Riwaya: Nitakupata tu

Duuu hakuna kimbilia!!!!

Inauma sana ila sina budi kusubiri huru na busara za mwenye nacho Mungu akubariki na akupatie nguvu ya kutukumbuka
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 016

Hisia za kwamba watu wale walitumwa na idara ya usalama wa taifa zilikuwa ndogo sana ukilinganisha na hisia kuhusu Jimmy. Ulikuwa mchana tu walipomtisha kwa bastola, lakini muda huu alikuwa akiwashuhudia watu wakiuruka uzio wa nyumba yao, watu ambao waliuonyesha kile ambacho kilimthibitishia kuwa watu waliomtembelea walikuwa na uwezo mkubwa sana, kutokana na namna ya utokaji wao. Hilo likampa wasiwasi, wasiwasi ambao hakuwa nao hapo mwanzo. Kwa nini watu hawa wamekuja hapa? Wametumwa na nani na kwa sababu ipi? Hilo likampa utimamu wa akili, utimamu wa kutokurupuka. Alitaka kuujua ukweli kuhusu watu hawa ambao bado walikiumiza kichwa chake. Kwa mara ya kwanza aliutamani uwepo wa Masimba. Kwa mara ya kwanza alimkumbuka masimba, hakuogopa kuhusu kujua kwake, muda ule alimhitaji kama msaada na mtu wa pekee katika hili. Lakini masimba hakuwepo na hakujua wapi alipo mpaka muda huo. Hata hilo lilimchanganya pia, kwa nini mpaka muda ule masimba hajarudi? Ama amekufa katika tukio la kulipuliwa kwa gari yao? Hilo likamfanya teddy aamue kurudi sehemu ya tukio. Alitaka kumsaka masimba ajue wapi alipo. Hilo likamrudisha mpaka ndani, macho yake yakiangaza huku na kuangalia kule, alitaka kujua kama watu wale wamefanya chochote. Ni kweli alikiona kile ambacho alikiwaza. Watu wale walikuwa wamepekua sebuleni mpaka chumbani kwa utaalam wa hali ya juu, kitu ambacho kwa macho ya mtu wa kawaida hawezi kugundua. Aliangalia kwa muda na kuchunguza kila kitu chake. Alipogundua kipo salama, alibadili mavazi yake, akachukua bastola zake mbili na kuzichomeka sehemu tofauti ndani ya mavazi yake. Akaurudisha mlango, safari ya kuelekea Mjimwema ikaanza. Alikuwa ameshakijenga kisasi na chuki juu ya Jimmy na washirika wake. Alijiapiza endapo kweli Jimmy yupo nyuma ya matukio haya, basi atahakikisha anampoteza.

******
Alishuka sehemu ya tukio na kupokelewa na askari waliovaa magwanda sambamba na utepe wa kuonyesha kwamba sehemu haikuwa salama. Akatembea mpaka pale akisalimiana na baadhi ya askari, lakini alipotaka kuingia ndani ya eneo lililozungushiwa utepe akazuiwa na makachero wa polisi waliovalia mavazi ya kiraia. Teddy hakuongea wala kujitambulisha kwa chochote, bali alimuangalia kachero yule kama sekunde mbili, kachero yule hakumuangalia tena teddy. Alitoa ruhusa kwa teddy kupita. Alipoingia akajikuta akitizamana na miili ya watu watatu ambayo ililazwa chini kuonyesha kuwa haikuwa na uhai. Akatembea akiiona hofu moyoni mwake, hofu kuwa masimba alikuwa ameuawa, hofu ya kumpoteza mpenzi wake na hofu ya kutishwa na watu. Ingawa hakuwahi kuogopa, lakini hili lilimtia hofu. Mikono yake iliokuwa akitetemeka sasa taratibu ilikuwa ikishuka tayari kwa kufunua shuka. Hatimaye akaikamata kisha kuifunua, moyo wake ukachanua kwa tabasamu, tabasamu mwanana baada ya kugundua kati ya miili ile mitatu, hapakuwa na mwili wa masimba. Akairudisha shuka, akainuka akitoka nje ya utepe wa polisi. Macho kadhaa yalikuwa yakimtizama katika aina ya maswali. Hilo halikumfanya aogope, bado alitembea macho yake yakitizama kila sura za makachero waliokuwwpo pale kwa chati. Alitaka kujua nani ambaye alikuwa akimtizama kwa hila. Tokea alipowaona watu wale kule nyumbani kwake, hakutaka kuamini kama hakuwa akitembea na macho ya watu ama kutembea sambamba na watu. Aliamini kuwa kama watu wamediriki kuingia ndani ya nyumba yake, kisha kuifanyia upekuzi katika muda usiozidi dakika moja, hakuamini kama wanaweza kumuacha atembee peke yake. Lazima watakuwepo watu ama mtu ambaye anaifanya shighuli ya kumfuatilia. Lakini macho yote aliotizamana nayo bado hayakuonyesha hila. Yalikuwa macho ya kawaida japokuwa palikuwa na giza.

********

Jumba lilikuwa na walinzi wenye silaha nzito, wote walikuwa katika suti nyeusi kuonyesha kuwa walikuwa watamu katika medani ya kimapigano. Wote walikuwa wameizunguka gari huku midomo ya silaha zao zikielekezwa ilipo simama ile gari. Hata mlango ulipofunguliwa watu wale hakuongea chochote zaidi ya kumpa ishara masimba ashuke. Masimba akatii huku bado midomo ya bastola sambamba na bunduki za walinzi zikimtizama. Alitembea akiwa amewekwa kati. Kila hatua yake na uchezaji wa mikono yake, ulikuwa ukiangaliwa kwa ukaribu. Kila mguu wake ulipokuwa ukipiga hatua na kutua chini, macho ya Walinzi wale nayo yalikwenda sambamba. Wakaufikia mlango mmoja mkubwa wa vioo. Kufika hapo tu mlango ukajifungua na wote wakaingia ndani wakiwaacha walinzi nje. Kutoka hapo wakaongoza mpaka ndani ya lifti ambayo iliwapaleka mpaka ghorofa ya saba. Wakashuka na kupokewa na watu wengine, hawa ndio waliomchukua masimba huku wale waliokuja naye wakirudi na ile lifti. Bado akili ya masimba ilikuwa haipo katika utimamu wake. Alitambua sehemu alipo, aliitambua kwa kuwa hata yeye alikuwa jasusi. Lakini kitendo cha kuletwa ndani ya jengo hilo akichanganya na maneno ya Chief, alitambua kuwa lazima kuna jambo kubwa nyuma ya pazia. Akajiambia asubiri, alikuwa akiamini subira tu ndio ingeweza kumfanya ajue kile kinachoendelea. Watu hawa waliomuongoza kwa mara ya pili, walikuwa zaidi ya watu, hawa hawakuwa hata na tabasamu. Kila mmoja alikuwa akiatizama kila kinachotokea. Macho yao yalikuwa yakizunguka kama kinyongo. Yalimtizama na kumchunguza, yalimuangalia kwa kina. Hata pale macho yao yalipokuwa yakitizamana, kila mmoja alimtambua mwenzake.

Wakaufikia mlango mwingine, mlango huu haukufanana na kote walikopita, mlango huu haukuonekana kama ulikuwa mlango, lakini kule kukanyaga sehemu ya nje kuukaribia, kukaonekana kitu mfano wa shimo. Masimba akasita kuingia, akataka Kurudu nyuma. Hakufanikiwa hilo, kitu kizito kikatua tena kichwani. Akakiona kiza mbele yake. Akajaribu kupambana na giza lile, lakini akashindwa. Akaruhusu Macho Yake Kuingia giza. NI KWELI YAKAINGIA GIZA. HAKUJUA KILICHOENDELEA.
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 017

Alipambana akikataa giza kuuchukua mwanga wa mboni za macho yake, lakini haikusaidia kitu. Akakubali giza liyafunike macho yake. Na kweli ndivyo ilivyokuwa.

Alikuja kushtuka baada ya masaa mawili na kujikuta katika chumba kidogo. Chumba ambacho hakikuwa na kitanda isipokuwa maji tu. Tena maji ya baridi kupindukia. Mwanzo wakati anapatwa na fahamu alidhani labda alikuwa pembezoni mwa bahari ya hindi kutokana na maji yale. Akafumbua macho zaidi na zaidi, akayaona mazingira yale. Akahisi kukata tamaaa. Aliyajua matumizi ya chumba kile. Hakuna mtu ambaye aliwahi kutoka akiwa hai kati ya wote walioingizwa. Akainua kichwa chake na kuangalia juu, akakumbuka mengi aliowahi kulifanyia taifa lake, akakumbuka aliponusurika vifo mara kadhaa kwa sababu ya usalama wa taifa lake. Lakini yote yamesahaurika, lakini yote yalisahaulika kwa sababu ya watu wachache. Hata yeye alipelekwa ndani ya chumba kile ambacho hutambulika kama kuzimu. Alitakiwa naye afe, alitakiwa naye asirudi akiwa hai. Bado maji yaliendelea kumtesa na kumsulubu. Akainua macho na kutizama mwisho kabisa wa chumba kile. Aliamua kujaribu bahati yake, hakutaka kamwe kufa kikondoo, hakuamini kama angeshindwa kutoka pale. Aliamini atatoka tena atatoka akiwa salama. Akauvaa ujasiri na kuutoa uoga na ukataji tamaaa. Akainuka kutoka pale chini, akasimama kwa muda akiendelea kutupa macho yake kila pembe ya chumba kile. Akaunyoosha mwili wake kuupima kama una nguvu, aliporidhika akaanza sasa kutembea ndani ya kichumba kile. Kwa kuwa maji yalikuwa yamejaa mpaka kiunoni, hakuwa akiona chini alipokuwa akitembea. Alipokuwa akipiga hatua nyingine akajikuta akijikwaa kwenye kitu mfano wa mwili wa binadamu. Hilo likamfanya asite kuendelea kutembea, alikuwa amesimama akijishauri kitu. Alishaamua kufanya chochote, akili yake ikahitaji kufanyakazi mara mia zaidi ya kawaida yake. Hakutaka kushughulika na kitu mfano wa mwili wa binadamu aliyoukwaa. Alihitaji kufanya kitu kikubwa cha kumuondoa pale ndani. Akajaribu tena kutembea lakini safari bado alikikanyaga kile kitu mfano wa mwili wa binadamu. Kitu kama hisia kikamjia kichwani, hisia ya kwamba mtu huyu anaweza kumsaidia. Kwa kuwa siku zote aliziheshimu hisia zake, Masimba akainama na kuanza kutafuta chini ya maji. Kweli mikono yake ikagusa mwili wa binadamu. Baada ya kuugusa, akahakikisha mikono yake inaukamata ule mwili na kuanza kuusimamisha. Alipambana kwa muda na alipofanikiwa kuusimamisha akashangaa kumuona mtu anayemjua. Mwili wa mtu yule ulikuwa ni wa mmoja kati ya vijana ambao walikuwa wakimsaidia katika kazi yake.

Hilo hakulitegemea, kengele za hatari zikakigonga kichwa chake. Mmoja kati ya vijana waliokuwa wakimsaidia kazi kuuawa, alijua ilikuwa ni mbinu ya watu waliomfikisha pale. Alitambua vijana wote aliokuwa anasaidiana nao watauawa iwapo kama yeye ataendelea kuwepo pale mahabusu ya kuZimu. Akaendelea kuutizama wili wa kijana yule, hasira zikaonekana usoni. Kuuawa kwa maafisa usalama wa taifa kwa sababu ya manufaa ya watu wachache kulimpa sana hasira. Aliitambua hizi zilikuwa hila za Jimmy Lambert na maafisa waandamizi wa serikali. Alijua wote hawa walikuwa wakishinikizwa kusema wapi ulipo mzigo wa madawa ya kulevya aliouchukua nyumbani kwa Jimmy. Hilo likamfanya aihisi hatari hata kwa teddy, alihisi hata yeye ipo hatari atageukwa na kitakachofuatia ni yeye kupotezwa kama walivyofanya kwake. Kwa mara ya kwanza alitamani amuone teddy amwambie, kwa mara ya kwanza alitaka kumwambia teddy hatari iliombele yake. Alitaka kumwambia ukweli wa mambo. Lakini angetokaje wakati yupo kuzimu, alitokaje wakati muda mfupi ujao atakuwa maiti. Masimba akasonya huku akikifanya kitu ambacho hakuwa amekiwaza. Mikono yake ilizama kwenye mavazi ya marehemu yule. Akahisi kukigusa kitu katika mavazi ya marehemu yule. Akaongeza kasi ya mikono punde akakitoa kitu kile ambacho kilikuwa mfano wa golori. Tabasamu likachanua usoni mwake. Kilikuwa kitu maalum cha kufungulia sehemu zisizowezekana. Kitu ambacho hutumiwa sana na mashirika makubwa ya Kijasusi Hasa CIA na M15 pamoja na M16 ya Uingereza. Akakitizama kwa muda, harafu akakiwasha na kuanza kukizungusha kwa mikono yake akikielekeza kila upande. Sekunde kumi hazi kufika, maji yote yakapotea kisha chini kwa pembeni pakaachia. Mlango mkubwa ukaonekana mbele yake. Hakutaka kusubiri kwa kuwa alitambua huwa kuna muda maalumu. Sekunde ya kumi na mbili alikuwa nje ya chumba kile akitembea kuifuata korido ambayo ilikuwa akielekea kama Chini ya ardhi. Hakuwa na bastola, hakuwa na silaha ya aina yoyote, lakini alikuwa tayari kwa lolote. Jengo lillikuwa kimya kanakwamba hapakuwa na mtu ndani yake. Macho yalikuwa yakiangalia kila kona ya Jengo. Muda mfupi alikuwa ameibukia sehemu ambayo haikuwa kimya. Sauti za watu zilikuwa zikisikika kwa umbali mfupi kutoka mahala aliposimama. Wakati akifikiria nini afanye akavisikia vishindo vya mtu akisogea mahala pale. Akajiandaa kumkabili kwa mikono yake. Punde akamuona mtu akipita, alikuwa mwanamke. Alionekana na mlinzi wa Jengo lile. Alikuwa na Bunduki aina ya Oxcelf SG mkono. Alikuwa akitembea akiangalia huku na huko. Masimba akaona ulikuwa muda sahihi wa kufanya kitu. Alichokifanya ni kumtokea yule msichana kwa nyuma na kumpigia mluzi. Msichana yule akageuka akidhani aliitwa na mwenzake. Lakini alijikuta akikutana na flying kicks kutoka kwa masimba. Kwa kuwa hakutarajia kitendo kile, mwanamke yule akajikuta akishindwa kuzuia mapigo yale, na kuruhusu mateke yale kumtupa chini kama furushi.
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 017

Alipambana akikataa giza kuuchukua mwanga wa mboni za macho yake, lakini haikusaidia kitu. Akakubali giza liyafunike macho yake. Na kweli ndivyo ilivyokuwa.

