Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

Wakuu mi nna wazo!! Naamin watunzi wote wanaopost riwaya humu jf wanaweza kuchanganya mawazo Na kui develop hii riwaya ya Marehemu IBRA! Nas nashauri kuwa wenzetu mnaotunga Na kupost mkutane may be PM au tuunde kundi WhatsApp ili story hii ikamilike Na isiletwe humu kwanza hadi tujichange tutengeneze kutabu tumuenzi mwenzetu huyu kwani ndoto yake ulikuwa kutoa kitabu!! Angalizo! Kama kuna msomaji ambaye anaifahamu familia atusaidiw kuishirikisha kwenye kwa Jambo hili ili kurahisisha mambo ya management ! Ni hayo tu
 
Kwa huzuni naamua Ku unwatch thread, hakika kaburi ni katili, kaburi dhulmat, pumzika kwa amani kaka IBRA Mungu atujalie mwisho mwema
 
R.I.P kaka Ibra njia ni moja nasi tupo safarin twaja,
Mwanzo wakati naanza kusoma hii story sikujua kama mtunzi ameshatangulia mbele za haki.
Inauma sana unapokuwa na ndoto lakin ukaondoka bila kuzitimiza,
Pumzika kwa Aman.
 
Aah...hii riwaya ilikuwa kiboko..basi tu..hakuna hata wa kuendeleza.
RIP...kipenzi...
Kaondoka mapema na kipaji chake..
 
Ndiyo mkuu Ibra87 ni Mimi haswaaa vipi umeipenda kachero wetu??

Ndiyo mkuu Ibra87 ni Mimi haswaaa vipi umeipenda kachero wetu??
81ea8bff350cc07a98f13929537b99fe.jpg
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 086

"Tulieni Hivyo hivyo, kisha wewe tupa silaha yako chini." Ilikuwa sauti kutoka nyuma yao. Sauti ambayo haikuonyesha utani ndani yake. Veronica Akatii kwa kuitupa Bastola Chini. Akatulia tuli huku akiamini kuwa inaweza kuwa amesalitiwa na huyu Dereva. Wakati akiwaza hilo akakatishwa na sauti ya mtu huyu. "Nyie ni nani? Na kwa nini mko hapa?. Veronica akabaki kimya huku akimuangalia dereva ambaye alimtia tumaini kwa kuwa hakuonyesha kujali. "Ni mimi Charles, nimemleta huyu dada ana mgonjwa ambaye hali yake sio nzuri." Alijibu dereva huku akionyoosha kidole kama ishara ya kumuonyesha. Huku akiwa amekamatia Sub Machine Gun Mtu yule aliyekuwa akionekana kama mtu mzima. Kitendo cha kuiona ile bunduki kulimpa Veronica hisia. Hisia kuhusu mtu huyu ambaye alijibadilisha ili aonekane Mganga. Mganga gani amejengeka kimazoezi kwa aina Hii? Mganga gani ameweza kuikamata SMS kwa Staili hii? Yalikuwa maswali ambayo hayakuwa na majibu. Maswali magumu. Kwa mara nyingine sauti ya mwanaume huyu ikatamalaki katika ngoma za Masikio yao. "Muingizeni Ndani mtu huyu, fanyeni haraka." Veronica na dereva wakasaidiana kumuingiza Masimba ndani akiwa bado na Hali ile. Baada ya Masimba kuingizwa ndani. Taa za kijumba kile zikawashwa. Baada ya Taa kuwashwa, dereva na Veronica wakaangaliana. Kuangaliana kulikotokea baada ya mtu yule kumuita Jina Masimba. Veronica ndiye aliyeshikwa na mshangao kuliko hata dereva. Kile alichokuwa akikiwaza mwanzo, kitu ambacho alikuwa na uhakika nacho kuhusu mtu huyu. Alihisi alikuwa usalama , alihisi alikuwa ni mtu ambaye aliwahi kuwa sehemu fulani. "Masimba, masimba, unatatizo gani? " aliita mtu yule huku akimtingisha masimba. Lakini bado masimba hakuweza kuitika. Alikuwa ametulia kama Maiti.. Veronica bado alikuwa kwenye bumbuwazi. Bado alikuwa kwenye mshangao. Hata mwanaume yule alipoingia kwenye kichumba kidogo, bado Veronica alikuwa katika mshangao. Maswali lukuki yalikuwa yakikipita kichwani kwake. Bado alitaka kumfahamu huyu mtu, akalazimisha macho yake yamuangalie mwanaume huyu ambaye mara hii alikuwa ametoka akiwa na kiboksi mkononi. Hata huyu mwanaume naye akamtizama, akamtizama kwa aina ya kutaka Veronica ajue kuwa yeye alikuwa nani. Wakaangaliana tena na Tena. Veronica alikuwa akikitizama kile alichokuwa anataka kukijua. Alikuwa anamuangalia Mtu ambaye alikuwa ni mmoja kati yao. Macho yao yakatizamana tena na tena huku yakiongea. Mwanaume yule alimruhusu Veronica kusoma kila kilichopo ndani yake. Ni muda huo ambao Veronica akimtizama mtu huyu, akakiona kingine mkononi kwa Mtu yule. Kitu ambacho kilimthibitishia kile ambacho alihitaji kukijua. Mtu yule alikuwa ameishika sindano na kichupa chenye dawa ambayo ilitumika kutolea sumu kwa mtu yoyote ambaye angehisiwa kuchomwa sindano ya Sumu. Hakubisha kuwa huyu mtu alikuwa jasusi. Licha ya kuwa Jasusi, lakini bado hakujua alikuwa nani na alimtambuaje ama kumjua Masimba.

