Riwaya: "Cabo-delgado"-part 01

Riwaya: "Cabo-delgado"-part 01

Daaah mkuu mpasta umetisha ,hii story nimeipenda sana maeneo mengi uliyoyataja nayafahamu sana
 
CABO-DELGADO ANCHANJA MBUGA
MPAKA BARA LA AMERICA
Screenshot_20200523-193919.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
CABO-DELGADO-PART 27

Usijaribu kuleta ujanja wowote, jaribio lolote utakalofanya litagharimu uhai wao, kula ujisosomole kuondosha njaa yako" alisema yule baradhuli aliyebeba SMG huku akiwa amemuelekezea Kachero Manu mdomo wa bunduki. Dr.Anabella akawa nae kaisogelea meza ile chakavu akatoa baadhi ya chupa za madawa, mkasi na pamba akaweka juu ya meza kisha akaegemea meza anamuangalia Kachero Manu anavyopokea chakula.
Kwa njaa aliyokuwa nayo, aliuchovya ule mkate wa Boflo wote kwenye supu kisha akaula kama uji, kisha akaanza kuokoteza marapu rapu ya nyama akichanganya na matandu akawa anakula. Nyama ambayo harufu yake inaonyesha kama imekaa muda mrefu kwenye friza ambalo lilikuwa halifati kanuni za uhifadhi kwa kufunguliwa ovyo mara kwa mara hivyo kusababisha nyama kuanza kupoteza ubora wake. Kwa njaa aliyokuwa nayo Kachero hata kama ungempa nyama iliyotupwa jalalani wiki moja angekula, kisha akakombelezea mchuzi wa supu na kuiacha sahani ya matandu na bakuli la supu likiwa halina hata chembe ya mabaki ya chakula zaidi ya mifupa michache.
Baada ya kumaliza mlo wake akaomba apelekwe chooni. Choo kilikuwa upande mkabala na meza aliyoegemea Dr.Anabella, akasindikizwa huku ameshika bega la yule mbeba chakula huku anaruka ruka katika kutembea kama mtu mwenye mguu mmoja huku baradhuli aliyebeba bunduki anawafuatia kwa nyuma kwa umakini mkubwa bila kupepesa macho kama mpambe wa Rais anavyokuwa makini.
Kilikuwa ni choo ambacho hakifai kwa matumizi ya binadamu. Tundu la choo cha sinki lilikuwa limeziba na kusababisha uchafu wa haja za wanaotumia kuelea juu juu, huku mikojo ikiwa imetiririka kila kona. Sakafu yake ilikuwa imesakafiwa na marumaru nyeupe ila kutokana na ukoko wa uchafu zilikuwa mithili ya sakafu ya rangi njano na kijani kutokana na kuunguzwa na chumvi chumvi ya madini ya urea inayotoka kwenye mikojo ya binadamu. Huku inzi wenye ukubwa kama nyuki walikuwa wanasheherekea rundo la uchavu katika tundu la choo.
Ila hilo halikumshtua Kachero Manu kwani huwa Makomandoo wanapitia mazingira magumu ya kukujengea ujasiri zaidi. Alishawahi kusimama kwenye shimo la kubeba uchafu wa choo muda wa siku mbili huku uchafu umefika mpaka kifuani mwako. Hivyo kwa choo hicho kwake kilikuwa ni kama choo cha Ikulu kwa upande wake akilinganisha na mazito aliyopitia.
Wakati anarudishwa toka chooni, alitupia jicho mezani na kufanikiwa kuona miongoni mwa baadhi ya chupa za dawa. Aliona kuna spiriti, na chupa zinginezo ambazo hazifahamu. Alikuwa anajaribu kuangalia labda kuna kitu kitakachomsaidia, kama ujuavyo "mfa maji haachi kutapatapa". Alipotulia sakafuni, akafungwa tena kamba za mikononi, kwa ustadi mkubwa zaidi mpaka akahisi damu haipiti vizuri. Baada ya harakati hizo akaitwa Dr.Anabella ili ampe huduma ya kwanza. Akaja akamsafisha vidonda vyake na kumpaka dawa kisha akamchoma sindano ya kupunguza maumivu. Baada ya kumpa huduma ya kwanza akabeba vifaa vyake akaelekea usawa wa lango la kutokea akamuona anatupa vitu kama takataka kwenye pipa dogo la takataka. Baada ya hapo akageuka kumuangalia Kachero Manu kisha akamkonyeza ukope kwa jicho legevu la mahaba na kutabasamu, halafu akaongoza njia ya kutoka. Kitendo hicho cha kukonyezwa kilimfanya asisimukwe mwili na kuanza kuwaza mambo mengi sana.
"Ina maana huyu Dr.Anabella amenizimia kimapenzi ameamua kuelezea hisia zake kwangu kwa ishara mpaka ananilegezea jicho kiasi kile na kunikonyeza" mawazo machafu yalipata katika fikra zake. Akaanza kujiuliza tena nafsini mwake "ametupa takataka gani mule mpaka akaamua anigeukie, anikonyeze na kutabasamu".
Wale mabaradhuli wawili wakashika uelekeo wa kutoka nje ya selo kuu wakimfuata Dr.Anabella. Walipofika mlango wakati wengine wameshatoka, akageuka nyuma yule aliyebeba bunduki akamuangalia Kachero Manu kisha akampayukia "Leo ndio siku yako ya mwisho kuishi duniani, usiku huu utakuja kuchukuliwa ukawaone hao unaowatafuta kabla hujatolewa roho yako, kwaheri ya kuonana wasalimie huko akhera ukienda" akabamiza geti na kuanza kufunga lango lako na kufuli na kwenda zao.
Kwa makadirio Kachero Manu akajua inaweza kuwa ni saa sita mchana, hivyo apumzishe mwili kisha aanze kuwaza njia za kutoroka vinginevyo wakija mara ingine ni kwenda kupelekwa kufa mbele ya vigogo wa Monte Branco Ltd.
Akaegemea ubavu mmoja huku uso wake unaitizama kurunzi ya karabai ambayo kioo chake kina nyufa za mpasuko. Ni kurunzi ambayo daima haizimwi kutokana na giza la ndani ya selo ile. Kachero Manu akapitiwa na usingizi mdogo wa mchana, akisubiri miujiza ya kuokoka.

Anasakwa Kachero Manu na Komandoo mstaafu 'JS'.
Wakati anapewa maagizo ya kwenda Jimboni Cabo-Delgado, Msumbiji Kachero Manu aliambiwa akiwasili salama awasiliane na Komandoo mstaafu wa Msumbiji Bwana Jacob Steven (JS), mmoja wa makomandoo watano bora katika bara la Afrika. Kachero Manu alitii maagizo ya Mkuu wake wa kazi, hakuleta ujuaji, alifanya nae mawasiliano kupitia wavuti.
Huyo ndiye yule aliyemsaidia Kachero Manu kupata nyumba Montepuez na kukodishiwa gari aina ya Volvo s60 anayoitumia kwenye misafara yake mbalimbali ya hapa na pale. Kampuni ya kukodisha magari ya "PAPADIOT". Kampuni ambayo magari yake yote yamefungwa mfumo wa kufuatilia wapi lilipo (car tracker) ili kuchunga usalama wa gari na mtumiaji.
Hivyo kitendo cha gari alilokodishwa Komandoo Jacob Steven (JS) kuonekana limeegeshwa pembezoni mwa ukumbi wa maonyesho kwa zaidi ya saa 12 bila kutembea kiliwapa mashaka. PAPADIOT wakaamua kumpa taarifa Bwana Jacob Steven (JS).
Alipofuatilia ndipo akalikuta gari kwenye maegesho. Akafanikiwa kufungua ndani akahisi yumkini Kachero Manu atakuwa matatizoni, kwa sababu alikuta zana za kazi zimefichwa ndani ya gari kwenye makanyagio ya miguu ya dereva.
Kwa utundu wake wa kipelelezi na kutoa mlungula au chauchau kwa mfanyakazi wa ukumbi wa maonyesho ilipoegeshwa gari anayedhibiti CCTV-Camera, akafanikiwa kumuona Kachero Manu namna anavyoegesha gari na kutokomea mtaani usiku wa manane akielekea upande wa "Pemba Magic Lodge". Akafanya mbinu tena kutoa chauchau kwa mdhibiti wa "CCTV-Camera" wa Pemba Magic Lodge, hapa hakufanikiwa kitu aliwekewa ngumu, waliogopa rungu la Mafioso wa Alfredo litawashukia wakigundua kuwa wao ndio wameuza mechi. akatengeneza mbinu ya pili ya kudukua "CCTV-Camera" ya nyumba hiyo ya kulaza wageni. Akatengeneza utundu wa njia tano kwa kutumia vifaa maalumu, kitaalamu vinaitwa "DVRs" na "IP" Camera, kisha akazielekeza kwenye mtandao wa wazi (open internet) hapo ndipo alipofanikiwa kuona tukio zima namna alivyotekwa Kachero Manu na gari lililotumika kumteka.
Haya mafunzo ya kudukua nyaraka za siri, mitandao na "Camera" kama "CCTV Camera" kwa Komandoo mzoefu kama yeye ni kitu cha nusu saa tu. Hapo sasa ikabaki kufuatilia hilo gari lililomteka limeelekea nae wapi.
Ilimchukua masaa kama mawili ya upelelezi na kulikuta gari hilo limeegeshwa kwenye kiwanda cha korosho kinachomilikiwa na kampuni ya Monte Branco Ltd anapofanyia kazi Dr.Anabella. Lengo lake halikuwa kumpata mmiliki ila ilikuwa ni kumpata kachero Manu yupo wapi tena akiwa hai.
Akatumia akili za kuzaliwa kwa kuchukua sampuli za vumbi la mbele ya gari chini ya boneti kijasusi bila kujulikana kisha akatuma sampuli kwenye maabara ya vijidudu inayoitwa "MICROCHEM" iliyopo nchini Afrika ya Kusini kutambua vijidudu wanaopatikana kwenye udongo uliokutwa kwenye gari ni wa maeneo gani. Ili iwe rahisi kujua wapi gari lililomteka Kachero Manu lilitembelea kwa mara ya mwisho.
Baada ya kupita saa 10 majibu kutoka "MICROCHEM" yakaanikwa hadharani. Yakaonyesha wadudu waliopatikana kwenye sampuli ya vumbi la gari wapo kwa wingi mbugani, na yakaonyesha gari inaweza kuwa ilikwenda maeneo ya Gorongosa.
Komandoo Jacob Steven (JS) ilipotimu saa kumi alasiri, saa 3 kabla ya Kachero Manu kuja kunyakuliwa mafichoni kwa ajili ya kupelekwa mbele ya mkutano wa Mafioso wa biashara ya rubi, akawa nae anaelekea kwenye kampuni ya helikopta ya kukodi. Lengo lilikuwa aweze kwenda maeneo ya Gorongosa maana asingeweza kwenda na gari akafika mapema kutokana na umbali huo.
Lakini bado Komandoo JS alikuwa kwenye kizungumkuti, hafahamu ni wapi atampata kijana wake. Ila akajipa moyo bahati itaangukia kwake. Akajisemea mwenyewe nafsini mwake "daima Mwenyezi Mungu huupigania upande wa wenye haki, na shetani husaidia upande wa waovu, maandiko ya dini ndivyo yanavyofundisha".


Sent using Jamii Forums mobile app
 
CABO-DELGADO-PART 29
Akakaa kitambo kifupi akifikiria mbinu nyingine ya kufanya, akaamua aanze kuvingirika kuelekea kwenye pipa la takataka. Matarajio yake huko yalikuwa huenda akakuta mkasi umetupwa ili ukiwepo aubane kwenye meno kisha autumie kukatia kamba ya mikononi. Akajipa matumaini atapata kifaa cha kujifungua.
"Kwa namna Dr.Anabella alivyokuwa anatupa kitu kwenye pipa, alivyoniangalia sana ile ni ishara kuna kitu cha kuniokoa aliniwekea" mawazo chanya yalipita kwenye fikra zake. Akaanza kujisogeza huku jasho linamtiririka mwilini kama maji kutokana na joto la mule selo.
Alipokuwa yupo karibu na nusu kufikia kwenye pipa la taka, ghafla akasikia vishindo vya mabaradhuli wanakuja selo kuu, hapo hapo akaanza kukata tamaa ya kutoroka akajua amekwisha wanakuja kumchukua. "Lakini mbona mapema sana wanakuja kunichukua kulikoni!" aliwaza sana Kachero Manu. Akaanza kusali sala maarufu kwa Wakatoliki, ya Baba yetu wa mbinguni akijua hapa tena hana ujanja alishakubali shingo upande kushindwa na maadui zake. Wakati amefunga macho yako yuko katika hisia nzito ghafla lango likafunguliwa wakaingia mabaradhuli wawili wapya ambao hawafahamu wakiwa wamembeba mzobe mzobe mtu mmoja.
Alikuwa ni shaibu wa makamo hakosi miaka 55 kwenda juu ukimkadiria. Alikuwa kirambi cha mtu, mfupi kama mbirikimo ana tumbo kubwa ambalo linatokana na ulaji mbovu wa vyakula na uvivu wa mazoezi na kujisaidia haja kubwa mara kwa mara. Cha kusikitisha huyu Mzee alikuwa yupo uchi wa mnyama analia kwa sauti mbaya kama ya punda kilongwe wa majumbani. Alitoa kilio mpaka sauti yake ikampwelea kabisa.
Walipoingia wale mabaradhuli hawakumjali kabisa Kachero Manu ambaye alijikunyata na kujifanya tongo hajui chochote kinachoendelea. Wakamfunga juu kwa juu yule Mzee kama nyama ya mbuzi wa ndafu anayesubiri kuliwa na maharusi. Mzee wa watu ukawa inamtoka mikojo ya uoga mfululizo utasema anaumwa ugonjwa wa kisukari hawezi kujizuia mkojo, au anaumwa ugonjwa unaoitwa nasuri uwapatao akina mama waliotoboka tundu la mkojo maarufu mtaani kama fisitula.
Kumbe kihoro chake ni cha uoga wa kifo cha kishenzi na cha kidhalili ugenini. Kachero Manu akawa anajichekea kimoyo moyo kuwa huyu Mzee atakuwa yupo ndani ya kumi bora ya watu waoga duniani. Kisha walivyomfunga wakamuacha anabembea huku kichwa kinaning'inia halafu wakafunga mlango na kuondoka. Mzee uso wake ulivimba vimba kidogo ulikuwa na manundu, inaonyesha alikuwa kuna kitu anakaidi kutekeleza wakamnasa mambata ya haja ya usoni. Na mdomo wa chini ulipasuka kidogo ukawa unamwaga damu.
Kachero Manu akavuta taswira ya huyu Mzee, akili yake ikamwambia kuwa anamfahamu vilivyo tena anamjua sana na ni mtu maarufu ila tu kupondeka kwa sura yake ikawa sura inaingia na kuondoka. Mwishowe Kachero Manu akaanza kuangua kicheko cha sauti kubwa na dharau mpaka Mzee wa watu akaanza kuogopa kuwa huenda kaletwa gereza la vichaa.
"Kumbe ni Mzee Andenga Kazimoto, kaletwa selo kuu, kazi ipo mwaka huu" alijiwazia baada ya kumtambua. Waswahili walisema "shukrani ya punda ni mateke. Amekipata alichokitafuta kwa mafia Alfredo. Inaonyesha Alfredo kaona hana umuhimu wa kuingia kwenye kikao wakati nyaraka wameshazipata" akazidi kuwaza Kachero Manu.
Kweli tamaa ilimuua fisi, 'kakosa mwana na maji ya moto'. Maana kwa Cheo cha huyu Mzee Andenga, alikuwa amebakiza miaka michache ya kustaafu angepata kiinua mgongo na pensheni nzuri tu ya kula na familia yake mpaka mwisho wa uhai wake.
"Komandoo Mstaafu uso kwa uso na NACATANAS"
Komandoo mstaafu Jacob Steven (JS) alipofanikiwa kugundua gari lililowapeleka akina Kachero Manu 'Gorongosa Camp', akaenda moja kwa moja kwenye kampuni ya helikopta ya kukodisha ili aelekee Gongorosa kumkomboa kijana wake.
Masaa matatu tu ya kufa au kupona yalikuwa yamebaki kabla ya Kachero Manu kuletwa kiwanda cha Korosho cha Monte Branco Ltd. Ilitakiwa komandoo 'JS' atumie 'kipawa cha liwa kutibu harara', afanye vyovyote iwavyo amnasue kijana wake. Kama angekwenda na gari asingeweza kufika wakati muafaka wa kuweza kumuokoa.
Umbali wa kutoka Pemba mpaka Gongorosa ni kama kutoka Dar esalaam mpaka Mbeya kwenda na kurudi. Eneo la Gongorosa lipo jimbo la kati la Sofala zaidi ya kilometa 1635.
Bahati nzuri akapata nafasi kwenye helikopta hiyo ya kukodi inayoelekea "Gongorosa National Park" (GNP) inayopeleka watalii mbugani. Mpaka saa 11 jioni akawa ameshawasili Gongorosa. Sasa kilichokuwa kinachomsumbua kichwani mwake ni kufahamu Kachero Manu kafichwa wapi?. Maana ni sawa na mwenyeji wako akuambie nipo Dar es salaam, lakini Sinza, Manzese, Mbagala, Kawe, Goba, Mbezi, Rehema, Masaki zote ni Dar es Salaam. Lakini bado hata ukifahamu ni Sinza bado Sinza ni kubwa sana, Kwa Remmy, Kumekucha, Palestina, Madukani, Shekilango bado vyote hivyo ni vitongoji vya Sinza.
Akaumiza kichwa akapata jawabu ni kuuliza wapi kuna Ukumbi wa starehe maarufu kuliko zote, huko ndio atapata majibu. Maana haiwezekani viongozi wa Gorongosa Camp wanaolipwa pesa nzuri sana washindwe kustarehe. Tabia za watu majambazi na maharamia ni kustarehe sana, ndio maana pesa wanazopata hazina fidi. Ukitaka kumsaka mtu swalihina basi ni kwenye nyumba ya ibada, lakini mtu fedhuli pesa zake huwa zinaishia kwenye pombe, muziki na kustarehe na vidosho.
Akauliza uliza kwa wenyeji klabu za fauka kwa starehe, wengi wao walimtajia kiwanja cha kisasa cha kujivinjari ukiwa Gongorosa kinaitwa "Montebelo Pub". Akafanikiwa kufika "Montebelo Pub" anayasoma mazingira.
Ilikuwa ni "Pub" yenye kuvutia kimazingira, ilijengwa ikajengeka vilivyo. Geti la kuingilia lilipambwa na bango kubwa lenye maandishi makubwa lililoandikwa jina la "Montebelo Pub". Kisha ilizungukwa na fensi fupi ya ukuta iliyopandwa miti iliyoshonana kuzunguka ukuta wote. Kwa ndani kulikuwa na midule mingi mingi iliyozungukwa ukumbi mzima kwa umbo la duara huku katikati kukiwa na ukumbi wa wazi uliozibwa kwa paa la makuti yanayotokana na mti wa mnazi.
Pia kulikuwa na wahudumu ambao ni wasichana wabichi na vipusa ambao wengi wao wapo katika rika la kufanana la kuanzia miaka 20 mpaka 25 wakiwa wamevalia mavazi yao ya sare za minisketi zenye kuacha sehemu kubwa ya mapaja yao nje nje bila kufunikwa vizuri, juu wana fulana nyeupe zilizowabana na kuzichongoa vilivyo chuchu zao konzi.
Alipoingia alikuta nje kuna magari mengi ya kifahari yameegeshwa kwenye maegesho kuonyesha kuwa ni "Pub" ya watu wazito wa Mji. Alipofika akachagua meza iliyokaribu na ukumbi wa kutumbuizia akavuta kiti na kukaa. Maana kulikuwa na "LIVE BAND" kutoka kwenye bendi maarufu ya "DJAAKA BAND".
Hiyo ni bendi ya muziki ya vijana wa Jimboni hapo hapo la Sofala. Bendi hiyo iliwahi kushinda tuzo ya "Crossroads in Southern Africa mwaka 2001. Watu walijaa pomoni kuja kuwaona vijana wao wakiwa wamerudi toka ziara za kimuziki nchi za ng'ambo za Uholanzi na Denmark ambapo walikuwa wamekaa huko zaidi ya mwezi mmoja huko Ughaibuni.
Alipotulia kwenye kiti akaja dada mmoja mrefu kavalia sare ambazo zilikuwa zinamtambulisha kuwa ni mhudumu wa hapo akiwa ameshika karatasi ngumu ya "MENU za aina na bei za vyakula na vinywaji" alipofika karibu na Komandoo mstaafu akamsalimia kwa unyenyekevu kisha akamkaribisha na kumpa Komandoo Jacob Steven (JS) ile karatasi ya orodha ya vinywaji na vyakula.
Komandoo akaipokea na kuisoma kimya kimya kisha akamwambia mhudumu "Naomba uniletee "Limoncello" ya baridi sana na maji ya moto ya kuzimulia tafadhali" alisisitiza Komandoo Jacob.
"Limoncello" kilikuwa ni kinywaji kimachotengenezwa kwa kutumia ndimu. Asili yake kinywaji hiki ni Italia ya kusini. Yule mhudumu akawa anaondoka kuelekea kaunta huku anatembea kwa madahiro huku anatikisa makalio yake kiufundi anayapandisha juu na kuyashusha kwa kuyapishanisha. Lakini madahiro hayo hayakumzuzua komandoo 'JS' alishazoea kukutana na vishawishi vya warembo mbalimbali tena wa nchi mbalimbali duniani. Akili yake ilikuwa inawaza kazi tu kwa sasa sio kitu kingine alitambua mshika mawili moja humponyoka.
Baada ya dakika kama tano, yule mhudumu akawa amesharudi mezani kwa Komandoo Jacob, wakati yule mhudumu anasaidia kumfungulia kinywaji komandoo ghafla umati wa watu wakawa wanashangilia kwa nderemo na vifijo huku macho yao yanaelekea mlango wa kuingilia. Kulikuwa na kipande cha mtu kibushuti mfupi kanyoa upara kichwani anatembea mguu mmoja kama mfupi huku amevaa miwani nyeusi, na pembezoni ana wapambe kama wawili wamenyoa nywele zao katika mtindo wa kishungi wanamsindikiza. Miondoko yao ilitambulisha kuwa ni watu mafedhuri na wajuba.
Huyu jamaa ndio yule aliyemtesa Kachero Manu katika handaki la mateso la "Gongorosa Camp" siku ya kwanza alivyopelekwa. Wakapita jirani kabisa na meza ya Komandoo Jacob kisha wakasogea jirani na meza ya kaunta ya "Pub".
Walipopita tu Komandoo Jacob akapatwa na hisia hawa ni mabaradhuli wa tabia sio watu wazuri hata kidogo. Akakata shauri amuulize yule dada mhudumu, "samahani mwanangu huyu ni nani aliyeingia hapa hivi sasa, naona watu wanashangilia kama mpira". Akaongea kwa sauti ya kumnong'oneza yule mhudumu.
"Babu wewe ni mgeni kumbee, yatakukuta mambo usiingie ngomani ukashindwa kuicheza bure, huyo ndio "Bob Chinanga" tunaskia tu ni Bosi wa kambi inayosemekana ni ya Usalama wa Taifa, anaogopwa zaidi ya kifo kinavyoogopwa hapa Sofala..!". Kisha haraka haraka akaondoka yule mhudumu kwa mwendo wa madaha akiwafuata wateja wengine aweze kuwahudumia.
Komandoo 'JS' akawa anaendelea kunywa kinywaji chake huku anafuatilia nyendo za yule "Bob-Chinanga", jitu katili lenye kuogopwa. Wakati muziki wa bendi unazidi kupamba moto, akamuona yule "Bob Chinanga anaelekea stejini kuwatunza pesa wanamuziki wa bendi huku wanamtaja taja jina na kumsifia sifia maneno ya kumpamba kama vile "Boob-Chinanga baba ya mapesa mengi, mlezi wa wana" na maneno kedekede ya kumsifu na kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa, ili mradi wamle pesa zake.
Alikuwa anawapa pesa za kigeni mfano wa dola au paundi maana stejini kulikuwa na mwanga khafifu. Kilichomshangaza Komandoo Jacob no kumuuona yupo peke yake wale wapambe wake wawili hawapo.
Akajiuliza wameenda wapi, kengele ya tahadhari ikagonga kichwani mwake akahisi kuna jambo wanafanya wale wapambe wake. Alipotupa macho kwenye meza waliyokuwa wamekaa hakuona mtu zaidi ya msitu wa bia zilizoachwa bila kuwa na mnywaji. Machale yakamcheza akaamua anyanyuke aende chooni huenda atakutana nao huko halafu atajua mbivu na mbichi wakikutana huko huko. Akanyanyuka kuelekea uelekeo wa chooni, huku akiiweka vizuri bastola yake yenye kiwambo cha kuzuia sauti.
Alipofika karibu na vyoo vya wanawake akasita kidogo kwenda, akawa anasikia kama kuna sauti ya kike inalalamika kwa maumivu makali. Akaichomoa kiunoni bastola yake tayari kwa matumizi itakapobidi. Akaanza kujongea taratibu akawa sasa amekaribia kabisa anaskia sauti ya mtu anayeugulia maumivu. "Naku....f...waaaa nisa..i... di... eeee...!" akakaza mwendo kusogelea inapotokea ile sauti.
Lahaula! alitanabahi kuwa yule dada mhudumu wa "Pub" aliyempa huduma ya kinywaji amechomwa kisu cha kwenye titi la kushoto, kimepenya kisawa sawa chini ya ziwa huku damu zinachuruzika kama bomba la maji la DAWASCO lililopasuka mtaani kutokana na shinikizo kubwa la maji. Akamfikia akamshika kichwani kwenye nywele zake na kuanza kumhoji.
"Umepatwa na nini mwanangu..nani kakufanyia unyama huu..."?. Akajibu yule dada kwa tabu sana huku pumzi zake za kuokoteza okoteza, "wame... n.. i...uaaa wame....ni...uli... zaaa we... we ni nanii...na nimeku....ku.... a.. mbi... a nii...ni, niokooooee pliiz". Komandoo Jacob Steven akapatwa na taharuki akajua hapa akijifanya msamaria mwema itakula kwake, atashushiwa jumba bovu la mauaji, akaondoka kama mwehu anarudi ukumbini kuwatafuta wale wapambe wa Bob Chinanga akimuacha yule dada anapigania roho yake.
Akakuta meza yao ipo tupu hawapo wameshasepa na hata Bob Chinanga mwenyewe karibu na pale stejini anapowatazama waimbaji hayupo. Haraka haraka akatoka nje ya lango la kuegesha magari, akaona kwa mbele yake kuna gari limewasha indiketa linataka kuondoka huku Bob Chinanga ndio anafungua mlango wa nyuma kuingia kwenye gari huku mkononi ameshika chupa yake ya pombe kali.
Hapo hapo akajikuta anapigiwa honi na gari aina ya "Range Rover" rangi nyeusi inataka kuegeshwa pale aliposimama Komandoo Jacob. Akili ya Komandoo ikachemka haraka haraka akaona fursa imejitokeza katika wakati muafaka, hakuondoka akazidi kulisogelea lile gari kisha ghafla akashtuka pembeni mwa upande wa mlango wa dereva, hapo hapo dereva akashusha kioo chake kisha akaanza kuporomosha bomba la matusi akamnyambua komandoo "JS" kwa kadri alivyoweza.
Komandoo Jacob hakuwa na muda wa kujibizana nae alimpa kisogo, alichofanya ni kuchomoa bastola yake na kumuamrisha yule dereva, "shuka chini haraka sana usilete utani na wanaume wakiwa kazini" alisema Komandoo Jacob huku anatishia kama anaweka sawa bastola yake kufyatua risasi. Bila ubishi yule baba cha matusi, akawa amegwaya akafungua mlango wake wa dereva. Alikuwa mpole ghafla kama "Mmasai anayesifika ushujaa wa kuua simba lakini anaogopa kula samaki eti macho ya samaki yanamtisha".
Aliposhuka tu kwenye gari yule jamaa, kufumba na kufumbua Komandoo Jacob akaingia kwenye gari na kuligeuza kuelekea uelekeo wa inapoelekea gari ya akina Bob Chinanga. Akaanza kuwakimbiza wabaya wake akina Bob Chinanga, akiwa ndani ya "Range Rover" huku wanatokomea nje ya Mji. Akimuacha yule baba wa kuporomosha matusi akiwa mikono kaweka kichwani, ametaharuki nusu majinuni hajui afanye kitu gani kuipata gari yake tena.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
CABO-DELGADO-PART 29
Akakaa kitambo kifupi akifikiria mbinu nyingine ya kufanya, akaamua aanze kuvingirika kuelekea kwenye pipa la takataka. Matarajio yake huko yalikuwa huenda akakuta mkasi umetupwa ili ukiwepo aubane kwenye meno kisha autumie kukatia kamba ya mikononi. Akajipa matumaini atapata kifaa cha kujifungua.
"Kwa namna Dr.Anabella alivyokuwa anatupa kitu kwenye pipa, alivyoniangalia sana ile ni ishara kuna kitu cha kuniokoa aliniwekea" mawazo chanya yalipita kwenye fikra zake. Akaanza kujisogeza huku jasho linamtiririka mwilini kama maji kutokana na joto la mule selo.
Alipokuwa yupo karibu na nusu kufikia kwenye pipa la taka, ghafla akasikia vishindo vya mabaradhuli wanakuja selo kuu, hapo hapo akaanza kukata tamaa ya kutoroka akajua amekwisha wanakuja kumchukua. "Lakini mbona mapema sana wanakuja kunichukua kulikoni!" aliwaza sana Kachero Manu. Akaanza kusali sala maarufu kwa Wakatoliki, ya Baba yetu wa mbinguni akijua hapa tena hana ujanja alishakubali shingo upande kushindwa na maadui zake. Wakati amefunga macho yako yuko katika hisia nzito ghafla lango likafunguliwa wakaingia mabaradhuli wawili wapya ambao hawafahamu wakiwa wamembeba mzobe mzobe mtu mmoja.
Alikuwa ni shaibu wa makamo hakosi miaka 55 kwenda juu ukimkadiria. Alikuwa kirambi cha mtu, mfupi kama mbirikimo ana tumbo kubwa ambalo linatokana na ulaji mbovu wa vyakula na uvivu wa mazoezi na kujisaidia haja kubwa mara kwa mara. Cha kusikitisha huyu Mzee alikuwa yupo uchi wa mnyama analia kwa sauti mbaya kama ya punda kilongwe wa majumbani. Alitoa kilio mpaka sauti yake ikampwelea kabisa.
Walipoingia wale mabaradhuli hawakumjali kabisa Kachero Manu ambaye alijikunyata na kujifanya tongo hajui chochote kinachoendelea. Wakamfunga juu kwa juu yule Mzee kama nyama ya mbuzi wa ndafu anayesubiri kuliwa na maharusi. Mzee wa watu ukawa inamtoka mikojo ya uoga mfululizo utasema anaumwa ugonjwa wa kisukari hawezi kujizuia mkojo, au anaumwa ugonjwa unaoitwa nasuri uwapatao akina mama waliotoboka tundu la mkojo maarufu mtaani kama fisitula.
Kumbe kihoro chake ni cha uoga wa kifo cha kishenzi na cha kidhalili ugenini. Kachero Manu akawa anajichekea kimoyo moyo kuwa huyu Mzee atakuwa yupo ndani ya kumi bora ya watu waoga duniani. Kisha walivyomfunga wakamuacha anabembea huku kichwa kinaning'inia halafu wakafunga mlango na kuondoka. Mzee uso wake ulivimba vimba kidogo ulikuwa na manundu, inaonyesha alikuwa kuna kitu anakaidi kutekeleza wakamnasa mambata ya haja ya usoni. Na mdomo wa chini ulipasuka kidogo ukawa unamwaga damu.
Kachero Manu akavuta taswira ya huyu Mzee, akili yake ikamwambia kuwa anamfahamu vilivyo tena anamjua sana na ni mtu maarufu ila tu kupondeka kwa sura yake ikawa sura inaingia na kuondoka. Mwishowe Kachero Manu akaanza kuangua kicheko cha sauti kubwa na dharau mpaka Mzee wa watu akaanza kuogopa kuwa huenda kaletwa gereza la vichaa.
"Kumbe ni Mzee Andenga Kazimoto, kaletwa selo kuu, kazi ipo mwaka huu" alijiwazia baada ya kumtambua. Waswahili walisema "shukrani ya punda ni mateke. Amekipata alichokitafuta kwa mafia Alfredo. Inaonyesha Alfredo kaona hana umuhimu wa kuingia kwenye kikao wakati nyaraka wameshazipata" akazidi kuwaza Kachero Manu.
Kweli tamaa ilimuua fisi, 'kakosa mwana na maji ya moto'. Maana kwa Cheo cha huyu Mzee Andenga, alikuwa amebakiza miaka michache ya kustaafu angepata kiinua mgongo na pensheni nzuri tu ya kula na familia yake mpaka mwisho wa uhai wake.
"Komandoo Mstaafu uso kwa uso na NACATANAS"
Komandoo mstaafu Jacob Steven (JS) alipofanikiwa kugundua gari lililowapeleka akina Kachero Manu 'Gorongosa Camp', akaenda moja kwa moja kwenye kampuni ya helikopta ya kukodisha ili aelekee Gongorosa kumkomboa kijana wake.
Masaa matatu tu ya kufa au kupona yalikuwa yamebaki kabla ya Kachero Manu kuletwa kiwanda cha Korosho cha Monte Branco Ltd. Ilitakiwa komandoo 'JS' atumie 'kipawa cha liwa kutibu harara', afanye vyovyote iwavyo amnasue kijana wake. Kama angekwenda na gari asingeweza kufika wakati muafaka wa kuweza kumuokoa.
Umbali wa kutoka Pemba mpaka Gongorosa ni kama kutoka Dar esalaam mpaka Mbeya kwenda na kurudi. Eneo la Gongorosa lipo jimbo la kati la Sofala zaidi ya kilometa 1635.
Bahati nzuri akapata nafasi kwenye helikopta hiyo ya kukodi inayoelekea "Gongorosa National Park" (GNP) inayopeleka watalii mbugani. Mpaka saa 11 jioni akawa ameshawasili Gongorosa. Sasa kilichokuwa kinachomsumbua kichwani mwake ni kufahamu Kachero Manu kafichwa wapi?. Maana ni sawa na mwenyeji wako akuambie nipo Dar es salaam, lakini Sinza, Manzese, Mbagala, Kawe, Goba, Mbezi, Rehema, Masaki zote ni Dar es Salaam. Lakini bado hata ukifahamu ni Sinza bado Sinza ni kubwa sana, Kwa Remmy, Kumekucha, Palestina, Madukani, Shekilango bado vyote hivyo ni vitongoji vya Sinza.
Akaumiza kichwa akapata jawabu ni kuuliza wapi kuna Ukumbi wa starehe maarufu kuliko zote, huko ndio atapata majibu. Maana haiwezekani viongozi wa Gorongosa Camp wanaolipwa pesa nzuri sana washindwe kustarehe. Tabia za watu majambazi na maharamia ni kustarehe sana, ndio maana pesa wanazopata hazina fidi. Ukitaka kumsaka mtu swalihina basi ni kwenye nyumba ya ibada, lakini mtu fedhuli pesa zake huwa zinaishia kwenye pombe, muziki na kustarehe na vidosho.
Akauliza uliza kwa wenyeji klabu za fauka kwa starehe, wengi wao walimtajia kiwanja cha kisasa cha kujivinjari ukiwa Gongorosa kinaitwa "Montebelo Pub". Akafanikiwa kufika "Montebelo Pub" anayasoma mazingira.
Ilikuwa ni "Pub" yenye kuvutia kimazingira, ilijengwa ikajengeka vilivyo. Geti la kuingilia lilipambwa na bango kubwa lenye maandishi makubwa lililoandikwa jina la "Montebelo Pub". Kisha ilizungukwa na fensi fupi ya ukuta iliyopandwa miti iliyoshonana kuzunguka ukuta wote. Kwa ndani kulikuwa na midule mingi mingi iliyozungukwa ukumbi mzima kwa umbo la duara huku katikati kukiwa na ukumbi wa wazi uliozibwa kwa paa la makuti yanayotokana na mti wa mnazi.
Pia kulikuwa na wahudumu ambao ni wasichana wabichi na vipusa ambao wengi wao wapo katika rika la kufanana la kuanzia miaka 20 mpaka 25 wakiwa wamevalia mavazi yao ya sare za minisketi zenye kuacha sehemu kubwa ya mapaja yao nje nje bila kufunikwa vizuri, juu wana fulana nyeupe zilizowabana na kuzichongoa vilivyo chuchu zao konzi.
Alipoingia alikuta nje kuna magari mengi ya kifahari yameegeshwa kwenye maegesho kuonyesha kuwa ni "Pub" ya watu wazito wa Mji. Alipofika akachagua meza iliyokaribu na ukumbi wa kutumbuizia akavuta kiti na kukaa. Maana kulikuwa na "LIVE BAND" kutoka kwenye bendi maarufu ya "DJAAKA BAND".
Hiyo ni bendi ya muziki ya vijana wa Jimboni hapo hapo la Sofala. Bendi hiyo iliwahi kushinda tuzo ya "Crossroads in Southern Africa mwaka 2001. Watu walijaa pomoni kuja kuwaona vijana wao wakiwa wamerudi toka ziara za kimuziki nchi za ng'ambo za Uholanzi na Denmark ambapo walikuwa wamekaa huko zaidi ya mwezi mmoja huko Ughaibuni.
Alipotulia kwenye kiti akaja dada mmoja mrefu kavalia sare ambazo zilikuwa zinamtambulisha kuwa ni mhudumu wa hapo akiwa ameshika karatasi ngumu ya "MENU za aina na bei za vyakula na vinywaji" alipofika karibu na Komandoo mstaafu akamsalimia kwa unyenyekevu kisha akamkaribisha na kumpa Komandoo Jacob Steven (JS) ile karatasi ya orodha ya vinywaji na vyakula.
Komandoo akaipokea na kuisoma kimya kimya kisha akamwambia mhudumu "Naomba uniletee "Limoncello" ya baridi sana na maji ya moto ya kuzimulia tafadhali" alisisitiza Komandoo Jacob.
"Limoncello" kilikuwa ni kinywaji kimachotengenezwa kwa kutumia ndimu. Asili yake kinywaji hiki ni Italia ya kusini. Yule mhudumu akawa anaondoka kuelekea kaunta huku anatembea kwa madahiro huku anatikisa makalio yake kiufundi anayapandisha juu na kuyashusha kwa kuyapishanisha. Lakini madahiro hayo hayakumzuzua komandoo 'JS' alishazoea kukutana na vishawishi vya warembo mbalimbali tena wa nchi mbalimbali duniani. Akili yake ilikuwa inawaza kazi tu kwa sasa sio kitu kingine alitambua mshika mawili moja humponyoka.
Baada ya dakika kama tano, yule mhudumu akawa amesharudi mezani kwa Komandoo Jacob, wakati yule mhudumu anasaidia kumfungulia kinywaji komandoo ghafla umati wa watu wakawa wanashangilia kwa nderemo na vifijo huku macho yao yanaelekea mlango wa kuingilia. Kulikuwa na kipande cha mtu kibushuti mfupi kanyoa upara kichwani anatembea mguu mmoja kama mfupi huku amevaa miwani nyeusi, na pembezoni ana wapambe kama wawili wamenyoa nywele zao katika mtindo wa kishungi wanamsindikiza. Miondoko yao ilitambulisha kuwa ni watu mafedhuri na wajuba.
Huyu jamaa ndio yule aliyemtesa Kachero Manu katika handaki la mateso la "Gongorosa Camp" siku ya kwanza alivyopelekwa. Wakapita jirani kabisa na meza ya Komandoo Jacob kisha wakasogea jirani na meza ya kaunta ya "Pub".
Walipopita tu Komandoo Jacob akapatwa na hisia hawa ni mabaradhuli wa tabia sio watu wazuri hata kidogo. Akakata shauri amuulize yule dada mhudumu, "samahani mwanangu huyu ni nani aliyeingia hapa hivi sasa, naona watu wanashangilia kama mpira". Akaongea kwa sauti ya kumnong'oneza yule mhudumu.
"Babu wewe ni mgeni kumbee, yatakukuta mambo usiingie ngomani ukashindwa kuicheza bure, huyo ndio "Bob Chinanga" tunaskia tu ni Bosi wa kambi inayosemekana ni ya Usalama wa Taifa, anaogopwa zaidi ya kifo kinavyoogopwa hapa Sofala..!". Kisha haraka haraka akaondoka yule mhudumu kwa mwendo wa madaha akiwafuata wateja wengine aweze kuwahudumia.
Komandoo 'JS' akawa anaendelea kunywa kinywaji chake huku anafuatilia nyendo za yule "Bob-Chinanga", jitu katili lenye kuogopwa. Wakati muziki wa bendi unazidi kupamba moto, akamuona yule "Bob Chinanga anaelekea stejini kuwatunza pesa wanamuziki wa bendi huku wanamtaja taja jina na kumsifia sifia maneno ya kumpamba kama vile "Boob-Chinanga baba ya mapesa mengi, mlezi wa wana" na maneno kedekede ya kumsifu na kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa, ili mradi wamle pesa zake.
Alikuwa anawapa pesa za kigeni mfano wa dola au paundi maana stejini kulikuwa na mwanga khafifu. Kilichomshangaza Komandoo Jacob no kumuuona yupo peke yake wale wapambe wake wawili hawapo.
Akajiuliza wameenda wapi, kengele ya tahadhari ikagonga kichwani mwake akahisi kuna jambo wanafanya wale wapambe wake. Alipotupa macho kwenye meza waliyokuwa wamekaa hakuona mtu zaidi ya msitu wa bia zilizoachwa bila kuwa na mnywaji. Machale yakamcheza akaamua anyanyuke aende chooni huenda atakutana nao huko halafu atajua mbivu na mbichi wakikutana huko huko. Akanyanyuka kuelekea uelekeo wa chooni, huku akiiweka vizuri bastola yake yenye kiwambo cha kuzuia sauti.
Alipofika karibu na vyoo vya wanawake akasita kidogo kwenda, akawa anasikia kama kuna sauti ya kike inalalamika kwa maumivu makali. Akaichomoa kiunoni bastola yake tayari kwa matumizi itakapobidi. Akaanza kujongea taratibu akawa sasa amekaribia kabisa anaskia sauti ya mtu anayeugulia maumivu. "Naku....f...waaaa nisa..i... di... eeee...!" akakaza mwendo kusogelea inapotokea ile sauti.
Lahaula! alitanabahi kuwa yule dada mhudumu wa "Pub" aliyempa huduma ya kinywaji amechomwa kisu cha kwenye titi la kushoto, kimepenya kisawa sawa chini ya ziwa huku damu zinachuruzika kama bomba la maji la DAWASCO lililopasuka mtaani kutokana na shinikizo kubwa la maji. Akamfikia akamshika kichwani kwenye nywele zake na kuanza kumhoji.
"Umepatwa na nini mwanangu..nani kakufanyia unyama huu..."?. Akajibu yule dada kwa tabu sana huku pumzi zake za kuokoteza okoteza, "wame... n.. i...uaaa wame....ni...uli... zaaa we... we ni nanii...na nimeku....ku.... a.. mbi... a nii...ni, niokooooee pliiz". Komandoo Jacob Steven akapatwa na taharuki akajua hapa akijifanya msamaria mwema itakula kwake, atashushiwa jumba bovu la mauaji, akaondoka kama mwehu anarudi ukumbini kuwatafuta wale wapambe wa Bob Chinanga akimuacha yule dada anapigania roho yake.
Akakuta meza yao ipo tupu hawapo wameshasepa na hata Bob Chinanga mwenyewe karibu na pale stejini anapowatazama waimbaji hayupo. Haraka haraka akatoka nje ya lango la kuegesha magari, akaona kwa mbele yake kuna gari limewasha indiketa linataka kuondoka huku Bob Chinanga ndio anafungua mlango wa nyuma kuingia kwenye gari huku mkononi ameshika chupa yake ya pombe kali.
Hapo hapo akajikuta anapigiwa honi na gari aina ya "Range Rover" rangi nyeusi inataka kuegeshwa pale aliposimama Komandoo Jacob. Akili ya Komandoo ikachemka haraka haraka akaona fursa imejitokeza katika wakati muafaka, hakuondoka akazidi kulisogelea lile gari kisha ghafla akashtuka pembeni mwa upande wa mlango wa dereva, hapo hapo dereva akashusha kioo chake kisha akaanza kuporomosha bomba la matusi akamnyambua komandoo "JS" kwa kadri alivyoweza.
Komandoo Jacob hakuwa na muda wa kujibizana nae alimpa kisogo, alichofanya ni kuchomoa bastola yake na kumuamrisha yule dereva, "shuka chini haraka sana usilete utani na wanaume wakiwa kazini" alisema Komandoo Jacob huku anatishia kama anaweka sawa bastola yake kufyatua risasi. Bila ubishi yule baba cha matusi, akawa amegwaya akafungua mlango wake wa dereva. Alikuwa mpole ghafla kama "Mmasai anayesifika ushujaa wa kuua simba lakini anaogopa kula samaki eti macho ya samaki yanamtisha".
Aliposhuka tu kwenye gari yule jamaa, kufumba na kufumbua Komandoo Jacob akaingia kwenye gari na kuligeuza kuelekea uelekeo wa inapoelekea gari ya akina Bob Chinanga. Akaanza kuwakimbiza wabaya wake akina Bob Chinanga, akiwa ndani ya "Range Rover" huku wanatokomea nje ya Mji. Akimuacha yule baba wa kuporomosha matusi akiwa mikono kaweka kichwani, ametaharuki nusu majinuni hajui afanye kitu gani kuipata gari yake tena.



Sent using Jamii Forums mobile app
safi sana
 
CABO-DELGADO-PART 30

Hapo hapo akajikuta anapigiwa honi na gari aina ya "Range Rover" rangi nyeusi inataka kuegeshwa pale aliposimama Komandoo Jacob. Akili ya Komandoo ikachemka haraka haraka akaona fursa imejitokeza katika wakati muafaka, hakuondoka akazidi kulisogelea lile gari kisha ghafla akashtuka pembeni mwa upande wa mlango wa dereva, hapo hapo dereva akashusha kioo chake kisha akaanza kuporomosha bomba la matusi akamnyambua komandoo "JS" kwa kadri alivyoweza.
Komandoo Jacob hakuwa na muda wa kujibizana nae alimpa kisogo, alichofanya ni kuchomoa bastola yake na kumuamrisha yule dereva, "shuka chini haraka sana usilete utani na wanaume wakiwa kazini" alisema Komandoo Jacob huku anatishia kama anaweka sawa bastola yake kufyatua risasi. Bila ubishi yule baba cha matusi, akawa amegwaya akafungua mlango wake wa dereva. Alikuwa mpole ghafla kama "Mmasai anayesifika ushujaa wa kuua simba lakini anaogopa kula samaki eti macho ya samaki yanamtisha".
Aliposhuka tu kwenye gari yule jamaa, kufumba na kufumbua Komandoo Jacob akaingia kwenye gari na kuligeuza kuelekea uelekeo wa inapoelekea gari ya akina Bob Chinanga. Akaanza kuwakimbiza wabaya wake akina Bob Chinanga, akiwa ndani ya "Range Rover" huku wanatokomea nje ya Mji. Akimuacha yule baba wa kuporomosha matusi akiwa mikono kaweka kichwani, ametaharuki nusu majinuni hajui afanye kitu gani kuipata gari yake tena.
Bob Chinanga na mabaradhuli wenzake walifanikiwa kupandikiza uoga katika nyoyo za raia wa maeneo yote ya Gorongosa. Walikuwa wanajitangaza kuwa wao ni wasimamizi wa kambi ya usalama wa taifa kwa watu wanaotishia maslahi ya nchi ndio huletwa kwao. Ilikuwa mgeni yoyote akifika Gorongosa maeneo ya karibu na kambi yao lazima wapewe taarifa na kama usipotoa taarifa basi wanakupa tiketi ya kuelekea kaburini.
Makondakta wa daladala za Mji, Wapiga kiwi viatu, Wauza magazeti, Wahudumu wa baa, Machinga wa bidhaa mitaani wote walikuwa ni "askari vidole wao", wakipata taarifa tu wanaifikisha kwa mawakala wao akina Bob Chinanga wanalipwa chao.
Sasa Komandoo Jacob Steven alivyokuwa pale "Pub" wakati anaongea na mhudumu wa "Pub", meza ya nyuma yake kulikuwa na muuza vitu vidogo vidogo anayetembeza kwenye kadamnasi ya watu akawa anaskiliza mazungumzo yao. Alivyonasa kila nukta ya mazungumzo yao haraka akapeleka taarifa kwa wakala wake ndio habari zilivyofika kwa wapambe wa Bob Chinanga.
Bila kuchelewesha wakamvutia chooni yule mhudumu na kumhoji kwanini hakutoa taarifa za yule Mzee aliyemuuliza habari za Bob-chinanga, hivyo adhabu yake ya usaliti ni kisu cha chini ya ziwa. Na kwa kuwa muda wa kumpeleka Kachero Manu kwenye mkutano ulikuwa umekaribia wakaona hawana muda wa kumkamata na kumhoji Komandoo Jacob Steven.
Walifahamu akipata taarifa za mauaji ya mhudumu aliyeongea nae zitakuwa ni salamu kwake hivyo atapatwa na uoga na hata kama alikuwa na nia ya kuwafuatilia atasitisha mipango yake. Ndio maana walipofanya mauaji wakatokomea kambini tayari kumsafirisha Kachero Manu kwa helikopta.

Kachero Manu ushindi unanukia kwake
Baada ya kuachwa mule selo kuu Kachero Manu saa kadhaa akiwa na sanjali wake msaliti Meneja Andenga Kazimoto. Kachero Manu akaachana na vilio vya Bwana Andenga akaanza kupanga mikakati upya ya kujiokoa.
Akafahamu mlango wa selo ukifunguliwa tena kwa mara ingine ni kuja kutolewa yeye kwa ajili ya kupelekwa mbele ya Mafioso wenye kiu ya damu za watu na pesa. Akajongea kwa bidii mpaka akalifikia pipa la taka la bati lililokuwa lina kutu kutu. Alipofika akalichota mtama kwa miguu yake yote miwili iliyofungwa lile pipa likaanguka chini na kumwaga vitu chini, mwaaaaah.
Akatawanya tawanya kwa kusasambua vitu vilivyomo kwa mikono yake miwili iliyofungwa. Kwa bahati mbaya hakuona chochote chenye uwezo wa kukata kamba ya mikononi mwake. Kijasho chembamba cha mpaka kwenye meno kilianza kumvuja. Kwa mara ya kwanza katika maisha yake Kachero Manu akaingiwa na hofu ya kifo.
Baada ya kuchemsha ubongo wake kwa dakika kadhaa akapata wazo jipya la kulifanyia kazi, akapiga moyo konde, akaanza kubiringika kuelekea kwenye ile meza chakavu iliyowekwa kurunzi ya karabai ya kutumia mafuta ya taa. Alipoikaribia meza hiyo, akaiona taa yake inaanza kuripuka ripuka dalili ya uchache wa mafuta ndani yake. Akajifikiria tena kama dakika 3, akapata wazo jipya la la kuyafuata mabaki ya pamba zilizotumika kwenye pipa la taka aliloliangusha. Kisha akiyapata aje nayo karibu na meza afu aifyatue meza ile kurunzi ikianguka chini kioo kikipasuka ule moto wake ukichanganyika na mafuta ya taa pamoja na pamba moto utawaka ndani ya selo halafu ukiwaka atatumia moto kuunguza kamba za mikononi. Akatabasamu kwa namna alivyopanga na kupangua mpaka amepata mbinu yenye matumaini kwake ya kujiokoa.
Akabiringika kwa kasi ya matumaini mapya ndani ya moyo wake ya kuokoka. Alipolifikia pipa la taka, akabana lundo la pamba chafu kwa kutumia mdomo wake kutoka kwenye takataka zilizotawanyika chini. Ilikuwa inahitaji uvumilivu maana ya pamba zilikuwa zinatoa harufu ya uvundo unaotokana na usaha wa kwenye vidonda vya mateka. Akavumilia kubana zile pamba mdomoni huku anasota mpaka akazifikisha salama chini ya meza ile yenye kurunzi. Sasa ikabaki pata potea ya mwishoni ya kuiangusha kurunzi ili ilipuke. Bahati nasibu ambayo kama akishindwa kuzichanga vyema karata zake, itakuwa imekula kwake kimoja.
Akavuta pumzi ndefu ndani kwa nguvu, akasali kimoyomoyo kisha akahesabu moja, mbili, tatu...kisha akaivuta ile meza kwa miguu yake, kurunzi ikaanguka chini ule msukumo wa mafuta ya taa ukasababisha mlipuko mkubwa ambao ukadaka zile pamba mlipuko ukazidi. Haraka haraka akasogeza mikono yake kwenye muwako ule. Zikaanza kuungua zile kamba za mikononi, maumivu yalikuwa makali sana kwa sababu ni kamba za plastiki hivyo zilikuwa zinaganda kwenye mikono lakini akawa anajitahidi kuzichambua huku amekaza roho yake kwa ujasiri mkubwa. Baada ya muda mfupi akafanikiwa kuifungua mikono yake na kamba.
Hima hima akaanza kujifungua kamba za miguuni, ili awe huru asilimia 100%. Yule msaliti bwana Andenga alikuwa ametumbua macho kama maiti iliyowekwa kwenye barafu akisubiri wazishi wake, huku anaangalia maajabu tu aliyokuwa anasoma kwenye vitabu vya riwaya na kuangalia kwenye filamu za maajabu ya Makomandoo. Lakini leo hii ndio kashuhudia mubashara bila chenga namna Komandoo alivyokuwa anaungua mikono bila hata kupiga kelele utasema ameng'atwa na mbu.
Kachero Manu akampuuza Bwana Andenga akaelekea tena kwenye pipa la taka akaanza kupekua pekua tena huenda akapata kitu cha kumsaidia. Imani yake ilikuwa bado inamtuma lazima Dr.Anabella afanye jambo la kumsaidia kutokana na shuhuda aliyopata toka kwa marehemu koplo Hamduni. Na pia Dr.Anabella mara ya mwisho alitupa kitu kwenye pipa la taka na alimtazama sana, hivyo lazima afuatilie hisia zake. Alivyopekua pekua akaanza kukata tamaa, maana takataka zilikuwa nyingi na mwangaza ulianza kuzidi kuwa khafifu kutokana na kuvunjwa kwa kurunzi na vidirisha kuwa viko juu sana. Wakati amekata shauri aachane na kuchakua chakua takataka ghafla akashika kitu kigumu kama chuma kimevirigiwa karatasi na mfuko wa plastiki.
Haraka haraka akaifungua ile plastiki akakutana na funguo tatu zilizochongwa na karatasi kubwa nyeupe ina michoro ya ramani ambayo haionekani vizuri kutokana na kagiza giza cha selo kilichoanza kushamiri. Akaamua kwenda kuchukua moja ya jeneza lililomo kwenye kile chumba akalisimamisha kiurefu. Kisha akaliparamia kama nyani mpaka juu kisha akarukia kwenye kidirisha akawa ananing'nia kwa mkono mmoja huku mkono mwingine ameshika ramani akaanza kuipitia kwa umakini mkubwa. Ilimchukua takribani dakika 20 tu kuielewa kuwa kuikariri ramani ya jengo zima la "Gorongosa Camp". Baada ya kumaliza kuisoma akatikisa kichwa na kumshukuru sana Dr.Anabella, maana bila ramani ile angetumia muda wa chini hata siku tatu ndio angetoka, lakini kupitia ramani ile alishazigundua njia za panya za kutoroka kwa haraka. Kwa kutumia ramani alikuwa na uhakika wa kutoka na kuwahi kikao kule kiwanda cha korosho kwa gharama yoyote.
Akaporomoka mpaka chini akachanachana ile ramani akaitafuna na kuimeza kama tonge la ugali ili kupoteza ushahidi na akaanza kusaka nguo ya kujisitiri kama atapata. Akakosa akaenda kwenye kile kitanda kupumzisha mgongo akiwasubiri waje awachakaze.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom