Ridhiwani achafua hali ya hewa Times FM

Ridhiwani achafua hali ya hewa Times FM

Ulishaambiwa alikuwa hana kichwa akawekewa boga akawa rais je mtoto wa mwenye kichwa cha boga itakuwaje?
 
Siamini kama maneno hayo yametoka kinywani wa mtoto wa rais, kama ni kweli basi kuna kakikundi kadogo kamefanya nchi hii ka familia yao! Inazewekanaje mtoto amabaye ni Warioba ni kama babu yake aseme anpayuka? Nani kampa kiburi cha kuropoka na kutukana waasisi wa nchi hii? Anadhani baba yake ataishi Ikulu milele? Mbona hatujawhi kumuona Dr Hussein Mwinyi akikosa adabu namna hii?

Kapewa kiburi na baba'ake!
Baba Rais na mtoto Rais.
 
Jana nlikua naangali kipindi kimoja it walikua wanawaoji jamaa wa chadema na ccm.sasa huyu wa cc anasema nanukuu..hawachadema haya mambo wanayachulia juu anasema mfano zanzibar wakijitenga watadai eneo lao walilonunua moshi hivyo watu wa baadhi ya maeneo moshi wajiandae kuwa wazanzibar iwapo serikali tatu zitapita..
 
images
chadema inamilikiwa na walevi wa gongo,viroba na bangi
 
Acha umbeya wako;
Kwani kasema uongo?

Angetoa hoja why anataka serikali 2 & nt 3 na sio kutoa maneno ya kejeli mpk nw wana ccm wengi wanaotaka serikaki 2 ukiwauliza kwann mnataka 2 hawana hoja za msingi example wasira alisha wai ulizwa why unatetea serikali 2 akadai tumezoea so hiyo c hoja & advice thnk b4 u do siyo kila kitu we unashabikia maadam kimetoka ccm..
 
Mkuu JERYSON, naweza kuona umejitahidi kuandika vizuri na kutoa source ya bandiko lako lakini inaniwia vigumu kuamini kama mdomo wa mtu aliyesoma vyuo vikuu zaidi ya vitatu tena vya kimataifa unaweza kuyatamka haya tena redioni!!!
Na huyu anagombea Ubunge huku akitarajia kupata hata uwaziri muda wowote, sitarajii kama anaweza tamka hivi!!
 
Acha umbeya wako;
Kwani kasema uongo?
aaah!?kuna watu ambao wamesha maliza muda wao wa kuishi hapa duniani MWENYEZI MUNGU ONA HAWA WALIOLEWA MADARAKA MPK KIASI CHA KUJARIBU KUKUSAHIHISHA KUHUSU UMRI WA WAJA WAKO KUISHI HAPA DUNIANI.
 
R1 kichwani si ni mweupe tu!!! Anadandia train kwa mbele!!! Shule yenyewe alisoma kwa mbinde pale laws akisaidiwa na kada asiyetaka umaarufu ambaye sasa wametemana!!! Fisadi mkubwa huyu.
 
Vichwa nazi,ni kawaida watoto wa maraisi wasiojielewa kubwatuka na kulewa sifa na madaraka ya baba zao. Baba kabakiza mwaka mmoja tuu.
 
Kwa wale ambao wamefika chuo kikuu na kupata angalau shahada moja, hemu tuwe mstari wa mbele kusaidia wale ambao hawakupata elimu.

Ndugu zangu, katika kukusanya maoni ya watu, kuna njia mbalimbali hutumika, na matumizi ya njia hizo ndio zitapelekea uhalali wa data zilizopatikana na hivyo matokeo ya tafiti.

Kwa njia alizotumia Warioba na vibaraka wake, ni wazi kuwa "data" zake hazina uhalali wowote kwa kuwa sio data za kisayansi.

Mtafiti hawezi kukusanya maoni ya kajikundi fulani cha wananchi (ambacho labda kanataka serikali 3) halafu aje ahitimishe kuwa wananchi wanataka serikali tatu. Huo ni wendawazimu.

Yeye kama mwenyekiti wa tume akupaswa ku-generalize, angesema tu kwa mujibu wa data, idadi hii ilitaka hivi, hiyo ilitosha. Ila sio kudanganyana kuwa Watanzania tunataka serikali tatu kwa kutumia maoni ya watu 30,000.

Hata standards za sampling pekee zinatosha kuikataa rasimu ya Warioba.
 
Kwenye waraka wa Mwalimu Nyerere "TUJISAHIHISHE" alioutoa Dar es Salaam May 1962 akiwalenga viongozi na wanachama wa TANU mojawapo wa maelekezo yake namnukuu ...." haifai kuchagua kiongozi kwa sababu ni mjomba, au ni binamu au ana sauti au ana sura nzuri.....jambo kubwa ni kuchagua kiongozi mwenye tabia nzuri na anayeiweza kazi..." Nafikiri viongozi wa serikali na chama cha mapinduzi wamelifumbia macho hili ndiyo maana wanateua hata girlfriends zao kwenye nafasi ambazo si kutokuziweza tu bali ni kuwafanya walioteuliwa kubainika ujuha wao! Quote me!

Mzee zipo topic hapa pia ukisearch utapata list ya ndugu wenye uongozi CDM.
Kwann unanukuu kitu kimazingira ya kujiaminisha kitu kisicho na ukweli?
Marekani imeongozwa na Bush wangapi?
Lakin wale wa viti maalumu ambao mmoja ni mke wa Slaa alokamatwa kule kalenga vipi hujamuona?
Mkya ambae ni hawara wa Mbowe vipi naye hujamuona?
Dada yake Tundu Lissu vipi nayeye?
Sasa njoo uangalie uhusiano uliopo baina ya Muasisi wa chama na Mwenyekiti wa Chadema!
Sasa lipi jipya ambalo CCM wamefanya?
 
Acha umbeya wako;
Kwani kasema uongo?

Yani we Mamndenyi unashabikia kijana anayetarajiwa kuwa Mbunge anavyotukana wazee, tena waliolitumikia Taifa hili. Sasa sisi wazee wengine tulio hohehae atatuambia nini wakati tukimtuma akawakilishe kero zetu, ama Chalinze anatarajia kuwawakiliasha vijana tu?
 
Last edited by a moderator:
Kwa wale ambao wamefika chuo kikuu na kupata angalau shahada moja, hemu tuwe mstari wa mbele kusaidia wale ambao hawakupata elimu.

Ndugu zangu, katika kukusanya maoni ya watu, kuna njia mbalimbali hutumika, na matumizi ya njia hizo ndio zitapelekea uhalali wa data zilizopatikana na hivyo matokeo ya tafiti.

Kwa njia alizotumia Warioba na vibaraka wake, ni wazi kuwa "data" zake hazina uhalali wowote kwa kuwa sio data za kisayansi.

Mtafiti hawezi kukusanya maoni ya kajikundi fulani cha wananchi (ambacho labda kanataka serikali 3) halafu aje ahitimishe kuwa wananchi wanataka serikali tatu. Huo ni wendawazimu.

Yeye kama mwenyekiti wa tume akupaswa ku-generalize, angesema tu kwa mujibu wa data, idadi hii ilitaka hivi, hiyo ilitosha. Ila sio kudanganyana kuwa Watanzania tunataka serikali tatu kwa kutumia maoni ya watu 30,000.

Hata standards za sampling pekee zinatosha kuikataa rasimu ya Warioba.

Wewe unapenda serikali ngapi?
 
Nilikuwa namsikiliza Riziwani mtoto wa Jk akiongea Times Fm leo hii… dah! Hata kama ni mtoto wa Mkuu wa Kaya ila ana dharau,

Namnukuu "Kuna watu ambao wameshamaliza muda wao wa kuishi,muda wao wa kucheka hapa duniani lakini ndio wa kwanza kushadadia Serikali tatu, namshangaa Warioba anavyopayuka kuwa anataka Serikali tatu, Kila siku anafanya interview kwenye redio tv na magazeti,ameshikilia maoni ya watu kama yake binafsi. Mbona wakati akiwa kijana na akiwa Waziri hakuwahi kudai Serikali tatu ila alikuwa anashikilia serikali mbili? Iweje leo anapayuka kudai serikali tatu?

Ila kwa sentensi hiyo kanikoroga akili! Kumbe naye anataka Serikali mbili,Warioba kutetea hoja za wananchi imekuwa nongwa sana kwa watu wa CCM?

Ridhiwani umeniboa!

Halafu akishakuboa? vunza watupu wamekujaa kichwani.
 
Back
Top Bottom