mpasta
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 919
- 2,007
- Thread starter
- #21
RIWAYA: "CABO-DELGADO"-PART 10














Chikulubu, Utingo msaliti hana fadhila
"Chikulubu Wa Chipoku" ni kijana aliyechukuliwa na dereva Masebbo tokea akiwa ghulamu wa miaka 15, na kwa bahati mbaya sana hakujaaliwa kusoma hata darasa moja maishani mwake, mbumbumbu mzungu wa reli hana lolote alijualo hapa duniani kuhusu elimu ya darasani.
Wazazi wake walikuwa ni Wamakonde Chale wa Msumbiji ambao kipindi cha msimu wa kilimo wanavuka mpaka na kwenda Tanzania kufanya vibarua vya kilimo katika vijijini vya mpakani kwa malipo ya mshahara tonge, mkia wa mbuzi usiokidhi mahitaji yao ipasavyo.
Msimu wa kilimo ukiisha wanarejea kwao Msumbiji kusubiri msimu ujao wa kilimo. Hayo ndio yalikuwa maisha yao daima dawamu wanacheza katika mnyororo wa umasikini.
Ilitokea siku moja isiyo na jina dereva Masebbo akiwa na Lori lake alipata pancha ya lori lake jirani na kijiji cha akina Chikulubu na utingo wake wa kawaida hakuwepo kwenye safari bila kutoa taarifa kwa dereva Masebbo hivyo kumpelekea dereva kusafiri bila Utingo.
Chikulubu ndio alimsaidia dereva Masebbo kubadili tairi la gari pamoja na kumtafutia chakula na maji. Kama zali la mentali vile, hiyo ikawa ni sababu ya Chikulubu kula maisha akapata ajira kama Taniboi wa Mzee Masebbo.
Sasa safari za mipakani kwenda Tanzania, Zambia na Zimbabwe zikawa kama kuingia chooni kwa Chikulubu, kismati kinamtembelea. Maisha yake sasa yakapata naizesheni na nafuu kubwa na akahama kijijini na kupanga chumba katika Mji wa Cabo-Delgado.
Amedumu na dereva Masebbo kwa muda wa miaka 10 mtawalia. Lakini hivi karibuni akaanza kubadilika tabia mambo yake yakaanza kuwa tumbitumbi yasiyo na kichwa wala miguu. Hasa baada ya kuanza kukaa vijiweni, akaanza kupenda wanawake, pombe na kila aina ya starehe za vijana wa Mjini.
Vijiwe vya vijana wa kihuni wenye hadithi za kwenda kutafuta maisha bora Afrika ya kusini na ulaya kwa kuzamia meli, na kupata maisha bora bila kufanya juhudi na maarifa. Akaanza tabia ya kuiba mafuta kwenye gari la Mzee Masebbo. Vijana wa mjini wanaita "kupiga nyoka" gari.
Mzee Masebbo alimuonya sana zaidi ya mara tatu hasa akimchukulia kama mtoto wake aliyemtoa kijijini zaidi ya miaka 10 iliyopita mpaka amebaleghe mikononi mwake. Lakini kama ujuavyo mtoto akinyea kiganja hakikatwi kinasafishwa tu, ndivyo namna Mzee Masebbo alivyokuwa anamvumilia Chikulubu.
Sasa kilichomzuzua Chikulubu ni tukio la hivi karibuni la Taniboi mwenzake ambae ni rafiki yake kipenzi cha kuwasakizia Wafanyabiashara wa madini kutoka Tanzania waliokuwa wamewapakiza kwenye gari lao kwa Mafioso wa Alfredo. Ambapo baada ya wale Wafanyabiashara kuporwa madini yao Taniboi huyo alilipwa pesa nzuri sana.
Pesa ambayo iliyomuwezesha kupanga nyumba nzima na kununua bodaboda mbili zinazovuka mpaka kati ya Tanzania na Msumbiji kubeba mizigo. Toka siku hiyo Chikulubu nae akawa ni mtu wa macho juu juu, shingo feni mwenye wahaka mkubwa kwa kila abiria anayehisi ni Mtanzania wanayempakia kwenye gari lao.
Sasa siku ile ya safari nadhani unakumbuka alikuwa anamtazama sana Kachero Manu mpaka Kachero akashtukia. Sasa hisia zake kuwa Kachero Manu ni mtu muhimu na anaingia nchini mwao Msumbiji kinyemela ni pale waliposimamishwa na askari barabarani halafu alipoulizwa dereva Masebbo kama wote ni raia wa Msumbiji, na dereva Masebbo akajibu wote ni raia hapo hapo akaanza kushikwa na tamaa ya utajiri kupitia Kachero Manu.
Akajua ni mtu muhimu ndio maana Mzee Masebbo anamficha kwa wale askari wasimkamate. Pia kitendo cha Mzee Masebbo kuzuga gari limeharibika ili kumsubiria Kachero Manu, Taniboi Chikulubu alishtukia mchezo mzima.
Kitendo hicho cha usanii wa dereva Masebbo kilimpa maono kuwa Kachero Manu sio mtu mzuri ndio maana analindwa na dereva Masebbo kwa hali na mali. Na kama akifikisha taarifa zake kwa Mafioso wa Alfredo chini ya uongozi wa Inspekta Mark Noble atalipwa pesa sufufu za kumfanya aishi maisha mazuri.
Hivyo walipofika tu Cabo-Delgado, pale Msikitini hakupata hata muda wa kuagana hata na dereva wake kwa kile kimuhemuhe na kiroho papu cha pesa ya madili. Akatokomea zake mtaani kumtafuta yule rafiki yake ampeleke kwa Mafioso wa Cabo-Delgado ili awape penyenye za Kachero Manu kuwa amebebwa kwenye gari la Bosi wake Mzee Masebbo.
Vijana wa kazi wa Inspekta Jenerali Mark Noble walivyoletewa taarifa tu kitu cha kwanza walienda kwenye kituo cha taksi na kuwaelezea wajihi wa mtu wanayemtafuta bahati nzuri wakampata yule dereva aliyempeleka Kachero Manu pale Nzuwa Lodge.
Mafioso walipofika Nzuwa Lodge, walijitambulisha kama maafisa usalama wakakagua kompyuta inayorekodi taarifa za wageni. Bahati mbaya mlengwa wao hakuandika taarifa zake mapema hivyo ikazidi kuwatia mashaka kuwa Kachero Manu sio mtu mzuri.
Hivyo wakaingia chumbani kufanya upekuzi nako hawakupata wanachokikusudia. Wakiwa mule chumbani wakapigiwa simu na kupewa taarifa mbaya ya kuuliwa Askari 6 wanaokagua Watanzania wanaoingia kupitia mpakani.
Pale pale ndio wakaondoka mbio mbio kuelekea nyumbani kwa dereva Masebbo kumfanyia mahojiano juu ya yule mgeni aliyembeba kwenye gari ni ni nani na kaja kufanya nini Cabo-Delgado, kama walivyopewa taarifa na Taniboi wake Chikulubu.
Taniboi msaliti asiyejua kulipa fadhila, ama kweli "shukrani ya punda ni mateke, daima tenda wema uende zako usingoje shukrani, fadhila mfadhili mbuzi utaambulia mchuzi, binadamu ana maudhi".















Mauaji mtaa wa Ruvuma nyumba namba 23B
Mzee Masebbo aliporudi safari yake baada ya kufikisha mzigo wa magendo wa watu salama alienda kwenye kampuni ya tajiri wake akaliegesha gari na kurudi nyumbani kwake kupumzika. Nyumbani kwake alikuwa amebaki peke yake, mkewe na watoto wake watatu wanaosoma sekondari walikuwa wamekwenda likizo eneo la Muidumbe moja ya Wilaya za "Cabo-Delgado".
Huko Muidumbe ndipo ambapo ndio walipo wakwe zake Mzee Masebbo. Alivyofika nyumbani kwake kwanza alikunywa chai kwa mkate alionunua njiani wakati anarejea nyumbani kisha alipitiliza kuoga. Baada ya hapo akaingia kulala kwa nia ya kuamka mchana, afanye usafi wa nyumba na kupika chakula ale.
Alivyopanda kitandani hii asubuhi Mzee Masebbo alikuwa na mawazo mengi sana, hasa juu ya uamuzi anaotaka kuchukua wa kuacha kazi. Alikuwa hapendezwi na namna kampuni yao ya usafirishaji ilivyoanza sasa kushiriki kubeba mizigo haramu ya Mafioso wa Alfredo.
Kitu ambacho hakupendezwa na dhulma anazoshiriki kufanya kwa kuiba Maliasili za Tanzania na kuwafanyia vitendo vya kikatili Watanzania. Aliweka nia mwisho wa mwezi ukifika akipokea mshahara wake tu, ndio utakuwa mwisho wa ajira yake.
Lakini pia akawa anawaza ataendeshaje familia yake bila kazi, hasa katika Mji mkubwa kama huu wa Cabo-Delgado ambao gharama za maisha zipo juu kupitiliza kutokana na ujio wa Watalii toka pande mbalimbali za dunia. Watoto wake bado wanasoma sekondari kwenye shule za kulipia gharama kubwa na mkewe ni mama wa nyumbani, golikipa maarufu mtaani hawezi hata kujitafutia senti tano nyeusi.
Pia na kijijini wazee wake wameshakuwa watu wazima wanamtegemea yeye kwa hali na mali, hawajiwezi kwa sukari wala si kwa chumvi. Fikra hizo zikamfanya ajiweke njia panda, achague mwenyewe kusuka ama kunyoa.
Lakini mwishowe akapiga moyo konde kuwa lolote liwalo na liwe atapeleka barua ya kuacha kazi itakapofika mwisho wa mwezi, hilo ndio likawa hitimisho lake.
"Penye nia pana njia, nitakapoacha kazi nitatafuta sehemu nyingine ya kupatia mkate wangu wa siku na Mungu atanifungulia njia", aliujaza moyo wake ushujaa. Akajikuta anapitiwa na usingizi muda huo wa saa 4 asubuhi.
Mzee Masebbo aliamshwa usingizini na sauti za vishindo vya kugongwa kwa mlango wake kwa nguvu. Mwanzoni alidhania kama yupo ndotoni lakini aliposhtuka akajua kuna watu wanagonga kiukweli sio njozi.
Akapatwa na hofu ya kutaka kufahamu nini kimetokea mpaka anaongewa mlango wake kibabe. Maana namna alivyokuwa anaishi na majirani zake kila mtu anashika hamsini zake.
Huwa wanaonana kwenye matukio ya msiba au sherehe lakini hawana utamaduni wa Kitanzania wa kutembeleana kujuliana hali hujambo sijambo. Akakurupuka toka kitandani, kitambi wazi na pajama yake mbio mbio kwenda kwenda kufungua.
"Nani mwenzangu"? aliuliza Mzee Masebbo wakati anajiandaa kukitegua kitasa cha mlango kwa funguo. Akajibiwa toka nje ya mlango "fungua sisi ni wana usalama tuna mahojiano na wewe". Mwili wake ukapigwa na ubaridi wa ghafla kwa sekunde kadhaa, haja zote kubwa na ndogo anazihisi zinagonga chupi kwa uoga.
Akaanza kutetemeka, kijasho chembamba kinamvuja huku akijiuliza bila kupata majibu kafanya kosa gani. Akapiga moyo konde, akajikaza kisabuni akaamua awafungulie maadamu dhamira yake ipo safi moyoni na hana kosa lolote.
Alipofungua tu wakaingia vijana wawili kwa kishindo. Walivalia suti za bluu na miwani.
"Yupo wapi abiria wako toka Tanzania uliyekuja nae leo usiku?" aliulizwa swali la kushtukiza Mzee Masebbo kwa ukali tena kuwa na ustaarabu. Akajibu kwa sauti ya kitete "mie sijapakiza Mtanzania, walikuwa wanafunzi wa madrasa na Maustaadhi wao basi", alidanganya Mzee Masebbo, huku akiomba Mungu kimya kimya uwongo wake ukubalike.
Hakujua kama wanazo taarifa zake zote, nje ndani toka kwa Taniboi wake Chikulubu. "Mzee mzima kama wewe unasema uwongo hata huoni aibu? Taniboi wako katueleza kila kitu usicheze na akili zetu wewe kikaragosi", alisema mmoja wao wale majambazi kwa hasira, huku akimsogelea amuadabishe.
Mzee Masebbo uso wake ukavaa taharuki, sasa akijua Chikulubu ameshamuuza. Chikulubu aligeuka zigo la misumari habebeki tena. Sasa tutakufundisha namna ya kusema ukweli, alisema mmoja wapo huku anamfuata Mzee Masebbo na kumpiga ngwara, Mzee Masebbo alianguka mzima mzima kama gunia la mahindi toka Zimbabwe la uzito wa kilo mia.
Akaangukia mdomo na kuvunja meno kadhaa. Damu zikaanza kumchuruzika kinywani bila kizuizi. Kisha akamkaba roho kwa kabali juu kidogo ya koo la Mzee Masebbo. Akaanza kukosa hewa safi, "mtani...u....aa.. bu... r.... .......e, mi...mi... simf....a.... h... a..... mu" alisema Mzee Masebbo kwa tabu sana, akikataa kuwa Yuda dhidi ya Kachero Manu.
"Jimmy muache kwanza huenda atasema, eheee wewe babu eleza haraka hatuna muda wa kupoteza tutakupoteza sasa hivi ukifanya mchezo" alisema mmoja wa wajuba wale aliyejipambanua kama ni kiongozi wa mwenzake.
Jimmy akamuachia koo Mzee Masebbo, akaanza kuhema kwa tabu kisha akakohoa makohozi yaliyochanganyika na damu, kisha akaanza kujieleza. "Ni kweli nilimpakia Mtanzania lakini simfahamu kiukweli shughuli zake, nilimsaidia tu kiubinadamu, kwa sababu hamna usafiri wa uhakika kwa sasa. Huo ndio ukweli wangu mtaniua bure lakini sina ninachokijua juu yake", alijieleza Mzee Masebbo kwa uchungu akijua fika anataka kutolewa sadaka bila kosa lolote.
"Kwanini sasa walipokuja Askari kukuuliza kama wote ni raia wa Msumbiji uliamua kumficha mgeni wako?" aliendelea kusailiwa na Jimmy. Mzee Masebbo akawa hana la kujibu anaangalia chini tu, amepatwa na fadhaa huku anajifuta damu kwenye ncha mdomo wake.
"Je unafahamu kuwa huyo mgeni wako uliyemleta mpaka Cabo-Delgado ameua askari wetu 6?, Sasa malipo ya umamluki ni risasi ya ubongo ukasimulie huko jongomeo unakokwenda kuwa usaliti haufai", bila kuchelewa Jimmy akafyatua risasi iliyompata Mzee Masebbo kisawasawa kwenye paji lake la uso na kukifumua kichwa chake kama tikitimaji lililopasuka.
Mzee Masebbo akaanguka chini na kuanza kufafaruka kwa kutupa tupa miguu yake kama mgonjwa kifafa akipigania roho yake. Bila kuchelewa wakatoka nje na kupanda gari lao wakatokomea zao, na kumuachia Mzee Masebbo anapigania uhai wake katika dakika za mwisho mwisho kabla hajaelekea jongomeo.













Sent using Jamii Forums mobile app














Chikulubu, Utingo msaliti hana fadhila
"Chikulubu Wa Chipoku" ni kijana aliyechukuliwa na dereva Masebbo tokea akiwa ghulamu wa miaka 15, na kwa bahati mbaya sana hakujaaliwa kusoma hata darasa moja maishani mwake, mbumbumbu mzungu wa reli hana lolote alijualo hapa duniani kuhusu elimu ya darasani.
Wazazi wake walikuwa ni Wamakonde Chale wa Msumbiji ambao kipindi cha msimu wa kilimo wanavuka mpaka na kwenda Tanzania kufanya vibarua vya kilimo katika vijijini vya mpakani kwa malipo ya mshahara tonge, mkia wa mbuzi usiokidhi mahitaji yao ipasavyo.
Msimu wa kilimo ukiisha wanarejea kwao Msumbiji kusubiri msimu ujao wa kilimo. Hayo ndio yalikuwa maisha yao daima dawamu wanacheza katika mnyororo wa umasikini.
Ilitokea siku moja isiyo na jina dereva Masebbo akiwa na Lori lake alipata pancha ya lori lake jirani na kijiji cha akina Chikulubu na utingo wake wa kawaida hakuwepo kwenye safari bila kutoa taarifa kwa dereva Masebbo hivyo kumpelekea dereva kusafiri bila Utingo.
Chikulubu ndio alimsaidia dereva Masebbo kubadili tairi la gari pamoja na kumtafutia chakula na maji. Kama zali la mentali vile, hiyo ikawa ni sababu ya Chikulubu kula maisha akapata ajira kama Taniboi wa Mzee Masebbo.
Sasa safari za mipakani kwenda Tanzania, Zambia na Zimbabwe zikawa kama kuingia chooni kwa Chikulubu, kismati kinamtembelea. Maisha yake sasa yakapata naizesheni na nafuu kubwa na akahama kijijini na kupanga chumba katika Mji wa Cabo-Delgado.
Amedumu na dereva Masebbo kwa muda wa miaka 10 mtawalia. Lakini hivi karibuni akaanza kubadilika tabia mambo yake yakaanza kuwa tumbitumbi yasiyo na kichwa wala miguu. Hasa baada ya kuanza kukaa vijiweni, akaanza kupenda wanawake, pombe na kila aina ya starehe za vijana wa Mjini.
Vijiwe vya vijana wa kihuni wenye hadithi za kwenda kutafuta maisha bora Afrika ya kusini na ulaya kwa kuzamia meli, na kupata maisha bora bila kufanya juhudi na maarifa. Akaanza tabia ya kuiba mafuta kwenye gari la Mzee Masebbo. Vijana wa mjini wanaita "kupiga nyoka" gari.
Mzee Masebbo alimuonya sana zaidi ya mara tatu hasa akimchukulia kama mtoto wake aliyemtoa kijijini zaidi ya miaka 10 iliyopita mpaka amebaleghe mikononi mwake. Lakini kama ujuavyo mtoto akinyea kiganja hakikatwi kinasafishwa tu, ndivyo namna Mzee Masebbo alivyokuwa anamvumilia Chikulubu.
Sasa kilichomzuzua Chikulubu ni tukio la hivi karibuni la Taniboi mwenzake ambae ni rafiki yake kipenzi cha kuwasakizia Wafanyabiashara wa madini kutoka Tanzania waliokuwa wamewapakiza kwenye gari lao kwa Mafioso wa Alfredo. Ambapo baada ya wale Wafanyabiashara kuporwa madini yao Taniboi huyo alilipwa pesa nzuri sana.
Pesa ambayo iliyomuwezesha kupanga nyumba nzima na kununua bodaboda mbili zinazovuka mpaka kati ya Tanzania na Msumbiji kubeba mizigo. Toka siku hiyo Chikulubu nae akawa ni mtu wa macho juu juu, shingo feni mwenye wahaka mkubwa kwa kila abiria anayehisi ni Mtanzania wanayempakia kwenye gari lao.
Sasa siku ile ya safari nadhani unakumbuka alikuwa anamtazama sana Kachero Manu mpaka Kachero akashtukia. Sasa hisia zake kuwa Kachero Manu ni mtu muhimu na anaingia nchini mwao Msumbiji kinyemela ni pale waliposimamishwa na askari barabarani halafu alipoulizwa dereva Masebbo kama wote ni raia wa Msumbiji, na dereva Masebbo akajibu wote ni raia hapo hapo akaanza kushikwa na tamaa ya utajiri kupitia Kachero Manu.
Akajua ni mtu muhimu ndio maana Mzee Masebbo anamficha kwa wale askari wasimkamate. Pia kitendo cha Mzee Masebbo kuzuga gari limeharibika ili kumsubiria Kachero Manu, Taniboi Chikulubu alishtukia mchezo mzima.
Kitendo hicho cha usanii wa dereva Masebbo kilimpa maono kuwa Kachero Manu sio mtu mzuri ndio maana analindwa na dereva Masebbo kwa hali na mali. Na kama akifikisha taarifa zake kwa Mafioso wa Alfredo chini ya uongozi wa Inspekta Mark Noble atalipwa pesa sufufu za kumfanya aishi maisha mazuri.
Hivyo walipofika tu Cabo-Delgado, pale Msikitini hakupata hata muda wa kuagana hata na dereva wake kwa kile kimuhemuhe na kiroho papu cha pesa ya madili. Akatokomea zake mtaani kumtafuta yule rafiki yake ampeleke kwa Mafioso wa Cabo-Delgado ili awape penyenye za Kachero Manu kuwa amebebwa kwenye gari la Bosi wake Mzee Masebbo.
Vijana wa kazi wa Inspekta Jenerali Mark Noble walivyoletewa taarifa tu kitu cha kwanza walienda kwenye kituo cha taksi na kuwaelezea wajihi wa mtu wanayemtafuta bahati nzuri wakampata yule dereva aliyempeleka Kachero Manu pale Nzuwa Lodge.
Mafioso walipofika Nzuwa Lodge, walijitambulisha kama maafisa usalama wakakagua kompyuta inayorekodi taarifa za wageni. Bahati mbaya mlengwa wao hakuandika taarifa zake mapema hivyo ikazidi kuwatia mashaka kuwa Kachero Manu sio mtu mzuri.
Hivyo wakaingia chumbani kufanya upekuzi nako hawakupata wanachokikusudia. Wakiwa mule chumbani wakapigiwa simu na kupewa taarifa mbaya ya kuuliwa Askari 6 wanaokagua Watanzania wanaoingia kupitia mpakani.
Pale pale ndio wakaondoka mbio mbio kuelekea nyumbani kwa dereva Masebbo kumfanyia mahojiano juu ya yule mgeni aliyembeba kwenye gari ni ni nani na kaja kufanya nini Cabo-Delgado, kama walivyopewa taarifa na Taniboi wake Chikulubu.
Taniboi msaliti asiyejua kulipa fadhila, ama kweli "shukrani ya punda ni mateke, daima tenda wema uende zako usingoje shukrani, fadhila mfadhili mbuzi utaambulia mchuzi, binadamu ana maudhi".















Mauaji mtaa wa Ruvuma nyumba namba 23B
Mzee Masebbo aliporudi safari yake baada ya kufikisha mzigo wa magendo wa watu salama alienda kwenye kampuni ya tajiri wake akaliegesha gari na kurudi nyumbani kwake kupumzika. Nyumbani kwake alikuwa amebaki peke yake, mkewe na watoto wake watatu wanaosoma sekondari walikuwa wamekwenda likizo eneo la Muidumbe moja ya Wilaya za "Cabo-Delgado".
Huko Muidumbe ndipo ambapo ndio walipo wakwe zake Mzee Masebbo. Alivyofika nyumbani kwake kwanza alikunywa chai kwa mkate alionunua njiani wakati anarejea nyumbani kisha alipitiliza kuoga. Baada ya hapo akaingia kulala kwa nia ya kuamka mchana, afanye usafi wa nyumba na kupika chakula ale.
Alivyopanda kitandani hii asubuhi Mzee Masebbo alikuwa na mawazo mengi sana, hasa juu ya uamuzi anaotaka kuchukua wa kuacha kazi. Alikuwa hapendezwi na namna kampuni yao ya usafirishaji ilivyoanza sasa kushiriki kubeba mizigo haramu ya Mafioso wa Alfredo.
Kitu ambacho hakupendezwa na dhulma anazoshiriki kufanya kwa kuiba Maliasili za Tanzania na kuwafanyia vitendo vya kikatili Watanzania. Aliweka nia mwisho wa mwezi ukifika akipokea mshahara wake tu, ndio utakuwa mwisho wa ajira yake.
Lakini pia akawa anawaza ataendeshaje familia yake bila kazi, hasa katika Mji mkubwa kama huu wa Cabo-Delgado ambao gharama za maisha zipo juu kupitiliza kutokana na ujio wa Watalii toka pande mbalimbali za dunia. Watoto wake bado wanasoma sekondari kwenye shule za kulipia gharama kubwa na mkewe ni mama wa nyumbani, golikipa maarufu mtaani hawezi hata kujitafutia senti tano nyeusi.
Pia na kijijini wazee wake wameshakuwa watu wazima wanamtegemea yeye kwa hali na mali, hawajiwezi kwa sukari wala si kwa chumvi. Fikra hizo zikamfanya ajiweke njia panda, achague mwenyewe kusuka ama kunyoa.
Lakini mwishowe akapiga moyo konde kuwa lolote liwalo na liwe atapeleka barua ya kuacha kazi itakapofika mwisho wa mwezi, hilo ndio likawa hitimisho lake.
"Penye nia pana njia, nitakapoacha kazi nitatafuta sehemu nyingine ya kupatia mkate wangu wa siku na Mungu atanifungulia njia", aliujaza moyo wake ushujaa. Akajikuta anapitiwa na usingizi muda huo wa saa 4 asubuhi.
Mzee Masebbo aliamshwa usingizini na sauti za vishindo vya kugongwa kwa mlango wake kwa nguvu. Mwanzoni alidhania kama yupo ndotoni lakini aliposhtuka akajua kuna watu wanagonga kiukweli sio njozi.
Akapatwa na hofu ya kutaka kufahamu nini kimetokea mpaka anaongewa mlango wake kibabe. Maana namna alivyokuwa anaishi na majirani zake kila mtu anashika hamsini zake.
Huwa wanaonana kwenye matukio ya msiba au sherehe lakini hawana utamaduni wa Kitanzania wa kutembeleana kujuliana hali hujambo sijambo. Akakurupuka toka kitandani, kitambi wazi na pajama yake mbio mbio kwenda kwenda kufungua.
"Nani mwenzangu"? aliuliza Mzee Masebbo wakati anajiandaa kukitegua kitasa cha mlango kwa funguo. Akajibiwa toka nje ya mlango "fungua sisi ni wana usalama tuna mahojiano na wewe". Mwili wake ukapigwa na ubaridi wa ghafla kwa sekunde kadhaa, haja zote kubwa na ndogo anazihisi zinagonga chupi kwa uoga.
Akaanza kutetemeka, kijasho chembamba kinamvuja huku akijiuliza bila kupata majibu kafanya kosa gani. Akapiga moyo konde, akajikaza kisabuni akaamua awafungulie maadamu dhamira yake ipo safi moyoni na hana kosa lolote.
Alipofungua tu wakaingia vijana wawili kwa kishindo. Walivalia suti za bluu na miwani.
"Yupo wapi abiria wako toka Tanzania uliyekuja nae leo usiku?" aliulizwa swali la kushtukiza Mzee Masebbo kwa ukali tena kuwa na ustaarabu. Akajibu kwa sauti ya kitete "mie sijapakiza Mtanzania, walikuwa wanafunzi wa madrasa na Maustaadhi wao basi", alidanganya Mzee Masebbo, huku akiomba Mungu kimya kimya uwongo wake ukubalike.
Hakujua kama wanazo taarifa zake zote, nje ndani toka kwa Taniboi wake Chikulubu. "Mzee mzima kama wewe unasema uwongo hata huoni aibu? Taniboi wako katueleza kila kitu usicheze na akili zetu wewe kikaragosi", alisema mmoja wao wale majambazi kwa hasira, huku akimsogelea amuadabishe.
Mzee Masebbo uso wake ukavaa taharuki, sasa akijua Chikulubu ameshamuuza. Chikulubu aligeuka zigo la misumari habebeki tena. Sasa tutakufundisha namna ya kusema ukweli, alisema mmoja wapo huku anamfuata Mzee Masebbo na kumpiga ngwara, Mzee Masebbo alianguka mzima mzima kama gunia la mahindi toka Zimbabwe la uzito wa kilo mia.
Akaangukia mdomo na kuvunja meno kadhaa. Damu zikaanza kumchuruzika kinywani bila kizuizi. Kisha akamkaba roho kwa kabali juu kidogo ya koo la Mzee Masebbo. Akaanza kukosa hewa safi, "mtani...u....aa.. bu... r.... .......e, mi...mi... simf....a.... h... a..... mu" alisema Mzee Masebbo kwa tabu sana, akikataa kuwa Yuda dhidi ya Kachero Manu.
"Jimmy muache kwanza huenda atasema, eheee wewe babu eleza haraka hatuna muda wa kupoteza tutakupoteza sasa hivi ukifanya mchezo" alisema mmoja wa wajuba wale aliyejipambanua kama ni kiongozi wa mwenzake.
Jimmy akamuachia koo Mzee Masebbo, akaanza kuhema kwa tabu kisha akakohoa makohozi yaliyochanganyika na damu, kisha akaanza kujieleza. "Ni kweli nilimpakia Mtanzania lakini simfahamu kiukweli shughuli zake, nilimsaidia tu kiubinadamu, kwa sababu hamna usafiri wa uhakika kwa sasa. Huo ndio ukweli wangu mtaniua bure lakini sina ninachokijua juu yake", alijieleza Mzee Masebbo kwa uchungu akijua fika anataka kutolewa sadaka bila kosa lolote.
"Kwanini sasa walipokuja Askari kukuuliza kama wote ni raia wa Msumbiji uliamua kumficha mgeni wako?" aliendelea kusailiwa na Jimmy. Mzee Masebbo akawa hana la kujibu anaangalia chini tu, amepatwa na fadhaa huku anajifuta damu kwenye ncha mdomo wake.
"Je unafahamu kuwa huyo mgeni wako uliyemleta mpaka Cabo-Delgado ameua askari wetu 6?, Sasa malipo ya umamluki ni risasi ya ubongo ukasimulie huko jongomeo unakokwenda kuwa usaliti haufai", bila kuchelewa Jimmy akafyatua risasi iliyompata Mzee Masebbo kisawasawa kwenye paji lake la uso na kukifumua kichwa chake kama tikitimaji lililopasuka.
Mzee Masebbo akaanguka chini na kuanza kufafaruka kwa kutupa tupa miguu yake kama mgonjwa kifafa akipigania roho yake. Bila kuchelewa wakatoka nje na kupanda gari lao wakatokomea zao, na kumuachia Mzee Masebbo anapigania uhai wake katika dakika za mwisho mwisho kabla hajaelekea jongomeo.













Sent using Jamii Forums mobile app

