Rais wa Msumbiji, Filipe Nyusi awasili Tanzania, aweka jiwe la msingi hospitali ya rufaa ya kanda Burigi, Chato

Rais wa Msumbiji, Filipe Nyusi ameweka jiwe la msingi katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda, Chato. Waziri wa Afya, Dorothy Gwajima amesema hospitali hiyo inatarajiwa kuhudumia takribani wananchi milioni 14 kutoka Kagera, Kigoma, Tabora, Rukwa, Geita na sehemu za Shinyanga & Mwanza.
 
Nyerere alitukosea sana wana mara hasa wana Musoma vijijini. Naona huyu mwamba wa Chato anaonesha watu maana ya kuwa raisi na namna eneo ulilotoka linavyonufaika zaidi. Huu ni ubinafsi lakini.

Ila Nyerere alijitahidi sana kuiachia Mara elimu hasa kwa kipindi kile.Shule nyingi kubwa zilijengwa pale, Mara sec, Musoma tech, Tarime sec, Songe girls bila kusahau za kidini zile kama Makoko, Kowak n.k
 
Rais anakuwa kazini saa24,kwa hiyo hata akiwa likizo anaruhusiwa kupokea wageni tofauti na wewe afisa mfawidhi mkuu-Maji taka,ukienda likizo,ni mpaka urudi
George Bush alikua anafanya mazungumzo ya upatanishi hata kupokea wageni wake shambani kwake Texas Crowford
Sasa habari ya likizo inatoka wapi hapo?

Kwanini wageni wa taifa wanapokelewa kweny makazi binafsi?
 
Nyerere alitukosea sana wana mara hasa wana Musoma vijijini. Naona huyu mwamba wa Chato anaonesha watu maana ya kuwa raisi na namna eneo ulilotoka linavyonufaika zaidi. Huu ni ubinafsi lakini....
Magufuli amefanya ubinafsi upi?

Kuna sehemu/maeneo ambayo unahisi Magufuli hajayatendea haki au unatumia chuki za kisiasa?
 
Rais anakuwa kazini saa24,kwa hiyo hata akiwa likizo anaruhusiwa kupokea wageni tofauti na wewe afisa mfawidhi mkuu-Maji taka,ukienda likizo,ni mpaka urudi
George Bush alikua anafanya mazungumzo ya upatanishi hata kupokea wageni wake shambani kwake Texas Crowford
 
Huu mziki lazima twenda nao sambamba hamna namna, ni kwende tu kuwekeza chato kwa hii miaka 5 iliyobaki
 
Hivi Rais anatembelewaje nyumbni keske ziara ya kikazi?? si angeahirisha mapumziko akampokea mgeni wake Ikulu theni mgeni akiondoka anarudi kwenye mapumziko yake?? huyu jamaa mi huwa simuelewi kabisa hatukuyaona huko nyuma.

Rais wa Musunbiji na Mwenyekiti wa Sadc anahusikaje kuweka jiwe la msingi hospitali ambato haikujengwa kwa msaada wa sadc au Msumbiji??
 
Hivi Rais anatembelewaje nyumbni keske ziara ya kikazi?? si angeahirisha mapumziko akampokea mgeni wake Ikulu theni mgeni akiondoka anarudi kwenye mapumziko yake?? huyu jamaa mi huwa simuelewi kabisa hatukuyaona huko nyuma.

Rais wa Musunbiji na Mwenyekiti wa Sadc anahusikaje kuweka jiwe la msingi hospitali ambato haikujengwa kwa msaada wa sadc au Msumbiji??
 
Back
Top Bottom