Riwaya: "Cabo-delgado"-part 01

CABO-DELGADO-PART 36


Bila kumchelewa Komandoo JS akamrusha teke la mguu wa kushoto kwenye mkono wa adui aliokuwa amekamatia bunduki ikamdondoka chini. Yule mlinzi akajibu mapigo akafanya kama anageuka nyuma kama anataka kukimbia lakini akajigeuza kwa haraka na kurusha teke moja maridhawa la mguu wake wa kulia kuelekea kwenye tumbo la Komandoo "JS". Teke ambalo lilimpata sawia maeneo ya tumboni, kwa sababu Komandoo "JS" alishindwa kujilinda.
Aliingia kwenye mtego wa kuzania adui yake anakimbia hivyo hakujiandaa na shambulio lile na ghafla. Teke lile lilimyumbisha Komandoo "JS" vilivyo na kumfanya mwili wake ukose uwiano linganifu. Yule mlinzi akamfuata Komandoo "JS" wakati amejiinamia kuugulia maumivu. Akamkamata mabega kwa nguvu kisha akamuinua kwa haraka halafu akamuinamisha kwa haraka na kumpiga vifuti viwili vya nguvu usoni mwake. Vifuti vile vilimuingia kisawasawa Komandoo "JS", akaanza kuona nyota nyota usoni. Alivyopeleka vidole vyake usoni na kujishika puani, akaona damu zinachuruzika churu churu kwenye mwamba wa pua yake.
Kitendo ambacho kilichochea hasira na kumpa hamasa ya kujibu mapigo kwa haraka na kwa umakini. Akaanza kujilaumu kimoyomoyo kwa kumdharau adui yake ambaye alimchukulia kuwa ni mzembe "lalavi buda", anayezembea lindoni kwa kulala. Kumbe adui yake ni mzuri sana kwenye mapambano ya ana kwa ana. Komandoo "JS" akaigiza kama amezidiwa sana akawa anayumbayumba mtego ambao aliuingia yule mlinzi akajua Komandoo "JS" ameshaelekea kibla mwenyewe anasubiri kuchinjwa tu.
Sasa akawa anamfuata bila kuchukua tahadhari yoyote, utasema anapambana na Bi.Harusi. Alipomkaribia tu yule Mlinzi akarusha teke la mguu wa kushoto la mbavuni.
Komandoo "JS" akaliona lile taka akalikwepa kisha akaudaka mguu na kuukunja kwa mbele, ilikuwa ni kitendo cha haraka ndani ya sekunde kadhaa. Mfupa wa maungio ya goti ulivunjika kama unavyovunjika muwa bungala, kwa kutoa sauti ya taaaah..!.
Mlinzi yule akawa anapiga kelele za maumivu utasema amejikwaa jiwe na kung'oa ukucha wa dole gumba la mguuni. Komandoo "JS" akamuwahi kumziba mdomo asije akawashtua waliomo kwenye helikopta pale uwanjani. Kisha akampiga kareti moja ya shingoni, akafa pale pale bila hata kuomba maji ya kunywa. Akamburuza yule mlinzi kwenye kichaka cha pembeni yake, akatoa kitambaa kidogo mfukoni mwake akajifuta damu za puani mwake kisha akamvua sare zake yule mlinzi na kuzivaa yeye na kofia yake ili aweze kwenda kwenye helikopta bila kutiliwa mashaka.
Alivyovaa alijicheka kidogo maana hazikumtoshea vizuri hasa suruali ya yule mlinzi ilikuwa fupi wakati Komandoo "JS" alikuwa ni mrefu. Alikuwa anaonekana kama wanamuziki wa Kikongo wale wanaovaa suruali pana za mabwanga kama mifuko ya mashineni. Baada ya kuvaa akaelekea getini na kuelekea ilipo helikopta. Akawa anatembea kuelekea kwenye helikopta bila wasiwasi wowote na ilikuwa ipo mbele ya upeo wa macho yake. Alipoikaribia akaongeza umakini lakini aliona taa za ndani za helikopta zimezimwa ila za nje zinawaka. Kumbe rubani alikuwa amejipumzisha yupo peke yake lakini anamuona jinsi komandoo "JS" anavyokuja.
"Mbona Bob Chinanga anazidi kuuweka usiku, hapa Inspekta Mark anapiga simu kila wakati na kachukia sana kitendo chetu cha kuchelewa kumpeleka mateka wetu" alisema yule rubani kumueleza Komandoo "JS" alipofika usawa wa kioo cha rubani.
Laiti rubani angefahamu kuwa anauza siri za kambi kwa adui hatari sana, angejifia kihoro kwa uoga. "Nadhani wanakuja muda sio mrefu maana nimeona gari linajiandaa kuja" alidanganya komandoo "JS" na kujisifu kimoyomoyo kuwa mbinu yake imefanikiwa. "Samahani naomba kuazima kiberiti nataka kuvuta sigara sasa kiberiti changu kimepotea sikioni " alisema Komandoo "JS".
"Ngoja basi nishuke tuvute wote maana na mie sijavuta muda mrefu nina kiu ya sigara balaa nilikuwa nategemea watakuja kwa haraka" alisema rubani yule huku akishuka nje ya helikopta.
Wakati anazunguka kwa mbele ya helikopta yule rubani kumfuata Komandoo "JS", lilikuwa kosa kwake alipotokeza mbele ya komandoo "JS" akakutana na mdomo wa bastola unamtazama. "Nyoosha mikono juu na usijaribu kuleta ujanja wowote ambao utagharimu uhai wako uende ukasalimie kuzimu usiku usiku kabla jogoo la asubuhi halijawika" alifoka Komandoo "JS" huku anamsogelea. Kiuhalisia alikuwa anamtisha tu hakupanga kabisa kumuua bali alipanga kumtumia rubani huyu huyu aendeshe hiyo helikopta.
Komandoo "JS" alikuwa mtaalamu wa kurusha helikopta na hata ndege ndogo ila tatizo alikuwa hayafahamu vizuri mazingira ambayo hiyo helikopta inatakiwa kutua. "Ongoza njia urudi ndani" alisema Komandoo "JS" kwa sauti ya ukali. Bila kuleta kukurukakara rubani yule akatii sheria bila shuruti akiongoza njia huku amenyoosha mikono juu.
Walipoingia ndani akamuamrisha akae kwenye siti ya urubani na kumfunga mikono na miguu kwa kamba ya manila, na kumshindilia matambala kinywani Kisha akampokonya simu zote za mawasiliano ya mkononi.
Akajipa nusu saa kama hatumuona Kachero Manu atamfuta kichwani mwake kwenye hesabu za watu hai, hivyo itabidi aingie kambini kuiteketeza kambi ili awatie hasara haswa mpaka wajute kumfahamu.

Tukutane kiwandani mkutanoni
Kachero Manu na Dr.Anabella walifanikiwa kufika kwenye gari linalowasubiri lango kuu bila kikwazo chochote na bila kutiliwa mashaka. Kwa sababu Dr.Anabella alikuwa anajulikana kinagaubaga, kambi nzima kuwa ni mchumba wa Bosi wao Mark na pia ni Daktari wa mateka mule kambini.
Walipofika geti kuu Dr.Anabella akapanda kwenye gari siti ya mbele jirani na dereva, huku Kachero Manu akizunguka kibanda cha walinzi wa getini akatokomea kwenye stoo za silaha zilizojipanga pembezoni umbali mchache kutokea kwenye kibanda cha walinzi.
Alipofika stoo kwa kutumia funguo alizochukua mfukoni kwa Bob Chinanga, akajaribisha mara kadhaa mpaka ufunguo mmoja wapo ukakubali kufungua. Kilikuwa ni chumba cha zana za kivita za kisasa, ni chumba ambacho walikuwa wanaingia watu watatu tu, ambapo kila mmoja alikuwa na funguo zake binafsi anazotumia. Watu hao ni Bob Chinanga, Inspekta Jenerali Mark na Bwana mkubwa Alfredo.
Bila kuchelewa akatafuta yalipo mabomu na rimoti za kulipulia mfano wa saa za mkononi akazipata, akayatega vizuri tayari kwa kulipuka. Akatoka na mabomu mawili madogo mfano wa ukubwa wa nazi za pemba zilizotolewa maganda yake lakini yana uwezo wa kuteketeza kijiji kizima ukiamua. Baada ya dakika 10 akawa kamaliza kazi ya kutega milipuko.
Akaharakisha kurejea kwenye gari na kudandia nyuma tayari kwa kutoka lango kuu lililokuwa likimsubiria yeye tu. "Ondosha gari haraka tumechelewa" alisema Kachero Manu kwa sauti ya juu akiwa amepakia nyuma ya "Pick-up". "Tunaondoka sawa lakini simuoni Bob Chinanga wala mlengwa mkuu wa safari wapo wapi? "alisema yule dereva kwa sauti ya wasiwasi huku mkono wake wa kulia unawasha gari.
"Mateka wetu ana hali mbaya sana, hawezi hata kuongea hivyo Bob Chinanga kamtuma huyu mwenzako akatoe taarifa kama kuna uwezekano ibadilishwe siku ya mahojiano ili apate nafuu na pia mimi nakwenda kufuata dawa za kumtibia huyo mgonjwa" alidanganya Dr.Anabella uwongo mkongwe kwa kutumia sauti ya huzuni. Uwongo ambao msikilizaji yoyote atadhania kuna ukweli ndani yake kutokana na sauti hiyo ya kubembeleza kubeba ujumbe wa huzuni.
Dereva yule hakutia neno lolote, ishara ya kukubaliana na maelezo ya Dr.Anabella akawa anaingiza gia na kuliondosha gari kwa mwendo wa wastani mpaka walipofunguliwa geti kuu na kutimua vumbi kuelekea uwanjani ilipo helikopta tayari kwa safari ya Pemba usiku huo. Bila kujijua kuwa wanaenda kukutana na Komandoo "JS" anayewasubiria kwa hamu kubwa waende kuanzisha vagi mkutanoni.
Komandoo "JS", macho yake yalikuwa hayabanduki kila wakati kwenye saa yake ya mshale ya gharama sana aina ya "Patek Philippe" kutoka Uswisi, aliyoivaa mkono wake wa kushoto. Saa ambayo mishale ya dakika na sekunde ilikuwa inashindana kujizungusha ili iweze kuleta mabadiliko ya muda. Muda ulikuwa unasomeka saa 2:45 usiku mbichi ikimaanisha zimebaki dakika zisizopungua 5 tu kutimia saa tatu kasoro dakika kumi ikiwa ndio muda wa mwisho aliojiwekea wa kuvumilia kuwangojea akina Kachero Manu na watekaji wake. Akiwa amezama kwenye tafakari ya mishale ya saa yake na kuanza kujiweka tayari kushuka kwenye helikopta akashtukia gari inakuja usawa wa ile helikopta kwa kasi kisha ikaenda kwenye maegesho madogo ya hapo uwanjani.
Wakashuka watu watatu, mwanamke mmoja akiwa amevaa koti la kidaktari na walinzi wawili wakiwa kwenye sare zao wakawa wanakuja kwenye helikopta alipo Komandoo "JS" na rubani ambaye sasa ni mateka wake. Komandoo JS alikuwa anausoma mchezo mzima kupitia kwenye kioo cha helikopta kwa kutumia mwangaza wa taa za uwanjani pia taa za helikopta zilikuwa zinawamulika vizuri sana. Ila wao walio nje walikuwa hawawezi kumuona kwa sababu alizima taa za ndani ya helikopta.
Komandoo "JS" akawa amepagawa hamuoni Kachero Manu ambaye alitegemea ataletwa na hawa walinzi. "Lakini mbona hawajafika nae?, kauliwa? au wamemfanya nini?", ni maswali aliyojiuliza lakini yakawa yanakosa majibu muafaka. Hivyo akajipanga wakiingia ndani ya helikopta lazima alianzishe varangati kwa kuwashtukiza kabla hawajamshtukia yeye uwepo wake ndani ya ile helikopta.
Mipango ya Kachero Manu na Dr.Anabella ilikuwa ni kuondoka na rubani na yule mlinzi ambaye ndio dereva wa Bob Chinanga mpaka Pemba, kisha watakapofika wawageuke na kuingia na mlinzi mkutanoni.
Hivyo walikuwa wanakuja ndani ya helikopta kizembe zembe bila kuchukua tahadhari yoyote bila kujua ndani ya helikopta kuna komandoo "JS" Ambaye malengo yake na yao yanashabihiana ila hawatambuani. Komandoo "JS" alijibanza chini ya kiti nyuma kabisa, huku akiwa ameshikilia bastola zake mbili mkononi.
Wa kwanza kuingia ndani ya helikopta alikuwa ni Dr.Anabella, akachagua siti akakaa tuli. Kisha akaingia mlinzi yule na akafuatia Kachero Manu akiwa wa mwisho kuingia. Wote kwa pamoja wakapatwa na mshtuko baada ya kumuona rubani amefungwa kamba za miguuni na mikononi na kazibwa na matambala kinywani mwake.
Kabla hawajatanabahi maamuzi ya kufanya walishtuliwa na sauti nzito toka kwa mwanaume wa kazi, Komandoo "JS". "Nyanyueni mikono yenu wote, msilete ujanja wowote utakaonilazimisha kulipua vichwa vyenu kwa risasi" alifoka Komandoo "JS", sauti ambayo haikuwa na chembe ya utani ikimaanisha anachokizungumza ndicho aatakachokifanya kwa kuwatwanga risasi mmoja mmoja kama wakileta ukaidi mbele yake.
Bila ubishi wowote wote kwa pamoja wakanyanyua mikono juu, huku tayari komandoo "JS" ameshajitokeza juu, kutokea chini ya siti ya nyuma.
 
CABO-DELGADO-PART 37

Komandoo "JS" akauliza, "Kachero Manu mmemuacha wapi? toeni jibu nyinyi makhabithi la sivyo na nyie naondosha roho zenu sasa hivi". Hapo hapo Kachero Manu akatambua huyu yupo upande wake kwa sababu kama angekuwa upande wa adui angekuwa anajua kila kitu kinachoendelea na asingemteka rubani yule. Akaibia Kachero Manu kumtazama kwa jicho pembe, akaona ni mtu aliyefuga masharafa mashavuni mwake yenye mvi nyeupe, akakumbuka Komandoo "JS" anafuga masharafa kutokana na picha aliyopewa ofisini Dar es salaam na Bosi wake.
Alichofanya Kachero Manu ni kujitambulisha kwa lugha ya siri (SPY-CODE) aliyopewa ya kuwasiliana na Komandoo "JS" pindi alipojitambulisha ujio wake na uhitaji wa gari na nyumba ya kukodi. Akasema kwa sauti ya juu "wewe ni CUT-OUT?" akimaanisha anamuuliza Komandoo "JS" ni kiunganishi kati ya ofisi ya Makachero wa Tanzania nchini Msumbiji?.
Makachero wazoefu wana lugha zao ambazo wanazitumia kuwasiliana ambazo ni ngumu kwa asiyemhusika kuzifahamu. Mfano ukiskia msemo, "EARS ONLY" maana yake ni taarifa ya siri mno haitakiwi kuandikwa ila inafikishwa kwa maneno pekee, au ukiskia "DEAD DROP" maana yake ni mzigo ambao Kachero mmoja ataupeleka sehemu fulani atauacha kisha mwingine ataupitia kuuchukua mzigo huo bila Makachero wawili hao kuonana uso kwa uso.
Hivyo kitendo cha kutumia neno "CUT OUT" hapo hapo wakatambuana, Komandoo "JS" akashusha bastola zake chini, na Kachero Manu akachomoa bastola yake na kumuweka chini ya ulinzi yule dereva wa Bob Chinanga na kumpa amri ya kumfungua kamba rubani wa helikopta.
Baada ya pilikapilika hizo za dakika chake safari ikaanza muda wa kama saa 3:05 usiku. Hawakuwa na muda wa kupoteza huku rubani akipewa tahadhari ya kutoleta ujanja wowote wa sungura utakaogharimu maisha yake. Wakati wakiwa juu angani wameanza kupaa meta chache tu ikasikika milipuko mikubwa ya mabomu huko chini kambini, 'Gorongosa Camp' inateketea kwa moto.
Dr.Anabella na Kachero Manu wakatazamana huku kila mmoja akitabasamu, alikuwa Kachero Manu amelipua mabomu aliyoyatega pale kambini kwa kutumia kitendambali (rimoti) ya mkononi mwake aliyovaa kama saa mkononi. Kiwingu kizito cha moto mwekundu kilitanda kuizunguka kambi ya Gorongosa usiku huo utasema siku ya kiama ndio imetoka. Kambi hiyo iliteketezwa kabisa bila kusaza kitu chochote.

SURA YA KUMI NA NANE
Mwisho wao Mafioso wa Cabo-Delgado umewadia
Soko la Baraca maana yake ni soko la vitu vya bei rahisi. Hili soko lipo katikati ya Mji wa Pemba kilometa takribani kama 2 tu kutokea barabara ya pwani (Coastal Road). Ni soko ambalo wakati wote limefurika limefurika Wafanyabiashara na wateja wao. Sokoni hapo ni maarufu pia kwa bidhaa za vinyago vya Kimakonde vya kila sampuli ikiwemo na bidhaa za baharini. Ni soko ambalo aghalabu utakutana na watalii wa kutoka nchi za ng'ambo kama China, Japani, Marekani na mataifa mengineyo ya kigeni wakiwa wametingwa kujitafutia zawadi za bidhaa asilia za kurejea nazo nchini kwao.
Waswahili wanasema kila kwenye msafara wa mamba na kenge nao hawakosekani, kwani katika harakati hizi za soko la Baraca za watu kujitafutia riziki zao za halali za kujiendeshea maisha kwa ajili yao na familia zao, kampuni ya "Monte Branco Ltd" nao walijichomeka katika eneo hili kwa kuwekeza kiwanda cha daraja la kati cha kusindika korosho, lakini ndani yake ilikuwa ni ofisi yao kuu ya kupanga mipango haramu yote ya kuhujumu nchi ya Msumbiji. Chini ya kiwanda inasemekana kulikuwa na ofisi za wapanga madili na wizi wa kila aina ambao walikuwa wanalipwa mishahara minono na mmiliki wa kampuni Bwana Alfredo.
Dr.Anabella ameshawahi kupelekwa huko chini ya kiwanda zaidi ya mara moja na mchumba wake Inspekta Jenerali Mark enzi mapenzi yao yamepamba moto. Mark katika kutaka kujionyesha kuwa ni mtu muhimu sana mbele ya Bwana Alfredo, siku ya kwanza alimchukua Dr.Anabella usiku wa manane siku ambayo Dr.Anabella alikuwa na zamu ya usiku katika hospitali ya kiwandani hapo akampeleka huko kwenye mahandaki chini ya kiwanda kumtembeza. Yalikuwa ni mahandaki yenye maofisi na chumba zenye starehe zote na mahitaji yote muhimu yanapatikana. Milango yake ilikuwa ni ya kufunguka kwa rimoti inayofunguliwa na namba za siri maalumu. Inspekta Mark alimdanganya Dr.Anabella kuwa anazitumia ofisi hizo za siri kupangia baadhi ya operesheni dhidi ya wahalifu.
Kiwandani hapo ndio palipangwa kufanyika mkutano wa Mwisho ambao utahitimisha uhai wa Kachero Manu, na kutoa onyo kali kwa wote wenye kufuatilia nyendo za Bwana Alfredo katika biashara zake za rubi na nyinginezo.
Mkutano ulipangwa uanze saa 4:00 kamili usiku, huku ukumbi ulikuwa umepambwa vikorombwezo vyote muhimu kwa mahitaji ya mkutano huo muhimu. Na washirika wote wa Bwana Alfredo, Mafioso wenzake kutoka Ureno na Afrika ya kusini walikuwa wameshawasili Pemba tayari kwa mkutano. Wengi walikuwa ni vigogo wana hisa wa kampuni na watendaji wakuu wa shughuli za kila siku za kampuni. Inspekta Jenerali Mark Noble alikuwa hatulii kama mbwa koko jike mwenye joto anayehitaji kupandwa. Alikuwa kama mtu mwenye mazonge yanayotokana kuelemewa na majukumu. Yeye kama akiwa Afisa Usalama Mkuu wa kampuni na kiongozi wa kikundi cha mateso cha "NACATANAS" alikuwa anahaha kuhakikisha mambo yanaenda kama yalivyopangwa bila kuharibiwa na mtu yoyote.
Lakini kilichokuwa kinamnyima raha ni kitendo cha helikopta kutokea Gorongosa kambini kuchelewa kufika Pemba. Alikuwa amempa maagizo Bob Chinanga ya kuhakikisha wanafika Pemba ifikapo saa 2:00 usiku. Sasa muda huo wa saa 3:15 usiku muda ukiwa unayoyoma haonekani Bob Chinanga wala wasaidizi wake. Mbaya zaidi ilikuwa mwanzoni anawasiliana na rubani na kule kambini lakini sasa alikuwa akipiga simu zote hazipatikani kabisa.
Kijasho chembamba kikaanza kumtiririka usoni na kwenye makwapa ya mikono yake jasho jekejeke likawa linamtiririka. Kengele ya hatari ikagonga kichwani mwake kuwa huenda Kachero kawazidi nguvu. Lakini kwa upande mwingine anajipa matumaini haiwezekani mtu mmoja aweze kuteketeza kikosi kizima cha zaidi ya watu elfu na ushee na kama akiweza basi itakuwa ni zaidi ya miujiza hashara ya Mtume Musa kwa Farao alipoenda kuwakomboa wana wa Israeli.
Inspekta Jenerali Mark Noble alikuwa ameshachoshwa na maisha haya ya mikiki mikiki. Aliweka nia na adhima ya kuacha kazi katika idara ya Polisi ya Msumbiji, kisha pia astaafu kazi kutoka "Monte Branco Ltd" kazi ambayo ilishakuwa hatarishi kwake. Ambapo suala la kupoteza uhai ilikuwa ni dakika sifuri. Alipanga achukue mafao yake kisha aondoke na mchumba wake Dr.Anabella kwenda kuishi kwenye visiwa vya Madagascar. Kwa mafao yake atakayopewa na Bwana Alfredo yalimpa jeuri na kiburi cha kuweza kuishi nchi yoyote ya Kiafrika bila kufanya kazi kwa muda hata wa miaka 50.
Inspekta Jenerali Mark akiwa amezama kwenye dimbwi la mawazo nje ya sehemu ya kuegeshea magari akiwa anawasubiri akina Bob Chinanga akasikia mlio wa simu yake unaita akaanza kupagawa. Akadhani anataka kuulizwa kuhusu ujio wa Kachero Manu. Ulikuwa ni mlio maalumu kwa ajili ya Bosi wake Bwana Alfredo, akajidhania kama yupo ndotoni maana hakutegemea kupokea simu ya Bwana Alfredo katika kipindi kigumu kama hiki. Alipoitoa simu yake akaipokea huku vidole vinatetemeka kama mlevi gongo.
"Habari za siku BIG BOSS" alisema Mark kwa sauti ya kujifaragua na kujilazimisha furaha. "Njoo ofisini mara moja kabla ya kikao nina mazungumzo nyeti na wewe...!" kisha kabla ya kujibu kitu chochote ikawa tayari simu imeshakatwa na Bwana Alfredo. Moyo wa Mark ukalipuka, na kuanza kwenda mbio kama mwanariadha anayeshindania medali ya dhahabu katika mbio za meta 100 moja. Akapiga moyo konde kuwa liwalo na liwe ngoja aende akamsikilize Bosi wake.
Akaanza kutembea kuelekea kwenye ofisi ya Bwana Alfredo iliyoko chini ya kiwanda kwenye handaki kwa kupitia kwenye maegesho ya magari, huku anajifanya kutikisa funguo za gari yake kupotezea hofu yake kuonyesha anajiamini. Lakini mawazoni alikuwa anajiambia leo kazi ipo kusuka au kunyoa.
 
CABO-DELGADO-PART 37

Komandoo "JS" akauliza, "Kachero Manu mmemuacha wapi? toeni jibu nyinyi makhabithi la sivyo na nyie naondosha roho zenu sasa hivi". Hapo hapo Kachero Manu akatambua huyu yupo upande wake kwa sababu kama angekuwa upande wa adui angekuwa anajua kila kitu kinachoendelea na asingemteka rubani yule. Akaibia Kachero Manu kumtazama kwa jicho pembe, akaona ni mtu aliyefuga masharafa mashavuni mwake yenye mvi nyeupe, akakumbuka Komandoo "JS" anafuga masharafa kutokana na picha aliyopewa ofisini Dar es salaam na Bosi wake.
Alichofanya Kachero Manu ni kujitambulisha kwa lugha ya siri (SPY-CODE) aliyopewa ya kuwasiliana na Komandoo "JS" pindi alipojitambulisha ujio wake na uhitaji wa gari na nyumba ya kukodi. Akasema kwa sauti ya juu "wewe ni CUT-OUT?" akimaanisha anamuuliza Komandoo "JS" ni kiunganishi kati ya ofisi ya Makachero wa Tanzania nchini Msumbiji?.
Makachero wazoefu wana lugha zao ambazo wanazitumia kuwasiliana ambazo ni ngumu kwa asiyemhusika kuzifahamu. Mfano ukiskia msemo, "EARS ONLY" maana yake ni taarifa ya siri mno haitakiwi kuandikwa ila inafikishwa kwa maneno pekee, au ukiskia "DEAD DROP" maana yake ni mzigo ambao Kachero mmoja ataupeleka sehemu fulani atauacha kisha mwingine ataupitia kuuchukua mzigo huo bila Makachero wawili hao kuonana uso kwa uso.
Hivyo kitendo cha kutumia neno "CUT OUT" hapo hapo wakatambuana, Komandoo "JS" akashusha bastola zake chini, na Kachero Manu akachomoa bastola yake na kumuweka chini ya ulinzi yule dereva wa Bob Chinanga na kumpa amri ya kumfungua kamba rubani wa helikopta.
Baada ya pilikapilika hizo za dakika chake safari ikaanza muda wa kama saa 3:05 usiku. Hawakuwa na muda wa kupoteza huku rubani akipewa tahadhari ya kutoleta ujanja wowote wa sungura utakaogharimu maisha yake. Wakati wakiwa juu angani wameanza kupaa meta chache tu ikasikika milipuko mikubwa ya mabomu huko chini kambini, 'Gorongosa Camp' inateketea kwa moto.
Dr.Anabella na Kachero Manu wakatazamana huku kila mmoja akitabasamu, alikuwa Kachero Manu amelipua mabomu aliyoyatega pale kambini kwa kutumia kitendambali (rimoti) ya mkononi mwake aliyovaa kama saa mkononi. Kiwingu kizito cha moto mwekundu kilitanda kuizunguka kambi ya Gorongosa usiku huo utasema siku ya kiama ndio imetoka. Kambi hiyo iliteketezwa kabisa bila kusaza kitu chochote.

SURA YA KUMI NA NANE
Mwisho wao Mafioso wa Cabo-Delgado umewadia
Soko la Baraca maana yake ni soko la vitu vya bei rahisi. Hili soko lipo katikati ya Mji wa Pemba kilometa takribani kama 2 tu kutokea barabara ya pwani (Coastal Road). Ni soko ambalo wakati wote limefurika limefurika Wafanyabiashara na wateja wao. Sokoni hapo ni maarufu pia kwa bidhaa za vinyago vya Kimakonde vya kila sampuli ikiwemo na bidhaa za baharini. Ni soko ambalo aghalabu utakutana na watalii wa kutoka nchi za ng'ambo kama China, Japani, Marekani na mataifa mengineyo ya kigeni wakiwa wametingwa kujitafutia zawadi za bidhaa asilia za kurejea nazo nchini kwao.
Waswahili wanasema kila kwenye msafara wa mamba na kenge nao hawakosekani, kwani katika harakati hizi za soko la Baraca za watu kujitafutia riziki zao za halali za kujiendeshea maisha kwa ajili yao na familia zao, kampuni ya "Monte Branco Ltd" nao walijichomeka katika eneo hili kwa kuwekeza kiwanda cha daraja la kati cha kusindika korosho, lakini ndani yake ilikuwa ni ofisi yao kuu ya kupanga mipango haramu yote ya kuhujumu nchi ya Msumbiji. Chini ya kiwanda inasemekana kulikuwa na ofisi za wapanga madili na wizi wa kila aina ambao walikuwa wanalipwa mishahara minono na mmiliki wa kampuni Bwana Alfredo.
Dr.Anabella ameshawahi kupelekwa huko chini ya kiwanda zaidi ya mara moja na mchumba wake Inspekta Jenerali Mark enzi mapenzi yao yamepamba moto. Mark katika kutaka kujionyesha kuwa ni mtu muhimu sana mbele ya Bwana Alfredo, siku ya kwanza alimchukua Dr.Anabella usiku wa manane siku ambayo Dr.Anabella alikuwa na zamu ya usiku katika hospitali ya kiwandani hapo akampeleka huko kwenye mahandaki chini ya kiwanda kumtembeza. Yalikuwa ni mahandaki yenye maofisi na chumba zenye starehe zote na mahitaji yote muhimu yanapatikana. Milango yake ilikuwa ni ya kufunguka kwa rimoti inayofunguliwa na namba za siri maalumu. Inspekta Mark alimdanganya Dr.Anabella kuwa anazitumia ofisi hizo za siri kupangia baadhi ya operesheni dhidi ya wahalifu.
Kiwandani hapo ndio palipangwa kufanyika mkutano wa Mwisho ambao utahitimisha uhai wa Kachero Manu, na kutoa onyo kali kwa wote wenye kufuatilia nyendo za Bwana Alfredo katika biashara zake za rubi na nyinginezo.
Mkutano ulipangwa uanze saa 4:00 kamili usiku, huku ukumbi ulikuwa umepambwa vikorombwezo vyote muhimu kwa mahitaji ya mkutano huo muhimu. Na washirika wote wa Bwana Alfredo, Mafioso wenzake kutoka Ureno na Afrika ya kusini walikuwa wameshawasili Pemba tayari kwa mkutano. Wengi walikuwa ni vigogo wana hisa wa kampuni na watendaji wakuu wa shughuli za kila siku za kampuni. Inspekta Jenerali Mark Noble alikuwa hatulii kama mbwa koko jike mwenye joto anayehitaji kupandwa. Alikuwa kama mtu mwenye mazonge yanayotokana kuelemewa na majukumu. Yeye kama akiwa Afisa Usalama Mkuu wa kampuni na kiongozi wa kikundi cha mateso cha "NACATANAS" alikuwa anahaha kuhakikisha mambo yanaenda kama yalivyopangwa bila kuharibiwa na mtu yoyote.
Lakini kilichokuwa kinamnyima raha ni kitendo cha helikopta kutokea Gorongosa kambini kuchelewa kufika Pemba. Alikuwa amempa maagizo Bob Chinanga ya kuhakikisha wanafika Pemba ifikapo saa 2:00 usiku. Sasa muda huo wa saa 3:15 usiku muda ukiwa unayoyoma haonekani Bob Chinanga wala wasaidizi wake. Mbaya zaidi ilikuwa mwanzoni anawasiliana na rubani na kule kambini lakini sasa alikuwa akipiga simu zote hazipatikani kabisa.
Kijasho chembamba kikaanza kumtiririka usoni na kwenye makwapa ya mikono yake jasho jekejeke likawa linamtiririka. Kengele ya hatari ikagonga kichwani mwake kuwa huenda Kachero kawazidi nguvu. Lakini kwa upande mwingine anajipa matumaini haiwezekani mtu mmoja aweze kuteketeza kikosi kizima cha zaidi ya watu elfu na ushee na kama akiweza basi itakuwa ni zaidi ya miujiza hashara ya Mtume Musa kwa Farao alipoenda kuwakomboa wana wa Israeli.
Inspekta Jenerali Mark Noble alikuwa ameshachoshwa na maisha haya ya mikiki mikiki. Aliweka nia na adhima ya kuacha kazi katika idara ya Polisi ya Msumbiji, kisha pia astaafu kazi kutoka "Monte Branco Ltd" kazi ambayo ilishakuwa hatarishi kwake. Ambapo suala la kupoteza uhai ilikuwa ni dakika sifuri. Alipanga achukue mafao yake kisha aondoke na mchumba wake Dr.Anabella kwenda kuishi kwenye visiwa vya Madagascar. Kwa mafao yake atakayopewa na Bwana Alfredo yalimpa jeuri na kiburi cha kuweza kuishi nchi yoyote ya Kiafrika bila kufanya kazi kwa muda hata wa miaka 50.
Inspekta Jenerali Mark akiwa amezama kwenye dimbwi la mawazo nje ya sehemu ya kuegeshea magari akiwa anawasubiri akina Bob Chinanga akasikia mlio wa simu yake unaita akaanza kupagawa. Akadhani anataka kuulizwa kuhusu ujio wa Kachero Manu. Ulikuwa ni mlio maalumu kwa ajili ya Bosi wake Bwana Alfredo, akajidhania kama yupo ndotoni maana hakutegemea kupokea simu ya Bwana Alfredo katika kipindi kigumu kama hiki. Alipoitoa simu yake akaipokea huku vidole vinatetemeka kama mlevi gongo.
"Habari za siku BIG BOSS" alisema Mark kwa sauti ya kujifaragua na kujilazimisha furaha. "Njoo ofisini mara moja kabla ya kikao nina mazungumzo nyeti na wewe...!" kisha kabla ya kujibu kitu chochote ikawa tayari simu imeshakatwa na Bwana Alfredo. Moyo wa Mark ukalipuka, na kuanza kwenda mbio kama mwanariadha anayeshindania medali ya dhahabu katika mbio za meta 100 moja. Akapiga moyo konde kuwa liwalo na liwe ngoja aende akamsikilize Bosi wake.
Akaanza kutembea kuelekea kwenye ofisi ya Bwana Alfredo iliyoko chini ya kiwanda kwenye handaki kwa kupitia kwenye maegesho ya magari, huku anajifanya kutikisa funguo za gari yake kupotezea hofu yake kuonyesha anajiamini. Lakini mawazoni alikuwa anajiambia leo kazi ipo kusuka au kunyoa.
Nomaaaaaaaaaaaaaaa

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
 
CABO-DELGADO-PART 39


Dr.Anabella akili yake ilifanya kazi haraka sana baada ya kukataliwa kuingia pale getini. Alifahamu taarifa zake za usaliti zitawafikia wakubwa zake na haitachukua muda atakamatwa kilaini. Hivyo moja kwa moja alikimbilia kwenye ofisi ya mchumba wake Inspekta Mark Noble. Alipoingia alimkuta Katibu Muhtasi wake Edina ameinamia kompyuta anaandika andika nyaraka mbalimbali.
Katibu muhtasi Edina na Dr.Anabella walikuwa wanafahamiana kitambo hasa kutokana na Dr.Anabella kuja ofisini kwa Mark mara kwa mara. "Samahani naingia ofisini kwa Mark kuna nyaraka za kumsafirishia mgonjwa, Mark kanielekeza nizifuate huku, zinahitajika haraka sana" aliomba Dr.Anabella kwa yule sekretari. Bila kipingamizi alijibiwa "hamna shida shemeji ingia tu kuwa na amani tu bila samahani, unataka nikuzuie kesho nikute barua ya kuachishwa kazi" wote kwa pamoja wakaangua kicheko cha nguvu, huku Dr.Anabella akielekea kufungua mlango. Dr.Anabella alitumia mwanya huo huo kujipenyeza ofisini kwa Mark.
Alipoingia moja kwa moja akaelekea kwenye kabati la mtoto wa meza karibu na kiti cha Mark, akavuta droo akautana na funguo nyingi pamoja na rimoti ndogo rangi nyeusi akaibeba akaihifadhi kwenye koti lake kisha akakizunguka kiti cha Mark. Akavuta kwa mbele kabati dogo la kuwekea mafaili ya taarifa za kipolisi alizokuwa anazishughulikia na vitabu mbalimbali.
Chini ya lile kabati kulikuwa na mfuniko wa chuma kama wa kufunikia chemba za choo. Akazitoa marumaru zilizoegeshwa juu ya ule mfuniko akaziweka pembeni. Akavuta ule mfuniko ukafunguka kisha akaingia kwenye shimo lile mpaka alipogusa ngazi ya kwanza ya kushukia chini akarudishia ule mfuniko vizuri kisha akaanza kuteremka ngazi kuelekea kwenye ofisi ya Mark ingine ambayo ipo chini ya handaki. Kwa msaada wa tochi ya simu yake akawa anashuka kwa haraka. Alipofika ngazi ya mwisho akazima tochi yake akajibanza dakika moja kuangalia kama kuna mtu yoyote, bahati ilikuwa kwake. Hakukuwa na mtu yoyote na korido nzima akawa akitembea taa zinawaka wenyewe kwenye korido.
Kulikuwa na mfumo wa kuleta mwanga pindi zinapohisi kuna binadamu anatembea. Akafika mpaka kwenye ofisi ya Mark ambayo ilikuwa ipo mkabala na ofisi ya Bwana Alfredo. Alipofika mlango akatoa rimoti mfukoni mwake akaanza kubonyeza bonyeza tarakimu za siri haikuchukua muda mrefu mlango ule uliotengenezwa kwa madini ya "aluminium" ukaachia ukaa wazi akaingia akaufunga tena kwa rimoti.
Kisha akaelekea kwenye runinga kubwa iliyopo ndani ya kile chumba akawasha umeme ukutani. Akaruhusu umeme uingie kwenye runinga hiyo kisha akaanza kuona kila kinachoendelea kwenye ukumbi wa mkutano mubashara.
Akashtushwa sana na alichokishuhudia kwa macho yake. Alikuwa hasikii sauti yao kinachozungumzwa mle ndani ya chumba cha mkutano ila aliwaona washirika wake, Kachero Manu na Komandoo "JS" wakiwa wamefungwa kwenye viti kwa kutumia mikanda, wakiwa hawana matumaini ya kujiokoa wao wenyewe.
Alivyowasoma wale walinzi wa ukumbi ndani ya muda mfupi namna walivyojipanga matumaini ya kuwaokoa yakaanza kufufuka upya.
Haraka haraka akatoka nje ya chumba cha Mark bila hata kuzima Televisheni. Akakimbilia ngazi za kupanda juu kuelekea kwenye chumba cha mkutano kutokea kule kwenye handaki akiwa na hamasa zote. Huku bastola yake ikiwa mkononi tahadhari kwa lolote litakalotokea, akaanza kupanda ngazi kwa kasi ya ajabu.

Kachero Manu alizindukia ukumbini akijikuta amemwagiwa maji ya baridi akiwa amefungwa kwenye kiti, pembezoni mwake yupo Komandoo "JS" nae akiwa amefungwa mikanda.
"Kachero Emmanuel Joseph" na "Komandoo Jacob Steven" karibuni sana kwenye mkutano ambao mlikuwa mnatamani mhudhurie, nadhani maombi na dua zenu zimekubaliwa na Mungu mmefika salama" alifungua mkutano huo Bwana Alfredo mwenyewe akiwa na kiko yake pembeni ameikamatia kwa mkono wa kushoto.
Kachero Manu na Komandoo "JS" wakatazamana wakionyeshwa kushangazwa kwa wao kujulikana majina yao kiufasaha. Walichokuwa hawakijui ni kuwa kulikuwa na "CCTV-Camera" zenye uwezo wa kuchukua matukio yote pale kiwandani kwa ufasaha. Hivyo ilivyojulikana kuwa kiwandani pamevamiwa, zilienda kuchukuliwa picha za maeneo yote wakaonekana namna walivyoingia, kisha picha za Kachero Manu na Komandoo "JS" zikatumwa kwa washirika wao Tanzania yakaja majibu ya utambuzi wa Kachero Manu lakini Komandoo "JS" hatambuliki. Zikatumwa picha ya Komandoo "JS" kwa washirika wao wa Msumbiji yakaja majibu ya kila kitu kinachomhusu Komandoo "JS".
"Pia nachukua fursa hii kukupongeza Komandoo Jacob Steven kwa kuteuliwa kwako kuiongoza Idara ya Usalama wa Taifa nchi ya Msumbiji, najua kuwa huna hizo taarifa kutokana na kujishughulisha na mambo yasiyokuhusu, mtaka nyingi nasaba hupata mengi majanga hivyo nasikitika huo uteuzi wako na pongezi zako zitaifikia maiti yako. Kesho asubuhi utaokotwa ukiwa maiti na hilo litakuwa ni onyo takatifu kwa wote wanaojifanya wazalendo wa nchi ya Msumbiji" alisema Bwana Alfredo kwa mbwembwe huku anaanza kuvuta kiko chake.
"Mwisho wako na vibaraka wenzako wa wakoloni Bwana Alfredo umefika, Msumbiji huru yenye kujitoa kwenye makucha ya wanyonyaji inakuja. Msumbiji yenye neema ya uchumi wa gesi, mafuta na madini inakuja, hata kama utatumaliza sisi lakini tutakuwa tumekufa kishujaa, aheri kufa mwili lakini mawazo yako yakawa hai vizazi na vizazi ...!" aliropoka Kachero Manu bila kupewa ruksa kwa kudakiza maneno kwa lengo la kupoteza muda ili kuangalia kama kuna fursa yoyote ya kujiokoa itajitokeza.
"Kelele wewe mbwa koko unaropoka bila kupewa ruksa ya kuongea ngoja tukutie adabu kidogo" alifoka Mark kwa hasira huku anamfuata Kachero Manu kwenye kiti chake kwa.
"Mark achana nae, daima mfa maji haachi kutapatapa hata ukimpiga ni kazi bure huyo ni maiti hai inayosubiri kutolewa roho tu" alisema Bwana Alfredo kwa sauti ya dharau. "Nyinyi ni waoga sana mnapambanaje na sisi hali ya kuwa mmetufunga mikono na miguu? mwanaume wa kweli hawi muoga kiasi hiki Bwana Alfredo, tambueni mshahara wa dhambi ni mauti mtakamatwa mapema iwezekanavyo " alisema Komandoo "JS", nae akijaribu kuvuta muda ili kuona kama kuna fursa yoyote ya kujiokoa itajitokeza.
Bwana Alfredo hakujibu kitu bali alikuwa anaangalia mlango wa mbele yake, alikuwa anaingia kipande cha mtu mrefu, amesokota rasta nywele zake, huku mkononi ameshika shoka kubwa limelowa damu damu iliyogandiana, kuonyesha sio shoka la kibisa ni shoka la kazi.
Mtu huyo alikuwa anatembea kwa mikogo analizungusha hewani shoka lake kwa mitindo tofauti tofauti kama Msolopagazi na Inkosikazi yake. Kachero Manu kwake sura hii haikuwa ngeni kwenye mboni zake za macho, akawa anajaribu kufikiria wapi alimuona huyu mtu. Lakini kutokana na maumivu ya kichwa anayohisi akashindwa kupata majibu ya fikra zake.
"Kachero Manu umefanya mauaji ya kikatili kwa Bob Chinanga, sasa rafiki yake kipenzi anaitwa "Nanga Boy" ameomba aje kutenganisha shingo yako kwa shoka yeye mwenyewe kulipiza kisasi cha rafiki yake" alisema Inspekta Mark Noble huku anacheka kicheko cha kebehi na dharau. Yule rafiki wa Bob Chinanga alikuwa anatokwa machozi ya uchungu mkali wa hasira. Kachero Manu akakumbuka yule jamaa alionana nae kambi ya mateso Gorongosa, ndio walimtesa yeye na Bob Chinanga.
Komandoo "JS" alikuwa ameinamisha kichwa chini kama kobe anayetunga sheria vile, huku Kachero Manu akiangaza angaza kwenye chumba kama mtu asiyekata tamaa akisaka fursa yoyote ya kujiokoa, akili yake ilikuwa inampa asilimia 98% kuwa ataokoka na asilimia 2% ndio ilikuwa inampa hofu ya kupata madhara.
"Ndugu wajumbe Kabla hatujaanza mkutano wetu hawa wawili wauwawe kikatili kwa shoka huku Mark nikikupa jukumu la kumtafuta hawara yako Dr.Anabella na kumpoteza haraka sana baada ya kikao hiki kama hatopatikana kwa haraka, jiandae kufa wewe kwa niaba yake kwa kosa la kutupandikizia kirusi kwenye kundi letu...! " alitoa amri Bwana Alfredo kwa sauti yenye hasira na hamaki kali akionyeshwa kuchukizwa na Mark.
"Sawa Bosi wangu nitatekeleza kwa uaminifu mkubwa" alijibu Inspekta Mark huku anatetemeka sura yake imemsawijika vilivyo, akijuta kumfahamu Dr.Anabella.
"Salini sala zenu za mwisho kabla Nanga Boy hajavunja shingo zenu" alisema Inspekta Jenerali Mark huku akimuangalia Nanga Boy ambaye alikuwa akisogelea kwenye kiti alichofungwa Kachero Manu. Alipofika karibu yake kabisa akanyanyua shoka juu kusubiri amri ya kukata shingo ya Kachero Manu. Ukumbi mzima ukapewa amri ya kusimama, kisha Mark akasogea karibu ya Nanga Boy, akaanza kuhesabu ili akifika tatu Nanga Boy ashushe shoka shingoni.
"Moja, mbili, taa....." kabla hajamalizia kuhesabu tatu, ghafla mlango wa nyuma ya kiti cha Bwana Alfredo ukavunjwa kwa kishindo kikubwa, huku Kachero Manu akitumia nguvu zake zote kujitupa pembeni. Shoka lile lililotupwa na "Nanga-Boy" likatua kwenye kingo ya kiti na kukata mikanda iliyomfunga Kachero Manu.
Ambapo bila kuzubaa Kachero Manu akaanza kujifungua mikanda iliyobakia. Risasi ya kutoka kwa Dr.Anabella ilitua sawia kwenye bega la mchumba wake Mark na kusababisha bastola yake kumponyoka. Kachero Manu akawa kashajifungua tayari. Kutupa macho pembeni akamuona Inspekta Jenerali Mark anajivuta kwa kutambaa kuifuatilia bastola yake iliyomponyoka huku damu zinamchuruzika.
Kachero Manu hakumkawiza akamchapa teke la begani mahali pale pale alipopigwa risasi na Dr.Anabella kama kulitonesha jeraha tena, akawa anagugumia kwa maumivu makali. Kisha akaiwahi yeye ile bastola sasa ikawa mikononi mwake. Akawa anamkinga nayo Dr.Anabella asishambuliwe ambaye alikuwa anamalizia kumfungua mikanda Komandoo "JS". Tayari, Nanga Boy alikuwa anakimbilia upande wa Bwana Alfredo kwenda kuwalinda baadhi ya viongozi.
Kabla Nanga Boy hajaifikia meza kuu ya viongozi, Bwana Alfredo akamrushia bastola, ghafla wakashtukia Dr.Anabella anagugumia kwa kali sauti ya maumivu, "Maaaamaaaaah naaa..kuf............ aaaaaaaah....!" alikuwa amepigwa risasi ya tumboni na Bwana Alfredo, akakaa chini kwa kupweteka.
Komandoo "JS" akawa anatambaa chini kwa chini akiwa anamvizia Bwana Alfredo huku Kachero Manu akiwa tayari ameshawachakaza kwa risasi Mafioso kama 6 kitendo ambacho kilimgutusha Bwana Alfredo na kujiona yumo hatarini. Huku mkono wake wa kulia akiwa amebeba faili rangi nyeusi, na mkono wa kushoto ana bastola yake na shingoni amening'iniza "USB-flash" akawa anamwaga risasi ovyo huku anaelekea upande wa kulia wa jengo.
Alipofika kwenye makutano ya kuta mbili, akarusha risasi iliyompata Inspekta Jenerali Mark kwenye usawa wa moyo wa Mark. "Aaaaaaaah.......My Boss you are killing me Whyyyyyy.....!" alilalama Inspekta Jenerali Mark kwa uchungu mkubwa wa maumivu. Risasi ambayo ilipoteza kabisa uhai wa Mark, asingeweza kupona hata kama apelekwe kwenye hospitali bora kama ile ya Apollo iliyopo nchini India.
Bwana Alfredo alikuwa anathibitisha ukomavu wake kwenye ujasusi hakutaka Mark akamatwe kirahisi aweze kuropoka siri zake. Kisha akatoa kitu kidogo mfukoni mfano wa rimoti ghafla kuta mbili zikatengana akatokemea na kuta mbili zikajifunga. Ilikuwa ni kama kiini macho kinafanyika mbele yao kitu ambacho hawakukitegemea. Ilikuwa ni jambo la sekunde kadhaa tu.
"Anatooo...ro...ookaaa...muwa...aaaa.... hini kw... eny....e... maaaeg...esh... o... ya maag...ariii...!" alitoa maelezo Dr.Anabella kwa sauti ya shida ya maumivu. Komandoo "JS" akampa ishara Kachero Manu kuwa anamfuatilia Bwana Alfredo yeye apambane na Nanga Boy.
Nanga Boy akajikuta bastola yake imeishiwa na risasi, Kachero Manu akatupa chini bastola yake akampa ishara wapambane kwa mikono. Ikawa wameshasogeleana kama mahasimu wawili wa kwenye masumbwi ni fursa adhimu ambayo Kachero Manu alikuwa anaitamani ya kulipiza kisasi cha mateso ya kifo aliyopewa kambini na mbwa hawa "Bob Chinanga" na "Nanga Boy".
Alikuwa ni Nanga Boy kuwa wa kwanza kutupa konde la mkono wa kushoto likatua sawia kwa Kachero Manu usawa wa shingo yake. Ilikuwa ni katika harakati za kujaribu kukwepesha konde hilo lisitue kwenye taya zake likaharibu mpangilio mzuri wa meno yake. Nanga Boy akarusha kombora la teke kali la usawa wa mbavuni, bahati nzuri Kachero Manu akakaza misuli ya tumboni. Teke hilo lilimyumbisha Kachero Manu akafanikiwa kujizuia asianguke chini. Akajibu mapigo kwa kurusha teke la sehemu za siri za "Nanga Boy". Nae akawa mwepesi akawahi kulipangua kwa mikono yake, vinginevyo angekuwa mgumba maisha yake yote yaliyobakia.
Kachero Manu hakuwa na muda wa kupoteza na huyu "Nanga Boy" hasa ukichukulia mlengwa wao, Bwana Alfredo hawajamkamata bado, kashawatimulia vumbi. Hivyo akaanza kuruka ruka huku amekunja ngumi mithili ya BRUCE-LEE huku anarudi nyuma nyuma, Nanga Boy akapotea maboya akadhani kurudi nyuma nyuma Kachero Manu anamuogopa akawa anakuja mzobe mzobe ili ambebe Kachero Manu na ampigize chini.
Alivyombeba tu Kachero Manu akampiga na vifuti vya mikono juu ya utosi wa Nanga Boy, damu zikaanza kumchuruzika kama bomba, akamtupa chini. "Nanga Boy" akawa amelewa kutokana na kupoteza kwa damu nyingi kwa wakati mmoja ikawa kila anavyokuja, Kachero Manu anamkwepa, anakwenda kujigonga kwenye viti vya kwenye chumba cha mkutano. Mara ya mwisho baada ya kuona anachezewa hangaisha bwege na Kachero Manu, akaliokota shoka lake akawa anakuja nalo kwa kasi ampige nalo Kachero Manu huku anapiga kelele za kupandisha mori kama morani wa Kimasai aliyepewa ahadi ya kupewa mke kama akiua Simba.
Kachero Manu akasimama wima huku akiwa ameipanua kidogo miguu yake kupata uimara wa mwili. Alivyofika kushusha shoka lake, Kachero Manu akaudaka mkono wake na kuuzungusha kidogo tu, Nanga Boy alipiga yowe la nguvu. Mfupa wake wa maungio ya bega ulikuwa umechomoka begani, kirungu cha maungio ya mfupa begani kinaning'inia nje ya bega.
Hakumkawiza akamchota mtama akaangukia kisogoni chini ya sakafu, akawa anatupa tupa miguu ya kushoto na kulia alikuwa anakata roho.
Kachero Manu akapata nafasi ya kukimbilia kwa Dr.Anabella ambaye alikuwa yupo kimya kama amefariki vile. Alikuwa amezimia kutokana na kupoteza damu nyingi sana. Alichofanya ni kushika maeneo ya kifuani, akabinya kwa nguvu kwa kutumia vidole vyake akawa anasikia mapigo ya moyo kwa mbali. Akaenda kwenye simu ya mezani kwenye kila chumba cha mkutano na kupiga simu ya dharura ili gari la kubeba wagonjwa mahututi lifike kuwapeleka majeruhi hospitalini. Pia akapiga simu idara ya usalama Ikulu moja kwa moja waje haraka sana kuwakamata watuhumiwa, kisha akakata simu na kukimbilia nje kusaidiana na Komandoo JS.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom