Rais Museveni amteua mwanae Muhoozi Kainerugaba kuwa CDF

Precious Diamond

JF-Expert Member
Jun 9, 2023
397
993
Screenshot_20240322_010432_Instagram.jpg

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amemteua Mtoto wake Jenerali Muhoozi Kainerugaba kuwa Mkuu mpya wa Majeshi (CDF) Nchini Uganda akichukua nafasi ya Jenerali Wilson Mbasu Mbadi ambaye ameteuliwa kuwa Waziri anayehusika na masuala ya biashara kwenye mabadiliko mapya aliyofanya katika Baraza la Mawaziri la Nchi hiyo usiku huu.

Muhoozi aliwahi kuwa kwenye nafasi ya Ukamanda wa Jeshi la Ardhini la Uganda lakini October 04,2022 Museveni aliamua kumuondoa na nafasi yake ikachukuliwa na Meja Jenerali Kayanja Muhanga ambaye alikuwa Kamanda wa Opereshemi Shujaa inayoendeshwa Nchini DRC.

Millard Ayo

Pia soma:

Jenerali Muhoozi Kainerugaba ni dhahiri sasa amelewa madaraka. Ni kweli kwamba hajui madhara ya kauli aliyotoa kuhusu kuivamia Kenya?

Mtoto wa Museveni atangaza kugombea Urais 2026
 
Yajayo yanafurahisha nchini Uganda.

Uteuzi wa Kainerubaga Muhoozi umetagazwa leo usiku wa manane. Aliyekuwa mkuu wa majeshi ameteuliwa kuwa waziri wa nchi.

Kuna tetesi nchini Uganda kuwa Rais anamuandaa mwanaye kuwa Rais.

Kabla ya hapo General Muhoozi alikuwa mkuu wa kikosi maalum cha ulinzi wa Rais na Special security force for installations.

Source: BBC Swahili.
 
Back
Top Bottom