Rais Samia: Tulifika uchumi wa kati tukarudishwa, tupambane turudi tulikokuwa

Wadau,
Heshima kwenu,
Inasikitisha kuona nchi inarudi nyuma kwa speed of light
2.0 × 10^8

"Tumeondolewa Katika Uchuni wa KATI Lakini Tutarudi" - Rais Samia

Udaku SpecialApril 05, 2022


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema kwamba ingawa Tanzania imeondolewa kwenye nchi zenye uchumi wa kati lakini kufikia mwaka 2025 Tanzania itakuwa imefika au imekaribia kurudi uchumi wa kati.

Mhe. Rais Samia ameyasema hayo leo Aprili 5, 2022 alipokuwa akihutubia katika hafla ya kufungua mkutano wa kitaifa wa haki, amani na maridhiano Tanzania ambao umefanyika Makao Makuu, Dodoma.

"Tanzania tuliingia uchumi wa kati tukarudishwa, siyo kwa mipango ya mtu, ni mipango ya Mungu. Kwahiyo tupambane kurudi tulipokuwa. Na kwa ninavyoiongoza serikali, natarajia kufikia 2025 tutakuwa tumefika au tunakaribia kurudi uchumi wa kati" - Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha katika hotuba yake, Rais Samia amewasisitiza viongozi wa vyama vya kisiasa kuhakikisha kwamba wanautumia mkutano huo vema na kumpelekea mapendekezo yenye tija kwa Tanzania na watu wake.

Rais Samia amewakumbusha wajumbe wa mkutano huo kuwa Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe na hivyo wajadili mambo ambayo yanaendana na mazingira ya Kitanzania na kuongeza kwamba kazi ya vyama vingi ni kuona yanayofanywa na serikali na kutoa maoni kwa serikali.
Rais alishakufa!
Na walisema kuingia uchumi wa kati ni juhudi za Kikwete na sio Magufuli... sasa tuone!
Hakya nani tukirudi tena uchumi wa kati NAJITOA JAMIIFORUM
 
Wadau,
Heshima kwenu,
Inasikitisha kuona nchi inarudi nyuma kwa speed of light
2.0 × 10^8

"Tumeondolewa Katika Uchuni wa KATI Lakini Tutarudi" - Rais Samia

Udaku SpecialApril 05, 2022


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema kwamba ingawa Tanzania imeondolewa kwenye nchi zenye uchumi wa kati lakini kufikia mwaka 2025 Tanzania itakuwa imefika au imekaribia kurudi uchumi wa kati.

Mhe. Rais Samia ameyasema hayo leo Aprili 5, 2022 alipokuwa akihutubia katika hafla ya kufungua mkutano wa kitaifa wa haki, amani na maridhiano Tanzania ambao umefanyika Makao Makuu, Dodoma.

"Tanzania tuliingia uchumi wa kati tukarudishwa, siyo kwa mipango ya mtu, ni mipango ya Mungu. Kwahiyo tupambane kurudi tulipokuwa. Na kwa ninavyoiongoza serikali, natarajia kufikia 2025 tutakuwa tumefika au tunakaribia kurudi uchumi wa kati" - Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha katika hotuba yake, Rais Samia amewasisitiza viongozi wa vyama vya kisiasa kuhakikisha kwamba wanautumia mkutano huo vema na kumpelekea mapendekezo yenye tija kwa Tanzania na watu wake.

Rais Samia amewakumbusha wajumbe wa mkutano huo kuwa Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe na hivyo wajadili mambo ambayo yanaendana na mazingira ya Kitanzania na kuongeza kwamba kazi ya vyama vingi ni kuona yanayofanywa na serikali na kutoa maoni kwa serikali.
Kwenda uchumi wa kati siyo kitu Cha bahati mbaya Bali ni mipango ya mwamba kutoka chato na kwasasa hayupo,kwaiyo aliuleta uchumi kati na sasa amaondoka nao,acha tuone hatima ya hili.
 
Kwanza hata speed of light haijui wala kuilewa unajiandikia na kujiropokea linamba huyo role model wako.

Speed of light ni 3*10^8 [m/s], got it?
 
ukitembelea maeneo ya vijijini halafu ukasikia tanzania kuingia uchumi wa kati utashangaa sana. uchumi wa kati na umaskini huu tulio nao!!!!! unemployment hii?

Tatizo la umasikini wetu wakati mwingine ni la kujitakia tu. Mfano unakuta mtu huko kijijini anamiliki ng’ombe 1000 lakini ukiangalia maisha anayoishi yeye na mifugo yake havina tofauti. Wakati ng’ombe mmoja akimleta mjini na kumuuza anapata sio chini ya laki 3-8 hivii, akiweza uza hata ng’ombe 500 huyu mtu anakuwa na hela nyingi sana na hii mifugo bado itaendelea kuzaliana kila kukicha.
Wengine wana ardhi ya kutoshaa, lakini bado sisi tunajiita masikini. Huu umasikini wetu huu upo vichwani zaidi.
Mwamba alijitahidi sana kutuondolea hizi fikra.
RIP JPM
 
Wewe umeangalia asichokijua tu lakini hujasema unachokijua hapa.. chuki ni upofu

Ninachokijua ni speed of light niliyomsahihisha, kulikuwa hamna haja ya kuandika kitu ambacho hakijui wala kukielewa, angeweza kuacha hiyo namba ya speed of light na wafuasi wake bado mngemuelewa tu, lkn anafanana na anayempigia debe hata hivyo, maneno meengi no substance!
 
Ukitolewa kwenye nchi zenye uchumi wa kati lazma kuna faida unazipata hasa zal misaada yenye nafuu kuliko uchumi wa kati.
Sijajua kama imefanyika makusudi au vipi maana kuingia uchumi wa kati sanasana wanaangalia kadirio la kipato cha mtu mmoja mmoja katika nchi (per capital income)

Sasa imeshuka ghafla!!
 
Mbona kama tunafanywa wajinga na baadhi mnakubali....
Tulikua uchumi wa Kati wa Chini hakuna kundi lingine hilo ndo la mwisho sasa ukisema tumeondolewa hapo ni ili tuwekwe wapi ama Sisi tumeanzishiwa kundi spesho?
Au pengune tumekua nchi fukara....

Anyway alikua makamu wa Rais....CCM NI ILE ILE
 
Hahahaha, haiwezekani kila mwaka tulioe trillioni 20 mariba matupa kwa waliotukopesha halafu tubaki salama. Pumzika kwa amani JPM, si mmesema mnafungua nchi nyie, imekuwaje?
 
Mbona kama tunafanywa wajinga na baadhi mnakubali....
Tulikua uchumi wa Kati wa Chini hakuna kundi lingine hilo ndo la mwisho sasa ukisema tumeondolewa hapo ni ili tuwekwe wapi ama Sisi tumeanzishiwa kundi spesho?
Maana yake tumerudi kwenye nchi masikini kabisa duniani za kutupwa
 
Back
Top Bottom