Rais Samia awapa shavu Wazanzibar: Ajira asilimia 21 za Muungano kuwa za Wazanzibar

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,502
51,098


Watu milioni 58 wanagombania asililia 79 ya Ajira

Ila watu milioni 1.5 unawapa asilimia 21 ya Ajira

Hongera mama, Charity begins at home.

Watanganyika huu ni muda wa kukaa na kutafakari huu muungano una faida na sisi au la?

Hebu tazama

1. Mzanzibar ana haki ya ardhi yote ya Tanzania (Tanganyika na Zanzibar) ila wewe Mtanganyika huko Zanzibar unaweza kupata ardhi kwa masharti ya wageni

2. Mzanzibar anahaki na Ajira zote za mambo hata yasiyo ya muungano kwa mfano TAMISEMI

3. Mzanzibar anaweza kushika nafasi yoyote ya uongozi huku Tanganyika hata kwa mambo yasiyo ya muungano kwa mfano balozi wa nyumba kumikumi lakini Mtanganyika hawezi kuwa kiongozi wa shehia kule Zanzibar

4. Ajira zote za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni exclusive kwa ajili ya Wazanzibar, Yaani Wao wanakula kotekote Tanganyika na kule Zanzibar

5. Wao wamepambana kuondoa mafuta kwenye mambo ya muungano, lakini sisi Ardhi yetu wanaitaka, na wanaienjoy sana tu kwa sababu nawajua Wazanzibar wanaomiliki ardhi TZ

Sasa katika hali kama hii, Huu muungano una faida kwa Watanganyika kweli?
 
Halafu cha ajabu, ikitangazwa kazi inayohusu mambo yasiyo ya muungano, bado wazenji wanaapply na hawawekwi pembeni sababu ya uzanzibar wao, Wanakuwa treated sawa na vijana wa Tanganyika.
Wapo watendaji wa serikali za Mitaa huku bara ni Wazanzibar, japo TAMISEMI siyo jambo la muungano!
 
Kwa hii ratio, wanzanzibari hawatakuwa na tatizo la ajira kamwe. Nadhani viongozi wetu hawajui hesabu. Ili haki itendeke walitakiwa waangalie population ya Wazanzibari against Watanganyika. Hiyo population ndio ingekuwa determinat factor ya kujua asilimia kiasi gani ya ajira iende visiwani na asilimia ngapi ibaki bara. Hii ya kusema tu 21% iende Zanzibar ni baseless, useless and groundless. It is purely thumbsuck.
 
Wazanzibari wanapata faida kubwa sana kwenye muungano. Ila wasijisahau kudhani wanakula sinia moja na wajinga.

Kama kuna ulazima kureserve nafasi za kazi kwa wazanzibari iwe sio zaidi ya asilimia 3 kwa wizara za muungano tu.

Kwenye maeneo mengine wazanzibari wana haki sawa na mtanzania mwingine yeyote.
 
Wazanzibari wanapata faida kubwa sana kwenye muungano. Ila wasijisahau kudhani wanakula sinia moja na wajinga. Kama kuna ulazima kureserve nafasi za kazi kwa wazanzibari iwe sio zaidi ya asilimia 3 kwa wizara za muungano tu. Kwenye maeneo mengine wazanzibari wana haki sawa na mtanzania mwingine yeyote.
Faida gani wanayoipata,idadi yao wapo ml.1.5 lakini shida walizonazo Ni Kama zetu,Shule,maji huduma za Afya ,miundo mbinu n.k,
Hakuma kisiwa masikini duniani isipokuwa Zanzibar.
 
Baniani mbaya kiatu chake dawa,vumilieni tu ,si tumekubaliana Muungano ,sasa sasa ile kauli ya kutesa kwa zamu iheshimiwe.

katika maono watanganyika ndio hawawezi uvumilivu,ila wanashindwa kutamka Muungano uvunjwe,hawawezi wala hawana uthubutu,waPemba kila leo tena walisema zamani Muungano hauna faida,uvunjwe ,leo inakuwaje machogo wanaona wanaonewa,semeni basi muungano uvunjwe .

Muone kama Wapemba watacherewesha hata sekunde ni kuitoa roho ya Muungano ili ufe. Na roho ni CCM.
 
View attachment 2015004

Watu milioni 58 wanagombania asililia 79 ya Ajira

Ila watu milioni 1.5 unawapa asilimia 21 ya Ajira

Hongera mama, Charity begibs at home.

Watanganyika huu ni muda wa kukaa na kutafakari huu muungano una faida na sisi au la?

Hebu tazama

1. Mzanzibar ana haki ya ardhi yote ya Tanzania (Tanganyika na Zanzibar) ila wewe Mtanganyika unaweza kupata ardhi kwa masharti ya wageni

2. Mzanzibar anahaki na Ajira zote za mambo hata yasiyo ya muungano kwa mfano TAMISEMI

3. Mzanzibar anaweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi huku Tanganyika hata kwa mambo yasiyo ya muungano kwa mfano balozi wa nyumba kumikumi lakini Mtanganyika hawezi kuwa shehia kule Zanzibar

4. Ajira zote za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni exclusive kwa ajili ya Wazanzibar, Yaani Wao wanakula kotekote Tanganyika na kule Zanzibar

5. Wao wamepambana kuondoa mafuta kwenye mambo ya muungano, lakini sisi Ardhi yetu wanaitaka, na wanaienjoy sana tu kwa sababu nawajua Wazanzibar wanaomiliki ardhi TZ

Sasa katika hali kama hii, Huu muungano una faida kwa Watanganyika kweli
Kwani huo utaratibu uliandaliwa na Raisi samia, au na maRaisi wakutoka Tanganyika? sasa huyu mama kutekeleza huo utaratibu ana kosa gani? Acheni Raisi afanye kazi, nyie Matanganyika mnajipendekeza kwenye muungano usio kua na manifaa kwenu.
 
Asilimia 21 ni kubwa sana, ilitakiwa wapewe asilimia moja au 0.95 , huu ni wakati wa watanganyika kuamka na kudai serikali ya Tanganyika kama ilivyo serikali ya zanzibar, ratio ilitakiwa igawiwe kutokana na idadi ya watu,
 
Kwani huo utaratibu uliandaliwa na Raisi samia, au na maRaisi wakutoka Tanganyika? sasa huyu mama kutekeleza huo utaratibu ana kosa gani? Acheni Raisi afanye kazi, nyie Matanganyika mnajipendekeza kwenye muungano usio kua na manifaa kwenu.
Hata Mimi nawashangaa Watanganyika wenzangu.

Hii asilimia 21 iliwekwa na awamu ya 4. Awamu ya 5 wakagoma kuitekeleza.

Huyu hangaya wanamuonea bure tu.
 
Back
Top Bottom