benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametoa tahadhari kwa wamiliki wa taasisi zisizo za kiserikali na asasi za kiraia zinazotoa misaada nchini kuhakikisha wanazingatia mila, tamaduni na maadili ya Watanzania.
Samia ameyasema hayo leo Jumapili Juni 25, 2023 katika kilele cha maadhimisho ya kitaifa ya kupinga matumizi na biashara ya dawa za kulevya duniani jijini Arusha alipokuwa akipita katika mabanda tofauti tofauti yanayotoa huduma kwa waraibu wa dawa za kulevya na kushughulikia biashara hiyo haramu.
“Ninataka niwaambie ninyi mashirika kuwa hao wafadhili ambao mnapokea fedha zao kwa ajili ya kuwasaidia vijana wetu kuna vijicondition (baadhi ya masharti) mnawekewa na hao wanaowapatia fedha, naomba niwaambie mbaki katika mstari kuhakikisha mnalinda mila na tamaduni za Watanzania,” amesema Rais Samia.
Samia ameyasema hayo leo Jumapili Juni 25, 2023 katika kilele cha maadhimisho ya kitaifa ya kupinga matumizi na biashara ya dawa za kulevya duniani jijini Arusha alipokuwa akipita katika mabanda tofauti tofauti yanayotoa huduma kwa waraibu wa dawa za kulevya na kushughulikia biashara hiyo haramu.
“Ninataka niwaambie ninyi mashirika kuwa hao wafadhili ambao mnapokea fedha zao kwa ajili ya kuwasaidia vijana wetu kuna vijicondition (baadhi ya masharti) mnawekewa na hao wanaowapatia fedha, naomba niwaambie mbaki katika mstari kuhakikisha mnalinda mila na tamaduni za Watanzania,” amesema Rais Samia.