MKE WA RAIS
SEHEMU YA 60
AKAUSIKIA MLIPUKO WA BUNDUKI, KISHA AKAISIKIA SAUTI YA MTU ANAYEMFAHAMU AKILALAMA. Hakusubiri kuambiwa, hakuosubiri kitokee kingine. Alirudi katika muda ule ule.. Mkononi kwake akiwa amekamatia bastola mbili. Haikumchukua muda kufika sehemu ya tukio. Sehemu amboyo ilitapakaa Moshi na Harufu ya Damu. Maiti za Wazungu wanne zikiwa zimetambarajika chini katikati kwa madimbwi ya Damu. Macho ya Mohamedi hayakuhitaji kuwaona wale Wazungu. Macho ya Mohamed hayakuhitaji kushangaa hilo, bali macho yake yalihitaji kuwaona watu. Watu ambao aliwahitaji kuliko alivyoihitaji Roho Yake. Alikuwa akiwatafuta Jenifer na Revina. Hakuwa akiwaona katikati Ya Moshi, hakuwa akiwaona katikati ya mapambano. Hakuwaona wakionyesha ujuzi wao na wala hakuwaona wakiwa sehemu. Macho yake yakashangaa, kichwa chake kikaunda maswali kisha mdomo wake ukaropoka wako wapi hawa? Hakuwa na Majibu kwa kipindi kile. Punde akavisikia ving'ora vya polisi. Punde akawaona Makomandoo wakitokea katikati Ya Moshi, Makomandoo ambao hawakujulikana wapi walipotokea. Wote wakanyoosha Bunduki Zao kuelekezwa pale alipo Mohamedi. Mshangao na bumbuwazi vikatamalaki usoni kwa Mohamedo Hasira Zikaupanda moyo Wake, akatamani afanye kitu, akatamani awaanzishie kuwaonyesha kuwa ni zaidi Ya wao.
Lakini alipomuwaza Revina na Jenifer alikubali kuwa mpole. Upole ambao ulikuwa katikati Ya mshangao. Mbele ya Uso wake akatokea mkuu wa kitendo cha kijasusi ndani ya Idara ya Usalama Wa Taifa. Pembeni alikuwa na Watu wawili, watu ambao walifunikwa nyuso Zao kwa vitambaa. Mmoja alikuwa Wa kiume na Mwingine alikuwa wa kike. Kutokea kwa Mr Fraidy Wellah kukaibua maswali kwa Mohamedi.. Bado alitamani kitu kinachoendelea kiwe hadithi. Ni wakati huo akishangaa, Akahisi kitu kama Sindano kikitua katika Mwili wake, kitu ambacho alishakijua kuwa ni Dawa ya kusaidia kumlevya. Ni kweli alilewa. Muda Mfupi baadae Macho Yake yalikuwa yameingia Giza. Yalikuwa mazito Yasioweza kufunguka. Akakubali kwa Mara ya kwanza kumezwa na Hali ile. Akakubali kwa Mara Ya kwanza kufungwa na kubebwa kama maiti.
*****
pembeni ya jengo moja kubwa katikati ya jiji la Dar es salaam, Maeneo ya Posta. Watu wasiopungua kumi walikuwa wameizunguka meza kubwa huku kila mmoja akionekana kuwa busy na computer Yake mpakato. Walikuwa wanaume saba na wanawake watatu. Wote walionekana wakifuatilia kitu fulani. Kitu ambacho kilionekana ni Muhimu. Taarifa Zilikuwa zikitumwa huku na huko, maswali Yakiulizwa na Mengine kujibiwa. Kikao kilikuwa kizito, kikao kilikuwa kizito kupindukia. Tayari Rais wa Nchi alikuwa haonekani wapi alipo. Huku baadhi ya Walinzi wake wakiokotwa wakiwa maiti. Bado taarifa Zilikuwa ndani kwa ndani, bado taarifa hazikuweka bayana katika hilo. Lakini wakiwa katika Jengo lile wakijadili hicho kitu ilikuja taarifa kuwa kuna baadhi ya Makomandoo walikuwa Wameasi. Na Sio hao tu, bali Mkuu Wa Ujasusi na Mkurugenzi Wake walikuwa ni wamojaapo katika Suala hilo. Kila mmoja alikuwa akihaha kutaka kujua ni wapi Rais wa Nchi Amepelekwa. Ni wapi atakuwa amehifadhiwa Rais wa nchi? Yalikuwa maswali yaliyopita Vichwani mwa wajumbe wa kikao kile. Wakati suala la Mheshimiwa Rais kupotea likiwa halijapatiwa Ufumbuzi, Likaja Suala kuwa Mpelelezi Mashuhuri Nchini Mohamedi naye ametekwa na Hajulikani alipo. Hapo wajumbe wote wakapigwa na butwaa, wote walikuwa wakiitambua harakati inayofanywa na Mohamedi, na Wote walitambua kuwa Mohamedi alikuwa ndio mtu pekee wa kulitatua hili. Sasa hii Taarifa ikazima ndoto Zao za kuisaidia Serikali kubaki Madarakani. Na taarifa iliyoingia Punde iliwajulisha kuwa Raisi alikuwa amehifadhiwa sehemu akishurutisha alitangazie Taifa kuwa Anaachia Madaraka ya kuongoza Nchi. Kila Mmoja akapagawa na kikao hakikuendelea tena.
*****
alikuwa mwanamke pekee na mtu pekee aliyeshuhudia kutekwa kwa wasichana wawili waliokuwa wakisaidiana na Mudy na Pia ni Yeye pekee aliyeshudia Mudy akitekwa baada ya Kudungwa Sindano Ya madawa Yenye kutia Usingizi. Huyu hakuwa mwingine bali alikuwa Inspekta Ummu Sammy. Kila kilichokuwa kikitendeka alikuwa akikishuhudia kutoka umbali mdogo jirani na Sehemu ya Tukio. Alikuwa hapo kwa muda mrefu sehemu ile akiwafuatilia Nyuma Mohamed, Jenifer na Revina walipotoka nyumbani kwa Waziri Wa Katiba.
Baada ya Mohamed, Revina na Jenifer Kuondolewa pale. Ummu hakutaka kuchelewa kuondoka pale. Alichokifanya ni kuchukua sura yake ya Bandia na kuivaa. Muda Mfupi alikuwa akionekana kama Msichana wa kizungu akitembea eneo lile umbali ule ule bila kuonyesha kushangazwa na kitendo kinachotokea pale. Alikuwa akitembea huku kila hatua yake ikiwaza kitu, alikuwa akitembea huku akili yake ikahama pale. Bastola Mbili Zilikuwa kiunoni. Alikuwa akihesabu kila Hatua yake, alikuwa akiupangia mkono wake kipi cha kufanya. Akazishuhudia gari zilizowachukua Mudy, Revina na Jenifer Zikiondoka.. Naye akaunga Nyuma akiwa katika pikipiki.. Pikipiki aliyompora mtu aliyekuwa akiiendesha. Akaunga msafara katika Kuzifuatilia Gari Zile. ULIKUWA MCHEZO HATARI SANA KUUCHEZA.....