John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Rais Samia Suluhu Hassan ameelezea kupanda kwa bei ya mafuta kwa kiasi inasababishwa na mgogoro unaoendelea kati ya Urusi na Ukraine.
“Mabadiliko ya kupanda kwa bei ya mafuta kiasi kidogo yamesababishwa na vita ya Ukraine na Urusi, yanapanda bei mno. Tanzania hatutanusurika, bidhaa zote zitapanda bei, nauli zitapanda bei kila kitu kitapanda, thamani ya kila kitu itapanda juu.
“Tumesikia minong’ono kuwa maisha yanakuwa magumu, ‘kila kitu kinapanda bei, wanasema ni hao viongozi wetu tulionao hawana baraka’.
"Si baraka ya kiongozi ni hali ya ulimwengu inavyokwenda,” amesema Rais Samia katika maadhimisho ya 'Siku ya Wanawake Duniani', Zanzibar, leo Machi 8, 2022.
“Mabadiliko ya kupanda kwa bei ya mafuta kiasi kidogo yamesababishwa na vita ya Ukraine na Urusi, yanapanda bei mno. Tanzania hatutanusurika, bidhaa zote zitapanda bei, nauli zitapanda bei kila kitu kitapanda, thamani ya kila kitu itapanda juu.
“Tumesikia minong’ono kuwa maisha yanakuwa magumu, ‘kila kitu kinapanda bei, wanasema ni hao viongozi wetu tulionao hawana baraka’.
"Si baraka ya kiongozi ni hali ya ulimwengu inavyokwenda,” amesema Rais Samia katika maadhimisho ya 'Siku ya Wanawake Duniani', Zanzibar, leo Machi 8, 2022.