Riwaya - Balaa

Riwaya - Balaa

SIMULIZI; BALAA
Mwandishi; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA MIA NA ISHIRINI NA MBILI

Kwa upande wa jeshi la Polisi nalo halikulala kabisa, tangu siku ya kwanza kutokea kwa mkasa huu wa ajabu wa kupotea watu kimaajabu bila sababu kujulikana, jeshi la Polisi waliingia kazini. Jeshi la Polisi walianza kufanya msako wao kimyakimya. Lakini kimyakimya yao haikusaidia chochote. Walikuwa wanazunguka palepale bila kujua chanzo cha upotevu wa watu wale, wala kujua ni nani akiyewaficha watu wale. Unaweza sema bora Dokta Yusha na Mwanasheria mlevi walipiga hatua kubwa sana kuwakaribia wahalifu kuliko jeshi la Polisi.
Jeshi la Polisi hawakuwa wanajua lolote kuhusu uwepo wa kundi hatari la Six Killers ndani ya Kilwa.
Mbinu ya kimyakimya ilivyoleta matokeo hasi hatimaye jeshi la Polisi waliamua kufanya msako wa hadharani. Makundi ya askari yalimwaga mitaani kujaribu kutafuta fununu yoyote juu ya kupotea kwa watu au mahali walikopelekwa na kwa lengo gani. Vijana wa Fresh Nigger walipata sana misukosuko ya kukamatwa na kupelekwa kituo cha polisi kwa mahojiano. Lakini hata hivyo hawakupata fununu yoyote ile, pamoja na kutumia hadi njia ya vitisho na mateso kwa wale waliokuwa wanawatilia shaka, kwa bahati mbaya kabisa hawakuwa wamepiga hatua yoyote ile.

*****

Inspekta Jasmine Wahabu, alikuwa askari wa kike. Askari shupavu na jasiri aliyekuwa anategemewa sana na jeshi la polisi nchini Tanzania. Inspekta Jasmine alishafanikiwa mara kadhaa kuwatia wahalifu nguli mbaroni. Kufanikiwa huko kwa Inspekta Jasmine kulifanya azidi kutegemewa na nchi, kutegemewa na jeshi la Polisi. Inspekta Jasmine alitegemewa pia na raia wema.

Baada ya wiki kadhaa za kuwatafuta wahalifu pamoja na watu na wanafunzi waliopotea katika mazingira ya kutatanisha kugonga mwamba. Inspekta Jasmine ndiye aliyepewa jukumu na Mkuu wa jeshi la Polisi nchini Tanzania ili kwenda Kilwa kupeleleza juu ya upotevu wa watu hao.

Inspekta Jasmine sasa alikuwa na siku ya pili ndani ya Kilwa lakini upelelezi wake ulikuwa haujamfikisha kabisa karibu na adui....

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA MIA NA ISHIRINI TATU

Ilikuwa siku ya tatu sasa tangu inspekta Jasmine Wahabu awasili Kilwa ili kwenda kutatua utata juu ya kupotea kimaajabu kwa watu ndani ya Kilwa, tena katika hali isiyoeleweka hadi sasa.

Siku hiyo ya tatu asubuhi na mapema Inspekta Jasmine ilimkuta akiwa amelala kitandani, katika nyumba ya kulala wageni aliyofikia. Ghafla alisikia sauti ya wimbo wa Daz P, simu yake ya mkononi ilikuwa inaita. Inspekta Jasmine alitupa shuka yake nyeupe pembeni na kuifata simu yake ambayo aliyokuwa anaichaji.

'Afande Dismas' inspekta Jasmine alisema kwa sauti ndogo.

Inspekta Jasmine alikuwa amepigiwa simu na askari polisi aitwaye Dismas. Alibonyeza kitufe cha kijani cha kupokelea simu na kuiweka sikioni ili kusikiliza.
Simu kutoka kwa Afande Dismas ilileta kwa inspekta Jasmine taarifa juu ya Dokta aliyekutwa amefungwa kamba katika nyumba ya kulala wageni ya Mikumi.
Ilikuwa asubuhi, Mhudumu alimkuta Dokta Kilumba akiwa kafungwa mle chumbani alipokuwa anaenda kufanya usafi wa kile chumba. Mhudumu aliamua kumtaarifu Bosi wake kisha kupiga simu Polisi.
Baada ya muda mfupi afande Dismas akiwa na askari wengine sita waliwasili pale. Na ndipo waliamua kumtaarifu inspekta Jasmine juu ya tukio lile.
Tokea kule nyumba ya kulala wageni, Inspekta Jasmine alivaa nguo za kiraia haraka, alivaa suruali aina ya jeans na tshirt nyeusi na kuelekea eneo la tukio.
Baada ya uchunguzi wa kiaskari mle chumbani walimchukua Dokta Kilumba na kumpeleka hospitali. Nia ni kuangalia athari aliyoipata Dokta Kilumba, huku askari Polisi wakiongozwa na inspekta Jasmine wakimsubiri kwa hamu apate nafuu kwa ajili ya mahojiano maalum ili awaeleze kitu kilichotokea mpaka ikatokea akafungwa namna ile.
Baada ya kumuacha Dokta Kilumba pale hospitali na kuacha askari kadhaa kwa sababu za ulinzi na usalama. Inspekta Jasmine alitoka hospitali na kuelekea kituo cha Polisi. Mahali ilipokuwepo ofisi yake kwa kipindi chote atakachokuwa Kilwa kwa ajili ya operesheni hii. Alipoweka kitako tu katika kiti chake, simu yake ya mkononi iliita tena. Safari hii jina lililosomeka katika kioo cha simu yake lilikuwa Songelael....

"Hallo" upande uliopiga ile simu ndio ulioanza kuita.
"Nambie Songe" inspekta Jasmine alijibu ile simu huku akiwa makini.
"Sasa nimegundua kila kitu Inspekta kuhusu huu mkasa" Songelael aliongea kwa sauti ndogo simuni. Sauti iliyoonesha hakuwa sehemu ya kawaida.
"Eeeh umegundua nini Songe" inspekta Jasmine aliuliza kwa shauku kubwa ya kutaka kujua hiko kitu alichokigundua Songelael.
" Tusiongee sana Inspekta....njoo katika pori la Ngome sasahivi, ukiwa unakaribia kufika nipigie ili nikupe maelekezo, njoo na askari wengi inspekta " Songelael aliongea kwa kirefu simuni.....

Huyu Songelael ni nani? Na amegundua kitu gani huko porini Ngome?

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
Naona kama utamu umepungua baada ya kuingia policcm kule kilwa...
 
Hongera sana dogo mapengo kwa kutupa huu mkasa....safi sana.
 
Duu mkasa uko vzr kwel itakuwa yule mwnasheria alikuwa mpelelz wa taifa pia
 
Ni kijana mrefu,mweusi,mwenye uso wa kung'aa huyu ni songalel
Je songale amegundua nini..!?
TUMA HELA M-PESA KUPATA MWENDELEZO....
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA MIA ISHIRINI NA NNE

Muda huohuo baada ya ile simu toka kwa Songelael gari tano za Polisi zikiwa na Polisi zaidi ya arobaini zilikuwa njiani kuelekea porini Ngome. Gari za polisi zilitembezwa kwa kasi sana huku zikiwa na Askari waliojipanga kivita, na silaha mzitomzito, walikuwa tayari kwa lolote, walikuwa na uhakika na wanachoenda kukifanya baada ya kuhakikishiwa na askari imara wa kike, inspekta Jasmine, kuwa wanakoenda ndio kwenye jibu la wahalifu wote wanaoisumbua Kilwa. Inspekta Jasmine mwenyewe alikuwa juu ya pikipiki kubwa aina ya Kawasaki, naye akielekea porini Ngome kwenda kuumaliza mchezo.

Kule ndani ya kambi sasa, Mpelelezi Daniel Mwaseba walikuwa wanatazamana macho kwa macho na Moja wa toka kundi la Six killers.
Kukutana ghafla na Mateka wao akiwa huru kulimfanya Moja asite kidogo, alibabaika kwakuwa hakujua Daniel katokaje katika chumba cha kifo, pia alibabaika kwa kuwa hakujua amfate yupi? amfate yule mtu aliyekuwa kule juu ya ukuta wa kambi yao ama aanze kupambana na huyu aliyepo mbele yake, Daniel Mwaseba. Kusitasita kwa Moja ilikuwa faida kubwa sana kwa Daniel Mwaseba. Baada moja alipata wazo la kutoa bastola yake iliyokuwa kotini, aliamua kuanza kummaliza Daniel Mwaseba kwa risasi, lakini alikuwa amechelewa sana........ Daniel aliruka sarakasi kwa kasi toka pale alipokuwa amesimama na kwenda kumvaa Moja kwa nguvu. Bastola ya Moja ilirudi tena ndani ya koti bila kupenda.

Kule juu ya ukuta alikokuwa Dokta Yusha, alikuwa anashuhudia kila kitu. Sasa Dokta Yusha alikuwa anatafuta namna ya kudumbukia ndani kutokea kule juu ya ukuta.

Baada ya kuvamiwa kwa nguvu na Daniel Mwaseba, Moja aliyumba kidogo kisha akasimama imara tayari kwa kupambana na Daniel Mwaseba. Ilhali sasa wote wakiwa mikono mitupu.

Kabla hawajaanza hata kurushiana ngumi, Tatu wa Six Killers alitoka nje ya ile nyumba ya bluu, akiwa na bastola mkononi.
Tayari kwa kuuwa!
Balaa!

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA MIA ISHIRINI NA TANO

Tatu wa Six Killers alivyotoka tu nje aliona mambo mawili kwa mpigo. Kwanza Komando Tatu alimwona Dokta Yusha akiwa anaelea hewani akiingia mle ndani ya kambi yao, Dokta Yusha aliamua kujirusha toka kule ukutani na wakati huohuo aliwaona Moja na Daniel Mwaseba wakiwa wanatazamana kwa chuki wakiwa tayari kwa kupambana. Bila kutegemea Tatu wa Six Killers nae akapatwa na mfadhaiko mkubwa, mfadhaiko kama alioupata Komando Moja wa Six Killers alivyokutana na hali hii.
Daniel Mwaseba nae alimwona Tatu pale mlangoni. Akili yake ilifanya kazi harakaharaka. Kwa muda ule aliona Tatu ni hatari zaidi ya Moja, kwa kuwa Tatu wa Six Killers alikuwa na silaha mkononi. Mpelelezi Daniel Mwaseba alitoka kwa kasi kubwa sana na kufanya kama anamvaa Moja lakini alipitiliza, moja kwa moja alienda kumvaa Tatu pale mlangoni kwa msukumo mkubwa. Msukumo ulioleta faida kubwa sana. Ughafla na nguvu ya msukumo ule uliomwacha Tatu wa Six Killers akiwa kalala chali ardhini bila bastola mkononi. Sasa Daniel Mwaseba ilimpasa kupambana na watu wawili hatari sana. Moja na Tatu wote toka kundi hatari la Six Killers.

Moja wa Six Killers alikuwa amefura kwa hasira. Sasa alikuwa anamfata Daniel Mwaseba kwa ghadhabu, lakini kwa bahati mbaya kabisa hakumfikia Daniel, akiwa katikati katika safari yake ya kumfata Daniel Mwaseba alikutana na MTU! Alikutana na Dokta kijana, Dokta makini, Dokta shujaa, Dokta msomi, Dokta Shupavu, Dokta Mzalendo......Moja alikutana na Dokta Yusha! Tena Dokta Yusha akiwa imara kupambana na jambazi namba moja toka kundi hatari la Six Killers.
Waligawana bila kutarajia, yaani ilitokea tu...sasa ilikuwa kila mtu na wake, Tatu wa Six killers na Daniel Mwaseba, Moja wa Six Killers na Dokta Yusha...

Je Dokta Yusha atamuweza jambazi hatari zaidi katika kundi hili hatari?
Daniel Mwaseba sina wasiwasi nae......

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU! 0757 633010

SEHEMU YA MIA ISHIRINI NA SITA

Kule nje ya kambi ile hatari ya Six killers askari lukuki wa jeshi la Polisi walikuwa wameshakamilisha zoezi la kuizunguka ile kambi pande zote. Lilikuwa zoezi rahisi sana kwa askari Polisi tofauti kabisa na walivyotegemea, urahisi huo ulitokana na umakini wa Six Killers ulikuwa umepungua kutokana na upinzani wa watu wawili mle ndani, upinzani toka kwa Dokta Yusha na Mpelelezi Daniel Mwaseba.
Askari Polisi walikuwa wanaongozwa na yule jamaa aliyempigia simu inspekta Jasmine, aliyejulikana kwa jina la Songelael Ntenga. Jamaa makini aliyewapigia simu askari Polisi na kuwaeleza uwepo wa watu hatari mahala pale.

Kule ndani kabisa ya ile nyumba ya bluu. Walikuwa wamebaki watu wawili tu, komando Nne wa Six Killers na mkuu wa kundi hili hatari, Don Genge. Walikuwa wapo sebuleni wakiangalia runinga, bila kujua wala kuhisi kwamba walikuwa katika hatari kubwa sana. Walikuwa wamezungukwa na askari Polisi kwa nje, walikuwa wamevamiwa na Daniel Mwaseba na Dokta Yusha kwa ndani. Wao walikuwa hawana wasiwasi wowote ule, wakijua kuwa hali ya usalama tayari imedhibitiwa vizuri, na vijana wao wawili, Moja na Tatu wa Six Killers, laiti wangejua.....

Pale nje mapambano yalianza......Tatu wa Six Killers alimfata kwa kasi Daniel Mwaseba huku akitanguliza kichwa chake mbele, lengo lake kuu ni kwenda kumzoa Daniel Mwaseba kwa kutumia kichwa chake kilichokomaa kwa shuruba na mazoezi.....

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
Back
Top Bottom