Rais Samia kununua kwa milioni 10 kila goli la Taifa Stars kufuzu AFCON

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,035
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa Tsh. Milioni 10 kwa kila goli ambalo Taifa Stars itafunga katika michuano ya kufuzu fainali ya michuano ya AFCON inayoendelea.

Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa imesema Rais Samia ameahidi kuanza kutoa fedha hizo kuanzia mechi ijayo ambapo Taifa Stars itarudiana na Timu ya Taifa ya Uganda (Uganda Cranes) katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Ahadi hiyo inakuja wakati ambapo pia ameahidi kuipatia timu hiyo donge nono la TZS milioni 500, endapo itafanikiwa kufuzu mashindano hayo ambayo yatafanyika Januari 2024 nchini Ivory Coast.

Aidha, Rais Samia amewapongeza Wachezaji, Benchi la Ufundi, TFF na Wadau wote walioshiriki katika maandalizi ya Taifa Stars.

Pia soma: Rais Samia kununua kila goli Tsh. Milioni 5 mechi za Simba, Yanga CAF
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa Tsh. Milioni 10 kwa kila goli ambalo Taifa Stars itafunga katika michuano ya kufuzu fainali ya michuano ya AFCON inayoendelea.

Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa imesema Rais Samia ameahidi kuanza kutoa fedha hizo kuanzia mechi ijayo ambapo Taifa Stars itarudiana na Timu ya Taifa ya Uganda (Uganda Cranes) katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam

Ahadi hiyo inakuja wakati ambapo pia ameahidi kuipatia timu hiyo donge nono la TZS milioni 500, endapo itafanikiwa kufuzu mashindano hayo ambayo yatafanyika Januari 2024 nchini Ivory Coast.

Aidha, Rais Samia amewapongeza Wachezaji, Benchi la Ufundi, TFF na Wadau wote walioshiriki katika maandalizi ya Taifa Stars.
Magufuli alilaumiwa eti alikuwa anagawa fedha huyu naona anatawanya kabisa hizo pesa
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa Tsh. Milioni 10 kwa kila goli ambalo Taifa Stars itafunga katika michuano ya kufuzu fainali ya michuano ya AFCON inayoendelea.

Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa imesema Rais Samia ameahidi kuanza kutoa fedha hizo kuanzia mechi ijayo ambapo Taifa Stars itarudiana na Timu ya Taifa ya Uganda (Uganda Cranes) katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam

Ahadi hiyo inakuja wakati ambapo pia ameahidi kuipatia timu hiyo donge nono la TZS milioni 500, endapo itafanikiwa kufuzu mashindano hayo ambayo yatafanyika Januari 2024 nchini Ivory Coast.

Aidha, Rais Samia amewapongeza Wachezaji, Benchi la Ufundi, TFF na Wadau wote walioshiriki katika maandalizi ya Taifa Stars.
Asante sana mama samia! Amin amin nakuambieni watanzania wenziwangu, kama tukifuzu afcon na kucheza kiufundi pasi za sukari uwanjani, basi tutavutia watu wengi kuipenda taifa stars na mwishoe vijana wetu kupata mashati ya kuvaa vilabu vya ulaya(kuwa wachezaji wa kulipwa)
 
Samia hafai kuwa rais wa hii nchii....anatupoteza wa tanzania...anachukulia jukwaa la mpira kufanya siasa...uwekezaji wa mpira ni long strategic plan siyo kudandia kwa mbele...mnazani izo hela anaweza kutoa kwa miaka 2 mfululizo anatumia vibaya pesa za wananchi wakati kuna mambo mengi ya msingi ya kufanya
 
Samia hafai kuwa rais wa hii nchii....anatupoteza wa tanzania...anachukulia jukwaa la mpira kufanya siasa...uwekezaji wa mpira ni long strategic plan siyo kudandia kwa mbele...mnazani izo hela anaweza kutoa kwa miaka 2 mfululizo anatumia vibaya pesa za wananchi wakati kuna mambo mengi ya msingi ya kufanya
Unajifanya una uchungu sanaa ilhali pesa nyingne nyingi hujui zinaenda wapi?
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa Tsh. Milioni 10 kwa kila goli ambalo Taifa Stars itafunga katika michuano ya kufuzu fainali ya michuano ya AFCON inayoendelea.

Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa imesema Rais Samia ameahidi kuanza kutoa fedha hizo kuanzia mechi ijayo ambapo Taifa Stars itarudiana na Timu ya Taifa ya Uganda (Uganda Cranes) katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Ahadi hiyo inakuja wakati ambapo pia ameahidi kuipatia timu hiyo donge nono la TZS milioni 500, endapo itafanikiwa kufuzu mashindano hayo ambayo yatafanyika Januari 2024 nchini Ivory Coast.

Aidha, Rais Samia amewapongeza Wachezaji, Benchi la Ufundi, TFF na Wadau wote walioshiriki katika maandalizi ya Taifa Stars.
Hongera sana mama Samia, hamasa yako inaonekana
 
Samia hafai kuwa rais wa hii nchii....anatupoteza wa tanzania...anachukulia jukwaa la mpira kufanya siasa...uwekezaji wa mpira ni long strategic plan siyo kudandia kwa mbele...mnazani izo hela anaweza kutoa kwa miaka 2 mfululizo anatumia vibaya pesa za wananchi wakati kuna mambo mengi ya msingi ya kufanya
Unaposema anatumia vibaya fedha za wananchi, wale anaowapa siyo wananchi? Hebu fikiria mfano huu, kisima cha maji kimejengwa huko Simanjiro kwa fedha za kodi zetu kama ilivyo kwenye mpira, MTU ALIYEKO LIULI HUKO NYASA ANAFAIDIKA NINI NA KISIMA HICHO? Ni sawa na hili la kutoa fedha kwenye michezo..!! Hakuna mradi au jambo litafanywa kwa kodi zetu halafu liguse watanzania wote kwa usawa. Hawa wanapata hili na wale wanapata lile. Hata wakati daraja la mkapa linajengwa, mtu aliyeko Karagwe wala halikumuhusu
 
Back
Top Bottom