[4/14, 13:47] ibrahim: NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 031
alihitaji kuongea chochote na masimba, alihitaji kuuomba msamaha katika matendo yote aliyoyatenda. lakini masimba hakuwepo, hakumuona mbele ya macho yake. kwa mara nyingine akajaribu kuirudisha kumbukumbu, kumbukumbu ambayo hakuwa nayo. amefikaje mikononi kwa masimba? wakati alikuwa sambamba na mwamvita na wanausalama wengine? nini kilinitokea? hapo akauruhusu mkono wake kushika nyuma ya kisogo. jeraha dogo ndio kitu kilichoirudisha kumbukumbu. naam alikumbuka kile kilichofanywa juu yake pale waliposimama pale kinondoni. hapo tukio zima likajirudia. akasimama na kuyaendea mavazi yake ambayo yalikuwa pembeni kidogo mwa kitanda. akayavaa. akafunua mtoto wa kitanda, macho yake yakatua kwenye bastola yake sambamba na vitu vyake vingine. akavichukua na kuvisunda mifukoni. dakika zilizofuata alikuwa akishuka ngazi akiicha nyumba ile huku kichwa kikiwa kizito. hakujua kile kilichosababisha wenzake wamgeuke. aliua na kumsaliti masimba lakini bado hakuonekana kufanya lolote kwa wenzake. kwa wakati huu hakuwa muoga tena. aliamua kupambana nakundi lake. kama mzigo wa madawa alikuwa na uhakika kuwa anao masimba, sasa kipi ambacho kina mfanya asisaidiane na masimba? .alimaliza kushuka ngazi na kuufikia mlango wa kutokea nje, akaufungua taratibu na kutupia macho yake kwa nje, alishangaa kukutana na vichaka, vichaka ambavyo viliizunguka nyumba nzima. katikati kulikuwa na kijinjia chembamba ambacho kilitumika kama njia kwa watu wanaoishi hapo. Hilo likamshangaza kwanza. hakuwa anapajua pale, hakuwa anaijua sehemu ile. akajipa moyo na kutoka katika nyumba ile akikifuata kile kinjia chembamba. alitembea katikati huku macho yake yakizunguka huku na huko, mazingira hayakuwa rafiki sana ki usalama kwake. sehemu ile haikuonyesha kuwa makazi ya watu na hapakuwa dalili ya uwepo wa watu. alitembea kwa muda wa dakika kumi bila kukutana na mtu. hilo likaendelea kumtisha na kumtia hofu. lakini ni ndani ya muda ule akausikia ngurumo wa pikipiki.
[4/14, 14:01] ibrahim: Ni katika muda ule ule akausikia mngurumo wa pikipiki katika maeneo ya jirani na pale alipokuwa akiendelea kutembea. Mngurumo ule ukaendelea kusogea, sasa alikuwa akiusikia ukisogea karibu kabisa na yeye. Muda mfupi teddy alikuwa amehama pale njiani na kujitupa pembezoni mwa barabara. Sasa alikuwa nyuma ya kichaka akitizama kule barabarani. Haikupita hata dakika akaiona pikipiki aina ya Honda ikitokea. Juu yake alikaa MTU ambaye alimfahamu. Juu yake alikaa mwana usalama dee plus. Alikuwa akiiendesha pikipiki kanakwanba hapa kuwa na hatari kwake. Teddy akamuangalia sana dee plus mpaka alipopotea machoni. Masimba, kisha dee plus! Kuna nini hapa? Ina maaana Dee yupo na Masimba katika suala hili? Yalikuwa maswali ambayo hayakuwa na majibu.
*****
Walichoka vichwa vyao, hawakuwa wameupata usingizi tokea walipopata taarifa ya kifo cha waziri mkuu. Walikuwa wakikesha wakinusa hiki na kile. Mkanganyiko uliojitokeza katika kifo cha waziri mkuu. Kitendo cha watu ambao wangeweza kuwapa mwanga katika mkasa huu kuuawa kulizidi kuwapa ugumu katika kumjua muuaji kwa kuwa mpaka sasa walikuwa wakimhisi Masimba kutokana na wajihi wa muuaji waliopewa na dereva tax. Simu zilikuwa zikimiminika kutoka kwa wana usalama mbalimbali
[4/14, 18:39] ibrahim: Wana usalama walikua wakiripoti kutoka kila sehemu. Licha ya hivyo hakuna ripoti yoyote ambayo iliwasaidia kumpata muuaji ama kusaidia japo kupatikana kwa mwanga katika hili. Walihangaika zaidi ya kuhangaika. Walipekuwa kila sehemu lakini bado hawakupata chochote cha kuwasaidia. Sasa kila mmoja alikuwa amechoka na kuchoka, kila mmoja alitamani kusema ameshindwa, kila mmoja alitamani japo kupata dakika tatu za usingizi. Lakini haikuwa hivyo. Simu za chief zilikuwa zikiwasumbua sana. Kila wakati alihitaji kujua walipoishia katika hili. Ni wakati kila mmoja ameinama chini akifikiria hilo, simu ya mmoja kati yao ikaupata uhai. Simu ilikuwa ikiita. Mwana usalama yule akaichukua simu kisha kuitizama. Aliikuta namba mpya, aliikuta namba ambayo haikuwa imehifadhiwa. Kabla hajaipokea akatoa ishara ya kuiunganisha simu ile. Baada ya hapo akaipokea.. " Magomeni Makuti nyumba namba 089 kuna MTU atawafaa katika tukio hili." Baada ya kauli hiyo simu ikakatwa na simu kuzimwa kabisa. Wote wakatizamana... Hawakutaka kuchelewa, simu zikapigwa sehemu mbalimbali, wapelelezi waliokaribu na sehemu lilipotokea tukio wakaanza kusogea sehemu walioambiwa. Hata wale waliokuwa katika ofisi za muda nao walitoka wakielekea huko. Kila mmoja alikuwa akiifikiria ile simu. Simu iliyopigwa na MTU asiefahamika. Dakika kumi na tano baadae walikuwa karibu kabisa na nyumba husika. Macho yao yakiwanusa askari kanzu kibao waliosimama kama wahuni ama watu wenye mambo yao. Makachero wale wakashuka kisha wawili wakaongoza kuelekea kwenye ile nyumba. Wakati wanaukaribia mlango mkubwa wa kuingilia ndani ya nyumba ile, wakawaona wasichana wawili wamesimama wakionyesha kuongea kitu. Maafisa wale wakasogea mpaka karibu yao. Kabla hawajatoa salamu, wakamsikia msichana mmoja kati ya wale waliosimama akimuaga mwenzake. Hawakujishuhulisha naye, macho yao yote yalikuwa katika mazingira yanayoizunguka nyumba ile. Kila sehemu ilijaa watu wao.. Wakamfikia mwana Dada yule kisha kumsabahi. Baada ya salamu wakamueleza kile ambacho walikifuata pale. Kubwa likiwa ni kuwa wanamgeni wao katika nyumba ile.
Binti akakitigisha kichwa chake huku akiwatizama vijana waliosimama mbele yake. " Nyie ndio wageni wa Khadija? hatimaye akauliza binti .
"Ndiyo, sisi ndiye haswa wageni." Baada ya kuangaliana kwa nukta hatimaye wakajibu. Binti hakuongea tena, aliwakaribisha na kuwaongoza kuelekea chumba cha huyo Khadija. Wana usalama walikuwa makini kwa kila hatua. Mazingira ya jumba lile , yalikuwa yakitia mashaka. Kufika mbele kidogo binti akaonyesha kidole akiwaonyesha makachero wale chumba cha huyo Khadija. Wana usalama wakamtaka wangozane ili awe mgongaji. Binti hakubisha, hatua tano mbele wote walikuwa wamesimama mlangoni mwa chumba cha Khadija. Binti waliyemkuta akaanza kuugonga mlango, licha ya kuugonga kwa muda mrefu, lakini hapakuwa na uitikiaji kutoka ndani. Kengele za hatari zikagonga vichwani mwa makachero wale. Mikono ikashuka na kuingia mifukoni mwao, wakampa ishara binti. Ishara ya kujaribu kuufungua mlango.. Binti akashika kitasa na kukinyonga. Mlango ukafunguka, wakati huo huo macho ya wana usalama yakatua ndani "Damu" ni neno lililogonga vichwa vyao.. Hatua iliyofuata wote walikuwa wamesimama mbele ya maiti ya mwanamke, Kisu kikubwa kikionekana kuzama tumboni.. WAKATIZAMANA