Riwaya: Mke wa Rais

Riwaya: Mke wa Rais

MKE WA RAIS

SEHEMU YA 51

Miili ya watu ilikuwa imetambarajika kuonyesha kuwa Mohamed alikuwa akikifanya kile ambacho hakukitegemea. Akatabasamu.. Kila hatua moja aliyopiga alikuwa akikutana na Maiti.. Punde akamuana Rugimbana akichupa kuingia ndani ya jengo lile. Ulikuwa ni uchupaji uliyompa Burudani katika macho Yake. Alipenda kuitazama michezo kama ile.. Alipenda kuona watu wakicheza michezo Ya Hatari kama mfano ule.. Hakuchelewa katika kujiunga ndani ya Jengo.. Hakutaka kutafuniwa na wenzake.. Akaudandia mti ulio pembeni mwa jumba lile mfano wa Nyani ama ngedere.. Muda mfupi alikuwa akitua ndani bila kutoa kishindo.. Akajivingirisha na kutulia kwanza. Macho yake yaliendelea kutizama Burudani, Burudani kutoka kwa Mudi na Rugimbana.. Walikuwa wakifanya kile ambacho kilitoa burudani kutizama.. Mudy alikuwa katika aina ya mapigo ambayo hakuwahi kuyaona kabla.. Wote walikuwa wakitembea na mapigo ya Martial Kombart.. Walikuwa wakinesa na kuinuka.. Walikuwa wakiruka sarakasi na kuua... Hakutaka kuangalia kile alichokuwa akikishuhudia..

Akainuka kwa Mwendo usio na mlio wala mchakato wa majani. Akazunguka mpaka upande wa kusini mwa Jumba lile.. Akiwa hapo akashuhudia watu wawili wakitoka ndani huku wakionekana lolote linalotokea katika Jumba lile. Akautumia mwanya huo kutambaa na vivuli vya miti mpaka alipowafikia karibu.. Bado hakuwa ameonekana kwa watu wale na bado hawakuwa wameshtuka kwa lolote. Jenifer akajinyonga mfano wa Nyoka.. Sekunde mbili alikuwa amechupa na kusimama katikati Yao.. Walinzi wote wakashtuka na kuhamaki.. Jenifer hakuwapa nafasi ya kujiandaa.. Mateke matatu ya hewani yalitosha kuwanyamazisha walinzi wale. Akaokota Bunduki zao, mbili akaziweka begani na Moja aliikamatia mikononi. Akaanza kusonga kuingia ndani Ya Jumba lile.. Jumba ambalo lilikuwa kubwa na lenye giza la kutosha.. Akaufikia mlango na kuusukuma.. Akaruka kuingia ndani.. Kuingia kwake kulifuatiea na milio ya Risasi kuelekea kule alipo.. Akachupa kwa haraka na kuangukia pembani kabisa.. Bada watu wale waliendelea kufyatua risasi pasipo na mpangilio.

Bado Jenifer aliendelea kutulia,, kutulia huku akiwasoma watu wale wanapotokea.. Punde akasikia mayowe na sekunde Nyingine ukimya wa Ajabu Ukatawala Eneo lote. Jenifer bado aliendelea kutulia kuangalia kinachoendelea.. Mara akashangaa kuona taa Za jumba lile Zikiwaka.. Akapeleka macho Yake kwa Haraka kule kulipokuwa kunatokea Milio ya Risasi. Macho Yake yakamuona Rugimbana lakini kilichomburudisha Zaidi ni kuwaona watu watano wakiwa wamelaliana Jini wakivuja Damu.. Jenifer Akainuka na Kujitokeza. Walipotizamana na kugunduana kila mmoja alionyesha kidole gumba kuonyesha mambo yako sawa.. Muda mfupi baadae Mudy naye akafika na kuungana na wenzake. Hakujua kama Jenifer alikuwa pale, walipoonana wakakumbatiana na walipoachiana wote kwa pamoja wakagawana kuangalia kila kitu katika Jumba lile. Ulikuwa ni Uchunguzi uliochukua Muda mfupi sana kutokana na kugundua uwepo wa ghala la silaha katika mahandaki ambayo yalichimbwa ndani Ya Jumba lile.. Kulikuwa na Silaha Nyingi na mabomu makubwa makubwa.. Kulikuwa na ndege za Kirusi aina Ya Rocket Rangers, kulikuwa na ndege za mashambulizi za B52.. Pia kulikuwa na Bunduki Za kila aina, kuanzia Rifle, Rpg, Ak 47, SmG na Bunduki Nyingine nyingi nyingi..

