Rais Samia: Madarasa 8000+ ya Sekondari kujengwa kabla ya 2023

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Akiendelea na ziara mkoani Mbeya, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri nchini, pamoja na Wakuu wa Wilaya kuanza kujipanga kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya 8,000 kwa ajili ya shule za Sekondari ambayo yatahitajika ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi watakaoanza kidato cha Kwanza mwaka 2023.

Kwa mujibu wa takwimu jumla ya wanafunzi 1,534,141 wanatarajiwa kumaliza darasa la Saba mwaka huu (2022), ambapo kati yao wanafunzi 1,257,996 wanatarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza. Ongezeko hilo litapelekea hitaji wa vyumba vya madara 7,986 ii kuwezesha Wanafunzi wote kujiunga na kidato cha kwanza.

Bajeti ya Serikali mwaka wa fedha 2022/23 imeonesha kuwa madarasa hayo yatajengwa kwa kupitia ruzuku kutoka Serikali Kuu, mapato ya ndani ya Halmashauri na fedha za washirika wa maendeleo.

Njiani.jpeg
 
Akazilete hizo za wadau wa maendeleo, zije ziliwe, hakyanani, ukiwa uko nje ya system ya awamu ya sita, unakosa mapesa hasa. Ngoja zije, akitoka huko aende hata Urusi akasaini madolari...
 
Akiendelea na ziara mkoani Mbeya, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri nchini, pamoja na Wakuu wa Wilaya kuanza kujipanga kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya 8,000 kwa ajili ya shule za Sekondari ambayo yatahitajika ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi watakaoanza kidato cha Kwanza mwaka 2023.

Kwa mujibu wa takwimu jumla ya wanafunzi 1,534,141 wanatarajiwa kumaliza darasa la Saba mwaka huu (2022), ambapo kati yao wanafunzi 1,257,996 wanatarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza. Ongezeko hilo litapelekea hitaji wa vyumba vya madara 7,986 ii kuwezesha Wanafunzi wote kujiunga na kidato cha kwanza.

Bajeti ya Serikali mwaka wa fedha 2022/23 imeonesha kuwa madarasa hayo yatajengwa kwa kupitia ruzuku kutoka Serikali Kuu, mapato ya ndani ya Halmashauri na fedha za washirika wa maendeleo.View attachment 2316387
Mama yuko kazini hataki masihara katika kazi za kiwaletea maendeleo wananchi wa Tanzania
 
Mungu ampe nguvu na afya. Wananchi tunamkubali sana.
Akiendelea na ziara mkoani Mbeya, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri nchini, pamoja na Wakuu wa Wilaya kuanza kujipanga kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya 8,000 kwa ajili ya shule za Sekondari ambayo yatahitajika ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi watakaoanza kidato cha Kwanza mwaka 2023.

Kwa mujibu wa takwimu jumla ya wanafunzi 1,534,141 wanatarajiwa kumaliza darasa la Saba mwaka huu (2022), ambapo kati yao wanafunzi 1,257,996 wanatarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza. Ongezeko hilo litapelekea hitaji wa vyumba vya madara 7,986 ii kuwezesha Wanafunzi wote kujiunga na kidato cha kwanza.

Bajeti ya Serikali mwaka wa fedha 2022/23 imeonesha kuwa madarasa hayo yatajengwa kwa kupitia ruzuku kutoka Serikali Kuu, mapato ya ndani ya Halmashauri na fedha za washirika wa maendeleo.View attachment 2316387
 
Akiendelea na ziara mkoani Mbeya, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri nchini, pamoja na Wakuu wa Wilaya kuanza kujipanga kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya 8,000 kwa ajili ya shule za Sekondari ambayo yatahitajika ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi watakaoanza kidato cha Kwanza mwaka 2023.

Kwa mujibu wa takwimu jumla ya wanafunzi 1,534,141 wanatarajiwa kumaliza darasa la Saba mwaka huu (2022), ambapo kati yao wanafunzi 1,257,996 wanatarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza. Ongezeko hilo litapelekea hitaji wa vyumba vya madara 7,986 ii kuwezesha Wanafunzi wote kujiunga na kidato cha kwanza.

Bajeti ya Serikali mwaka wa fedha 2022/23 imeonesha kuwa madarasa hayo yatajengwa kwa kupitia ruzuku kutoka Serikali Kuu, mapato ya ndani ya Halmashauri na fedha za washirika wa maendeleo.View attachment 2316387

Sasa ni kawaida sana serikali kupika data na kuwalisha wananchi. Usishangae hiyo idadi inayotajwa ni uongo wa wazi kabisa. Ikitokea shirika la binafsi kukagua hiyo idadi utakuta ni jambo la uongo. Ukitaka kujua hiyo idadi ni ya uongo, waambie watengeneze jedwali la hiyo idadi ya madarasa, mkoa, wilaya, tarafa, kijiji/kata yalipo ili tujiridhishe uone kama watakubali. Hakuna wajinga siku hizi, bali watu tumewapuuza.
 
Samia Suluhu Hassan amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri nchini, pamoja na Wakuu wa Wilaya kuanza kujipanga kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya 8,000 kwa ajili ya shule za Sekondari ambayo yatahitajika ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi watakaoanza kidato cha Kwanza mwaka 2023.
Uwekezaji wa miundombinu uende sambamba na mabadiliko ya mitaala kwenye elimu ili kukabiliana na wimbi la kukosekana kwa ajira nchini, ikumbukwe watu wanapokosa ajira wanakuwa idle, wakiwa idle moja ya mambo wanayoweza kufanya ni kupata burudani, na moja ya burudani ni hiyo inayosababisha kuongezeka kwa population nchini (rejea mimba zilizopatikana wakati wa likizo ndefu ya korona 2020, pia miaka kadhaa nyuma huko Marekani umeme ulikatika kwa muda mrefu zikapatikana mimba za kutosha)
 
Sasa ni kawaida sana serikali kupika data na kuwalisha wananchi. Usishangae hiyo idadi inayotajwa ni uongo wa wazi kabisa. Ikitokea shirika la binafsi kukagua hiyo idadi utakuta ni jambo la uongo. Ukitaka kujua hiyo idadi ni ya uongo, waambie watengeneze jedwali la hiyo idadi ya madarasa, mkoa, wilaya, tarafa, kijiji/kata yalipo ili tujiridhishe uone kama watakubali. Hakuna wajinga siku hizi, bali watu tumewapuuza.
Mwakani ndio "output" ya kwanza ya wanafunzi walioanza masomo bila ada kwa shule za msingi, namba zimetolewa hapo kwa ujumla ambazo ni mchanganuo wa mwaka mzima.. Wakati mwingine tusikaze vichwa na kuandika upupu mbele ya umma, tembelea TAMISEMI kuna data zote, uvivu wako usitulishe sisi matangopori
 
Uwekezaji wa miundombinu uende sambamba na mabadiliko ya mitaala kwenye elimu ili kukabiliana na wimbi la kukosekana kwa ajira nchini, ikumbukwe watu wanapokosa ajira wanakuwa idle, wakiwa idle moja ya mambo wanayoweza kufanya ni kupata burudani, na moja ya burudani ni hiyo inayosababisha kuongezeka kwa population nchini (rejea mimba zilizopatikana wakati wa likizo ndefu ya korona 2020, pia miaka kadhaa nyuma huko Marekani umeme ulikatika kwa muda mrefu zikapatikana mimba za kutosha)
Umeainisha vyema kabisa
 
Mwakani ndio "output" ya kwanza ya wanafunzi walioanza masomo bila ada kwa shule za msingi, namba zimetolewa hapo kwa ujumla ambazo ni mchanganuo wa mwaka mzima.. Wakati mwingine tusikaze vichwa na kuandika upupu mbele ya umma, tembelea TAMISEMI kuna data zote, uvivu wako usitulishe sisi matangopori

Huko TAMISEMI ndio hawawezi kupika data mpaka nitembelee?
 
Back
Top Bottom