Ridhiwani achafua hali ya hewa Times FM

Ridhiwani achafua hali ya hewa Times FM

Leo hii dogo anamwambia warioba hivo cjui itakuaje huko mbeleni
 
Nilikuwa namsikiliza Riziwani mtoto wa Jk akiongea Times Fm leo hii… dah! Hata kama ni mtoto wa Mkuu wa Kaya ila ana dharau,

Namnukuu "Kuna watu ambao wameshamaliza muda wao wa kuishi,muda wao wa kucheka hapa duniani lakini ndio wa kwanza kushadadia Serikali tatu, namshangaa Warioba anavyopayuka kuwa anataka Serikali tatu, Kila siku anafanya interview kwenye redio tv na magazeti,ameshikilia maoni ya watu kama yake binafsi. Mbona wakati akiwa kijana na akiwa Waziri hakuwahi kudai Serikali tatu ila alikuwa anashikilia serikali mbili? Iweje leo anapayuka kudai serikali tatu?

Ila kwa sentensi hiyo kanikoroga akili! Kumbe naye anataka Serikali mbili,Warioba kutetea hoja za wananchi imekuwa nongwa sana kwa watu wa CCM?

Ridhiwani umeniboa!

Riziwani ameongea Mengi kweli ya Muhimu, wewe umesikia tu hilo alilozungumzia serikali Tatu...!!!!
 
huyu dogo anapata jeuri kwa baba, ngoja raisi ajaye toka upinzani mfano cdm atahama nchi kweupee
 
Haya, sema wewe kasema kweli? Yawezekana Warioba pia anapenda serikali mbili, ila wananchi wanataka serikali tatu. Kuna ubaya gani Warioba akisema maoni ya watu. Na huyu RizMoko ni nani mpaka apewe attention namna hii? haka karedio kumbe nako ka kisengenye, ndo nimejua leo.

Mi nshasema apewe ulinzi mzee warioba
 
Kwenye waraka wa Mwalimu Nyerere "TUJISAHIHISHE" alioutoa Dar es Salaam May 1962 akiwalenga viongozi na wanachama wa TANU mojawapo wa maelekezo yake namnukuu ...." haifai kuchagua kiongozi kwa sababu ni mjomba, au ni binamu au ana sauti au ana sura nzuri.....jambo kubwa ni kuchagua kiongozi mwenye tabia nzuri na anayeiweza kazi..." Nafikiri viongozi wa serikali na chama cha mapinduzi wamelifumbia macho hili ndiyo maana wanateua hata girlfriends zao kwenye nafasi ambazo si kutokuziweza tu bali ni kuwafanya walioteuliwa kubainika ujuha wao! Quote me!

Ni kweli aisee kama chadema vile wanavyofanya, ukabila na udini ndiyo vigezo vyao Muhimu. Nyerere aliona mbali sanaa yule Mzee.
 
Kwenye hadidu rejea hakuna suala la muundo wa muungano
basi tukienda kwa mwendo huu tunaweza kuelewana. Kwa hiyo unataka kusema hadidu za rejea zilitoa contents zote za rasimu au zilielekeza tume ikusanye maoni ya wananchi na kujumuisha walichoambiwa!?
Inawezekana hukufuatilia jinsi pale Zanzibar walivyokataa kuwa hakitajadiliwa chochote kama hiyo sehemu haijajumuisha hadi wajumbe wengine wakafikia hatua ya kuichana ile document hadharani?

 
Tusubiri naye Ridhiwani akizeeka, ataanza kudai serikali tatu. Kumbe serikali tatu ni ya sisi wazee tuliomaliza muda wa kucheka.
Eti Katibu mkuu wa CCM mtarajiwa.........kijana mdogo anakuwa na akili za kizee namna hii, akizeeka si atakuwa na akili za bata bukini huyu?!!!
 

'Mtoto wa raisi ndiye raisi wa watoto' the slogan says.
 
Sasa ulitaka atetee serikali Tatu wakati chama kinataka Serikali mbili?Sasa kama wakati wa Warioba umekwisha yeye anauhakika wakuishi kufikia miaka ya Warioba?Na baba yake ana miaka mingapi leo?Naye tuseme muda wake wa kuishi umefika?

Ni asiye na akili tu anauwezo wa kuongea haya aliyoongea kama kweli ameongea,kwani hakuna mtu aijuaye siku wala saa yake ya kuondoka si kijana,mtoto,mzee na hata mgonjwa.

Pole zake lakini,msamehe pia NAFASI aliyonayo ndiyo inamfanya aseme hayo aliyosema.

Waswahili wana msemo kuwa Mbwa wa Bwana Naye Bwana
 
Mzee zipo topic hapa pia ukisearch utapata list ya ndugu wenye uongozi CDM.
Kwann unanukuu kitu kimazingira ya kujiaminisha kitu kisicho na ukweli?
Marekani imeongozwa na Bush wangapi?
Lakin wale wa viti maalumu ambao mmoja ni mke wa Slaa alokamatwa kule kalenga vipi hujamuona?
Mkya ambae ni hawara wa Mbowe vipi naye hujamuona?
Dada yake Tundu Lissu vipi nayeye?
Sasa njoo uangalie uhusiano uliopo baina ya Muasisi wa chama na Mwenyekiti wa Chadema!
Sasa lipi jipya ambalo CCM wamefanya?

Hakika umeongea cha maana sana, Hawa BAVICHA shida yao wanataka kukifanya chama chao kitakatifu sanaa... wakati wanayofanya ccm na wao ndio hayo hayo kama ulivyoelezea. Siku zote wanasiasa wapo kwa manufaa yao Binafsi na Familia zao.
 
Nilikuwa namsikiliza Riziwani mtoto wa Jk akiongea Times Fm leo hii… dah! Hata kama ni mtoto wa Mkuu wa Kaya ila ana dharau,

Namnukuu "Kuna watu ambao wameshamaliza muda wao wa kuishi,muda wao wa kucheka hapa duniani lakini ndio wa kwanza kushadadia Serikali tatu, namshangaa Warioba anavyopayuka kuwa anataka Serikali tatu, Kila siku anafanya interview kwenye redio tv na magazeti,ameshikilia maoni ya watu kama yake binafsi. Mbona wakati akiwa kijana na akiwa Waziri hakuwahi kudai Serikali tatu ila alikuwa anashikilia serikali mbili? Iweje leo anapayuka kudai serikali tatu?

Ila kwa sentensi hiyo kanikoroga akili! Kumbe naye anataka Serikali mbili,Warioba kutetea hoja za wananchi imekuwa nongwa sana kwa watu wa CCM?

Ridhiwani umeniboa!

Ana uhakika gani kwamba warioba kamaliza mda wa kuishi?( kama ni kweli kasema) anaeza ye ndo akafa akamwacha babu wa watu.
 
Back
Top Bottom