SIMULIZI; BALAAMWANDISHI! HALFANI SUDYSIMU; 0757 633010SEHEMU YA MIA NA KUMI NA SABAKwa mkupuo mmoja Daniel Mwaseba alifungua macho yake yote mawili. Alivuta pumzi kwa haraka na kunyanyuka taratibu. Daniel alitembea kwa mwendo wa kimyakimya lakini wa haraka akimuwahi mbili pale mlangoni. Alimshika Mbili shingoni na kumrudisha Mbili ndani kwa nguvu. Sasa mkao ulibadirika....Daniel Mwaseba akakaa ule upande ulikokuwa mlango huku Mbili akiwa kwa ndani. Wote wakiwa wamejipanga tayari kwa mapambano. Mbili alikuwa na silaha ya kisu tu ambayo ilikuwa imetulia kiunoni, kisu alichotumia kukata suruali ya Daniel Mwaseba. Daniel alikiona kile kisu pale kiunoni. Lakini hakujari. Sasa Daniel alikuwa anautambua vizuri sana uwezo wa watu wale kimapambano. Sasa aliamua kupiga mapigo ya nguvu! Mapigo hatari wanayofunzwa watu maalum ili kuwapiga watu maalum. Mbili nae alisimama imara....tayari kwa lolote. Daniel nd'o alianza kushambulia, alirusha kareti ya nguvu iliyokuwa inaelekea moja kwa moja katika shingo ya Mbili, lakini mbili aliiona. Kwa kasi ya haraka aliinama kidogo huku akiachia ngumi ya kwa mkono wa kushoto, ngumi iliyokwenda katika tumbo la Daniel. Lakini Daniel nae alijiandaa kwa hilo, aliikwepa ile ngumi kiufundi mkubwa. Sasa mafahari hawa wawili wakawa wanatazama. Kila mmoja kasimama, tayari kwa lolote, tayari kwa chochote, muda wowote. Daniel ndiye alikuwa wa kwanza tena kuamua, alirusha ngumi nane za harakaharaka, nne kwa mkono wa kulia, nne kwa mkono wa kushoto lakini Mbili alizipangua zote, kirahisi sana. Zilikuwa ni ngumi mzito sana, ngumi moja ikitosha kabisa kumpeleka kuzimu mtu dhaifu kama wewe, lakini Mbili hakuwa mtu dhaifu, alikuwa mtu imara kabisa. Cha ajabu Mbili alikisahau kile kisu kiunoni....alikiacha kimetulia tu, labda alidhani atamuweza Daniel kwa mikono mitupu.Mbili nae alirusha ngumi usawa wa mwamba wa pua wa Daniel Mwaseba, lakini Daniel aliiona ngumi ile, aliikwepa huku akiachia ngumi ya nguvu sana kuelekea katika mbavu za Mbili. Mbili aliguna kwa maumivu, alishika mbavu zake kwa mkono wa kulia, lilikuwa kosa! Daniel Mwaseba alipeleka ngumi ya nguvu katikati ya sura ya Mbili. Mbili alipepesuka huku akiwa amechanganyikiwa, ashike mbavu ama sura. Kubabaika kwake kulitoa mwanya mwengine kwa Daniel, aliruka juu huku akipiga teke la kinyumenyume, teke lilomkumba kwa nguvu Mbili na kwenda kumgongesha ukutani vibaya sana! Mbili alikuwa amepatikana.Daniel hakutaka kumpa nafasi, alienda na kifuti pale ukutani na kulipata tumbo la Mbili barabara. Mbili alitapika damu! Daniel alimkaba kabali Mbili, akainyonga ile shingo kwa nguvu kuelekea upande wa kushoto! Roho mbaya ya Mbili ilisalimu amri, roho iliuacha ule mwili dhaifu na kuelekea kusikojulikana.....ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA