Riwaya: Mke wa Rais

Riwaya: Mke wa Rais

Ubarikiwe mkuu sijui unaendelea au ndo kesho tujilalie
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 55

MOHAMED HAKUOGOPA! AKAINGIA.
macho yake yakapokewa tena na mwili wa mwanamke, mwanamke aliyelala chini, paji la uso wake lilikuwa limefumuliwa kwa risasi.. Ubongo ulikuwa umezagaa sehemu yote. Mudy akaduwaa, akaduwaa kwa kuwa hakumuona mtu kuingia ndani.. Na hata wale aliowaona na kuwatilia mashaka walikuwa wameuawa.. Wameuawa kinyama kuonyesha kuwa muuaji alikuwa ni mtaalam kupindukia.. Mudy akainama kuushika mwili wa mwanamke Yule.. Wakati akiinama alihisi uwepo wa mtu nyuma yake, Mtu ambaye alikuwa akimtizama tayari kumuondoa.. Hakuwahi kugeuka, hakutaka kufanya hivyo kwa kuwa alihisi yule mtu Yupo mbali.. Akaendelea kuinama kuona kama mtu aliyenyuma Yake atasogea. Haikuwa hivyo na hapa kuwa na Muda wa kusogea.. Ni ndani ya Sekunde ile akashuhudia kishindo kutoka Nyuma Yake, pale ambapo alihisi kusimama mtu.. Bastola mkononi tayari kwa Mapigano. Mudy akageuka.. Lakini kile alichokitegemea Sicho alichokikuta.. Sicho alichokiona na sicho alichokuwa akikitizama.. Alichokuwa akitizima Ulikuwa mwili wa Mtu ukiwa umetambarajika Chini.. Kama wele marehemu waliopita.. Na huyu alikuwa amepigwa Risasi, risasi ya kisogoni.. Amepigwa bila kusikika kwa kelele.. Muuaji Alikuwa ni muaji Mkubwa, Mwenye ujuzi wa hali ya Juu, Ujuzi Uliyomfanya Mudy atabasamu.. Hakuwahi kuona katika Tanzania Hii uuaji wa Namna hii.. Uaji Wa Aina Hii mara Ya mwisho Aliouna Kule afghanstan.. Alipokwenda kuwaokoa wafanyakazi wa Shirika la kuhudumia wakimbizi Duniani waliokuwa wametekwa na kufungiwa Chini Ya mapango.

Hakumjua anayefanya Mauaji na wala hakuweza kuhisi kuwa ni mtu furani.. Alichokifanya ni kuondoka.. Katika akili yake ya kimapambano kuna kitu ambacho alikuwa akikihisi.. Kitu ambacho alikiona kama kitisho kwake.. Kuuawa kwa watu kwa aina hii tena na mtu asiyefahamika ni picha kuwa alikuwa akizuiwa kwenda sehemu.. Sehemu ambayo kungesababisha kutokea kwa Mambo Mengi.. Lakini kwa nini Muuaji Hakuwa na Shida naye.. Kwa nini auwe watu ambao ni wa upande Fulani? Bado akauona Ugumu katika kulipangua hilo tatizo.. Hakuwahi kuogopa wala kutishwa.. Alikuwa akisubiriwa Yeye atoe tamko Ili Rais Awasili Sehemu Husika.. Alipofikiria hilo akili Yake ikachemka Haraka.. Akazipanda Ngazi kuelekea Juu.. Bado alikutana na kile alichokutana nacho mwanzo.. Muuaji alikuwa akiuwa kimya kimya.. Uaji ambao Ulikuwa burudani katika Macho Ya Mohamedi.. Burudani katika kuitizama na Hata kuicheza pia.. Watu walikuwa wamelaliana mfano wa magunia.. Mohamedi akasonga na Kusonga, alikuwa akichungulia hapa na pale, Alikuwa akipita hapa na kutokea pale.. Bastola Mkononi akitambaa na kuambaa Na Jumba Lile.. Kabla hajafikia mwisho akasikia sauti Ya mtu akipiga kelele.. Lakini kelele Zikitokea Chini, Mara kukafuatiwa na kitu kama Mlipuko.. Ni Wakati huo milio Ya Risasi ikatawala katika Eneo la Chini.

Mudy Hakujishughulisha na Hilo.. Bado alihitaji kufika mwisho na bado alikuwa akihitaji kumuona Muuaji.. Akaendelea kusonga mbele.. Alipotokea Sehemu Yenye uwazi mpana.. Macho Yake yakawashuhudia Wanawake Wawili wakipambana.. Wanawake ambao wote walionekana kuchoka, kuchoka kutokana na kupigana kwa Muda Mrefu.. Macho Yake yakawatambua Wote.. Alikuwa Revina Michael na Kanali Jamila Hassan.. Wote walikuwa hoi.. Kila mmoja hakuwa na Uwezo wa Kurusha Ngumi.. Mohamedi Hakutaka kanali Jamila Auawe.. Alitaka kupata kila kitu kutoka kwake Juu Ya Ushiriki wao katika Mapinduzi Yao... Alitaka kujua nani alimuua Mke Wa Rais.. Wakati Akiliangalia Hilo, likatokea tukio ambalo hakulitegemea.. Tukio ambalo lilimuacha akichupa na kuangukia kando.. Risasi Kutoka Nje kwa kupitia Dirishani Ilitosha kumnyamazisha Kanali Jamila. Risasi iliufumua Ubongo Wake Na Kumtupa Umbali Mrefu, alipoanguka Chini alikuwa tayari ni Marehemu.. Mohamed hakuinuka kwa Muda ule.. Bado alendelea kutizama.. Hata pale ambapo alikuwepo Revina Alishangaa kutokumuona.. Alishangaa kutoweka kwake katika Mazingira Ya ajabu kama Yale.. Wakati Akichungulia Huku na Kule macho Yake yakamuona Revina.. Hakuwa Revina peke Yake bali alikuwa ameshikwa na Luteni Sevenlee Huku bastola Ikikilenga kichwa Chake. Mohamedi akaendelea kubana pale pale Chini. Hakutaka kutokea kwa upesi.. Akaendelea kuwa pale Chini.. Hata pale alipokuwa akiita jina la Mohamedi na Kumtaka Ajitokeze ili iwe salama kwa Revina, Bado Mudy Hakufanya Hivyo.. Bado alikuwa akipanga na kupangua nini afanye ili kumuondoa Revina mikononi Mwa Luteni.

Akaishika bastola Yake, akainua mkono na kuitupa Sehemu tofauti na alipokuwa Luteni Sevenlee.. Kishindo cha bastola Kutua chini kikamfanya Luteni Sevenlee Ageuze macho kutizama kule.. Hilo likawa kosa kubwa sana, kosa ambalo lilimgharimu.. Hakuwahi kurudisha macho Yake.. alijikuta akipigwa Pigo Moja la Kung fu.. Pigo kutoka kwa mwanadada Revina.. Pigo lililomuangusha. Akainuka kwa Kuruka Sarakasi. Alipokuja kukaa sawa, Alijikuta Akitizamana na MIDOMO MITATU YA BASTOLA.. AKATULIA
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 056

Alipokuja kukaa sawa.. AKAJIKUTA AKIZIMANA NA MIDOMO MITATU YA BASTOLA.. AKATULIA... mbele ya macho yake alikuwa amesimama Mohamedi na Revina.. Hawakuonyesha kucheka wala kutabasamu.. Macho yao yaliakisi kazi wa Ifanyayo, kazi ambayo ilikuwa maalumu kwa kuiokoa nchi kutoka mikononi kwa wachache. Macho ya Mudy yalikuwa usoni kwa Luteni Sevenlee.. Luteni aliyeamua kuasi na kukisaliti kiapo chake.. Hakuondoa jicho lake usoni.. Alikuwa akikisoma kile awazacho Luteni yule, alikuwa akikisoma kile ambacho kilikuwa kikipita mawazoni mwake.. Hawakutaka kutoa nafasi katika kufanyika kwa kitu chochote.. Bado midomo ya bastola ilimtizama na bado macho ya makomandoo wawili waliofuzu mafunzo ya aina zote yakimtizama. Wakati wakitizamana kikatokea kitendo ambacho kiliwaacha wote kwenye taharuki. Hakukuwa na Aliyeamini kama kingefanyika kitu kama kile tena kwa haraka katika muda wa sekunde tano.. Mwanamke mrembo aliyetoka kama mpangaji katika jumba lile.. Akawapita Mohamedi na Revina katikati huku akionyesha kutetemeka. Lakini nimsichana Huyo huyo aliyefanya kitu alipomfikia luteni Sevenlee.. Kitu kilichofanywa katika Muda mchache na muda ambao hakukutarajiwa..

Mohamedi na Revina walijikuta wakikiangalia kitendo kile kwa burudani kubwa.. Pale damu kutoka kwenye kichwa cha luteni Sevenlee iliporuka na kuchafua sehemu Yote.. Risasi kutoka kwenye Bastola ndogo mfano Wa kalamu ilikamilisha safari ya maisha ya Luteni Sevenlee.. Akaanguka chini huku mkono wake akiuweka Juu ya Kichwa kuonyesha kuwa alikuwa kitoa heshima ya Saluti.. Heshima ambayo ni kuonyesha heshima kwa mtu aliyekuzidi.. Revina Akaipokea Saluti ile katika Heshima ile ile ya kijeshi.. Binti aliyefanya tukio akapotea, akapotea mbele ya Macho Ya Mohamedi na Revina.. Hata walipotupa macho huku na kule hawakuambulia kitu.. Muaji Wa Luteni alishatokomea na kupotea.. Hawakujua wala kutambua kuwa ni nani, hawakumjua kabisa.. Wakatizama kwa mara Nyingine. Bado hawakuambulia kumuona mtu huyo.. Ni mwanamke gani Huyu? Lilikuwa swali lililowazindua Mohamedi na Revina.. Wakauacha mwili Wa Luteni Sevenlee, wakaongoza nje kumsaka mwanamke Yule.. Lakini kile ambacho hawakukiwaza hapa wakakiona, bado wahudumu na Wapelelezi kadhaa walikuwa chini wakivuja Damu.. Matundu Ya risasi hayakufichiki kwenye miili Yao... Wote walikuwa chini maiti.. Mohamedi akapata Ghadhabu Kubwa.. Kuuawa kwa vijana wa Usalama wa Taifa kulimuumiza Sana.. Akainua macho yake na Kuanza kutizama Sura Za vijana wale.. Chozi la Uchungu likamtoka... Likamtoka Pale Alipoushuhudia Mwili wa kijana Shupavu Didas Rugimbana Ukiwa umelala katikati Ya Dimbwi la damu bila kuwa na uhai.. Akainua mguu wake kupiga hatua.. Alikuwa akielekea ulipo mwili wa Shupavu na mpiganaji wake.. Kijana kutoka kitengo cha walinzi binafsi wa Rais. Alipoufikia Mwili Wa Rugimbana akapiga magoti na Kuyafumba Macho Ya kijana Yule... ''NITAMUUA YOYOTE ALIYEHUSIKA NA KIFO CHAKO, DAMU YAKO HAITAKWENDA BURE.'' alipomaliza kuongea maneno hayo akainuka na kutoka ndani Ya Jengo lile akionekana ni Mtu mwenye Hasira Sana. Safari Yake haikuishia mbali na pale, bali ilikuwa imeishia upande wa pili wa mtaa Ule ambapo ndipo palikuwa na Msiba wa Captain George Simon.

Hapo aliongea machache na vijana fulani ambao walionyesha kuwa ni wanausalama na baada ya Muda mfupi ukasikika king'ora Kuashiria kuwa Msafara wa Rais ulikuwa ukiingia maeneo yale. Sehemu yote ilikuwa amewekwa nje Ndani.. Kila kitengo cha Usalama na Idara Zote zilihakikisha ulinzi ni Wakutosha. Kila mtu alikuwa akipekuliwa na kila gari lilikuwa kikisimamishwa na kuchekiwa pia.

Mohamedi akaitumia nafasi ya uwepo wa viongozi sehemu ile kujipenyeza na kuondoka mahali pale bila kuonekana. Kifo Cha Didas Rugimbana Bado kilimuumiza sana.. Alikuwa kijana ambaye hakupaswa kufa mapema kiasi hiki.. Kuondolewa kwake lilikuwa pengo kubwa sana nchini kwa kuwa Serikali ilipoteza Pesa Nyingi kumsomesha. Aliamua kuitembelea Nyumba ya Waziri Wa Mambo Ya Ndani Mh Salim Salim.. Alitaka kumalizana na Mmoja baada ya Mwingine.. Hakutaka kucheka na mtu kwa sasa.. Zilitumika Dakika Chache kutoka Kindondoni Mpaka Masaki.. Akipita hapa na Kupita pale.. Ingawa ulikuwa mchana lakini hilo halikumtia hofu kutokana na Mazingira Ya masaki kuwa kimya Muda Mwingi sana. Mudy Akaitumia Nafasi Hiyo kulifikia Jumba la Waziri. Akalisogelea geti la Kuingila kwa kuwa hakupenda kuingia kwa mbinu zake, akawasabahi maaskari Waliokuwa wakilinda UsAlama Nyumbani Hapo Kwa Waziri, kisha akaomba kuonana na Mh Waziri..

Askari wale wakatizamana, lakini wakati wakiwa bado hawajaamua MOhamed alikuwa tayari Ameshalisukuma geti na Kuingia Ndani.. Askari Wakapigwa na Butwaa kisha kuanza kumfuata kwa nyuma.. Mohamedi hakujali, akaendelea kutembea akiwa hana Wasiwasi Wowote.. Hata waliomfikia na Kumsimamisha Huku Bunduki Zao Zikimtizama, Mudy Akachomoa moja ya kitambulisho chake kinachomtambulisha kama Kamishna Msaidizi Wa Jeshi La Polisi. Punde saluti Zikapigwa, akaruhusiwa Kuingia ndani Ya Jumba la Waziri....
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 57

Akiwapita Walinzi kama hakuwa na muda nao.. Hakusubiri kupewa wala kuletewa kitamburisho chake. Bastola mbili zilikuwa mgongoni akielekea ndani Ya jumba la Waziri Wa Ulinzi. Kila alipokuwa akipiga hatua alizidi kuhisi ukimya wa hatari, bado alihisi alikuwa afuatiliwa na macho ya mtu kutoka sehemu fulani. Alijuwa uwepo wa watu katika jumba hilo lakini Mohamedi Hakutaka kuogopa. Alizamilia kukijua kila kilichoendelea mpaka kuuawa kwa Mke Wa Rais. Akauvuka mlango na kuingia ndani.. Aliukuta mlango wazi kuonyesha kuwa ulikuwa umefunguliwa kwa makusudi.. Huyu alikuwa Mudy, komandoo na mkufuzi wa Masuala yote ya kujasusi.. Alikuwa akitambua kila mtego, alikuwa akitambua kila hila zinazofanywa.. Hakubabaika na kuachwa wazi kwa mlango, Hakuogopeshwa na Ukimya wa Jumba lile.. Aliamini kulikuwa na watu kwa ndani Yake. Akatembea kwa hatua za tahadhali, mikono yake myepesi ikiwa tayari kuzifikia bastola Zake pale inapopaswa kuwa hivyo. Akauvuka mlango wa pili na kutokea kwenye sebule kubwa katika Jumba la waziri.. Kuingia akapokelewa na tukio ambalo lilimshtua na kuusisimua mwili wake. Mwili wa waziri wa mambo ya Ndani ulikuwa chali pale sebuleni huku damu ikionekana kuganda kuonyesha kuwa, Waziri Aliuawa mda mrefu sana..

Mkono wa Mudy ukawa tayari umeshaifikia bastola, ulikuwa umeshaishika bastola. Akausogelea mwili wa Waziri pale chini, akauangalia kwa makini ule mwili. Mkono wa kulia Wa Marehemu ulikuwa umekamata bastola.. Bastola ambayo ilionekana kama ndio imetumika kufanya mauaji. Kwa ushikaji ule wa bastola kulimaanisha kuwa waziri alikuwa amejiua mwenyewe na hata kwa mtu mwenye macho yasio na Udadisi anaweza kuhisi Hivyo. Lakini kwa upande wa Mudy alihisi kitu kingine kabisa, aliyaona mauaji katika macho Yake. Hata bastola iliyomkononi kwa Waziri ni bastola ambayo ilionekana kama ameshikishwa na watu.. Mohadedi akahama hapo na kuanza kuangalia huku na huko.. Kila aalipokuwa akipita alikuta vurugu za hapa na pale.. Vitu vilikuwa chini na vingine kupasuka kuonyesha kuwa kabla ya kuuawa kwa Waziri Wa Mambo Ya ndani kulikuwa na mapambano makali sana katika Jumba hilo.

Akaanza kuangalia kimoja baada ya kingine huku akiwa makini asiharibu ushahidi. Kutoka hapo sebuleni akakifuata Chumba ambacho alihisi ndicho anacholala Waziri.. Alipokishika kitasa akagundua kuwa mlango hakuwa umefungwa, mlango ulikuwa wazi.. Akasita huku neno MTEGO likigonga kichwani kwake. Akaufungua mlango kwa tahadhali huku mdomo wa bastola ukitangulia.. Akaupeleka uso wake ndani kutizama, macho Yake yakatua kwenye mwili wa binti wa makamo ukiwa Uchi kitandani huku ukivuja damu kutoka upande wa kushoto wa kifua chake. Risasi ilikuwa imeumaliza Uhai wa mwanadasa Yule. Mudy akausukuma mlango Zaidi na kujitupa ndani. Hapo akashuhudia matone ya damu na michirizi ambayo ilionekana kuelekea kwenye choo cha chumba kile. Kila hatua yake aliopiga Mudy masikio yake yalikuwa yakisikiliza kila kitu.. Hata kama ulikuwa mchakacho wa sisiminzi bado Mohamedi angeweza kuusikia pasipo na wasiwasi.

Akaendelea kuufuatilia mchirizi ule wa damu, punde akaiona miguu mingine bila kiwiliwili.. Mwili ukaendelea kusisimka. Alipoufikia mlango wa bafuni akachungulia kuiona sura Ya mwenye miguu.. Macho Yake Yakagota kwenye Mwili wa Mke wa Waziri Ukiwa umechinjwa kama Kuku.. Damu ilikuwa imezagaa Choo kizima.. Harufu ya mauti ilikuwa imetamalaki katika jumba la Waziri Salim Salim. Mohamedi akairudisha mlango na kutoka katika chumba kile, alipotokea tu Sebuleni macho Yake yakakutana na Macho Ya Inspekta Ummu Sammy.. Alikuwa ameikamata bastola mkononi huku akimlenga Mohamedi.. Lakini Mohamed hakujali wala hakumuangalia.. Akaendelea kuangalia Hiki na kile, alishika hapa na kuangalia kile.. Aliacha hiki na kwenda kukamata kile. Kulikuwa na kitu ambacho alikuwa akikitafuta, kitu ambacho kilionyesha kumtia wazimu.. Aligusa kila palipo na makablasha lakini bado hakufanikiwa hilo..

Wakati akianza kukata tamaa na kuondoka kutaka kuondoka katika jumba hilo, akaiona Bahasha, bahasha ndogo iliyotuna kuonyesha uwepo wa kitu ndani yake.. Akainama kuiokota.. Hapi hapo akakisikia kitu cha baridi kikimgusa kisogoni. Mohamedi akatabasamu. Tabasamu ambalo lilifutika ndani ya kipindi kifupi.. Lilifutika pale alipogeuka kwa mapigo kadhaa ambayo yaliwatupa chini askari kadhaa Akiwemo Ummu Sammy.. Mudy Hakuwa na Muda nao.. Hata pale Ummu alipoinuka ili kupambana na Mohamedi, akanywea baada ya kukutana na Macho ambayo hakuwahi kukutana nayo tokea alipoanza kumjua Mohamedi. Akatulia Huku akimtizama Mohamedi akiondoka katika Jumba lile. Akiondoka huku akionekana ni mtu tofauti.. Ni utofauti huo uliyomfanya Ummu Kujiuliza maswali Mengi.. Bado hakuwa anajua kile ambacho kilikuwa kikiendelea kwa wakati wote, hawakuwa anajua kipi Mohamedi alikifuata Arusha, lakini alipokuja kupata Siri Ya njama Za kumuua Rais ndipo alipohisi kuwa Kulikuwa na kitu kizito kilichokuwa kikiendelea Nchini.. Hapo ndipo alipoipata Hamu ya Kujua kile Ambacho HAKUKIJUA HAPO MWANZO
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 58

Akayaacha macho yake yamshuhudie Mohamedi akiondoka. Akiondoka katika namna ya kuvutia machoni mwa watu.. Alikuwa akitembea kana kwamba hakukuwa na lolote lililotokea. Akashuhudia Mohamedi akipotea machoni mwake mfano wa kivuli ama karatasi iliyopeperushwa na Baridi. Ummu akatabasamu huku akitamani kama angekuwa na Mohamedi.. Bado alijiona yupo gizani katika kile ambacho kilikuwa kikiendelea kutokea, alikuwa mgeni katika kutambua na kulijua jukumu lililobebwa na Mohamedi. Akasahau kwamba yupo kazini, alisahau kuwa anatakiwa kuripoti makao makuu kuhusu tukio la kuuawa kwa bosi wao. Lakini alionekana kutabasamu kila alipokuwa akimkumbuka Mohamedi, alikuwa akiyakumbuka mapigo yake. Alikuwa ni kama kichaa aliyepekee mbele ya Jumba la Waziri..

Baada ya kutoka katika jumba la waziri wa mambo ya Ndani, Mohamefi alikuwa njiani akielekea nyumbani kwa Waziri Wa katiba na Sheria bibie CeCilia Bruno Peter. Bado alikuwa akiwaza na kujiuliza juu ya mtu aliyefanya mauaji nyumbani kwa Waziri. Kitendo cha Waziri kuuawa akiwa na familia yake tena walinzi wakiwepo. Kulimpa picha kuwa kazi Ile Ilifanywa na mtu mmoja, mtu ambaye nu mtaalamu wa kazi Ya mauaji.

Kukuta vitu vikiwa vimesambaa huku na huko kulionyesha kuwepo kwa mapambano makali kabla ya mauaji yenyewe. Pia kulionyesha ni jinsi gani watu hao walivyokuwa wakikitafuta kitu, kitu ambacho kilionekana kutopatikana. Purukushani aliyoiona kwenye jumba la Waziri ilikuwa purukushani iliyomvutia kupita kiasi. Alitamani kuwapata watu hao, alitamani kuimaliza kazi mapema sana. Akaendelea kutembea kwa kupitia njia za mkato, alipoufikia Uzio Uliotenganisha jumba la Waziri wa katiba na Jumba la mtu mwingine. Mohamedi alishuhudia gari Ndogo Aina Ya Vitz ikiondoka kwa mwendo wa kazi huku nyuma akitokea mwanamke ambaye alionekana kuvuja damu kuonyesha kuwa alikuwa amepigwa Risasi. Mwanamke Yule alikuwa akiifuatilia ile gari kuonyesha kuwa kulikuwa na uvamivi kutoka ndani Ya Jumba la Mheshimiwa Waziri. Wakati Mudy akiendelea kuliangalia lile tukio, akashuhudia watu wengine wakitokea Nyuma ya Yule mwanamke. Hawa walikuwa wauaji haswa, hawa walionekana ni watu wasio na Huruma. Wote walikuwa na Bastola mkononi.. Wote walikuwa wakifanana na Wote walikuwa wakitembea mwendo mmoja.. Sekunde Ya kwanza Mohamedi alikuwa akiwaona wakitoka Ndani, na Sekunde Ya pili akauona Ubongo wa Yule mama Ukiruka Angani baada Ya kufumuliwa na risasi ya bastola Aina Ya Revolver colt 43.. Mama akarushwa juu na kwenda kuangukia umbali kidogo kutoka pale alipo. Kila kitu kilikuwa kikifanyika Huku Mohamedi akiangalia.. Alikuwa akiona kile ambacho kilikuwa kikifanyika mchana kweupe.. Hakuiona Sababu Ya kuendelea kujibanza.. Alihitaji kuwajua watu hawa, watu ambao walikuwa wakimuua waziri mchana kweupe.. Hakutaka kufikieia sana, Hakutaka kusubiri watoweke Machoni mwake na pia hakutaka kuitumia bastola kufanya chochote kile, alitaka kuwaonyesha kwamba hata Yeye ni Mpiganaji, Mpiganaji aliyeaminiwa na Rais. Akauparamia Ukuta mithiri ya Ninja.. Akatua kama Unyoya wa Kuku bila kutoa kishindo. Akatembea kama Upepo bila kuonekana.. Akawazunguka kwa Utembeaji wa kishaolin, Mfupo baadae alikuwa amesimama Mbele Yao, mbele ya Watu wale wawili. Watu ambao hawakuuficha mshtuko wao baada ya kumuona Mudy akiwa amesimama Mbele yao. Ulikuwa kama muujiza kwa kuwa muda mfupi walikuwa wakijitanua wenyewe lakini sekunde ya pili wakashangaa kumuona mtu.. Mtu ambaye alikuwa amekamatia bastola mkononi, Bastola ambayo ingekuwa na Uwezo Wa Kuwamaliza hata kabla ya kufika pale. Kwa nini hakuwaua? Kwa nini aliamua kujitokeza kuonyesha kuwa hana wasiwasi? Huyu ni nani na kwa nini Yupo hapa? Hawakumaliza kile walichokuwa wakijiuliza pale mapigo mawili ya Mohamedi Yalipowatupa chini.. Wakati wanachupa na kusimama ili kukabiliana na Mohamedi, wakashangaa kuliona geti likusukumwa.. Wakaingia wasichana wawili warembo, wasichana walioingia mithiri Ya makomandoo.. Alikuwa Jenifer na Revina. Watu wale wakageuka kutizama Kule getini, wakasahau kuwa Mohamed alikuwa mbele Yao.. Akawashtua kwa mapigo matatu Ya Kung fu, mapigo ambayo Yaliwaingia na kuwawika Sawa.. Hawakuwa wataalam wa mapigano kama Mudy alivyodhania.. Walikuwa waoga kupindukia, walikuwa hawana lolote katika nyanja za kimapigano.. Ndani ya Sekunde kumi wote walikuwa Chini Wakitweta. Walikuwa wakitweta kama Majogoo.. Wakatiwa Pingu na kuinuliwa kutolewa katika jumba lile.. Wakati Watu wale Wakitolewa Nje, Mohamedi pamoja na Jenifer wakaingia ndani ya jumba lile. Kuufungua mlango tu Wa Kuingilia Ndani Macho Yao Yakapokewa na mwili wa mtu Ukiwa umelala Chali katikati ya Dimbwi la Damu. Mwili ambao ulikuwa Umezungukwa na Makaratasi mengi sana.. Wote wakaaangaliana kisha kupiga hatua kuufuata Mwili wa mtu Yule. Walipoufikia Wote Wakapigwa na Butwaa Wasiamini kile wanachokiona.. Mwili uliokuwa Umelala Chini Ulikuwa Mwili Wa WAZIRI MKUU WA NCHI ukiwa na matundu mengi Ya RISASI.. WOTE WAKACHOKA
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 59

MWILI WA WAZIRI MKUU ULIKUWA UMELALA KATIKATI YA DIMBWI LA DAMU. Mudy na Jenifer wakatizamana, hawakutegemea kukishuhudia kile walichokuwa wakikitazama mbele ya macho yao. Mwili wa Waziri Mkuu ulikuwa umejaa matundu Ya Risasi kuonyesha kuwa palikuwa na purukushani nzito. Mazingira ya kifo cha Waziri Mkuu yalikuwa yakifanana kabisa na Mazingira ya kifo cha Waziri wa mambo ya ndani. Tofauti ilikuwa ni wingi wa risasi zilizotumika kumuua Waziri mkuu na zile zilizotumika kumuua waziri wa Mambo Ya ndani. Waliangalia kwa muda mfupi kisha wakatizamana tena. Wote walikuwa wakiwaza kitu kimoja, kitu ambacho ndicho kilichoonekana kwenye mazingira Ya vifo hivi. Muuaji alikuwa mmoja katika vifo vyote. Kila mmoja akabaki akimtizama mwenzake.. Haukupita muda wakaungana na Revina kuondoka kati Jumba la Waziri wa katiba. Mohamed akapiga simu ikulu kueleza kile ambacho kimetokea. Baada ya simu hiyo wakaongoza Njia kuelekea Nyumbani Kwa Mkurugenzi Wa Idara Ya Usalama wa Taifa. Mr Adnan Kassim Kwangaya. Wote walikuwa wakienda kule wakiamini kuwa walikuwa wakienda kupambana na Jasusi. Jasusi kupindukia. Alimjua na kumtambua Adnan kiundani Zaidi. Alimtambua kwa mbinu na pia alimtambua kwa weledi uliotukuka katika kazi Zake. Mohamedi akatamani kwenda peke yake, alitamani kwenda kumkabiri akiwa peke Yake. Hakutaka kuwapoteza Jenifer na Revina. Lakini angewatoroka vipi ikiwa tayari wapo naye bega kwa bega. Wakatembea kwa kuachiana nafasi, kila mmoja alikuwa akimtizama mwenzake.. Ulikuwa mwendo wa kawaida, mwendo wawatu ambao wapo pamoja. Watu ambao hawakutiliwa mashaka wala kuonekana kuwa ni wa moja. Mohamedi akiwaacha umbali wa Hatua ishirini. Akiwa Nyuma wao wakiwa mbele.. Bastola zake mbili zilikuwa sehemu yake. Akairuhusu miguu yake kutembea na kuyaacha masikio yake kusikia kila kitakachotoa mlio. Aliupa mwili wake wepesi tayari kwa mapambano. Akaonyesha kutokujali Chochote.. Lakini Wakati akifanya hivyo ghafla katika masikio yake kukasikika mlio, mlio wa gari ambalo haukuwa mlio mgeni.. Mikono yake ikawahi sehemu, sehemu ambayo iliwahi kukamata kile ambacho alihitaji..

Mluzi uliopigwa ilikuwa ishara tosha, mbele ya macho yake na Mbele ya Revina na Jenifer akaona gari aina Ya benzi ikitembea taratibu. Ikitembea huku kukiwa hakuna ishara kuwa ilikuwa na Hatari.. Hisia za Mohamed Zikafanya kazi.. Kazi ambayo ilifanywa pia na wasichana wale, wote walikuwa hawapo barabarani, wote walikuwa wamechupa katika mtindo wa zigzag.. Mtindo wa kupishana hapa na pale. Punde mlango wa ile Benz ukafunguliwa. Mdomo wa Bunduki aina Ak 47 ukachungulia kwa kutokea kwenye Kioo.. Mudy alishaondoka pale Muda mrefu, risasi zilikuwa zikimfuata kule aendako.. Mohamedi alikuwa Akiruka Sarakasi kukwepa Risasi. Alikuwa akichupa na kujigeuza akiwa hewani. Ilivutia sana Machoni katika kutizama kile ambacho kilikuwa kikifanywa na Mohamedi.

Alipokuwa akitua Chini, akausikia mlipuko, mlipuko ambao ulimuonyesha kitu ambacho hakuwa amekitegemea. Benz ilikuwa juu ikiwaka moto. Hapo ndipo alipowaona watu wanne wakitoka katika benz wakiwa na Bunduki Nzito mikononi. Hawakuwa waafrika wala wachina. Hawa walikuwa wazungu, tena Wazungu kutoka Urusi. Hata Bunduki ambazo zilikuwa mikononi mwao zilikuwa ni bunduki za Kirusi.. Ushukaji wao ulikuwa ni Sawa na ule wa Makomandoo Wa Israel walivyoshuka pale Entebe Nchini Uganda Kuwaokoa Raia Wao Waliokuwa wakishikiliwa na Nduli Iddi Amini Dada. Yalikuwa mapambano Ya masaa Mawili tu ambayo Yalitosha kuwafanya wanajeshi wa Uganda Kusalimu Amri. Kitendo cha kuwaona Majasusi Wa KGB wakiwa katika mapambano kulimpa picha kuwa hili suala liliandaliwa kikamilifu. Hapo ndipo alipoamua kuwaonyesha kuwa hata yeye ni Zaidi Ya KGB na Hata CIA. akatambaa Chini kwa Chini katika vichochoro Vya Majumba yale.. Kila alipokuwa akitambaa bado alikuwa akisikia mapambano Ya kipambamoto. Akainua Uso kutizama mbele Yake. Akakiona kile ambacho hakuwahi kukiona kutoka kwa Jenifer Wala Kwa Revina. Watoto wakike walikuwa wakishambulia kwa mbinu ambazo zilimzuzua Mohamed.. Alikuwa akitabasamu kila pale Jenifer na Revina walipokuwa wakijipindua kwa ustadi Mkubwa. Walikuwa wakikwepa na Wakati Huo huo wakishambulia. Walikuwa ni Zaidi Ya wale Majasusi, Walikuwa ni Zaidi ya wajuzi wa Mapigano. Walikuwa wakiwaendesha kw mapigo.. Mapigo ambayo Yalimsisimua Mohamedi.. Akatamani Kujiunga nao.. Lakini alipokumbuka alitakiwa kwenda Kwa Mkurugenzi. Akaona ndio Muda Sahihi Wa kwenda kwa Mkurugenzi.

Akaondoka akiwaacha Revina na jenifer wakiikamilisha kazi. Yeye akachepuka kwa mwendo wa Haraka. Hakutaka kuonekana na jenife wala Revina. Alitaka kumjua nani alimuua mke wa Rais, alitaka kujua nani alimuua Waziri Mkuu na Nani aliwaua wale Mawaziri Wengine.

Alitaka kuyajua yote katika Siku hii.. Alitaka kukamilisha kila kila kitu.. Wakati akiwa UmbaLi mrefu kidogo kutoka alipowaacha Wakina Jenifer na Revina Wakipambana na Wale Wazungu, Akausikia Mlio Wa Bunduki, Mlio ambao Ulifuatiwa na Sauti ambayo aliitambua Masikioni Mwake..

JE NI NANI
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 60

AKAUSIKIA MLIPUKO WA BUNDUKI, KISHA AKAISIKIA SAUTI YA MTU ANAYEMFAHAMU AKILALAMA. Hakusubiri kuambiwa, hakuosubiri kitokee kingine. Alirudi katika muda ule ule.. Mkononi kwake akiwa amekamatia bastola mbili. Haikumchukua muda kufika sehemu ya tukio. Sehemu amboyo ilitapakaa Moshi na Harufu ya Damu. Maiti za Wazungu wanne zikiwa zimetambarajika chini katikati kwa madimbwi ya Damu. Macho ya Mohamedi hayakuhitaji kuwaona wale Wazungu. Macho ya Mohamed hayakuhitaji kushangaa hilo, bali macho yake yalihitaji kuwaona watu. Watu ambao aliwahitaji kuliko alivyoihitaji Roho Yake. Alikuwa akiwatafuta Jenifer na Revina. Hakuwa akiwaona katikati Ya Moshi, hakuwa akiwaona katikati ya mapambano. Hakuwaona wakionyesha ujuzi wao na wala hakuwaona wakiwa sehemu. Macho yake yakashangaa, kichwa chake kikaunda maswali kisha mdomo wake ukaropoka wako wapi hawa? Hakuwa na Majibu kwa kipindi kile. Punde akavisikia ving'ora vya polisi. Punde akawaona Makomandoo wakitokea katikati Ya Moshi, Makomandoo ambao hawakujulikana wapi walipotokea. Wote wakanyoosha Bunduki Zao kuelekezwa pale alipo Mohamedi. Mshangao na bumbuwazi vikatamalaki usoni kwa Mohamedo Hasira Zikaupanda moyo Wake, akatamani afanye kitu, akatamani awaanzishie kuwaonyesha kuwa ni zaidi Ya wao.

Lakini alipomuwaza Revina na Jenifer alikubali kuwa mpole. Upole ambao ulikuwa katikati Ya mshangao. Mbele ya Uso wake akatokea mkuu wa kitendo cha kijasusi ndani ya Idara ya Usalama Wa Taifa. Pembeni alikuwa na Watu wawili, watu ambao walifunikwa nyuso Zao kwa vitambaa. Mmoja alikuwa Wa kiume na Mwingine alikuwa wa kike. Kutokea kwa Mr Fraidy Wellah kukaibua maswali kwa Mohamedi.. Bado alitamani kitu kinachoendelea kiwe hadithi. Ni wakati huo akishangaa, Akahisi kitu kama Sindano kikitua katika Mwili wake, kitu ambacho alishakijua kuwa ni Dawa ya kusaidia kumlevya. Ni kweli alilewa. Muda Mfupi baadae Macho Yake yalikuwa yameingia Giza. Yalikuwa mazito Yasioweza kufunguka. Akakubali kwa Mara ya kwanza kumezwa na Hali ile. Akakubali kwa Mara Ya kwanza kufungwa na kubebwa kama maiti.

*****
pembeni ya jengo moja kubwa katikati ya jiji la Dar es salaam, Maeneo ya Posta. Watu wasiopungua kumi walikuwa wameizunguka meza kubwa huku kila mmoja akionekana kuwa busy na computer Yake mpakato. Walikuwa wanaume saba na wanawake watatu. Wote walionekana wakifuatilia kitu fulani. Kitu ambacho kilionekana ni Muhimu. Taarifa Zilikuwa zikitumwa huku na huko, maswali Yakiulizwa na Mengine kujibiwa. Kikao kilikuwa kizito, kikao kilikuwa kizito kupindukia. Tayari Rais wa Nchi alikuwa haonekani wapi alipo. Huku baadhi ya Walinzi wake wakiokotwa wakiwa maiti. Bado taarifa Zilikuwa ndani kwa ndani, bado taarifa hazikuweka bayana katika hilo. Lakini wakiwa katika Jengo lile wakijadili hicho kitu ilikuja taarifa kuwa kuna baadhi ya Makomandoo walikuwa Wameasi. Na Sio hao tu, bali Mkuu Wa Ujasusi na Mkurugenzi Wake walikuwa ni wamojaapo katika Suala hilo. Kila mmoja alikuwa akihaha kutaka kujua ni wapi Rais wa Nchi Amepelekwa. Ni wapi atakuwa amehifadhiwa Rais wa nchi? Yalikuwa maswali yaliyopita Vichwani mwa wajumbe wa kikao kile. Wakati suala la Mheshimiwa Rais kupotea likiwa halijapatiwa Ufumbuzi, Likaja Suala kuwa Mpelelezi Mashuhuri Nchini Mohamedi naye ametekwa na Hajulikani alipo. Hapo wajumbe wote wakapigwa na butwaa, wote walikuwa wakiitambua harakati inayofanywa na Mohamedi, na Wote walitambua kuwa Mohamedi alikuwa ndio mtu pekee wa kulitatua hili. Sasa hii Taarifa ikazima ndoto Zao za kuisaidia Serikali kubaki Madarakani. Na taarifa iliyoingia Punde iliwajulisha kuwa Raisi alikuwa amehifadhiwa sehemu akishurutisha alitangazie Taifa kuwa Anaachia Madaraka ya kuongoza Nchi. Kila Mmoja akapagawa na kikao hakikuendelea tena.

*****

alikuwa mwanamke pekee na mtu pekee aliyeshuhudia kutekwa kwa wasichana wawili waliokuwa wakisaidiana na Mudy na Pia ni Yeye pekee aliyeshudia Mudy akitekwa baada ya Kudungwa Sindano Ya madawa Yenye kutia Usingizi. Huyu hakuwa mwingine bali alikuwa Inspekta Ummu Sammy. Kila kilichokuwa kikitendeka alikuwa akikishuhudia kutoka umbali mdogo jirani na Sehemu ya Tukio. Alikuwa hapo kwa muda mrefu sehemu ile akiwafuatilia Nyuma Mohamed, Jenifer na Revina walipotoka nyumbani kwa Waziri Wa Katiba.

Baada ya Mohamed, Revina na Jenifer Kuondolewa pale. Ummu hakutaka kuchelewa kuondoka pale. Alichokifanya ni kuchukua sura yake ya Bandia na kuivaa. Muda Mfupi alikuwa akionekana kama Msichana wa kizungu akitembea eneo lile umbali ule ule bila kuonyesha kushangazwa na kitendo kinachotokea pale. Alikuwa akitembea huku kila hatua yake ikiwaza kitu, alikuwa akitembea huku akili yake ikahama pale. Bastola Mbili Zilikuwa kiunoni. Alikuwa akihesabu kila Hatua yake, alikuwa akiupangia mkono wake kipi cha kufanya. Akazishuhudia gari zilizowachukua Mudy, Revina na Jenifer Zikiondoka.. Naye akaunga Nyuma akiwa katika pikipiki.. Pikipiki aliyompora mtu aliyekuwa akiiendesha. Akaunga msafara katika Kuzifuatilia Gari Zile. ULIKUWA MCHEZO HATARI SANA KUUCHEZA.....
 
Back
Top Bottom