwel alijibu kwa swali huku akiyainua mabega na kuyashusha, akitawanya mikono kuonesha msisitizo. “Demu wake kaondoka usiku uleule hata hakuchukua nusu saa. Sasa huyu sijui kaona kafika kwake?”
Akaja kijana mwingine. Yeye akagonga kwa nguvu zaidi ya Samwel, lakini hakukuwa na majibu! Huyu akaamua kutumia akili ya pili. Akainama na kuchungulia kwenye kitasa. Mara akashtuka na kunyanyuka! Akawatazama wenzake kwa macho yenye taharuki!
“Vipi?” Samwel akamuuliza.
“Hebu chungulia!” aliambiwa.

Samwel naye akainama na kuchungulia kwenye kitasa. Ni hapo alipoushuhudia mwili wa mtu ukiwa sakafuni chali, macho yamekodoa na mdomo ukiwa wazi. Chupa za bia zilikuwa zimetawanyika kitandani na shka ile nyeupe ikiwa imeenea doa kubwa la pombe hizo.
Samwel na huyu kijana mwingine walitazamana kwa wasiwasi. Kila mmoja aliamini kuwa kuna jambo zaidi ya jambo humo chumbani. Alichofanya Samwel ni kukimbilia mapokezi ambako alichukua ufunguo wa akiba na kurudi kufungua mlango huo!

Walipoingia na kumtazama kwa makini Kisengo aliyekuwa sakafuni, taswira iliyowajia si kwamba mtu huyo kazirai bali kafa! Haukuwa mwonekano wa mtu ambaye bado yu hai. Sasa wakaipeleka taarifa kwa meneja wa gesti hiyo. Robo saa baadaye taarifa zikawa zimeshafikishwa polisi. Askari wakaja.
Pamoja na vipimo hivi na vile, uchunguzi huu na ule ukifanywa, maswali haya na yale yakiulizwa kwa wafanyakazi hao, hatimaye, Samwel na wafanyakazi wale wawili walichukuliwa. Mwili wa Kisengo ulipelekwa hospitali kwa uchunguzi wa daktari.

Kule kituo cha polisi, baada ya takriban saa nzima, hatimaye wale wafanyakazi wawili wa usafi waliachiwa kwa kuonekana hawana chochote cha ziada cha kuwafanya wakae pale. Aliyebaki ni mhudumu wa mapokezi, Samwel.
Aliketi kwenye kiti kilichokuwa ndani ya ofisi maalum, kulikokuwa na meza moja na viti viwili. Kiti kimoja alikaa Inspekta Materu na cha pili kilichokuwa kikimwelekea ndiko alikoketi Samwel.

Kwa muda wa dakika mbili hivi, askari huyo ambaye hakuwa amevaa sare za kiaskari, alikuwa akiandikaandika kwenye leja kubwa, huku kila baada ya muda mfupi akinywa funda la maji baridi yaliyokuwa chupani.
Alipoyainua macho, alimtazama Samwel kwa makini, kama anayesoma kitu fulani usoni pake. Kisha akamuuliza, “Wewe ndiye uliyekuwa reception wakati marehemu akiingia?”
“Ndiyo, afande,” Samwel alijibu haraka kwa sauti ya kutojiamini.
“Jina lako?”
“Samwel.”
“Jina la baba’ako?”
“John.”
“Kwa hiyo unaitwa Samwel John, sio?”
“Ndiyo, afande.”
Inspekta Materu alimtazama kwa macho makali kama asomaye kitu fulani usoni pake. Kisha: “Unaingia na kutoka kazini muda gani?”
“Naingia saa nne asubuhi na kutoka siku ya pili saa nne au tano asubuhi anapokuja mwenzangu kunipokea.”
“Wakati marehemu alipoingia wewe ulikuwa kazini?” alitupa swali hilo huku akizidi kumtazama Samwel kama asiyemwamini.
“Nilikuwapo, afande.”
“Hapo kwenye gesti yenu kuna eneo la mapokezi. Wewe ulikuwa kwenye eneo lako la kazi au ulikuwa nje ya eneo hilo?”
“Nilikuwa palepale kwenye kitengo changu.”
Kwa mara nyingine baada ya kuandika-andika, Inspekta Materu akaitwaa chupa ya maji na kunywa funda moja kubwa. Kisha akamrudia Samwel. “Ok, sasa nieleze kila kitu. Hatua kwa hatua, kuanzia jana mteja huyo alipoingia mpaka leo ulipogundua kuwa kuna mteja kafia chumbani. Ukijitia kuyumbisha ukweli, nakusweka ndani na kukusahau wiki!”
Zikafuata dakika chache ambazo Samwel alizitumia kwa kutoa maelezo ya tangu Kisengo na Scolastica walivyoingia mpaka asubuhi ya siku hii alipoona Kisengo hatoki na kuamua kwenda kumgongea. Hata hivyo, katika maelezo yake hakuwa na kumbukumbu sahihi ya muda ambao wateja wake walikuwa chumbani kabla ya mmoja kuondoka.
“Samwel!” Inspekta alimwita kwa ukali.
“Naam, afande!”
“Niliiona saa ya ukutani pale ofisini kwako. Unataka kun’ambia ile saa ni mbovu?”
"Hapana, afande. Ni nzima. Haijamaliza hata wiki tangu inunuliwe.”
“Na wewe hapo mkononi nakuona una saa. Isitoshe, una simu ambayo nayo ina saa. Vyote hivyo ni vizima au ni maboya tu?”
“Zote ni nzima, afande,” Samwel alijibu huku akiitazama simu yake aliyoishika mkono wa kulia na saa aliyovaa mkono wa kushoto.”
“Kwa hiyo unataka kun’ambia hujui kusoma saa, si nd’o maana’ake?”
“Hapana, afande.”
“Ila?”
Kimya.
“Ok, kuanzia sasa zungumza kitu kinachoeleweka, la sivyo, kesho utasimama kizimbani, kisha Keko au Segerea rumande. Utakavyokaribishwa huko, we' mwenyewe utaomba ardhi ipasuke. Si ajabu utakapopelekwa tena mahakamani kwa kesi yako tayari utakuwa na mimba kama si mtoto.”

***ITAENDELEA


Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 25



TULIPOKOMEA....
Kimya.
“Ok, kuanzia sasa zungumza kitu kinachoeleweka, la sivyo, kesho utasimama kizimbani, kisha Keko au Segerea rumande. Utakavyokaribishwa huko, we mwenyewe utaomba ardhi ipasuke. Si ajabu utakapopelekwa tena mahakamani kwa kesi yako tayari utakuwa na mimba kama si mtoto.”
Maneno hayo yalimtia uchungu Samwel, lakini akakumbuka kuwa huyo anayemwambia hivyo ni askari ambaye kikohozi chake tu, kinatosha kumfikisha mtu mahabusu na kusahauliwa kwa muda. Akajihadharisha kuwa alipaswa kuuchunga ulimi wake na kufuata kila atakaloamriwa.
“N’ambie muda aliotoka huyo mwanamke,” Inspekta Materu alimzindua.
“Kwa kweli afande, ilikuwa inaelekea kwenye saa sita hivi,” Samwel alijibu.
“Hakuna kingine ulichosahau au kuficha?”
“Hakuna afande. Na wala siioni sababu ya kukuficha,” sasa Samwel alijibu kwa kujiamini.
“Kabla ya jana hakuna siku nyingine ambayo marehemu na huyo mwanamke walikuja katika gesti yenu?”
“Marehemu alikuwa akifika mara kwa mara lakini akiwa na wanawake tofauti.”
“Hajawahi kuja na huyu aliyekuwa naye jana?”
“Hapana, afande,” Samwel alijibu. “Huyu nilikuwa sijawahi kumwona pale. Labda kama alikuja siku ambazo mimi nilikuwa off.”
Inspekta Materu alikitwaa kitabu cha wageni wa Madina Guest House, akafunua kurasa kadhaa kabla hajakwamia katika ukurasa aliouhitaji. Kisha akamtazama tena Samwel usoni na kumuuliza, “Hii si ndiyo leja yenu maalum kwa ajili ya wageni?”
“Ndiyo, afande.”
“Mbona katika kumbukumbu zenu hakuna panapoonyesha kuwa kuna wageni walioingia jana usiku?”
Samwel alikumbwa na kigugumizi cha ghafla. Ni kweli hakuwa ameyaandika majina ya Scolastica na Kisengo katika kitabu hicho, na alifanya hivyo ili ‘azitafune’ fedha alizopewa na Kisengo.
“Nakuuliza wewe,” Inspekta Materu alimshtua. “Kama hao watu waliingia usiku katika huo muda unaodai wewe, mbona kwenye hii rejista hakuna majina yao?”
“Nadhani nilipitiwa, afande,” sauti ya Samwel ilikuwa na kitetetmeshi cha mbali.
“Hukupitiwa,” Materu alimpinga. “Sema kweli tu kuwa ulitaka kula hela uliyolipwa. Kwani unadhani hatujui mnavyowaibia waajiri wenu? Lakini hayanihusu hayo. N’nachotaka uniambie kingine ni je, yule mwanamke hukuwahi kumwoina siku yoyote au mahali popote kabla ya jana?”
“Yaani zaidi ya pale gesti?”
“Nd’o maana’ake.”
Samwel alikunja uso na kuonesha kufikiri. Kisha kwa kusitasita akasema, “Kwa kweli si…sina uhakika kama nilisha…”
“Samwel!” Inspekta Materu aligonga meza kwa nguvu. “U’shawahi kulala gerezani walao kwa siku moja tu?”
“Bado, afande.”
“Na una hamu ya kufika huko?”
“Hapana….hapana afande!”
“Ok, nasema kwa mara ya mwisho; zungumza kitu kinachoeleweka! Vinginevyo…”
Ukimya ukapita kwa sekunde chache. Kisha Materu akaibuka, “Nakusubiri wewe, ujue!”
Akionekana sasa kuwa na uhakika na anachokisema, Samwel akasema, “Kwa kweli afande, yule dada sijawahi kumwona sehemu nyingine yoyote ila tu namfananisha na msichana mmoja niliyesoma naye shule ya msingi huko Kigoma. Yaani wanafanana sana!”
“Huna hakika kama huyo ndiye yule uliyesoma naye?” Materu alimkazia macho.
“Kwa hilo sina hakika. Ninachoweza kukiri ni kuwa wanafanana sana tu!”
“Huyo uliyesoma naye alikuwa akiitwa nani?”
“Scola.”
“Scola?”
“Ndiyo, Scolastica Temu.”
“Scolastica Temu,” Materu alirudia kulitamka jina hilo kwa sauti ya chini huku akiliandika katika ile karatasi yake.
“Ulikuwa naye darasa moja?”
“Hapana, afande. Wakati yeye alipokuwa akiingia darasa la saba, mimi nd’o nilikuwa naingia la tano.”
“Na aliishia hapohapo primary?”
“Hapana, nakumbuka katika darasa lao ni yeye pekee aliyepasi kuingia form one. Nasikia alikuja huku akasoma Shule ya Sekondari ya Zanaki hadi form six, halafu eti akaenda Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda. Huko nasikia alisomea Sheria.”
Inspekta Materu alitikisa kichwa huku akiandika-andika kwenye karatasi. Kisha akanyanyua kichwa na kumtazama tena Samwel kwa macho makali. “Mara ya mwisho ulimwona lini huyo unayemfananisha na huyu mwanamke wa jana?”
“Wakati alipokuwa likizo akisoma sekondari. Ni zaidi ya miaka minne iliyopita.”
“Na hujawahi kumwona mwanamke mwingine hapa Dar anayefanana na huyu Scolastica unayemsema, zaidi ya huyo uliyemwona jana?”
Samwel alitikisa kichwa kwa nguvu akiashiria kukataa. Kisha: “Hapana afande. Sijawahi kumwona.”
“Una miaka mingapi hapa Dar?’
“Miwili.”
Inspekta Materu akashusha pumzi na kujiegemeza kwenye kiti. Akaitwaa chupa ya maji na kunywa mafunda mawili makubwa. Alipoirudisha mezani, akanyanyua kiwiko cha simu ya mezani na kubonyeza hapa na pale kisha akakitega sikioni. Baada ya sekunde chache akasikika akisema, “Namhitaji Sajenti Rahma aje ofisini kwangu haraka.”
Kisha akamrudia Samwel na kumwambia, “Rafiki yangu, bado utakuwa mgeni wetu. Kwa sasa utapewa mahali pa kupumzika na hata chakula utapata bure. Usiwe na wasiwasi.”
Muda mfupi baadaye, askari wa kike, mwenye cheo cha sajini, Rahma Mohammed, aliingia ofisini humo, naye akiwa ndani ya mavazi ya kiraia. Inspekta Materu akampa jukumu la kuwasiliana na Wizara ya Sheria ili kujua kama kuna mtua mwenye jina la Scolastica Temu aliyewahi kusomea Sheria Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda. “Ikibidi, uwasiliane pia na Wizara ya Elimu. Naamini saa moja itakutosha,” aliongeza.
Alipobaki peke yake ofisini, Inspekta Materu alikuwa akiisubiri kwa hamu taarifa ya kutoka kwa daktari kuwa kifo kile kimesababishwa na nini. Kwa nini mtu akutwe amekufa huku katoa macho pima na mdomo ukiwa wazi? Mbona hakukuonekana kama kulikuwa na purukushani kubwa iliyomdhuru mwili?
Hata ile taswira ya chupa za bia kuangukia kitandani ilikuwa ikionesha tu kuwa ni ulevi tu ulimzidia. Ina maana kiwango kikubwa cha pombe ndicho kinaweza kumuua?
Wakati akiendelea kuwaza, mara Sajini Geranija aliingia huku akiwa na mfuko uliokuwa na simu pamoja na zile chupa za bia.
“Hizi chupa zinapaswa kufanyiwa uchunguzi wa kina,” Materu alimwambia. “Isije kuwa alikunywa pombe yenye sumu.”
“Anayeweza kututhibitishia kuwa humu kwenye chupa kulikuwa na kinywaji chenye sumu ni nani, afande? Si ni suala la mkemia?”
“Ndiyo. Lakini unajua hata hivyo, mambo mengine mi' naona ni ya kutupotezea muda tu. Jamaa inasemekana alikuwa mteja sana wa gesti ile. Ninachohisi mimi ni kwamba, huenda alikuwa na tatizo la afya. Sasa kanywa mipombe ya kumzidi nguvu halafu akajitia umwamba kifuani kwa mwanamke. Pumzi zikamzidi akamfia. Unadhani kama ni hivyo, huyo mwanamke angefanya nini? Ni lazima amsukumie kando na kuondoka kinyemela anaikwepa ‘murder case.’
“Yaani Geranija, hili ni suala la malaya wawili waliobebana huko na labda hawajuani sana. Unajua pale jirani na gesti ile kuna baa inayokesha na kuna machangudoa lukuki! Labda akjizoelea pale change mwenye pumzi kubwa, change akampeleksha, jamaa ,akazima.”
Maneno hayo yalimchekesha Geranija, akijihisi kuna aina ya masihara yametumbukizwa. Lakini pia akaona kuwa huenda anachokisema bosi huyo kina ukweli. “Inaweza kuwa hivyo, lakini tusubiri pia taarifa ya daktari,” alisema.
“Yeah, ni muhimu taarifa hiyo. Ila pia kama itasema sumu ilitumika basi tusichukulie kama ni jambo la ajabu. Machangu wengi wana tabia ya kuwanyonyesha chuchu za matiti yao mabwana wanaowachukua, kumbe kwenye chuchu zile wamepaka dawa za kulevya. Baada ya muda mfupi sana mwanaume analewa na kupoteza fahamu. Hapo sasa changudoa anamwibia na kusepa.”
***ITAENDELEA KESHO ASUBUHI

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 26




TULIPOKOMEA....
Maneno hayo yalimchekesha Geranija, akijihisi kuna aina ya masihara yametumbukizwa. Lakini pia akaona kuwa huenda anachokisema bosi huyo kina ukweli. “Inaweza kuwa hivyo, lakini tusubiri pia taarifa ya daktari,” alisema.
“Yeah, ni muhimu taarifa hiyo. Ila pia kama itasema sumu ilitumika basi tusichukulie kama ni jambo la ajabu. Machangu wengi wana tabia ya kuwanyonyesha chuchu za matiti yao mabwana wanaowachukua, kumbe kwenye chuchu zile wamepaka dawa za kulevya. Baada ya muda mfupi sana mwanaume analewa na kupoteza fahamu. Hapo sasa changu anamwibia na kusepa.”
***ENDELEA***
“LAKINI afande,” Geranija alisema, “mbona hili la huyu ni tofauti? Yaani marehemu kakutwa na pesa, zaidi ya shilingi laki na nusu na hii simu ya kisasa tena ya bei. Changudoa gani anaweza kuviacha hivi vitu?”
Inspekta Materu a;likunja uso akifikiri. Kisha akasema, “Hebu tuanze na hiyo simu kwanza. Kwani ina password?”
Geranija aliiwasha na kusubiri kwa muda mfupi kisha wakaanza kuangalia mawasiliano na majina ya waliomo. Wakakuta na picha nyingi ambazo Kisengo alikuwa amepiga na marafiki zake. Nyingi ni zile alizokuwa na Kibutu na Machemba na nyingine akiwa na wanawake katika mikao ya hasara.
Mara Geranija akaonekana kuzama akiiangalia sana sura ya mmoja wa watu hao. Picha iliyomteka sana ni ya Machemba. “Huyu aliye na huyu jamaa aliyekufa ni kama namfahamu,” alimwambia Materu huku akiendelea kumtazama.
“Yupi?” Materu alimuuliza.
“Huyu hapa,” Geranija alimwonesha. Hiyo picha ilimwonesha Machemba, Kibutu, na Kisengo wakiwa wameegemea gari, wote wakiwa na nyuso zenye tabasamu na kila mmoja akiwa ameshika chupa ya bia.
“Na wewe umeanza ishu kama za Samwel. Unataka kuanza kufananisha watu hapa.”
“Hapana, afande,” Geranija alisema huku naye akitabasamu. “Kisha akakunja uso kidogo na kusema. “Huyu ni Machemba. Namfahamu.”
“Sawa, kumfahamu kwako kutasaidia nini? Suala hapa ni kufa kwa huyu jamaa wa jana. Umekiona kitambulisho chake cha utaifa. Anaitwa Kisengo Mabati. Aliyekufa ni yeye, lakini hakuna chochote cha kumshirikisha huyo unayesema unamfahamu na kifo hiki. Tungempata yule malaya aliyekuwa naye nd’o tungejua tunafanya nini!”
“Nakuelewa sana, afande,” Geranija alisema kwa kujiamini. Akaendelea, “N’nachotaka kukwambia ni kwamba, tusichukulie mapema kuwa mwanamke aliyekuwa na huyo marehemu Kisengo eti ni changudoa. Tusihukumu hivyo mapema. Huenda alikuwa ni mtu wake wa kweli, namaanisha mpenzi wake. Kama tukimpata Machemba ambaye kwa taswira iliyoko hapa inaonyesha walikuwa ni maswahiba wakubwa, basi tunaweza kupata kitu. Huenda kama tukimpata huyo Machemba basi tutapata picha pia fulani kuhusu huyo mwanamke.”
“Lakini kwa nini unajipa matumaini kiasi hicho?” Inspekta Materu alimuuliza huku akiimtazama kwa makini.
“Sijui, lakini najipa matumaini na ninahisi kuna tutakachopata kama tukimpata huyu jamaa.”
“Ni wazo zuri,” Materu alisema. “Na hakuna kitu kingine cha maana mlicchokipata kule chumbani, gesti?”
“Tulitarajia tupate hata vocha za simu ambazo zimetumika lakini hatukuambulia kitu,” Geranija alijibu. “Kama tungepata hata vocha moja. basi tungekaa na watu wa TCRA na huenda tungepiga hatua kubwa.”
“Hilo ni suala la kubahatisha,” Materu alisema. “Watu wengine huwa wanaweka muda wa maongezi dakika za wiki nzima, hukuti anahangaika kushikashika mavocha. Na wengine siku hizi wako makini. Akishaitumia vocha, haitupi ovyo, anaificha na kwenda kuitupa mbele na eneo la tukio kama alikuwa amefanya tukio analojua litamtia hatiani. Si unakumbuka tukio la yule jamaa aliyetekwa na jamaa sijui wa wapi vile? ”
“Yule Mgiriki?”
“Yeah. Waliomteka walikuwa makini sana. Inasemekana walikuwa busy wakiuongea na simu mara nyingi tu na vocha walikuwa wakinunua na kuziweka. Lakini walipokipata walichokuwa wakikitaka, wakapotea na pale hutukukuta hata vocha iliyooza kwa matumizi ya muda mrefu! Walikuwa makini sana. Wanajua kuna TCRA! Hata simu ambazo walizokuwa wakizitumia tulizikuta! Simu nne! Nzuri! Bado mpya! Zimetupwa chumbani, Mgiriki kakutwa hoi lakini wao inasemekana waliondoka na dola nyingi kutoka kwa ndugu za mtekwaji!”
Kufikia hapo Materu alitwaa chupa na kunywa maji kwa nguvu kisha akahema kwa nguvu. Mara akamrudia Geranija. “Kwa hiyo Geranija haya mambo ya vocha ni mazuri yanasaidia lakini kaa ukijua kwa dunia ya sasa unapambana na wengi wenye akili sana vichwani. Hakuna wepesi. Kwa hiyo tufikirie mengine, achana na vivocha hivyo.”
Geranija alitikisa kichwa akionesha kukubali.
Upekuzi uliendelea kwenye simu ile, hatimaye Inspekta Materu alishtuka. Alikuwa amesoma ujumbe uliomfanya ashtuke. Ulikuwa ndani ya mtandao wa WhatSapp. Ulisomeka hivi: ‘Ishu imetiki. Nitakuwa Maranatha kesho saa 11 jioni, ukiweza uje. Sms hii nimekutumia pia kwenye ile namba nyingine, usishangae. Na nashangaa Kibutu hapatikani. Kapoteza simu au?’
Ujumbe huo ulionekana umetumwa kwa Kisengo. Naye Kisengo akajibu, ‘hata mimi sijampata tangu jana sijui vipi. Kesho hiyo basi nitakupitia twende tukamwone. Labda ana tatizo.’
Materu akakohoa kidogo kisha akamwonesha Geranija hayo mawasiliano ya WhatsApp. “Unaona? Huyo marehemu alikuwa na miadi na huyo Machemba leo Maranatha Grocery saa kumi na moja jioni.’
“Aisee.”
Kwa hiyo nadhani sisi tufanye mpango wa kumchukua yeye, atueleze kuhusu Kisengo na malaya zake. Naamini pia kuwa anaweza kumfahamu shemeji yake huyo aliyekuwa na Kisengo huko gesti.”
“Ndivyo hata mimi naamini. Na…”
“Vipi?”
“Pamoja na yote nadhani tusubiri taarifa ya daktari na pia kuna umuhimu wa kufanyika kwa kina uchunguzi kupitia macho ya Kisengo. Kafa katoa mimacho kama vile kanyongwa! Tutajua tu! Si wapo wa kitengo hicho? Washughulikie ishu hiyo!”
“Achana nao,” Inspekta Materu aliponda. “Ingekuwa kauawa mtu wa maana tungepitia yote hayo. Mlevi mmoja-malaya na malaya mwenzake, wamefanyiana ushenzi gesti, ni ishu ya kawaida sana. Tusisumbue vichwa vyetu. Labda tu wasiliana na wale vijana walioko Hospitali ya Mwananyamala watuhatarakishie taarifa ya daktari.”
“Sawa afande.”
Dakika kama ishirini baadaye Sajini Geranija alirejea akiwa na askari wengine wawili. Mkononi alikuwa na bahasha ambayo ilihifadhi taarifa rasmi kutoka kwa daktari. Wale askari wengine walimpigia saluti Inspekta Materu na kusimama kando labda wakisubiri maagizo yoyote zaidi.
Baada ya kuifungua bahasha hiyo na kuiangalia kwa makini karatasi yenye taarifa kutoka kwa daktari, hatimaye aliunyanyua tena uso na kuwaambia wale askari wengine, “Mnaweza kwenda tu. Ila Geranija keti kwanza.”
Wale askari walipoondoka, Inspekta Materu alimtazama Geranija kwa uso wenye mikunjo, kisha akasema, “Unajua sajenti, hiki kifo kinaonesha kilitekelezwa kwa sababu maalum.”
“Kwa nini, afande?”
“Ni kifo chenye utata. Inaonyesha marehemu alivuta hewa yenye sumu kali sana iliyosababisha kifo chake. Hewa hiyo iliingiaje ndani ya chumba alicholala?”
“Hapo ndipo penye utata,” Geranija alisema. “Hatuwezi kudai kuwa watu wa gesti wanaweza kuhusika na kifo hicho. Akilini mwangu hilo haliniingia akilini. Mtu n’nayeweza kumhisi na kumtuhumu ni huyo mwanamke aliyekuwa na marehemu. Kwanza ni kwa nini aondoke mapema kiasi kile kama kweli hakuwa na dhamira mbaya?”
“Atakuwa ni huyo malaya tu!” Inspekta Materu alisema kwa jazba. “Ingawa pia hatuwezi kudai kuwa ni malaya kama malaya wengine. Anaweza kuwa ni mwanamke aliyeamua kuua kutokana na sababu maalum. Labda walikuwa na mgogoro ambao sisi hatuujui; mwanamke akaamua kumaliza mchezo kwa kumuua mwanaume kisayansi.
“Labda kuna biashara walikuwa wanafanya pamoja, na mwanamke yule labda akaamua kumuua mwanamume ili yeye abaki na umiliki wa kila kitu. Na kama walikuwa na nyumba, labda mwanamke kaamua kumuua bwana’ake ili achukue nyumba na hata kama kuna mali nyingine, zote zibaki katika himaya yake. Kwani hujasikia siku hizi hata mke anaweza kumuua mume wake ili arithi nyumba na mali zote?”
“Ni kweli, afande,” Geranija alisema. “Na ninadhani muhimu kwetu tufanye hivi, tufike hapo Maranatha Grocery jioni. Ikibidi tumhoji huyo Machemba kwa nguvu. Naamini tutapata chochote kitakachotusaid
ia.”
***ITAENDELEA KESHO

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 27



TULIPOKOMEA....
“Labda kuna biashara walikuwa wanafanya pamoja, na mwanamke yule labda akaamua kumuua mwanamume ili yeye abaki na umiliki wa kila kitu. Na kama walikuwa na nyumba, labda mwanamke kaamua kumuua bwana’ake ili achukue nyumba na hata kama kuna mali nyingine, zote zibaki katika himaya yake. Kwani hujasikia siku hizi hata mke anaweza kumuua mume wake ili arithi nyumba na mali zote?”
“Ni kweli, afande,” Geranija alisema. “Na ninadhani muhimu kwetu tufanye hivi, tufike hapo Maranatha Grocery jioni. Ikibidi tumhoji huyo Machemba kwa nguvu. Naamini tutapata chochote kitakachotusaid
ia.”
***ENDELEA***
Ukimya wa muda mfupi ukapita huku Inspekta Materu akiwa anapitia jalada hili na lile kati ya majalada kadhaa yaliyokuwa mbele yake. Kisha akaunyanyua tena uso na kumtazama Geranija huku akionesha kutokuwa na furaha. Kwa sauti ya unyonge wa mbali akasema, “Sajenti, hii kazi ya upolisi wakati mwingine huwa najilaumu ni kwa nini nilijiingiza humu.”
“Kwa nini, afande?” Geranija alimuuliza huku akiachia tabasamu kubwa, akikaribia kucheka.
“Yaani wakati mwingine mtu unashindwa kukaa na familia yako kwa muda unaotosha; unahangaika tu kufuatilia mambo ya watu wengine! Upuuzi mtupu!”
Sasa Geranija aliachia cheko dogo. Akaendelea kumtazama mkuu wake huku sasa tabasamu likien delea kuchanua. Hakuamini kuwa hayo maneno yaliyomtoka Inspekta Materu yalikuwa ya moyoni. Aliamini kuwa ni miongoni mwa mizaha ambayo huwa wakati mwingine mkuu huyo huifanya.
“Unadhani Sajenti?” Materu alikazia. “Eti mtu unaacha kukaa na mkeo unaishia kuangalia kifo cha jamaa limbukeni wa mwanamake aliyefia gesti kwa umalaya wake. Unaanza kuhangaika kumtafuta kahaba aliyemuua kahaba mwenzake! Kati yao hakuna hata mmoja anayekuhusu hata kwa mbali! Ni ujinga tu huu! Hizi kazi kwa kweli sijui ni shetani gani alinifanya niingie. Sijui kwa kweli.”
“Lakini afande, nd’o kazi yetu,” Geranija alisema kwa upole. “Tayari tumeshakuwa watumishi wa serikali tunaopaswa kulitumikia taifa kwa faida ya Watanzania kwa jumla. Isitoshe, tambua kuwa kwa sasa umri umekwenda, ni vyema tuendelee kulitumikia taifa tukielekea kustaafu. Hatuna miaka mingi sana ya kuwa katika ajira. Hatuna budi kuvumilia. Halafu afande, kumbuka bila ya kazi, watoto wetu hawatakwenda msalani.”
“Ni kweli tupu,” Materu alikiri.
“Na bia hazitanyweka.”
“Sajenti una maneno.”
Wakacheka. Kisha Materu akaongeza, “Ni kweli pia. Bia tutazisikia redioni.”
“Unaona, afande? Ni kuvumilia tu.”
Huku akitikisa kichwa kuafikiana na maneno ya Geranija, Inspekta Materu aliendelea kulipekua jalada moja ambalo lililetwa hapo ofisini kwake jana asubuhi na askari wengine wa kitengo cha uchunguzi. Halafu akaunyanyua uso na kumtazama tena Geranija. “Unakumbuka jana kuna taarifa ililetwa na vijana wetu wa kituo kidogo cha Komakoma kuwa kuna mtu kakutwa ndani kwake kafa?”
Geranija aliitika kwa kutikisa kichwa. “Si ni yule ambaye wanasema anaitwa sijui Kibutu….sijui nani vile?”
“Yeah, Kibutu Malingumu,” Materu alijibu huku akisoma kwenye jalada lile. “Kwa kweli sikupenda kulichukulia uzito suala lile. Tukianza kufuatilia kila tukio la kifo cha mtu kwa hapa Dar au tuseme kwa Kinondoni hii, tutakuwa vichaa siku si nyingi. Hasa hivi vifo vya uswahilini, vya mazingira yasiyoeleweka bayana.
“Lakini tukichukulia hiki cha leo, nd’o nimekumbuka na kile cha juzi. Inasemekana taarifa ya daktari kuhusu kifo cha huyo Kibutu nayo inadai alikufa kwa kuvuta hewa yenye sumu kali.”
“Duh! Tena?!” Geranija alishangaa.
“Ndiyo hivyo, kwa mujibu ya taarifa hii, na jinsi mmoja wa vijana wetu jana alivyoniambia. Sema sikutilia maanani.”
“Enhe?” Geranija alijiweka sawa kusikiliza.
“Huyo aligundulika baada ya jamaa mmoja ambaye inadaiwa alikuwa anamdai pesa zake, kuja pale na kugonga sana mlango asubuhi. Wapangaji wenzake wakasema hata wao hawajui kama yupo au hayupo kwa hawakuwepo usiku.
“Jamaa yule, kwa mujibu wa wale wapangaji, alikuwa na hasira sana na ni kama alikuwa na mning’inio-ziada kichwani mwake. Nikisema mning’inio ziada, sijui unanielewa?”
Geranija alitikisa kichwa akiashiria kukataa.
“Namaanisha ‘hang over’ kwa lugha yenu nyie ‘Waingereza.”
Geranija akacheka kidogo. “Hapo nimekusoma, afande,” alisema.
“Sasa kwa kuwa alikuwa na hasira, akadai kuwa Kibutu yumo na amekausha tu. Inadaiwa alikuwa anamdai shilingi laki nne zake. Ndipo akaamua kuchukua hatua. Jamaa mwenyewe wanadai alikuwa pande la mtu. Akapiga teke mlango kama mara tatu
kitasa kikaachia!
“Ile kuingia tu kwanza akashtuka. Akawaambia wapangaji wengine. Hapo wakaenda kwa mjumbe na mjumbe ndiye alitoa taarifa kwetu. Hakuna yeyote aliyemwona huyo Kibutu akiingia na mtu yeyote mle ndani. Lakini kutokana na aina tofauti za bia, inaonesha alikuwa labda na mwanamke. Vijana wetu walipokuwa wakifuatilia ratiba zake za siku ya nyuma, ndipo ikabainika alitoka na mwanamke mmoja kule Mood Bar, Kinondoni, Mtaa wa Togo usiku kama saa nne, tano hivi.
“Wateja wengi wanaomjua pale Mood Bar walithibitisha kuwa kuna mwanamke mmoja mrefu ana umbo la Kinyarwanda, aliingia hapo baa na alikuwa peke yake. Kwa kuwa Kibutu hakuitaka kumkosa na alikuwa na tupesa mfukoni, akajitosa. Na inadaiwa kuwa walielewana kwani waliagiza bia wakanywa kwa muda tu.
“Baadaye ndipo walipoondoka wote. Hakuna anayekumbuka usafiri uliowachukua, labda hiyo pia ingesaidia kuthibitisha kuwa walikwenda wote mpaka mwisho hapo kwa Kibutu na wakatermka wote. Hilo lingethibitishwa na aliyewapa usafiri.
“Cha ajabu hawa watu wawili wamekufa vifo vya kufanana na walikuwa wakifahamiana. Wa kwanza alikuwa na mwanamke kabla ya kifo chake. Wa pili naye inadaiwa alikuwa na mwanamke. Wote wamekufa kwa kuvuta hewa yenye sumu kali. Huoni kama hapo tunaweza kuwa tunamzungumzia muuaji mmoja tu? Na kwa nini afanye hivyo? Maana hachukui pesa wala simu zao. Naamini kuna kitu hapo. Huenda alikuwa analipa visasi, kama kweli muuaji ni huyohuyo!”
“Atakuwa ni mmoja, afande. Na ana sababu maalum!”
*****
ROBO saa baada ya Geranija kuondoka ofisini kwa Inspekta Materu, Sajini Rahma Mohammed aliingia. Inspekta Materu alikuwa akimsubiri ili ampe taarifa ya kule alikomwagiza kuchukua taarifa zilizomhusu mtu aliyeitwa Scolastica Temu.
“Afadhali umekuja,” Materu alimwambia akionesha kuwa na shauku ya ripoti “Enhe, lete habari. Najua uko vizuri.”
“Yap, habari ninayo, afande,” Rahma alisema.
“Ok, vuta kiti uketi, unipe kila kitu.”
“Nikupe kila kitu? Hapa ofisini? Huna pesa ya gesti?” Rahma alitumbukiza utani.
“Haina shida,” Inspekta Materu alijibu mapigo. “Kipi cha ajabu kwani? Ambacho kingefanyika gesti ndicho tutakachoweza kukifanya humu. Ni kiasi tu cha kufunga mlango kwa funguo, kisha tunaiondoa ile picha ya Baba wa Taifa na ile rais, basi! Tayari hiki kitakuwa chumba cha kawaida kama vile kwako, kwangu au gesti.”
“Kha! Mbona kitanda hakuna?” bado Rahma alichombeza.
“Achana na mambo ya vitanda,” Materu aliponda. “Siyo lazima watu mgaragazane kitandani. We Mpare vipi? Ushamba utakutoka lini? Umesoma primary, secondary, chuo lakini bado ni mbumumbu tu! Hebu sogea hapa nikuonyeshe jinsi Wachaga tunavyojua kuwasulubisha nyie Wapare daaadek!”
****ITAENDELEA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 27



TULIPOKOMEA....
“Labda kuna biashara walikuwa wanafanya pamoja, na mwanamke yule labda akaamua kumuua mwanamume ili yeye abaki na umiliki wa kila kitu. Na kama walikuwa na nyumba, labda mwanamke kaamua kumuua bwana’ake ili achukue nyumba na hata kama kuna mali nyingine, zote zibaki katika himaya yake. Kwani hujasikia siku hizi hata mke anaweza kumuua mume wake ili arithi nyumba na mali zote?”
“Ni kweli, afande,” Geranija alisema. “Na ninadhani muhimu kwetu tufanye hivi, tufike hapo Maranatha Grocery jioni. Ikibidi tumhoji huyo Machemba kwa nguvu. Naamini tutapata chochote kitakachotusaid
ia.”
***ENDELEA***
Ukimya wa muda mfupi ukapita huku Inspekta Materu akiwa anapitia jalada hili na lile kati ya majalada kadhaa yaliyokuwa mbele yake. Kisha akaunyanyua tena uso na kumtazama Geranija huku akionesha kutokuwa na furaha. Kwa sauti ya unyonge wa mbali akasema, “Sajenti, hii kazi ya upolisi wakati mwingine huwa najilaumu ni kwa nini nilijiingiza humu.”
“Kwa nini, afande?” Geranija alimuuliza huku akiachia tabasamu kubwa, akikaribia kucheka.
“Yaani wakati mwingine mtu unashindwa kukaa na familia yako kwa muda unaotosha; unahangaika tu kufuatilia mambo ya watu wengine! Upuuzi mtupu!”
Sasa Geranija aliachia cheko dogo. Akaendelea kumtazama mkuu wake huku sasa tabasamu likien delea kuchanua. Hakuamini kuwa hayo maneno yaliyomtoka Inspekta Materu yalikuwa ya moyoni. Aliamini kuwa ni miongoni mwa mizaha ambayo huwa wakati mwingine mkuu huyo huifanya.
“Unadhani Sajenti?” Materu alikazia. “Eti mtu unaacha kukaa na mkeo unaishia kuangalia kifo cha jamaa limbukeni wa mwanamake aliyefia gesti kwa umalaya wake. Unaanza kuhangaika kumtafuta kahaba aliyemuua kahaba mwenzake! Kati yao hakuna hata mmoja anayekuhusu hata kwa mbali! Ni ujinga tu huu! Hizi kazi kwa kweli sijui ni shetani gani alinifanya niingie. Sijui kwa kweli.”
“Lakini afande, nd’o kazi yetu,” Geranija alisema kwa upole. “Tayari tumeshakuwa watumishi wa serikali tunaopaswa kulitumikia taifa kwa faida ya Watanzania kwa jumla. Isitoshe, tambua kuwa kwa sasa umri umekwenda, ni vyema tuendelee kulitumikia taifa tukielekea kustaafu. Hatuna miaka mingi sana ya kuwa katika ajira. Hatuna budi kuvumilia. Halafu afande, kumbuka bila ya kazi, watoto wetu hawatakwenda msalani.”
“Ni kweli tupu,” Materu alikiri.
“Na bia hazitanyweka.”
“Sajenti una maneno.”
Wakacheka. Kisha Materu akaongeza, “Ni kweli pia. Bia tutazisikia redioni.”
“Unaona, afande? Ni kuvumilia tu.”
Huku akitikisa kichwa kuafikiana na maneno ya Geranija, Inspekta Materu aliendelea kulipekua jalada moja ambalo lililetwa hapo ofisini kwake jana asubuhi na askari wengine wa kitengo cha uchunguzi. Halafu akaunyanyua uso na kumtazama tena Geranija. “Unakumbuka jana kuna taarifa ililetwa na vijana wetu wa kituo kidogo cha Komakoma kuwa kuna mtu kakutwa ndani kwake kafa?”
Geranija aliitika kwa kutikisa kichwa. “Si ni yule ambaye wanasema anaitwa sijui Kibutu….sijui nani vile?”
“Yeah, Kibutu Malingumu,” Materu alijibu huku akisoma kwenye jalada lile. “Kwa kweli sikupenda kulichukulia uzito suala lile. Tukianza kufuatilia kila tukio la kifo cha mtu kwa hapa Dar au tuseme kwa Kinondoni hii, tutakuwa vichaa siku si nyingi. Hasa hivi vifo vya uswahilini, vya mazingira yasiyoeleweka bayana.
“Lakini tukichukulia hiki cha leo, nd’o nimekumbuka na kile cha juzi. Inasemekana taarifa ya daktari kuhusu kifo cha huyo Kibutu nayo inadai alikufa kwa kuvuta hewa yenye sumu kali.”
“Duh! Tena?!” Geranija alishangaa.
“Ndiyo hivyo, kwa mujibu ya taarifa hii, na jinsi mmoja wa vijana wetu jana alivyoniambia. Sema sikutilia maanani.”
“Enhe?” Geranija alijiweka sawa kusikiliza.
“Huyo aligundulika baada ya jamaa mmoja ambaye inadaiwa alikuwa anamdai pesa zake, kuja pale na kugonga sana mlango asubuhi. Wapangaji wenzake wakasema hata wao hawajui kama yupo au hayupo kwa hawakuwepo usiku.
“Jamaa yule, kwa mujibu wa wale wapangaji, alikuwa na hasira sana na ni kama alikuwa na mning’inio-ziada kichwani mwake. Nikisema mning’inio ziada, sijui unanielewa?”
Geranija alitikisa kichwa akiashiria kukataa.
“Namaanisha ‘hang over’ kwa lugha yenu nyie ‘Waingereza.”
Geranija akacheka kidogo. “Hapo nimekusoma, afande,” alisema.
“Sasa kwa kuwa alikuwa na hasira, akadai kuwa Kibutu yumo na amekausha tu. Inadaiwa alikuwa anamdai shilingi laki nne zake. Ndipo akaamua kuchukua hatua. Jamaa mwenyewe wanadai alikuwa pande la mtu. Akapiga teke mlango kama mara tatu
kitasa kikaachia!
“Ile kuingia tu kwanza akashtuka. Akawaambia wapangaji wengine. Hapo wakaenda kwa mjumbe na mjumbe ndiye alitoa taarifa kwetu. Hakuna yeyote aliyemwona huyo Kibutu akiingia na mtu yeyote mle ndani. Lakini kutokana na aina tofauti za bia, inaonesha alikuwa labda na mwanamke. Vijana wetu walipokuwa wakifuatilia ratiba zake za siku ya nyuma, ndipo ikabainika alitoka na mwanamke mmoja kule Mood Bar, Kinondoni, Mtaa wa Togo usiku kama saa nne, tano hivi.
“Wateja wengi wanaomjua pale Mood Bar walithibitisha kuwa kuna mwanamke mmoja mrefu ana umbo la Kinyarwanda, aliingia hapo baa na alikuwa peke yake. Kwa kuwa Kibutu hakuitaka kumkosa na alikuwa na tupesa mfukoni, akajitosa. Na inadaiwa kuwa walielewana kwani waliagiza bia wakanywa kwa muda tu.
“Baadaye ndipo walipoondoka wote. Hakuna anayekumbuka usafiri uliowachukua, labda hiyo pia ingesaidia kuthibitisha kuwa walikwenda wote mpaka mwisho hapo kwa Kibutu na wakatermka wote. Hilo lingethibitishwa na aliyewapa usafiri.
“Cha ajabu hawa watu wawili wamekufa vifo vya kufanana na walikuwa wakifahamiana. Wa kwanza alikuwa na mwanamke kabla ya kifo chake. Wa pili naye inadaiwa alikuwa na mwanamke. Wote wamekufa kwa kuvuta hewa yenye sumu kali. Huoni kama hapo tunaweza kuwa tunamzungumzia muuaji mmoja tu? Na kwa nini afanye hivyo? Maana hachukui pesa wala simu zao. Naamini kuna kitu hapo. Huenda alikuwa analipa visasi, kama kweli muuaji ni huyohuyo!”
“Atakuwa ni mmoja, afande. Na ana sababu maalum!”
*****
ROBO saa baada ya Geranija kuondoka ofisini kwa Inspekta Materu, Sajini Rahma Mohammed aliingia. Inspekta Materu alikuwa akimsubiri ili ampe taarifa ya kule alikomwagiza kuchukua taarifa zilizomhusu mtu aliyeitwa Scolastica Temu.
“Afadhali umekuja,” Materu alimwambia akionesha kuwa na shauku ya ripoti “Enhe, lete habari. Najua uko vizuri.”
“Yap, habari ninayo, afande,” Rahma alisema.
“Ok, vuta kiti uketi, unipe kila kitu.”
“Nikupe kila kitu? Hapa ofisini? Huna pesa ya gesti?” Rahma alitumbukiza utani.
“Haina shida,” Inspekta Materu alijibu mapigo. “Kipi cha ajabu kwani? Ambacho kingefanyika gesti ndicho tutakachoweza kukifanya humu. Ni kiasi tu cha kufunga mlango kwa funguo, kisha tunaiondoa ile picha ya Baba wa Taifa na ile rais, basi! Tayari hiki kitakuwa chumba cha kawaida kama vile kwako, kwangu au gesti.”
“Kha! Mbona kitanda hakuna?” bado Rahma alichombeza.
“Achana na mambo ya vitanda,” Materu aliponda. “Siyo lazima watu mgaragazane kitandani. We Mpare vipi? Ushamba utakutoka lini? Umesoma primary, secondary, chuo lakini bado ni mbumumbu tu! Hebu sogea hapa nikuonyeshe jinsi Wachaga tunavyojua kuwasulubisha nyie Wapare daaadek!”
****ITAENDELEA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 28




TULIPOKOMEA....
“Kha! Mbona kitanda hakuna?” bado Rahma alichombeza.
“Achana na mambo ya vitanda,” Materu aliponda. “Siyo lazima watu mgaragazane kitandani. We Mpare vipi? Ushamba utakutoka lini? Umesoma primary, secondary, chuo lakini bado ni mbumumbu tu! Hebu sogea hapa nikuonyeshe jinsi Wachaga tunavyojua kuwasulubisha nyie Wapare daaadek!”
***ENDELEA***
“Hamna lolote,” Rahma alimponda. “Mnajitapa tu maneno mengiii… kumbe hamna kitu… wanawake huko Rombo wanatafuta wanaume nje ya Uchagani maana’ake nyie m’shashindwa! Sema we’ Mchaga mwingine mwenye maneno mengi. Sema usikike!” Kufikia hapo akaachia cheko la dhihaka huku akimtazama sawia Inspekta Materu usoni.
“We’ mwanamke sasa unatuvunjia heshima Wachaga,” Materu alisema huku akiachia tabasamu la mbali. “Unajua mimi ni mkuu wako? Naweza kukubadilishia somo ghafla! Na wala nisitake kusikia ripoti yako ya huko wizarani.” Kufikia hapo akacheka kidogo na kupokewa na Rahma.
“Afande, tuache kwanza hayo masihara,” Rahma alisema huku sasa akivuta kiti na kuketi, tabasamu likiyeyuka taratibu usoni.
Dakika iliyofuata nyuso zao zilikuwa zimerudi kikazi zaidi, utani na mizaha vikiwa vimekwishapewa likizo ndefu. “Ok, kinachoendelea?” Materu alimtazama tena Rahma.
Rahma alivuta na kushusha pumzi ndefu kwa nguvu. Akafungua mkoba wake na kutoa karatasi yenye maandishi mengi mwanzo mpaka mwisho. Kisha: “Taarifa niliyopata kule Wizara ya Sheria ni kwamba, Mtanzania mwenye jina la Scolastica Temu alikuwa ni miongoni mwa Watanzania wengine ishirini na watatu waliosoma Chuo Kikuu cha Makerere kiasi cha miaka mitatu iliyopita. Na baada ya kurudi alifanya kazi pale wizarani kwa muda mfupi kabla hajapangiwa kituo ambacho hakukiafiki.
“Inasemekana,” aliendelea, “bila taarifa aliacha kazi baada ya miezi mitatu tu. Baadaye alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni binafsi ya uwakili hapahapa Dar. Sijaambiwa ni kampuni gani. Hakuna kumbukumbu sahihi kuhusu hilo. Na mfanyakazi mmoja ameniambia kuwa anasikia mwanamke huyo anaishi Kinondoni, ila hakuna anayejua anaishi Kinondoni pande zipi.
“Nimewataka wanionyeshe picha yake na wamenirushia kwenye simu yangu kwa njia ya WhatsApp. Zipo picha tatu hapa za mwanamke mzuri sana anayefanana kama Mnyarwanda hivi. Yupo Kitutsi-tutsi. Hata hivyo, taarifa zake pia zinaonyesha baba yake alikuwa Mchaga na mama yake alikuwa Mnyarwanda aliyekuwa akiishi Kigoma.”
“Kwa mchanganyiko huo wa damu lazima aonekane hivyo. Hebu tuzione” Materu alimwambia.
Rahma akaitwaa simu yake kubwa na kuifungua kwenye programu ya picha za mtandao wa WhatsApp. Akazungukia upande alikoketi Inspekta Materu na kuziangalia picha hizo kwa pamoja.
“Yuko vizuri,” Materu alisema kwa sauti ya chini akiziangalia kwa makni picha hizo. “Ni Mtutsi hasa. Cheki na minywele yake daaah!”
“Kwa kweli ni mwanamke mzuri,” Rahma naye aliafiki. “Na kama kweli watu wa Mood Bar wanadai mwanamke aliyekuwa na Kibutu alikuwa ni mzuri na ana mwonekano wa Kinyarwanda, basi anaweza kuwa huyu.”
“Hapana, tusimhukumu bure mwanamke wa watu mapema hivyo,” Materu alisema. “Anaweza kuwa siye kabisa. Lakini pia kama taarifa aliyosema Samwel kuwa Scolastica anayemfahamu alikuwa akisomea Sheria huko Uganda, basi pia anaweza kuwa huyu! Suala ni kwamba, huyu ndiye alikuwa na Kisengo kule Madina Guest House au siye?
“Samwel kamfananisha tu; huenda ndiye au siye. Raha ingekuwa ni kama ingetokea tena Samwel na mwanamke huyu wakaonana ana kwa ana, hapo kitendawili kingeteguliwa. Samwel angekiri kuwa huyu ndiye aliyekwenda gesti usiku ule au sio yeye.”
“Kweli,” Rahma alisema huku akiirudisha simu mkobani.
Inspekta Materu alijitanua kifua, akainyoosha mikono na kupiga mwayo kisha akashusha pumzi na kutulia kwa sekunde chache, macho yakiwa yametua kwenye karatasi zake zilitapakaa mezani. Alipoyainua tena macho na kumtazama Rahma, alisema, “Sasa fanya hivi, kaniitie Geranija. Na wewe ujiandae kwa safari ya Kinondoni jioni. Tutakuwa wote.”
*****
SAJINI Geranija alipoingia ofisini kwa Inspekta Materu alimkuta akiwa amekodoa macho kwenye skrini ya kompyuta huku akidonoadonoa ‘batani.’ Na hata alipovuta kiti na kuketi, bado Materu alikuwa ameyagandisha tu macho kwenye kompyuta.
Baada ya kama nusu dakika hivi, ndipo alipomrudia Geranija.
Akampa taarifa yote aliyopewa na Rahma kwa kina. Mwishoni akamwambia, “Inasadikika kuwa mtu huyo anaishi Kinondoni hii. Ni mwanamke mwenye mvuto mkali kama walivyosema waliomwona kule Mood Bar, Mtaa wa Togo. Yupo Kitutsi hasa!”
“Anaweza kuwa ndiye aliyemlaza jamaa kule Madina?” Geranija aliuliza kama ategemeaye jibu kutoka kwa Materu.
“Nani anajua?” Inspekta Materu naye aliuliza huku akipunga mikono huku na huku. “Samwel kamfananisha tu. Hatuna hakika yoyote. Lakini sisi ile safari yetu ya Maranatha iko palepale! Saa kumi tuwe pale. Ni vizuri kuwahi zaidi. Najisikia kuamini huenda tukapata kitu fulani cha faida katika sakata hili.”
*****
KUENDELEA kumfikiria yule kijana wa mapokezi wa kule Madina Guest House, Scolastica hakuona kuwa kutamsaidia. Japo aliamni kabisa kuna mahali aliwahi kumwona, lakini kwa usiku huo, akiwa amekwishatekeleza kazi nyingine iliyokusudiwa, hakuona kuwa kuna haja ya kumfikiria tena kijana huyo.
Alipokwishauweka mkoba wake mezani, alivua nguo na kwenda bafuni kuoga. Aliporudi chumbani alijisikia tofauti. Hakuwa na uchovu wowote lakini pia alihisi kukosa usingizi. Zaidi alikuwa akimkumbuka Kisengo alivyokuwa na pupa ya kufanya mapenzi.
Alikuwa na papara ya kumpapasa na kumbusu kilevilevi.
Kicheko kikamjia naye alipokumbuka jinsi alivyoupeleka mkono wake mahala fulani mwilini mwa Kisengo, akakitelezesha kiganja chake laini mahali hapo, akipapasa, akatomasa kisha akashikashika, akaminyaminya, akatofya, Kisengo akatofyeka hasa na kuhemea juujuu!
“Bwege lilitarajia nilivulie nguo!” alinong’ona huku akiendelea kuachia tabasamu lililokaribia kicheko Akajitupa sofani huku akiwa na vazi la kanga pekee, akaukunja mguu mmoja na kuliacha paja lake kubwa hadharani.
Akatabasamu zaidi na kukaribia kucheka alipokumbuka jinsi Kisengo alivyotaka kuonesha ujasiri wa kutoanguka wakati akivua suruali, huku tayari akiwa amekunywa mafunda kadhaa ya ile bia iliyokuwa na unga wa tembe ya Olanzapin. Tembe ikamzidi nguvu! Mwanamume akaenda mzima-mzima mezani na kuziangukia chupa za bia!
Kicheko cha chinichini sasa kikamtoka pale alipojiwa na picha ya jinsi Kisengo alivyojinyanyua kwa nguvu kutoka pale alipoziangukia bia mezani. Akafanikiwa kusimama, lakini papohapo akarudi kinyumenyume kama gari bovu na kuanguka kama gunia la mashudu chali!
“Kaanguka kama nguruwe pori!” alinong’ona huku akiendelea kucheka kwa sauti ya chini.
Akaitwaa simu na kuangalia muda. “Saa sita u nusu! Na usingizi sina nakalia kuuwazia ujinga wa marehemu!” alijisemea kimoyomoyo huku akinyanyuka na kufungua geti. Akiwa amesimama nje, akasikia wale wapangaji wenzake wa upande wa pili wakizungumza.
Sauti iliyokuwa ikisikika zaidi ilikuwa ya Zinduna. Hakujua kama aliyekuwa akiongea naye ni mwenzie, Janeth au la. Sauti zao zilionesha kuwa pombe zimewakolea. Akajua kuwa kama atawapa ofa hawatakataa. Akaufuata mlango na kuwagongea.
Dakika chache baadaye, Zinduna akiwa na furaha isiyo kifani, aliondoka kwa mwendo mkali na chupa sita tupu za bia akienda Pazi Social Club. Janeth na Scolastica walibaki pale nje wakiongea. Zinduna aliporejea, Scolastica alichukua chupa zake mbili na kuingia ndani mwake akiwaachia bia nyingine.
Alijitambua kuwa yeye siye wa kiwango cha kina Zinduna. Ataongea nini cha maana watu ambao kila wakati wanawajadili wanaume ambao ama waliwahonga pesa nyingi, walikuwa hodari kitandani, walikuwa dhaifu nguo zilipochojolewa, watanashati, wachafu, wenye unene uliochusha, wembamba uliokithiri, walevi-mbwa na kadhalika na kadhalika. Akilini mwake alijua kuwa kuna watu wa kukaa na kuongea na watu wa aina hiyo. Siyo yeye!
Alijitupa sofani na kurudia kukaa kihasarahasara vilevile; aogope nini ilhali yuko peke yake? Akaiwasha runinga na kuangalia chaneli yenye miziki mfululizo. Saa nane kasoro dakika kadhaa, chupa ya pili ikiwa nusu, alipitiwa na usingizi akiwa amekaa vilevile sofani, kihasarahasara!


ITAENDELEA

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom