Riwaya - Balaa

Riwaya - Balaa

SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA MIA NA KUMI NA TATU

Daniel Mwaseba alijinyanyua taratibu pale chini, akiwa bado yuko makini na kile kiti cha moto, kiti cha kifo! Daniel Mwaseba alikuwa anakiangalia kiti cha kifo huku akitabasamu. Kwa mwendo wa taratibu alianza kukisogelea kile kiti cha kifo!
Daniel Mwaseba alikitambua kile kiti cha kifo.
Naam...alikitambua!

Daniel Mwaseba alikuwa anazijua vizuri sana habari za kile kiti cha kifo. Ni yeye ndiye aliyetumwa na waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kukileta kile kiti nchini, toka katika Jamhuri ya watu wa China. Alikumbuka vizuri kuwa alimuuliza Waziri mkuu kuhusu matumizi ya kiti kile hatari, na alikumbuka kuwa jibu la Waziri mkuu lilikuwa fupi tu..

'Ni kwa sababu za kiusalama'

Daniel Mwaseba alienda China kwa shingo upande. Kwa kuwa hakuridhika kabisa na jibu alilopewa na Waziri mkuu wakati huo. Alikuwa anajua vizuri uwezo na maajabu wa kiti kile. Ni kiti hatari kuliko hatari yenyewe. Pamoja na kuwa na muonekano wa kiti kwa sasa lakini kilikuwa na uwezo wa kubadirishwa na kuwa silaha mbalimbali hatari. Kiti kilikuwa na uwezo wa kuwa Bomu kubwa hatari la Maangamizi na kuleta athari kubwa sana sehemu litakaporushwa ama kutegwa. Kiti pia kilikuwa kinaweza kubadirika na kuwa bunduki kubwa za kivita. Uwezo hatari wa kiti kile nd'o sababu iliyomfanya Daniel Mwaseba aende China kukifata kiti kile kwa shingo upande. Sababu kuu ya mashaka ya Daniel ilikuwa.....Wakati huo nchi haikuwa na uhaba wa silaha katika maghala yake...na wala hakukuwa na tishio la usalama kwa nchi. Sasa kwanini nchi inunue gharama ghali na hatari namna ile? Pamoja na mashaka yake lakini Daniel Mwaseba alienda China, hakutaka kupinga kabisa agizo la Waziri mkuu. Alienda China salama na alirudi Tanzania salama. Na ni yeye mwenyewe ndiye aliyemkabidhi kiti kile Waziri mkuu tena nyumbani kwake. Utaratibu uliotumika kuleta kiti kile na kukabidhi uliendelea kuongeza mashaka kichwani mwa mpelelezi Daniel Mwaseba. Ashaenda kufata ama kuongoza msafara wa kwenda kuchukua silaha mara nyingi, na mara zote hukabidhi kwa Mkuu wa majeshi na wanajeshi wengine wenye vyeo vya juu huku wakishuhudiwa na Amiri jeshi mkuu. Kwa ujumla utaratibu uliotumika kuleta kiti kile ulimshangaza sana Daniel.
Lakini mshangao na wasiwasi wa Daniel Mwaseba leo hii ulileta jibu, kiti kile hatari sana alikikuta ndani ya kambi hatari ya Six killers.
Kimefikaje?

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI: BALAA
Mwandishi: HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA MIA NA KUMI NA NNE

Maswali mengi sana yalipita katika kichwa cha mpelelezi Daniel Mwaseba. Lakini maswali yote hakuwa na majibu yake kabisa, pamoja na kutopata majibu ya maswali yake lakini Daniel hakuacha kujiuliza maswali ingawa alijua hakukuwa na wa kumjibu . Lakini alijiuliza.....

"Je kiti hiki kimekuja kwa bahati mbaya au makusudi katika kambi ya watu hawa hatari?" Daniel Mwaseba alijiuliza kimoyomoyo huku akikiangalia kile kiti.

Bahati mbaya kwa maana kundi lile hatari labda walikiiba kiti kile toka mikononi kwa Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Justus Bitesigile, au Waziri mkuu alikuwa na dhamira tangu mwanzoni, dhamira ya kuwaletea kiti kile kundi hatari la Six Killers. Kwa dhamira hii wanayoifanya watu hawa. Daniel Mwaseba akajua umakini mkubwa zaidi unahitajika katika kutatua mkasa huu mzito! Mkasa wenye sura ya usaliti, mkasa wenye sura ya usiri mkubwa sana. Mkasa wenye nia mbaya kwa nchi ya Tanzania.

Hisia kuwa kuna viongozi wakubwa toka serikalini pia wanahusika katika mkasa huu mzito zikatamalaki katika kichwa cha Daniel Mwaseba. Uwepo wa kiti kile mahali pale ulidhihirisha hilo.

"Wakubwa, kwa dhamira ipi sasa? Iweje viongozi wa nchi wauwe wananchi wao?, kosa la wananchi ni lipi? Wananchi ndio waliowachagua hao viongozi, kwa hiyo moja kwa moja viongozi wana dhima ya kuwalinda wananchi, kuwahudumia wananchi, Kuhakikisha wananchi wanapata huduma zote za kijamii" Daniel Mwaseba aliendelea kujiuliza mwenyewe na kujielezea mwenyewe. Tena sasa sio kimoyomoyo tena, alikuwa anaongea kwa sauti ndogondogo...ya kunong'ona.

"Sasa kwa mfano wananchi wote wakiuwawa na kundi hatari la Six Killers, tena kuuwawa kikatili na kwa makusudi watawaongoza kina nani hao viongozi waliopo katika mpango huu?"

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
Unazingua sana mapengo unaweka unavyojickia, unaweka fupi fupi, halaf haujib hata coment za wasomaj, sijui tunajipendekeza

Inaboa sana mtu akishaona anapata suport inakua shida hata insta mtu anaanzisha story then mbele anazingua
 
Inaboa sana mtu akishaona anapata suport inakua shida hata insta mtu anaanzisha story then mbele anazingua

We ngoja hawajui kama nakalibia kupewa ajila Jf, xaxa ww mapengo Ni mwendo wa kukupiga ban hzo ctor utajiandikia mwenyew
 
Potezea n makosa ya kiufund
Mfano; Dr.yusha ikabidi achukue bodaboda baada ya kumuona mwanasheria yupo mbele kapora pikpik na kumfukuzia...! ENZ HZO HAKUNA BODABODA,CJUI HUKO KILWA.
Juu ya yote,hadith ni tamu lete uhondo.

Imebidi nicheke mkuu.Binafsi nilishasahau hata kama story inazungumzia mwaka 89
 
Hapa hadi kesho nishamnote huyu anapost after two days
 
Hapa hadi kesho nishamnote huyu anapost after two days

After two days?!,it's too long to wait.
Mapengo anaturushia stimu,kwa nini asiache tu,kwani tutakufa tusiposoma turiwaya twake tufupitufupi?,mariwaya meeengi google.
Oyaa,ma-admin mko wapi mum-uunguze huyu?
 
After two days?!,it's too long to wait.
Mapengo anaturushia stimu,kwa nini asiache tu,kwani tutakufa tusiposoma turiwaya twake tufupitufupi?,mariwaya meeengi google.
Oyaa,ma-admin mko wapi mum-uunguze huyu?

Sasa c Ni bora angekuwa ameumiza kichwa yy kuitunga, kucopy Na kupaste halaf bado analinga eti, wa design hii wangetiwa ban tu ili apate adabu
 
NAombeni link zenye riwaya nzuri za kiswahili huyu jamaa anatuchosha tu
 
Sasa c Ni bora angekuwa ameumiza kichwa yy kuitunga, kucopy Na kupaste halaf bado analinga eti, wa design hii wangetiwa ban tu ili apate adabu

Si anadai eti ndo inaandikwa ndo mana anapost taratibu,sijui aliianza ya nini kama alijua bado hajamaliza kuiandika,
 
NAombeni link zenye riwaya nzuri za kiswahili huyu jamaa anatuchosha tu

Facebook tafuta RIWAYA RELOADED kama sijakosea.
kuna mariwaya humo.... Ya Tuwa, Beka Mfaume, na wengine watunzi wazuri na vimeo.
 
Facebook tafuta RIWAYA RELOADED kama sijakosea.
kuna mariwaya humo.... Ya Tuwa, Beka Mfaume, na wengine watunzi wazuri na vimeo.

Huku jf hamna ukiacha zike za kimzimu mzimu za mti mkavu
 
Si anadai eti ndo inaandikwa ndo mana anapost taratibu,sijui aliianza ya nini kama alijua bado hajamaliza kuiandika,

Tukutane kesho hapa..." binadam kumridhisha yataka moyo" nilishasema hii riwaya ndio ipo jikoni asante kwa ukumbusho
 
Back
Top Bottom