MKE WA RAIS
SEHEMU YA 063
Wakati anataka kupiga hatua ya tatu, mlango wa mbele yake akasukumwa. Kilikuwa kitendo cha sekunde moja mkono wa Mudy kushuka ilipo bastola na sekunde ya pili Bastola ikakohoa. Ikahoa huku watu wanne wakianguka chini. Walikuwa maiti na hawakuwa wakipumua. Mudy akawaacha na kuendelea kusonga mbele. Alikuwa akitembea katika namna ya kivuli, alikuwa akitoka hapa na kuingia pale. Alikuwa akifanya hiki na kufanya kile. Kila sehemu kulisikika milio ya Bunduki, kila Sehemu kulisika mapambano. Mapambano matakatifu kwa sababu ya ukombozi wa Nchi. Kila kitu kilikuwa kikitakiwa kukamilishwa katika Muda ule. Muda ambao ulikuwa mahsusi kuyazima mapinduzi. Revina alikuwa akiutumia Ujuzi wake Wote alioupata katika Kikosi maalum Kilichokuwa kinailinda Ikulu ya Rwanda. Alikuwa Akipiga na kuua.. Hakupenda kuacha mtu hai, hakupenda kuwaona wakipumua. Kila mapigo yake matatu, basi pigo la tano lilikuwa ni kuchinja shingo. Alikuwa akiuburudisha Moyo wake pale alipokuwa akiichezea damu, alikuwa akitabasamu na kujisikia furaha pale alipokuwa akichinja watu. Alipiga mateke na alipiga ngumi. Alitumia Karate na Hata Kung fu. Pale alipokuja kubadilisha Tai Kwond ilikuwa burudani tosha. Yalikuwa mapambano makali kuwahi kutokea. Jenifer na Ummu walikuwa wakipokelezana hili na lile. Kila mmoja alikuwa akionyesha kile ambacho alikuwa nacho. Mudy hakuwa Nyuma, Bado alikuwa akisonga kukitafuta chumba walichofungiwa watoto wa Rais. Chumba ambacho kingempa mwanga wa kujua pale alipo Mheshimiwa Rais. Bado alikuwa akichungulia Huku na Kule. Alipotokea kwenye kaukumbi kadogo ndani ya Jumba lile akashangazwa na Milango kufunguka na Kufunga. Kila alipokuwa akitembea bado milango ilikuwa akifunguka na Kufunga. Akaendelea kutembea kwa Umakini Zaidi. Akitembea huku miguu na mikono ikiwa tayari. Masikio yakinasa kila mlio na Macho kuangalia kwa Hila. Akaifikia nusu ya Ukumbi akiwa bado hajamuona wala kumgundua mtu. Akataka kuipita ile Nusu. Hapo ndipo alishuhudia watu watano wakiingia katika chumba kile. Walikuwa wanaume watano walioshiba. Walikuwa katika vazi la Jeshi, vazi ambalo lilipambwa na Kitu mfano wa Bawa katika Moja ya Sehemu za Vazi lile. Juu walikuwa na Kofia Nyekundu. Walikuwa Makomandoo. Makomandoo Ambao thamani ya comandoo mmoja ni Sawa na Askari wa Kawaida mia tatu. Alama ya Bawa iliyokwenye Mavazi Yao, ilikuwa alama inayotambulisha kiwango cha juu cha Ufaulu wa comando Husika. Ufaulu Ambao ni lazima Umalize Zoezi la Kutupwa Umbali mrefu kutoka angani. tena Ukiwa Ndani Ya Helkopta Huku ukitakiwa utue ardhinI Bila kusaidiwaa na Msaada wa Parachuti. Hilo ndilo funzo la Mwisho katika kuhitimu mafunzo ya ukomandoo.
Pale walipoingia na kutizamana na Mudy, wote walitambuana. Walitambuana kuwa walikuwa wamoja katika fani moja. Fani ya mapambano. Wakaangaliana tena na Tena. Mohamedi akiwalazimisha wamtazame Usoni ili wakisome kile kilichopo ndani yake. Naam kile alichopenda wakione wakakiona. Hapo ndipo mapigano Yalipoanza kila mmoja akitumia Ujuzi wote katika kuzuia na Kushambulia. Yalikuwa mapigano mazito. Haikuwa kazi ndogo kupambana na comando mwenzako aliyeiva. Ndani ya Sekunde kumi na Mbili Mudy Alijikuta akiwa chini akivuja Damu juu Ya Jicho baada ya kupata kipigo mfululizo. Akainuka huku akuiweka Mwili wake kwenye Uimara, akailamba damu yake iliyokuwa ikimvuja Juu Ya Jicho. Punde Mohamed akaonekana akichupa hewani huku akiachia mapigo.
Yalikuwa mapigo mazito, mapigo ambayo alitumia uwezo wake wa ziada. Lakini hayakufanikiwa kufika katika miili au kuwagusa kabisa makomandoo wale. Akajikuta akiisalimia Ardhi kwa mara Ya pili baada ya kupigwa mapigo kadhaa. Mudy Alikuwa chini akigalagala, alikuwa amekutana na watu ambao hawakuwa wepesi kama alivyotarajia. Hapo ndio akauona Umuhimu wa kuirudisha Akili yake katika Mapambano. Akasimama tena kwa Mara Ya pili. Akisoma kila hatua za makomandoo wale, ikisoma kila kitendo kutoka kwa Makomandoo wale. Akasimama vizuri kukabiliana nao. Akaona aubadili Mfumo wake Wa kupigana. Ni hapa makomandoo wale waliposhangaa, ni hapo makomandoo wale walibaki midomo wazi. Huyu alikuwa Mohamed Yule wa MOSSAD, huyu alikuwa Mohamed Wa KGB na huyu alikuwa Yule Mohamed Wa Scotland Yard. Aliinua kwa kujigeuza mfano wa tairi, akajiachia akiwa hewani huku akiachia mapigo.. Mapigo mazito.. Mapigo ambayo kwa mara ya kwanza yaliigusa miili Ya makomandoo, na sio kuwagusa tu, bali yaliweza kuwaangusha Chini. Sasa ukawa muda wa mapambano. Mapambano mazito, mapambano ambayo yalikuwa ni Kufa na Kupona.. Haukupita Muda mlango ukasukumwa, wakaingia Jenifer na Kisha Ummu. Wakakutana na kile ambacho hawakukiamini.. Ummu Hakusubiri, Hakusubiri kuupoteza Muda Kumuangalia Mudy Akipambana. Akaruka kwa Aina zao, aliruka akiutanguliza Mguu mbele.. Kilichofuata Hakikusemekana wala Kuhadithika. Lakini ndani Ya Muda Wa Dakika kumi wale makomandoo Wote Walikuwa Chini. Hawakuupoteza Muda, Wakatoka Mle ndani na Kuendelea Kusonga mbele. Wakati Wakitaka kutokea Upande wa Pili. Wakamuona REVINA AMELALA..