Blackcornshman
JF-Expert Member
- Aug 25, 2016
- 6,082
- 13,959
Hasa kwanini serikali haikumpiga marufuku kukanyaga Tanzania na kipindi cha uchaguzi alitupasha habari kama kawaida akiwa Tanzania.Kuhusu jina unamfahamu Afande mmoja alikuwa anaitwa Advera Senso,siku hizi ni mkuu wa Wilaya moja kanda ya ziwa na anaitwa Advera Bulimba.Kama ulikuwa unaangalia taarifa zake basi nafikiri jibu unalo na unalijua ila kama ulikuwa huangalii hapo nafikiri itachukua mda mrefu na mambo mengi kukuelezea, ila ningekuomba kunifanyia kitu kimoja kizuri; tafuta Youtube kama kuna critic yeyote ile ambayo Zuhura Yunus na Salim Kikeke wameitoa kwa nchi yao England?
Mbili identity ya huyu mtangazaji ambaye anajulikana kama presenter wa BBC ki-profession, haijulikani. Inakuwaje mda wote huo aiitwe Zuhura Yunus na sasa Zuhura Yunus Abdalah? Hili jina la Abfalah linatumika kivipi na kwa vigezo gani?
Huyu mwanamke, nafikiri watazania wengi mtakuwa mmesahau, alikuwa anatoa taarifa mbovu sana kuhusu sakata la Serikali ya Tanzania na Kampuni ya BARRICK Gold, kiasi kwamba kuna siku alifanya dhahiri kitendo cha kuwapotosha wasilikzaji kwa ku-divert story ya majadiliano yaliyokuwa yakifanyika kati ya serikali ya Tanzania na kampuni ya BARRICK Gold nchini kwa kuhojiana na mtanzania aliyesadikika kama ni mbobebezi katika mambo ya mikataba kama hii huko Canada.
Huyu mtangazaji alikuwa mstari wa mbele sana kwenye kuwapotosha matajiri dunuani walio taka kuwekeza nchini kwa taarifa zake za habari ambazo zilijaa negativity juu ya policy ya nchi yetu, alafu leo tutegemee mtu kama huyu kweli kuibariki nchi yetu ipate mafanikio ya kiuchumi?
Watanzania mnafanya utani na nchi yenu au maisha yenu sio? Mnafikiri huyu mama anauchungu na nyie kweli?