Alikuja kushtuka baada ya masaa mawili na kujikuta katika chumba kidogo. Chumba ambacho hakikuwa na kitanda isipokuwa maji tu. Tena maji ya baridi kupindukia. Mwanzo wakati anapatwa na fahamu alidhani labda alikuwa pembezoni mwa bahari ya hindi kutokana na maji yale. Akafumbua macho zaidi na zaidi, akayaona mazingira yale. Akahisi kukata tamaaa. Aliyajua matumizi ya chumba kile. Hakuna mtu ambaye aliwahi kutoka akiwa hai kati ya wote walioingizwa. Akainua kichwa chake na kuangalia juu, akakumbuka mengi aliowahi kulifanyia taifa lake, akakumbuka aliponusurika vifo mara kadhaa kwa sababu ya usalama wa taifa lake. Lakini yote yamesahaurika, lakini yote yalisahaulika kwa sababu ya watu wachache. Hata yeye alipelekwa ndani ya chumba kile ambacho hutambulika kama kuzimu. Alitakiwa naye afe, alitakiwa naye asirudi akiwa hai. Bado maji yaliendelea kumtesa na kumsulubu. Akainua macho na kutizama mwisho kabisa wa chumba kile. Aliamua kujaribu bahati yake, hakutaka kamwe kufa kikondoo, hakuamini kama angeshindwa kutoka pale. Aliamini atatoka tena atatoka akiwa salama. Akauvaa ujasiri na kuutoa uoga na ukataji tamaaa. Akainuka kutoka pale chini, akasimama kwa muda akiendelea kutupa macho yake kila pembe ya chumba kile. Akaunyoosha mwili wake kuupima kama una nguvu, aliporidhika akaanza sasa kutembea ndani ya kichumba kile. Kwa kuwa maji yalikuwa yamejaa mpaka kiunoni, hakuwa akiona chini alipokuwa akitembea. Alipokuwa akipiga hatua nyingine akajikuta akijikwaa kwenye kitu mfano wa mwili wa binadamu. Hilo likamfanya asite kuendelea kutembea, alikuwa amesimama akijishauri kitu. Alishaamua kufanya chochote, akili yake ikahitaji kufanyakazi mara mia zaidi ya kawaida yake. Hakutaka kushughulika na kitu mfano wa mwili wa binadamu aliyoukwaa. Alihitaji kufanya kitu kikubwa cha kumuondoa pale ndani. Akajaribu tena kutembea lakini safari bado alikikanyaga kile kitu mfano wa mwili wa binadamu. Kitu kama hisia kikamjia kichwani, hisia ya kwamba mtu huyu anaweza kumsaidia. Kwa kuwa siku zote aliziheshimu hisia zake, Masimba akainama na kuanza kutafuta chini ya maji. Kweli mikono yake ikagusa mwili wa binadamu. Baada ya kuugusa, akahakikisha mikono yake inaukamata ule mwili na kuanza kuusimamisha. Alipambana kwa muda na alipofanikiwa kuusimamisha akashangaa kumuona mtu anayemjua. Mwili wa mtu yule ulikuwa ni wa mmoja kati ya vijana ambao walikuwa wakimsaidia katika kazi yake.

Hilo hakulitegemea, kengele za hatari zikakigonga kichwa chake. Mmoja kati ya vijana waliokuwa wakimsaidia kazi kuuawa, alijua ilikuwa ni mbinu ya watu waliomfikisha pale. Alitambua vijana wote aliokuwa anasaidiana nao watauawa iwapo kama yeye ataendelea kuwepo pale mahabusu ya kuZimu. Akaendelea kuutizama wili wa kijana yule, hasira zikaonekana usoni. Kuuawa kwa maafisa usalama wa taifa kwa sababu ya manufaa ya watu wachache kulimpa sana hasira. Aliitambua hizi zilikuwa hila za Jimmy Lambert na maafisa waandamizi wa serikali. Alijua wote hawa walikuwa wakishinikizwa kusema wapi ulipo mzigo wa madawa ya kulevya aliouchukua nyumbani kwa Jimmy. Hilo likamfanya aihisi hatari hata kwa teddy, alihisi hata yeye ipo hatari atageukwa na kitakachofuatia ni yeye kupotezwa kama walivyofanya kwake. Kwa mara ya kwanza alitamani amuone teddy amwambie, kwa mara ya kwanza alitaka kumwambia teddy hatari iliombele yake. Alitaka kumwambia ukweli wa mambo. Lakini angetokaje wakati yupo kuzimu, alitokaje wakati muda mfupi ujao atakuwa maiti. Masimba akasonya huku akikifanya kitu ambacho hakuwa amekiwaza. Mikono yake ilizama kwenye mavazi ya marehemu yule. Akahisi kukigusa kitu katika mavazi ya marehemu yule. Akaongeza kasi ya mikono punde akakitoa kitu kile ambacho kilikuwa mfano wa golori. Tabasamu likachanua usoni mwake. Kilikuwa kitu maalum cha kufungulia sehemu zisizowezekana. Kitu ambacho hutumiwa sana na mashirika makubwa ya Kijasusi Hasa CIA na M15 pamoja na M16 ya Uingereza. Akakitizama kwa muda, harafu akakiwasha na kuanza kukizungusha kwa mikono yake akikielekeza kila upande. Sekunde kumi hazi kufika, maji yote yakapotea kisha chini kwa pembeni pakaachia. Mlango mkubwa ukaonekana mbele yake. Hakutaka kusubiri kwa kuwa alitambua huwa kuna muda maalumu. Sekunde ya kumi na mbili alikuwa nje ya chumba kile akitembea kuifuata korido ambayo ilikuwa akielekea kama Chini ya ardhi. Hakuwa na bastola, hakuwa na silaha ya aina yoyote, lakini alikuwa tayari kwa lolote. Jengo lillikuwa kimya kanakwamba hapakuwa na mtu ndani yake. Macho yalikuwa yakiangalia kila kona ya Jengo. Muda mfupi alikuwa ameibukia sehemu ambayo haikuwa kimya. Sauti za watu zilikuwa zikisikika kwa umbali mfupi kutoka mahala aliposimama. Wakati akifikiria nini afanye akavisikia vishindo vya mtu akisogea mahala pale. Akajiandaa kumkabili kwa mikono yake. Punde akamuona mtu akipita, alikuwa mwanamke. Alionekana na mlinzi wa Jengo lile. Alikuwa na Bunduki aina ya Oxcelf SG mkono. Alikuwa akitembea akiangalia huku na huko. Masimba akaona ulikuwa muda sahihi wa kufanya kitu. Alichokifanya ni kumtokea yule msichana kwa nyuma na kumpigia mluzi. Msichana yule akageuka akidhani aliitwa na mwenzake. Lakini alijikuta akikutana na flying kicks kutoka kwa masimba. Kwa kuwa hakutarajia kitendo kile, mwanamke yule akajikuta akishindwa kuzuia mapigo yale, na kuruhusu mateke yale kumtupa chini kama furushi.
naomba uwe unanitagg
 
NITAKUPA TU

SEHEMU YA 018

Yalikuwa mateke mazito kwake, mateke ambayo yalipigwa katika aina ya kushtukiza. Alianguka kama furushi la mahindi. Hakuweza kuinuka. Alikuwa ametulia akionyesha kupotewa na fahamu. Masimba hakusubiri, alimfuata pale chini kisha kumpekua. Vitendo vyote hivyo vilitendeka katika muda mfupi tu. Alichukua bastola ambayo aliikuta kwenye mavazi ya binti yule, akaondoka akimuacha amelala sambamba na bunduki yake. Kwa kuwa alikuwa analitambua jengo lile, na kwa vile alishawahi kupita katika majengo yanamna ile. Haikuwa kazi ngumu kuzikwepq camera za usalama ndani ya jengo lile. Safari hii aliubadilisha mwelekeo, aliubadilisha mwelekeo sababu hakutaka kuua ama kukutana na wanausalama wasiolijua tatizo. Alitaka kuondoka bila kumwaga damu ya mtu isipokuwa pale itakapobidi kufanya hivyo. Akachepuka hapa na kutokea pale, mpaka alipofika karibu na lango la kutokea baharini ndipo aliposikia king'ora cha hatari. Hapo akahisi kwamba alikuwa hatarini. Akaondoka akiongeza kasi kuwahi kutoka ndani ya jengo. Hakutaka kukamatwa tena, hakutaka kurudi tena mikononi mwa watu wa usalama wa taifa. Alitaka kwenda kuwafikishia ujumbe wale waliomsingizia. Wale waliomuwekea mtego na kusababisha yeye kukamatwa..

******

Muda ulikuwa unakwenda lakini bado hakumuona Masimba, alikuwa amezoea kutokumuona masimba akiwa nje ya nyumba, lakini hili la leo lilimshangaza na kumtia wasiwasi. Matukio ya muda mfupi uliopita, kisha kutokufika kwa masimba mpaka muda ule, ni kitu ambacho kilimpa wasiwasi. Akaendelea kuivuta subira huku muda wote macho yake yakiitizama saa iliokuwa ukutani. Muda uliendelea kusogea, hakumuona Masimba, hakuiona ishara kwamba masimba atarudi. Hilo likaufanya usingizi wake upae, hakuiona sababu ya kulala. Kwa mara ya kwanza alikuwa akimuhitaji Masimba kuliko siku yoyote nyingine. Angelalaje wakati masimba hakurudi. Angelalaje wakati amegeukwa na watu aliowaamini? Akainuka kutoka kitandani kwa mara nyingine. Hakuuona usalama wa kuendelea kuwepo pale. Akayapitia mavazi yake sambamba na bastola zake mbili. Akazivuta hatua kuliacha jumba lao. Wakati anamaliza kufunga mlango wa nje akausikia mngurumo wa magari, magari zaidi ya moja, michuno ya matairi ndio kitu pekee kilichomfanya Teddy ahisi uhatari. Uhatari ambao alianza kuuona pale watu waliovalia suti nyeusi wakipaa angani na kutua ndani katika namna inayovutia, namna ambayo ingekuwa burudani kama ungekuwa ukiitizama. Teddy hakuwa mgeni na kikundi hiki, kikundi maalum cha kulinda viongozi wa taifa hili. Kuwaona wakitua pale katika aina ile, lilikuwa jibu kuwa Masimba ameshageukwa, masimba ameshaharibu. Kutua kwa watu wale kukafuatiwa na kitendo ambacho kilimuacha Teddy akiwaangalia. Walipotua kwa ndani kila mmoja alikuwa akichupa katika namna yake na kwa upande wake, hata walipomkaribia Teddy hawakuonyesha kutaka utani. Midomo ya bastola ilielekezwa kwake, macho ya watu yakimtizama katika aina ya kumuuliza maswali. Ni katika maswali hayo kupitia macho yao Teddy alipohisi kitu. Kitu ambacho hakikuwa cha kawaida. Masimba hakufika, watu kuivamia nyumba yao, gari yao kulipuliwa na sasa kuvamiwa na kikosi maalum cha kumlinda Rais ni suala zito sana. Aliiona siku ile haikuwa nzuri kwako, haikuwa nzuri kwa kilichotokea. Macho yalikuwa yakimuangalia yeye kwa aina ya maswali. Naye akajibu kwa aina ya sijui kwa kutumia macho. Hawakutaka kumsikiliza, wawili wakapita huku wangine wakiendelea kumuweka kati. Hazi kupita sekunde hata ishirini walikwisha toka wakiwa na baadhi vitu mikononi mwao. Hawakuongea tena na mwanamke yule zaidi ya kumpita na kuondoka wakimuacha amesumama. Muda huo huo akayasikia magari yakiondolewa kwa kasi. Bado Teddy alikuwa ameduwaa, bado teddy alikuwa akisafiri mbali kimawazo. Kupotea kwa madawa ya kulevya, kushikiwa bastola na washirika wenzake haikuwa picha nzuri kwake. Alijua kutakuwa na msukumo kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine. Lakini bado hakulipata jawabu, nani amelazimisha hili? Masimba atakuwa wapi muda huu? Kwa nini Kikosi maalum cha kumlinda Rais kiwe kwenye hili suala la kumtafuta masimba? Hayo na maswali mengine mengi ndio yaliomchanganya teddy.

Hakuona sababu ya kuendelea kubaki pale. Aliondoka usiku ule ule akiamua kwenda nyumbani kwa Jimmy Lambert. Aliamua kwenda huko kwa kuwa alitaka kuujua ukweli kuhusu hiki kinachoendelea kutokea. Pia alitaka kujua ni nani ambao walikuja nyumbani kwake. Ilikuwa safari ambayo alihisi ingekuwa ya Hatari. Wakati akiwa juu ya usafiri akielekea nyumbani kwa Jimmy, akamuona mtu, hakumtilia manani pale alipomuona mara ya kwanza, lakini akajikuta akimuangalia yule mtu ambaye sasa alikuwa akitembea kama mlevi. Macho yake yakavutika kumuangalia mtu yule tena na tena. "Masimba!? Yalikuwa maneno pekee kutoka kinywani kwake. Kilichofuata ni kuufungua mlango ili kushuka,lakini ya kufanya hivyo akaliona gari, gari ambalo hapo mwanzo aliliona karibu na nyumbani kwake. Hapo akagundua alikuwa akifuatiliwa. Mawazo yakumfuatilia yule mtu mlevi yakaisha. Alimtambua kuwa mtu yule ni Masimba. Alimtambua kwa urahisi kwa kuwa alimjua masimba.
******

Aliendesha gari mpaka maeneo ya Ambience club, akaipaki gari na kushuka kisha kuongoza moja kwa moja mpaka ndani ya ukumbi. Akatafuta sehemu nzuri ya kukaa. Katika kuangaza kwake akaiona meza moja ikiwa tupu. Akasogea hapo, akavuta kiti nakukaa. Baada ya kukaa hapo, mhudumu akasogea na kumuuliza kinywaji gani ambacho angetaka kutumia. Teddy akamjibu na baada ya hapo akaendelea kutulia akiwaza na kuwazua kile alichokiona kule njiani. Masimba akiyumba njiani, masimba akitembea katika aina hii ya ulevi? Kuna nini kimemtokea Masimba? Kuna nini kimetokea nyuma ya hiki anachokifanya masimba? Ina maana kuna hili tu ama kuna kingine nyuma? Mawazo yake hayo yakakatizwa na mtu aliyemuona akiingia. Huyu alihisi kumuona mahala, wakati akiendelea kuangalia hilo akamuona mtu mwingine akiingia. Huyu alikuwa amejibadilisha sana. Licha kujibadilisha huko lakini alimjua licha ya kujibadilisha kwake. HUYU ALIKUWA MASIMBA

