Lyimo
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 3,826
- 2,023
Kule chalinze atawawakilisha hata nyie wazee, na atapata tu Nafasi hiyo maana hao wapinzani hawana cha maana wanachoongea kwenye mikutano yao ya kuomba nafasi ya ubunge, Mfano chadema wanaelezea tu historia ya matukio yao, mala polisi wanatupiga sana, mala oooh... polisi wametuua sana... mala mwenzetu Daudi Mwangosi aliuawa na polisi..." sasa nikasema marehemu Daudi Mwangosi kwani si aliendaga kule kwenye mkutano wa chadema kama Mwandishi wa habari na sio kama kada wa chadema.
Kupata najua atapata tu, sasa kwa jinsi anavyotudharau na kutudhalilisha wazee ni kama hatuhitajiki nchi hii wala hatutakiwi kudai chochote tunachokiona hakiko sawa. Hayo ya CDM hayahusiki kwenye huu uzi na wala Mzee JAji Warioba hakuzeeshwa na CDM, ni muda tu umesogea na kubahatika kula chumvi nyingi.