Kumbe ndio maana hakuja kwenye lile igizo la kumuapisha akawaachia wasanii wengine kina Museveni.
Jamaa ana uelewa wa juu sana hasa linapokuja suala la mahusiano kati ya wanasiasa, amepevuka sana kidiplomasia, kagonga pale pale hajataka unafiki.
Kwa kauli zake anaonesha jinsi alivyo mwepesi kujirudi na kufanya mazungumzo na mahasimu wake kisiasa, sio hapa kwetu, ni uadui tu miaka yote.
Haya yanayotokea hapa kwetu atakuwa anayaona mambo ya kishamba sana, kutofutiana itikadi ndio unamuona mwenzio adui, mpaka anakimbia nchi aliyozaliwa upo kimya husemi chochote?!