Riwaya: "Cabo-delgado"-part 01

Riwaya: "Cabo-delgado"-part 01

RIWAYA: CABO DELGADO-PART 21

SURA YA KUMI NA MBILI
"Mjue Daktari wa handaki la mateso"
Moja ya kazi ambayo ina miiko yake madhubuti hapa duniani ukiachilia kazi ya Ualimu basi ni kazi ya Udaktari. Ni kazi ambayo siku ya mwisho ya kuhitimu elimu hiyo, madaktari hula kiapo cha utii wa maadili ya kazi yao.
Kiapo ambacho huwa kinawafunga kutenda kazi zao kwa kufuata weledi wa kazi yao hiyo kwa kuwataka kuwahudumia wagonjwa wao bila ubaguzi, wawe na moyo wa huruma na uvumilivu na kutanguliza kuokoa uhai wa wagonjwa wao kwa gharama yoyote.
Ni kazi ya wito ambayo hautakiwi kutanguliza maslahi yako binafsi, kazi ya udaktari ni kama vile umechagua kifo ni bora kwako kuliko uhai, ndio maana ukitokea mlipuko wa ugonjwa wowote wa hatari wa kuambukiza kama "Ebola", "Covid-19" na mengineyo huwezi kusikia madaktari wametoka nduki na kuwatelekeza wagonjwa wao hospitalini.
Sasa ukiona mtu ni daktari kama alivyo Dr.Anabella anashirikiana na wahalifu kwa kutoa huduma kwa wagonjwa na amepewa Cheo kama "Daktari wa Mateso", kengele ya tahadhari lazima ilie kichwani mwako.
Lazima utajiuliza zaidi ya mara mbili, "huyu daktari anaijua kweli miiko ya kazi yake au anatanguliza mbele maslahi yake binafsi au nini kimemsibu mpaka anashirikiana na wahalifu?". Lakini kumbe mazonge na maswahibu tunayokumbana hapa duniani huwa kuna wakati yanawabadilisha watu wema kuwa waovu na waovu kuwa wema.
Mfano wapo watu hapo zamani walikuwa majambazi, walawiti, wanyang'anyi lakini wakarejea kumtumikia Mungu wao baada ya kupatwa na ajali, au magonjwa yasiyotibika. Na wapo watu ambao zamani walikuwa swalihina sana, kwenye nyumba za ibada hawakosekani, wanashinda mahospitalini kuangalia wagonjwa, wanatoa zaka na sadaka kila wakati lakini misukosuko ya walimwengu iliyowasibu ikawabadilisha na kuwafanya wawe watu waovu maishani, Ibilisi mwenyewe ambaye ni Shetani Mkuu anasubiri nyuma.
Nakama na misukosuko aliyokumbana nao maishani mwake, Dr.Anabella pamoja na familia yake ndio iliyomsababisha ajiunge na kundi hili ovu na katili la NACATANAS linaloongozwa na Inspekta Jenerali Mark Noble.
Dr."Anabella Julio" ni mzaliwa wa kijiji cha Nthoro katika wilaya ya Montepuez, nchini Msumbiji. Alizaliwa mwaka 1979 miaka minne tokea kupatikana uhuru wa Msumbiji. Alimaliza masomo yake ya udaktari wa binadamu katika chuo kikuu cha "The Eduardo Mondlane University" kilichopo ndani ya viunga vya Jiji la Maputo, nchini Msumbiji. Hicho ndio Chuo Kikuu kikubwa zaidi nchini Msumbiji kikiwa na uwezo wa kudahili wanafunzi takribani elfu 40 katika kila mwaka wa masomo.
Baba yake mzazi, Mzee "Julio Munambo" alikuwa ni mkulima mdogo wa mihogo na korosho. Ni Mzee ambaye amewahi kuishi Tanzania kwa miaka 13 mtawalia katika kambi ya wakimbizi ya Rutamba mkoani Lindi. Hiyo ilikuwa ni kati ya mwaka 1971-1984.
Alitoroka Msumbiji kama mkimbizi na kuja kuishi Tanzania, kipindi cha vita baina ya Wareno na Wapigania Uhuru wa FRELIMO. Baada ya uhuru wa Msumbiji uliopatikana mwaka 1975, Mzee Mnambo alikuwa ana mipango ya kurudi nyumbani akalijenge Taifa lake changa. Ila vilipoibuka vita ya wenyewe kwa wenyewe baada ya Uhuru kati ya vyama hasimu nchini Msumbiji, chama cha RENAMO na FRELIMO akakata shauri la kuendelea kubakia Tanzania mpaka amani ya kweli ipatikane nchini Msumbiji.
Dr.Anabella, kifungua mimba wa Mzee Mnambo, akawa ni mhanga wa sarakasi zisizokoma baina ya FRELIMO na RENAMO. Akajikuta anazaliwa na kukulia ukimbizini nchini Tanzania bila hata kuwahi kunusa harufu ya udongo wa nchi yake ya asili. Sarakasi ambazo zilizaa Mkataba wa NKOMAT na kusababisha Dr.Anabella anapelekwa nchini Msumbiji na baba yake kwa mara ya kwanza katika maisha yake.
Chama cha RENAMO kiliundwa mwaka 1975 kilikuwa kikipinga sera za ukomonisti za chama tawala cha FRELIMO. Chama hiki kilianzishwa kwa msaada wa serikali ya wazungu wa Rhodesia (Zimbabwe) na serikali ya makaburu wa Afrika ya Kusini.
Lengo la wazungu kuanzisha na kuipa misaada RENAMO ilikuwa ni kuivunja nguvu serikali ya Msumbiji inayoongozwa na FRELIMO kuwasaidia wapigania uhuru wa Afrika ya kusini na Zimbabwe. Baada ya uhuru yakaibuka mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini Msumbiji kati ya chama cha FRELIMO na RENAMO, mapigano ambayo yalikuwa ni janga la kimataifa kwa wapenda amani na uhuru wote duniani.
Miundo mbinu kama shule, vyuo, hospitali na barabara ziliharibiwa, wananchi waliuliwa na kuchinjwa ovyo kama kuku, huku wengine wakiambulia ulemavu wa maisha na maelfu kwa maelfu ya wakazi wa Msumbiji hasa waishio kaskazini walitorokea nchini Tanzania kama wakimbizi.
Duniani tumepata kuona na kusikia vikundi mbalimbali vya waasi ambao ni wakatili kama Talebani wa kule nchini Afghanistani, au Al-Shabaab wa kule Somalia na makundi mengineyo lakini hawafikii hata robo ya ukatili wa askari wa RENAMO, waasi hao walikuwa kiboko yao.
Katika baadhi ya simulizi za kuelezea ukatili wao zinasema ulikuwa ukikamatwa na waasi wa RENAMO kama ukiwa adui yao unaulizwa swali kwa lugha ya Kimakonde "ulambela kununa au kusunala"? (Unachagua kununa au kucheka). Ukichagua kununa unatobolewa mdomo wa juu na wa chini kisha unafungwa na kufuli, ukichagua kucheka unakatwa midomo ya juu na chini.
FRELIMO ilifanya makosa kadhaa ya kiufundi yaliyowafanya wakazi wa upande wa Kaskazini mwa nchi kuiunga mkono RENAMO licha ya kwamba walitambua kuwa sio kundi sahihi kwao. Moja ya makosa yaliyofanywa na FRELIMO baada ya nchi kupata uhuru ni kunyakua nafasi nyingi za juu za uongozi na kuwapatia watu wa kusini mwa Msumbiji, hivyo watu wa kaskazini kujiona kama ni watoto wa kambo. Wametengwa ndani ya nchi yao waliyoipigania uhuru wake kwa kuvuja jasho na damu, kwa kupoteza uhai na mali zao.
Pia sera za Ukomonisti zilitekelezwa vibaya na baadhi ya viongozi wa FRELIMO. Mpaka ikafikia hatua baadhi yao kuamuru makanisa na misikiti ifungwe kwa kigezo cha kwamba Msumbiji ni nchi ya kisekula isiyo na dini yoyote. Maelfu ya viongozi wa dini walinyanyaswa na kuteswa mpaka wengineo kuikimbia nchi yao ya Msumbiji.
Zipo taarifa ambazo zinaenezwa sana na wafuasi wa RENAMO kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa FRELIMO alipata kuingia kanisani siku moja na nyundo yake mkononi inapepea hewani kama kishada. Kwa kutumia nyundo ile akavunjavunja 'Altare' siku ya Ibada ya Jumapili huku waumini wamejaa pomoni kanisani na kutangaza Msumbiji hairuhusu ibada zozote.
Mapigano kati ya makundi haya hasimu, FRELIMO na RENAMO yalizidi kushika moto zaidi mara baada ya Maafisa wa usalama wa serikali ya Msumbiji kumuua Bwana "André Matsangaissa" kiongozi mkuu wa RENAMO. Bwana Matsangaissa mwanzoni alijiunga na FRELIMO mwaka 1972 kisha baada ya uhuru mwaka 1975 aliajiriwa kama mwanajeshi akapewa cheo cha "Mfawidhi Mkuu wa Kikosi" (quartermaster).
Kituo chake cha kazi kilikuwa maeneo ya Dondo karibu na Beira, akihusika na manunuzi, uhifadhi na ugawaji wa vifaa vya jeshi. Baada ya muda mfupi tu akafukuzwa kazi akituhumiwa kwa wizi kisha akapelekwa jela ya Gorongosa.
Sasa mwaka 1977 kambi ya Gorongosa ikavamiwa na wazungu wa Rhodesia wakamtorosha Bwana "André Matsangaissa" wakaenda nae Rhodesia baadae akatangazwa kama mkuu wa kikundi cha RENAMO.
Kwa hiyo FRELIMO wakawa wanapambana na mtu ambaye anawajua nje ndani katika medani zao za kivita, ni kama kinyago walichokichonga wenyewe kinawatisha sasa.
Amani ya kwanza kati ya FRELIMO na RENAMO ilianza kupatikana tarehe 16 mwezi Machi mwaka 1984 kuliposainiwa mkataba maarufu unaitwa "NKOMAT ACCORD". Mkataba huu ulikuwa ni kati ya serikali ya Msumbiji ikiwakilishwa na Rais Samora Machel na Waziri Mkuu wa serikali ya kikaburu ya Afrika ya Kusini kipindi hicho Bwana P. W. Botha.
Huyu Kaburu Botha ndiye ambaye wazalendo weusi wa Afrika ya kusini wanamuita kwa jina la utani la "The great crocodile". Ile miaka ambayo watoto wa shule wanapigwa risasi hadharani 1976 huko Afrika ya kusini, na mpaka filamu maarufu ya Sarafina ikaigiza tukio hilo la kinyama, huyu Bwana mkubwa Botha alikuwa ndio Waziri wa ulinzi na baadae kuanzia mwaka 1984-1989 alikuja kuwa Rais wa Afrika ya kusini.
Huyu ndio ndio mhandisi aliyeufuma na kuusuka vilivyo mkataba wa NKOMAT. Mkataba huo uliweka matakwa ya serikali ya Msumbiji kuacha kusaidia wapigania uhuru wa Afrika ya kusini wa chama cha "African National Congress"(ANC), pia uliwataka serikali ya makaburu kuacha kuwapa msaada wa vifaa na pesa chama cha upinzani cha RENAMO.
Mkataba huu ulikuwa ni pigo takatifu kwa wapigania uhuru wa ANC na nchi zote zilizokuwa zinazosaidia kupatikana kwa uhuru wa Afrika ya kusini.
Siku ya kusainiwa kwa mkataba huo, Marais wote wa SADC kuanzia Mwalimu Nyerere, Keneth Kaunda na wenzao walisusia mkataba huu hawakutokea kwenye sherehe licha ya kwamba Rais wa Msumbiji Bwana Samora aliwapa mualiko.
Waliona ni kama vile Rais Samora amewasaliti, amekuwa mbinafsi kwa kujali maslahi yake kwa kuamua kukaa meza moja na adui yake wanafaidi mapochopocho na mahanjumati wakati wapigania uhuru wenzao wa nchini Afrika ya Kusini wanateseka.
Baada ya mkataba wa NKOMAT kusainiwa, Mzee "Julio Martine Munambo", baba wa Dr.Anabella aliamua kurejea nchini Msumbij. Akiambatana na mkewe, Binti yake mkubwa, Anabella, na wadogo zake Anabella wakiume wawili, Munambo Jr na Athanas. Hawa watoto wote walikuwa wanarejea Msumbiji kwa mara ya kwanza, kwa maana walizaliwa katika kambi ya wakimbizi hawaijui hata Msumbiji inafananaje kimuonekano.
Mzee Julio Munambo akaanza maisha mapya katika kijiji chao cha asili ya mababu zake cha "Nthoro".
Kipindi hicho kulikuwa na watu wachache vijijini, wengi wao wakiwa wamekimbia kutokana na mfumo ulioachwa na RENAMO vijijini unaoitwa "Gandira". Mfumo huo ulitaka vijiji viwe vinazalisha chakula kwa ajili ya wapiganaji wa RENAMO, pia wanakijiji wahusike kusafirisha bidhaa na silaha za RENAMO na pia wanawake wa kijiji baadhi yao wawe ni watumwa wa kingono wa wanajeshi wa RENAMO.
Kipindi hicho cha miaka ya 1980's chama cha RENAMO kilikuwa kina nguvu zaidi katika Majimbo ya Kaskazini na Mashariki kuliko hata FRELIMO. Sasa huu mfumo wa Gandira ulikuwa unasababisha baadhi ya wanakijiji wakimbilie tena Tanzania hasa msimu wa kilimo kwenda kufanya vibarua katika mashamba ya wanakijiji wa mpakani ili wafaidike na jasho lao.
Watanzania walikuwa wakiwapata hawa vibarua wanashangilia maana "Wamakonde" wa Msumbiji kwa uhodari wao wa kulima waliwapa lakabu ya "trekta", hawachoki kwa haraka wakiingia shambani.
Katika mazingira magumu hayo hayo aliyoyakuta Mzee Julio alihamasisha na kuamsha ari mpya na nguvu mpya kwa wanakijiji wenzake akiwaelekeza namna nzuri ya kuboresha maisha yao na kuwa bora kupitia kilimo. Hasa ukichukulia ametoka kuishi maisha ya kambini ambayo ni maisha ya nidhamu na utiifu kama shuleni.
Pia alijifunza mfumo wa uendeshaji wa vijiji vya Ujamaa na Kujitegemea kutoka Tanzania alipoishi kwa muda mrefu hivyo mpaka kufika mwaka 1992 wakati wa mkataba wa kusitisha mapigano ya yenyewe kwa wenyewe kati ya FRELIMO na RENAMO unasainiwa. Ndani ya muda mfupi kwa hamasa na ushawishi wa Mzee Julio Munambo, kijiji cha "Nthoro" kikawa ni kijiji cha kupigiwa mfano kwa katika namna ya kujiletea maendeleo yao, kati ya vijiji vyote vya Jimbo la Cabo-Delgado.
Kwa umoja wao walijenga shule ya msingi hapo hapo kijiji kwao, shule ambayo ndio Dr.Anabella alianzia hapo darasa la kwanza mwaka 1989 na kumaliza 1995. Mwanzoni masomo yalikuwa magumu kwa Dr.Anabella kwa sababu yalikuwa yanafundishwa kwa lugha ya Kireno na sio kwa lugha yake ya asili ya kimakonde, lakini baada ya muda mfupi alikuwa anaongea kireno kizuri kana kwamba kazaliwa katika viunga vya "Lisbon" huko nchini Ureno.
Alipomaliza elimu yake ya msingi akafaulu kwenda kusoma sekondari katika shule ya sekondari Montepuez. Alisoma hapo kwa muda wa miaka mitano mfululizo. Kwa mfumo wa elimu ya nchi ya Msumbiji, elimu ya sekondari imegawanywa mafungu mawili, kidato cha kwanza mpaka cha tatu mwisho halafu ukifaulu unaendelea kidato cha tano na cha sita kwa muda wa miaka miwili.
Alivyomaliza sekondari alifaulu vizuri sana, alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi kumi bora kwa jimbo zima la Cabo-Delgado na akiwa ni wa kwanza katika wilaya yake ya Montepuez. Siku ya kutoka kwa matokeo na kujulikana kuwa binti yao mpendwa Anabella kachaguliwa Chuo kikuu bora kuliko vyote nchini Msumbiji cha 'Eduardo Mondlane' kusomea Shahada ya Udaktari wa Binadamu "Doctor of Medicine" ilikuwa ni hoihoi, shangwe, nderemo, vigeregere na vifijo kijijini kizima.
Walimuona kama ndio mkombozi wao kielimu atakayekuja kuwatoa kwenye utumwa wa umasikini uliotopea na kuwaletea maisha bora kwa kutumia kipawa chake cha elimu.
Furaha ya kusomea udaktari Dr. Anabella ilitumbukia nyongo kuanzia mwaka 2008 akiwa ndio yupo mwaka wa mwisho wa masomo yake. Hiyo ni baada ya kuwa wazazi yake hawapatikani mara kwa mara kwenye simu ya mkononi kama alivyozoea kuwasiliana nao. Na siku akibahatika kuongea na baba yake basi alikuwa anaonekana ni kama mtu mwenye wasiwasi mwingi. Kama vile kulikuwa kuna kitu wanamficha binti yao wakihofia wasije wakamchanganya kwenye masomo yake.
Subira yavuta heri, Aliweka nia thabiti moyoni mwake, Dr. Anabella kuwa akimaliza masomo yake ataenda kijijini kwao kiguu na njia kutafiti nini kinachowasibu wazazi wake haswa. Na kama akikuta kuna matatizo yasiyotatulika kwa haraka itabidi awachukue wazazi wake na kwenda kuishi nao katika Jiji la Maputo. Huko ndio alipanga aendeshe maisha yake baada ya kumaliza Chuo Kikuu. Ingawa alijua ni ngumu sana kwa baba yake mzazi kukubali kuondoka kijiji cha Nthoro, kijiji ambacho ameshiriki kwa asilimia nyingi kukipa hadhi inayoonekana leo akiwa kama muasisi.
Alikuwa anatamani arudi kijijini mara kwa mara ila umbali ulikuwa ni kikwazo kikubwa. Kutoka Maputo mpaka Montepuez kwa usafiri wa gari ni zaidi ya saa 35, na kulipa nauli ya ndege ambayo angetumia saa 2 tu hakuwa nazo hizo pesa, hivyo ikawa kila mwaka anarudi mara moja nyumbani kusalimia familia yake.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA: CABO DELGADO-PART 22




"Kiu ya kisasi ya Dr.Anabella"
Zikiwa zimebaki wiki mbili tu Dr. Anabella arejee nyumbani kwao kijiji cha Nthoro akiwa tayari ni mhitimu wa fani ya Udaktari, furaha yake ilikuwa haielezeki. Alikuwa anawaza furaha ya wazazi wake jinsi itakavyokuwa. Akawa anavuta picha sherehe kubwa atakayoandaliwa na kijiji ya kuhitimu masomo yake.
Akakumbuka sherehe yake ya unyago maarufu kama "Chiputu" aliyofanyiwa kipindi ana miaka 12 namna ilivyopambwa na ngoma za utamaduni za "Mapiko" zilizorindima wiki nzima. Na akakumbuka namna vyakula vya kila aina na nyama za kila aina kama panya, nyoka, nguruwe na vinginevyo vililiwa siku hiyo na kusazwa.
Nikumegee siri moja ndugu msomaji, Wamakonde wa Msumbiji wana tofauti kidogo na Wamakonde wa Tanzania. Wamakonde wa Msumbiji wengi wao hawachagui nyama ya kula wana msemo wao wa kimakonde kuwa "chiumbile Nnungu chakumemena" wakimaanisha "kila alichokiumba Mungu kinatakiwa kiliwe".
Dr.Anabella ilikuwa akipita mitaa mbalimbali ya jiji la Maputo kama mitaa ya "Bustani ya Tunduru", mitaa ya stesheni huko kote alikuwa hakosi kununua zawadi ndogo ndogo kama za nguo kwa ajili ya wazazi na ndugu zake wa karibu ambao bado walikuwa wanaishi kijijini ambao hawakuendelea na masomo ya juu kama yeye Dr.Anabella.
Ilikuwa tarehe 13/04/2009 itabaki kuwa ni siku ya kumbukumbu mbaya sana kwa Dr.Anabella mpaka siku anakufa. Ni siku ambayo iliamsha kiu yake ya kulipa kisasi kwa wabaya wake wote. Siku hiyo aliamka na taarifa mbaya sana kutoka kijijini kwao Nthoro.
Usiku wa kuamkia siku hiyo alikuwa zamu ya usiku kucha katika hospitali ya "Maputo Central Hospital" alipokuwa anafanya mazoezi ya vitendo ya Udaktari, hivyo hakupata muda wa kuangalia taarifa ya habari kwenye runinga. Aliporudi nyumbani alfajiri moja kwa moja akapitiliza chumbani kuuchapa usingizi.
Alipoamka asubuhi baada ya kuoga wakati anafanya maandalizi ya chai ya asubuhi akaweka televisheni ya Afrika ya kusini ya "SABC NEWS" ndipo alipoona habari ya kusikitisha ya mauaji ya baadhi ya wanakijiji wa kijiji cha Nthoro, waliouwawa kwa kukatwa katwa mapanga na viungo vyao kukusanywa kama nyama za buchani.
Akataharuki na kuamua kupiga simu kijiji kwao ili kufahamu usalama wa familia yake, ikawa namba za wazazi wake na wadogo zake wote hawapo hewani ndio akazidi kuchanganyikiwa. Hamu ya chai ikatoweka kabisa, ikabidi aende kwa muuza magazeti mtaani kwao kutafuta gazeti lolote lenye habari hizo za kusikitisha. Kwa bahati nzuri akapata gazeti la "Expresso da tarde" linalotoka kila siku.
Humo ndipo akapata habari kuwa zaidi ya wanakijiji 50 wameuliwa. Wameuawa kikatili kwa mapanga na mashoka kwa kukatwa vichwa vyao na watu wasiojulikana. Aliposoma orodha ya wahanga aliishiwa nguvu na kuzimia palepale pembeni mwa kibanda cha kuuza magazeti. Alikuta miongoni mwa majina ya waliofariki ni familia yake yote.
Alizinduka akijikuta yupo hospitali huku amezungukwa na madaktari wenzake wakimfariji kwa maneno ya kumtia moyo kuwa maisha lazima yaendelee anatakiwa kukubaliana na matokeo. Kwa bahati nzuri uongozi wa hospitali na wafanyakazi wenzake wakamchangia pesa ya kutosha kuendeshea mazishi. Akarejea kijijini kwao kushughulikia mazishi ya wazazi na ndugu zake.
Baada ya shughuli za matanga kupita, siku moja akiwa anapangapanga vitu vizuri nyumbani kwao ili aweze kurejea Jijini Maputo, akaendelee na maisha yake mapya, ndipo alipofungua sanduku la marehemu baba yake. Humo kwenye sanduku alikutana na taarifa iliyompa mshtuko mkubwa wa moyo na taharuki jadidi.
Aliifuma barua ya siri aliyoiandika marehemu baba yake mzazi na kuihifadhi kwenye sanduku hilo. Barua iliandikwa juu ya bahasha maandishi makubwa yanasomeka "NACATANAS". Alipoifungua na kuisoma hiyo barua alilia sana siku hiyo, kutokana na maelezo yaliyoandikwa na baba yake kuhusu kundi la "NACATANAS".
Majonzi ya msiba yakaibuka upya moyoni mwake. Ndio akafahamu kwanini baba yake siku za mwisho za uhai wake alikuwa hana maisha ya furaha kama zamani ambapo ilikuwa haipiti wiki atampigia simu mtoto wake chuoni kuulizia afya yake na maendeleo yake.
Mipango yake ya kurejea Maputo akaizika rasmi. Akaapa kuwa kuanzia sasa hatolia tena kwa sababu kilio kinapunguza hasira na kuondoka joto la hasira moyoni, badala yake atalipa kisasi kwa wote waliohusika kuiteketeza familia yake kikatili.
Akaweka nadhiri kuwa fursa itakavyopatikana lazima atawatekeza NACATANAS kwa mkono wake mwenyewe na wote waliohusika kufanya mauaji ya kikatili kwa familia yake. Kila uchao nyakati za Alfajiri akawa anazuru makaburi ya wazazi wake na kula yamini ya kulipiza kisasi. Kiu ya kisasi ikatawala katika fikra za "Dr.Anabella".

KUPATA HARDCOPY YAKO NITAFUTE KUPITIA NAMBA 0625920847
VITABU VIPO PIA MIKOANI
(1)LINDI(2)MTWARA(3) MOROGORO (4)MBEYA(5)KIGOMA(6)ARUSHA NA (7)TANGA
IMG-20200517-WA0066.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA: CABO DELGADO-PART 23

SURA YA KUMI NA TATU
Kachero Manu kifungoni ndani ya Selo kuu
Kachero Manu alitupwa selo kuu usiku wa giza totoro na akiwa hana fahamu kabisa. Alikuja kuzinduka katikati ya usiku akiwa anatetemeka na baridi, alipoangaza kwenye chumba hicho akaona mambo ya kutisha na kuogofya zaidi ya kule selo ndogo alipotolewa. Kwake aliona ni mfano wa mtu aliyeruka mkojo na kukanyaga kinyesi.
Kulikuwa na mwangaza hafifu wa kurunzi ya taa ya karabai iliyowekwa juu ya meza chakavu ya mbao. Akayaona majeneza kama 7 yamepangwa safusafu na kufungwa na kufuli za chuma cha pua. Alikuwa anasikia kwa mbali sana sauti hafifu za watu wanapiga kelele ndani ya yale majeneza wakilalamika kutokana na kukosa pumzi lakini sauti zao hazitoki vizuri.
Yale majeneza ndani yake kulikuwa na wadudu wakali kama nge na tandu pamoja na mende kwa lengo la kuwanyima usingizi mateka waliletwa humu kwenye selo kuu. Alipoangaza pembezoni ya meza yenye kurunzi akaona lundo la mabaki ya mifupa ya binadamu na mafuvu ya vichwa yamekusanywa pamoja kwenye magunia, ambayo yamezidiwa na mizigo mpaka mifupa mingine imejitokeza nje.
Akatulia na kuwaza, akajisemea moyoni mwake asipotumia akili za kuzaliwa imsaidie kutoroka humu, hatoweza kutoka salama. Atafia Cabo-Delgado na maiti yake haitoonekana tena, itatupwa katika mto Ruvuma, iwe chakula cha samaki.
Akawa anawaza jinsi kifo chake kitakavyomsikitisha mpenzi wake Faith Magayane ambaye walipanga huu mwaka usiishe wawe ni mke na mume mpaka kifo kiwatenganishe. Akawaza jinsi baba yake kule Mahiwa watakavyopokea taarifa ya kifo chake kwa mshtuko mkubwa, baada ya kumpoteza mkewe kwa kuchinjwa na kumpoteza mtoto wake ndani ya wiki moja. Pia Bosi wake Mzee Mathew Kilanga na Taifa kwa ujumla litapigwa na mshtuko mkubwa, litakuwa limempoteza Kachero wake mzoefu aliyepikwa akapikika kwa miaka kadhaa.
Ghafla Kachero Manu akiwa kwenye mkururu wa mawazo, akashtushwa na sauti ya kikohozi, ni kama kikohozi cha mtu aliyepigwa na baridi kali ya mule ndani. Akatulia kidogo, hakutaka kuyaamini kwa haraka masikio yake. Akasikia tena kwa ufasaha sauti ya mtu anaye jikohoa. Akaangaza macho yake chumba kizima kumtafuta huyo mtu. Kwenye kona ya chumba upande wa kushoto akafanikiwa kuona kwa tabu sana kama vile kuna mtu amelala juu ya kitanda. Akafanya maamuzi ya kumfuata kwa kujiviringisha ili akamfahamu huyo aliyelazwa. Huenda akapata msaada kwake wa kumsaidia kutoka ndani ya selo.
Akaanza kusota kwa njia ya kubiringika taratibu anajigeuza mwili mzima mzima kwa sababu alifungwa kamba za mikononi na miguuni. Akawa anasota huku anaugulia maumivu kwa sababu kulikuwa na misumari na vyupa vilivyovunjwa ovyo ndani ya kile chumba. Alikuwa anachomwa na ile misumari iliyopigiliwa chini ya sakafu kwa lengo la mateso kwa mateka. Akajikaza kisabuni hivyo hivyo, alijua kama atajidekeza kesho ndio mwisho wake wa kuishi duniani.
Hasa akikumbukia mazungumzo aliyoyanyaka kule Nantilus Hotel kuwa kesho kutwa usiku, tarehe 18/02/2016 kutakuwa na kikao kikubwa. Kikao ambacho Mkuu wa Mafioso wa Cabo-Delgado, Alfredo atakuwepo na mgeni wao toka Tanzania Bwana Andenga Kazimoto atakuja akiwa na nyaraka zote za siri alizozikwapua nchini Tanzania. Pia aliagizwa Inspekta Jenerali Mark Noble ahakikishe anamkamata Kachero Manu na kumleta kwenye kikao hicho ili ahojiwe kisha kuuliwa jambo ambalo tayari walishafanikiwa kumkamata.
Hivyo kwanza alijiamini mateso yote anayopewa ni vitisho tu lakini ahadi ni lazima apelekwe mbele ya kikao hicho akiwa yupo hai. Fursa ambayo alikuwa anaitamani sana ya kupelekwa kwenye kikao kikubwa cha washirika wa siri wa kampuni ya Monte Branco Ltd. Hivyo akajifariji hata kama huyo anayemfuata ambaye anakohoa kitandani atakuwa ni adui yake hana ubavu wa kumuua yeye kabla hajaonana na Bwana Alfredo.
Akaendelea kuburuzika kwa tabu, ilimchukua kama takribani dakika 38 mpaka kufika pembezoni mwa kitanda kile. Alipomkaribia yule mtu akamuona kwa tabu anajilazimisha kuunda tabasamu usoni mwake. Kachero Manu akajipa matumaini ni mtu mwema, asilani hawezi kuwa adui. Nuru ya matumaini ya kuokoka ikawa imechanua katika moyo wake, mithili ya mmea unavyochangamka pindi ukinyunyiziwa maji.
Alipomkaribia karibu zaidi akamsikia yule mtu anajikohoza tena kisha akaongea “Kiongozi tupo pamoja, usiogope, njoo karibu yangu zaidi”.
Kusikia hivyo Kachero Manu akaongeza bidii ya kujiburuza, baada dakika 3 akawa amelifikia tofali lililoweka kwa pembeni jirani na tendegu la kitanda. Akaegesha kichwa chake kwa tabu kisha, akamuuliza yule jamaa "wewe ni nani na umeletwa humu kwa kosa"? .
Yule jamaa bila ajizi akajitambulisha, “Mimi Naitwa Koplo Hamduni, wa Kituo kikuu cha Polisi Mtwara mjini, nimeambiwa ujio wako na Dr.Anabella Yule mwanadada anayetutibu mateka wa humu selo” akaongea Koplo Hamduni huku amekenua meno yake ya rangi ya manjano, machafu kutokana na kutopigwa mswaki kwa muda wa wiki nzima.
Kachero Manu akaanza kupata matumaini ya kutoka mule kwa kumtumia yule daktari ambaye hata jina lake alikuwa halijui, lakini alionyesha ana utu nafsini mwake. Kisha bila kusita akamkumbushia tena swali alilouliza, ”hujajibu swali langu ni kosa gani limekuleta humu selo ya kifo?” ingawa hisia zake zilimtuma kuwa huenda huyu ni miongoni mwa askari wapelelezi 6 waliotumwa Cabo-Delgado ambao inasemekana wamekamatwa na kuuliwa hivyo ikasababisha atumwe yeye.
Koplo Hamduni kwa sauti hafifu ya kukwaruza yenye kusikika kwa mbali akaanza kumsimulia mkasa wao wote tokea walivyoondoka Mtwara mpaka kufika Cabo-Delgado na namna kila mmoja wao alivyokamatwa. Mkasa ambao ulimsaidia sana kachero Manu kupata picha halisi ya chanzo cha machafuko dhidi ya Watanzania, Jimboni Cabo-Delgado.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA: CABO DELGADO-PART 23

SURA YA KUMI NA TATU
Kachero Manu kifungoni ndani ya Selo kuu
Kachero Manu alitupwa selo kuu usiku wa giza totoro na akiwa hana fahamu kabisa. Alikuja kuzinduka katikati ya usiku akiwa anatetemeka na baridi, alipoangaza kwenye chumba hicho akaona mambo ya kutisha na kuogofya zaidi ya kule selo ndogo alipotolewa. Kwake aliona ni mfano wa mtu aliyeruka mkojo na kukanyaga kinyesi.
Kulikuwa na mwangaza hafifu wa kurunzi ya taa ya karabai iliyowekwa juu ya meza chakavu ya mbao. Akayaona majeneza kama 7 yamepangwa safusafu na kufungwa na kufuli za chuma cha pua. Alikuwa anasikia kwa mbali sana sauti hafifu za watu wanapiga kelele ndani ya yale majeneza wakilalamika kutokana na kukosa pumzi lakini sauti zao hazitoki vizuri.
Yale majeneza ndani yake kulikuwa na wadudu wakali kama nge na tandu pamoja na mende kwa lengo la kuwanyima usingizi mateka waliletwa humu kwenye selo kuu. Alipoangaza pembezoni ya meza yenye kurunzi akaona lundo la mabaki ya mifupa ya binadamu na mafuvu ya vichwa yamekusanywa pamoja kwenye magunia, ambayo yamezidiwa na mizigo mpaka mifupa mingine imejitokeza nje.
Akatulia na kuwaza, akajisemea moyoni mwake asipotumia akili za kuzaliwa imsaidie kutoroka humu, hatoweza kutoka salama. Atafia Cabo-Delgado na maiti yake haitoonekana tena, itatupwa katika mto Ruvuma, iwe chakula cha samaki.
Akawa anawaza jinsi kifo chake kitakavyomsikitisha mpenzi wake Faith Magayane ambaye walipanga huu mwaka usiishe wawe ni mke na mume mpaka kifo kiwatenganishe. Akawaza jinsi baba yake kule Mahiwa watakavyopokea taarifa ya kifo chake kwa mshtuko mkubwa, baada ya kumpoteza mkewe kwa kuchinjwa na kumpoteza mtoto wake ndani ya wiki moja. Pia Bosi wake Mzee Mathew Kilanga na Taifa kwa ujumla litapigwa na mshtuko mkubwa, litakuwa limempoteza Kachero wake mzoefu aliyepikwa akapikika kwa miaka kadhaa.
Ghafla Kachero Manu akiwa kwenye mkururu wa mawazo, akashtushwa na sauti ya kikohozi, ni kama kikohozi cha mtu aliyepigwa na baridi kali ya mule ndani. Akatulia kidogo, hakutaka kuyaamini kwa haraka masikio yake. Akasikia tena kwa ufasaha sauti ya mtu anaye jikohoa. Akaangaza macho yake chumba kizima kumtafuta huyo mtu. Kwenye kona ya chumba upande wa kushoto akafanikiwa kuona kwa tabu sana kama vile kuna mtu amelala juu ya kitanda. Akafanya maamuzi ya kumfuata kwa kujiviringisha ili akamfahamu huyo aliyelazwa. Huenda akapata msaada kwake wa kumsaidia kutoka ndani ya selo.
Akaanza kusota kwa njia ya kubiringika taratibu anajigeuza mwili mzima mzima kwa sababu alifungwa kamba za mikononi na miguuni. Akawa anasota huku anaugulia maumivu kwa sababu kulikuwa na misumari na vyupa vilivyovunjwa ovyo ndani ya kile chumba. Alikuwa anachomwa na ile misumari iliyopigiliwa chini ya sakafu kwa lengo la mateso kwa mateka. Akajikaza kisabuni hivyo hivyo, alijua kama atajidekeza kesho ndio mwisho wake wa kuishi duniani.
Hasa akikumbukia mazungumzo aliyoyanyaka kule Nantilus Hotel kuwa kesho kutwa usiku, tarehe 18/02/2016 kutakuwa na kikao kikubwa. Kikao ambacho Mkuu wa Mafioso wa Cabo-Delgado, Alfredo atakuwepo na mgeni wao toka Tanzania Bwana Andenga Kazimoto atakuja akiwa na nyaraka zote za siri alizozikwapua nchini Tanzania. Pia aliagizwa Inspekta Jenerali Mark Noble ahakikishe anamkamata Kachero Manu na kumleta kwenye kikao hicho ili ahojiwe kisha kuuliwa jambo ambalo tayari walishafanikiwa kumkamata.
Hivyo kwanza alijiamini mateso yote anayopewa ni vitisho tu lakini ahadi ni lazima apelekwe mbele ya kikao hicho akiwa yupo hai. Fursa ambayo alikuwa anaitamani sana ya kupelekwa kwenye kikao kikubwa cha washirika wa siri wa kampuni ya Monte Branco Ltd. Hivyo akajifariji hata kama huyo anayemfuata ambaye anakohoa kitandani atakuwa ni adui yake hana ubavu wa kumuua yeye kabla hajaonana na Bwana Alfredo.
Akaendelea kuburuzika kwa tabu, ilimchukua kama takribani dakika 38 mpaka kufika pembezoni mwa kitanda kile. Alipomkaribia yule mtu akamuona kwa tabu anajilazimisha kuunda tabasamu usoni mwake. Kachero Manu akajipa matumaini ni mtu mwema, asilani hawezi kuwa adui. Nuru ya matumaini ya kuokoka ikawa imechanua katika moyo wake, mithili ya mmea unavyochangamka pindi ukinyunyiziwa maji.
Alipomkaribia karibu zaidi akamsikia yule mtu anajikohoza tena kisha akaongea “Kiongozi tupo pamoja, usiogope, njoo karibu yangu zaidi”.
Kusikia hivyo Kachero Manu akaongeza bidii ya kujiburuza, baada dakika 3 akawa amelifikia tofali lililoweka kwa pembeni jirani na tendegu la kitanda. Akaegesha kichwa chake kwa tabu kisha, akamuuliza yule jamaa "wewe ni nani na umeletwa humu kwa kosa"? .
Yule jamaa bila ajizi akajitambulisha, “Mimi Naitwa Koplo Hamduni, wa Kituo kikuu cha Polisi Mtwara mjini, nimeambiwa ujio wako na Dr.Anabella Yule mwanadada anayetutibu mateka wa humu selo” akaongea Koplo Hamduni huku amekenua meno yake ya rangi ya manjano, machafu kutokana na kutopigwa mswaki kwa muda wa wiki nzima.
Kachero Manu akaanza kupata matumaini ya kutoka mule kwa kumtumia yule daktari ambaye hata jina lake alikuwa halijui, lakini alionyesha ana utu nafsini mwake. Kisha bila kusita akamkumbushia tena swali alilouliza, ”hujajibu swali langu ni kosa gani limekuleta humu selo ya kifo?” ingawa hisia zake zilimtuma kuwa huenda huyu ni miongoni mwa askari wapelelezi 6 waliotumwa Cabo-Delgado ambao inasemekana wamekamatwa na kuuliwa hivyo ikasababisha atumwe yeye.
Koplo Hamduni kwa sauti hafifu ya kukwaruza yenye kusikika kwa mbali akaanza kumsimulia mkasa wao wote tokea walivyoondoka Mtwara mpaka kufika Cabo-Delgado na namna kila mmoja wao alivyokamatwa. Mkasa ambao ulimsaidia sana kachero Manu kupata picha halisi ya chanzo cha machafuko dhidi ya Watanzania, Jimboni Cabo-Delgado.


Sent using Jamii Forums mobile app
asante sana mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA: CABO DELGADO-PART 24


Safari ya Koplo Hamduni na wenzake Jimboni Cabo-Delgado
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mtwara chini ya Mwenyekiti wake, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, ilitoa maagizo kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa-(RPC) kutuma vijana wake kwenda Jimbo la Cabo-Delgado, Msumbiji kuchokonoa chanzo cha machafuko dhidi ya Watanzania wanaoishi huko.
Hivyo kikosi cha askari kanzu 6 wakiongozwa na Koplo Hamduni waliteuliwa kwenda huko wakiwa wamejikamilisha ipasavyo. Safari ya Koplo Hamduni na askari kanzu wenzake 5 ilikuwa ni kwa mafungu, wenzao 2 walitangulia kwa njia ya anga na 4 waliobaki walisafiri kwa njia ya nchi kavu.
Wale wa njia ya anga walitoka Mtwara na ndege ya shirika la ndege la ATCL mpaka Dar es Salaam. Kisha wakaunganisha moja kwa moja na ndege ya shirika la ndege la Msumbiji Linhas Aéreas de Moçambique, Ltd (LAM), ambayo huwa inatoka Dare s Salaam mpaka Pemba nchini Msumbiji, mara mbili kwa wiki.
Pemba ndio Makao Makuu ya Jimbo la Cabo-Delgado. Kisha wakaondoka Pemba kwa usafiri wa daladala kuelekea Montepuez tayari kuwasubiria wenzao wanaokuja kwa usafiri wa basi waungane pamoja. Walitumia hekima za wahenga zinazosema “usiweke mayai yote kwenye kapu moja, kapu likidondoka hutoi kitu”, walikuwa wanachukua tahadhari ili baadhi wakikwama wengine watimize lengo walilotumwa, afe beki afe kipa lengo litimie.
Koplo Hamduni na wenzake watatu waliosafiri kwa njia ya barabara safari yao iliyoanzia nyumba ya wageni ya “Chilindima” iliyopo Mtwara Mjini, mtaa wa pili tu toka stendi kuu. Hapo huwa ndio Gesti wanayopenda sana kufikia Wafanyabiashara wanaoelekea Cabo-Delgado na kuna daladala inaanzia safari zake hapo hapo nje ya gesti asubuhi na mapema.
Hivyo Koplo Hamduni na wenzake nao walijifanya ni Wafanyabiashara wanaelekea huko Cabo-Delgado wakaanza kupata alife bee tee za huko wanakoelekea kutoka kwa Wafanyabiashara wengine. Ingawa malengo yao ilikuwa wakifika wajitambulishe kama waandishi wa habari wa kimataifa ili waingie kirahisi eneo la tukio.
Walianza safari yao asubuhi kwa daladala iliyowafikisha mpakani mwa mto Ruvuma. Hapo walivushwa kwa mtumbwi mpaka ng'ambo ya Msumbiji kisha wakapanda daladala za kuelekea Msimbwa, nauli yake ni kama Mitikashi 400 kwa pesa za Msumbiji. Walipofika Msimbwa wakalala tena kwenye gesti ya “Marehemu Mzee Yahya”, ni gesti maarufu sana kwa Watanzania wanaoelekea Msumbiji.
Ila Gesti za Msumbiji ni kichefuchefu tupu kama hujazoea hasa zile za kawaida ustaarabu hamna kabisa. Mfano huwa hawaweki kandambili za kuingilia chooni inabidi ubebe za kwako mwenyewe la sivyo utapekua chooni. Pia chumba kinawezakuwa kina choo cha ndani "self-contained" lakini kumbe mnatumia watu wawili tofauti wa chumba tofauti kila mtu ana mlango wake wa kuingilia chooni.
Kutokana na mazungumzo na wazoefu wa kusafiri kwenda Montepuez,Jimboni Cabo-Delgado akina Koplo Hamduni wakafanya maamuzi tena wajigawanye asubuhi yake. Kwa kuwa hawakuwa na askari mwenye uwezo wa kufanya tarjama ya lugha Kireno kwa Kiswahili, wakaamua koplo Hamduni akapande gari linaitwa “Micula”. Hizo ni gari za kigogo mmoja wa zamani wa serikali ya Msumbiji huwa hazisimamishwi na askari usalama yoyote barabarani. Wale wenzake wakaondoka na basi la "ManingNice" zinazotoka Msimbwa kwenda Montepuez. Wenzake walikuwa afadhali wanaambulia maneno mawili matatu ya lugha ya Kireno hivyo hawakuwa na uwoga wowote wa askari wa Msumbiji iwapo itatokea wamesimamishwa njiani na kuhojiwa.
Askari wa Msumbiji ni wasumbufu sana na hata kama wanajua Kiswahili na Kiingereza wanajifanya kuongea Kireno ili wakukamate mgeni unayeenda nchini kwao kwa mara ya kwanza, ili wakusumbue wakuombe kitu kidogo.
Mfano askari anaweza kuingia kwenye gari la abiria akasalimia kwa kireno wakati wa asubuhi akasema “Boa-ndia”(habari za asubuhi), wewe unatakiwa umjibu “Boa-ndia shefuu”(Habari ni nzuri mkuu). Sasa askari anakuwa makini kuangalia abiria ambaye mdomo wake haujatikisika, akikugundua anakujua wewe ni mgeni, lazima akung'ang'anie kama ruba.
Anakufuata kwa mbwembwe zote kibonde wake, akikufikia atakuliza tena “Vai para aonde?”(Unakwenda wapi). Huo sasa hapo ni mtego wa panya, usijaribu kabisa kujibu “Montepuez”. Ukijibu hivyo tu wanajua huyu ndio Mtanzania kama kawaida yao anaenda kwenye machimbo ya rubi chamoto utakiona. Wewe ukiulizwa jibu tu sehemu ingine labda "Nampula" au "Mweda" lakini usitaje kuwa unaenda "Montepuez" kuwa ndio unapoelekea. Ukivuka kikwazo hicho, litakuja swali lingine “Vai para fazero ke?”(Unakwenda kufanya nini). Ukipigwa swali hilo wewe mjibu kwa upole kabisa, “Vizitari meo limao”(kumtembelea ndugu). Pia jiandae na usumbufu kibao, kama onyesha kitambulisho, ukiruka viunzi vyote mwishowe lazima atakuambia tu, “Dala refureshiko”. Yaani anakuomba ela ya soda, tayari hapo anataka uzunguke mbuyu ili akuache uende kwa salama, hapo sasa unaweza tu kumpa Mitikashi 50 unamalizana nae kwa usalama.
Hivi vikwazo vyote wale askari kanzu waliviruka wote 6 wakakutana Montepuez wakiwa salama salimini. Baada ya masimulizi marefu, Kachero Manu alimkatiza Koplo Hamduni, kwa swali la udadisi, "sasa ilikuwaje mpaka mkashikwa wote kama mlifika salama Montepuez?". Koplo Hamduni akaendelea na simulizi yake. "Tulifika salama na tukaelekea mpaka eneo la tukio katika kijiji cha Nthoro, tuliingia kijijini tukijifanya ni wandishi wa habari wa kimataifa wa haki za binadamu kutoka Afrika ya kusini na ndani ya siku mbili tulipata habari nyingi sana za kipelelezi toka kwa wananchi wakazi wa pale kijijini, lakini tunahisi kuna shinikizo la kigogo serikalini anayeshirikiana na hawa mabaradhuli, ambaye alikuwa anaogopa ukweli halisi ukianikwa ukajulikana kimataifa, taswira ya Msumbiji itachafuka na huenda baadhi ya viongozi wasio waadilifu wakapelekwa katika mahakama ya uhalifu ya Kimataifa. Tulikuta taarifa za mauaji makubwa ya mwaka 2009 ya wanakijiji kukatwa mapanga na watu wanaojiita "NACATANAS", mpaka leo hawajakamatwa sasa ukijumlisha na tukio hili jipya la Watanzania. Hivyo tukakamatwa na kuletwa kwenye hii selo na hamna yoyote aliyefanikiwa kutoroka toka humu, wenzangu wameshakufa hata mimi sina uhai mrefu ni mipango tu ya Dr.Anabella mie na wewe tukutane nikiwa hai na walitupokonya kila kitu chetu tulichokipeleleza". Baada ya kusikia maelezo hayo akashusha pumzi ndefu Kachero Manu.
"Mligundua nini chanzo cha machafuko haya yanayoendelea ya Montepuez"? aliuliza tena kiudadisi. Koplo Hamduni akajikohoza kuliweka koo lake sawa, ili aweze kuendelea na simulizi ya rubi iliyolowa damu ya Montepuez, Jimboni Cabo-Delgado.
Simulizi yake ilikuwa ni msaada mkubwa sana kwa Kachero Manu. Lakini sasa alianza kuongea kwa shida na alikuwa akikohoa anatema makohozi ya damu. Kachero Manu akaongeza umakini kumsikiliza alifahamu huyu hana muda mrefu atakuwa maiti mtarajiwa, anaelekea jongomeo.
“Eneo la Montepuez upande wa kaskazini-mashariki mwa jimbo la Cabo-Delgado iligundulika rubi yenye thamani ya juu kabisa duniani mwishoni mwa mwaka 2008. Eneo lenye madini ya rubi ni zaidi ya hekta za mraba 33600. Rubi hiyo iliyogunduliwa Msumbiji ni sawa na asilimia arobaini (40%) ya rubi yote iliyopo duniani. Ugunduzi uliopongezwa na shirika la Marekani “Gemological Institute of America” na kuitwa ni ugunduzi wa karne ya 21.
Aina za hizo rubi zilizogunduliwa Montepuez ni aina ya kifaru Rhino Ruby (40.23 carats) na macho ya dragoni Eyes of the Dragon (45 carats). Iligunduliwa na mkulima mdogo anayeishi eneo la kijiji cha Nthoro. Ilikuwa ni kawaida yao kuchimba chimba na kuuza kwa wageni vimawe vidogo.
Sasa yale mawe yalipelekwa nchini Thailand kuuzwa, yalipopimwa na wataalamu wakataka kufahamu wapi yalipotokea madini hayo ya rubi ndio ikajulikana ni Montepuez, Jimbo la Cabo-Delgado, Msumbiji. Kigogo wa serikalini kutoka chama cha FRELIMO ambaye aliwahi kuwa gavana wa Cabo-Delgado siku za nyuma. Alipopata taarifa za ugunduzi huo akanunua ardhi ya wakulima wadogo wa eneo hilo. Huyu kigogo alikuwa na kampuni yake aliyoisajili iliyokuwa inajihusisha na uuzaji wa jumla na rejareja wa vifaa vya ofisini. Ila baada ya ununuzi wa ardhi hiyo akaisajili kampuni yake kama mchimbaji wa madini ya rubi na kisha akaingia ubia na kampuni moja ya Kiingereza inayojihusisha na madini ya rubi ya ambayo ni kampuni kubwa sana duniani inayojishughulisha na uchimbaji na uuzaji wa madini ya rubi. Walipoingia ubia wakatengeneza kampuni moja mpya inayoitwa “Cabo-Delgado Ruby Mining”(CRM) ambapo kampuni ya Uingereza ikachukua asilimia sabini na tano (75%) ya hisa za kampuni na asilimia ishirini na tano(25%) ya hisa zikachukuliwa na kampuni ya kigogo mstaafu wa Msumbiji.
Kampuni ya "CRM ikapewa kibali halali cha serikali ya Msumbiji cha uchimbaji cha miaka 25 cha kuchimba eneo ya ekari 81,000. Sasa tatizo likaibuliwa na wachimbaji wadogo wadogo wakajikuta wanaondolewa kwenye maeneo yao ya uchimbaji. Na inasemekana hawa wachimbaji wadogo wadogo walikuwepo wengi wao ni wenyeji wa Msumbiji lakini pia Watanzania, Wasenegali na Wasomali pia walikuwepo.
Sasa inavyoonyesha kuna kampuni moja inaitwa "Monte Branco Ltd" ilitaka kujiingiza nayo kwenye biashara ya uchimbaji wa rubi bila kufuata sheria za Msumbiji na wala kulipa fidia halali kwa wazawa ambao ndio wamiliki halali wa ardhi ya vijiji vya Nthoro na Namanhumbir, ambavyo ndio vijiji vyenye rubi nyingi. Sasa ghafla kukaibuka kikundi kinajiita “NACATANAS” ambacho hakijulikani nani hasa mmiliki wa hiki kikundi. Wakawa wanapita kupiga mapanga wachimbaji ambao wanajifanya viherehere kutetea haki za wenzao.
Kampuni ya "CRM" ikakanusha kuwa haihusiki na kikundi hicho kwa sababu wao wana vibali vya serikali vya kumiliki eneo hilo, sasa vidole vya lawama vinaelekezwa kwa hawa "Monte Branco Ltd" kuwa huenda ndio wanaofadhili hawa NACATANAS ili kupandikiza hofu kwa jamii halafu na wao waweze kujitwalia eneo la kuchimba rubi. Ingawa hizi zote ni hisia hamna ushahidi kamili wa kuthibitisha kuwa wao ni wahusika, na daima vikundi vikubwa vya kimafia huwa haviachi alama za ushahidi kirahisi, hivyo ni juu yako “Kiongozi” kwenda ndani zaidi kufanya upelelezi kuwagundua kama hawa "Monte Branco Ltd" wanahusika au hapana na hicho kikundi cha NACATANAS nani mmiliki wake, maana kila mwananchi anawataja hao ndio wanaofanya fujo machimboni".
Ghafla akaanza kukohoa mfululizo Koplo Hamduni baada ya kukaribia kumaliza simulizi yake. Akaanza kuhema kwa nguvu kama mtu aliyetwishwa mzigo mzito kichwani. Kisha akamalizia simulizi yake “Kii..o…oo.ngozi nak..uta…kia kazi njeeee..ma.....Aluta Kontinua!” kisha akatumbua macho kodo angani akakata roho kuelekea kwa Mola wake.
Machungu ya Kachero Manu ya kumshuhudia Koplo Hamduni anafariki mbele ya macho yake yalikuwa hayaelezeki nae akajikuta machozi yanamtiririka kwa uchungu. Akashukuru Mungu kwa kumkutanisha na Koplo Hamduni aliyempatia maelezo mazuri. Maelezo ambayo yalimpa mwangaza mkubwa kwenye taftishi yake na yamemrahisishia kazi yake aliyotakiwa kuifanya kwa kiasi kikubwa.
Akakumbuka kuna wakati kwenye maisha binadamu unaweza ukapatwa na balaa na ukalaumu Mungu kumbe ndani ya hilo balaa Mungu kaweka neema ndani yake. Inamaanisha yeye alivyotekwa kuletwa huku selo aliona ni balaa lakini kumbe amekuja kukutanishwa na Koplo Hamduni ambaye amempa taarifa nyeti sana.
Akasifu uhodari wa Koplo Hamduni, kwani ya muda mfupi wa siku chache tayari alishajikusanyia taarifa muhimu sana za upelelezi. Akajisemea huyu kama asingefariki ningependekeza kwa Bosi Mathew Kilanga aletwe Makao Makuu akapewe mafunzo zaidi na angekuwa msaada kwa idara yetu ya usalama. Lakini haikuwa bahati yake kashapoteza uhai wake.
Akaanza kujiburuta Kachero Manu kurudi eneo alilotupwa na wale vijana wawili waliopewa maagizo ya kumpeleka kwenye selo kubwa.
Screenshot_20200518-141845.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
CABO-DELGADO-PART 25

SURA YA KUMI NA NNE
Dr.Anabella anasa ripoti nyeti nyumbani kwa Inspekta Jenerali Mark Noble
Dr.Anabella baada ya kusoma barua iliyoachwa na marehemu baba yake iliyoelezea dhuluma kubwa waliyofanyiwa ya kuporwa ardhi yao na vitisho walivyokuwa wanapokea kutoka kwa kikundi cha "NACATANAS", ikabidi azime ndoto zake zote za kufanya kazi ndani ya Maputo Jiji kuu la Msumbiji.
Wanakijiji aliwakuta wameshakata tamaa sasa wakawa wanamtazama yeye kama ndio msomi wa kijiji mwenye jukumu la kuwaonyesha dira na njia ya kupata haki zao kutokana na dhuluma wanazofanyiwa. Dr.Anabella akavaa koti la uanaharakati na kuliweka kando koti la Utabibu wa binadamu kwa muda. Akaitisha mkutano wa wahanga wote, kisha wakachagua kamati ya kijiji ya kufuatilia haki zao. Hatua ya kwanza ya ufuatiliaji ilikuwa ni kutoa ripoti polisi na kujua walipofikia Kwenye upelelezi wao. Hatua ya pili ilikuwa ni kufanya mazungumzo na mgodi wa 'Cabo-Delgado Ruby Mining'-("CRM") uweze kulipa fidia na kuisaidia jamii kujijenga upya baada ya kuhamishwa maeneo yao ya asili.
Juhudi za Dr.Anabella zilizaa matunda chanya kwani mgodi wa 'Cabo-Delgado Ruby Mining'-("CRM") ulikubali kujenga nyumba mpya kwa ajili ya familia 500 za wana kijiji cha Nthoro katika eneo jipya. Nyumba hizo zilijengwa kwa thamani ya dola za kimarekani milioni 10. Pia walikubali kujenga soko, hospitali, shule, kanisa, msikiti, chuo cha ufundi na eneo la makaburi.
Upande wa hawa wahalifu wa 'NACATANAS' taarifa ya hatua walizochukuliwa na vyombo vya dola ikawa ni danadana za nenda rudi nenda rudi toka jeshi la polisi. Mwishoni mwa mwaka 2012, baada ya kuona usumbufu wa Dr.Anabella umezidi kikomo katika ufuatiliaji wa sakata hilo, Inspekta Jenerali mwenyewe wa Jimbo la Cabo-Delgado Bwana Mark Noble akajibebesha mwenyewe zigo. Akajiteua kuwa ndio awe anashughulika na upelelezi wa sakata la machafuko ya machimboni.
Mark safari za kijiji cha Nthoro zikawa sasa hazikauki, kila wakati anafanya mikutano ya siri na ya wazi na kamati ya Dr.Anabella anajifanya anashughulikia tatizo lao kumbe "kikulacho ki nguoni wako" kumbe wangejua kuwa Mark ndio kiongozi mkuu wa "NACATANAS" yeye ndio anawapangia matukio yote, na alikuwa anatumia nafasi yake ya Ukuu katika jeshi la polisi kuwakwepesha na mkono wa sheria. Ndio maana NACATANAS wakawa hawafanyi uhalifu wao kwa mficho, wakiringia ukaribu wao na Inspekta Jenerali Mark Noble.
Ule ukaribu wa Dr.Anabella na Mark na kufahamiana kwao kwenye suala la wanakijiji kukazalisha kujuana zaidi. Wakajikuta wameingia katika mahusiano ya kimapenzi bila wenyewe kutarajia.
Katika vitu vilikuwa vinamkosesha majibu ya moja kwa moja Dr.Anabella na kumpa mawazo juu ya mpenzi wake Inspekta Jenerali Mark toka siku za mwanzo mwanzo za mahusiano yao ni utajiri wa kupindukia aliokuwa nao Mark.
Nchi ya Msumbiji ipo miongoni mwa nchi 10 masikini duniani, haina mishahara mikubwa kwa watumishi wa umma. Mfano kima cha chini cha Mshahara ni Mitikashi 2,900 sawa na kama Sh. 100,000/= ya Tanzania. Lakini Inspekta Jenerali Mark Noble alikuwa anamiliki majumba ya kifahari karibia katika kila wilaya ya Cabo-Delgado. Alikuwa anabadilisha magari ya kifahari kila wakati na vitega uchumi mbalimbali. Baadhi ya likizo zao walikuwa wanaenda Jijini Paris, Ufaransa na Dubai kutumbua raha za dunia.
Dr.Anabella kila anapomuuliza kwa kumchokonoa wapi alipopata utajiri wa kupindukia, alikuwa anakuja juu kama moto wa kifuu hataki kufuatiliwa mambo yake binafsi.
Kitu kingine kilichokuwa kinamkera Dr.Anabella kwa mpenzi wake Inspekta Jenerali Mark, ni tabia ya ulevi wa kupindukia hasa anapokuwa na msongo wa mawazo. Tabia ambayo Dr.Anabella alikuwa tayari wavunje hata mahusiano yao ya kimapenzi. Ila Mark kila mara alikuwa anaomba msamaha na kutoa ahadi kemkem za kutorudia tena lakini "lakuvunda halina ubani" baada ya muda anarudia tena yale yale ya zamani kama sio yeye aliyahidi kwa viapo kabisa kuwa hatorudia pombe.
Siku moja baradhuli Mark alirudi nyumbani usiku wa manane akiwa amelewa chakari. Akaingia kwenye chumba cha kujisomea nyumbani kwake akawa anapitia nyaraka zake za kwenye mkoba wake aliorudi nao akapitiwa na usingizi wa fefefe hapo hapo mezani. Dr.Anabella alifanikiwa kumvua viatu mpenzi wake na kumburuza mpaka kitandani kwake na kumlaza.
Ila wakati anamtoa mezani Dr.Anabella aliona bahasha kubwa ya kaki imechapwa maandishi rangi nyeusi kwa herufi kubwa "CONFIDENTIAL". Jakamoyo likamuwaka kifuani kwake na dukuduku la moyo la kutaka kufahamu hiyo barua inahusu nini na siri iliyopo.
Akaamua aende kuisoma huenda atapata majibu ya maswali anayojiuliza kila leo kuhusiana na shughuli za Inspekta Jenerali Mark nje ya shughuli rasmi za jeshi la polisi hasa akitilia wasiwasi ukaribu wa kupitiliza wa Inspekta Jenerali Mark na vigogo wa kampuni ya Monte Branco Ltd. Ilifikia hatua hadi kupewa ofisi ya kufanyia shughuli zake ndani ya ofisi za kampuni hiyo.
Akaanza kuifungua hiyo bahasha huku vidole vinatetemeka akiombea Mark asije kushtuka usingizini ukazuka msala mpya kwake. Alipoifungua tu hiyo bahasha akakuta kuna barua ya onyo imetoka kwa Alfredo Bosi mkuu wa "Monte Branco Ltd" ikimlaumu sana Mark kwa uzembe wa upotevu wa madini yao ya rubi huko nchini Thailand uliofanywa na vijana wa Kitanzania waliotumwa Thailand na Inspekta Mark Noble, wakaleta ujanja wao wa Kariakoo na kutokomea na mzigo wa madini wote bila kuleta hata senti moja.
Hapo akatambua kumbe Mark utajiri wake unatokana na madini ya rubi, na kule kujifanya amezoeana nao vigogo wa kampuni hiyo sio bure ni kwa kazi maalumu ya kuwalinda na mkono mrefu wa dola. Hiyo barua ikampa udadisi sasa wa kupekua nyaraka zingine zilizopo kwenye mkoba huo, humo ndio akakuta taarifa ya mchezo mzima wa biashara ya rubi ya Montepuez.
Humo akakuta kwamba michezo mbalimbali wanayofanya katika kusafirisha ni kuwatumia Wafanyabiashara wenye vibali vya Msumbiji vya kusafirisha madini nje ya nchi. Ambao wanaandikiwa barua ya kutoka Wizara ya Madini kuonyesha aina ya madini, uzito na yanapoelekea na wanasindikizwa mpaka Uwanja wa ndege na vijana wa Inspekta Jenerali Mark Noble halafu kuna kamisheni unawalipa.
Njia nyingine ni kutorosha madini ya Msumbiji kupitia nchini Kenya. Wanawatuma vijana wao wanabeba madini kwa njia za panya mpaka nchini Kenya. Wakifika Kenya wanayaacha madini kastamu. Wanaacha na vibali vyao, Maafisa wa kastamu wanayapokea na kutoa risiti, kisha wanaenda kuomba viza ya kwenda Thailand baada ya siku mbili wanakuwa tayari wamekamilisha taratibu zote. Wanachukua madini yao bila gharama zozote wanayapekeka nchini Thailand kwa ndege ya Kenya Airways au ndege ingine yoyote yenye safari ya huko.
Hii mbinu ni kama wanawatumia wasafirishaji ambao sio wazawa hivyo wanaogopa watanyimwa viza na mamlaka za Msumbiji. Wakifika Thailand wanalipia vibali husika uwanja wa ndege kisha wanaruhusiwa kuingia nayo madini Jijini Bangkok, Thailand. Wakitoka Bangkok wanasafiri kwa Basi kwenda jimbo la Chanthaburi lililopo kusini mashariki mwa nchi ya Thailand. Jimbo lililo umbali wa takribani saa tatu au wanaweza kupanda ndege za ndani. Huko Chanthaburi ndio kuna gulio kuu la rubi kila siku ya Ijumaa na Jumamosi.
Huko ndiko Matajiri kutoka Australia, nchi za mbalimbali za Ulaya na nchi za Scandavia wanachuana kununua madini hayo kwenye mnada. Alishangazwa Dr.Anabella aliposoma imeshawahi kuuzwa rubi ya gramu 30 kutoka Montepuez kwa dola za kimarekani milioni 1($1,000,000).
Nyaraka zilizomchefua zaidi Dr.Anabella ni alipoona orodha ya wapokea mshahara wa kikundi cha "NACATANAS", hapo ndio akajua kumbe joka lililohusika na mauaji ya familia yake yupo nae nyumba moja anakula nae na kulala nae.
Alikaribia kupoteza fahamu kwa kugundua muuaji yupo nae miaka yote nyumba moja, kumbe ametajirika kwa mgongo wa damu ya familia yake. Alitamani aende jikoni akabebe kisu kikubwa kile kisu kinachotumika kuchinjia mbuzi wa sikukuu ya Pasaka amchome nacho kifuani amalize shughuli mara moja.
Lakini akajipa subira ili amteketeze wakati muafaka ukifika na aweze kusambaratisha Mafioso wote wa biashara haramu ya madini ya rubi. Dola haitomuelewa hata kidogo kama akifanya mauaji chumbani. Alijua muda sahihi kwake utawadia wa kutekeleza kisasi chake. Daima subira yavuta kheri ingawa chelewa chelewa utakuta mwana sio wako, hivyo akajiona anatakiwa afanye jambo muafaka, katika nyakati muafaka na mahali muafaka.
Nyaraka zote za siri alizosoma usiku ule, Dr.Anabellah hakuziacha bure. Alizitoa nakala kwa kutumia mashine iliyomo kwenye chumba cha kujisomea, akahifadhi sehemu salama akisubiri muda muafaka wa kutoa ushahidi wake kwenye vyombo husika itakapobidi.
IMG-20200519-WA0051.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
CABO-DELGADO-PART 25

SURA YA KUMI NA NNE
Dr.Anabella anasa ripoti nyeti nyumbani kwa Inspekta Jenerali Mark Noble
Dr.Anabella baada ya kusoma barua iliyoachwa na marehemu baba yake iliyoelezea dhuluma kubwa waliyofanyiwa ya kuporwa ardhi yao na vitisho walivyokuwa wanapokea kutoka kwa kikundi cha "NACATANAS", ikabidi azime ndoto zake zote za kufanya kazi ndani ya Maputo Jiji kuu la Msumbiji.
Wanakijiji aliwakuta wameshakata tamaa sasa wakawa wanamtazama yeye kama ndio msomi wa kijiji mwenye jukumu la kuwaonyesha dira na njia ya kupata haki zao kutokana na dhuluma wanazofanyiwa. Dr.Anabella akavaa koti la uanaharakati na kuliweka kando koti la Utabibu wa binadamu kwa muda. Akaitisha mkutano wa wahanga wote, kisha wakachagua kamati ya kijiji ya kufuatilia haki zao. Hatua ya kwanza ya ufuatiliaji ilikuwa ni kutoa ripoti polisi na kujua walipofikia Kwenye upelelezi wao. Hatua ya pili ilikuwa ni kufanya mazungumzo na mgodi wa 'Cabo-Delgado Ruby Mining'-("CRM") uweze kulipa fidia na kuisaidia jamii kujijenga upya baada ya kuhamishwa maeneo yao ya asili.
Juhudi za Dr.Anabella zilizaa matunda chanya kwani mgodi wa 'Cabo-Delgado Ruby Mining'-("CRM") ulikubali kujenga nyumba mpya kwa ajili ya familia 500 za wana kijiji cha Nthoro katika eneo jipya. Nyumba hizo zilijengwa kwa thamani ya dola za kimarekani milioni 10. Pia walikubali kujenga soko, hospitali, shule, kanisa, msikiti, chuo cha ufundi na eneo la makaburi.
Upande wa hawa wahalifu wa 'NACATANAS' taarifa ya hatua walizochukuliwa na vyombo vya dola ikawa ni danadana za nenda rudi nenda rudi toka jeshi la polisi. Mwishoni mwa mwaka 2012, baada ya kuona usumbufu wa Dr.Anabella umezidi kikomo katika ufuatiliaji wa sakata hilo, Inspekta Jenerali mwenyewe wa Jimbo la Cabo-Delgado Bwana Mark Noble akajibebesha mwenyewe zigo. Akajiteua kuwa ndio awe anashughulika na upelelezi wa sakata la machafuko ya machimboni.
Mark safari za kijiji cha Nthoro zikawa sasa hazikauki, kila wakati anafanya mikutano ya siri na ya wazi na kamati ya Dr.Anabella anajifanya anashughulikia tatizo lao kumbe "kikulacho ki nguoni wako" kumbe wangejua kuwa Mark ndio kiongozi mkuu wa "NACATANAS" yeye ndio anawapangia matukio yote, na alikuwa anatumia nafasi yake ya Ukuu katika jeshi la polisi kuwakwepesha na mkono wa sheria. Ndio maana NACATANAS wakawa hawafanyi uhalifu wao kwa mficho, wakiringia ukaribu wao na Inspekta Jenerali Mark Noble.
Ule ukaribu wa Dr.Anabella na Mark na kufahamiana kwao kwenye suala la wanakijiji kukazalisha kujuana zaidi. Wakajikuta wameingia katika mahusiano ya kimapenzi bila wenyewe kutarajia.
Katika vitu vilikuwa vinamkosesha majibu ya moja kwa moja Dr.Anabella na kumpa mawazo juu ya mpenzi wake Inspekta Jenerali Mark toka siku za mwanzo mwanzo za mahusiano yao ni utajiri wa kupindukia aliokuwa nao Mark.
Nchi ya Msumbiji ipo miongoni mwa nchi 10 masikini duniani, haina mishahara mikubwa kwa watumishi wa umma. Mfano kima cha chini cha Mshahara ni Mitikashi 2,900 sawa na kama Sh. 100,000/= ya Tanzania. Lakini Inspekta Jenerali Mark Noble alikuwa anamiliki majumba ya kifahari karibia katika kila wilaya ya Cabo-Delgado. Alikuwa anabadilisha magari ya kifahari kila wakati na vitega uchumi mbalimbali. Baadhi ya likizo zao walikuwa wanaenda Jijini Paris, Ufaransa na Dubai kutumbua raha za dunia.
Dr.Anabella kila anapomuuliza kwa kumchokonoa wapi alipopata utajiri wa kupindukia, alikuwa anakuja juu kama moto wa kifuu hataki kufuatiliwa mambo yake binafsi.
Kitu kingine kilichokuwa kinamkera Dr.Anabella kwa mpenzi wake Inspekta Jenerali Mark, ni tabia ya ulevi wa kupindukia hasa anapokuwa na msongo wa mawazo. Tabia ambayo Dr.Anabella alikuwa tayari wavunje hata mahusiano yao ya kimapenzi. Ila Mark kila mara alikuwa anaomba msamaha na kutoa ahadi kemkem za kutorudia tena lakini "lakuvunda halina ubani" baada ya muda anarudia tena yale yale ya zamani kama sio yeye aliyahidi kwa viapo kabisa kuwa hatorudia pombe.
Siku moja baradhuli Mark alirudi nyumbani usiku wa manane akiwa amelewa chakari. Akaingia kwenye chumba cha kujisomea nyumbani kwake akawa anapitia nyaraka zake za kwenye mkoba wake aliorudi nao akapitiwa na usingizi wa fefefe hapo hapo mezani. Dr.Anabella alifanikiwa kumvua viatu mpenzi wake na kumburuza mpaka kitandani kwake na kumlaza.
Ila wakati anamtoa mezani Dr.Anabella aliona bahasha kubwa ya kaki imechapwa maandishi rangi nyeusi kwa herufi kubwa "CONFIDENTIAL". Jakamoyo likamuwaka kifuani kwake na dukuduku la moyo la kutaka kufahamu hiyo barua inahusu nini na siri iliyopo.
Akaamua aende kuisoma huenda atapata majibu ya maswali anayojiuliza kila leo kuhusiana na shughuli za Inspekta Jenerali Mark nje ya shughuli rasmi za jeshi la polisi hasa akitilia wasiwasi ukaribu wa kupitiliza wa Inspekta Jenerali Mark na vigogo wa kampuni ya Monte Branco Ltd. Ilifikia hatua hadi kupewa ofisi ya kufanyia shughuli zake ndani ya ofisi za kampuni hiyo.
Akaanza kuifungua hiyo bahasha huku vidole vinatetemeka akiombea Mark asije kushtuka usingizini ukazuka msala mpya kwake. Alipoifungua tu hiyo bahasha akakuta kuna barua ya onyo imetoka kwa Alfredo Bosi mkuu wa "Monte Branco Ltd" ikimlaumu sana Mark kwa uzembe wa upotevu wa madini yao ya rubi huko nchini Thailand uliofanywa na vijana wa Kitanzania waliotumwa Thailand na Inspekta Mark Noble, wakaleta ujanja wao wa Kariakoo na kutokomea na mzigo wa madini wote bila kuleta hata senti moja.
Hapo akatambua kumbe Mark utajiri wake unatokana na madini ya rubi, na kule kujifanya amezoeana nao vigogo wa kampuni hiyo sio bure ni kwa kazi maalumu ya kuwalinda na mkono mrefu wa dola. Hiyo barua ikampa udadisi sasa wa kupekua nyaraka zingine zilizopo kwenye mkoba huo, humo ndio akakuta taarifa ya mchezo mzima wa biashara ya rubi ya Montepuez.
Humo akakuta kwamba michezo mbalimbali wanayofanya katika kusafirisha ni kuwatumia Wafanyabiashara wenye vibali vya Msumbiji vya kusafirisha madini nje ya nchi. Ambao wanaandikiwa barua ya kutoka Wizara ya Madini kuonyesha aina ya madini, uzito na yanapoelekea na wanasindikizwa mpaka Uwanja wa ndege na vijana wa Inspekta Jenerali Mark Noble halafu kuna kamisheni unawalipa.
Njia nyingine ni kutorosha madini ya Msumbiji kupitia nchini Kenya. Wanawatuma vijana wao wanabeba madini kwa njia za panya mpaka nchini Kenya. Wakifika Kenya wanayaacha madini kastamu. Wanaacha na vibali vyao, Maafisa wa kastamu wanayapokea na kutoa risiti, kisha wanaenda kuomba viza ya kwenda Thailand baada ya siku mbili wanakuwa tayari wamekamilisha taratibu zote. Wanachukua madini yao bila gharama zozote wanayapekeka nchini Thailand kwa ndege ya Kenya Airways au ndege ingine yoyote yenye safari ya huko.
Hii mbinu ni kama wanawatumia wasafirishaji ambao sio wazawa hivyo wanaogopa watanyimwa viza na mamlaka za Msumbiji. Wakifika Thailand wanalipia vibali husika uwanja wa ndege kisha wanaruhusiwa kuingia nayo madini Jijini Bangkok, Thailand. Wakitoka Bangkok wanasafiri kwa Basi kwenda jimbo la Chanthaburi lililopo kusini mashariki mwa nchi ya Thailand. Jimbo lililo umbali wa takribani saa tatu au wanaweza kupanda ndege za ndani. Huko Chanthaburi ndio kuna gulio kuu la rubi kila siku ya Ijumaa na Jumamosi.
Huko ndiko Matajiri kutoka Australia, nchi za mbalimbali za Ulaya na nchi za Scandavia wanachuana kununua madini hayo kwenye mnada. Alishangazwa Dr.Anabella aliposoma imeshawahi kuuzwa rubi ya gramu 30 kutoka Montepuez kwa dola za kimarekani milioni 1($1,000,000).
Nyaraka zilizomchefua zaidi Dr.Anabella ni alipoona orodha ya wapokea mshahara wa kikundi cha "NACATANAS", hapo ndio akajua kumbe joka lililohusika na mauaji ya familia yake yupo nae nyumba moja anakula nae na kulala nae.
Alikaribia kupoteza fahamu kwa kugundua muuaji yupo nae miaka yote nyumba moja, kumbe ametajirika kwa mgongo wa damu ya familia yake. Alitamani aende jikoni akabebe kisu kikubwa kile kisu kinachotumika kuchinjia mbuzi wa sikukuu ya Pasaka amchome nacho kifuani amalize shughuli mara moja.
Lakini akajipa subira ili amteketeze wakati muafaka ukifika na aweze kusambaratisha Mafioso wote wa biashara haramu ya madini ya rubi. Dola haitomuelewa hata kidogo kama akifanya mauaji chumbani. Alijua muda sahihi kwake utawadia wa kutekeleza kisasi chake. Daima subira yavuta kheri ingawa chelewa chelewa utakuta mwana sio wako, hivyo akajiona anatakiwa afanye jambo muafaka, katika nyakati muafaka na mahali muafaka.
Nyaraka zote za siri alizosoma usiku ule, Dr.Anabellah hakuziacha bure. Alizitoa nakala kwa kutumia mashine iliyomo kwenye chumba cha kujisomea, akahifadhi sehemu salama akisubiri muda muafaka wa kutoa ushahidi wake kwenye vyombo husika itakapobidi. View attachment 1455247

Sent using Jamii Forums mobile app
Thank mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CABO-DELGADO-PART 26



Nyaraka zote za siri alizosoma usiku ule, Dr.Anabellah hakuziacha bure. Alizitoa nakala kwa kutumia mashine iliyomo kwenye chumba cha kujisomea, akahifadhi sehemu salama akisubiri muda muafaka wa kutoa ushahidi wake kwenye vyombo husika itakapobidi.
Dr.Anabella hakutaka kumuonyesha dalili yoyote Inspekta Jenerali Mark Noble kuwa sasa anafahamu kinagaubaga kumhusu mafungamano yake na wamiliki wa kampuni. Alificha siri yake moyoni huku anatamani fursa ya kuwa karibu na vigogo wa Monte Branco Ltd, ambao ndio wahusika namba moja wa kifo cha wazazi wake na nduguze ijitokeze.
Ikatokea wakati mmoja kiwanda kikubwa cha kusindika korosho cha Monte Branco Ltd kinataka daktari wa kusimamia hospitali ya kiwanda. Mark ikabidi akamfanyie mpango mchumba wake Dr.Anabella ale shavu hiyo ajira. Bila kufanya ajizi akakubali hiyo nafasi mara moja bila pingamizi lolote. Rasmi Dr.Anabella akawa yupo kiwandani anafanya kazi. Majukumu yake ikawa ni kuwapa matibabu madogo madogo wafanyakazi wa kiwanda na pia kuandaa rufaa za wagonjwa wanaohitaji matibabu zaidi katika hospitali kubwa.
Mategemeo ya Dr.Anabella alidhani labda na vigogo wa Monte Branco Ltd watakuwa wanatibiwa pale wao na familia zao ili awamalize taratibu kwa madawa ya sumu. Kumbe ikawa tofauti, vigogo wote walikuwa wanatibiwa hospitali kubwa za Jijini Maputo na Cape-Town, Afrika ya kusini.
Alibaki kidogo tu aache kazi kwa sababu lengo lake aliona haliwezi kutimia kwa haraka. Ndipo ilipokuja nafasi aliyokuwa anaisubiria kwa hamu ya kukata kiu yake ya kisasi. Daktari Mkuu wa selo ya mateso ya mabaradhuli ya 'Gorongosa Camp' alipata ajali mbaya ya barabarani katika wiki ambayo Koplo Hamduni na wenzake wamekamatwa. Ikabidi atafutwe Daktari wa dharura msiri wa kuendesha matibabu ya kambi hiyo ya siri kwa mateka. Na ni kazi iliyokuwa na marupurupu makubwa, na baradhuli Mark alikuwa ndio mkuu wa Gorongosa Camp hivyo haraka haraka akamteua mchumba wake Dr.Anabella ashikie hiyo nafasi.
Alimdanganya hiyo ni kambi ya serikali ya Msumbiji kitengo cha Usalama wa Taifa, hivyo asikatae hayo majukumu na iwe ni siri yake akitoa anaweza kuupoteza hata uhai. Waswahili walisema 'mla kunde husahau ila mtupa maganda hawezi kusahau', Mark alishasahau kuwa Dr.Anabella anawajua NACATANAS ambao waliteketeza baadhi ya wanakijiji, na sare za kambi zilikuwa na maandishi yenye maneno hayo.
Tahadhari waliyokuwa wanaichukua ni kumfunga kitambaa cha usoni mpaka ndani ya kambi kisha wanamfungua ili asijue kambi ipo eneo gani. Lakini siku ya kwanza kuwaona wale watesaji wakuu wamevaa zile fulana nyeusi zimeandikwa NACATANAS akajua hawa ndio wahalifu wake aliokuwa anawatuhumu kwa mauaji ya familia yake na baadhi ya wanakijiji.
Mwanzoni alikuwa anasindikizwa na baradhuli mpaka selo wakati wa kutoa huduma, walipomzoea Dr.Anabella hasa walipojua ni mchumba wa Bosi wao Mark Noble wakaanza kumuamini na kuvunja miiko ya kazi, wakawa wanamuacha aingie peke yake kwa masharti asichelewe kutoka. Wao wanakuwa kwenye sehemu yao ya mapumziko wanakunywa pombe kali na kufurahia starehe. Hilo likawa ni kosa la mwaka kwao, ambalo hawakujua kuwa watakuja kujutia milele.
Kuna siku walipopelekwa kuhojiwa akina Koplo Hamduni, aliyewarudisha selo alifuatana na Dr.Anabella akiwa na pombe yake mkononi, alipokuwa ameshughulishwa na kuwadhibiti akina Koplo Hamduni, Dr.Anabella alifanikiwa kuchanganya vidonge aina ya “Amoxapine” kwenye pombe ya baradhuli yule mlevi buda.
"Amoxapine" ni vidonge vinavyotumika kumrudishia mtu uchangamfu akiwa hana furaha sasa vikichanganywa na pombe vinasababisha usingizi uje kwa haraka. Baradhuli alipokunywa tu akapatwa na usingizi mzito, hapo Dr. Anabella akafanikiwa kuongea na Koplo Hamduni kinagaubaga sababu za kukamatwa kwao. Koplo akamueleza kwa ufupi maana Koplo alikuwa na maumivu makali anaongea kwa shida na Dr.Anabella alijua muda sio mrefu watafuatwa wakiona wanachelewa kurudi.
Hivyo Dr.Anabella pindi alivyokamatwa Kachero Manu, alipatwa na hisia ni washirika wa Koplo Hamduni, ndio maana akamuambia ile siku ya kwanza kazinduka kutoka kuzimia alimuambia kwa NACATANAS watakufuata kukuhoji ili kumpa fununu juu ya watu waliomteka. Ili kama hawajui ila ameshawahi kusikia habari zao apate kutanabahi.
Nafasi ya mwisho ya dhahabu aliyoitumia Dr.Anabella ni kujaribu kuwakutanisha kati ya Koplo Hamduni na Kachero Manu. Alipewa amri Dr.Anabella awachome sindano za sumu Koplo Hamduni na wenzake wakiwa wamefungiwa kwenye majeneza, huku Koplo Hamduni akiwa amefungwa kitandani.
Wale mabaradhuli walikuwa wanamuogopa sana Koplo Hamduni huenda akifungiwa kwenye jeneza anaweza kujitoa kutokana na ukakamavu wake alioonyesha wakati wanamtia mbaroni. Alichofanya Dr.Anabella ni kumchoma Koplo Hamduni sindamu ya sumu chini ya dozi inayotakiwa, ili Koplo Hamduni na Kachero Manu waweze kukutana, na dhana yake njema alijua wakikutana watabadilishana taarifa za kipelelezi, huku akiombea mabaradhuli watakaomleta Kachero Manu selo kubwa wasiwe makini kuchunguza kama Koplo Hamduni na wenzake wamekufa au bado wapo hai.
Lengo la Dr. Anabella lilifanikiwa, Kachero Manu na koplo Hamduni walikutana na kuongea maongezi yaliyokuwa na tija sana kwa Kachero Manu kwa kumpa mwangaza halisi wa upelelezi wake.


SURA YA KUMI NA TANO
Kachero Manu bado hali tete
Kachero Manu usiku ule baada ya maongezi na marehemu Koplo Hamduni, alipigwa na baridi kali hasa ukichukulia alikuwa hajavishwa nguo yoyote mwilini mwake. Akafanikiwa kusota mpaka jirani na jeneza moja akaliegemea ikamsaidia kupunguza joto.
Akapatwa na usingizi mzuri sana uliosaidia kupumzisha mwili wake kiasi fulani. Aliamshwa toka usingizini na mionzi ya jua iliyokuwa inapenya kwenye vidirisha vidogo vya mule chumbani. Akakisia huenda ikawa ni saa mbili na nusu au saa tatu kasoro asubuhi. Sasa akawa ametimiza siku nzima kamili ndani ya selo kuu.
Akaanza kuhisi njaa kali inatafuna utumbo wake, mpaka akaanza kutetemeka kwa njaa. Baada ya kupita kama nusu saa akasikia nyayo za watu zinakaribia mlango wa ile selo kuu alipofungiwa.
Likafunguliwa lango kuu wakaingia watu kama 7 pamoja na Dr. Anabella akiwemo. Walipoingia hawakumsemesha chochote wengine wakashughulishwa na kutoa nje majeneza ambayo sasa yalikuwa na maiti zilizofia ndani yake, na mmoja wao akaenda kwenye kitanda alichofia Koplo Hamduni akamfungua kamba zake na kuiburuta maiti yake nje ya chumba, kitendo ambacho kilimfanya Kachero Manu amuangalie Dr.Anabella kwa umakini akamuona kwa mbali machozi yanamlenga lenga alivyokuwa anaangalia maiti ya Koplo Hamduni. Ila usingeweza kugundua kwa haraka kwa sababu alikuwa amevaa miwani.
Dhamira ya Dr.Anabella ilikuwa inamsuta kwa kufanya mauaji ya Koplo Hamduni kutokana na sindano ya sumu aliyomchoma. Katika maisha yake yote alikuwa hajawahi kuua kiumbe chochote zaidi ya kuua mbu wa Malaria, hata kuua mende alikuwa anaogopa hivi leo baradhuli Mark amempelekea mpaka kuua binadamu wenzake.
Baada kama ya nusu saa wakaondoka na kufunga mlango wa geti la selo. Kachero Manu akazidi kuchanganyikiwa akawa anajiuliza, "hawa watu ni binadamu kweli au ni roboti? Hata chembe ya utu mbona hawana. Wamenichukua toka jana hawajali hata kama nina njaa au hapana". Alikuwa hajawahi hata siku moja maishani mwake kukata tamaa ya kuokoka lakini alianza kuhisi hatopata njia ya kutoroka ndani ya selo hiyo.
Na Dr.Anabella aliyeanza kuwa na matumaini nae kuwa huenda akamukoa nae hakuona kama ana msaada wowote. Maana hata kumuongelesha kuhusu namna ya kutoroka hajawahi. Wala hajawahi kuonyesha ishara yoyote kuwa wapo pamoja kama alivyosimuliwa na Koplo Hamduni.
Akaanza kuiona kurunzi ya mule chumbani kama inaanza kufifia kutokana na kuanza kuishiwa kwa mafuta ya taa. Baada ya kupita kama saa moja kwa kukadiria ni kama saa nne asubuhi akaanza kusikia tena michakato ya miguu ya watu wanakuja tena kwenye selo yake. Ila idadi yao kwa makadirio ilionyesha ni wachache sio kama wale wa mwanzoni, akaanza kufufua matumaini ya kuokoka.
Wale watu walipofika wakafungua lango la selo na kuingia ndani. Alikuwa ni tena Dr.Anabella tena na vijana wa kundi hatari la NACATANAS wapatao wawili. Mmoja alikuwa amebeba trei ya chakula, ilikuwa ni supu ya nyama, matandu meusi ya wali yale ya juu na mkate wa boflo mmoja. Huku mwingine amebeba bunduki aina ya SMG begani hana hata chembe la tabasamu utasema malaika wa motoni kwa jinsi alivyokunja ndita usoni.
Dr.Anabella alikuwa amevaa shingoni mwake kifaa cha kupimia mapigo ya moyo huku koti lake jeupe mifuko yake ikionekana imetuna tuna. Yule aliyebeba trei la chakula akaenda mpaka kwenye meza chakavu iliyokuwa na kurunzi ya mafuta ya taa inayosaidia kueneza mwanga katika selo yenye mwanga khafifu, akaweka trei mezani kisha akamfuata Kachero Manu kumfungua kamba zake za mikononi pekee, kisha akamletea chakula ale.
"Usijaribu kuleta ujanja wowote, jaribio lolote utakalofanya litagharimu uhai wao, kula ujisosomole kuondosha njaa yako" alisema yule baradhuli aliyebeba SMG huku akiwa amemuelekezea Kachero Manu mdomo wa bunduki. Dr.Anabella akawa nae kaisogelea meza ile chakavu akatoa baadhi ya chupa za madawa, mkasi na pamba akaweka juu ya meza kisha akaegemea meza anamuangalia Kachero Manu anavyopokea chakula.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
CABO-DELGADO-PART 26



Nyaraka zote za siri alizosoma usiku ule, Dr.Anabellah hakuziacha bure. Alizitoa nakala kwa kutumia mashine iliyomo kwenye chumba cha kujisomea, akahifadhi sehemu salama akisubiri muda muafaka wa kutoa ushahidi wake kwenye vyombo husika itakapobidi.
Dr.Anabella hakutaka kumuonyesha dalili yoyote Inspekta Jenerali Mark Noble kuwa sasa anafahamu kinagaubaga kumhusu mafungamano yake na wamiliki wa kampuni. Alificha siri yake moyoni huku anatamani fursa ya kuwa karibu na vigogo wa Monte Branco Ltd, ambao ndio wahusika namba moja wa kifo cha wazazi wake na nduguze ijitokeze.
Ikatokea wakati mmoja kiwanda kikubwa cha kusindika korosho cha Monte Branco Ltd kinataka daktari wa kusimamia hospitali ya kiwanda. Mark ikabidi akamfanyie mpango mchumba wake Dr.Anabella ale shavu hiyo ajira. Bila kufanya ajizi akakubali hiyo nafasi mara moja bila pingamizi lolote. Rasmi Dr.Anabella akawa yupo kiwandani anafanya kazi. Majukumu yake ikawa ni kuwapa matibabu madogo madogo wafanyakazi wa kiwanda na pia kuandaa rufaa za wagonjwa wanaohitaji matibabu zaidi katika hospitali kubwa.
Mategemeo ya Dr.Anabella alidhani labda na vigogo wa Monte Branco Ltd watakuwa wanatibiwa pale wao na familia zao ili awamalize taratibu kwa madawa ya sumu. Kumbe ikawa tofauti, vigogo wote walikuwa wanatibiwa hospitali kubwa za Jijini Maputo na Cape-Town, Afrika ya kusini.
Alibaki kidogo tu aache kazi kwa sababu lengo lake aliona haliwezi kutimia kwa haraka. Ndipo ilipokuja nafasi aliyokuwa anaisubiria kwa hamu ya kukata kiu yake ya kisasi. Daktari Mkuu wa selo ya mateso ya mabaradhuli ya 'Gorongosa Camp' alipata ajali mbaya ya barabarani katika wiki ambayo Koplo Hamduni na wenzake wamekamatwa. Ikabidi atafutwe Daktari wa dharura msiri wa kuendesha matibabu ya kambi hiyo ya siri kwa mateka. Na ni kazi iliyokuwa na marupurupu makubwa, na baradhuli Mark alikuwa ndio mkuu wa Gorongosa Camp hivyo haraka haraka akamteua mchumba wake Dr.Anabella ashikie hiyo nafasi.
Alimdanganya hiyo ni kambi ya serikali ya Msumbiji kitengo cha Usalama wa Taifa, hivyo asikatae hayo majukumu na iwe ni siri yake akitoa anaweza kuupoteza hata uhai. Waswahili walisema 'mla kunde husahau ila mtupa maganda hawezi kusahau', Mark alishasahau kuwa Dr.Anabella anawajua NACATANAS ambao waliteketeza baadhi ya wanakijiji, na sare za kambi zilikuwa na maandishi yenye maneno hayo.
Tahadhari waliyokuwa wanaichukua ni kumfunga kitambaa cha usoni mpaka ndani ya kambi kisha wanamfungua ili asijue kambi ipo eneo gani. Lakini siku ya kwanza kuwaona wale watesaji wakuu wamevaa zile fulana nyeusi zimeandikwa NACATANAS akajua hawa ndio wahalifu wake aliokuwa anawatuhumu kwa mauaji ya familia yake na baadhi ya wanakijiji.
Mwanzoni alikuwa anasindikizwa na baradhuli mpaka selo wakati wa kutoa huduma, walipomzoea Dr.Anabella hasa walipojua ni mchumba wa Bosi wao Mark Noble wakaanza kumuamini na kuvunja miiko ya kazi, wakawa wanamuacha aingie peke yake kwa masharti asichelewe kutoka. Wao wanakuwa kwenye sehemu yao ya mapumziko wanakunywa pombe kali na kufurahia starehe. Hilo likawa ni kosa la mwaka kwao, ambalo hawakujua kuwa watakuja kujutia milele.
Kuna siku walipopelekwa kuhojiwa akina Koplo Hamduni, aliyewarudisha selo alifuatana na Dr.Anabella akiwa na pombe yake mkononi, alipokuwa ameshughulishwa na kuwadhibiti akina Koplo Hamduni, Dr.Anabella alifanikiwa kuchanganya vidonge aina ya “Amoxapine” kwenye pombe ya baradhuli yule mlevi buda.
"Amoxapine" ni vidonge vinavyotumika kumrudishia mtu uchangamfu akiwa hana furaha sasa vikichanganywa na pombe vinasababisha usingizi uje kwa haraka. Baradhuli alipokunywa tu akapatwa na usingizi mzito, hapo Dr. Anabella akafanikiwa kuongea na Koplo Hamduni kinagaubaga sababu za kukamatwa kwao. Koplo akamueleza kwa ufupi maana Koplo alikuwa na maumivu makali anaongea kwa shida na Dr.Anabella alijua muda sio mrefu watafuatwa wakiona wanachelewa kurudi.
Hivyo Dr.Anabella pindi alivyokamatwa Kachero Manu, alipatwa na hisia ni washirika wa Koplo Hamduni, ndio maana akamuambia ile siku ya kwanza kazinduka kutoka kuzimia alimuambia kwa NACATANAS watakufuata kukuhoji ili kumpa fununu juu ya watu waliomteka. Ili kama hawajui ila ameshawahi kusikia habari zao apate kutanabahi.
Nafasi ya mwisho ya dhahabu aliyoitumia Dr.Anabella ni kujaribu kuwakutanisha kati ya Koplo Hamduni na Kachero Manu. Alipewa amri Dr.Anabella awachome sindano za sumu Koplo Hamduni na wenzake wakiwa wamefungiwa kwenye majeneza, huku Koplo Hamduni akiwa amefungwa kitandani.
Wale mabaradhuli walikuwa wanamuogopa sana Koplo Hamduni huenda akifungiwa kwenye jeneza anaweza kujitoa kutokana na ukakamavu wake alioonyesha wakati wanamtia mbaroni. Alichofanya Dr.Anabella ni kumchoma Koplo Hamduni sindamu ya sumu chini ya dozi inayotakiwa, ili Koplo Hamduni na Kachero Manu waweze kukutana, na dhana yake njema alijua wakikutana watabadilishana taarifa za kipelelezi, huku akiombea mabaradhuli watakaomleta Kachero Manu selo kubwa wasiwe makini kuchunguza kama Koplo Hamduni na wenzake wamekufa au bado wapo hai.
Lengo la Dr. Anabella lilifanikiwa, Kachero Manu na koplo Hamduni walikutana na kuongea maongezi yaliyokuwa na tija sana kwa Kachero Manu kwa kumpa mwangaza halisi wa upelelezi wake.


SURA YA KUMI NA TANO
Kachero Manu bado hali tete
Kachero Manu usiku ule baada ya maongezi na marehemu Koplo Hamduni, alipigwa na baridi kali hasa ukichukulia alikuwa hajavishwa nguo yoyote mwilini mwake. Akafanikiwa kusota mpaka jirani na jeneza moja akaliegemea ikamsaidia kupunguza joto.
Akapatwa na usingizi mzuri sana uliosaidia kupumzisha mwili wake kiasi fulani. Aliamshwa toka usingizini na mionzi ya jua iliyokuwa inapenya kwenye vidirisha vidogo vya mule chumbani. Akakisia huenda ikawa ni saa mbili na nusu au saa tatu kasoro asubuhi. Sasa akawa ametimiza siku nzima kamili ndani ya selo kuu.
Akaanza kuhisi njaa kali inatafuna utumbo wake, mpaka akaanza kutetemeka kwa njaa. Baada ya kupita kama nusu saa akasikia nyayo za watu zinakaribia mlango wa ile selo kuu alipofungiwa.
Likafunguliwa lango kuu wakaingia watu kama 7 pamoja na Dr. Anabella akiwemo. Walipoingia hawakumsemesha chochote wengine wakashughulishwa na kutoa nje majeneza ambayo sasa yalikuwa na maiti zilizofia ndani yake, na mmoja wao akaenda kwenye kitanda alichofia Koplo Hamduni akamfungua kamba zake na kuiburuta maiti yake nje ya chumba, kitendo ambacho kilimfanya Kachero Manu amuangalie Dr.Anabella kwa umakini akamuona kwa mbali machozi yanamlenga lenga alivyokuwa anaangalia maiti ya Koplo Hamduni. Ila usingeweza kugundua kwa haraka kwa sababu alikuwa amevaa miwani.
Dhamira ya Dr.Anabella ilikuwa inamsuta kwa kufanya mauaji ya Koplo Hamduni kutokana na sindano ya sumu aliyomchoma. Katika maisha yake yote alikuwa hajawahi kuua kiumbe chochote zaidi ya kuua mbu wa Malaria, hata kuua mende alikuwa anaogopa hivi leo baradhuli Mark amempelekea mpaka kuua binadamu wenzake.
Baada kama ya nusu saa wakaondoka na kufunga mlango wa geti la selo. Kachero Manu akazidi kuchanganyikiwa akawa anajiuliza, "hawa watu ni binadamu kweli au ni roboti? Hata chembe ya utu mbona hawana. Wamenichukua toka jana hawajali hata kama nina njaa au hapana". Alikuwa hajawahi hata siku moja maishani mwake kukata tamaa ya kuokoka lakini alianza kuhisi hatopata njia ya kutoroka ndani ya selo hiyo.
Na Dr.Anabella aliyeanza kuwa na matumaini nae kuwa huenda akamukoa nae hakuona kama ana msaada wowote. Maana hata kumuongelesha kuhusu namna ya kutoroka hajawahi. Wala hajawahi kuonyesha ishara yoyote kuwa wapo pamoja kama alivyosimuliwa na Koplo Hamduni.
Akaanza kuiona kurunzi ya mule chumbani kama inaanza kufifia kutokana na kuanza kuishiwa kwa mafuta ya taa. Baada ya kupita kama saa moja kwa kukadiria ni kama saa nne asubuhi akaanza kusikia tena michakato ya miguu ya watu wanakuja tena kwenye selo yake. Ila idadi yao kwa makadirio ilionyesha ni wachache sio kama wale wa mwanzoni, akaanza kufufua matumaini ya kuokoka.
Wale watu walipofika wakafungua lango la selo na kuingia ndani. Alikuwa ni tena Dr.Anabella tena na vijana wa kundi hatari la NACATANAS wapatao wawili. Mmoja alikuwa amebeba trei ya chakula, ilikuwa ni supu ya nyama, matandu meusi ya wali yale ya juu na mkate wa boflo mmoja. Huku mwingine amebeba bunduki aina ya SMG begani hana hata chembe la tabasamu utasema malaika wa motoni kwa jinsi alivyokunja ndita usoni.
Dr.Anabella alikuwa amevaa shingoni mwake kifaa cha kupimia mapigo ya moyo huku koti lake jeupe mifuko yake ikionekana imetuna tuna. Yule aliyebeba trei la chakula akaenda mpaka kwenye meza chakavu iliyokuwa na kurunzi ya mafuta ya taa inayosaidia kueneza mwanga katika selo yenye mwanga khafifu, akaweka trei mezani kisha akamfuata Kachero Manu kumfungua kamba zake za mikononi pekee, kisha akamletea chakula ale.
"Usijaribu kuleta ujanja wowote, jaribio lolote utakalofanya litagharimu uhai wao, kula ujisosomole kuondosha njaa yako" alisema yule baradhuli aliyebeba SMG huku akiwa amemuelekezea Kachero Manu mdomo wa bunduki. Dr.Anabella akawa nae kaisogelea meza ile chakavu akatoa baadhi ya chupa za madawa, mkasi na pamba akaweka juu ya meza kisha akaegemea meza anamuangalia Kachero Manu anavyopokea chakula.


Sent using Jamii Forums mobile app
Kitu matata sana kimekatikia patamu..
 
Back
Top Bottom