Tena fastaaa kabla mzukka haujashuka haya ndo mastory nayoyapenda miye ya mapambanoooibra87 Fanya mchakato wa muendelezo wa hii kitu
Sana mkuu hongera mtunziHadithi nzuri mno mkuu
DuuhMKE WA RAIS
SEHEMU YA 025
Wakati anaendelea kutazama kilichokuwemo kwenye makablasha aliyopewa na rais, Mlango ukafunguliwa kwa kasi watu wenye silaha wakaingia kwa kasi ile ile.. Mudy alikuwa amewahi kuruka na kuangukia Nyuma ya kitanda huku bastola Yake ikiwa Imara mkononi. Akatulia kuwaangalia watu wale katika namna ambayo walionyesha kuhamanika kutokana na kutokumuona Mudy. Hawakujua alipo mudy na hawakujua Jinsi alivyojitoa pale.. Muda Mfupi baadae Bastola ya Mudy Ikakohoa Mfululizo.. Watu watatu wakaanguka chini wakiwa wanavuja damu. Mudy akainuka kwa samasoti na kutua sehemu nyingine kutoka pale alipo. Bado bastola yake ilikuwa mkononi alipowaendea maiti wale na kuanza kuwasachi mifukoni.. Alichukua kila alichokiona kina Umuhimu kisha Muda mfupi alikuwa Akiondoka katika Chumba kile akiwaacha maiti wale wakiwa wamelaliana. Kutoka pale hoteli safari yake ilimpeleka mpaka maeneo ya vingunguti.. Akatafuta guest ya kawaida na baada ya kupata akalipa na kuingia Chumbani... Muda mfupi alikuwa akipangua na kupekuwa baadhi ya kadi na vitambulisho ambavyo vilikuwa ni moja kati ya Vitu alivyovichukua kutoka kwa Maiti Wale.
Kila alichokuwa akikichukua alikuwa akikisoma kwa umakini mkubwa... Hakutaka kudharau kila alichokiona kutoka katika mifuko ya wakora wale aliyowaua kule hotelini. Katika kuangalia huko akakutana na picha ya mwanamke Mzuri Sana.. Alikuwa mzuri kuliko wale ambao hakuwahi Kuwaona au kuwa nao.. Licha Ya Uzuri wa mwanamke Yule, lakini hilo halikumvutia katika picha ile. Kilichomvutia ni kule kuliona neno WANTED katika picha ile. Neno ambalo lilimpa ugumu kidogo katika kujua kwani picha ile Iwe na neno kama lile. Aliendelea Kuingalia Ile picha kwa muda huku akiwaza hiki na kile mpaka pale ambapo aliamua kuigeuza ile Picha kwa nyuma. Hapo ndipo alipokutana na namba ya Simu na namba ya Nyumba ya mwanamke Yule... Mudy akatabasamu. Baada Ya kuridhika na Kile alichokiona akayachukua makablasha Aliyopewa na Rais na kuanza kuyapekua.
*******
Ulikuwa muda mzuri kwa kepteni George na Luteni Sevenlee kuelekea kwenye hoteli alipowekwa yule msichana mfanyakazi wa kampuni ya Simu Ili kumdodosa mawili matatu kama wataweza kupata mwanga katika Kazi Inayowakabiri. Walikuwa bado hawakupata Usingizi lakini waliona ni lazima waende kwanza wa kamuhoji mwanamke yule. Gari ilitembea kwa mwendo wa Taratibu Huku wakitizama huku na huko kuona kama wanafuatiliwa, lakini haikuwa hivyo.. Walipofika maeneo ya Morocco wakashangaa wakipitwa na gari moja kwa kasi sana.. Kasi Ya ile gari Iliwafanya kepteni George na Luteni Sevenlee watizamane kwa muda. Lakini kwa kuwa walikuwa wakiwahi sehemu wakaona waongeze Mwendo Ili kuwahi sehemu husika. Wakiwa hatua Hamsini kutoka Ilipo hoteli alipowekwa Yule Mhudumu, wakaiona ile gari Iliyowapita kwa kasi pale Morocco ikiwa imepaki pale. Kengele ya Tahadhali Ikagonga katika kichwa Cha Kepteni George.. Akajikuta akiipapasa na kuishika bastola Yake.. Kisha akamwangalia luteni Sevenlee na muda ule ule akaufungua mlango wa gari Yao na kushuka kwa Ustadi bila kuonekana. Akatembea kwa mguu kama wafanyavyo wateja Wengine.. Alipokaribia mapokezi Macho Yake yakatua kwa vijana Wawili ambao tazama Yao tu ilimpa picha kuwa mwanamke yule yupo msambweni. Akazama ndani ya Hoteli ile kama mteja, lakini hatua tatu mbele akatizama Nyuma kwa Chati, akawaona watu wale wawili aliyowaona Nje wakimfuata lakini Uzuri Zaidi Nyuma Ya Vijana wale alikuwepo Luteni Sevenlee Akiingia kama mtu tofauti na ambaye hajui kile kilichokuwa kinaendelea. Ikawa mbele George, Kati Wale Wakora na Nyuma Alikuwepo Luteni Sevenlee... George Akaendelea kusonga mbele.. Wakati anapanda ngazi kuelekea Ghorofa ya Pili, akamuona mtu, mtu huyo aliyemuona alikuwa ni mtu ambaye Hakukusudia kumuona Pale... Kwa mbali macho Ya kachero George Yalikuwa Yamemuona Mudy Akitoka Juu wanapoelekea akishuka Chini Huku tabasamu lake likiwa katika uso wake.. Tabasamu ambalo lilimpa George hamu ya kujua kile ambacho kilikuwa kimefanywa na Mudy. Wakapishana na Mudy Kama hawajuani lakini kupishana kwao kulifuatiwa na Tukio ambalo hakuna ambaye alitarajia... Kupishana kwao kulifuatiwa na Tukio la Vijana Waliokuwa Wakimfuatilia Kepteni George kuanguka chini Huku damu zikivuja, na Muda Huo Mudy akiondoka kwa kumpita Luteni Sevenlee bila Hata kumuangalia . Kepteni George hakushuhulika na Mudy, alichofanya nikuongeza kasi Kuelekea Chumba Ambacho alimuwacha Yule msichana... Akaufikia mlango huku bastola Ikiwa mkononi mwake.. Akanyonga kitasa, akatanguliza macho kutizama ndani.. Macho Yake yakakutana na Dimbwi la Damu Huku juu yake kukiwa na Miili mitatu Ya Wanaume. Kuiona Hali ile, akajichoma ndani kabisa.. Alichokutana nacho kilimfanya atamani kupiga kelele.. Mwanamke Waliyedhani Angewapa Siri katika kuwapa mwanga katika upelelezi wao, Alikuwa Ameuawa kinyama kwa kuchomwa Kisu katikati Ya Tumbo Huku Utumbo Wote Ukiwa Nje tena akiwa amelazwa Uchi katikti ya Kitanda, Damu Zikichuruzika Kama Maji..