NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 039
Kid0le kikashuka mpaka kwenye kitufe cha kufyatulia risasi. Akaivuta pumzi kwa muda. Akili yake ilikuwa ikikinzana na moyo wake. Moyo ulihitaji atende kile, lakini akili ikakataa kutii matakwa ya moyo. Bado akatulia kidole kikiwa kwenye kitufe. Alikuwa ametulia akiusikilizia uamuzi wa vitu viwili. Uamuzi wa kukatisha maisha yake ama kufuata kingine. Ni katika kuwaza huko akapata maamuzi mapya. Maamuzi ambayo yalimfanya aishushe bastola yake. Akatulia akiufikiria uamuzi mpya alioupata. Akili yake ilimwambia aondoke hapa Tanzania aende nchi yoyote akatafute sehemu ya kuishi akiwa sambamba na France. Huo ulikuwa uamuzi wake, maamuzi ambayo hakutaka kumshirikisha mtu. Akatoka ndani ya chumba kile na kurudi kule alipomuacha Daktari akimtibia France. Akaufungua mlango na kuingia macho yake yakakutana na macho ya france yakimtizama kwa wasiwasi. Teddy akatabasamu tayari kwa kuuondoa wasiwasi ule. Akapiga hatua mpaka pale alipokuwa amelala. Akapiga magoti na kuushika mkono wake. Akayapeleka macho yake usoni kwa france. Akahisi kama alikuwa akitizamana na Masimba kutokana na kufanana kwao. France alikuwa ni Masimba mtupu. Alimuangalia sana mwisho wake akashindwa kuyazuia machozi yake yasishuke. Bado mwili wa mama yake masimba ulipopaa angani baada ya kupigwa risasi na Rukia ulikuwa ukijirudia. Roho ikamuuma na kumuuma. Ule ushujaa wote ukapotea kabisa. Sasa alikuwa ameivaa hofu na kuuvaa woga. Alikuwa aki0gopa kukutana na masimba. Hapo ndipo alipozidi kuona umuhimu wa kuondoka hapa nchini. "Nakupenda sana mwanangu Frances. Wewe ndio pekee furaha yangu pekee iliyobaki. Najua baba yako atanitafuta na hata kuniua. Lakini kabla hajaniua nataka nikwambie kuwa Nakupenda mwanangu na ninataka tuondoke hapa tukaishi Ulaya. Nia yangu nikukufanya uishi kwa furaha." Baada ya kuongea hayo akainuka na kuondoka pale nyumbani. Alitaka kuipanga mipango kimya kimya pasipo ku0ngea na mtu yoyote. Hata kupokea simu ya Mwamvita hakuwa akifanya hivyo ndio maana leo hii hakuwa katika makazi yake yanayojulikana.
****
Bado hakuwa na fahamu na hakuwa akijua kile kilichokuwa kinaendelea. Handeni ikazizima kwa majonzi na vilio. Kila mmoja aliyesikia kifo cha mama huyu alisikitika sana. Watu wakaendelea kumiminika kutoka maeneo mbalimbali. Muda mfupi nyumbani ulijaa umati wa watu. Kila mmoja alikuwa akisikitika na kulaani kile kilichotokea. Vijana wenye uchungu wakataka kuleta fujo kwa kuwalaumu polisi. Lakini hawakujua, hawakujua kuwa Polisi hawakuwa na kosa lolote. Masimba bado hakuwa na fahamu, ndio kwanza madrip ya maji yalikuwa yakimiminika kwenye mishipa. Habari zikasambaa kama moto wa kifuu. Idara ya ujasusi ikaipata taarifa hiyo. Ilikuwa taarifa iliyowashtua wengi. Katika wote hao Dee plus pekee ndiye aliyeumia sana. Alimjua mama wa Masimba kwa kuwa waliishi jirani kabisa nyumba zao zipakana kwa hatua tano tu. Hakutaka kuliamini hilo katu. Akaona kulikuwa na umuhimu wa kumpigia masimba. Licha ya kupiga sana na simu kuita, lakini simu haikupokelewa. Dee plus akaamua kuipanga safari katika muda ule kuelekea Handeni. Hakutaka kuchelewa.. muda mfupi baadaye alikuwa barabarani akielekea handeni. Asingeweza kubaki Dar wakati Vibaoni imepatwa na msiba. Aliitembeza gari kwa mwendo wa kutisha, trafiki walio jaribu kumsimamisha njiani walikutana na kitanbulisho. Wakamuacha aendelee kwenye safari yake. Saa tano na nusu asubuhi alikuwa akiingia katika viunga vya vibaoni. Alipokelewa na umati wa watu sambamba na vilio. Aliufungua mlango na kushuka. Hakuongea na mtu zaidi ya kuongoza mpaka nyumbani kwa kina masimba. Alipokuwa akikaribia macho yake yakakiona kitu ambacho kilitafanya machozi ya mdondoke. Chini ya ardhi ya nyumba ya Wanamchiwa mbele kidogo ya uwanja wa nyumba, damu nyingi ilikuwa imetuwama chini. Akasogea mbele huku miguu ikimtetemeka. Akaiangalia ile damu kwa muda wa dakika mbili bila kuongea kitu. Baada ya kuangalia akageuka na kurudi ndani ya gari. Akaliwasha gari na kuliondoa gari kuelekea hospital ya Wilaya ya Handeni. Moyo ulikuwa ukibubujikwa na damu, hakuwahi kufikiria kama Teddy angekuwa mnyama kiasi kile. Moyoni mwake hata yeye akaapa kumuondoa katika uso wa dunia hii. Teddy lazima uilipe hii damu ya mama. Lazima uilipe kwa gharama yote. Muda mfupi alikuwa kwenye maegesho ya magari hospital pale. Alishuka na kukutana na makachero wengine ambao walitoka Dar es salaam. Akawasalimia, kisha akawapita na kuelekea chumba cha kuhifadhia maiti. Wakati anausukuma mlango kuingia ndani.. macho yake yakatua juu ya mwili wa mama wa masimba. Matundu matano ya risasi yalikuwa yamekiharibu kifua. Dee plus akashikwa na butwaa.. miguu ikawa mizito kupiga hatua. Akasimama akiutizama mwili wa mwanamke yule asiye na hatia. Punde mlango ukafunguliwa akahisi kilio cha kwikwi kikitokea kwa nyuma yake. Akageuka taratibu kumtizama huyu anayelia. Macho yake yakamuona masimba akiwa ameshikiliwa huku na huko. Alikuwa akitia huruma sana.. machozi yalikuwa yakishuka kama maji. Akamuangalia huku akisogea. Kufika karibu yake akasimama mbele yake. "Don.!!! Aliita Dee..
"Teddy amenilazimisha nimuue. Teddy amekitafuta kifo ambacho nilikuwa tayari kukighairisha. Wameniulia mama yangu na kuwaumiza wanangu. Yaseer yupo mahututi amesafirishwa leo na makao, lakini france wameondoka naye na sijui hali yake." Aliongea masimba akiendelea kulia akitembea kuelekea pale ulipo mwili wa mama yake
******
Ulikuwa muda wa mazishi ya mama yake. Alikuwa amesimama pembeni akilia wakati masheikh walipokuwa wakiuombea mwili wa mama yake. Dada zake na kaka zake hawakuwa na hali, kila mmoja alikuwa akigalagala kwa vilio. Wajukuu na ndugu wengine hawakukamatika. Kwa masimba alikuwa bado haamini. Haamini kama ndio mwisho wa mama yake. Taswira ya mwamvita akimshuti mama yake iliendelea kujirudia kichwani kwake. Bado alikuwa akikunbuka risasi zili zilivyomtupa chini mama yake. "Mwamvita nitakuua kwa mikono yangu." Akanong'ona taratibu. Swala ya kuuswalia mwili wa marehemu ikaendelea kama kawaida na mwisho watu wakaubeba mwili ma marehemu kuupeleka katika nyumba yake ya milele. Umati uliohudhuria ulimshangaza kila mmoja hasa wale majasusi waliokuja kumpa msaada masimba. Kila alipokuwa akitembea taswira ya mwamvita haikuondoka usoni mwake. Mazishi yakafanyika na watu wote wakarudi nyumbani. Lakini cha ajabu alipotafutwa masimba hakuonekana. Hata kaka yake samwebondo alipotumwa akamtizame makaburini hakumuona. Na hakuwa masimba pekee bali hata Dee plus hakuwepo. Hilo likawashangaza wana ndugu wote simu yake haikupatikana na hata sehemu zote alizotafutwa hakuonekana. Kila mmoja akaongea anachokijua ili mradi tu. Masimba hakuonekana hata usiku ulipoingia.
******
Upepo ulikuwa ukivuma mithiri ya milipuko. Ndio kwanza Masimba alikuwa akiingia katika jiji la dar es salaam. Safari hii aliamua kuendesha gari mpaka Bunju nje kidogo ya jiji la dar es salaam. Kuelekea huko kulitokana na kuogopa kundulika mapema na watu wanaomtafuta. Kingine kilichomsogeza Huko ni ukaribu wa sehemu anapoishi mwamvita. Aliendesha gari mpaka bunju A nyumbani kwa Neema Mtobwa. Aliipaki gari umbali mfupi kutoka nyumba alioishi neema. Akatembea kwa miguu mpaka usawa wa jumba analoishi Neema. Hakutaka kupitia mlangoni, alichupa na kudondokea kwa ndani. Hapo akatembea tena na kuufungua mlango wa nyuma. Mlango ukamtiii!! Hapo akaingia ndani bila wasiwasi. Akatembea mpaka sebuleni. Hapi akakutana na Neema mtobwa akiwa amejilaza kwenye kiti. Akamsogelea na kumtingisha. Neema akafumbua macho yake, akajikuta akitizamana na masimba. Akainuka na kumkumbatia kwa nguvu. "Pole sana Masimba. Nimesikia kutoka ndani kilichotokea. Lakini kwa nini uko hapa wakati ndio kwanza mama amezikwa leo!!!!@ aliongea neema aki0nyesha kushangaa.
"Neema, mama yangu ameuawa na hatarudi tena. Nitabaki vipi handeni wakati waliomuua mama yangu wanafurahi? Nimekuja kuwapeleka kuzimu wakaungane na Mama Yangu.""....