SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA MIA NA ISHIRINI
Dokta Yusha alifika hadi pale kileleni, juu ya ukuta. Kutokea kule kwa juu alishuhudia vizuri mandhari ya kule ndani ya kambi, ambayo yeye alikuwa anayafahamu vizuri kabla......
Kumbuka Dokta Yusha alipanda ule ukuta wa kambi ile hatarii asubuhi jua likiwa limechomoza, na pia Dokta Yusha alikuwa kashawahi kuingia katika kambi ile, na kwa bahati nzuri zaidi alibahatika kutoka salama. Akiwa pale kwa juu alipeleka macho yake katika kibanda kilichokuwa pembeni kidogo mwa ile nyumba ya bluu. Dokta Yusha alikumbuka mengi sana wakati anakiangalia kibanda kile. Alimkumbuka yule askari aliyepoteza uhai wake katika kiti cha kifo ndani ya kibanda kile. Askari aliyekufa kwa kubadirika rangi na kuwa nyekundu sambamba na kiti kile na kupotea katika ulimwengu kwa kuyeyuka palepale katika kiti cha kifo.
Dokta Yusha alimkumbuka yule jamaa aliyepambana nae katika kibanda kile, na kufanikiwa kumsukuma katika kiti cha kifo! Kilichopo ndani ya kibanda alichokuwa anakitazama. Nae aliyeyuka huku akibadirika rangi sambamba na kiti. Akiwa kule juu Dokta Yusha alijipa moyo, huku akijivika ujasiri kuwa lazima akapambane!
Sasa dokta Yusha alifuta kabisa hali ya hofu katika moyo wake na kuona ni heri kufa kishujaa, kuliko kuishi ukiwa unashuhudia maovu yakiendelea kufanyika ulimwenguni. Kilikuwa ni kiapo alichoapa Dokta Yusha akiwa juu ya ukuta hatari....na alipania kukitekeleza kiapo chake.
"Nitakufa nikipambana..." Dokta Yusha alihitimisha mawazo yake kwa kujisemea mwenyewe kimoyomoyo.
Kwa taarifa tu, ule mti uliokaribu na ukuta wa kambi ya Six Killers uliachwa kwa makusudi na kundi la Six killers sehemu ile. Hawakutaka kuukata ingawa walikuwa na uwezo huo. Ni Moja wa six Killers ndiye aliyeshauri mti ule uachwe, kwa makusudi ili utumike kama mtego. Ndio...... Waliuacha mti ule wakijua adui yoyote akitaka kuingia katika ile nyumba lazima atautumia ule mti. Maana ndo sehemu pekee iliyokuwepo kwa mtu mjanja kuingia mle ndani ya kambi yao. Nao kule ndani hawakuzubaa hata chembe, wakiwa kule kwa ndani walikuwa wanaulinda kwa kuuangalia ule mti kila baada ya dakika tatu....
ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA