Rais Magufuli, sasa serikali ihamie Dodoma

Rais Magufuli, sasa serikali ihamie Dodoma

Dodoma imekaa vizuri sana kila idara.
Hongera Mh. Rais JPM hakika ndoto za Baba wa Taifa umeanza kuzitengenezea njia iliyonyooka.
beach pia ipo Dodoma je raisi akijisikia kuvua dagaa yaani mpk aje dar? muwe mnafikiria bhana
 
Karibuni Dodoma.

Kuna sehemu moja pamejengwa apartments za kuvutia yaitwa Medeli, naona kufikia 2017 patakuwa pamejaa.


Medeli Apartments.
 
safi sana. lazima tuwe tunajiwekea commitment na kuwa results oriented.

stock-vector-tanzania-political-map-political-map-of-tanzania-with-the-capital-dodoma-national-borders-most-151269227.jpg

Aise we Red Giant! Hii ramani ni 'feki' au umekosea kuchora mpaka wa nchi maeneo ya Ziwa Nyasa?
 
Rais Wetu Anadhamira Dhabiti, Atatimiza Na Pia Historia Ya Nchi Itamkumbuka Na Atakuwa Amechochea Ukuaji Wa Mikoa Jirani Na Dodoma
 
beach pia ipo Dodoma je raisi akijisikia kuvua dagaa yaani mpk aje dar? muwe mnafikiria bhana
Wataalamu tupo tutatengeneza mabwawa makubwa pale itakapoonekana inafaa.
Dodoma maeneo yapo mengi Tu(catchment areas) ya kuweza kufanya hivyo.
 
Kuhamia Dom?
Angefuta huo usemi kwa sasa.
Hana bajeti ya kufanya hivyo. Wizara zote hazina ofisi ya kutosha watumishi wake kama walivyo huku Dar. Nyumba za kuishi zenye hadhi zao ndo usiseme. Kwa sasa wanaishi mahotelini wakienda Dom. Balozi na Mashirika ya kimataifa yameshawekeza Dar majengo ya ofisi zao nk. Uwanja wa ndege wa Dom hamna kitu.
Ukilifanyia cost-benefit utaona cost ni kubwa. Sijaongelea maeneo ya burudani.shule za watoto.na huduma za mbalimbali wanazotumia mabalozi na watu mashuhuri.
Labda aaamue tu kuwakomoa !
 
Rais Wetu Anadhamira Dhabiti, Atatimiza Na Pia Historia Ya Nchi Itamkumbuka Na Atakuwa Amechochea Ukuaji Wa Mikoa Jirani Na Dodoma
Maendeleo yatasambaa Nchi nzima badala ya kulundikana jijini Dsm pekee.
 
Kuhamia Dom?
Angefuta huo usemi kwa sasa.
Hana bajeti ya kufanya hivyo. Wizara zote hazina ofisi ya kutosha watumishi wake kama walivyo huku Dar. Nyumba za kuishi zenye hadhi zao ndo usiseme. Kwa sasa wanaishi mahotelini wakienda Dom. Balozi na Mashirika ya kimataifa yameshawekeza Dar majengo ya ofisi zao nk. Uwanja wa ndege wa Dom hamna kitu.
Ukilifanyia cost-benefit utaona cost ni kubwa. Sijaongelea maeneo ya burudani.shule za watoto.na huduma za mbalimbali wanazotumia mabalozi na watu mashuhuri.
Labda aaamue tu kuwakomoa !
Malawi , Nigeria serikali zilihamia miji mipya vitu vingi vikiwa havipo tayari lakini wakakomaa hivyo hivyo vingi vimefanyika wakiwa huko huko kwenye miji mipya japo baadhi ya balozi na wizara zingine bado wapo miji ya zamani, wakiamua kuhamia Dodoma Kwa moyo mmoja nina hakika wapo Nchi wafadhili watasaidia bajeti na ujenzi wa miundo mbinu nk.
 
Wakati huu wa science na technologia bado kuna haja ya kuhamia Dodoma. Ni faida zipi tutapata kwa serikali kuhamia Dodoma?
Kama hujui bora ukakaa zako kimya kama miki nafuatilia tu walichosema wenzangu
Na mpaka nafikia yako nilishajua faida nyingi sana
 
Acha kufananisha ratiba za YESU na vitu vya kijinga
Rais , makamu wake, waziri Mkuu , wizara nyeti wakihamia jumla nina hakika wengi watahamia huko Kwa kasi ya ajabu na huenda bei ya viwanja na nyumba za kununua vikaanza kupanda bei ,
 
Kama hujui bora ukakaa zako kimya kama miki nafuatilia tu walichosema wenzangu
Na mpaka nafikia yako nilishajua faida nyingi sana
Faida ni nyingi Mkuu maana Kwa sasa ni Tanzania pekee Duniani ambapo wabunge wote wakuu wa wilaya, mikoa,mawaziri,wakurugenzi , mabalozi nk ni wakazi wa Dsm huko walipo wanafanya kazi lakini wakistaafu wakiwa rikizo wapo Dsm hawataki kujenga kwao wasambaze maendeleo mikoani, wilayani kote , endapo serikali itahamia Dodoma itasambaza maendeleo kwa kasi Nchi nzima pia itakuwa imemuenzi Nyerere na uchumi utakuwa kutokana na mahitaji ya bidhaa kuongezeka
 
Nchi zingine wabunge wanaishi majimboni kwao lakini Tanzania viongozi wote wanaishi Dsm , huko majimboni huenda kuomba kura Kisha kurejea Dsm Kwa style hii ni vigumu maendeleo kusambaa Nchi nzima Kama China au South Africa .
 
Back
Top Bottom