Rais Samia atoa angalizo kwa NGO's, ataka Masharti ya wafadhili yaendane na Maadili, Utamaduni wa Tanzania

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametoa tahadhari kwa wamiliki wa taasisi zisizo za kiserikali na asasi za kiraia zinazotoa misaada nchini kuhakikisha wanazingatia mila, tamaduni na maadili ya Watanzania.

Samia ameyasema hayo leo Jumapili Juni 25, 2023 katika kilele cha maadhimisho ya kitaifa ya kupinga matumizi na biashara ya dawa za kulevya duniani jijini Arusha alipokuwa akipita katika mabanda tofauti tofauti yanayotoa huduma kwa waraibu wa dawa za kulevya na kushughulikia biashara hiyo haramu.

“Ninataka niwaambie ninyi mashirika kuwa hao wafadhili ambao mnapokea fedha zao kwa ajili ya kuwasaidia vijana wetu kuna vijicondition (baadhi ya masharti) mnawekewa na hao wanaowapatia fedha, naomba niwaambie mbaki katika mstari kuhakikisha mnalinda mila na tamaduni za Watanzania,” amesema Rais Samia.
 
Angeweza kutatua tatizo la bangi arusha ingekuwa vyema sana..wanafunzi kuanzia shule za msingi wanateketea.
 
Alizungumzia kuhusu madaraka kulevya pia?

Kwamba madaraka ni kilevi kibaya zaidi yakikulevya na ukalewa?
 
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametoa tahadhari kwa wamiliki wa taasisi zisizo za kiserikali na asasi za kiraia zinazotoa misaada nchini kuhakikisha wanazingatia mila, tamaduni na maadili ya Watanzania.

Samia ameyasema hayo leo Jumapili Juni 25, 2023 katika kilele cha maadhimisho ya kitaifa ya kupinga matumizi na biashara ya dawa za kulevya duniani jijini Arusha alipokuwa akipita katika mabanda tofauti tofauti yanayotoa huduma kwa waraibu wa dawa za kulevya na kushughulikia biashara hiyo haramu.

“Ninataka niwaambie ninyi mashirika kuwa hao wafadhili ambao mnapokea fedha zao kwa ajili ya kuwasaidia vijana wetu kuna vijicondition (baadhi ya masharti) mnawekewa na hao wanaowapatia fedha, naomba niwaambie mbaki katika mstari kuhakikisha mnalinda mila na tamaduni za Watanzania,” amesema Rais Samia.​
Safi
 
Kwanza Mimi Huwa naona Hawa NGO wawe wanafanya kazi kujazilizia pale Serikali haijafikia maana Kwa ujumla wao Wanatumia zaidi ya Tilioni 1 ila Tija yake Huwa haipo.
 
“Ninataka niwaambie ninyi mashirika kuwa hao wafadhili ambao mnapokea fedha zao kwa ajili ya kuwasaidia vijana wetu kuna vijicondition (baadhi ya masharti) mnawekewa na hao wanaowapatia fedha, naomba niwaambie mbaki katika mstari kuhakikisha mnalinda mila na tamaduni za Watanzania,” amesema Rais Samia.

Nami naomba hayo maagizo yajumuishe pia mkataba wa IGA
 
Yeye kafungua nchi atulie
Tuchangamkie fursa zinazotokana na nchi kufunguliwa kuliko kulalama na kulialia tu.

Tujiongeze kwa kutafuta maarifa mengi ya kisasa kuhusu fani tunazosomea ili tusije kupotezwa kabisa.

Dunia hii haina huruma hata kidogo. Samaki mkubwa anamtafuna yule mdogo upesi sana.
 
  • Thanks
Reactions: apk
Upo sahihi kabisa.
Na tena wamepiga hatua zaidi kuna biscuit na caje za bangi.. wanafunzi wanatumia kama karanga
biscut sijashuhudiaa lakini arusha bangi inavutwa hata sokoni na watu hawashangai ,stendi harufu ya bangi inafuka na polisi wapo,unaweza kukaa sahemu ya wazi unatazama mpira au unapata juice ghafla inafuka harufu ya bangi na watu wamezoea nakuona ni sawa mimi ndio mana kuna matukio yakitokea arusha hata sishangai
 
Back
Top Bottom