Raisi wangu Samia naandika post hii nikiamini kwa huwa unapitia jukwaa hili kama siku moja ulivyotwambia. kama siyo wewe kuusoma mwenyewe basi naomba wasaidizi wako wakufikishie ujumbe huu.
Kuna wazee wastaafu waliolitumikia taifa hili kwa uaminifu, na unajua kuwa huko myuma hapakuwepo ujanja ujanja unaofanywa na waajiriwa wa siku hizi.
Mshahara ulikuwa mdogo na bado waajiriwa walikuwa waaminifu. mpaka mtu anastaafu hana nyumba wala shamba, mategemeo ni kuwa atakapo staafu atalipwa pension itakayomtunza mpaka kufa. Lakini wastaafu wa namna hiyo (waliostaafu miaka mingi ya nyuma) sasa hivi wanalipwa sh 100,000 kwa mwezi.
Hii ilipandishwa (kama sikosei) miaka zaidi ya 5 iliyopita. Toka wakati huo bei za vitu zimepanda bei mara dufu. Wanalipwa hela kwa siku ambayo haiwezi hata kununua kilo ya sukari au mchele. Mahitaji ya wazee ni mengi na nguvu ya kufanyakazi hawana. Wataishije hawa?
Hawa wazee hawana mtetezi. Mfanyakazi anapostaafu, vyama vya wafanyakazi ukoma kumtetea. Wastaafu hawana mtetezi bungeni kama walivyo wanawake. Wabuge wanaangalia masilahi yao tu. Mara moja niliwahi kumsikia mbunge mmoja (Mwijage ) akiongea juu ya hili. Wazee hawa wakati mwingine wanazidiwa na wanaopata hela ya TASAFU.
Wazee hawa nina imani siyo wengi kiasi cha kushindwa kulipwa vizuri na mifuko ya Pension. Juzi mfuko mmoja ulikuwa unajinadi kuwa na kiasi cha ma-trilion za hela za Kitanzania. Kwa hesabu za haraka haraka, hata wangekuwa na idadi ya 100,000 tuseme walipwe sh 200,000 kwa mwezi, watalipwa kama 20 billion. Ni kitu kidogo sana ambacho serikali inaweza.
Hebu fikiria wabunge wanalipwa kiasi gani kwa siku pale Dodoma, hebu fikiria hela zinazofujwa na watumishi walioko kazini, hebu fikiria viongozi wastaafu wanaolipwa asilimia 80 za walioko kazini, hebu fikiria wake za viongozi wanavyolipwa, hebu fikiria hata wanavyuo wanaolipiwa na HESLB (10,000) kwa siku., hebu fikiria wafanyakazi wa mifuko ya jamii (NSSF, PSSSF nk) mishahara yao kwa mwezi
Kwanini hawa wazee wateswe hivyo, kwa nini waishi kama vile walikosea kutumia muda wao kulitumikia taifa lisilowakumbuka. Ni mawazo yangu kuwa kitendo cha kuwalipa wazee pension mbovu kinaweza kuwafanya wafanyakazi waliopo kazi kuiba hela za umma ili kujitengenezea maisha yao ya baadae yasije kuwa mabaya huko mbeleni.
Wewe ni mama na mzee pia. Hebu vaa viatu vya mzee mstaafu anayelipwa sh 100,000, piga bajeti ya namna ya kutumia pension. Unahitaji kununua sukari, mchele, mboga n.k, unahitaji kwenda hospital, matumizi ni mengi na hayaelezeki. Wengi wao wanakufa kwa mtimanyongo.
Wanaishi kwa masimango kwamba hawakuwa wajanja wa kutumia mali ya umma, walitumia muda wao vibaya walipokuwa kazini. Kwanini mtumishi mstaafu wa umma awe omba omba?
Mapendekezo yangu mawili:-
-Kima cha pension kipandishwa na kuwa sh 200,000 kwa mwezi.
-Kila unapopandishwa mshahara, angalau nao wape 80% ya kima cha chini, kama ilivyo kwa viongozi wastaafu,
-Vyama vya wafanyakazi (najua wapo humu wanasoma) wasikome kuwatetea waliokuwa wafanyakazi wao, Wajue na wao ipo siku watastaafu. Nani atawatetea?
Nawasilisha
Kuna wazee wastaafu waliolitumikia taifa hili kwa uaminifu, na unajua kuwa huko myuma hapakuwepo ujanja ujanja unaofanywa na waajiriwa wa siku hizi.
Mshahara ulikuwa mdogo na bado waajiriwa walikuwa waaminifu. mpaka mtu anastaafu hana nyumba wala shamba, mategemeo ni kuwa atakapo staafu atalipwa pension itakayomtunza mpaka kufa. Lakini wastaafu wa namna hiyo (waliostaafu miaka mingi ya nyuma) sasa hivi wanalipwa sh 100,000 kwa mwezi.
Hii ilipandishwa (kama sikosei) miaka zaidi ya 5 iliyopita. Toka wakati huo bei za vitu zimepanda bei mara dufu. Wanalipwa hela kwa siku ambayo haiwezi hata kununua kilo ya sukari au mchele. Mahitaji ya wazee ni mengi na nguvu ya kufanyakazi hawana. Wataishije hawa?
Hawa wazee hawana mtetezi. Mfanyakazi anapostaafu, vyama vya wafanyakazi ukoma kumtetea. Wastaafu hawana mtetezi bungeni kama walivyo wanawake. Wabuge wanaangalia masilahi yao tu. Mara moja niliwahi kumsikia mbunge mmoja (Mwijage ) akiongea juu ya hili. Wazee hawa wakati mwingine wanazidiwa na wanaopata hela ya TASAFU.
Wazee hawa nina imani siyo wengi kiasi cha kushindwa kulipwa vizuri na mifuko ya Pension. Juzi mfuko mmoja ulikuwa unajinadi kuwa na kiasi cha ma-trilion za hela za Kitanzania. Kwa hesabu za haraka haraka, hata wangekuwa na idadi ya 100,000 tuseme walipwe sh 200,000 kwa mwezi, watalipwa kama 20 billion. Ni kitu kidogo sana ambacho serikali inaweza.
Hebu fikiria wabunge wanalipwa kiasi gani kwa siku pale Dodoma, hebu fikiria hela zinazofujwa na watumishi walioko kazini, hebu fikiria viongozi wastaafu wanaolipwa asilimia 80 za walioko kazini, hebu fikiria wake za viongozi wanavyolipwa, hebu fikiria hata wanavyuo wanaolipiwa na HESLB (10,000) kwa siku., hebu fikiria wafanyakazi wa mifuko ya jamii (NSSF, PSSSF nk) mishahara yao kwa mwezi
Kwanini hawa wazee wateswe hivyo, kwa nini waishi kama vile walikosea kutumia muda wao kulitumikia taifa lisilowakumbuka. Ni mawazo yangu kuwa kitendo cha kuwalipa wazee pension mbovu kinaweza kuwafanya wafanyakazi waliopo kazi kuiba hela za umma ili kujitengenezea maisha yao ya baadae yasije kuwa mabaya huko mbeleni.
Wewe ni mama na mzee pia. Hebu vaa viatu vya mzee mstaafu anayelipwa sh 100,000, piga bajeti ya namna ya kutumia pension. Unahitaji kununua sukari, mchele, mboga n.k, unahitaji kwenda hospital, matumizi ni mengi na hayaelezeki. Wengi wao wanakufa kwa mtimanyongo.
Wanaishi kwa masimango kwamba hawakuwa wajanja wa kutumia mali ya umma, walitumia muda wao vibaya walipokuwa kazini. Kwanini mtumishi mstaafu wa umma awe omba omba?
Mapendekezo yangu mawili:-
-Kima cha pension kipandishwa na kuwa sh 200,000 kwa mwezi.
-Kila unapopandishwa mshahara, angalau nao wape 80% ya kima cha chini, kama ilivyo kwa viongozi wastaafu,
-Vyama vya wafanyakazi (najua wapo humu wanasoma) wasikome kuwatetea waliokuwa wafanyakazi wao, Wajue na wao ipo siku watastaafu. Nani atawatetea?
Nawasilisha