Rais Magufuli alifanya mambo yasiyofaa na Rais Samia anarekebisha mabaya yaliyofanywa

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Bila kuficha wala kuogopa, kwamba Rais Magufuli alifanya mambo ambayo ni kinyume kabisa na uongozi bora na alikuwa akitupeleka kwenye hali mbaya sana kama taifa la Tanzania. Alikuwa na kauli za kinafiki na hata kuamuru taasisi za serikali kubambikia watu kesi. Kuna mengi sana ambayo yote yakiwekwa wazi hakuna atakaetaka jina la Magufuli lionekane popote nchini, labda hayo mengine tuyaache kwa sasa.

Lakini sasa kazi kubwa anayofanya Rais Samia ni kuturudisha kwenye mstari sahihi wa uongozi kwa maslahi ya Watanzania wote. Rais Samia anastahili pongezi toka kwa kila Mtanzania mwenye akili timamu, sio lawama na shutuma. Wito wangu kwa Raisi Samia ni kuwaondoa au angalau kuwabadilisha kazi viongozi wa taasisi wote waliomtumikia Magufuli katika kutekeleza mambo maovu dhidi ya serikali na wananchi - iwe kwa kuwadhuru watu au kuhujumu mali na fedha za taifa. Nenda mbali zaidi ya Takukuru - angalia pia katika taasisi zote za serikali, za kijeshi na kiraia kutia ndani wakuu wa mikoa na wilaya. Watu hawa wamekosa imani toka kwa wananchi na hawafai tena katika nafasi zao, hawana legitimacy ya kuendelea kushika nafasi walizotumiwa vibaya. Wanaweza kuwa walitumika na si kosa lao la moja kwa moja, lakini kanuni za uongozi zinalazimu waondoke au waondolewe.

Ni vizuri watu wakaelewa haya ili kumwelewa Rais Samia. Haisaidii lolote kuficha ficha mambo. Tuko pamoja nawe Rais Samia, kwa maslahi ya Watanzania na Afrika kwa ujumla. Hongera sana mama, ziba masikio usisikie kelele za vyura wanaodhani watamzuia ng'ombe kunywa maji wakizidisha kelele.


 
Bila kuficha wala kuogopa, kwamba Rais Magufuli alifanya mambo ambayo ni kinyume kabisa na uongozi bora na alikuwa akitupeleka kwenye hali mbaya sana kama taifa la Tanzania. Alikuwa na kauli za kinafiki na hata kuamuru taasisi za serikali kubambikia watu kesi. Kuna mengi sana ambayo yote yakiwekwa wazi hakuna atakaetaka jina la Magufuli lionekane popote nchini, labda hayo mengine tuyaache kwa sasa.

Lakini sasa kazi kubwa anayofanya Rais Samia ni kuturudisha kwenye mstari sahihi wa uongozi kwa maslahi ya Watanzania wote. Rais Samia anastahili pongezi toka kwa kila Mtanzania mwenye akili timamu, sio lawama na shutuma. Wito wangu kwako Raisi Samia ni kwamba waondoe watu wote katika taasisi za serikali za kijeshi na kiraia waliotumika na Raisi Magufuli katika kunajisi nchi na wananchi, hata kama walifanya hiyo kwa kushurutishwa au kumwogopa Magufuli, kutia ndani wakuu wa mikoa na wilaya. Wananchi hawawezi kuwa na imani nao tena. Wapo wengi waliofanya uovu kwa kivuli cha kutumwa na Raisi, wakijua wazi walikuwa wakifanya uovu. Wanatakiwa wajiuzulu lakini wasipokuwa tayari kufanya hiyo waondolewe.

Ni vizuri watu wakaelewa haya ili kumwelewa Rais Samia. Haisaidii lolote kuficha ficha mambo. Tuko pamoja nawe Rais Samia, kwa maslahi ya Watanzania na Afrika kwa ujumla. Hongera sana mama, ziba masikio usisikie kelele za vyura wanaodhani watamzuia ng'ombe kunywa maji wakizidisha kelele.


View attachment 2196325
Sitiii Neno,nawaachia akina Dudumizi, yehodava,Comte,Muda wote,umkhontosizwe na wenzao watupe mrejesho.
 
278855974_140729108494107_2484514947621839905_n.jpg
 
Bila kuficha wala kuogopa, kwamba Rais Magufuli alifanya mambo ambayo ni kinyume kabisa na uongozi bora na alikuwa akitupeleka kwenye hali mbaya sana kama taifa la Tanzania. Alikuwa na kauli za kinafiki na hata kuamuru taasisi za serikali kubambikia watu kesi. Kuna mengi sana ambayo yote yakiwekwa wazi hakuna atakaetaka jina la Magufuli lionekane popote nchini, labda hayo mengine tuyaache kwa sasa.

