BWANKU M BWANKU
JF-Expert Member
- Jan 12, 2019
- 328
- 414
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze ameanza ziara ya Mkoa wa Mara kwa kutembelea na kuongea na Watumishi wa Manispaa ya Musoma na kisha kufanya ziara kukagua utekelezaji wa mpango wa kuondoa Umaskini yaani TASAF katika jiji hili.
Naibu Waziri ambaye ana ziara ya siku tatu katika Mkoa huo alikuwaelekeza Watumishi wa Umma kujikita katika kuhakikisha wanazingatia na kutafsiri maono ya Rais Samia Suluhu Hassan pale aliwahimiza kuwe na Utumishi wenye kuleta tija, mbora, ulio kimkakati unaolenga kuwatumikia Wateja ambao ni wananchi. Akizungumza na watumishi, Ndg. Naibu Waziri aliwaasa kuwa wabunifu na wenye mikakati ili kufikia malengo.
Pia katika tukio jengine,Naibu waziri Ndg. Kikwete amewaondoa kwenye Uratibu wa mpango wa TASAF waratibu wa Mkoa na Wale wa Wilaya kwa kile alichokiita kushindwa kufikia malengo ya kuwahudumia wananchi wangonge ambao wanahitaji sana huduma hii katika muda. Akionyesha kukaairishwa na kushindwa kwao , Ndg. Kikwete alimuelza RAS wa Mkoa wa Mara ndugu Makungu kutoelewa kwa nini hadi leo wahitaji hao hawajalipwa wakati Fedha kwa ajili ya wanufaika zilishatumwa wakalipwe wanufaika. Naibu Waziri anaendelea na ziara Mkoani hapo kwa kuelekea Wilayani Tarime.
Naibu Waziri ambaye ana ziara ya siku tatu katika Mkoa huo alikuwaelekeza Watumishi wa Umma kujikita katika kuhakikisha wanazingatia na kutafsiri maono ya Rais Samia Suluhu Hassan pale aliwahimiza kuwe na Utumishi wenye kuleta tija, mbora, ulio kimkakati unaolenga kuwatumikia Wateja ambao ni wananchi. Akizungumza na watumishi, Ndg. Naibu Waziri aliwaasa kuwa wabunifu na wenye mikakati ili kufikia malengo.
Pia katika tukio jengine,Naibu waziri Ndg. Kikwete amewaondoa kwenye Uratibu wa mpango wa TASAF waratibu wa Mkoa na Wale wa Wilaya kwa kile alichokiita kushindwa kufikia malengo ya kuwahudumia wananchi wangonge ambao wanahitaji sana huduma hii katika muda. Akionyesha kukaairishwa na kushindwa kwao , Ndg. Kikwete alimuelza RAS wa Mkoa wa Mara ndugu Makungu kutoelewa kwa nini hadi leo wahitaji hao hawajalipwa wakati Fedha kwa ajili ya wanufaika zilishatumwa wakalipwe wanufaika. Naibu Waziri anaendelea na ziara Mkoani hapo kwa kuelekea Wilayani Tarime.