KESHO
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 019

Licha ya kujibadilisha sana, licha ya kuonekana kama mtu mwingine, lakini kwa teddy haikuwa hivyo. Alimjua Masimba, alimjua kama alivyokuwa akiujua mwili wake. Akayahamisha macho yake sasa akimtizama mtu yule aliyeingia. Mtu ambaye aliwahi kumuona sehemu, mtu ambaye uingiaji wake ulikuwa wa kinamna fulani. Bado mtu yule alikuwa amesimama akiangaza kama mtu mwenye kutafuta kitu. Hilo lilimpa uhakika kuwa kijana yule alikuwa akimtafuta yeye, lakini hili la kufika pale kwa masimba nalo hilo kiasi fulani likakipa kichwa wakati mgumu wa kufikiria. Muda mfupi alikuwa akitembea kama mlevi akiyumba, lakini muda huu hakuwa yule wa kuyumba. Na alifika pale akiwa mwingine. Jibu lake lilikuwa moja tu, jibu lake lilikuwa ni kwamba, masimba alimuona wakati anaondoka na ile gari, masimba alikuwa karibu na nyumbani na inawezekana masimba alishuhudia kila kitu kilichotokea. Hilo likausisimua mwili wake, alijikuta tabasamu matata likichanua usoni mwake. Lakini licha ya tabasamu hilo, macho yake hayakuganduka kumuangalia kijana yule. Alikuwa akimtizama kwa uhuru kutokana na uwepo wa kiza sehemu alipokaa. Kijana yule baada ya kuangaza huku na huko bila kuona kitu, akatoka ndani ya ukumbi akionyesha kuelekea sehemu za nje. Bado Teddy alijipa subira. Alitaka kuhakikisha kama kuna watu wengine ama. Licha ya kuvuta subira kwa dakika mbili, hakumuona mtu yeyote akitoka kumfuata kijana aliyetoka. Hilo likamfanya atake kusimama kuelekea huko, lakini kabla ya kufanya hivyo alitaka kumuangalia masimba kama alikuwepo ama lah! Akafanya hivyo, lakini hakumuona masimba, akaangaza tena na tena lakini bado hakumuona Masimba Akainuka naye akielekea nje ya ukumbi wa club. Alitembea akidance kufuata midundo ya muziki uliokuwa ukiporomoshwa. Alipotokea nje, macho yake yakapokewa na makelele ya watu wakionekana kupagawa. Hilo likamvutia, akaamua kuelekea kule zinapotokea kelele. Muda wote mikono yake ilikuwa tayari kwa chochote ambacho kingetokea. Akafanikiwa kujipenyeza katikati ya umati na kusogea mpaka mbele kabisa. Mwili wake ukamsisimka baada ya kuuona mwili wa mtu ukiwa umelala kifudifudi huku sehemu ya mgongoni kukiwa na mpini wa kisu kuonyesha mtu yule alikuwa amechomwa. Akasogea zaidi na zaidi mpaka karibu kabisa. Alikuwa yule yule kijana aliyetoka ndani muda sio mrefu akiwa amelala katikati ya dimbwi la damu. Hilo likamshangaza, katika yote aliyoyategemea hakuwaza kama mtu yule angeuawa kwa aina ile. Swali likabaki kwake ni nani aliyemuua kijana huyu? Swali hilo likamfanya arudi tena ndani ya Club, kurudi kumuangalia masimba kama yupo ama lah. Alitaka kwenda kumuangalia masimba. Kitendo cha masimba kuingia na kijana yule, kisha muda mchache mtu huyu auawe katika namna hii! Hapo akajua kuna kitu. Teddy akahisi akili yake ikishindwa kufanyqkazi. Mambo yaliomtokea siku hii ya leo yalikivuruga kichwa chake, alitakiwa kutulia kwanza, alitakiwa kuituliza akili yake kwanza. Alitambua anapitia katika wakati mgumu na wahatari sana. Akaingia tena ukumbini safari hii akiwa makini tofauti na mwanzo. Macho yake yalimtizama kila mtu, yakamdadisi na kumchunguza. Muziki bado ulikuwa ukiporomoshwa, watu walikuwa wakiserebuka pasipokujua chochote kilichotokea nje. Akajimwaga katikati akinengua kwa staili hatari sana. Alikuwa akisakata katika staili ambayo ilisababisha macho kadhaa ya watu wamtizame na wamuangalie. Wanaume wa kwale walianza kukitamani kiuno cha teddy. Kule kukata kiuno na kwenda mpaka chini kiliwafanya watu wa wehuke. Sasa vitu havikalika.

Hilo halikuwastaabisha hao tu, hata masimba aliyekuwa amebana pembeni alikuwa akimtizama mama watoto wake akikizunguusha kiuno. Hata pale alipokuwa akienda mpaka chini bado macho yake hayakuamini. Ni kweli ni mume mtarajiwa wa teddy, nikweli anaishi na Teddy lakini hakuwahi kufikiria kama ni mtamu kiasi hiki katika kudance, hakufikiria kama ule utamu wa kitandani una utamu mwingine. Hakumwangalia teddy tu, macho yake yaliangaza kila upande akiutizama usalama wa mwanamke huyu. Alitizama kama ataona hila zozote lakini hakuziona.

*********

"Haiwezekani, nasema tena haiwezekani!!!" Ilikuwa sauti ya jimmy lambert ikinguruma katika chumba kimoja chenye watu wasiopungua watano. Alikuwa amechukia kupita kiasi. Mishipa ilikuwa imemtoka usoni huku mikono yake ikiwa imekunjwa. Alikuwa akitoka upande huu wa chumba kwenda upande ule. Alikuwa amechanganyikiwa vya kutosha. Taarifa kuwa Masimba ametoroka akiwa chini ya ulinzi wa Idara ya Usalama wa Taifa ilimchanganya sana. Hakuitegemea hiyo taarifa, alichokitegemea kilikuwa ni kupatikana kwa mzigo wao ambao uliibiwa na Masimba. Lakini hazikuwa taarifa hizo, hazikuwa taarifa nzuri kwake.

"Mtu anatoroka chini ya usalama wa taifa? Mtu anatoroka pasipokuua? Mtu ambaye anaishi na mamilioni ya pesa yetu. Kwa nini asingeuawa tu? Aliendelea kufoka huku akiendelea kuzunguka mle chumbani. Wajumbe wengine walikuwa kimya wakumuangalia. Hakuna ambaye aliinua kinywa chake kumjibu kitu chochote. Kila mmoja alikaa kimya akifikiria jinsi ya kujinasua katika hili.

"Tumemkosa Masimba, na mpaka sasa hajulikani aliko, pia nina mashaka teddy amegundua kitu kutoka kwetu. Ameonekana Ambience club akicheza na akionekana ni mwenye furaha sana. Yaani sisi tunaumiza vichwa huku, mwenzetu anafurahi huk.... alikatizwa na mlio wa simu yake ikiitakuonyesha kwamba alikuwa akipigiwa. Aliichomoa mfukoni kabla ya kupokea akaangalia jina la mpigaji. SILENT KILLER lilisomeka Jina juu ya kioo cha simu yake. Jimmy akasita kuipokea simu. Hakujua kwa nini lakini alihisi haikuwa simu ya usalama. Macho yake yaliwaka mithili ya paka, pia alikuwa akiwatizama wajumbe wenzake mmoja baada ya mwingine. Hata wao walimtizama sura zao zikiacha maswali, sura zao zikiachwa na mshangao. Hata simu ilipokatwa na mpigaji kurudia tena ndipo Jimmy akakurupuka na kuipokea. Hakuongea kitu kingine zaidi ya kuitoa simu sikioni na kuwageukia washirika wenzake. Huku midomo ikimtetemeka kwa hasira akajiondoa pale na kusogea kisha kujibweteka Juu ya kitu.

"Saidi Mbega ameuawa muda huu katika mazingira ya kutatanisha, nje ya Ambience Club. Vijana wetu waliweka mtego wa kumnasa Teddy lakini kabla hawalifanya hilo, wakapewa taarifa za kifo cha mwenzao. Aliongea Jimmy akionyesha kuchoka kimwili, kiakili mpaka kimawazo.

Ilikuwa taarifa iliyopokelewa kwa mshtuko na wajumbe wale. Walitambua kuwa wanatakiwa kufanya kazi usiku na mchana kufanikisha kujua pale alipo masimba.

********

Sauti za mbwa zilikuwa pekee zikiosikika usiku ule, hapakuwa na sauti ya binadamu katika eneo lote. Ukimya ulikuwa umechukua sehemu kubwa ya sehemu yote ya mikocheni. Hilo halikumsumbua sana Teddy, alikuwa hapo kwa kazi moja, kazi ya kuonana na Jimmy. Kuongea na Jimmy sambamba na kujibiwa maswali yake. Ukimya wa eneo na giza la usiku vilimsaidia teddy kuifikia nyumba ya Jimmy pasipo kizuizi chochote. Hata alipozunguka kwa kupita kwenye vivuli vya miti bado hapakuwa na kizuizi. Bado hakupata ugumu wowote. Hilo likamfanya apate mashaka. Mashaka ambayo yalimfanya ajiulize swali. Wako wapi walinzi wa Jimmy? Kabla hajapata majibu Akahisi kitu cha baridi kikimgusa kisogoni. TULIA HIVYO HIVYO...
 
Story imefika sehemu nzuri sana,I hope Teddy atacheza Karate za hatari kujichomoa hapo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom