Rais Samia anasema 'hili tunalichukua'. Hayati John Magufuli aliamua pale pale jukwaani

Tatizo lako Ame ni la watanzania wengi tu. Kudhani kuwa kumkosoa JPM ni kuwa upande unaomchukia, you are very wrong.

Maamuzi ya haraka siku zote yanazo hasara nyingi tu. Mfano ni pale alipokuwa anawatumbua watu halafu wanaendelea kuwa ni sehemu ya pay roll ya serikali wakipata haki na stahiki zile zile wanazopata wafanyakazi wengine.

Maamuzi mengine ya haraka ni kupeleka pesa ya sherehe za uhuru za mwaka 2016 kujengea barabara ya Morocco halafu baada ya miaka michache inabomolewa na kujengwa upya kwa pesa nyingine!. Kwanini ujenzi usifanyike wote kwa mara moja?.
Kuna kukosoa na kum demonize...Ni vitu viwili tofauti...Umesema kweli tatizo langu ni la watanzania wengi, kwakua watanzania wengi walimkubali JPM kuwa alikuwa na dhamira njema kwa taifa lake, hilo tu linatosha kumwona hafai kufanyiwa hayo mnayotaka kuyafanya
 
Si kweli..ama hujui au ulikuwa haufatilii ziara za Jiwe. Mara nyingi Jiwe alifanya ziara akiwa na timu ya viongozi mbalimbali na hata kama hatokuwepo kwenye msafara kiongozi basi ikiibuka hoja inayohusu sekta fulani basi kiongozi atapigiwa simu huko huko alipo.

Magufuli alipenda kusikiliza kero za watu. Mama toka siku ya kwanza alitangaza hataki mabango.

Magufuli alikuwa na uwezo wa kupewa changamoto akaichambua kwa vifungu vya sheria na kanuni na akapambana kwa hoja na viongozi wake. Na inapobidi anatuma watu wake kama ilivyotokea yule mama kule mbeya aliposema aliyembaka mtoto wake kule tunduru aliachiwa huru, magufuli alituma watu wake na siku iliyofuata alimpa mrejesho kuwa yule mtu yupo ndani.

Sote ni mashahidi. Kuna wakati magufuli aliwatoa nishai walalmikaji kwa kuwaambia wafuate sheria. Na hakutatua matatizo peke yake, ilikuwa lazima ashirikishe mamlaka husika na ikibidi mlalamikaji anakabidhiwa kwa wahusika.

Kutatua matatizo papo kwa papo inahitaji uwe na uwezo wa kufatilia taarifa na kujua sheria na kanuni. Tukubali tu kuwa si kila kiongozi anaweza hilo. Wengi huwa wanaishia kusema nalichukua nitalifanyia kazi. Kisha imeisha hiyo.
 
Bado kitambo kidogo, tutaweza kubadili upepo,maana kuimba kwa midundo ya mpiga ngoma imesha kuwa jadi yetu ingawa muda ni mwalimu mzuri
 
Kuna kukosoa na kum demonize...Ni vitu viwili tofauti...Umesema kweli tatizo langu ni la watanzania wengi, kwakua watanzania wengi walimkubali JPM kuwa alikuwa na dhamira njema kwa taifa lake, hilo tu linatosha kumwona hafai kufanyiwa hayo mnayotaka kuyafanya
Kum demonize umekwenda mbali sana mkuu. Mwanasiasa anadumu miaka na miaka baada ya kifo chake kwa kuyaweka hai yote aliyoyafanya.

Viongozi kama Sokoine na Lumumba wapo hai mioyoni mwa watu kwa sababu yale waliyoyafanya ndio yanayoendelea kuwahukumu. Dhamira njema kwa taifa ni suala moja na udhaifu wake wa maamuzi ni suala jingine tofauti kabisa.
 
Si kweli..ama hujui au ulikuwa haufatilii ziara za Jiwe. Mara nyingi Jiwe alifanya ziara akiwa na timu ya viongozi mbalimbali na hata kama hatokuwepo kwenye msafara kiongozi basi ikiibuka hoja inayohusu sekta fulani basi kiongozi atapigiwa simu huko huko alipo.

Magufuli alipenda kusikiliza kero za watu. Mama toka siku ya kwanza alitangaza hataki mabango.

Magufuli alikuwa na uwezo wa kupewa changamoto akaichambua kwa vifungu vya sheria na kanuni na akapambana kwa hoja na viongozi wake. Na inapobidi anatuma watu wake kama ilivyotokea yule mama kule mbeya aliposema aliyembaka mtoto wake kule tunduru aliachiwa huru, magufuli alituma watu wake na siku iliyofuata alimpa mrejesho kuwa yule mtu yupo ndani.

Sote ni mashahidi. Kuna wakati magufuli aliwatoa nishai walalmikaji kwa kuwaambia wafuate sheria. Na hakutatua matatizo peke yake, ilikuwa lazima ashirikishe mamlaka husika na ikibidi mlalamikaji anakabidhiwa kwa wahusika.

Kutatua matatizo papo kwa papo inahitaji uwe na uwezo wa kufatilia taarifa na kujua sheria na kanuni. Tukubali tu kuwa si kila kiongozi anaweza hilo. Wengi huwa wanaishia kusema nalichukua nitalifanyia kazi. Kisha imeisha hiyo.
Mkuu nilifuatilia sana ziara za Jiwe nchi nzima. Nilichokiandika ninakifahamu na ninao uhakika nacho. JPM alipenda kushiriki kila kitu kinachoendelea nchini, ni mpaka siku zake chache za mwishoni kuelekea kifo chake alikuwa bado anawapigia simu wasaidizi wake akifanya kazi.

Huko kupenda kuwa sehemu ya maamuzi iwe ni nyeti au ya kawaida ndio ilikuwemo tabia ya maamuzi ya haraka yanayokuja kupingwa baadae.
 
Uongozi ni kuamua tu kuchukua njia unayopita, unapita unaenda zako bila ya kujali kelele za kutoridhika au vigelegele vya kuridhika.....,miaka yenyewe mingapi ya uongozi ya kuridhisha wote!!

Maamuzi ya papo kwa papo yana uwezekano mkubwa wa kukosea kunakotokana na kukosa taarifa sahihi na mwisho wa siku mtu anaonewa (nina uhakika katika kila maamuzi natano ya papo kwa papo, mawili yanakuwa sivyo). Faida ya hii ni kuwa watu ni kweli wanakuogopa na hujitahidi kuwa 'sio wao' ili kubaki salama

Style ya mama ya 'kulichukua' ina uwezekano wa kutenda haki lakini ina shida ya kuchelewa na......nchi ni kubwa sana yatachukuliwa mangapi miaka yenyewe mitano au 10 tu!

Suluhisho: nenda tu na unachoamini ni sahihi!
Bora uchelewe lakini utende haki, kuliko kuwahi na utende dhulma.

Suala ni kuongeza washauri na kupanua taasisi. Ni uongo kudhani kuwa Mtu mmoja "Rais" atatatua kero za watu milioni 60 kama ulivyokiri mwenyewe kuwa nchi hii ni kubwa.
 
Kuna hasara nyingi sana za kuhukumu hapo hapo endapo tu jambo hilo halina haja na ulazima wa kuhukumu hapo hapo.

Kuhukumu hapo hapo kuna madhara makubwa kwa sababu mara nyingi mtu anahukumu kwa utashi na kufurahisha kundi fulani na pengine ukamkosesha haki mtu mwingine.

Mama samia alipojibu hoja ya chato kuwa mkoa alijibu kwa hekima sana kwamba vitaangaliwa vigezo kama vitakidhi basi chato utakuwa mkoa.

Hekima iliyoje kwa mama yule,pale alijua fika kwamba akijibu moja kwa moja chato kwamba itakuwa mkoa atawafurahisha sana wana chato msibani na angewafariji zaidi,lakini jibu halikuwa na ulazima wa kutolewa pale pale kwa sababu baadae utakuja kuonekana muongo.

Hekima na kufikiria kwanza kisha ndipo unajibu.
Mama hana huo ujinga
 
Uongozi ni kuamua tu kuchukua njia unayopita, unapita unaenda zako bila ya kujali kelele za kutoridhika au vigelegele vya kuridhika.....,miaka yenyewe mingapi ya uongozi ya kuridhisha wote!!

Maamuzi ya papo kwa papo yana uwezekano mkubwa wa kukosea kunakotokana na kukosa taarifa sahihi na mwisho wa siku mtu anaonewa (nina uhakika katika kila maamuzi natano ya papo kwa papo, mawili yanakuwa sivyo). Faida ya hii ni kuwa watu ni kweli wanakuogopa na hujitahidi kuwa 'sio wao' ili kubaki salama

Style ya mama ya 'kulichukua' ina uwezekano wa kutenda haki lakini ina shida ya kuchelewa na......nchi ni kubwa sana yatachukuliwa mangapi miaka yenyewe mitano au 10 tu!

Suluhisho: nenda tu na unachoamini ni sahihi!
Mama mtu mkweli mpenda haki asiyeyumbishwa
 
Ni mwendo huo huo unaowafaa watanzania kwa sasa baadaye huko wakikaa sawa tunaweza kushift tu automatically...

Sasa kiongozi mpumbavu anayeisababishia nchi hasara kwa upumbavu wake unategemea aachwe bila naye kudhalilishwa kama alivyowakosea na kuwadhalilisha mamilioni ya watanzania....? abembelezwe, afichwefichwe, anyenyekewe nk HAPANA aisee, kuna mijitu mijinga inahitaji adhabu kali sana..
Yaani yule kayafa alikuwa anavuruga bajeti haheshimu mipango anakurupuka Ili tuu afurahishe wajinga,stupid na robo.
 
Hii chuki mliyonayo kwa JPM kwahakika itawa haunt maisha yenu yote...Hivi kwanza hamuoni kuwa ni laana kugombana na maiti? Mtu anaweza dhani mlimloga daah, mbona mnajichora hivi?
Chuki gani yule mtu wenu alikuwa mwehu? Si ajabu tumeambiwa Tzn kuna wagonjwa wengi wa akili mfano ndio huo wa huyo Mwendazake..
 
Mkuu nilifuatilia sana ziara za Jiwe nchi nzima. Nilichokiandika ninakifahamu na ninao uhakika nacho. JPM alipenda kushiriki kila kitu kinachoendelea nchini, ni mpaka siku zake chache za mwishoni kuelekea kifo chake alikuwa bado anawapigia simu wasaidizi wake akifanya kazi.

Huko kupenda kuwa sehemu ya maamuzi iwe ni nyeti au ya kawaida ndio ilikuwemo tabia ya maamuzi ya haraka yanayokuja kupingwa baadae.
Ulitaka nae awe mlalamikaji au asubiri michakato.? Yawezekana ni wewe uliyekuwa haupendezwi na maamuzi ila zile nyomi zilizokuwa zinajaa barabarani zilikuwa zinafurahishwa namna matatizo yanavyomalizwa papo kwa papo ama basi mchakato wa kuyashughulikia uwe wa uhakika badala ya kusubiri michakato.

Kuna vitu havihitaji michakato mzee.
 
Idadi ya samaki hahaha, mkuu umemalizia kwa kichekesho ulichokiandika kwa umakini kama kina ukweli wowote ule.

Alikuwa ana hasira za haraka zinazomnyima busara kama alivyomtukana yule mkurugenzi mbele ya hadhara.

Unapotoa maamuzi ya hapo hapo ni lazima ujiridhishe na taarifa na usahihi wake kwa asilimia angalau tisini na tano. Unasema alikuwa anajiridhisha na taarifa alizokuja nazo kikaoni, vipi kama kuna tukio limetokea baada ya yeye kuwa na taarifa hizo?.
Mwulize Kikwete hapa kuanzia dakika ya 11

 
Si kweli..ama hujui au ulikuwa haufatilii ziara za Jiwe. Mara nyingi Jiwe alifanya ziara akiwa na timu ya viongozi mbalimbali na hata kama hatokuwepo kwenye msafara kiongozi basi ikiibuka hoja inayohusu sekta fulani basi kiongozi atapigiwa simu huko huko alipo.

Magufuli alipenda kusikiliza kero za watu. Mama toka siku ya kwanza alitangaza hataki mabango.

Magufuli alikuwa na uwezo wa kupewa changamoto akaichambua kwa vifungu vya sheria na kanuni na akapambana kwa hoja na viongozi wake. Na inapobidi anatuma watu wake kama ilivyotokea yule mama kule mbeya aliposema aliyembaka mtoto wake kule tunduru aliachiwa huru, magufuli alituma watu wake na siku iliyofuata alimpa mrejesho kuwa yule mtu yupo ndani.

Sote ni mashahidi. Kuna wakati magufuli aliwatoa nishai walalmikaji kwa kuwaambia wafuate sheria. Na hakutatua matatizo peke yake, ilikuwa lazima ashirikishe mamlaka husika na ikibidi mlalamikaji anakabidhiwa kwa wahusika.

Kutatua matatizo papo kwa papo inahitaji uwe na uwezo wa kufatilia taarifa na kujua sheria na kanuni. Tukubali tu kuwa si kila kiongozi anaweza hilo. Wengi huwa wanaishia kusema nalichukua nitalifanyia kazi. Kisha imeisha hiyo.
Ni indicator ya kiongozi kuwa informed na kuwa effective katika maamuzi yake...Wengi ni wavivu, hawasomi, hawatafuti taarifa wanasubiri zije mezani kwao na husingizia ushirikishwaji...Kwnai sote si mashaidi zile ngonjera za njoo kesho rudi Juma fulani si ziliisha? Why? Kwakua alikuwa mfano hai wakutolaza cases za watu bila kuzishughulikia...Wengi wa watanzania wanapenda umangi meza ndiyo sababu wanaona alikuwa hajui afanyalo
 
Ipo tofauti nimeiona ndani ya miezi saba tangu JPM aage dunia na Rais Samia apewe nchi. Tofauti ya uwezo wa kusikiliza na kufanya maamuzi yenye mizania sahihi. JPM hakubarikiwa busara za utatuzi wa matatizo mengi ya kiutekelezaji japokuwa alikuwa na sifa ya utatuzi huo. Hayati JPM alipenda kuamua suala pale pale jukwaani yaani muda ule ule alipokuwa ndio kwanza kalifahamu.

Rais Samia anaukwepa huu mzigo wa lawama ya wananchi. Hana pupa ya maamuzi na hutumia busara ya kusema 'mimi na wasaidizi wangu hili tunalichukua na tunakwenda kulifanyia kazi'. JPM aliamua muda ule ule, matokeo yake baada ya siku kadhaa kupita yale maamuzi yanakuwa yakifahamika kuwapendelea baadhi ya watu na kuwaumiza wengine. Baada ya siku kadhaa kupita inakuja kujulikana kuwa maamuzi yameegemea upande mmoja badala ya kuwa ni ya haki. Hulka hii ilisababisha baadhi ya watendaji serikalini kumuogopa Hayati JPM.

Na wengine hawakumuogopa bali walianzisha tabia ya kuharibu kazi makusudi ili wamuachie ofisi ateue watu wengine anaoona wanafaa kupewa ofisi. Rais Samia anakubali kutumia muda mrefu kupata utatuzi wa matatizo akijiridhisha na maamuzi yatakayofikiwa baada ya kulitazama suala husika kwa pande zote mbili. Unaweza kudhan ni udhaifu kumbe ni sifa ya uongozi, kuepuka kuleta mifarakano miongoni mwa watu wako wa karibu.

Kwani udhaifu wa tabia ya maamuzi ya jukwaani ni kiongozi kuwa wapendwa zaidi wanaoaminiwa na yeye na wapendwa wa kawaida tu. Watu wasioogopa wala kuona aibu ya kuwaharibia wenzao walio wengi kwa sifa ya muda mfupi tu.

Rais Samia ameonyesha utulivu wa kufanya maamuzi. Hajaonyesha pupa wala hasira pale anapochokozwa, mfano alichokifanya Baba Mchungaji Gwajima kingeweza kabisa kuiamsha hasira ya Samia lakini akatulia kama hakuna linalotokea. Aliweza kuonyesha ukomavu wa kiuongozi kwa kuweza kuistahimili misukosuko ya kisiasa kwa utulivu mkubwa.

Hayati JPM alipendwa kwa kusimamia haki za wananchi lakini upande mwingine wa sifa hiyo ulimpatia maadui haswa miongoni mwa wale waliokwazwa. Rais Samia ameweza kueleweka pale anaposema 'hili tunalichukua'. Hataki kufanya maamuzi halafu yakaleta msingi mbaya (precedent) wa siku zijazo.
Nadhani ulikuwa humfahamu Magu vizuri wewe,ile style yake ndio inafaa zaidi na yenye matokeo kwenye taifa linalokuwa kama hili.

Kwanza mpe heshima yake kama kiongozi mwenye ujasiri wa kusimama popote pale hasa vijiji vya njiani kusikiliza kero za wananchi na mkutano kwenda live Tanzania nzima ambapo shida za kijiji hicho inaweza kuwakilisha matatizo ya vijiji kama 10000 Tanzania hii.
Na ambalo hulikuwa hulijui ni kuwa huyu mzee alikuwa anatembea na viongozi wa ngazi zote kuanzia mkoa mpaka kijiji na kabla ajatoa hukumu alikuwa anaitisha viongozi wote ambao walipaswa kuwajibika kwenye hiyo kadhia.

Nenda youtube kapitie kesi moja ya kisima cha maji huko wilaya ya kongwa Dosoma ya mheshimiwa aweso uone jinsi viongozi wenye dhamana walivyo wazembe mpaka ikamlazimu mheshimiwa waziri atoe hukumu pale pale mbele ya wananchi maana inatia hasira ukiangalia jinsi wananchi wanavyokosa huduma ya msingi kwa uzembe wa kipumbavu wa watu wachache waliokabidhiwa dhamana hiyo.

Mwisho najua umeandika hili kuwafurahisha mabwana zako kumendea teuzi ila sijapenda kumlinganisha hayati Magufuli hapa,nikukumbushe kusimama kusikiliza,na kutatua kero za watu ambao sio hata ndugu zako huo ni wito sio kila binadamu au kiongozi anazaliwa nao,usikute hata wewe mtoa mada kukaa na ndugu zako kusikiliza shida zao pasi na kuwasaidia kifedha hata kuwapa ushauri tu mawazo courage hiyo huna sasa tukikupa uongozi utaruhusu watu wapenye ofisini kwako waje walie shida zako.

Kama hukunufaika na uongozi wa Magufuli basi kuna maskini na wanyonge huko ndani ndani walipitiwa na baraka zake mpaka leo ndio hao wanamkumbuka na kumuombea huko aliko kwa sasa sema tu uwezo wa kuingia hapa Jf na kutoa ushuhuda hawana.

Uongozi wa kusikiliza na kutatua shida za wananchi wanyonge ni wito,na huu wito ni inborn character mtu anazaliwa nao.
 
Nadhani ulikuwa humfahamu Magu vizuri wewe,ile style yake ndio inafaa zaidi na yenye matokeo kwenye taifa linalokuwa kama hili.

Kwanza mpe heshima yake kama kiongozi mwenye ujasiri wa kusimama popote pale hasa vijiji vya njiani kusikiliza kero za wananchi na mkutano kwenda live Tanzania nzima ambapo shida za kijiji hicho inaweza kuwakilisha matatizo ya vijiji kama 10000 Tanzania hii.
Na ambalo hulikuwa hulijui ni kuwa huyu mzee alikuwa anatembea na viongozi wa ngazi zote kuanzia mkoa mpaka kijiji na kabla ajatoa hukumu alikuwa anaitisha viongozi wote ambao walipaswa kuwajibika kwenye hiyo kadhia.

Nenda youtube kapitie kesi moja ya kisima cha maji huko wilaya ya kongwa Dosoma ya mheshimiwa aweso uone jinsi viongozi wenye dhamana walivyo wazembe mpaka ikamlazimu mheshimiwa waziri atoe hukumu pale pale mbele ya wananchi maana inatia hasira ukiangalia jinsi wananchi wanavyokosa huduma ya msingi kwa uzembe wa kipumbavu wa watu wachache waliokabidhiwa dhamana hiyo.

Mwisho najua umeandika hili kuwafurahisha mabwana zako kumendea teuzi ila sijapenda kumlinganisha hayati Magufuli hapa,nikukumbushe kusimama kusikiliza,na kutatua kero za watu ambao sio hata ndugu zako huo ni wito sio kila binadamu au kiongozi anazaliwa nao,usikute hata wewe mtoa mada kukaa na ndugu zako kusikiliza shida zao pasi na kuwasaidia kifedha hata kuwapa ushauri tu mawazo courage hiyo huna sasa tukikupa uongozi utaruhusu watu wapenye ofisini kwako waje walie shida zako.

Kama hukunufaika na uongozi wa Magufuli basi kuna maskini na wanyonge huko ndani ndani walipitiwa na baraka zake mpaka leo ndio hao wanamkumbuka na kumuombea huko aliko kwa sasa sema tu uwezo wa kuingia hapa Jf na kutoa ushuhuda hawana.

Uongozi wa kusikiliza na kutatua shida za wananchi wanyonge ni wito,na huu wito ni inborn character mtu anazaliwa nao.
Umeandika kwa mahaba makubwa sana uliyonayo kwa RIP Magufuli na unayo haki ya kuwa na maoni haya.
 
Back
Top Bottom