Rais Samia amteua Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu kupangiwa kazi nyingine

Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, amepasiwa mpira na Charles Hillary ambaye alifanyia mpango kwenda BBC.​

Sasa Charles Hillary ni Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu,zanzibar.​

Kwahiyo hii dana dana inachezwa bila watanzania kuunganisha matukio.​

Hillary kapelekwa zenji akitokea bara na Yunus kaletwa bara akitokea zenji. Hii imechezwa kupumbaza wabongo.​

Mkuu naomba kueleweshwa hiv ni sheria au Ni utaratib, mtu mwenye asili ya bara anaweza kufanya kazi Zanzibar?? As Kama mwenye asili ya Zanzibar anaweza kufanya kazi bara?? Yaan inaweza kutokea mmakonde akagombea uRais Zanzibar?? Au kuwa waziri/ au kuajiliwa kwenye idara za mhim serikalini??
 
Kweli Ila watu walikua kimyaa tujifunze kukubali mabadiliko kila MTU na watu wake...Magu baraza la mawaziri alijaza Kanda ya Ziwa tupu!!wasukuma ndo waljaa kila sehemu ajira zilikua zinatolewa kimya kimya na watu walikua kimya...
Umesika. Shukrani.
 
Itoshe kusema tu nampenda sana..Sina zaidi...kama ameweza kufanya kazi BBC kwa miaka 14 bila makandokando,. Baasi ni vetting tosha kupitia kwa wazungu wale..hata kama alikuwa akicheza ngoja yao..mtu ambaye amepinda angecheza na mwishowe angeteleza..somehow...
Factor ya kuthibitisha uadilifu na weledi huko BBC mtizamo wangu ni kwamba Mazingira aliyofanyia kazi yamelazimu kuwa hivyo. Pia ninaamini hata kwa hiyo nafasi aliyopewa hapo Jengo Jeupe atafanya vizuri kutokana na mazingira kumlazimu kuwa SMART. Ni kazi isiyo Pasua kichwa, ni kazi isiyo na furusa za ubadhilifu,upendeleo, uonezi, wizi au Michongo. Ni kazi ya Kuwasiliana na Uma/Hadhira tena kwa kibali.

Vinginevyo Uadilifu wake Utapimwa vizuri akiteuliwa ktk nafasi ambayo atakuwa na Maamuzi kwa anaowaongoza/ hudumia na Mafungu.

SO FAR NAMKUBALI KAMA UNAVYOMKUBALI. Haiba yake nzuri sana
 
Mwaka wa Waislamu huu, Ndugu yangu Jaffar Haniu kakosea wapi? Sitaki kuamini kakubali kirahisi hivyo kuacha yale mapochopocho mix kuku sambusa wa ikulu.

Mwezake Msigwa tangu afutwe kazi ikulu siku hizi kapauka kweli, Ikulu ikulu tu.
Mwaka wa waislam halafu hapo hapo umemtaja Jaffari Haniu kama vile ni mkristu!.
 
Kinachonipa taabu ni kitu kimoja hivi serikalini umri wa mwisho kuajiriwa ni miaka mingapi? Naona watu wana miaka 50, wengine 55 bado wanaajiriwa serikalini hapo hapo kuna vijana under 25 wapo wengi mitaani tena wahitimu wa Masters degree fani fani mbali mbali
 
67 Reactions
Reply
Back
Top Bottom