Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Meli Mpya ya hapa kazi tu katika Bandari ya mkoani wa Mwanza leo tarehe 14 Juni, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiteremka kutoka ndani ya Meli Mpya ya Abiria na Mizigo ya MV Mwanza inayoendelea kujengwa katika bandari ya Mwanza South Mkoani Mwanza mara baada ya kagua maendeleo ya Ujenzi wa Meli hiyo tarehe 14 Juni, 2023.
Meli Mpya ya Abiria na Mizigo ya MV Mwanza inayoendelea kujengwa katika bandari ya Mwanza South Mkoani Mwanza.
Jengo la Hoteli itakayokuwa na hadhi ya Nyota tano ambayo inaendelea kujengwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF Mkoani Mwanza.
Rais Samia Hassan amefanya ziara kwenye jiji la Mwanza na kufanya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya kimkakati lakini alipoingia kukagua meli ya MV Mwanza hapa kazi tu alionyesha kuikubali na kushangazwa na ukubwa na uzuri wake.
Meli ya mpya ya MV Mwanza itakapokamilika itakuwa na uwezo wa kubeba zaidi ya abiria elfu moja na tani 400 za mizigo.
Ikumbukwe tangu kuzama kwa MV Victoria mwaka 1996 jiji la Mwanza lilibaki ukiwa bila mradi wowote wa maana mpaka alipoingia Hayati Magufuli na akanzisha miradi ya matrillioni ya pesa ndani ya jiji la Mwanza.
Rais Samia Hassan amefanya ziara kwenye jiji la Mwanza na kufanya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya kimkakati lakini alipoingia kukagua meli ya MV Mwanza hapa kazi tu alionyesha kuikubali na kushangazwa na ukubwa na uzuri wake...