Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 710
- 1,157
Tanzania tumeanza utamaduni mbaya sana siku hizi. Yeyote anayelisema zuri lolote la serikali anaitwa chawa, kibaraka na maneno mengine mengi ya hovyo hovyo.
Siku hizi ukweli hautokani tena na hali halisi, bali ni chochote kile kinachoonekana kimesemwa na mwenzetu. Jambo hili ni hatari sana, kwani sasa nyeusi tutaita nyeupe maadam tu mwenzetu kasema.
Chukulia kwa mfano uamuzi wa serikali ya awamu ya sita kuondoa "retation fee" kwenye madeni ya mikopo ya elimu ya juu. Ingawa jambo hili limetua mzigo kwa wanufaika wa mikopo hiyo wa kuwa na deni linalokua kila mwaka, lakini bado tunaaminishwa serikali haijali vijana.
Vijana walioingia kwenye soko la ajira katika kipindi cha mwaka 2015-2021, na watuambie katika kipindi hicho waliona matangazo mangapi ya ajira za serikali?
Ni kipindi hicho hicho watumishi hususani wa serikali kuu walikaa bila kupanda cheo wala kimo na wakaufyata. Lakini leo hali ni tofauti.
Sipo hapa kusema selikali ya awamu ya sita ni serikali ya malaika, hapana! Inayomapungu yake, lakini hayo mapungufu yasiwe sababu ya kuiona kuwa haijafanya zuri lolote, kwani kusema hivyo ni kujidanganya wenyewe.
Kama nchi tutanufaika sana kujenga utamaduni wa kupenda mijadala ya maswala na hoja kuliko ushabiki wa kivyama
Siku hizi ukweli hautokani tena na hali halisi, bali ni chochote kile kinachoonekana kimesemwa na mwenzetu. Jambo hili ni hatari sana, kwani sasa nyeusi tutaita nyeupe maadam tu mwenzetu kasema.
Chukulia kwa mfano uamuzi wa serikali ya awamu ya sita kuondoa "retation fee" kwenye madeni ya mikopo ya elimu ya juu. Ingawa jambo hili limetua mzigo kwa wanufaika wa mikopo hiyo wa kuwa na deni linalokua kila mwaka, lakini bado tunaaminishwa serikali haijali vijana.
Vijana walioingia kwenye soko la ajira katika kipindi cha mwaka 2015-2021, na watuambie katika kipindi hicho waliona matangazo mangapi ya ajira za serikali?
Ni kipindi hicho hicho watumishi hususani wa serikali kuu walikaa bila kupanda cheo wala kimo na wakaufyata. Lakini leo hali ni tofauti.
Sipo hapa kusema selikali ya awamu ya sita ni serikali ya malaika, hapana! Inayomapungu yake, lakini hayo mapungufu yasiwe sababu ya kuiona kuwa haijafanya zuri lolote, kwani kusema hivyo ni kujidanganya wenyewe.
Kama nchi tutanufaika sana kujenga utamaduni wa kupenda mijadala ya maswala na hoja kuliko ushabiki wa kivyama