Lakini sasa kazi kubwa anayofanya Rais Samia ni kuturudisha kwenye mstari sahihi wa uongozi kwa maslahi ya Watanzania wote. Rais Samia anastahili pongezi toka kwa kila Mtanzania mwenye akili timamu, sio lawama na shutuma. Wito wangu kwako Raisi Samia ni kwamba waondoe watu wote katika taasisi za serikali za kijeshi na kiraia waliotumika na Raisi Magufuli katika kunajisi nchi na wananchi, hata kama walifanya hiyo kwa kushurutishwa au kumwogopa Magufuli, kutia ndani wakuu wa mikoa na wilaya. Wananchi hawawezi kuwa na imani nao tena. Wapo wengi waliofanya uovu kwa kivuli cha kutumwa na Raisi, wakijua wazi walikuwa wakifanya uovu. Wanatakiwa wajiuzulu lakini wasipokuwa tayari kufanya hivyo waondolewe.

Ni vizuri watu wakaelewa haya ili kumwelewa Rais Samia. Haisaidii lolote kuficha ficha mambo. Tuko pamoja nawe Rais Samia, kwa maslahi ya Watanzania na Afrika kwa ujumla. Hongera sana mama, ziba masikio usisikilize kelele za vyura wanaodhani watamzuia ng'ombe kunywa maji wakizidisha kelele.


View attachment 2196325
NDIO MAANA MAKADA WA CCM WAPO KIMYA WAKATI WALIMTANGAZA KUWA MAGUFULI NI ZAIDI YA YESU NA MUNGU

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Labda hapo ndio tatizo - Magufuli hakuwa nyuma ya CCM, la siyo kina Kinana wasingeondoka na kurudi
Mkuu ngoja tuendelee kujifunza aina ya uongozi wetu Tanzania maana kila unae mwona kiongozi wa juu ana mapungufu mengi sana ya kiutendaji yanayo pelekea ufisadi ndani ya nchi
 
UOVU UPI??.

Vipi yaliyo mengi Mazuri yake ??
Uovu mmoja, japo wa mara moja, hubatilisha maovu yote mazuri, japo ya miaka mingi

Tenda wema na ukarimu mtaani kwako kwa miaka kumi, halafu siku mmoja mbake mtoto wa miaka mitano wa jirani yako, utajifunza jambo, kama utabakishwa hai.
 
Aki solve la watumishi wa umma na wasiojulikana atazika kabisa lagesi ya awamu ya 5.
 
Aki solve la watumishi wa umma na wasiojulikana atazika kabisa lagesi ya awamu ya 5.
Suala la wasijulikana ni sensitive sana kwa sasa, na litahitaji busara za pamoja sio Raisi Samia peke yake - kwanza lijadiliwe katika vikao vya ndani kama Raisi, KInana, Kikwete, Mwinyi wa Zanzibar nk, ndio upatikane ufumbuzi.

Lakini pia ni aibu na doa kubwa sana kwa Tanzania kiasi kwamba inawezekana uamuzi ukachukuliwa libaki limefunikwa
 
Magufuri amefanya maovu mengi sana.

Kama ulivyoshauri, nakubaliana na wewe kuwa jina lake lifutwe.

Stand ya mabasi mbezi, jina libadilishwe liitwe MBEZI bas terminal.

Magufuri afutwe kwenye kumbukumbu alituharibia diplomasia.

Kumbuka kuchoma vifaranga kutoka Kenya ilikuwa sio akili ilikuwa ni matope.

Tuliumizwa sana, alijenga roho ya visasi, ubaguzi, mauwaji utekaji.

Kifupi CCM ilikosea Sana kutuletea magufuri.
 
Magufuri amefanya maovu mengi sana.

Kama ulivyoshauri, nakubaliana na wewe kuwa jina lake lifutwe.

Stand ya mabasi mbezi, jina libadilishwe liitwe MBEZI bas terminal.

Magufuri afutwe kwenye kumbukumbu alituharibia diplomasia.

Kumbuka kuchoma vifaranga kutoka Kenya ilikuwa sio akili ilikuwa ni matope.

Tuliumizwa sana, alijenga roho ya visasi, ubaguzi, mauwaji utekaji.

Kifupi CCM ilikosea Sana kutuletea magufuri.
Jifunze kwanza kuandika vizuri aliitwa Magufuli.
Aliekulisha hayo maovu kakupa nondo chache sana.
 
Aliua, alitesa na akazikwa na yupo mavumbini akisubiri hukumu, sawa.

Hebu wahafidhina tuseme haya mabaya mengi na madogo mazuri aliyofanya ni yapi?.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom