Rais Samia: Tanzania kuchora ramani yake mpya

Rais Samia: Tanzania kuchora ramani yake mpya

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,437
Reaction score
14,672
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ipo mbioni kuanza mchakato wa kuchora ramani mpya ili kuendana na mabadiliko yaliyojitokeza.

Pia, Soma: Rais Samia aikabidhi Wizara ya Ardhi magari 70

Rais Samia amesema mara ya mwisho ramani ya Tanzania ilichorwa mwaka 1978 huku vitu vingi vikibadilika.

"Hii tukimaliza, itatuwezesha kuchora ramani mpya ya Tanzania, ramani ya mwisho ya Tanzania, ilichorwa mwaka 1978, kwa kiasi kikubwa kuna mabadiliko makubwa hata ukichua tu, Jiji la Dar es Salaam, la mwaka 1978 na leo tofauti, mfumo huu utatuwezesha kutengeneza mipango ya kidijitali," amesema Rais Samia.

 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali iko kwenye mchakato wa kuchora ramani mpya ili kuendana na mabadiliko yaliyopo. Amesema mara ya mwisho ramani ya Tanzania ilichorwa mwaka 1978.

Rais samia ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995 (Toleo la 2023) uliofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC) - Dodoma.
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali iko kwenye mchakato wa kuchora ramani mpya ili kuendana na mabadiliko yaliyopo. Amesema mara ya mwisho ramani ya Tanzania ilichorwa mwaka 1978.

Rais samia ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995 (Toleo la 2023) uliofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC) - Dodoma.
Daaaa vipi kuhusu Ziwa Nyasa Malawi? Mpaka utawekwa wapi ?? Wasisahau Kzmkz kuionyeshaa najua ndio sbb kuuuuu hakuna jipya....
 
Maandalizi ya upigaji.

Hapo utasikia zimetumika bilioni kadhaa, mwisho wa siku itaitwa Ramani ya Mama.

Kina Mwijaku washapata kula hapo, maana watazunguka nchi nzima kunadi ramani mpya ya Tanzania.

Hitimisho itakuwa bonge moja la festival litakalosheheni wasanii wa kutosha, na litaitwa Tamasha la Ramani ya Mama.
 
Hii hatua kubwa sana, tulilala sana. Malawi wamesambaza mitandaoni ramani yao inayoonyesha ziwa nyasa halimilikiwi kabisa na Tz na marais wetu waliopita hawakufanya lolote. kati ya vitu Rais wa nchi unatakiwa kuwa mkali ni kwenye ardhi, unakumbuka mijingo kwa kenya na uganda. ardhi hata ikinyofolewa heka moja unatakiwa kuwa mkali kama mbogo. hata kiwanja chako nyumbani kwako mtu akitaka kuiba mahindi unaweza msamehe ila akiiba mpaka, changamka.
 
Daaaa vipi kuhusu Ziwa Nyasa Malawi? Mpaka utawekwa wapi ?? Wasisahau Kzmkz kuionyeshaa najua ndio sbb kuuuuu hakuna jipya....
mpaka unatakiwa kupita katikati ya ziwa, kwa sababu hata msumbiji mpaka upo katikati, ila ukija kaskazini malawi wanasema tz isiwe katikati. hoja yao kuu ni kwamba, kulishawahi kuwa na mkataba wa kikoloni, na hoja nyingine ni kwamba Tanzania ina maziwa mengi nje ya nyasa.
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali iko kwenye mchakato wa kuchora ramani mpya ili kuendana na mabadiliko yaliyopo. Amesema mara ya mwisho ramani ya Tanzania ilichorwa mwaka 1978.

Rais samia ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995 (Toleo la 2023) uliofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC) - Dodoma.
Itachora yenyewe au itakodi wachoraji kutoka Ulaya
 
BIBI PLEASE,
RAMANI MPYA YA NINI TENA SI TUMEIZOEA HII HII,
kwanza ramani hii nzuri tu tunayo,watu wana maisha mabovu tu badala ya kutafuta njia za kusaidia kuokoa jahazi we unatoa vipaumbele vya hovyo tu.
mara uchinje ngombe,sijui picha na macomedian,mara ramani,mara.......
Jamani hii nchi sijui tunaenda wapi
 
mpaka unatakiwa kupita katikati ya ziwa, kwa sababu hata msumbiji mpaka upo katikati, ila ukija kaskazini malawi wanasema tz isiwe katikati. hoja yao kuu ni kwamba, kulishawahi kuwa na mkataba wa kikoloni, na hoja nyingine ni kwamba Tanzania ina maziwa mengi nje ya nyasa.
Kwaiyo wanataka tuwakaushie kisa tuna maziwa mengi hahahaha wanazingua. Ila Kama vipi watupe pesa tuwauzie ziwa upande wote wa Tanzania alafu pesa ijenge bandari kubwa kavu Morogoro
 
Back
Top Bottom