Riwaya: "Cabo-delgado"-part 01

Kitaingia Mtaani SOON hiyo RIWAYA ni matata sana usipime
MSAKO%20WA%20MWEHU%20BOOK%20MOCKUP.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
CABO DELGADO-31

Alivyokaa kama dakika 5 kitandani akapata mawazo mapya kuwa aanze kuchukua maelezo kwa Bwana Andenga Kazimoto ambaye ni mshirika mwenzao hawa mabaradhuli toka Tanzania. Akamsogelea Bwana Andenga akamkuta anaanza kusinzia, Kachero Manu akatabasamu akafikiria ule msemo kuwa usingizi ni mwanaume kweli, hamna kiumbe mgumu mbele ya usingizi katika mazingira yoyote lazima utalala tu hata ukalazwa sehemu mbaya kama chooni. Kama ulivyo mkate wa boflo kiboko yake chai ya rangi, unene wote wa mkate ukiingizwa kwenye chai unabwaka. Akakumbuka picha za Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe zilizokuwa zinasambaa mitandaoni zikimuonyesha anasinzia mkutanoni hali ya kuwa akiwa macho ni mkali kama mbogo, mpaka wazungu wenyewe wanaufyata mkia.
Akamshtua kwa kibao matata sana cha kwenye mafuta ya kitambi, sauti iliyotoka kwenye kitambi kilichochapwa kofi utasema "mpira wa baiskeli uliopata pancha, ilisikika paaaaah..!. "Amka haraka sana haupo Kempisiky Hotel hapa nyamafu wewe" alisema Kachero Manu kwa sauti ya ukali kumuambia Bwana Andenga, ambaye alikuwa hamuoni vizuri Kachero Manu kutokana na giza.
Muda wakati huo ulikuwa ni saa 12:30 magharibi ila kiza chake sasa, utasema kama saa 2 za usiku. "Umefikaje toka Tanzania mpaka humu selo?" aliulizwa Bwana Andenga na Kachero Manu wakati anafanyiwa usaili. Akajibu Bwana Andenga bila kufanya ajizi, "niliitwa kuhudhuria kikao cha leo usiku saa 4:00 usiku" alimalizia Bwana Andenga. "Unadhani kwanini msaliti umesalitiwa na wenzako?, ni kama umelipa pesa bandia kununua bidhaa feki!" alisema Kachero Manu kwa dhihaka.
"Wamenisaliti kwa sababu wamekipata walichokitaka, mikataba yote ya siri ya nchi yetu ambayo haitakiwi ijulikane na nchi zingine wameipata, hivyo hawana tena umuhimu na mimi, wamenifanyia ghiliba nami nikadanganyika. Malipo niliyopata ni matunda ya usaliti wangu, tamaa mbele mauti nyuma" aliongea Meneja Andenga kwa uchungu na masikitiko makubwa huku machozi yanamtiririka kama ngamia.
" Acha kulia kwa unafiki mtovu wa haya wewe, ulikamatajwe"? aliendeleza mahojiano yake Kachero Manu huku akiwa amekasirika kisawasawa. "Nilipotua uwanja wa ndege wa Pemba, nilipokewa vizuri tu sasa njiani wakati wananipeleka hoteli waliyoniandalia kufikia ndio wakanipokonya brifkesi langu la nyaraka zote. Kisha wakanipiga, nikafungwa kitambaa usoni na kupandishwa helikopta mpaka kuletwa huku" alijibu kwa umakini Bwana Andenga.
"Nani alikupa hii kazi ya kudukua na kuvuruga maslahi ya Tanzania kwenye sekta ya gesi na mafuta" aliuliza Kachero Manu huku akiyasimamisha dede masikio yake.
"Ni Bwana Alfredo mmiliki wa Monte Branco Ltd, tulijuana alipokuja Tanzania na msafara wa Wafanyabiashara wa Msumbiji katika kuangalia fursa za uwekezaji nchini Tanzania wakati wa sherehe za uzinduzi wa daraja la Umoja la Mtambaswala". Akapumzika kuongea ili ameze mate Bwana Andenga kisha akaendelea.
"Sasa yeye alijifanya anataka fursa za uwekezaji kwenye gesi na mafuta. Na akanitembelea ofisini kwangu mara kadhaa ndio maelewano yetu na urafiki wetu ukapelekea nijiingize kwenye haya majanga. Aliniahidi mengi sana ikiwemo kunipa ushirikiano wa kuja kuwa Rais wa Tanzania mwaka 2025, ndio maana ukaona kila tukio naonekana kwenye vyombo vya habari huku wahariri wakubwa wote wakiwa mfukoni mwangu kuhakikisha habari inayonihusu mimi lazima itafutiwe nafasi ukurasa wa mbele wa gazeti" aliongea Bwana Andenga kwa uchungu sana huku ameinika kichwa chake chini kama kobe anayetunga sheria.
"Haya wewe subiri hukumu yako, ukipona hapa utapelekwa Tanzania kwenye mikono ya sheria ukajibu tuhuma zako. Waswahili wanasema kiendacho mavani "makaburini" hakina marejeo, ulikuwa ni mtu mahashumu sana lakini heshima na hadhi yako Tanzania uliyoijenga kwa miaka mingi ya utumishi wako imekufa kabisa huwezi kuirudisha tena, kwa taarifa yako "TAKUKURU" na "Tume ya kudhibiti ufisadi Tanzania (TKUT) wamekamata mali zako zote na akaunti zako za benki za nje na za ndani zimegandishwa kwa maombi ya serikali ya Tanzania kwa nchi husika na wamekubali hivyo hapo ulivyo bila nguo ndio hata Tanzania upo hivyo hivyo huna chako. Umechezea kamari maisha yako, na kawaida ya kamari ina pande mbili, kuvuna au kuparia, sasa wewe wamekuparia. Tanzania mliigeuza shamba la bibi, mkageuza gesi na madini kuwa mali za mahonyo mnaiba mtakavyotaka, mlikuwa mnaishi maisha ya fawaishi mnaenda likizo Ulaya, watoto wenu mnawasomesha nje ya nchi, mnajenga makasri ya ajabu kwa jasho letu walalahoi, sasa chamoto utakiona, humu utaishi maisha ya paka na mbwa hamna tena utukufu humu, pole sana" aliongea Kachero Manu kwa nyodo bila kupindisha maneno wala kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa, akimchamba utasema Kachero ni Mzaramo kwa ufundi wa kuzodoa mtu kwa maneno.
Kauli hizo zilimshtua sana Bwana Andenga, ghafla akaanza kutokwa na mapovu puani na kinywani huku damu ikitiririka masikio, halafu akawa anaugulia maumivu, kisha akatulia kama mzoga. Kachero Manu akatambua, Bwana Andenga amepatwa na shambulio la ghafla la moyo na shinikizo la damu kutokana na kupata taarifa ya mali zake kuzuia kwa amri ya serikali.
Akaamua kumfanyia ubinaadamu wa kumfungua kutoka juu ya vyuma na kuilaza maiti ya Bwana Andenga juu ya kitanda, huku anaisimanga ile maiti na kuisoza kwa vidole utasema inasikia vile.
"Wewe utakuwa chakula kitamu kwa samaki wa mto Ruvuma hatutopoteza kodi za Watanzania kusafirisha maiti ya msaliti, umekufa polo huna hata senti moja uliyowaachia familia yako kwa tamaa zako. Umesomeshwa kwa kodi za Watanzania wa jembe la mkono wewe umeamua kuwasaliti, sasa mshahara wa dhambi ni mauti" aliongea Kachero Manu kwa sauti kubwa kama vile Bwana Andenga anamsikiliza kumbe anaongelesha mzoga wa jana.

Komandoo mstaafu "JS" majaribuni
Bob Chinanga na wenzake walipotoka pale "Montebello Pub" walikuwa wamepigiwa simu kuwa helikopta iliyokuja kumchukua Kachero Manu akahojiwe mbele ya Alfredo ilikuwa imeshawasili "Gorongosa Camp" hivyo waje kumpakiza adui yao haraka apelekwe wilaya ya Pemba, makao makuu ya Jimbo la Cabo-Delgado akahojiwe.
Hivyo mwendokasi aliotoka nao dereva mmoja wa wale wapambe ulikuwa ni wa kuwahi kambini hawakutegemea kama kuna mtu atakuwa anawafukuzia kwa nyuma. Bob Chinanga na wenzake walikuwa wanatumia gari aina ya "Subaru Forester" toleo jipya ambazo zina zinatimua kasi kama gari za mashindano.
Walipotembea kama umbali wa dakika dakika 45 tu mshale wa mafuta ya gari ukaonyesha mafuta yanakaribia kwisha, Bob Chinanga alivimba kwa hasira kama kichwa cha chura mpaka akawa anataka kupasuka kisha akampasha makavu dereva wake.
"Uzembe wa kijinga sana, huwezi kuniendesha mimi Bosi wa kambi halafu hujui kama gari inatakiwa ijae mafuta muda wote" kisha akamalizia hasira kwa kumtukana tusi kwa lugha ya kireno akamwambia "estúpido" akimaanisha mpumbavu au kwa lugha ya kimombo "stupid". ""Samahani Bosi tutawahi tu usiwe na hofu" alijibu dereva yule akijitetea huku akifahamu fika Bosi wake kashazidiwa na kileo ndio maana anatukana ovyo matusi ya nguoni.
Baada ya dakika chache dereva akaanza kupunguza mwendokasi wa gari akawasha indiketa ya kushoto kuonyesha anaingia kituo cha mafuta. Kilikuwa ni kituo kikubwa cha mafuta kimeandika maandishi ya kireno kwa rangi nyekundu "Unidade estação de petróleo" ikimaanisha " ni kituo cha mafuta jina lake ni "umoja".
Komandoo mstaafu hakutegemea upunguzaji ule wa mwendokasi alikuwa anakimbiza asije akaachwa maana hakujui hawa wanapokwenda hivyo kwa kupitia kioo cha pembeni Bob Chinanga akaliona gari "Range Rover" kwa nyuma yao, hakujali sana. Wao wakaingia kituo cha mafuta ile "Range Rover" ikapita kwa kasi ya mshale. Wakajaza mafuta yao wakaondoka kwa kasi dereva akili yake yote asije kumchelewesha Bob Chinanga kibarua chake kikaota nyasi bure.
Walipotembea kama umbali wa nusu saa tu hivi, Bob Chinanga alipoangalia kwenye kioo akaona kama kuna gari linafanana la lile aliloliona pale kituo cha mafuta, imeegesha porini kidogo na wameipita. Inabidi uwe mtaalamu sana kugundua maana iliegeshwa kuficha viakisi mwanga (reflector) na komandoo mstaafu, ni mzoefu wa shughuli sio mnemba kwenye fani.
Walipotembea kama dakika 20 tu, Bob Chinanga akamwambia dereva punguza mwendokasi wa gari nahisi kuna mjinga anatufuatilia Dereva kupitia vioo vyake vya pembeni akaanza kuliona gari la Komandoo mstaafu kwa mbali nalo likawa linapunguza mwendokasi. Bob Chinanga akamwambia dereva wake ongeza mwendokasi wa juu sana halafu tafuta kichochoro chochote uliingize gari kisha tumvizie.
Mbinu yao ilifanikiwa vizuri maana komandoo Jacob Steven (JS) hakutegemea kama atakimbiwa namna ile. Nae ilibidi aongeze kasi akawa haoni gari yoyote akaanza kupunguza kasi ya gari kuangalia labda kuna kuna njia ya mchepuko kuona kama labda gari ya Bob Chinanga imekata huko.
Ghafla akaona ile gari "Subaru Forester" imesimama kwa pembeni kabla hajamaliza taharuki yake akashtukia mvua ya zinarushwa usawa wa kioo chake cha dereva.
 
CABO-DELGADO-PART 32

Ghafla akaona ile gari "Subaru Forester" imesimama kwa pembeni kabla hajamaliza taharuki yake akashtukia mvua ya zinarushwa usawa wa kioo chake cha dereva. Zikapasua kioo cha mbele kwa bahati nzuri zote zilimkosa. Alichofanya ni kuinamia na kuishikilia steringi la gari yake ili lisiyumbe barabarani asingeweza kufunga breki ya ghafla lazima angekula dafrao mbaya.
Haraka haraka akachomoa bastola yake halafu akawashtukiza alivyofika usawa wa lile "Subaru Forester" kwa kupiga risasi tairi la kushoto la mbele. Akasogea kwa kulipita kidogo kisha akasimamisha gari na kushuka kwa kupitia mlango wa abiria wa mbele, kama alijua maana risasi zilirushwa bila mpangilio usawa mlango wa dereva.
Alichofanya ni kutambaa chini kwa chini mpaka nyuma ya gari lake kisha akamlenga mmoja wao risasi usawa wa kifua na ilimpata kisawa sawa akafa pale pale. Ghafla likawa linakuja lori wangu wangu nyuma yake kwa hiyo akaogopa kumulikwa na mwanga aonekane kirahisi hivyo akaamua aingine chini ya gari atambae kwa chini kisha Lori likipita awashambulie kwa kushtukiza tena.
Alichokiona hakuamini macho yake. Lile Lori lilipofika usawa wa gari la Bob Chinanga alimuona Bob Chinanga anatoka mbio za ajabu na anadandia Lori kwa nyuma, huku nae mpambe wake anamfuata kwa nyuma haraka haraka.
Kachero Manu akafanikiwa kumpiga risasi ya mguu yule mpambe wake. Lakini Bob Chinanga akawa amesalimika ila yule mpambe alianguka chini anagaa gaa chini kwa maumivu. Kilichomchekesha Komandoo JS ni zile mbio za Bob Chinanga mithili ya bingwa wa nchi wa mbio za meta 100 na ule mguu mmoja mrefu na mwingine mfupi basi ilikuwa burudani sana kumuangalia anavyokimbia.
Inaonyesha akina Bob Chinanga waliishiwa na risasi maana walikuwa wanarusha bila mahesabu yoyote. Akatulia kidogo kabla hajamfuata akiogopa huenda ukawa ni mtego anategwa ili wamkamate kirahisi alivyoona kimya kama dakika 5 akachomoka chini ya gari akawa anamfuata yule mpambe alipomfikia akamkwida shati lake na kumnyanyua juu huku amekandamizia mguu wake kwenye jeraha la risasi la mguuni. Yule mpambe wa Bob Chinanga alikuwa anapiga yowe la maumivu makali.
"Kwanini mmemuua yule mhudumu wa Pub" aliuliza Kachero mstaafu kwa hasira. Kwa jeuri yule mpambe akakusanya makohozi kinywani kisha akamtemea usoni komandoo mstaafu.
Akajibu mapigo kwa kumpiga yule mpambe kichwa cha kwenye mwamba wa pua. Tahamaki damu zikawa zinamchuruzika usoni yule adui. Kisha akampiga makofi ya kubambanya sikio la kushoto na kulia. Yule mpambe alipiga kelele kama mtoto mdogo anayetahiriwa jandoni na ngariba mwenye kisu butu.
Kisha ghafla yule mpambe akawa anamung'unya kitu kama pipi. Komandoo akawahi kumkaba shingoni kumzuia asimeze ila alikuwa ameshachelewa kwani kilishapita ilikuwa ni sumu inayotumiwa na majasusi kujipoteza uhai ili wasitoe siri. Ni vidonge vidogo vinazungushiwa glasi nyembamba kisha vinazungushiwa juu yake raba ya rangi ya udongo, halafu zinatengenezwa kama umbile la jino bandia. Kwa hiyo ile raba inamlinda kama amemeza kwa bahati mbaya haimdhuru inapita tumboni bila madhara. Ila anapokusudia kujiua inabidi aitafune tafune kuivunja ile glasi ili sumu iliyowekwa ndani aina ya "Potasium Cyaninde" ifanye kazi.
Hii sumu inaua ubongo ndani ya dakika moja tu na inasababisha moyo wa mwanadamu usimamishe mapigo yake kwa muda mfupi sana.
Haraka haraka akaingia kwenye gari lao lile akaanza kupekua kupekua huenda atapata kitu cha kumsaidia akakuta bastola tupu zisizo na risasi. Wakati anataka ashuke aondoke akakumbuka kitu akapanda tena akatafuta "Log book" inayotumiwa na dereva. Akaifungua akapitia pitia akapata anachokitaka. Alikuwa anaangalia umbali wa kutoka pale "Pub" mpaka "Gorongosa Camp". Akawasha gari na kuongeza mwendokasi kuwahi kambini kabla Kachero Manu hajachukuliwa.

SURA YA KUMI NA SABA
Mlima Gorongosa, kichaka cha waovu tokea asili na jadi.
Wilaya ya Gorongosa katika Jimbo la Sofala, Kaskazini mwa Wilaya hii kuna Mlima Gorongosa ambapo kilele chake cha Mlima kinaitwa Gogogo. Mashariki yake ndio kuna mbuga ya wanyama ya Gorongosa (Gorongosa National Park). Hiyo ni moja ya mbuga iliyobarikiwa sana kwa urithi wa asili wa Afrika.
Mbuga hiyo ina zaidi ya aina za wanyama elfu sabini na mbili (72,000). Na imezungukwa na zaidi ya mito minne kama mto Vunduzi, Chitunga, Muera na Nhandare. Mito hiyo ndio chanzo cha maji ya kunywa katika Wilaya nzima ya Gorongosa na inamwaga maji yake Bahari ya Hindi.
Licha ya utajiri huu wa asili, bahati mbaya sana hili ni eneo ambalo lina mikosi ya kutokupata amani ya kudumu. Kipindi cha vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya FRELIMO na RENAMO, Mlima Gorongosa na mbuga yake ndio ilikuwa uwanja wa vita. Kwa muda wa miaka 16 mtawalia kuanzia 1976-1992, eneo hili lilikuwa linashuhudia ulipuaji wa mabomu, uwindaji haramu wa wanyama kwa ajili ya kutorosha maliasili kama pembe za ndovu, ngozi za simba na nyara zinginezo. Hali ilikuwa mbaya zaidi mwaka 1983 mpaka serikali ya FRELIMO ikaamua kufunga shughuli za kitalii eneo la Gorongosa hasa baada ya tukio la kutekwa kwa watafiti wa maliasili wazawa na wanasayansi wawili wa kigeni.
Baada ya mkataba wa amani wa mwaka 1992 hali ya usalama ilirejea na Benki Maendeleo ya Afrika (ADB) pamoja na Umoja wa Ulaya (EU) pamoja na Shirika ya Kimataifa Ulinzi wa Mazingira (IUCN) wakaaanda mpango mkakati na utekelezaji wake wa kurudisha hali ya kawaida katika mbuga ya Gorongosa.
Mwaka 2014 eneo hili tena likakosa amani baada ya aliyekuwa kiongozi wa RENAMO Bwana "Afonso Dhlakama" kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu baada ya kushindwa uchaguzi na chama cha FRELIMO, hivyo kuamua yeye na jeshi lake kuhamia mlima Gorongosa hivyo kuzua tena hali ya taharuki.
Hali hiyo tete ya eneo la Gorongosa kwa Tanzania unaweza kufananiza na hali tete na taharuki ya eneo la Kibiti na Ikwiriri namna magaidi walivyotawala eneo hilo kipindi cha nyuma na kuendesha mauaji ya kutisha kwa viongozi wa vijiji na polisi, kabla hawajadhibitiwa na jeshi la wananchi. Ni eneo ambalo ukiamua kufanya makazi basi roho yako umeiweka rehani inatakiwa uwe na tahadhari ya hali ya juu.
Kibaraka wa wazungu katika kuchota utajiri wa Msumbiji na Afrika kwa ujumla Chotara Alfredo alikuwa ni mtu wa maneno machache sana lakini mipango mingi sana. Kila kitu kinachopita mbele yake yeye alikuwa anaangalia atapata fursa gani hapo aitumie kujinufaisha. Inasemekana alikuwa hata akiliona gari la kubeba vinyesi vya binadamu linapita barabarani alikuwa anasikitikia sana kinyesi hicho kumwaga bure. Mawazo yake ni kutaka kuzalisha mbogamboga na matunda ya kulisha Afrika nzima kwa kutumia mbolea ya kinyesi cha binadamu.
Hivyo alivyorudi masomoni na kukabidhiwa umiliki wa kampuni ya Monte Branco Ltd, machafuko ya Gorongosa ikawa fursa kwake ya kufanya uwindaji haramu hivyo akajenga ndani ya milima, kambi ya kuhifadhia nyara haramu kama meno ya tembo na nyinginezo. Kisha nyara hizo zilikuwa zinasafirishwa kupitia bandari ya Beira iliyopo hapo hapo jimbo la Sofala, moja ya bandari tegemezi kwa nchi za Zimbambwe, Zambia na Malawi.
Baada ya amani kurudi Msumbiji akawa anawazuga watu ni ghala la kutunzia mazao kama korosho na mihogo mikavu kumbe ikawa ni kambi ya mateso kwa wabaya wake. Akaajiri vijana ambao zamani kazi yao ilikuwa ni wapiga mapanga watu mitaani na machimboni maarufu "NACATANAS" ambao kwa Tanzania ni mfano wa "KOMANDO YOSSO" walivyosumbua miaka ya 90's na kiongozi wao akijiita "Jenerali Nyau". Hawa KOMANDO YOSSO walisumbua sana kuanzia Manzese, Tandika mpaka bonde la Mwananyamala. Ndio kama hawa NACATANAS huko Msumbiji na kiongozi wao Bob-Chinanga chini ya uratibu wa Inspekta Jenerali Mark Noble.
Bob Chinanga yeye matumizi ya akili kwake ni madogo sana kwake kila kitu anatumia nguvu, hivyo Inspekta Jenerali Mark Noble askari polisi mwenye cheo cha juu kabisa akawa ni kibaraka wa Alfredo (under cover) katika kuijenga NACATANAS kisasa.
Mark akawa anaunganisha ujuzi wake kwa hawa NACATANAS, akawapika wakaiva mafunzo. Kuingia kambini kwao hawa NACATANAS kama walivyomuingiza Kachero Manu kisha ukatoka salama inabidi uwe na roho saba kama za paka. Maana ukikosea njia ya kuingia milimani unatokeza kwenye msitu wa wanyama wakali kama simba na chui au kwenye majoka yenye sumu kali. Huo ulikuwa ni ulinzi wa asili wa kambi hiyo.
Iwapo ukifanikiwa kuvuka vikwazo hivyo unakutana na fensi ya waya za senyenge za umeme uliozunguka kambi yote ambao usipovaa nguo zao maalumu kwa kupita eneo lisiloruhusiwa unakauka kama mkaa ukiwa umbali wa meta 5 kutoka kwenye fensi. Ulinzi mkubwa ulikuwa ni wa teknolojia za kisasa.
Pia kulikuwa na ulinzi wa kutumia mbwa maarufu kama mbwa wa polisi wanaitwa K-9 aina ya "German sherphed", mbwa ambao walikuwa wanaelewa alama za ishara na maneno. Walipitia mafunzo maalumu na walikuwa wanatibiwa vizuri na wanalishwa vyakula vya kwenye Masupamaketi sio makombo ya kwenye migahawa kama hawa mbwa koko wetu wanaotusumbua majumbani kuiba kuku wetu.
Kisha ndani kulikuwa na wafanyakazi maalumu kwa mateso ya watu wanaokamatwa. Watesaji hao wanaishi kwenye nyumba zao za kota ndogo za kisasa, wakiwa na viwanja vya mazoezi, mabwawa ya kuogelea na vikorombwezo kibao vya kunakshi nakshi mazingira yao. Kutwa nzima walikuwa wanashindana wenyewe kwa wenyewe kufanya mazoezi kama kunyanyua vyuma, kucheza karate, mieleka, judo, kukimbia na mazoezi mengineyo na huku wanashindana kula vyakula mbalimbali. Vifua vyao vilikuwa vimejaa kama mataruma ya reli kwa wingi wa nguvu walizonazo.
Mfano Bob Chinanga alikuwa akimaliza mazoezi ya asubuhi ana uwezo wa kunywa supu ya kuku mzima lile jogoo la kienyeji linalowika kuanzia saa 9 usiku kwa chupa nzima ya chai kwa mikate ya Boflo mitano, kama marehemu Pepe Kalle mwanamuziki wa Congo alivyokuwa na mshipa wa kula.
Selo zao zilikuwa za aina tatu tu, Kulikuwa na selo ya mateso ya kuanzia watu watano afu kulikuwa na selo kubwa inayoweka zaidi ya watu kumi na selo ya mtu mmoja mmoja, kutegemeana na makosa ya mkosaji. Hizi selo zote zilikuwa na kuta ngumu za plastiki kuzuia mateka kujiua wenyewe kama ataamua ajigongeshe kichwa ukutani na zilikuwa na vifaa vya mateso ikiwemo viti vya umeme kwa ajili kupiga shoti ya umeme.
Gharama ya siku moja tu kwa ajili ya kuendesha shughuli zote za usalama, umeme, maji, mawasiliano na vyakula ilikuwa si chini ya milioni tano za Kitanzania kwa siku. Hapo ndio utaona kwa namna gani Bwana Alfredo alijipanga haswa kutikisa uchumi wa Msumbiji na nchi za kusini mwa jangwa la Afrika kwa ujumla.
 
CABO-DELGADO-PART 33


Bob-Chinanga katimba kambini tayari kumnyakua Kachero Manu
Bob Chinanga alifanikiwa kumtoroka Komandoo mstaafu Jacob Steven (JS) katika sekeseke la kurushia risasi, kwa kurukia lori la mizigo.
Lori hilo la mizigo kwa bahati nzuri lilikuwa linaelekea karibu kabisa na kambi ya "Gorongosa Camp" kwa karibia kilomita 7 Lilikuwa ni Lori la "Gorongosa National Park" likiwa linatoka bandari ya Beira kubeba mizigo ya vifaa mbalimbali vya kutumiwa mbugani kwa ajili ya ofisi na wataliii.
Dereva wa Lori aliziona zile gari mbili akawa yupo makini katika kuongeza mwendokasi wa gari lake hakutaka kusimama maana anafahamu njia ya kuelekea mbuga ya Gorongosa haikuwa nzuri sana kiusalama. Hivyo Bob-Chinanga alipodandia lori alifanikiwa kupasua turubai lililoziba mizigo kwa kisu chake cha kukunja ambacho ni moja ya silaha zake anazolala na kuamka nazo.
Akafanikiwa kujisweka katikati ya lundo la mizigo kukwepa baridi kali ya milimani. Wakati wote alikuwa anaangalia saa yake maana alijua uzembe wowote wa kumchelewesha kachero Manu kufikishwa mbele ya Bwana mkubwa Alfredo ungepelekea kupoteza kazi na hata kupoteza uhai wake.
Kama kuna mtu NACATANAS wote mpaka Inspekta Mark mwenyewe walikuwa wanamuogopa basi ni Alfredo. Inasemekana Alfredo alipoenda kusoma Chicago, Marekani alipitia pia mafunzo ya kijasusi ila wengi walikuwa hawajui na alikuwa hapendi ajulikane kama ni bobezi kwenye fani. Inasemekana siri hii ilitolewa na majambazi wa Cabo-Delgado waliwahi majambazi kama 6 waliwahi kuvamia nyumbani kwake usiku wa manane alichowafanyia ni gumzo mpaka leo.
Wenyewe walijua ni tajiri kibonde kibonde nyama uzembe, mwili yai kama hawa matajiri wetu wanavyojiweka. Inasemekana aliwaona kwenye mifumo yake ya ulinzi wakati wanaingia ndani ya nyumba akawaagiza walinzi wake wakiwakamata wawany'ang'anye silaha kisha wawaache waje ndani, alipokutana nao alipigana nao wote majambazi 6 kwa pamoja, akawafirigisa sawia. Ambapo 3 kati yao walivunjwa viuno vyao na mmoja alikufa palepale hawa 2 waliponea tundu la sindano lakini wakiwa wamevunjwa mikono. Hao ndio walioenda kuvujisha siri kwenye vijiwe kuwa hawajawahi kuona mtu mtaaalamu wa sanaa za mapigano kama Bwana Alfredo.
Hivyo Bob Chinanga alifahamu hana uwezo wa kumuepuka Alfredo bali ni kutekeleza maagizo yake kama anavyotaka. Alipokaribia karibia na mbuga, Bob Chinanga aliteremka bila kuonekana na dereva wa lori.
Kwa mtu kama Bob Chinanga ilimchukua nusu saa tu kupata usafiri wa kufika kambini, ni hivi alienda kwenye vichochoro vinavyotumiwa na wawindaji haramu wanaotumia bodaboda kusafiri mizigo usiku usiku kuipeleka Gorongosa mjini. Huko akafanikiwa kupora bodaboda moja bila hata kuua inzi maana dereva bodaboda alivyomuona tu aliachia mwenyewe funguo maana alijua kubishana na Bob Chinanga ni sawa na kujitafutia kifo cha makusudi.
Mpaka kufika muda saa tatu kasoro usiku Bob Chinanga alikuwa anaingia kambini, huku akiacha maagizo makali ya ulinzi wa kambi kuimarishwa maradufu na kutoa onyo kuwa uzembe wowote utakaoruhusu kambi kuvamiwa haotuvumilika kwa mhusika yoyote kwenye idara yake.
Baada ya kutolewa amri hiyo mkuu wa kikosi cha mbwa alikuwa yupo nje na wasaidizi wake kuimarisha ulinzi, wale wanaozunguka ukuta wa kambi kila mmoja akiwa na silaha yake iliyojazwa risasi alikuwa kwenye eneo lake ili mradi ulikuwa ni usiku wa hekaheka mtindo mmoja. Na kila mmoja alikuwa kwenye sare zao za rangi ya kaki, kofia na buti nyeusi ili iwe rahisi kutambuana inapotokea tatizo.
"Showdown" ya kibabe "Mwiba wa Tasi" vs "Bob-Chinanga"
Kachero Manu aliona giza linazidi kuwa totoro mule selo kuu huku hamna dalili yoyote ya kuja kwa mabaradhuli wale. Alipoisogelea maiti ya msaliti Bwana Andenga Kazimoto alikuta imeanza kufutuka. Akajisema ndio kawaida ya maiti za watu wenye vitambi huwa zinavimba sana. Akapatwa na huruma ya mzazi kwa mtoto akawa anawafikiria watoto wa Mzee Andenga watakuwa wanamsubiria baba yao arudi safari toka Msumbiji na zawadi za kutambishia watoto wenzao shuleni. Lakini ndio basi tena hawatamuona baba yao ataishia kuwa chakula cha ndege na fisi porini, au chakula ya samaki mtoni.
Akiwa amezama katika dimbwi lenye kina kirefu la fikra, akapata wazo la kukitega kile kitanda cha chuma mlango na kwa kuwa wakiona giza wataingia kwa pupa watakapojikwaa watapoteza umakini hapo hapo itakuwa rahisi kuwavamia na kuwamaliza. Akakisogeza kitanda kwa kutumia nguvu zote huku juu yake kuna maiti ya Bwana Andenga mpaka akafanikiwa kukitega kitanda meta chache kutoka kwenye geti la kuingia kwenye selo kuu, kisha yeye akajibanza pembeni. Akasikia kama mlango unagongwa akajiweka tayari kwa lolote. Lakini kumbe walikuwa ni popo wa ndani ya selo wanajigonga kwenye kwenye mlango.
Kumbe popo walikuwa wanamletea habari njema haikuzidi hata dakika 5 akawa anaskia nyayo za vishindo vya viatu vinatembea akajisemea kazo iliyonileta Cabo-Delgado ndio inaanza. Akajibana vizuri pembeni mwa kitanda, na kwa haraka alivyopima mlio wa zile nyayo za viatu akaamini hawazidi zaidi ya kati ya watu wawili au watatu. Mlango ukawa unafunguliwa kwa vishindo vyote huku wanajiamini adui yetu Kachero Manu yupo mahututi kwenye kamba alizofungwa hajiwezi kumbe "Mwiba wa Tasi" alikuwa anawasubiri tu waingine kichwa kichwa awafunze adabu. Awaonyeshe cha mtema kuni kilichomnyoa kanga manyoya.
Wa kwanza kuingia alikuwa ni Bob Chinanga na bangi yake mkononi analipuliza ili kujipa stimu za kuwajibika. Alipagawa baada ya kuona giza nene akaingia ndani kichwa kichwa akajikuta anaparamia kitanda mpaka kaparamia maiti ya Bwana Andenga Kazimoto. "Fyatua risasi" alipiga kelele Bob Chinanga kwa hamaki kama mwehu, alishajua maji yamezidi unga tayari.
Alikuwa ameshachelewa, kwani Kachero Manu alishamrushia teke la mkononi yule mwenye bunduki mkononi ikamponyoka lakini akawahi yule msaidizi wa Bob-Chinanga kuchomoa tochi kiunoni na kuwasha, ilikuwa ni zile tochi kubwa sana chumba kikaenea mwangaza.
Ule mwangaza ukawa kosa kwao sasa Kachero Manu akawa anawaona wote vizuri. Haraka haraka Kachero Manu akaruka kurukia tumbo la maiti ya Bwana Andenga kisha akajibinua hewani na kumchapa teke moja matata sana la kifuani Bob Chinanga ambaye alikuwa ametoka kujizoazoa chini. Lakini licha ya ukali wa lile teke la Kachero Manu lilipofika kifuani kwa Bob Chinanga hakutikisika hata kidogo.
Isipokuwa alichezesha matiti yake kifuani huku anacheka mithili ya wale wacheza mieleka wa miaka ile ya 90's walivyokuwa wanachezesha matiti yao akina "Power Bernado", "Power Marungusi", "Power Bukuku" au "Power TX-Chaka".
Yule msaidizi wa Bob Chinanga akawa anatambaa kiujanja kwenda kuiwahi bunduki iliyodondoka. Kachero Manu hakumchelewesha alimuwahi akamrukia mgongoni kisha akakamata shingo yake na kuinyonga mara moja, akafa pale pale bila kuomba maji.
Kitendo cha kupoteza uhai wa msaidizi wake, Bob Chinanga kilimkasirisha vibaya sana, alipandisha morali na kumfuata Kachero Manu pale alipo kama mbogo huku anapiga ukelele wa hasira mithili ya Morani wa Kimasai. Wakawa sasa wamekaribiana wanaviziana, Bob Chinanga akawa anaruka ruka kama nyani, mara amerukia zile bomba zinazoning'inia za kutesea mateka mara ameshuka anavizia ashambulie kwa kushtukiza.
Hapo Kachero Manu akajua huyu anatumia staili ya kizamani kabisa za akina "Koo Ting Sang" alizokuwa anazitumia katika filamu ya "Snake in the monkey's shadow". Kachero Manu akaamua kutumia staili ya "Chang Quan" ambayo ni mpya kabisa haujazoeleka na wengi. Mtindo ambao unapoanza unasimamisha mguu wa kulia na unaukunja mguu wa kushoto mpaka maeneo ya goti la mguu wa kulia huku mkono wa kulia unanyooka huku wa kushoto unakuja chini, ni staili ambayo ilikuwa ni ngeni kabisa machoni kwa "Bob Chinanga".
Alivyokunja ule mguu Kachero Manu, Bob Chinanga akaona kapata nafasi ya kushambulia akaruka kumrukia Kachero mzima mzima, lilikuwa ni kosa baya sana kwake. Alipokuja Kachero aliukunja mguu wa kulia kisha ule mguu wa kushoto ambao ulikuwa upo juu ukapita kwenye shingo la Bob Chinanga, ikawa sinema ya mbwa aliyeingiza kichwa kwenye ndoo yenye mdomo mdogo anashindwa kutoa kichwa chake. Ikawa kila anapojichomoa ndio kabali ya mguu inazidi kujikaza mpaka Bob Chinanga aanza kuhisi anataka kuishiwa pumzi, huku anatoa mishuzi ovyo.
Alichofanya Bob Chinanga ni kujisukuma kichwa kwa nguvu zote kikachomoka na kupiga sehemu za siri za Kachero Manu. Jaribio lake lilifanikiwa kwani Kachero Manu aliachia mguu na kupiga kelele utasema amekanyagwa na tairi la trekta. Bob Chinanga bila kuchelewa akampiga Kachero Manu farasi teke la nguvu eneo la tumboni ambalo lilimfanya kachero Manu apepesuke kama mlevi wa gongo. Bob Chinanga akajua ameshamaliza kazi akawa anamfuata Kachero Manu kizembe bila kuchukua tahadhari.
Kachero Manu akazuga kama amezidiwa na kipigo cha Bob Chinanga kumbe anamvizia asogee karibu amalize kazi. Alipomsogelea karibu zaidi akawa anajiandaa kumsukumizia makonde ya usoni Kachero Manu, aliporusha konde la mkono wa kushoto, Kachero Manu akaliona akakwepesha kichwa chake kuelekea kushoto kidogo tu, konde likapita patupu hewani. Bob Chinanga akapoteza uelekeo kutokana na kuyumba.
Hapo ndipo Kachero Manu akatupa konde la nguvu la mkono wa kulia, konde ambalo lilimuangusha chini Bob Chinanga kwa kishindo. Haraka haraka akajinyanyua chini akajifuta kwenye pembe ya ncha ya mdomo wake akaona damu zinachuruzika. Akaanza kurusha ngumi mtawalia bila umakini, ambazo ngumi zote Kachero Manu alikuwa anazikwepa huku anarudi nyuma nyuma. Kitendo cha kuona damu yake inamwagika kilichochea hasira za Bob Chinanga na kupunguza uwezo wake finyu wa kufikiri akawa anakuja kumvamia Kachero Manu kama anakuja kubeba gunia la viazi lumbesa.
Kachero Manu hakumkawiza, akajipindua sarakasi kurudi nyuma kisha akaruka na teke moja kali sana la mguu wa kushoto lililotua kwenye usawa wa koo la Bob Chinanga ambalo lilimtupa chini kwa mara ya pili akafikia chali upande wa kisogoni akawa anajaribu kunyanyuka anashindwa.
Hapo hapo Kachero Manu akamrukia na kumkaba kabali ya mbao huku magoti ya Kachero Manu yamekanyaga tumbo la Bob Chinanga, akawa kila Bob Chinanga akijaribu kujitoa hawezi kujitoa, mpaka akaanza kukoroma kwa kukosa hewa, akanyonga kwa nguvu shingo ya Bob Chinanga mpaka akapoteza uhai. Kachero Manu akawa anahema kwa nguvu huku jasho linamtiririka haamini kama amemuangamiza Bob Chinanga.
IMG-20200527-WA0017.jpg
 
CABO-DELGADO-PART 33


Bob-Chinanga katimba kambini tayari kumnyakua Kachero Manu
Bob Chinanga alifanikiwa kumtoroka Komandoo mstaafu Jacob Steven (JS) katika sekeseke la kurushia risasi, kwa kurukia lori la mizigo.
Lori hilo la mizigo kwa bahati nzuri lilikuwa linaelekea karibu kabisa na kambi ya "Gorongosa Camp" kwa karibia kilomita 7 Lilikuwa ni Lori la "Gorongosa National Park" likiwa linatoka bandari ya Beira kubeba mizigo ya vifaa mbalimbali vya kutumiwa mbugani kwa ajili ya ofisi na wataliii.
Dereva wa Lori aliziona zile gari mbili akawa yupo makini katika kuongeza mwendokasi wa gari lake hakutaka kusimama maana anafahamu njia ya kuelekea mbuga ya Gorongosa haikuwa nzuri sana kiusalama. Hivyo Bob-Chinanga alipodandia lori alifanikiwa kupasua turubai lililoziba mizigo kwa kisu chake cha kukunja ambacho ni moja ya silaha zake anazolala na kuamka nazo.
Akafanikiwa kujisweka katikati ya lundo la mizigo kukwepa baridi kali ya milimani. Wakati wote alikuwa anaangalia saa yake maana alijua uzembe wowote wa kumchelewesha kachero Manu kufikishwa mbele ya Bwana mkubwa Alfredo ungepelekea kupoteza kazi na hata kupoteza uhai wake.
Kama kuna mtu NACATANAS wote mpaka Inspekta Mark mwenyewe walikuwa wanamuogopa basi ni Alfredo. Inasemekana Alfredo alipoenda kusoma Chicago, Marekani alipitia pia mafunzo ya kijasusi ila wengi walikuwa hawajui na alikuwa hapendi ajulikane kama ni bobezi kwenye fani. Inasemekana siri hii ilitolewa na majambazi wa Cabo-Delgado waliwahi majambazi kama 6 waliwahi kuvamia nyumbani kwake usiku wa manane alichowafanyia ni gumzo mpaka leo.
Wenyewe walijua ni tajiri kibonde kibonde nyama uzembe, mwili yai kama hawa matajiri wetu wanavyojiweka. Inasemekana aliwaona kwenye mifumo yake ya ulinzi wakati wanaingia ndani ya nyumba akawaagiza walinzi wake wakiwakamata wawany'ang'anye silaha kisha wawaache waje ndani, alipokutana nao alipigana nao wote majambazi 6 kwa pamoja, akawafirigisa sawia. Ambapo 3 kati yao walivunjwa viuno vyao na mmoja alikufa palepale hawa 2 waliponea tundu la sindano lakini wakiwa wamevunjwa mikono. Hao ndio walioenda kuvujisha siri kwenye vijiwe kuwa hawajawahi kuona mtu mtaaalamu wa sanaa za mapigano kama Bwana Alfredo.
Hivyo Bob Chinanga alifahamu hana uwezo wa kumuepuka Alfredo bali ni kutekeleza maagizo yake kama anavyotaka. Alipokaribia karibia na mbuga, Bob Chinanga aliteremka bila kuonekana na dereva wa lori.
Kwa mtu kama Bob Chinanga ilimchukua nusu saa tu kupata usafiri wa kufika kambini, ni hivi alienda kwenye vichochoro vinavyotumiwa na wawindaji haramu wanaotumia bodaboda kusafiri mizigo usiku usiku kuipeleka Gorongosa mjini. Huko akafanikiwa kupora bodaboda moja bila hata kuua inzi maana dereva bodaboda alivyomuona tu aliachia mwenyewe funguo maana alijua kubishana na Bob Chinanga ni sawa na kujitafutia kifo cha makusudi.
Mpaka kufika muda saa tatu kasoro usiku Bob Chinanga alikuwa anaingia kambini, huku akiacha maagizo makali ya ulinzi wa kambi kuimarishwa maradufu na kutoa onyo kuwa uzembe wowote utakaoruhusu kambi kuvamiwa haotuvumilika kwa mhusika yoyote kwenye idara yake.
Baada ya kutolewa amri hiyo mkuu wa kikosi cha mbwa alikuwa yupo nje na wasaidizi wake kuimarisha ulinzi, wale wanaozunguka ukuta wa kambi kila mmoja akiwa na silaha yake iliyojazwa risasi alikuwa kwenye eneo lake ili mradi ulikuwa ni usiku wa hekaheka mtindo mmoja. Na kila mmoja alikuwa kwenye sare zao za rangi ya kaki, kofia na buti nyeusi ili iwe rahisi kutambuana inapotokea tatizo.
"Showdown" ya kibabe "Mwiba wa Tasi" vs "Bob-Chinanga"
Kachero Manu aliona giza linazidi kuwa totoro mule selo kuu huku hamna dalili yoyote ya kuja kwa mabaradhuli wale. Alipoisogelea maiti ya msaliti Bwana Andenga Kazimoto alikuta imeanza kufutuka. Akajisema ndio kawaida ya maiti za watu wenye vitambi huwa zinavimba sana. Akapatwa na huruma ya mzazi kwa mtoto akawa anawafikiria watoto wa Mzee Andenga watakuwa wanamsubiria baba yao arudi safari toka Msumbiji na zawadi za kutambishia watoto wenzao shuleni. Lakini ndio basi tena hawatamuona baba yao ataishia kuwa chakula cha ndege na fisi porini, au chakula ya samaki mtoni.
Akiwa amezama katika dimbwi lenye kina kirefu la fikra, akapata wazo la kukitega kile kitanda cha chuma mlango na kwa kuwa wakiona giza wataingia kwa pupa watakapojikwaa watapoteza umakini hapo hapo itakuwa rahisi kuwavamia na kuwamaliza. Akakisogeza kitanda kwa kutumia nguvu zote huku juu yake kuna maiti ya Bwana Andenga mpaka akafanikiwa kukitega kitanda meta chache kutoka kwenye geti la kuingia kwenye selo kuu, kisha yeye akajibanza pembeni. Akasikia kama mlango unagongwa akajiweka tayari kwa lolote. Lakini kumbe walikuwa ni popo wa ndani ya selo wanajigonga kwenye kwenye mlango.
Kumbe popo walikuwa wanamletea habari njema haikuzidi hata dakika 5 akawa anaskia nyayo za vishindo vya viatu vinatembea akajisemea kazo iliyonileta Cabo-Delgado ndio inaanza. Akajibana vizuri pembeni mwa kitanda, na kwa haraka alivyopima mlio wa zile nyayo za viatu akaamini hawazidi zaidi ya kati ya watu wawili au watatu. Mlango ukawa unafunguliwa kwa vishindo vyote huku wanajiamini adui yetu Kachero Manu yupo mahututi kwenye kamba alizofungwa hajiwezi kumbe "Mwiba wa Tasi" alikuwa anawasubiri tu waingine kichwa kichwa awafunze adabu. Awaonyeshe cha mtema kuni kilichomnyoa kanga manyoya.
Wa kwanza kuingia alikuwa ni Bob Chinanga na bangi yake mkononi analipuliza ili kujipa stimu za kuwajibika. Alipagawa baada ya kuona giza nene akaingia ndani kichwa kichwa akajikuta anaparamia kitanda mpaka kaparamia maiti ya Bwana Andenga Kazimoto. "Fyatua risasi" alipiga kelele Bob Chinanga kwa hamaki kama mwehu, alishajua maji yamezidi unga tayari.
Alikuwa ameshachelewa, kwani Kachero Manu alishamrushia teke la mkononi yule mwenye bunduki mkononi ikamponyoka lakini akawahi yule msaidizi wa Bob-Chinanga kuchomoa tochi kiunoni na kuwasha, ilikuwa ni zile tochi kubwa sana chumba kikaenea mwangaza.
Ule mwangaza ukawa kosa kwao sasa Kachero Manu akawa anawaona wote vizuri. Haraka haraka Kachero Manu akaruka kurukia tumbo la maiti ya Bwana Andenga kisha akajibinua hewani na kumchapa teke moja matata sana la kifuani Bob Chinanga ambaye alikuwa ametoka kujizoazoa chini. Lakini licha ya ukali wa lile teke la Kachero Manu lilipofika kifuani kwa Bob Chinanga hakutikisika hata kidogo.
Isipokuwa alichezesha matiti yake kifuani huku anacheka mithili ya wale wacheza mieleka wa miaka ile ya 90's walivyokuwa wanachezesha matiti yao akina "Power Bernado", "Power Marungusi", "Power Bukuku" au "Power TX-Chaka".
Yule msaidizi wa Bob Chinanga akawa anatambaa kiujanja kwenda kuiwahi bunduki iliyodondoka. Kachero Manu hakumchelewesha alimuwahi akamrukia mgongoni kisha akakamata shingo yake na kuinyonga mara moja, akafa pale pale bila kuomba maji.
Kitendo cha kupoteza uhai wa msaidizi wake, Bob Chinanga kilimkasirisha vibaya sana, alipandisha morali na kumfuata Kachero Manu pale alipo kama mbogo huku anapiga ukelele wa hasira mithili ya Morani wa Kimasai. Wakawa sasa wamekaribiana wanaviziana, Bob Chinanga akawa anaruka ruka kama nyani, mara amerukia zile bomba zinazoning'inia za kutesea mateka mara ameshuka anavizia ashambulie kwa kushtukiza.
Hapo Kachero Manu akajua huyu anatumia staili ya kizamani kabisa za akina "Koo Ting Sang" alizokuwa anazitumia katika filamu ya "Snake in the monkey's shadow". Kachero Manu akaamua kutumia staili ya "Chang Quan" ambayo ni mpya kabisa haujazoeleka na wengi. Mtindo ambao unapoanza unasimamisha mguu wa kulia na unaukunja mguu wa kushoto mpaka maeneo ya goti la mguu wa kulia huku mkono wa kulia unanyooka huku wa kushoto unakuja chini, ni staili ambayo ilikuwa ni ngeni kabisa machoni kwa "Bob Chinanga".
Alivyokunja ule mguu Kachero Manu, Bob Chinanga akaona kapata nafasi ya kushambulia akaruka kumrukia Kachero mzima mzima, lilikuwa ni kosa baya sana kwake. Alipokuja Kachero aliukunja mguu wa kulia kisha ule mguu wa kushoto ambao ulikuwa upo juu ukapita kwenye shingo la Bob Chinanga, ikawa sinema ya mbwa aliyeingiza kichwa kwenye ndoo yenye mdomo mdogo anashindwa kutoa kichwa chake. Ikawa kila anapojichomoa ndio kabali ya mguu inazidi kujikaza mpaka Bob Chinanga aanza kuhisi anataka kuishiwa pumzi, huku anatoa mishuzi ovyo.
Alichofanya Bob Chinanga ni kujisukuma kichwa kwa nguvu zote kikachomoka na kupiga sehemu za siri za Kachero Manu. Jaribio lake lilifanikiwa kwani Kachero Manu aliachia mguu na kupiga kelele utasema amekanyagwa na tairi la trekta. Bob Chinanga bila kuchelewa akampiga Kachero Manu farasi teke la nguvu eneo la tumboni ambalo lilimfanya kachero Manu apepesuke kama mlevi wa gongo. Bob Chinanga akajua ameshamaliza kazi akawa anamfuata Kachero Manu kizembe bila kuchukua tahadhari.
Kachero Manu akazuga kama amezidiwa na kipigo cha Bob Chinanga kumbe anamvizia asogee karibu amalize kazi. Alipomsogelea karibu zaidi akawa anajiandaa kumsukumizia makonde ya usoni Kachero Manu, aliporusha konde la mkono wa kushoto, Kachero Manu akaliona akakwepesha kichwa chake kuelekea kushoto kidogo tu, konde likapita patupu hewani. Bob Chinanga akapoteza uelekeo kutokana na kuyumba.
Hapo ndipo Kachero Manu akatupa konde la nguvu la mkono wa kulia, konde ambalo lilimuangusha chini Bob Chinanga kwa kishindo. Haraka haraka akajinyanyua chini akajifuta kwenye pembe ya ncha ya mdomo wake akaona damu zinachuruzika. Akaanza kurusha ngumi mtawalia bila umakini, ambazo ngumi zote Kachero Manu alikuwa anazikwepa huku anarudi nyuma nyuma. Kitendo cha kuona damu yake inamwagika kilichochea hasira za Bob Chinanga na kupunguza uwezo wake finyu wa kufikiri akawa anakuja kumvamia Kachero Manu kama anakuja kubeba gunia la viazi lumbesa.
Kachero Manu hakumkawiza, akajipindua sarakasi kurudi nyuma kisha akaruka na teke moja kali sana la mguu wa kushoto lililotua kwenye usawa wa koo la Bob Chinanga ambalo lilimtupa chini kwa mara ya pili akafikia chali upande wa kisogoni akawa anajaribu kunyanyuka anashindwa.
Hapo hapo Kachero Manu akamrukia na kumkaba kabali ya mbao huku magoti ya Kachero Manu yamekanyaga tumbo la Bob Chinanga, akawa kila Bob Chinanga akijaribu kujitoa hawezi kujitoa, mpaka akaanza kukoroma kwa kukosa hewa, akanyonga kwa nguvu shingo ya Bob Chinanga mpaka akapoteza uhai. Kachero Manu akawa anahema kwa nguvu huku jasho linamtiririka haamini kama amemuangamiza Bob Chinanga.
View attachment 1460675
Daaaah mzigo unazidi kunoga tu big up mkuu mpasta
 
Back
Top Bottom