Ridhiwani Kikwete: Watakaoshindwa kusimamia fedha za TASAF kuondolewa, Rais Samia atoa Bilioni 51

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Jan 12, 2019
328
414
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema katika mwaka huu wa fedha 2023/24, Rais Samia Suluhu Hassan ameelekeza Jumla ya Bilioni 51 kwa ajili ya kwenda kunufaisha Watanzania waishio katika mazingira magumu kupitia Mpango wa kuokoa Kaya Maskini wa TASAF kote nchini.

Kikwete ameyasema hayo alipotembelea wanufaika wa TASAF katika manispaa ya Singida na kujionea maendeleo makubwa ya miradi ya TASAF wakati akiwa kwenye ziara yake mkoani humo.

"Niwaombe sana Waratibu wote katika manispaa na wilaya zote za Tanzania msiende kufanya vituko katika fedha hizi maana kituko chako kitakufanya urudi kwenu ili tumtafute mtu mwingine wa kuja kuhudumia Watanzania." Alisema Kikwete.

Naibu Waziri Kikwete amesema Rais Samia ameelekeza fedha nyingi zaidi za TASAF ziende kwa wananchi ili kuboresha maisha yao na kwamba wao kama wasaidizi wake watahakikisha maelekezo aliyotoa Rais Samia kwenye matumizi ya fedha kwa kuhakikisha fedha hizi zote zinawafikia walengwa.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Kikwete amesema Serikali itaendelea kuwapa nafasi wanufaika wa TASAF huku akiwahimiza kuendelea kuibua miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

"Serikali ya Rais Samia itaendelea kuwapa nafasi, lakini kubwa nyinyi wananchi katika maeneo yenu ni muhimu kubuni miradi yenu ya maendeleo ya kutengeneza rasilimali ili adhima ya Mpango wa TASAF kuondoa umaskini uendelee kuwa wa mafanikio makubwa." Alisema

Mpango wa TASAF wa kunusuru Kaya Maskini nchini umeendelea kuzaa matunda makubwa ikiwemo kuokoa hali duni ya maisha kwa Kaya nyingi za walengwa, kuanzisha miradi ya maendeleo ya kujikwamua kiuchumi, kujenga nyumba na kuboresha makazi, kusaidia elimu kwa watoto na mengine mengi.
 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema katika mwaka huu wa fedha 2023/24, Rais Samia Suluhu Hassan ameelekeza Jumla ya Bilioni 51 kwa ajili ya kwenda kunufaisha Watanzania waishio katika mazingira magumu kupitia Mpango wa kuokoa Kaya Maskini wa TASAF kote nchini.

Heading: Ridhiwani... why not start with Waziri wa...
Waliambiwa waseme serikali imeelekeza au imetoa lakini wamekazania ...
 
Kwenye bilioni 51, uwezekano ni mkubwa wa bilioni 30 zikatumika kwa lengo husika,bilioni 31 zikanufaisha walioambiwa wale kulingana na urefu wa kamba zao.
 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema katika mwaka huu wa fedha 2023/24, Rais Samia Suluhu Hassan ameelekeza Jumla ya Bilioni 51 kwa ajili ya kwenda kunufaisha Watanzania waishio katika mazingira magumu kupitia Mpango wa kuokoa Kaya Maskini wa TASAF kote nchini.

Kikwete ameyasema hayo alipotembelea wanufaika wa TASAF katika manispaa ya Singida na kujionea maendeleo makubwa ya miradi ya TASAF wakati akiwa kwenye ziara yake mkoani humo.

"Niwaombe sana Waratibu wote katika manispaa na wilaya zote za Tanzania msiende kufanya vituko katika fedha hizi maana kituko chako kitakufanya urudi kwenu ili tumtafute mtu mwingine wa kuja kuhudumia Watanzania." Alisema Kikwete.

Naibu Waziri Kikwete amesema Rais Samia ameelekeza fedha nyingi zaidi za TASAF ziende kwa wananchi ili kuboresha maisha yao na kwamba wao kama wasaidizi wake watahakikisha maelekezo aliyotoa Rais Samia kwenye matumizi ya fedha kwa kuhakikisha fedha hizi zote zinawafikia walengwa.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Kikwete amesema Serikali itaendelea kuwapa nafasi wanufaika wa TASAF huku akiwahimiza kuendelea kuibua miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

"Serikali ya Rais Samia itaendelea kuwapa nafasi, lakini kubwa nyinyi wananchi katika maeneo yenu ni muhimu kubuni miradi yenu ya maendeleo ya kutengeneza rasilimali ili adhima ya Mpango wa TASAF kuondoa umaskini uendelee kuwa wa mafanikio makubwa." Alisema

Mpango wa TASAF wa kunusuru Kaya Maskini nchini umeendelea kuzaa matunda makubwa ikiwemo kuokoa hali duni ya maisha kwa Kaya nyingi za walengwa, kuanzisha miradi ya maendeleo ya kujikwamua kiuchumi, kujenga nyumba na kuboresha makazi, kusaidia elimu kwa watoto na mengine mengi.
Yaan mtu afanye kituko kupiga madili na wizi then anaondolewa arudi nyumban ili mwingine achukue nafasi!! Mamb ya hovyo kbs, ndio maan ufisadi wizi haviwez isha!! Hivi tukisema CCM ndio wana entertain ufisadi na wizi kuna anaepinga humu?
 
Kwenye bilioni 51, uwezekano ni mkubwa wa bilioni 30 zikatumika kwa lengo husika,bilioni 31 zikanufaisha walioambiwa wale kulingana na urefu wa kamba zao.
Hii nchi kwenye kila idara ya serikali kumejaa mchwa.
 
Huu mradi wa TASAF hauna manufaa kwa taifa ungefutwa tuu eti miradi ya kuchimba barabara na majembe ya mkono haya si matusi haya.
 
naon VXR tu japo,tunafukia matuta garama ya matengenezo kodi ya kaya masikini,pesa yao tumenunua. VXR😂 Bongo nyoso
 
Back
Top Bottom