baharia 1
JF-Expert Member
- Sep 13, 2019
- 2,982
- 4,363
Wakuu naombani majibu
Siri ya Chumba cha Maiti,
Hivi nyie "Team Osha na Kamua" yale maji na uchafu mnaoukamua mnapeleka wapi?
Acheni na roho mbaya, leo nataka tuvunje mwiko wa usiri na tuingie moja kwa moja kwenye lile eneo linaloleta hofu na maswali mengi zaidi kwenye jamii yetu.
Tunajua kuna hawa wataalamu wanaojidai kuosha miili ya marehemu, lakini leo hatuongelei tu juu juu tunaongelea yale maji yanayotumika kuoshea na ule uchafu mnaoukamua matumboni mwa watu wetu,
Inakuwaje kile chumba kinawekwa usiri mkubwa kiasi hicho hata ndugu wa karibu hawaruhusiwi kusogea wala kuchungulia? Huu usiri uliopitiliza ndio unaothibitisha kuwa kuna madudu ya hovyo na unyama unafanyika huko ndani. Na leo lazima niongee mashaka yote mazito na skendo zinazovuma mtaani kuhusu kile kinachoendelea na yale maji.
Kwanza, kile kisingizio chenye ujinga wa hali ya juu cha kuminya na kukua matumbo. Mnamkanyaga marehemu na kumkamua kwa nguvu zote ili kutoa vinyesi na mabaki ya chakula kuelekea puruni. Sasa swali la msingi: Yale maji yaliyochanganyika na sabuni, damu, na ule uchafu wa matumboni.
Mbona kuna skendo nzito mtaani kuwa maji hayo hayatupwi kikawaida?
na mambo ya giza na ushirikina unaotisha. Kuna uvumi mkubwa sana uswahilini na majukwaani kuwa baadhi ya waoshaji wasio na ubinadamu na wenye roho mbaya, huchukua yale maji ya maiti na yale makamasi au uchafu wa tumboni na kuwauzia watu wenye nia ovu.
Inasemekana maji hayo yanauzwa kwa bei mbaya kwenda kutumika kwenye ramli chonganishi, kafara, na kuwadhuru binadamu wengine. Huu ni upumbavu na ukatili wa kiwango cha kikubwa
Tatu, skendo ya kuchanganywa kwenye vyakula vya shughul I,Misosi. Hili ndilo linaogopesha zaidi, kuna maneno yapo wazi kuwa maji hayo ya hovyo hutumiwa na baadhi ya watu wenye biashara au wanaotaka nyota za biashara ziwake, ambapo wanayachukua kwa siri na kwenda kuyachanganya kwenye vyakula vya shughuli au mikahawa ili kuvuta wateja au kuzuia watu wasihoji huduma zao.
Huu ufal na unyama uliopitiliza unatokana na usiri wenu wa hovyo chumbani. Kama mambo yenu ni masafi, mbona hamtaki kuwe na uwazi wa wapi hayo maji yanamwagwa?
Hapa ndipo pointi kuu inapokuja, Kama utaratibu wenu huu wa siri unahusisha fujo za kukamua watu matumbo, ambapo kama mtu alikuwa kwenye koma nzito ndio mnamalizia kabisa uhai wake, halafu bado kuna hizi hofu za yale maji kuchezewa na kwenda kudhuru jamii, kwa nini huu utaratibu usipigwe marufuku?
Acheni ushamb, ukatili na roho mbaya ya kufanya mambo ya giza chini ya kivuli cha mifumo yetu, Kama mtu amefariki, mwili wake uoshwe kisasa hospitalini au kwa uwazi mbele ya ndugu, na maji yamwagike kwenye mifumo rasmi ya majitaka inayofahamika. Huu uhuni na ukatili wa chumba cha siri ukomeshwe mara moja.
Siri ya Chumba cha Maiti,
Hivi nyie "Team Osha na Kamua" yale maji na uchafu mnaoukamua mnapeleka wapi?
Acheni na roho mbaya, leo nataka tuvunje mwiko wa usiri na tuingie moja kwa moja kwenye lile eneo linaloleta hofu na maswali mengi zaidi kwenye jamii yetu.
Tunajua kuna hawa wataalamu wanaojidai kuosha miili ya marehemu, lakini leo hatuongelei tu juu juu tunaongelea yale maji yanayotumika kuoshea na ule uchafu mnaoukamua matumboni mwa watu wetu,
Inakuwaje kile chumba kinawekwa usiri mkubwa kiasi hicho hata ndugu wa karibu hawaruhusiwi kusogea wala kuchungulia? Huu usiri uliopitiliza ndio unaothibitisha kuwa kuna madudu ya hovyo na unyama unafanyika huko ndani. Na leo lazima niongee mashaka yote mazito na skendo zinazovuma mtaani kuhusu kile kinachoendelea na yale maji.
Kwanza, kile kisingizio chenye ujinga wa hali ya juu cha kuminya na kukua matumbo. Mnamkanyaga marehemu na kumkamua kwa nguvu zote ili kutoa vinyesi na mabaki ya chakula kuelekea puruni. Sasa swali la msingi: Yale maji yaliyochanganyika na sabuni, damu, na ule uchafu wa matumboni.
Mbona kuna skendo nzito mtaani kuwa maji hayo hayatupwi kikawaida?
na mambo ya giza na ushirikina unaotisha. Kuna uvumi mkubwa sana uswahilini na majukwaani kuwa baadhi ya waoshaji wasio na ubinadamu na wenye roho mbaya, huchukua yale maji ya maiti na yale makamasi au uchafu wa tumboni na kuwauzia watu wenye nia ovu.
Inasemekana maji hayo yanauzwa kwa bei mbaya kwenda kutumika kwenye ramli chonganishi, kafara, na kuwadhuru binadamu wengine. Huu ni upumbavu na ukatili wa kiwango cha kikubwa
Tatu, skendo ya kuchanganywa kwenye vyakula vya shughul I,Misosi. Hili ndilo linaogopesha zaidi, kuna maneno yapo wazi kuwa maji hayo ya hovyo hutumiwa na baadhi ya watu wenye biashara au wanaotaka nyota za biashara ziwake, ambapo wanayachukua kwa siri na kwenda kuyachanganya kwenye vyakula vya shughuli au mikahawa ili kuvuta wateja au kuzuia watu wasihoji huduma zao.
Huu ufal na unyama uliopitiliza unatokana na usiri wenu wa hovyo chumbani. Kama mambo yenu ni masafi, mbona hamtaki kuwe na uwazi wa wapi hayo maji yanamwagwa?
Hapa ndipo pointi kuu inapokuja, Kama utaratibu wenu huu wa siri unahusisha fujo za kukamua watu matumbo, ambapo kama mtu alikuwa kwenye koma nzito ndio mnamalizia kabisa uhai wake, halafu bado kuna hizi hofu za yale maji kuchezewa na kwenda kudhuru jamii, kwa nini huu utaratibu usipigwe marufuku?
Acheni ushamb, ukatili na roho mbaya ya kufanya mambo ya giza chini ya kivuli cha mifumo yetu, Kama mtu amefariki, mwili wake uoshwe kisasa hospitalini au kwa uwazi mbele ya ndugu, na maji yamwagike kwenye mifumo rasmi ya majitaka inayofahamika. Huu uhuni na ukatili wa chumba cha siri ukomeshwe mara moja.