Kila Mmoja wao hakuwa anakiamini kile ambacho alikuwa akikishuhudia.. Kilikuwa kitu ambacho huwezi kukidhania kuandaliwa na watanzania Wenyewe.. Uroho Wa Madaraka wa Baadhi Ya Viongozi ulitaka kulipeleka Taifa katika Taharuki. Taharuki ambayo ingeharibu sifa ya Nchi hii. Kwa nini walitaka kufanya mapinduzi, kwa nini Walithubutu kumuua Mke Wa Rasi? Ni nani yupo Nyuma Ya Hili ukimuondoa Waziri Mkuu? Je mke Wa Rais Alikuwa mmoja Wao? Na kama ni ndio kwanini aliuawa mwanzo kabisa? Au walitaka kumtumia kupata baadhi Ya vitu kisha watekeleze Mauaji Juu Yake? Hapana ni lazima tulijue hili, ni lazima tulifichue kwa Uwezo wetu.. Hata kama ni kufa nipo Tayari Kufa. Alikuwa akiwaza Mohamed Huku akiangalia Silaha Zale... Wote walikuwa wakisubiri Neno kwa Mudy Ili wajue kipi cha kufanya.

Mohamed hakuongea kitu kama Walivyotarajia.. Wakashuhudia Akichomoa bomu moja kutoka kwenye Hadhina ya Mabomo.. Akalifungua kwa kutoa Ufunguo wake kisha kuliseti katika Dakika Walizojua Wanaweza kutumia mpaka kufika nje, Kisha Wao wakatoka kwa haraka kutoka Eneo hilo kuelekea mahali walipoliacha gari lao Kwa Safari Ya Kurudi Dar Es Salaam ndani Ya Usiku Huo. Walitaka kuacha vilio vya kusaga meno kutoka kwa Viongozi wale.. Wote wakafanikiwa kutoka katika Jumba lile.. Wakaingia katika Chochoro moja baada Ya Nyingine walipokuja kusimama Walikuwa wamefika karibu na Walipoiacha Gari Yao. Lakini hawakuifikia na hawakuipanda.. Wakashuhudia Mlipuko mkubwa ukiisambaratisha Gari Yao.. Wote Wakachupa na Kuangukia upande mwingine.. Sekunde tano Baadae mlipuko mwingine Mkubwa Zaidi Ukasikika.. Jiji la Arusha lilikuwa katika Hali ambayo Haikutazamika.. Moto Mkubwa Ulikuwa Umetanda Angani.. Hawakuchelewa, Ilikuwa ni lazima waondoke pale.
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 52

Ilikuwa ni lazima waondoke Arusha na nilazima uwe usiku ule. Lakini hawakujua wangeondokaje kwa kuwa tayari gari yao ilishasambaratishwa. Hawakutaka kuupoteza muda pale.. Kwani walijua kitendo cha kulipuliwa kwa gari Yao ni kwamba tayari walishajulikana kuwa wapo eneo lile. Wakatawanyika kila mmoja kwa njia yake.. Kila mmoja akiwa na mguu wa kuku mkononi. Walikuwa wakitembea mwendo wa kulindana na kuchungana.. Mwendo ambao ulijulikana kama Never leave man Behind.. Kila mmoja alikuwa akihakikisha mwenzake anakuwa salama bila kumuacha nyuma.. Tembea yao na ushupavu wao kuliwakumbusha mbali sana.. Pale walipokuwa katika mafunzo ya ukomando kule msagara.. Ulikuwa ni mfano wa movie tamu ya kijasusi.. Ilikuwa ni picha iliyovutia kuitizama.. Jenifer mtaa wa pili, Rugimbana mtaa Wa kati... Mohamedi Mtaa wa mwisho wakiangaliwa kwa ukaribu na vijana kutoka Kitengo cha walinzi Binafsi Wa Mheshimiwa Rais. Jiji lote bado moto ulitanda hewani, milipuko bado ilikuwa ikihanikiza katika Anga lote la Jiji la Arusha. Wananchi walikuwa wakikimbia kunusuru maisha na Roho Zao.. Ingawa jumba lililolipuliwa lilikuwa mbali na makazi Yao, lakini bado mitikisiko ingeweza kuwaathiri.. Wakati watu wakikimbia Mohamedi na Watu wake walikuwa wakiingia katika Hoteli kwa kupishana Dakika kumi.. Alitangulia Jenifer, akafuatia Rugimbana kisha wakaja vijana kutoka kitengo cha Walinzi binafsi Wa Rais, kisha Mwisho akamalizia Mohamedi.. Akiwa amejibadilisha kabisa. Baada ya kuingia katika Hoteli na kila mmoja kwenda kubadili mavazi Chumbani Mwake. Simu ya Mohamedi ikapata uhai kuonyesha kulikuwa na mtu akimpigia.. Akataka kuipuuzia lakini akapata wazo la kuipokea. Alipoitizama namba ya mpigaji mwili wake ulimsisimka baada ya kuiona namba ya Mheshimiwa Rais.. Akaipeleka Sikioni... ''shikamoo Mzee'' alisalimia mohamedi..

''Marahaba kijana, vipi mbona sielewi kinachotokea huko? Aliitikia salaam kisha kuuliza swali. ''Mzee Hiki kinachoendelea Huku ndio dawa na Tiba ya kuiacha nchi katika mikono yako lasivyo ungeondoka madarakani siku sio Nyingi'' alijibu Mohamedi na kuamsha hofu Moyoni kwa Mheshimiwa Rais.. Ukimya wa muda mfupi ukatanda pande Zote kila mmoja akitafakari hili na lile.. Kauli ya Mohamed ilionekana kumtia Hofu mheshimiwa Rais.. Hofu ambayo ilimtia baridi na woga wa kutetemeka.

Alitamani kuendelea kuongea lakini sauti haikuwa inatoka. Akaendelea kuitolea macho simu yake.. Maneno ya Mohammed Yakijirudia katika kichwa chake. Hiki kinachoendelea huku ndio salama Ya Kuwepo kwako madarakani.. Kwa nini iwe hivyo? Nani alipanga hilo? Kifo cha mke Wangu kinahusiana nini na Mpango huu? Yalikuwa maswali mazito Yaliokosa majibu katika Kichwa chake.. Mudy alilitambua hilo mapema.. Aliitambua kuwa Alikuwa amempa hofu Rais wa Nchi.. Akajikohoza kidogo kisha kuuvunja Ule Ukimya. Alihitajika kumuweka kwenye Usawa Rais wake.. ''Usiwe na Hofu mzee, Muda sio Mrefu naimaliza kazi Uliyonipa.. Na utajua kila kitu ambacho hukijui.. Lakini Bila kulifanya hili, basi nadhani hali ingeendelea kuwa ngumu sana.'' Maneno hayo yalionyesha kumpa uhueni Rais.. Akaagana na kijana Wake.. Simu ikakatwa.

*****

lilikuwa patashika sana kwa upande wao.. Kila mmoja alikuwa haamini kile kilichokuwa kikitokea. Waziri wa Ulinzi, Waziri wa Mambo ya ndani na mkurugenzi wa Usalama wa Taifa walikuwa mbogo kila mmoja akiongea la kwake. Kila mmoja alikuwa akilaumu, akilaumu kile kilichokuwa kikitokea. Kwanza waliamini kulikuwa na msaliti kati yao, kulikuwa na msaliti ambaye allivujisha siri ya Uwepo wa Silaha katika maficho Yao.. Msaliti ambaye alikuwa yupo na wao bega kwa bega lakini huku akitoa Siri zao kwa watu wengine. Hakukuwa na hata mmoja aliyeweza kunyanyua Mdomo kuongea.. Angeongea kipi wakati Ghala lao la Silaha Zilikuwa zikiteketea.. Wangeongea kipi wakati kile walichokipanga kinaelekea kufeli? Watakuwa watu wa aina gani pale itakapogundulika wapo Nyuma ya mpango ule? Kila mmoja kijasho Chembamba kilimtoka.. Hawakuhitaji kuupoteza Muda.. Ilikuwa ni lazima Vijana Wao wafanyekazi Usiku na Mchana kuhakikisha Mohammedi Anapatikana akiwa maiti au hai.. Wakiwa bado wanajadili, simu ya Mkurugenzi Wa Usalama wa Taifa ikaita.. Akaitupia macho namba ya mpigaji... Moyo ukampiga paa! Baada ya kugundua mpigaji wa Simu alikuwa Rais.. Huku mikono ikitetemeka kwa hofu kuwa wameshagundulika, akaipokea Simu.. ''Ndio Mzee.''

''Uko wapi Muda huu.!?'' lilikuwa swali la kimtego, swali ambalo halikutakiwa kujibiwa kwa kukurupuka. Akatulia kupanga kipi cha kumjibu Rais. Lakini kabla yakulipata Jibu akasikia amri Nyingine iliyomtetemesha... ''Nakuhitaji Ikulu ndani Ya Nusu Saa Uwe Umefika.'' kisha Mheshimiwa Rais Akakata Simu.. Mkurugenzi Akachoka Zaidi... Wote waliopembeni wakamkazia Macho kutaka Kujua Kipi kinachoendelea. Kwa Sauti Ya uchovu na Kukata Tamaa akasema.. ''RAIS ANANIHITAJI IKULU NDANI YA DAKIKA 30... lilikuwa jibu lililoamsha Kengele na hisia Za Hatari katika Vichwa vyao.. Wote Wakauona Mwisho Wao.. WAKATIZAMANA BILA KUONGEA KITU.
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 53

LILIKUWA JAMBO LILILOAMSHA KENGELE ZA HATARI KATIKA VICHWA VYAO.. WOTE WAKATIZAMANA.. Hakutaka kuchelewa katika hilo.. Alichokifanywa Mr Adnan ni Kuinuka na kuanza kutoka ndani ya Hoteli ile Huku akionekana ni mwenye mawazo mengi sana kichwani kwake. Kuitwa na Rais Ikulu tena kwa kupewa dakika thelathini lilikuwa jambo ambo lilimstaajabisha na kumshtua sana.. Hukuwahi kuitwa na Mheshimiwa Rais kwa kupewa Amri kama ile. Alihisi Miguu Yake ikigongana pale alipoufikiria Mwisho Wake. Hakupenda kuiharibu sifa Aliyojiwekea Katika Nchi hii kutokana na Utendaji kazi Wake uliyotukuka. Akaiona aibu na dharau kubwa mbele Yake... Punde akalikumbuka Jambo, jambo ambalo aliliona ndio sahihi kufanywa katika kipindi kile. Akaitwaa Simu yake kutoka kwenye mifuko Yake.. Akatafuta namba fulani punde akairuhusu simu Yake.. Upande wa pili ukapokelewa na mwanadada.. Akaongea naye Maneno mawili matatu kisha simu ikakatwa.

****
Ilikuwa Jumapili tulivu Yenye kajua na mawingu kwa mbali.. Mohamedi, Jenifer na Didas Rugimbana walikuwa kwenye kikao kizito.. Kilikuwa kikao cha kuandaa Ushahidi na Ripoti Nzima Kuhusu Uhusika wa Waziri Mkuu na Mawaziri waandamizi katika mpango wa kufanya mapinduzi.. Lakini wakati wakiendelea kupanga hili na kupangua lile, Ukaingia Ujumbe kwenye Simu Ya Mohamedi.. Ulikuwa Ujumbe kutoka kwa mwanadada Ummu Sammy.. Ulikuwa Ujumbe ulioandikwa kwa Mafumbo na Kwa Lugha Maalum.. Ulikuwa Ujumbe uliomsisimua Mohamedy, Ulikuwa Ujumbe uliowasisimua Wote.. Ulikuwa ni Ujumbe uliOtumwa mahususi.. ''KUNA MPANGO WA KUMUUA RAIS LEO ATAKAPO HUDHURIA MAZISHI YA CAPTAIN GEORGE MICHAEL'' ulisomeka hivyo. Mohamedy akamuangalia Jenifer, Jenifer naye akamuangalia Didas.. Wote wakaangaliana kwa Muda huku Macho Ya kiongea.. Hawakuwa na Muda wa Kuchelewa.. Walitakiwa kuondoka pale kuwahi sehemu Husika.. Mohamedi Akawaomba Jenifer na Didas Kutangulia.. Yeye alitaka kwenda kuonana na Mheshimiwa Rais.. Alitaka kwenda kumwambia kile ambacho anatakiwa kukifanya pale.

Punde tu wote walikuwa njiani kila mmoja akielekea kwake.. Didas Alikuwa akizungumza na Walinzi binafsi wa Mheshimiwa Rais. Alikuwa akitoa maagizo Ya kufanyika hili na Lile kuhakikisha usalama wa Mheshimiwa rais Unakuwa Safi kabisa. Wakati Didas Akiongea na kikundi kile, Jenifer alikuwa akimtafuta Revina Michael Kwenye Simu.. Lakini alishangaa kutokupatikana kwake hewani licha ya kutafutwa kwa Juhudi Zote. Hilo lilianza kumpa Hofu Jenifer dhidi Ya Usalama Wa Revina.. Haiwezekani tokea jana hakuwa anapitana kuna tatizo gani? Ni maswali ambayo yalikatizwa na mtu ambaye aliwapita katika gari lakini huku akiwaangalia kwa Muda Mrefu.. Uangaliaji Ule Haukuwa Sahihi katika Macho Ya Jenifer na Hata Didas.. Kila Mmoja akaushushwa mkono katika kiuno chake, ulikuwa mkono uliyokwenda kushika bastola zao Zilizotulia.. Wote wakarudi kwenye Usawa kisha kuanza kutembea kwa Umakini Zaidi.

Wakati hilo likifanyika, Upande Wa Mudy ndio kwanza alikuwa akilivuka Geti la Kuingia ndani Ya Ikulu.. Alifuata utaratibu wote, baada ya Muda akaruhusiwa kuonana na Mheshimiwa Rais. Mazungumzo Yaliyofanywa kati ya Mohamedi na Rais Hayakuchukua Dakika Hata kumi.. Punde Mohamedi alionekana akiagana na Maafisa Usalama Wa Ikulu na kuondoka kuelekea maeneo Ya feri akitembea kwa miguu Bila kuwa na hofu Ya Aina Yoyote. Kila alipokuwa akitembea macho yake yalikuwa yakitizama Eneo lote kwa Hila.. Alikuwa akitizama kujua kama kuna watu waliokuwa wakimfuatilia.. Ni kweli aliwaona.. Ni Kweli Kulikuwa na Watu wawili waliokuwa wakimfuatillia.. Kati Ya hao mmoja alikuwa na Mvi kichwani kuonyesha kuwa Alikuwa mzee, na Mwingine alikuwa ni kijana ambaye alionekana kushika Mfuko wa Rambo kuonyesha kuwa alimsaidia yule jamaa mwenye mvi. Kwa watu Wenye macho Ya kawaida wangeweza kuamini kuwa wote walikuwa ni Mtu na Mwanawe, lakini kwa Mohamedi wale hawakuwa watu wa kawaida.. Alitambua walikuwa ni watu waliomfuatilia tokea aliposhushwa na Tax pale Wizara Ya Ardhi... Akaongeza Umakini huku mkono wake ukiwa tayari Kwa Lolote.. Ni Hapo alipokuwa Akikona kuelekea Barabara iendayo Kivukoni akamuona mwanamke Mmoja mwenye Baibui akimjia kwa Mbele.. Alikuwa Akitembea kama mwanamke Wa Kawaida. Lakini haukuwa Ukawaida Machoni kwa Mohamedi.. Alimuona Mwanamke Yule ni kama wenzake.. Punde akauona Mkono wa mwanamke Yule Ukizamishwa ndani Ya Baibui kitendo kilichofanyika katika Muda wa Nukta mbili tu.. Lakini hakuujua Wepese wa Aliyembele Yake, Hakuujua wepesi wa Mohamedi.. Kwani wakati Mkono wake ukizamishwa ndani Ya Baibui, Mohamedi alikuwa Tayari ameshachupa na Kuangukia Upande Wa Ndani Wa Soko la Samaki.. Risasi ikachimba Ukuta na kutokea Upande Mwingine.. Aliangukia hapo akachupa na kujiviringisha mfano wa Tairi.. Alipokuja Kusimama Akatabasamu Baada Ya kuwaona Wana Usalama wakija kwa kasi kubwa.. Kati Ya Wote hakuna Aliyejua kilichotokea.. Watu walikuwa wakikimbia Hovyo Kila mmoja akienda upande Wake.. Mudy Akatulia kutizama kilichokuwa kikiendelea lakini Ghafla Akasikia Yowe nyuma Yake, AKAGEUKA KUTIZAMA
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 054

AKASIKIA YOWE LIKITOKEA NYUMA YAKE. Mudy akageuka bastola ikiwa mkononi.. Macho yake yakatua kwenye mwili wa mtu uliyolala chini ukivuja damu. Mudy hakujiuliza mara mbili wala tatu, akaondoka katika purukushani zile. Aliondoka huku akijua vijana wake walikuwa Nyuma yake. Kitendo cha kuuona mwili wa mtu ukiwa na matundu ya Risasi lilikuwa ni jibu kuwa Yupo mtu, mtu ambaye alikuwa akisafisha masalia. Hakutaka kubaki katika giza.. Alihitaji kumuona Huyo kijana.. Alitaka kufahamu alitoka wapi? Lakini hakumuona, hakumuona kwa kuwa feri haikuwa salama tena. Watu walikuwa wakikimbia hovyo.. Mudy akajiunga kwenye mbio zile, mbio ambazo hakuujua mwisho wake utakuwa upi. Hakujali hilo, bali alihitaji kuliacha eneo lile. Huku mkono wake ukiwa umekamata bastola iliyofichwa na vazi lake, akatoweka katika macho ya watu.. Sasa alikuwa akielekea kule walipo Jenifer na Didas. Alihitaji kushiriki katika kumlinda Rais. Mawazo yake yalikuwa mbali sana huku akili Yake ikichemka katika kufikiria jinsi Ya kumuokoa Rais.

Wa kwanza kufika msibani alikuwa Jenifer.. Miwani myeusi machoni, mavazi meusi Ya heshima na kuonyesha msiba, alikuwa amewahi na kubana upande wa kushoto wa kuingilia.. Upande ambao ulikuwa na uwezo wa kuona kila kiumbe ambacho kinaingia Eneo lile. Macho yake hayakutulia Sehemu Moja.. Alikuwa akitizama kila upabde kwa hila.. Wakati akitizama akawaona watu wawili wakiingia.. Wa mbele aliweza kumtambua lakini wa nyuma hakuwahi kumuona popote. Mbele alitangulia REVINA MICHAEL na nyuma alikuwa akifuatia mwanadada mwingine.. Mwanadada ambaye hakuonyesha Uhatari wa Aina Yoyote.. Bado alikuwa akiwatizama.. Hata Macho Yake yalipokutana na Yale ya Revina akaliona tabasamu. Tabasamu Ambalo halikuwa Rasmi. Lilikuwa tabasam tofauti sana, tabasamu lililobeba maswali lukuki kichwani kwa Jenifer. Hakujua kwa nini alihisi kitu katika kutokana na tabasamu la revina.. Lakini aliona kuna Ujumbe ambao ulifikishwa kwake pasipokuambiwa. Akatulia.. Alitulia kwa muda wa Dakika kama Tano, punde akawaona wanaume wengine wawili wakiingia. Hawa walionekana kuwa ni wageni. Wageni katika jiji la Dar es salaam, na wageni katika nchi Ya Tanzania. Kila mmoja alikuwa katika suti matata, suti ambazo ziliwatoa na kuwafanya wapendeze sana.. Kengele Za hatari zikagonga kichwani mwake. Mwendo wa wanaume wale ulikuwa mwndo ambao aliufahamu.. Aliufahamu kwa kuuona Sehemu. Lakini hakujua aliuona wapi na katika Shughuli gani, alichokumbuka ni kwamba kuna mahali aliwahi kuuona huu mwendo wa watu hawa. Licha ya kutokukumbuka huu mwendo wa watu hawa bado alikuwa akiwatilia mashaka huku akiwatizama wanapoelekea.

Sehemu yote iliwekwa chini ya vijana kutoka Idara Ya Usalama wa Taifa. Kila mgeni aliyeingia alipewa utaratibu wa kukaa na kusubiri ratiba kamili ya Mazishi ya Captain George.

Wakati yote hayo yakiendelea, katika Jumba fulani karibu na sehemu yenye msiba alionekana mwanadada Akiingia. Aliingia kama mgeni wa kawaida.. Aliingia kama mteja, na hata alipoulizia Chumba hakusita kuambiwa kuwa vipo na vilikuwa vikimsubiri. Haukupita Muda mrefu kukamilisha ulipaji na kukabidhiwa Funguo ambazo zingemuwezesha kuingia chumbani kwake. Alipoondoka tu kuzikwea Ngazi Nyuma Yake akafika mtu mwingine.. Huyu alikuwa mwanaume wa makamo.. Alikuwa mwenye uwalaza na mwenye kuonekana na mvi kichwani. Macho yake yalionekana kuwaka yakitizama kila kona ya Jengo lile. Naye akakiulizia Chumba, alipotajiwa akataka kujua kama ni Jirani na mwanamke aliyeingia Muda mfupi Uliyopita.. Akajibiwa kama alivyotarajia kuwa ni karibu na chumba cha mwanadada aliyeingia hivi punde. Akatabasamu, akabeba mzigo wake na kuelekea juu. Alipanda ngazi huku akiwa makini kwa kila kitu, alitegemea chochote kutokea pale..Kuondoka kwa mwanaume Yule kukaleta ukimya... Ukimya ambao ulivunjwa na kuingia kwa mwanaume Mwingine.. Huyu alikuwa ni mwanaume ambaye alioneka kama mcheza Sinema. Suti yake aliovaa ilimpendeza Sana na kutengeneza maswali kwa Watoto wa kike.. Alipoingia tu hakwenda mapokezi kama waliomtangulia, yeye aliongoza moja kwa Moja kuelekea Juu.

Bastola ilikuwa ikichungulia kuwaonyesha watu kuwa huyu alikuwa mtu Hatari. Mtu ambayr hakuwa na Muda wa kucheka.. Akazipanda ngazi kwa Haraka bila kuhisiwa.. Alipomaliza ngazi akapokewa na Ukimya wa Ajabu.. Ukimya ambao ulimfanya mwanaume Yule kuongeza Umakini, Umakini Uliosababisha Achomoe Badstola Yake.. Akaongeza Hatua mbili mbele, akapokewa na Mwili wa Mwanaume Ukielea Katikati Ya dimbwi la DAMU HUKU KISU KIKUBWA KIKIONEKANA KIMEZAMISHWA TUMBONI. utumbo ulikuwa umetoka nje.. Mwanaume Yule hakujishuhulisha na Ule mwili.. Bado alihitaji kumpata Aliyemkusudia, Kumpata akiwa Hai au Mfu.. Hakuwa Mwanaume Mwingine, hakuwa mpiganaji Mwingine.. Huyu Alikuwa Mohamedi... Naam Huyu alikuwa Mudy akiutafuta ushahidi Kwa udi na Uvumba.. Bado Ukimya Ulitawala na Bado Damu ilinukia.. LANINI MOHAMED HAKUOGOPA..
 
Back
Top Bottom