Baada ya kuishika ile sindano, mtu huyu akasogea mpaka pale alipolala masimba na kupiga magoti. Akaichoma sindano kwenye mfuniko wa kichupa na Kuivuta. Baada ya dawa kujaa kwenye bomba akautafuta mshipa mmoja mwilini na kuchoma ile sindano. Baada ya Kuchoma na kuiruhusu dawa kuingia mwilini mtu yule akainuka na Kuingia chumbani. Safari hii akatoka na kitu mfano wa kalamu, lakini ndani yake kukiwa na dawa ya Majimaji. Baada ya kufika hapo tena akautanua Mdomo wa Masimba kisha kuimimina Dawa kinywani. Baada ya kufanya Hivyo.. akamfunika vizuri kisha kukaa pembeni Yake. Macho yake yalikuwa yakimtizama masimba tu kwa muda wote. Yalikuwa yakimuangalia kanakwamba hakuwa akikiamini alichokuwa akikiona. Macho yake yalionyesha kitu ambacho kilimvuta Veronica. Macho ya mtu huyu yalikuwa yakiongea na mwili wa masimba. Hakuwa akiongea kwa mdomo lakini macho yake yalikuwa yakikizungumza kitu fulani. Baada ya Dakika kumi kupita huku ukangaliana kule kukiichukua sehemu yote ya kijumba na kuuleta Ukimya. Masimba akaanza kukohoa mfululizo. Tabasamu usoni kwa veronica halikukauka. Nguvu na imani kuwa masimba alikuwa salama ikarudi kichwani mwake. Lakini aliporudisha macho kwa mtu huyu bado alikutana na hali ile ile, bado mtu yule alikuwa akimuangalia masimba huku macho yake yakizungumza. Yakizungumza kile ambacho kila Veronica alipotaka kukisoma hakufanikiwa. Masimba akaendelea kukohoa mfululizo, damu ikishuka Kutoka mdomoni, damu ikiruka kila pale alipokuwa akikohoa. Kwa mara ya pili mtu huyu aliinua uso na kumuangalia Veronica, kisha dereva aliyemleta Veronica. "Mnaweza kuondoka sasa mkamuacha mgonjwa hapa. Veronica hutakiwi kulala hapa usiku huu. Hutakiwi kwa kuwa ulichokifanya unaweza kupewa Adhabu ya kifo. Unajua adhabu za Kundi la Mafia lilivyo." Yalikuwa maneno yaliompumbaza veronica, maneno yaliomshtua na hata kumtia baridi. Hakutegemea kujulikana mapema hivi. Hakutegemea mtu huyu angeweza kumjua hivi. Huyu ni nani? Lilikuwa Swali lililohitaji majibu kutoka Kwa Mtu Huyu. Lilikuwa swali ambalo majibu angeweza kuyapata kumtoka kwa mtu huyu. Mtu ambaye alionyesha kumjua kuliko mwenyewe anavyojijua. Veronica akabaki ameduwaa akimuangalia mtu huyu. Alikuwa akimuangalia katika namna ambayo Ilimfanya mtu yule atambue kuwa kuna kitu kinahitajika. "Hii kazi ni ngumu Veronica. Nilitambua Masimba alikuwa akipambana pasipo kumjua Teddy na Pasipokukujua wewe. Lakini hayo yote tutayaongea baada ya kuupata muda. Unatakiwa kuondoka hapa usijekulifanya suala hili kuwa kubwa." Aliongea yule mtu huku safari hii akihamisha macho yake kumuangalia Dereca. "Charles naomba umpeleke huyu dada mpaka dar es salaam. Pitia barabara zile zile ambazo tulikuwa tumepita." Alitoa maagizo mtu huyu huku akisimama na kuingia tena Chumbani akiwaacha Veronica na Charles wakiendelea kuangaliana. "Tuondoke Hapa Veronica. Aliongea Dereva yule akisimama tayari kwa kuondoka. Veronica naye akafanya hivyo.

******

"Nahitaji kumjua yule mtu." Aliongea Veronica akimwambia Charles walipokuwa Njiani kurudi Jiji dar es salaam. "Unadhani mimi namjua?" Akauliza Charles Huku akiwa kwenye usukani. "Nafikiri unamjua ama kama Humjui, basi utakuwa na ufahamu kidogo juu ya mtu yule." Akajibu Veronica. Charles hakuongea chochote akanyamaza kwanza akionyesha kufikiria kitu. "Simfahamu Zaidi ya hapo. Ila kuna wakati niliwahi kuhisi kuwa labda mtu yule alikuwa Usalama Wa Taifa ama mtu ambaye aliwahi kuwa katika Shughuli inayofanana na kitu kama hicho." Akajibu Charles. "Kitu gani kilichokifanya uhisi kuwa labda alikuwa mtu Wa Idara nyeti? Akaendelea kuuliza Veronica. "Kuna wakati nilikuwa nikikutana na watu fulani ambao ukiwaangalia unaweza kudhani ni Makamandoo wale tunaowaona kwenye TV. Kuna wakati nilikuwa nikikuta mpaka Raia Wa Kigeni." Akajibu Charles, majibu ambayo yalianza kumfanya Veronica Aanze kuhisi kuwa alikuwa sahihi kuwaza. " wewe ulijuana naye vipi? Akauliza Tena Veronica.

"Tulikutana kwenye bar moja maeneo ya bagamoyo mjini. Yeye alikuwa pembeni akiwa amekaa sambamba na Binti mmoja mwembamba hivi. Nilikuwa hapo nikipata moja moto moja baridi. Sasa wakati tuko hapo wakatokea wababe fulani wakataka kumchukua mwanamke yule ki nguvu. Ndipo hapo nilipomuona akifanya kile ambacho hufanywa na watu tunaowaona kwenye Video. Jamaa alikuwa akipiga Ngumi na Mateke kama Jean Claud Van Damme. Alikuwa akiruka hewani na samasoti kama Jet Li. Hapo ndipo kila mtu pale akashangaa. Kwanza muonekano wake ulionyesha kuwa alikuwa Mtu mzima. Lakini kile alichokuwa akikifanya pale utadhani alikuwa kijana. Basi baada ya Valangati ile kuisha wale watu wakatupotea katika mazingira fulani ambayo hakuna mmoja kati yetu kwenye ile Bar Alitegemea. Waliondoka mfano wa kuyeyuka. Ni katika kuondoka hapo ndipo nilipookota pochi yake ambayo alionyesha kuidondosha wakati wa purukushani. Pochi Hiyo ndiyo iliouleta ukaribu na mtu Huyu. Ukaribu ambao ulinikutanisha na watu wengi wa Ajabu. Pia kuna siku niliiokota Hii picha katika eneo lile." Aliongea Charles Akimkabidhi Veronica picha ndogo. Vero akaichukua kisha kwa kutumia Mwanga Wa Simu Akaiangalia. "The Bastard.....??? Ilikuwa sauti kutoka kwa Veronica Huku mshangao ukigubika uso wake. Macho yake yalikuwa yakiitizama Sura ya Mwanaharamu, macho yake yalikuwa yakiitizama Picha ya Nemisis. Macho yake yalikuwa yakimtizama mpelelezi Mashuhuli Afrika. "Kuna kitu ndani yake na kuna namna kwa mtu yule kuwepo pale msituni. Nataka kumfahamu kwa nini yuko pale na Kwa nini picha ya mtu huyu imekutwa pale." Aliongea Veronica Akionyesha kushangaa.

"Una mfahamu huyo mtu?" Lilikuwa swali kutoka kwa Charles. "Yeah namfahamu zaidi. Sasa nimepata picha na kujua ni kwanini mtu huyu ananijua kiasi hiki na kwa nini anamjua Masimba. Nitamjua tu Ni Nani." Akajibu Veronica huku akiiendelea kuitizama picha ile.

******

Mji wa bagamoyo na vitongoji vyake ulikuwa katika hekaheka kubwa kutoka katika vyombo vya dora. Askari wenye makwanda na waliovaa kiraia walikuwa wakizunguka katika Mji wote wa bagamoyo wakiwa na picha ya Masimba mikononi mwao. Idara ya usalama wa Taifa ilikuwa imesambaza wapelelezi wengi katika kila kona kunusa huku na huko. Taarifa ya kutoroshwa kwa Masimba iliitingisha Serikali sambamba na Idara zake. Mikutano mitatu ya Siri ilikuwa imekwishafanyika katika sehemu tatu tofauti. Kikao cha kwanza kilifanyika Katika Ubalozi wa Marekani, Cha pili kilifanyika Kwenye nyumba za Siri za Serikali. Wakati cha tatu kilifanyika Ikulu. Vikao vyote hivyo havikufikia muafaka baada ya washirika kuhisi kuwa kuna usaliti umefanyika mpaka kufanikisha kutoroka kwa Masimba. Kila sehemu ilikuwa ikipekuliwa na kila nyumba ilikuwa ikiangaliwa kwa namna ya pekee. Askari walikuwa wakihaha huku kila wakati wakipokea maelezo kutoka kwa wakubwa zao. Mpaka inafikia saa kumi za Jioni hapakuwa na fununu ya wapi pale alipo masimba. Camera za usalama ndani ya kambi ya Siri ya Usalama wa Taifa zilionekana kutokuchukua picha ya aina yoyote. Kingine ambacho kiliongeza ugumu walinzi ambao walikuwa zamu usiku huo kila mmoja alikutwa akiwa amekufa kwenye Chumba chake. Kila mmoja alikuwa amechinjwa shingo. Hilo likavifanya vikao kuendelea kuitishwa ikulu. Kwa mujibu wa taarifa ambazo ikulu na Idara ya Usalama ilikuwa nayo ni kwamba. Masimba Hakuwa na Uwezo wa kutembea wala kusimama. Pia walikuwa na Taarifa kuwa sindano aliyochomwa asingeweza kuchukua wiki atakuwa Ameshapoteza Maisha. Sasa kama Taarifa Imekuja kwamba Masimba Ametoroshwa, Kwa nini Walinzi Waliokuwa zamu wameuawa sehemu zao walipokuwa wanaishi? Ina maana hawakuuawa usiku, bali waliuawa asubuhi. Kama ni Asubuhi ni nani ambaye ameua? Inaonyesha huyu muuaji alirudi kuja kuufuta Ushahidi baada ya usiku kumtorosha masimba. Kama hivyo ndivyo ilivyokuwa, aliyefanya mauaji haya ni mtu anayefahamika. Ni mtu ambaye analifahamu suala hili. Yalikuwa mawazo ya wajumbe wote waliokuwepo katika kikao kile. Kikao ambacho kiliirudisha Taharuki miongoni mwao. Taharuki ambayo haikutakiwa kupewa nafasi kwa wakati huo. Simu zikapigwa sehemu mbalumbali za Nchi. Majasusi Wa Idara ya usalama wa Taifa walikuwa wakihaha kila kona. Wakati Ndani Ya Nchi ya Tanzania Msako ukiendelea. Teddy alikuwa ndani ya Jiji la Nairobi Akiwa na majasusi wa CIA sambamba na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani. Walikuwa katika kikao kizito kilichokuwa kikijadili kuhusu uwezekano wa kuendeleza Biashara na Nchi ya Tanzania. Pia alikuwa hapo kupokea Zawadi ambayo ilitolewa na Rais Wa Marekani kama Pongezi ya Kufanikisha kwake kuipata betri. Ni wakati wakijadili hilo, Teddy akapokea Taarifa kutoka kwa Marafiki zake. Ni taarifa hiyo ambayo ilimfanya asimame haraka. Usimamaji wake Ulimshangaza kila mmoja pale ndani. Hata macho ya wajumbe wale yalipomtizama Teddy, wakayaona Mabadiliko makubwa. Alikuwa amebadilika kama sio kuchanganyikiwa. Midomo yake ilikuwa ikicheza akitaka kuongea kitu. Lakini hakuweza kufanya hilo. Hakuweza kuongea Tena. Punde akautwaa mkoba wake na Kutoka Nje ya kikao pasipo kuongea chochote. Ilikuwa ni lazima Arudi Dar es Salaam kwa wakati huo. Alitaka kwenda kuhakikisha kile alichoambiwa. "Ni nani aliyemtorosha masimba na kuwaua Walinzi? Lilikuwa Swali lililomkuta Teddy Akiwa Ndani ya Tax akielekea uwanja wa Ndege wa Jomo kenyatta TAYARI KWA KURUDI TANZANIA.
Dah RIP ibra
 
[14:58, 18/02/2017] Ibrahim Masimba: NITAKUPA TU

SEHEMU YA 001

Mwandishi Ibrahim Masimba

*********
Alihisi ilikuwa sauti ya mwanamke, sauti ambayo mwanzo alidhani haikuwa ya mwanamke kutoka na usiku ule kuwa vigumu. Lakini sauti ile bado ilikuwa ikisikika katika ngoma za masikio yake. Sauti ya mwanamke akilia na kuomba msaada, sauti ikipiga kelele za hali ya juu kuonyesha kwanba kunakitendo kiovu kinatendeka. Bado hakuijali sauti ile, alichukulia kwamba labda atakuwa ni malaya amekula pesa za watu sasa analazimishwa kulipa. Bado akapuuza akitembea kuelekea nyumbani kwake. Licha ya kupuuza lakini safari hii, sauti ikasikika tena kwa karibu. Sauti ambayo ilipita masikioni na kwenda kuweka kituo ndani ya kina cha moyo wake. Sauti nayo ikazidi kuhanikiza, lakini safari hii kwa aina ambayo ili msisimua. Aina ambayo ilifanya kengele za hatari kugonga kichwani. Binti anayefukuzwa kulitaja jina lake usiku ule kulimpa mashaka makubwa. Kwa mara ya kwanza mkono wake ukashuka mpaka alipoihifadhi bastola yake. Kitendo cha kuitwa jina katika mazingira yale kulimpa hisia kuwa kulikuwa na namna, namna ambayo ilitengenezwa kwa aina fulani ya kutaka kitu kutoka kwake. Wamejuaje niko hapa? Walijuaje nitapita njia hii tena katika muda huu? Yalikuwa maswali yaliokisumbua kichwa chake, yalikuwa maswali yaliomfanya aziamini hisia zake, hisia ambazo hazikuwahi kumuangusha. Sasa akatembea kwa umakini mkono ukiwa juu ya Bastola. Hakujali tena kelele za mwanadada yule. Licha ya kutokuwa na ulahai wowote katika sauti yake, lakini hakutaka kuliamini hilo, akaendelea kutembea.. lakini hakufika popote akausikia mlio wa bastola, mlio ambao uliambatana na yowe, yowe kutoka kwa mwanadada yule. Kwa mara ya kwanza akageuka nyuma, akageuka kukiangalia kilichotokea nyuma.. naam akamuona mwanadada amelala chini tena barabarani. Hakuonekana kama alikuwa hai. Mbele kidogo ya ulipoangukia mwili wa binti yule, aliwaona wanaume wawili waliovalia makoti meusi wamesimama. Walikuwa wanaume hasa kwa kuwaangalia. Hakutaka kuupoteza muda, hakutaka kuupoteza muda kuwepo eneo lile. Akatokomea akiwaacha wanaume wale wamesimama wakimuangalia. Alitembea akijiuliza maswali mengi sana. Kama lengo lilikuwa ni yeye kwa nini wamemuua yule msichana? Walitaka nishuhudie kitu gani na kwa madhumuni yapi? Haiwezekani watoke huko kisha waje wamuulie mtu mbele yangu harafu mimi wasinifanye kitu, kuna zaidi ya hili. Alijisemea peke yake akiufungua mlango wa nyumba yake, akaingia ndani moja kwa moja akaenda kujibweteka kwenye kiti. Sauti ya mwanamke yule bado ilikuwa ikijirudia kichwani mwake, bado aliisikia bado masikioni mwake. Akajaribu kuivuta kumbukumbu ya sauti ile kuona kama angeugundua ulahai katika sauti ya mwanamke yule, lakini hakukuwa na kitu chochote kilichoashiria kwamba mwanamke yule alikuwa akimrahai. Ilikuwa sauti iliokatika ukweli, haikuwa na hata shaka ndani yake. Lakini sasa kwa nini mazingira yake yalikuwa ya kutilia mashaka? Hilo likamfanya ainuke na kuelekea bafuni ambapo alijimwagia maji kisha akarudi chumbani kwake. Akachagua mavazi ya kimichezo akavaa na baada ya hapo akachukua bastola yake na kutoka pale kuelekea kule alipoangukia yule mwanamke. Muda wote aliutamani ukweli wa jambo lile. Haikuwahi kutokea mtu kuuawa mbele ya macho yake. Hii ilikuwa mara ya kwanza na ilimtia mashaka sana. Alitaka kwenda kumuona marehemu, alitaka kumuona kwa kuwa aliamini angekipata kile ambacho kingemsaidia katika kumfahamu marehemu. Akaurusisha mlango kisha akalifunga geti kwa ndani kisha yeye akauparamia ukuta na kuangukia upande wa nje. Hii ndio ilikuwa njia yake awapo katika shughuli ambayo alihisi ilikuwa na hatari mbele yake. Alipotua akachepuka na kutafuta njia mbadala tofauti na ile alioipita mwanzo. Alitembea usiku sambamba na vivuli vya miti, hata alipotokea sehemu ile bado palikuwa kimya na hata mwili wa mwanamke yule bado ulikuwepo ukionyesha kutokuwa na uhai. Macho yake yaliozoea giza yalikuwa yakizunguka maeneo yote, bado hakuiona dalili ya uwepo wa mtu katika eneo lile. Hakuiona dalili ya kufuatiliwa wala kuwekewa mtego. Mkono wake ulikuwa juu ya bastola akipiga hatua kuufuata mwili uliolala chini bila uhai. Damu ilikuwa imeunda dimbwi kubwa. Akaufikia mwili ule na kuanza kuuangalia kwa makini.

Kwa kuwa hakutaka kuupoteza ushahidi, alichokifanya ni kutoa gloves na kuzivaa mikononi. Akaushika mwili wa binti yule na kuugeuza. Cha kwanza kukiona ni matundu matatu ya Risasi kifuani. Lakini kilichomchanganya katika matundu yale ni jinsi matundu yale yalivyo. Mpigaji alionekana kusimama kwa mbele na sio nyuma kama alivyokuwa akidhani. Hilo likampa picha, picha ya kuwa yeye ndie alikuwa mlengwa. Alikuwa mlengwa kutokana na ukweli kwamba marehemu alionekana hakuwa akikimbia. Bali alikuwa ameshikwa na alikuwa akilazimishwa kukifanya kitu. Alikuwa akilazimishwa kumuita yeye. Hapo akapata picha nzima kuwa alikuwa akihitajika yeye na sio huyu msichana. Alichokifanya nikuupekua ule mwili, hapo akakutana na vitamburisho vitatu, pamoja na kadi moja kubwa ambayo hii iliikuta kwenye Mkoba, pamoja na Simu yake ya mkononi. Akavichukua vyote na kuvisunda mifukoni. Baada ya hapo akapata wasaa wa kuiangalia sura ya mwanadada huyu. Hapo akakutana na sura nzuri na yakuvutia.

"Watu wanaroho ngumu, ya nini kumuua mtoto mzuri kama huyu? Alinong'ona huku akiinuka tayari kwa kurudi kwake.

***********

Chumba chote kilikuwa kimya, kila mmoja alikuwa ametulia akitizama mbele kuliko na Tv kubwa. Walikuwa wakiangalia taarifa ya habari kutoka shirika la utangazaji nchini. Kila mmoja alikuwa akitarajia kutangazwa kwa habari fulani ambazo zingewafurahisha. Kila mmoja ndani ya chumba kile alikuwa akiisubiri taarifa hiyo kwa hamu. Alikuwa akisubiri kile ambacho kingewafanya wao wawe katika kiwango cha juu katika biashara zao. Lakini ilikuwa kinyume wa kile walichokitarajia. Taarifa ambayo walikuwa wakiisubiri kwa hamu haikuja kama vile walivyotarajia. Bali vijana wao wanne walikuwa wamekamatwa wakiwa na mzigo wa madawa ya kulevya. Walikamatwa na maafisa wa usalama uwanjani hapo. Kila mmoja akapagawa, kila mmoja akahisi labda yupo ndotoni. Mzigo wao wenye thamani ya bilioni ishirini na mbili za kitanzania ulikuwa umekamatwa. Wakawaona vijana wao wakisukumwa kuelekea katika chumba maalum kwa ajili ya mahojiano zaidi. Chumba kikazizima kwa taharuki. Mmoja akaiendea simu yake na kupiga namba fulani. Muda mfupi simu ya upande wa pili ilikuwa ikiita. Iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa. Hata aliporudia bado hali ilikuwa pale pale.. hilo likawafanya watu wale watizamane.

"Haiwezekani!! Mmoja akanguruma.

"Kuna mchezo, huyu mwingine aliongea huku akishindwa kuuhimili presha.

"Jimmy hawezi kutufanyia hivi!!!" Mwingine akaongeza.

Lakini bado haikuondoa ukweli kwamba Mzigo wao ulikuwa umekamatwa na kulikuwa na uwezekano hata wao wenyewe wakatajwa. Bado simu haikupokelewa, bado iliendelea kuita kwa muda mrefu. Wajumbe wote wakazidi kushangazwa na hali ile. Lakini kabla hawajakaa sawa wakaisikia simu ikiita. Safari hii ilikuwa ikipigwa.

"Jimmy!!" Aliita.

"Jackson!!" Naye akaita..

"Atafutwe Teddy Harryson!!" Aliongea Jimmy kisha bila kusubiri maelezo yoyote akakata simu. Wajumbe wote wakaangaliana, hakuna alieamini maneno ya Jimmy. Kila mmoja alikuwa akiwaza mzigo wao uliokamatwa. Kitendo cha kuambiwa wamtafute Teddy Harryson bila kupewa maelezo yoyote kuliwakera baadhi ya wajumbe. Lakini wakiwa bado kwenye Mshangao wa kutokumuelewa Jimmy, simu ikatoa mliokuonyesha kuna ujumbe umeingia.

"Mpigie Teddy Mwambie akailete Roho ya Binti mmoja ambaye alikuwa chanzo cha kukamatwa kwa mzigo wetu. Nataka nikikupigia simu kwa mara nyingine unipe taarifa ya Roho Ya huyo Binti kuwasili hapo." Ulisomeka Ujumbe Ule.

ITAENDELEA
[18:28, 18/02/2017] Ibrahim Masimba: NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 002

Mwandishi Ibrahim Masimba
*******

Ilihitajika Roho ya Binti aliesababisha kukamatwa kwa mzigo wao. Mzigo ambao ulikuwa wa mamilioni ya shilingi. Ilikuwa ni lazima wampigie simu Teddy kwa kuifanya kazi ya kuileta roho ya mwanamke huyo. Ilikuwa ni amri kutoka Kwa Jimmy, amri ambayo ilitakuwa kutekelezwa katika usiku ule. Hilo likafanyika na Roho ya mwanamke alietakiwa ikaletwa sehemu husika. Licha ya kumuua mwanamke yule lakini bado hawakuridhika kwa hilo kutokana na kutokuupata mzigo wao. Wajumbe wote waliokuwepo ndani ya Chumba, wakaufanya mkutano wa kujadili kipi cha kuufanya ili kuupata mzigo wao. Ni ndani ya mkutano huo likapitishwa Jina la Masimba. Alitakiwa kutafutwa kwa lazima, alitakiwa kutafutwa ndani ya muda ule. Kutafutwa kwa kazi maalum. Kazi ya kujua nani alikuwa nyuma ya ukamatwaji wa Mzigo wao wa madawa. Hawakuamini kuwa mwanamke yule pekee anaweza kuwa chanzo cha kupotea kwa mzigo wao. Walitambua kuna mchezo mchafu, mchezo ambao ulikuwa ukichezwa nyuma ya pazia. Muda mfupi kijana mmoja alitoa simu yake na kutafuta namba, alipoipata akabonyeza batani ya kijani, muda wa sekunde tano simu ikaanza kuita.

"Dogo!" Ilisikika sauti upande wa pili.

"Yeah Mkuu!!" Alijibu kijana Yule.

"Kuna nyekundu au kijani?" Lilikuwa swali kutoka kwa masimba. Alitambua simu nyingi za usiku kutoka kwa kijana huyo hazikuwa za usalama hata kidogo.

"Nyekundu Mkuu, kuna kitu tunahitaji ukifanyie kitu, lakini hatuwezi kuongea kwenye simu. Tukutane coco beach muda huu kama muda upo." Akajibu dogo.

"Nitakuwa hapo muda mfupi, mtanikuta pale kwenye mishkaki." Akajibu Masimba huku akikata simu. Hakutaka kupoteza muda, alichofanya ni kumuamsha Mpenzi wake, akamuaga kuwa anakwenda coco beach na asingechelewa kurudi. Akaruhusiwa huku akiombwa kutozidisha masaa mawili. Alitoka nyumbani kwake kinondoni manyanya, akaelekea kituo cha pikipiki, hapo akamueleza dereva wapi anaelekea. Muda mfupi alikuwa juu ya pikipiki akielekea coco beach kuitikia wito. Kuambia kuwa kuna nyekundu ni dalili ya kuwepo kwa kazi ya umwagaji damu. Alikuwa ni mtu wa kutumainiwa katika mipango mbalimbali. Alishapewa kazi nyingi na zote alizifanya katika weledi wa hali ya juu. Siku zote aliishi kutokana na kufanyakazi ambazo ni tofauti na kazi yake ya halali. Licha ya kuwa afisa usalama wa Taifa tena wa kutegemewa, lakini upande mwingine alikuwa akishiriki mipango mingi ya hatari. Baada ya Dakika tano walikuwa wamewasili eneo la coco beach. Akashuka kwenye pikipiki, akaingiza mkono mfukoni akatoa noti ya Elfu tano akampa dereva, kisha bila kusubiri chenji akapiga hatua kuelekea pale alipowaambia wakutane. Alitembea kama mtu wa kawaida, suruali ya Jeans, tshirt nyeupe na raba nyeupe miguuni zilimfanya abadirike na kuonekana kama kijana. Akaendelea kutembea macho yake yakitembea huku na huko. Mbele kidogo akaiona gari ambayo aliifahamu. Ilikuwa gari inayotumiwa na watu wake. Hii ilimaanisha kuwa wao walishafika kabla yake. Akaendelea kutembea akiipita gari ile kama hakuiona, alipoipita akainama na kuzuga kama anafunga viatu. Lakini muda huo huo macho yake yakitembezwa kwa ustadi mkubwa. Ni hapo alipokiona kitu ambacho kwanza kilimshangaza na pili kilimtia hofu. Wakati ameinama akifunga viatu, alimuona mtu kama Mpenzi wake. Alimuona mwanamke kama Teddy akitembea kwa kificho ndani ya fukwe za coco. Hilo lilimshangaza, halikuishia kwenye kumshangaza tu, bali lilimpa hisia tofauti. Hakuwa amemfananisha Na haitatokea amfananishe Teddy. Lakini amefuata nini hapa? Mbona kama alikuwa akinifuatilia? Yalikuwa maswali, maswali ambayo alihitaji kupata majibu katika wakati ule.

Akaendelea bila kugeuka nyuma, hakutaka kufanya hivyo kuogopa kumshtua Teddy. Hatua kama tano kabla hajawafikia watu wake, masimba akaitoa Ishara kwa watu ambao walikuwa wamekaa mbele yake. Ishara ambayo ilijibiwa haraka na watu wale, kilichofuatia ni kuingia ndani ya gari na muda ule gari likaondoshwa pale coco na kurudi katikati ya mji. Ulikuwa mchezo ambao hakuna ambaye aliuelewa mapema. Wote walijua kwamba lazima wangezungumza palepale ufukweni. Lakini haikuwa hivyo, kila mmoja alishangazwa na mabadiliko ya Masimba.

"Nipeni kazi nishukie hapa." Ilikuwa sauti kutoka kwa masimba. Wajumbe wote wakashangazwa na haraka ile. Mmoja akataka kuhoji lakini alipoangaliana na macho ya Masimba akafumba mdomo na hakukumbuka tena kutaka kuuliza.

"Tuokoeni muda, aliongea tena masimba, safari hii akitaka kuufungua mlango.. lakini akashikwa bega na kijana yule. "Nadhani umeisikia taarifa habari ya jana kuhusu kukamatwa kwa mzigo wa madawa ya kulevya? Akauliza huku akimuangalia masimba usoni.

"Yeah nimeona na nilikuwepo eneo hilo." Akajibu akiangalia nyuma.

"Basi ule mzigo ni wa kwetu na tunahisi kuna mmoja wetu atakuwa ameivujisha taarifa za kukamatwa kwa mzigo wetu kwa faida zake." Alieleza kijana yule kwa kirefu kisha akaongeza "Tuna mashaka na Jimmy Lambert, tuna mashaka kwa kuwa anaonyesha kutokuwa na uchungu na mabilioni yetu yaliopotea.


"Umesema mnamuhisi kuwa amewageuka? Akauliza masimba.

"Ndio, tunahisi kwa kuwa hana uchungu na Bilioni ishirini na mbili. Safari alijibu mtu mwingine tofauti na kijana. Masimba akakaa kimya kwanza akionekana kuwaza kitu. Alipokuja kuinua kichwa chake akatingisha kichwa kuonyesha kubaliana na kazi ile. "Tambueni hii kazi ni ngumu na ya hatari sana, ninakwenda kuifanya kwa kuwa pesa iliopotea ni nyingi. Lakini pia naenda kinyume na kazi yangu. Hivyo basi naomba nitakapoanza kuifanya kazi hii sitaki kusikia chochote kikizungumzwa. Pia pesa yangu nusu niingizieni kwenye account yangu.. kisha tukutane Mbagala rangi tatu baada ya sikutano nitakuwa na chochote cha kuwaeleza!!" Akaongea masimba akishuka ndani ya gari tayari kwa kuelekea kwake. Ule wasiwasi wa kumuona mkewe pale coco beach ndio kwanza ukaanza baada kushuka kwenye gari. Kila alipojaribu kutafuta sababu ya mkewe kumfuatilia nyuma nyuma hakuipata. Hakuwahi kumuhisi mkewe tofauti lakini kwa kitendo cha leo akahisi kuna kitu mpenzi wake amekihisi ama labda wivu ndio unamsumbua.

*******
Aliingia nyumbani akiwa hana wasiwasi, baada ya kuingia akaongoza chumbani ambapo alimkuta mkewe akiwa amelala. Akamuangalia kwa muda mrefu bila kufanya lolote. Alimuangalia mpenzi wake huyu kwa muda mrefu bila kufanya kitu chochote. Hakutaka kwenda pale kitandani, kuna kitu alitaka kukifanya kwa wakati ule.alivikumbuka vitamburisho na mkoba wa yule dada alieuawa usiku wa jana. Akatembea mpaka sehemu yake ya siri ambayo ndio huhifadhi mambo yake mengi. Akavichomoa vitu alivyovichukua kwa marehemu yule, akatoka nje kabisa na kuanza kuvitizama. Jina lake mwanamke yule lilisomeka kama Asteria Paul. Alikuwa mfanyakazi wa Uwanja wa ndege. Akahisi kitu kama kengele zikigonga kichwani mwake. Alihisi kuna kitu kipo nyuma ya mauaji yale. Akarudisha vitambulisho na kuiwasha simu ya binti yule. Baada ya muda akaenda kwenye majina ya watu waliompigia.. Hakuamini Macho yake Pale alipokutana na namba ya Mpenzi wake ikiwa ndio namba ya mwisho kumpigia marehemu..
Kaliiii sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom