Riwaya - Balaa

Riwaya - Balaa

Siyo kweli,riwaya nyingine unaposoma unajua tu hii ni fupi na hii ndefu,chukulia TUTARUDI NA ROHO ZETU? na BARUA KUTOKA JELA,je,unaposoma riwaya hizi unaziona fupi?.

So u mean jamaa anairefusha hii hadithi au umemaanisha nini mkuu??
 
Siyo kweli,riwaya nyingine unaposoma unajua tu hii ni fupi na hii ndefu,chukulia TUTARUDI NA ROHO ZETU? na BARUA KUTOKA JELA,je,unaposoma riwaya hizi unaziona fupi?.

Kibishi we mbishi km jina lako. ..zote nimezisoma...una shida wewe
 
🚶🚶🚶🚶🚶🚶🚶🚶🚶
 
Sasa mapengo junior huu muda badala ya kutupia riwaya,wewe unabishana?

Wewe pia kichwa maji...na mbishi sijui mpuuzi au usomi comment..nawasiwasi na ubongo wako...sipendi kujibu comments sababu ntatukana watu bureee ukipenda subiria autaki Acha kusoma
 
Wewe pia kichwa maji...na mbishi sijui mpuuzi au usomi comment..nawasiwasi na ubongo wako...sipendi kujibu comments sababu ntatukana watu bureee ukipenda subiria autaki Acha kusoma


Kweli jina lako linafanana na unavyotupia hii hadithi yako. Unatupia kwa kurusha muda mrefu, ki mapengo mapengo!
 
Wewe pia kichwa maji...na mbishi sijui mpuuzi au usomi comment..nawasiwasi na ubongo wako...sipendi kujibu comments sababu ntatukana watu bureee ukipenda subiria autaki Acha kusoma

Kutukana ilipaswa tukutane wewe.
Hasira ilipaswa kuwa nazo sisi.
 
Kutukana ilipaswa tukutane wewe.
Hasira ilipaswa kuwa nazo sisi.

Ila kabla hujatukana mkuu jiulize ni kiasi gani unalipia hii hadithi.Yawezekana jamaa anazingua kwa kuzileta fupi au kwa kuzichelewesha.Lakini pia kumbuka kuwa ww unapokuwa free ndio unaingia huku kuperuzi hadithi,ukibanwa na majukumu hutokei humu ndani,so hata mapengo junior nae anaratiba zake.

Ila mkuu mapengo junior kuepusha matusi na jazba za wasomaji unaweza ukawapa ratiba ya utokaji wa hii hadithi ili mtu awe anajua siku flan akiingia ataikuta.Maana hii kukaripiana wakati hata kujuana hatujuani inakuwa sio vzr
 
Last edited by a moderator:
Ila kabla hujatukana mkuu jiulize ni kiasi gani unalipia hii hadithi.Yawezekana jamaa anazingua kwa kuzileta fupi au kwa kuzichelewesha.Lakini pia kumbuka kuwa ww unapokuwa free ndio unaingia huku kuperuzi hadithi,ukibanwa na majukumu hutokei humu ndani,so hata mapengo junior nae anaratiba zake.

Ila mkuu mapengo junior kuepusha matusi na jazba za wasomaji unaweza ukawapa ratiba ya utokaji wa hii hadithi ili mtu awe anajua siku flan akiingia ataikuta.Maana hii kukaripiana wakati hata kujuana hatujuani inakuwa sio vzr

Nilishasema huko nyuma...ratiba kila siku naweka moja watu wakapiga kelele sana haiwezeka nkawa naeka mbili watu wakaona haitoshi nikawa naeka tatu pia haitoshi mwisho nikaishiwa vipande vyoote nilivyo navyo...
Mkumbuke mm sio mtunzi wa hii riwaya ila ni member wa JF nikaona si mbaya kushea na wanajamii forum wezangu..
Istoshe mm naisoma kwa kulipia ktk group la WhatsApp la huyo mtunzi na nilishaweka matangazo sana humu anaetaka ajiunge..
Ratiba maalumu siwezi toa kwa sababu me sio mtunzi pia hata ktk group letu mtunzi mara nyingine hatumi anatuomba radhi kwa kuwa tumelipia...kuhusu vpande vdg mm na copy na kupaste hivyo lipo nje ya uwezo wangu...
Anaeweza kusubiri asubiri asieweza a ache. comments nyingine hazivumiliki watu wanapenda kusemwa vibaya
Big up analyse kwa comments nzuri zenye kujenga
 
Last edited by a moderator:
Nilishasema huko nyuma...ratiba kila siku naweka moja watu wakapiga kelele sana haiwezeka nkawa naeka mbili watu wakaona haitoshi nikawa naeka tatu pia haitoshi mwisho nikaishiwa vipande vyoote nilivyo navyo...
Mkumbuke mm sio mtunzi wa hii riwaya ila ni member wa JF nikaona si mbaya kushea na wanajamii forum wezangu..
Istoshe mm naisoma kwa kulipia ktk group la WhatsApp la huyo mtunzi na nilishaweka matangazo sana humu anaetaka ajiunge..
Ratiba maalumu siwezi toa kwa sababu me sio mtunzi pia hata ktk group letu mtunzi mara nyingine hatumi anatuomba radhi kwa kuwa tumelipia...kuhusu vpande vdg mm na copy na kupaste hivyo lipo nje ya uwezo wangu...
Anaeweza kusubiri asubiri asieweza a ache. comments nyingine hazivumiliki watu wanapenda kusemwa vibaya
Big up analyse kwa comments nzuri zenye kujenga

Pamoja mkuu mapengo junior,nadhani kwa maelezo yako ya sasa hivi sidhani kama kuna atakayekuja kulalamika au kutukana tena.
 
SIMULIZI.. BALAA
MWANDISHI.. HALFANI SUDY

SEHEMU YA SABA

Dokta Yusha sasa alikumbuka hali atakayokuwa nayo mke wake kipenzi Nasra kwa tukio lile baya alilolifanya. Alikumbuka pia huzuni atakayokuwa kawaachia wazazi wake wapendwa kule ukumbini baada ya kuondoka bila kuaga. Alijiona kafanya kosa kubwa sana.
Ghafla, majimaji mepesi yalitiririka katika mashavu yake, Dokta Yusha alikuwa analia. Kwa kosa kubwa alilolifanya usiku ule.

Wakati Dokta Yusha akiwaza yale, na chozi la uchungu kumdondoka pale hospitali. Muuaji namba tano alikuwa hatua chache sana na pale alipokaa Dokta Yusha, akifikiria jinsi ya kumuua. Aliona kumuua kwa risasi itazua tafrani kubwa pale hosptali, alipanga kumuuwa Dokta Yusha kwa mikono yake ama kwa kisu. Alihisi njia hizo ni salama zaidi. Sasa alikuwa anasubiri Dokta Yusha afanye kosa lolote lile.

Kule Kilwa Masoko, hali ile ya taharuki na huzuni iliendelea mle ukumbini.
Baada ya saa moja watu wote waliamua kurudi majumbani kwao. Huku kila mmoja akiliongelea kwa aina yake tukio la kukimbia kwa bwana harusi katikati ya sherehe. Wapo waliolifanya kama hadithi nzuri ya kufurahisha, wapo waliolifanya kama hadithi mbaya ya kusikitisha na kuhuzunisha.
Watu wa mwisho kurudi nyumbani katika usiku ule wa sherehe ya harusi ni familia mbili zilizokumbwa na kisanga kile cha kuajabisha, familia ya Dokta Yusha na familia ya Nasra. Waliweka kikao kidogo mlemle ukumbini kulizungumzia tukio lile. Kikao kilichoisha bila maelewano yoyote. Walijaribu kumpigia Dokta Yusha, simu iliita tu bila kupokelewa. Sasa familia zile mbili wakiwa na Bi harusi walikuwa wanarudi nyumbani, katika gari mbili tofauti, wakiwa na huzuni na simanzi tele. Huku wanawake wachache ndani ya familia zile walikuwa wanalia, wakiongozwa vizuri na Bi harusi, Nasra.

Katika gari aliyopanda Nasra, kulikuwa na watu watano, Kulikuwemo na dereva, baba yake Nasra, mzee Mpaukha, mama yake Nasra, mama Mpaukha, na mpambe wa Bi harusi, rafiki yake kipenzi Nasra, Hasina Omary.
Dereva wa gari ile, alikuwa anaitwa Musa. Dereva wa siku nyingi sana wa familia ya mzee Mpaukha.
Musa alikuwa amelewa sana pombe, pombe ambayo aliinywa vilivyo na marafiki zake mle ukumbini. Pombe ilimfanya apoteze umakini pale katika sukani na kuleta balaa kubwa sana.
Walitoka vizuri pale ukumbini, lakini gari lilivyokamata lami mwendo ulibadirika. Musa akawa anaendesha gari bila umakini wowote, siku zote pombe haziongopi.
Hakukuwa na mtu aliyekuwa makini na mwendo ule, wakati Musa alikuwa amelewa pombe, watu wengine wote waliobaki walikuwa wamelewa na kitendo alichokifanya Dokta Yusha kule ukumbini. Gari zima walilewa kwa aina mbili tofauti. Kila mmoja alikuwa amekaa mkao wa kuchoka katika siti yake.
Gari wakati inakata kona ya kuelekea nyumbani kwa mzee Mpaukha, dereva ilimshinda. Ilikuwa kona kali sana, iliyomshinda kabisa Musa, gari liliacha njia na kujisweka kwenye kapori kadogo....ilikuwa balaa !
Gari ilijipiga kwa nguvu sana katika mti mkubwa kule kwenye kapori. Kishindo kikuu kilisikika......

ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA
Maoni/ Ushauri 0757 633010

Hapo nilipokoleza wino ndipo penye shida,inaonekana mpaka leo mungu hajapenda riwaya hii iendelee,na sijui huyu mungu tunaemsingizia mabaya atapenda lini.
 
Mkumbuke mm sio mtunzi wa hii riwaya ila ni member wa JF naisoma kwa kulipia ktk group la WhatsApp la huyo mtunzi na nilishaweka matangazo sana humu anaetaka ajiunge..

Haya sasa.... mnaoipenda sana mkalipie.
 
Pamoja mkuu mapengo junior,nadhani kwa maelezo yako ya sasa hivi sidhani kama kuna atakayekuja kulalamika au kutukana tena.

Hamna hata mmoja aliyemtukana.Malalamiko makali tunayotoa ndiyo ANAYOHISI tunamtukana.
 
Nilishasema huko nyuma...ratiba kila siku naweka moja watu wakapiga kelele sana haiwezeka nkawa naeka mbili watu wakaona haitoshi nikawa naeka tatu pia haitoshi mwisho nikaishiwa vipande vyoote nilivyo navyo...
Mkumbuke mm sio mtunzi wa hii riwaya ila ni member wa JF nikaona si mbaya kushea na wanajamii forum wezangu..
Istoshe mm naisoma kwa kulipia ktk group la WhatsApp la huyo mtunzi na nilishaweka matangazo sana humu anaetaka ajiunge..
Ratiba maalumu siwezi toa kwa sababu me sio mtunzi pia hata ktk group letu mtunzi mara nyingine hatumi anatuomba radhi kwa kuwa tumelipia...kuhusu vpande vdg mm na copy na kupaste hivyo lipo nje ya uwezo wangu...
Anaeweza kusubiri asubiri asieweza a ache. comments nyingine hazivumiliki watu wanapenda kusemwa vibaya
Big up analyse kwa comments nzuri zenye kujenga

Sasa mbona mwanzo ulibisha kama una copy Na Ku paste? Kazi njema mkuu
 
Back
Top Bottom