Nikiwa bado naendelea kuomboleza msiba huu na kutafakari kuhusu kuondoka kwa ghafla kwa dada Regia, mengi yamenijia kichwani mwangu, nimejiuliza why Regia alikuja na maneno ya namna ile ya kufungia mwaka? tunao wabunge wangapi JF akiwemo Mnyika na wengineo, tunao viongozi wa vyama wangapi JF, tunao member wangapi ambao wanajulikana nje yaJF lakini hakuna hata mmoja alikuja na kauli zenye mguso kiasi kile.....jibu ni kwamba ni wengi lakin kwanini Regia peke yake? Kiroho napaswa kukubali kwamba huenda roho wa Mungu alishamuonesha kwamba safari yake duniani imekaribia kikomo, hivo atengeneze mambo yake yaliyosalia.......,Kwa kauli zile alizozisema na namna watu wanavomshuhudia mema nina imani ya kumuona dada huyu baada ya masha haya ya dhiki (kama nitatengeneza maisha yangu kabla ya umauti wangu) kwani nashawishika kuamini kwamba hakuondoka na deni bali Mungu alimsafisha na yeye alijisafisha kabla ya safari yake......
Ndugu zangu, tulie na tuomboleze lakin tukumbuke pia kuzililia nafsi zetu kwani kazi imebaki kwetu sasa, je tutaondoka kama Regia ambaye aliisafisha njia yake kabla ya safari yake ya kurudi mavumbini, na je watu watatushuhudia mema kama ambavyo Regia ameshuhudiwa mema na jamii yake yote tokea alipokuwa machame sec hadi leo hii.
Regia, umeniachia somo, umenifundisha namna ya kuishi na watu, umenifundisha nini hasa natakiwa kufanya nikiwa hai!! Nenda dada yangu, kila mmoja kwa zamu yake, hii ni zamu yako ila najua na mimi zamu yangu itafika kwani biblia inasema kila nafsi lazima itaonja mauti!!