Riwaya: "Cabo-delgado"-part 01

Riwaya: "Cabo-delgado"-part 01

CABO-DELGADO-PART 40


Komandoo "JS" alipotoka nje akaelekea kule alikoelekezwa na Dr.Anabella kwenye maegesho ya chini kwa chini ya magari. Ilionekana hamna njia ingine ya kutokea kule kwenye handaki isipokuwa kwenye maegesho haya.
Akawa anatambaa chini kwa chini kuelekea kule kwenye magari ya thamani kubwa ambapo alihisi gari mojawapo ni la Bwana Alfredo. Ghafla mvua ya risasi ikaanza kumfuata, salama yake kulikuwa na kigiza giza hivyo walengaji wakawa wanakosa risasi akabingirika mpaka akafanikiwa kuingia chini ya uvungu wa gari.
Kisha akapata wazo la kuwachanganya, akatoa rimoti kama saa mfukoni mwake, akabonyeza bonyeza vitufe vyake. Ghafla bin vuu mabomu aliyotega nje ya ukuta wa jengo la kiwanda yakanza kulipuka. Mbinu ambayo ilifanikiwa wale washambuliaji wake wakawa wanakimbizana kuokoa maisha yao, wengine walitupa mpaka silaha zao.
Bwana Alfredo nae akatimka mbio na faili lake mkononi na bastola akitokea kwenye karakana alikokuwa amejichimbia kwenye mashine mbovu na kukimbilia kuingia kwenye gari lile lile ambalo chini yake kuna Komandoo "JS".
Komandoo akawa anatambaa chini ya chasesi ya gari alipofika mwishoni kwenye buti gari ikaanza kuondoka. Komandoo "JS" akafanikisha kushika chuma cha kingo za nyuma kinacholinda gari na ajali akawa anaburutwa chini lakini haliachii gari.
Kachero Manu akiwa anatokeza kwenye maegesho akawa anaona gari inakuja usawa wake akarusha risasi moja iliyotua kwenye tairi la kushoto la gari ikaanza kuyumba huku tayari Komandoo "JS" yupo juu ya gari kashaipandia anatambaa kwenye bodi ya gari mpaka akafika usawa wa siti ya abiria kiti cha nyuma.
Bwana Alfredo alikuwa ametingwa na kujibizana risasi na Kachero Manu akajisahau kuwa kuna namba ingine chafu sana kuliko hata huyo Kachero Manu nayo inamuwinda imfikishe katika mikono ya sheria.
Alichofanya Komandoo "JS" ni kutoa kioo cha dirisha la gari kwa kutumia pete yake ya almasi aliyovaa mkono wake wa kushoto, kisha akaingia kwenye kupitia dirishani kisha akajikohoza. Bwana Alfredo akageuka, mshtuko alioupata hakuamini mpaka bastola yake ikamponyoka ikaingia chini ya uvungu wa siti ya kiti cha dereva.
Alikuwa haamini anachokia kwenye mboni za macho yake. Akawa anachochea mwendokasi wa gari kuelekea kwenye tanki la mafuta mkabala na geti la kutokea. Akili ya Komandoo "JS" ikausoma mchezo wote kuwa ana lengo la kujitoa mhanga kama magaidi kwa kwenda kulipigiza gari kwenye tanki la kuhifadhia mafuta na kusababisha mlipuko ili wafe wote.
Komandoo "JS" akarukia kiti cha mbele wakawa wanapimana ubavu wa nguvu za mikono kwa kugombaniana usukani wa gari, mpaka walipokaribia meta chache kulifikia tenki la mafuta, Bwana Alfredo akafungua mlango wa dereva na kurusha nje faili lake jeusi kisha yeye mwenyewe kuruka nje ya gari.
Kishindo kikubwa cha mlipuko kilisikika baada ya gari kwenda kujibamiza kwenye tenki na kushika moto. Wakati huo huo gari ya kubeba wagonjwa mahututi na gari za polisi zikawa zimewasili kiwandani.
Dr.Anabella na Komandoo "JS" ambaye nae alifanikiwa kuruka nje ya gari walikuwa wamepoteza fahamu hivyo wakawa wa kwanza kupakizwa na kuwahishwa hospitali kwa matibabu. Bwana Alfredo alikuwa amevunjika kiuno kutokana na risasi tano alizopigwa kiunoni akiwa hewani na Kachero Manu alipokuwa anaruka nje ya gari, akapigwa pingu za mikononi na miguuni tayari kwa safari ya kituo cha polisi. Shughuli yote ya kuwashikisha adabu vibaraka wa wakoloni ilikamilika saa saba kamili usiku.

SURA YA KUMI NA TISA
La Mgambo limelia Ushindi hadharani
Asubuhi ilipambazuka kwa Kachero Manu akiwa amelala katika moja ya hoteli kubwa na ya kifahari inayoitwa "Cardoso" iliyopo Jijini Maputo. Ilikuwa ni hoteli ambayo hawafikii hapo ila watu wenye sharafu na pesa nyingi. Alipelekwa usiku usiku na ndege binafsi ya Rais wa Msumbiji na kupewa ulinzi wenye hadhi ya kibalozi.
Rais wa Msumbiji alikuwa amefurahishwa na ushujaa wa Kachero Manu kwa kufanikiwa kukisambaratisha kikosi cha Mafioso waliokuwa wanachafua jina na hadhi ya Msumbiji kitaifa na kimataifa.
Mafioso ambao kama wangechekewa wangeziingiza kwenye uhusiano tete nchi za Msumbiji na Tanzania na kuvunja misingi ya waasisi wa mataifa hayo.
Hivyo akaagiza Kachero Manu apewe ulinzi mkubwa asije akapata madhara kutoka kwa wanyonya mirija waliobaki kwenye mfumo wa vibaraka walioujenga toka enzi za mapambano ya kudai uhuru wa Msumbiji. Akaenda kuwekwa kwenye hoteli ambayo usingizi wake kwa siku ni zaidi ya milioni mbili kwa pesa za kitanzania.
Aliamshwa Kachero Manu asubuhi hiyo na miale ya jua isiyo na makali iliyokuwa inapenya katika vioo vya dirisha lake ambalo hakufunga pazia lake kutokana na uchovu wa mapambano ya usiku kucha. Alitupa pembeni blangeti lake la kujifunika na baridi akachukua rimoti ya kipoza hewa cha chumba akazima. Kisha akapiga magoti akaanza kusali kumshukuru Mungu kwa kumpa nafasi ingine ya kuwa hai hasa ukichukulia kwenye majukumu haya mazito aliyopewa nchini Msumbiji ndani ya siku kadhaa hizi amechungulia mdomo wa kifo mara nyingi sana kisha anaponea chupuchupu.
Baada ya kumaliza sala fupi akanyanyuka akapiga simu jikoni kuagiza kifungua kinywa, kisha akawasha runinga iliyotundikwa juu katika ukuta wa chumbani kwake, ilikuwa ni saa mbili asubuhi akakutana na taarifa ya habari ya Shirika la Habari la Afrika ya Kusini (SABC). Akawa anajongea mlango wa maliwatoni kwenda kuoga maji ili mwili upate nguvu mpya alipofika mlango wa maliwato kabla hajaingia, akamsikia msomaji wa taarifa ya habari anaelezea habari zilizowafikia hivi punde, akasimama kuangalia hiyo taarifa.
"Kachero bobezi kutokana nchini Tanzania kwa kushirikiana na Komandoo mkongwe wa nchini Msumbiji wamefanikiwa kuwatia mbaroni viongozi wahalifu wa kundi la NACATANAS lililokuwa linaongoza mauaji ya raia wasio na hatia pamoja na uporaji katika machimbo mbalimbali ya madini nchini Msumbiji. Pia jeshi la Msumbiji limefanikiwa usiku wa kuamkia leo kukamata shehena ya madawa ya kulevya na kontena mbili za madini ya rubi ziliyokuwa zimefichwa katika kiwanda cha korosho tayari kwa kusafirishwa nje ya nchi. Pia jeshi la polisi linamshikilia mmiliki wa kampuni ya Monte Branco Ltd Bwana Alfredo kwa tuhuma za kuendesha shughuli mbalimbali haramu nchini Msumbiji ikiwemo kufadhili kikundi cha "NACATANAS", na atapandishwa kizimbani mara tu baada ya upelelezi kukamilika. Pia jeshi la polisi limefanikiwa kunasa majina ya washirika wote wa Bwana Alfredo waliopo serikalini na kwenye taasisi binafsi. Uchunguzi bado unaendelea nao watafikishwa mahakamani mara moja baada ya upelelezi kukamilika. Wakati huo huo Rais wa Msumbiji amemteua ndugu Jacob Steven kuwa mkuu mpya wa Idara ya Ujasusi na Usalama nchini Msumbiji. Uteuzi huo unaanza mara moja kuanzia leo. Pia mheshimiwa Rais amemuagiza katibu mkuu wa Wizara ya Afya kumpangia mara moja kituo cha kazi Dr.Anabella katika hospitali yoyote nchini Msumbiji atakayopenda kufanyia kazi".
Kachero Manu akatabasamu, akiacha na habari hiyo na kufungua mlango wa maliwato kwenda kumwaga maji. Alikuwa akijiandaa aelekee hospitalini kabla hajapaa kurejea Tanzania.
Baada ya kupata staftahi yake akiwa tayari amevalia mavazi yake nadhifu, saa 4:00 kamili juu ya alama za asubuhi, Kachero Manu alikuwa ndio anawasili katika viunga vya hospitali binafsi ya kisasa inayoitwa "Hospital Privado de Maputo" iliyopo eneo la "Ruo do Rio Inhamiara", Jijini Maputo. Alikuja kuwazuru wenzake Dr.Anabella na Komandoo "JS", wenzake ambao alishirikiana nao bega kwa bega katika misheni takatifu ya kuwaangamiza wahujumu wa uchumi wa nchi ya Msumbiji. Dr.Anabella na Komandoo "JS" nao walikimbizwa usiku usiku Jijini Maputo kwa ndege maalumu ambayo inavifaa vyote vya kuhudumia wagonjwa mahututi.
Kachero Manu alisindikizwa pale hospitalini na msafara wa ulinzi madhubuti wa Jeshi la Msumbiji utasema Rais wa Taifa kubwa kama Marekani ametua nchini Msumbiji. Komandoo "JS" hakufanikiwa kuongea nae alimkuta yupo kwenye chumba cha wagonjwa mahututi 'ICU' amezinduka tayari, lakini ana maumivu makali. Hivyo alishauriwa na Daktari amuache mgonjwa apumzike vya kutosha. Ila Dr.Anabella alifanikiwa kuongea nae kwa tabu sana, huku akionekana kuwa na furaha sheshe inayotokana na kushiriki kulipiza kisasi cha walioua familia yake.
Baada ya kutoka hospitali akarudi hotelini kujiandaa na safari ya kurejea Tanzania usiku wake. Alishaongea na kwenye simu na Bosi wake wa Idara ya Usalama wa Taifa Bwana Mathew Kilanga, huku akimpongeza na kumuahidi mapokezi ya kishindo ya kishujaa.

MWISHO
 
Safi sana kiongozi, tulikuwa bega kwa bega mpk hitimisho. Naamini utatuletea burudani nyingine iliyo tukuka wahenga walisema "mwisho mwa riwaya hii, Ni mwanzo mwa riwaya nyingine"
 
CABO-DELGADO-PART 40


Komandoo "JS" alipotoka nje akaelekea kule alikoelekezwa na Dr.Anabella kwenye maegesho ya chini kwa chini ya magari. Ilionekana hamna njia ingine ya kutokea kule kwenye handaki isipokuwa kwenye maegesho haya.
Akawa anatambaa chini kwa chini kuelekea kule kwenye magari ya thamani kubwa ambapo alihisi gari mojawapo ni la Bwana Alfredo. Ghafla mvua ya risasi ikaanza kumfuata, salama yake kulikuwa na kigiza giza hivyo walengaji wakawa wanakosa risasi akabingirika mpaka akafanikiwa kuingia chini ya uvungu wa gari.
Kisha akapata wazo la kuwachanganya, akatoa rimoti kama saa mfukoni mwake, akabonyeza bonyeza vitufe vyake. Ghafla bin vuu mabomu aliyotega nje ya ukuta wa jengo la kiwanda yakanza kulipuka. Mbinu ambayo ilifanikiwa wale washambuliaji wake wakawa wanakimbizana kuokoa maisha yao, wengine walitupa mpaka silaha zao.
Bwana Alfredo nae akatimka mbio na faili lake mkononi na bastola akitokea kwenye karakana alikokuwa amejichimbia kwenye mashine mbovu na kukimbilia kuingia kwenye gari lile lile ambalo chini yake kuna Komandoo "JS".
Komandoo akawa anatambaa chini ya chasesi ya gari alipofika mwishoni kwenye buti gari ikaanza kuondoka. Komandoo "JS" akafanikisha kushika chuma cha kingo za nyuma kinacholinda gari na ajali akawa anaburutwa chini lakini haliachii gari.
Kachero Manu akiwa anatokeza kwenye maegesho akawa anaona gari inakuja usawa wake akarusha risasi moja iliyotua kwenye tairi la kushoto la gari ikaanza kuyumba huku tayari Komandoo "JS" yupo juu ya gari kashaipandia anatambaa kwenye bodi ya gari mpaka akafika usawa wa siti ya abiria kiti cha nyuma.
Bwana Alfredo alikuwa ametingwa na kujibizana risasi na Kachero Manu akajisahau kuwa kuna namba ingine chafu sana kuliko hata huyo Kachero Manu nayo inamuwinda imfikishe katika mikono ya sheria.
Alichofanya Komandoo "JS" ni kutoa kioo cha dirisha la gari kwa kutumia pete yake ya almasi aliyovaa mkono wake wa kushoto, kisha akaingia kwenye kupitia dirishani kisha akajikohoza. Bwana Alfredo akageuka, mshtuko alioupata hakuamini mpaka bastola yake ikamponyoka ikaingia chini ya uvungu wa siti ya kiti cha dereva.
Alikuwa haamini anachokia kwenye mboni za macho yake. Akawa anachochea mwendokasi wa gari kuelekea kwenye tanki la mafuta mkabala na geti la kutokea. Akili ya Komandoo "JS" ikausoma mchezo wote kuwa ana lengo la kujitoa mhanga kama magaidi kwa kwenda kulipigiza gari kwenye tanki la kuhifadhia mafuta na kusababisha mlipuko ili wafe wote.
Komandoo "JS" akarukia kiti cha mbele wakawa wanapimana ubavu wa nguvu za mikono kwa kugombaniana usukani wa gari, mpaka walipokaribia meta chache kulifikia tenki la mafuta, Bwana Alfredo akafungua mlango wa dereva na kurusha nje faili lake jeusi kisha yeye mwenyewe kuruka nje ya gari.
Kishindo kikubwa cha mlipuko kilisikika baada ya gari kwenda kujibamiza kwenye tenki na kushika moto. Wakati huo huo gari ya kubeba wagonjwa mahututi na gari za polisi zikawa zimewasili kiwandani.
Dr.Anabella na Komandoo "JS" ambaye nae alifanikiwa kuruka nje ya gari walikuwa wamepoteza fahamu hivyo wakawa wa kwanza kupakizwa na kuwahishwa hospitali kwa matibabu. Bwana Alfredo alikuwa amevunjika kiuno kutokana na risasi tano alizopigwa kiunoni akiwa hewani na Kachero Manu alipokuwa anaruka nje ya gari, akapigwa pingu za mikononi na miguuni tayari kwa safari ya kituo cha polisi. Shughuli yote ya kuwashikisha adabu vibaraka wa wakoloni ilikamilika saa saba kamili usiku.

SURA YA KUMI NA TISA
La Mgambo limelia Ushindi hadharani
Asubuhi ilipambazuka kwa Kachero Manu akiwa amelala katika moja ya hoteli kubwa na ya kifahari inayoitwa "Cardoso" iliyopo Jijini Maputo. Ilikuwa ni hoteli ambayo hawafikii hapo ila watu wenye sharafu na pesa nyingi. Alipelekwa usiku usiku na ndege binafsi ya Rais wa Msumbiji na kupewa ulinzi wenye hadhi ya kibalozi.
Rais wa Msumbiji alikuwa amefurahishwa na ushujaa wa Kachero Manu kwa kufanikiwa kukisambaratisha kikosi cha Mafioso waliokuwa wanachafua jina na hadhi ya Msumbiji kitaifa na kimataifa.
Mafioso ambao kama wangechekewa wangeziingiza kwenye uhusiano tete nchi za Msumbiji na Tanzania na kuvunja misingi ya waasisi wa mataifa hayo.
Hivyo akaagiza Kachero Manu apewe ulinzi mkubwa asije akapata madhara kutoka kwa wanyonya mirija waliobaki kwenye mfumo wa vibaraka walioujenga toka enzi za mapambano ya kudai uhuru wa Msumbiji. Akaenda kuwekwa kwenye hoteli ambayo usingizi wake kwa siku ni zaidi ya milioni mbili kwa pesa za kitanzania.
Aliamshwa Kachero Manu asubuhi hiyo na miale ya jua isiyo na makali iliyokuwa inapenya katika vioo vya dirisha lake ambalo hakufunga pazia lake kutokana na uchovu wa mapambano ya usiku kucha. Alitupa pembeni blangeti lake la kujifunika na baridi akachukua rimoti ya kipoza hewa cha chumba akazima. Kisha akapiga magoti akaanza kusali kumshukuru Mungu kwa kumpa nafasi ingine ya kuwa hai hasa ukichukulia kwenye majukumu haya mazito aliyopewa nchini Msumbiji ndani ya siku kadhaa hizi amechungulia mdomo wa kifo mara nyingi sana kisha anaponea chupuchupu.
Baada ya kumaliza sala fupi akanyanyuka akapiga simu jikoni kuagiza kifungua kinywa, kisha akawasha runinga iliyotundikwa juu katika ukuta wa chumbani kwake, ilikuwa ni saa mbili asubuhi akakutana na taarifa ya habari ya Shirika la Habari la Afrika ya Kusini (SABC). Akawa anajongea mlango wa maliwatoni kwenda kuoga maji ili mwili upate nguvu mpya alipofika mlango wa maliwato kabla hajaingia, akamsikia msomaji wa taarifa ya habari anaelezea habari zilizowafikia hivi punde, akasimama kuangalia hiyo taarifa.
"Kachero bobezi kutokana nchini Tanzania kwa kushirikiana na Komandoo mkongwe wa nchini Msumbiji wamefanikiwa kuwatia mbaroni viongozi wahalifu wa kundi la NACATANAS lililokuwa linaongoza mauaji ya raia wasio na hatia pamoja na uporaji katika machimbo mbalimbali ya madini nchini Msumbiji. Pia jeshi la Msumbiji limefanikiwa usiku wa kuamkia leo kukamata shehena ya madawa ya kulevya na kontena mbili za madini ya rubi ziliyokuwa zimefichwa katika kiwanda cha korosho tayari kwa kusafirishwa nje ya nchi. Pia jeshi la polisi linamshikilia mmiliki wa kampuni ya Monte Branco Ltd Bwana Alfredo kwa tuhuma za kuendesha shughuli mbalimbali haramu nchini Msumbiji ikiwemo kufadhili kikundi cha "NACATANAS", na atapandishwa kizimbani mara tu baada ya upelelezi kukamilika. Pia jeshi la polisi limefanikiwa kunasa majina ya washirika wote wa Bwana Alfredo waliopo serikalini na kwenye taasisi binafsi. Uchunguzi bado unaendelea nao watafikishwa mahakamani mara moja baada ya upelelezi kukamilika. Wakati huo huo Rais wa Msumbiji amemteua ndugu Jacob Steven kuwa mkuu mpya wa Idara ya Ujasusi na Usalama nchini Msumbiji. Uteuzi huo unaanza mara moja kuanzia leo. Pia mheshimiwa Rais amemuagiza katibu mkuu wa Wizara ya Afya kumpangia mara moja kituo cha kazi Dr.Anabella katika hospitali yoyote nchini Msumbiji atakayopenda kufanyia kazi".
Kachero Manu akatabasamu, akiacha na habari hiyo na kufungua mlango wa maliwato kwenda kumwaga maji. Alikuwa akijiandaa aelekee hospitalini kabla hajapaa kurejea Tanzania.
Baada ya kupata staftahi yake akiwa tayari amevalia mavazi yake nadhifu, saa 4:00 kamili juu ya alama za asubuhi, Kachero Manu alikuwa ndio anawasili katika viunga vya hospitali binafsi ya kisasa inayoitwa "Hospital Privado de Maputo" iliyopo eneo la "Ruo do Rio Inhamiara", Jijini Maputo. Alikuja kuwazuru wenzake Dr.Anabella na Komandoo "JS", wenzake ambao alishirikiana nao bega kwa bega katika misheni takatifu ya kuwaangamiza wahujumu wa uchumi wa nchi ya Msumbiji. Dr.Anabella na Komandoo "JS" nao walikimbizwa usiku usiku Jijini Maputo kwa ndege maalumu ambayo inavifaa vyote vya kuhudumia wagonjwa mahututi.
Kachero Manu alisindikizwa pale hospitalini na msafara wa ulinzi madhubuti wa Jeshi la Msumbiji utasema Rais wa Taifa kubwa kama Marekani ametua nchini Msumbiji. Komandoo "JS" hakufanikiwa kuongea nae alimkuta yupo kwenye chumba cha wagonjwa mahututi 'ICU' amezinduka tayari, lakini ana maumivu makali. Hivyo alishauriwa na Daktari amuache mgonjwa apumzike vya kutosha. Ila Dr.Anabella alifanikiwa kuongea nae kwa tabu sana, huku akionekana kuwa na furaha sheshe inayotokana na kushiriki kulipiza kisasi cha walioua familia yake.
Baada ya kutoka hospitali akarudi hotelini kujiandaa na safari ya kurejea Tanzania usiku wake. Alishaongea na kwenye simu na Bosi wake wa Idara ya Usalama wa Taifa Bwana Mathew Kilanga, huku akimpongeza na kumuahidi mapokezi ya kishindo ya kishujaa.

MWISHO


Safi sana... Story nzuri sana...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 
Back
Top Bottom