MKE WA RAIS
SEHEMU YA 65
HALI ILIKUWA TETE!
akairuhusu mikono yake kushuka chini alipohifadhi bastola yake. Akauruhusu mkono wake kuichomoa bastola ile kwa wepesi wa ajabu. Ikaikamata mkononi, akiangalia kilichokuwa kikitokea. Alikuwa akishangaa mwanadada yule alivyokuwa akichinja na kukata vichwa. Aliushangaa wepesi wa mtu huyu, akaushangaa urukaji wake. Alikuwa akiruka huku upanga umetangulizwa mbele. Kila alipokuwa akiruka upanga ulikuwa akiifacha kazi nzuri. Hatimaye mwanamke yule akatua mbele ya Mohamedi. Kutua kwake kulifuatiwa na mtazamano wa sekunde Zisizozidi tano. Alikuwa akimuangalia Mohamedi Kwa Jicho lenye maswali. Bado Mudy aliduwaa bastola mkononi, bado aliduwaa kutokana na kutokea kile ambacho hakukiamini. Mwanamke aliyekuwa akiuwa kumbe Alikuwa Ummu Sammy. Hilo ndilo lililomfanya Mohamedi kuduwaa. Alimfahamu sana Ummu lakini hakumfahamu katika aina ile ya kininja. Aina ya Ninja mpambanaji. Tabasamu likachanua kwenye nyuso Zao. Wakajiondoa na kuelekea upande mwingine. Kila chumba walichokuwa wakiingia Kumuangalia Rais, Bado hawakuwa wakimuona. Wote wakajigawa kwa mara nyingine. Jengo zima likatawaliwa na milio ya risasi.
Hawakumuacha kila aliyejitokeza mbele yao. Kila mmoja alikuwa akipambana kuhakikisha nchi inarudi kwenye mikono ya Rais aliyemadarakani. Wakauvuka uzio unaotenganisha majengo yale, bado hawakumuacha mtu, bado hawakumuacha yoyote yule. Kuuvuka uzio unaotenganisha jengo lile, kukawafanya watokee sehemu yenye milango mingi. Mohamed akamrudisha Ummu Nyuma, Kisha Yeye kutangulia mbele. Hakuwa akiogopa na hakuwa akihofia. Akauendea mlango mmoja na kujaribu kuufungua lakini ulikuwa mgumu. Hakutaka kutumia risasi wala funguo malaya Alizonazo. Alichokifanya ni Kurudi nyuma na Kuruka kwa Miguu yake miwili na kutua kwenye mlango. Mlango haukuwa na jinsi. Akasalimu amri. Mohamed akaangukia kwa ndani akifuatiwa na Ummu. Baada ya kuingia kwenye Chumba kile walitambaa mpaka nyuma ya mbao zilikuwa chumbani mle. Wakatulia huku wakiangalia kule na Huku. Lakini hawakuambulia kukiona chochote. Wakatulia huku kila mmoja akiwa makini na tayari kwa lolote. Muda ulizidi kuyoyoma huku ukimya ukitawala. Wakaendelea kuuvuta muda lakini hawakuona chochote isipokuwa ukimya tu. Zikapita kama dakika kumi na Tano bila kutokea chochote. Wakiwa wanakaribia kujiondoa pale, wakasikia mlio kama wa nyayo za binadamu zikisogea karibu yao.
Wakatizamana kisha kupeana Ishara. Punde wakashangaa kuiona sehemu yenye ukuta ikifunguka kisha wasichana watatu waliovalia mavazi Ya kijeshi wakatokea. Walikuwa wasichana warembo lakini wakakamavu. Hawakufanana na wanajeshi wa Tanzania. Hawa walionekana ni wanajeshi kutoka nchini Rwanda. Mohamed na Ummu hawakutaka kusubiri. Wakatokea Mbele yao mfano wa Vivuli. Kinyume na walivyotarajia kuwa, Wale madada watashtuka baada ya kuwaona. Haikuwa Hivyo. Sura zao zilibaki kwenye uzuri wao ule ule. Hawakuonyesha kubabaika wala kufanyakitu chochote. Wote wakawatolea macho Mohamedi na Ummu. Waliwatazama kanakwamba wanatizama kinyeshi. Hawakuionyesha Hofu kabisa Machoni mwao. Hili likamshtua Mohamedi. Likamshtua kwa aina tatu tofauti. Kwanza ni Kule kujiamini kwao.
Pili, nikule kuwaangalia kwa kuwadhihaki na chatatu ni kule kuendelea kuongea kwa Lugha Yao bila kujali wapo sehemu gani na Wapo na watu gani.
Tabasamu la kebehi lilizipamba nyuso Zao. Wakata kuwapita wakina Mudy ili waendelee na Safari yao. Hapo ndipo kulichotokea kile ambacho hakikutarajiwa. Walipotaka kupita Mohamed alisogea pembeni kutoa Nafasi kwao. Lakini ni wakati wakiukaribia usawa wa aliposimama Mohamed na Ummu Sammy, mikono mypesi ya wasichana wale ikazama katika mifuko ya Magwanda Yao. Lakini ikaishia kuzama tu, haikuweza kutoka tena, haikuweza kupewa nafasi kutoka na chochote kile. Haikuruhusiwa hata kucheza. Muda ule ule Mohamedi alikuwa hewani Sambamba na Ummu. Kila Mmoja akaachia mapigo matatu mazito. Mapigo ambayo yalishindwa kuzuiwa na Wasichana wale. Wote wakayumba nusura ya kuanguka. Hawakupewa muda wa kusimama Sawa. Mudy na Ummu wakawaendea kwa mitindo tofauti. Wasichana wale wakakaa imara na kuanza kujibu mashambulizi. Yalikuwa mapambano makali sana, mapambano yalioumaliza ufundi wote. Wasichana wale walionyesha kuhimili kila aina ya mapigo. Kila pigo walikuwa wakijibu. Kila pigo walikuwa wakijaribu kuzuia na kushambulia. Lakini mwisho hawakuweza tena kuhimili, kuhimili mapigo, mapigo ambayo yalipigwa kwa Ufundi, utaalam na hata uzoefu. Walishindwa kuzuia staili za Ninja kutoka kwa Ummu. Wote wakaregea na kutambarajika. Damu zilikuwa zikiwavuja, sura zao na Urembo wao ulikuwa Umepotea kwa Sababu ya kipigo. Kila Mmoja alionekana kama amekanyagwa na kusagwa na Mashine. Hawakutaka kuwaua, bali walitaka kuwatumia kujua Wapi alipofungiwa rais. Lakini hawakuambulia kitu, kwani walipotaka kuanza kuwahoji Wakashangaa Kuwaona mateka Wao Wakiwa wamepoa Huku macho yao yakiwa Yametoka. Ndipo walipowagusa kuangalia kilichotokea: WAKASHANGAA KUKUTA WOTE NI MAITI KILA MMOJA AKITOKA MAPOVU MDOMONI