Wengi wamesema hivyoRiwaya ni nzuri sana tu...ingekuwa kitabu hakijatoka ningekushauri ubadilishe jina
Sent using Jamii Forums mobile app
Subiri tumtumikie mwajiri lunch time tutarushaKimya sana pande hii tunaisubiri Cabo Delgado full arosto
Daaaah mzigo unazidi kunoga tu big up mkuu mpastaCABO-DELGADO-PART 33
️
Bob-Chinanga katimba kambini tayari kumnyakua Kachero Manu
Bob Chinanga alifanikiwa kumtoroka Komandoo mstaafu Jacob Steven (JS) katika sekeseke la kurushia risasi, kwa kurukia lori la mizigo.
Lori hilo la mizigo kwa bahati nzuri lilikuwa linaelekea karibu kabisa na kambi ya "Gorongosa Camp" kwa karibia kilomita 7 Lilikuwa ni Lori la "Gorongosa National Park" likiwa linatoka bandari ya Beira kubeba mizigo ya vifaa mbalimbali vya kutumiwa mbugani kwa ajili ya ofisi na wataliii.
Dereva wa Lori aliziona zile gari mbili akawa yupo makini katika kuongeza mwendokasi wa gari lake hakutaka kusimama maana anafahamu njia ya kuelekea mbuga ya Gorongosa haikuwa nzuri sana kiusalama. Hivyo Bob-Chinanga alipodandia lori alifanikiwa kupasua turubai lililoziba mizigo kwa kisu chake cha kukunja ambacho ni moja ya silaha zake anazolala na kuamka nazo.
Akafanikiwa kujisweka katikati ya lundo la mizigo kukwepa baridi kali ya milimani. Wakati wote alikuwa anaangalia saa yake maana alijua uzembe wowote wa kumchelewesha kachero Manu kufikishwa mbele ya Bwana mkubwa Alfredo ungepelekea kupoteza kazi na hata kupoteza uhai wake.
Kama kuna mtu NACATANAS wote mpaka Inspekta Mark mwenyewe walikuwa wanamuogopa basi ni Alfredo. Inasemekana Alfredo alipoenda kusoma Chicago, Marekani alipitia pia mafunzo ya kijasusi ila wengi walikuwa hawajui na alikuwa hapendi ajulikane kama ni bobezi kwenye fani. Inasemekana siri hii ilitolewa na majambazi wa Cabo-Delgado waliwahi majambazi kama 6 waliwahi kuvamia nyumbani kwake usiku wa manane alichowafanyia ni gumzo mpaka leo.
Wenyewe walijua ni tajiri kibonde kibonde nyama uzembe, mwili yai kama hawa matajiri wetu wanavyojiweka. Inasemekana aliwaona kwenye mifumo yake ya ulinzi wakati wanaingia ndani ya nyumba akawaagiza walinzi wake wakiwakamata wawany'ang'anye silaha kisha wawaache waje ndani, alipokutana nao alipigana nao wote majambazi 6 kwa pamoja, akawafirigisa sawia. Ambapo 3 kati yao walivunjwa viuno vyao na mmoja alikufa palepale hawa 2 waliponea tundu la sindano lakini wakiwa wamevunjwa mikono. Hao ndio walioenda kuvujisha siri kwenye vijiwe kuwa hawajawahi kuona mtu mtaaalamu wa sanaa za mapigano kama Bwana Alfredo.
Hivyo Bob Chinanga alifahamu hana uwezo wa kumuepuka Alfredo bali ni kutekeleza maagizo yake kama anavyotaka. Alipokaribia karibia na mbuga, Bob Chinanga aliteremka bila kuonekana na dereva wa lori.
Kwa mtu kama Bob Chinanga ilimchukua nusu saa tu kupata usafiri wa kufika kambini, ni hivi alienda kwenye vichochoro vinavyotumiwa na wawindaji haramu wanaotumia bodaboda kusafiri mizigo usiku usiku kuipeleka Gorongosa mjini. Huko akafanikiwa kupora bodaboda moja bila hata kuua inzi maana dereva bodaboda alivyomuona tu aliachia mwenyewe funguo maana alijua kubishana na Bob Chinanga ni sawa na kujitafutia kifo cha makusudi.
Mpaka kufika muda saa tatu kasoro usiku Bob Chinanga alikuwa anaingia kambini, huku akiacha maagizo makali ya ulinzi wa kambi kuimarishwa maradufu na kutoa onyo kuwa uzembe wowote utakaoruhusu kambi kuvamiwa haotuvumilika kwa mhusika yoyote kwenye idara yake.
Baada ya kutolewa amri hiyo mkuu wa kikosi cha mbwa alikuwa yupo nje na wasaidizi wake kuimarisha ulinzi, wale wanaozunguka ukuta wa kambi kila mmoja akiwa na silaha yake iliyojazwa risasi alikuwa kwenye eneo lake ili mradi ulikuwa ni usiku wa hekaheka mtindo mmoja. Na kila mmoja alikuwa kwenye sare zao za rangi ya kaki, kofia na buti nyeusi ili iwe rahisi kutambuana inapotokea tatizo.
"Showdown" ya kibabe "Mwiba wa Tasi" vs "Bob-Chinanga"
Kachero Manu aliona giza linazidi kuwa totoro mule selo kuu huku hamna dalili yoyote ya kuja kwa mabaradhuli wale. Alipoisogelea maiti ya msaliti Bwana Andenga Kazimoto alikuta imeanza kufutuka. Akajisema ndio kawaida ya maiti za watu wenye vitambi huwa zinavimba sana. Akapatwa na huruma ya mzazi kwa mtoto akawa anawafikiria watoto wa Mzee Andenga watakuwa wanamsubiria baba yao arudi safari toka Msumbiji na zawadi za kutambishia watoto wenzao shuleni. Lakini ndio basi tena hawatamuona baba yao ataishia kuwa chakula cha ndege na fisi porini, au chakula ya samaki mtoni.
Akiwa amezama katika dimbwi lenye kina kirefu la fikra, akapata wazo la kukitega kile kitanda cha chuma mlango na kwa kuwa wakiona giza wataingia kwa pupa watakapojikwaa watapoteza umakini hapo hapo itakuwa rahisi kuwavamia na kuwamaliza. Akakisogeza kitanda kwa kutumia nguvu zote huku juu yake kuna maiti ya Bwana Andenga mpaka akafanikiwa kukitega kitanda meta chache kutoka kwenye geti la kuingia kwenye selo kuu, kisha yeye akajibanza pembeni. Akasikia kama mlango unagongwa akajiweka tayari kwa lolote. Lakini kumbe walikuwa ni popo wa ndani ya selo wanajigonga kwenye kwenye mlango.
Kumbe popo walikuwa wanamletea habari njema haikuzidi hata dakika 5 akawa anaskia nyayo za vishindo vya viatu vinatembea akajisemea kazo iliyonileta Cabo-Delgado ndio inaanza. Akajibana vizuri pembeni mwa kitanda, na kwa haraka alivyopima mlio wa zile nyayo za viatu akaamini hawazidi zaidi ya kati ya watu wawili au watatu. Mlango ukawa unafunguliwa kwa vishindo vyote huku wanajiamini adui yetu Kachero Manu yupo mahututi kwenye kamba alizofungwa hajiwezi kumbe "Mwiba wa Tasi" alikuwa anawasubiri tu waingine kichwa kichwa awafunze adabu. Awaonyeshe cha mtema kuni kilichomnyoa kanga manyoya.
Wa kwanza kuingia alikuwa ni Bob Chinanga na bangi yake mkononi analipuliza ili kujipa stimu za kuwajibika. Alipagawa baada ya kuona giza nene akaingia ndani kichwa kichwa akajikuta anaparamia kitanda mpaka kaparamia maiti ya Bwana Andenga Kazimoto. "Fyatua risasi" alipiga kelele Bob Chinanga kwa hamaki kama mwehu, alishajua maji yamezidi unga tayari.
Alikuwa ameshachelewa, kwani Kachero Manu alishamrushia teke la mkononi yule mwenye bunduki mkononi ikamponyoka lakini akawahi yule msaidizi wa Bob-Chinanga kuchomoa tochi kiunoni na kuwasha, ilikuwa ni zile tochi kubwa sana chumba kikaenea mwangaza.
Ule mwangaza ukawa kosa kwao sasa Kachero Manu akawa anawaona wote vizuri. Haraka haraka Kachero Manu akaruka kurukia tumbo la maiti ya Bwana Andenga kisha akajibinua hewani na kumchapa teke moja matata sana la kifuani Bob Chinanga ambaye alikuwa ametoka kujizoazoa chini. Lakini licha ya ukali wa lile teke la Kachero Manu lilipofika kifuani kwa Bob Chinanga hakutikisika hata kidogo.
Isipokuwa alichezesha matiti yake kifuani huku anacheka mithili ya wale wacheza mieleka wa miaka ile ya 90's walivyokuwa wanachezesha matiti yao akina "Power Bernado", "Power Marungusi", "Power Bukuku" au "Power TX-Chaka".
Yule msaidizi wa Bob Chinanga akawa anatambaa kiujanja kwenda kuiwahi bunduki iliyodondoka. Kachero Manu hakumchelewesha alimuwahi akamrukia mgongoni kisha akakamata shingo yake na kuinyonga mara moja, akafa pale pale bila kuomba maji.
Kitendo cha kupoteza uhai wa msaidizi wake, Bob Chinanga kilimkasirisha vibaya sana, alipandisha morali na kumfuata Kachero Manu pale alipo kama mbogo huku anapiga ukelele wa hasira mithili ya Morani wa Kimasai. Wakawa sasa wamekaribiana wanaviziana, Bob Chinanga akawa anaruka ruka kama nyani, mara amerukia zile bomba zinazoning'inia za kutesea mateka mara ameshuka anavizia ashambulie kwa kushtukiza.
Hapo Kachero Manu akajua huyu anatumia staili ya kizamani kabisa za akina "Koo Ting Sang" alizokuwa anazitumia katika filamu ya "Snake in the monkey's shadow". Kachero Manu akaamua kutumia staili ya "Chang Quan" ambayo ni mpya kabisa haujazoeleka na wengi. Mtindo ambao unapoanza unasimamisha mguu wa kulia na unaukunja mguu wa kushoto mpaka maeneo ya goti la mguu wa kulia huku mkono wa kulia unanyooka huku wa kushoto unakuja chini, ni staili ambayo ilikuwa ni ngeni kabisa machoni kwa "Bob Chinanga".
Alivyokunja ule mguu Kachero Manu, Bob Chinanga akaona kapata nafasi ya kushambulia akaruka kumrukia Kachero mzima mzima, lilikuwa ni kosa baya sana kwake. Alipokuja Kachero aliukunja mguu wa kulia kisha ule mguu wa kushoto ambao ulikuwa upo juu ukapita kwenye shingo la Bob Chinanga, ikawa sinema ya mbwa aliyeingiza kichwa kwenye ndoo yenye mdomo mdogo anashindwa kutoa kichwa chake. Ikawa kila anapojichomoa ndio kabali ya mguu inazidi kujikaza mpaka Bob Chinanga aanza kuhisi anataka kuishiwa pumzi, huku anatoa mishuzi ovyo.
Alichofanya Bob Chinanga ni kujisukuma kichwa kwa nguvu zote kikachomoka na kupiga sehemu za siri za Kachero Manu. Jaribio lake lilifanikiwa kwani Kachero Manu aliachia mguu na kupiga kelele utasema amekanyagwa na tairi la trekta. Bob Chinanga bila kuchelewa akampiga Kachero Manu farasi teke la nguvu eneo la tumboni ambalo lilimfanya kachero Manu apepesuke kama mlevi wa gongo. Bob Chinanga akajua ameshamaliza kazi akawa anamfuata Kachero Manu kizembe bila kuchukua tahadhari.
Kachero Manu akazuga kama amezidiwa na kipigo cha Bob Chinanga kumbe anamvizia asogee karibu amalize kazi. Alipomsogelea karibu zaidi akawa anajiandaa kumsukumizia makonde ya usoni Kachero Manu, aliporusha konde la mkono wa kushoto, Kachero Manu akaliona akakwepesha kichwa chake kuelekea kushoto kidogo tu, konde likapita patupu hewani. Bob Chinanga akapoteza uelekeo kutokana na kuyumba.
Hapo ndipo Kachero Manu akatupa konde la nguvu la mkono wa kulia, konde ambalo lilimuangusha chini Bob Chinanga kwa kishindo. Haraka haraka akajinyanyua chini akajifuta kwenye pembe ya ncha ya mdomo wake akaona damu zinachuruzika. Akaanza kurusha ngumi mtawalia bila umakini, ambazo ngumi zote Kachero Manu alikuwa anazikwepa huku anarudi nyuma nyuma. Kitendo cha kuona damu yake inamwagika kilichochea hasira za Bob Chinanga na kupunguza uwezo wake finyu wa kufikiri akawa anakuja kumvamia Kachero Manu kama anakuja kubeba gunia la viazi lumbesa.
Kachero Manu hakumkawiza, akajipindua sarakasi kurudi nyuma kisha akaruka na teke moja kali sana la mguu wa kushoto lililotua kwenye usawa wa koo la Bob Chinanga ambalo lilimtupa chini kwa mara ya pili akafikia chali upande wa kisogoni akawa anajaribu kunyanyuka anashindwa.
Hapo hapo Kachero Manu akamrukia na kumkaba kabali ya mbao huku magoti ya Kachero Manu yamekanyaga tumbo la Bob Chinanga, akawa kila Bob Chinanga akijaribu kujitoa hawezi kujitoa, mpaka akaanza kukoroma kwa kukosa hewa, akanyonga kwa nguvu shingo ya Bob Chinanga mpaka akapoteza uhai. Kachero Manu akawa anahema kwa nguvu huku jasho linamtiririka haamini kama amemuangamiza Bob Chinanga.
View attachment 1460675